text
stringlengths
43
182k
timestamp
timestamp[s]
url
stringlengths
16
3.37k
zanzibar padre apigwa risasi na watu wasiojulikana | jamiiforums | the home of great thinkers zanzibar padre apigwa risasi na watu wasiojulikana discussion in 'habari na hoja mchanganyiko' started by dsn dec 25 2012 kwa mujibu wa breaking news sasa hivi toka radio one padre anayejulikana kwa jina la ambrose mkenda amepigwa risasi na watu wasiofahamika kwenye gate la nyumbani kwake wakati akifunguliwa gate aingie nyumbani kwake maeneo kitomondo mjini zanzibar ambako ndiko makazi yake yalipo akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha pekee yake hali yake sio nzuri kwani risasi aliyopigwa imemdhuru maeneo ya mdomoni waliompiga risasi padre huyo inasemekana ni watu waliokuwa kwenye pikipiki ambao walimvamia akisubilia afunguliwe gate kuingia nyumbani kwake kuna nini katika siku muhimu kwa waumini wa kikristo kufanyika kwa tendo kama ilo kwa kiongozi wa madhehebu makubwa kama roman catholic wanaojua kinachojili huko zanzibar watujuze tafadhari kulikoni katika siku njema kama hii ya christmas note ujumbe mkuu wa kanisa la roman catholic katika christmas ya mwaka huu 2012 upendo na amani ndio ujumbe mkumbwa wa sikukuu hiyo picha kwa niaba ya mwanajamii forum kwa id ya mchami taarifa ya leo tarehe 26/12/2012 kwenye vyombo vya habari kuhusu tukio father ambros mkenda wa parokia ya mpendae katika kanisa katoliki mjini zanzibar amepigwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni wakati akitokea kanisani kamanda wa polisi wa mkoa wa mjini magharibi aziz juma mohammed amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema father amepigwa risasi na ameumizwa sehemu ya kichwa na amekuwa akitoka damu nyingi kichwani na tayari anapatiwa matibabu katika hospitali kuu ya mnazi mmoja “sisi tunahesabu kuwa kitendo hiki ni kitendo cha kihalifu na tunawatafuta wahalifu waliofanya kitendo hiki kwa hivyo bado ni mapema kusema kwamba kitendo hiki kimefanywa na nani kwa kuwa bado uchunguzi wetu unaendelea na hadi sasa hakuna mtu tuliyemshika kuhusikana na tukio hili” alisema kamanda “tumekuta mabaki ya risasi ndani ya gari yake na katika vioo vyake vya gari vimevunjika na tumekuta damu chini pale” alisema kamanda aidha kamanda azizi alisema father ambros yeye ni mhasibu pale kanisani na hivyo mara nyingi watu wananaamini kwamba katika siku za krismass mara nyingi sadaka hukusanywa fedha nyingi na hivyo wanamini kwamba alikuwa fedha mikononi na ndipo inawezekana waliamua kumpiga risasi wakitaka kuchukua fedha hizo hata hivyo alisema uchunguzi wa awali ndio utakaoeleza ni suala gani lililopelekea kupigwa risasi lakini wanaendelea na uchunguzi huo ambapo uchunguzi ndio utakaojulikana sababu kamili ya tukio hilo akizungumzia tukio hilo askofu michael hafidh wa kanisa la anglikan la mkunazini amesema wamesikitishwa na wamepokea kwa mshituko mkubwa tukio hilo hasa kwa kuzingatia matukio kama hayo hayajawahi kutokea ya kuwahujumu viongozi wa dini alisema tukio hilo ni miongoni mwa matukio ya kushtusha na yanaashiria hali mbaya ya kiusalama na kuwaomba viongozi wa serikali kuchukua hatua za tahadhari kubwa kwani matukio kama hayo yameanza kutokea kwa viongozi wa dini ambapo mwanzo ilianzia kwa sheikh soraga na baadae kutokea kwa father ambros “ hii ni hali ya hatari katika nchi yetu na haipendezi lakini serikali lazima ijue sisi hatuwezi kujua wala hatuwezi kujilinda lakini serikali inapaswa kutulinda sisi ndio wananchi wake” alisema askofu hafidh askofu hafidh alisema hivi karibuni kumekuwepo vipeperushi vilivyosambazwa na watu vikiwatisha watu wenye imani ya kikristo ambapo alisema miongoni mwao walikuwa na khofu juu ya kusambazwa kwa vipeperushi hivyo na kuiomba serikali iongeze ulinzi “tumeona hivi vipeperushi na kwa kweli tulikuwa na khofu juu ya vipeperushi hivi lakini ndio tunasema tunaelekea wapi katika maisha haya” alisema akofu hafidh “sisi hatuamini kwamba kuna kisasi kwa viongozi wa dini lakini tunachukulia hilo ni tukio la kihalifu na pia hatuna vipeperushi vya aina yoyote vinavyoelezea kuwatisha viongozi wa dini kwa hivyo tunachukulia hayo ni matukio ya kihalifu na wala hatuamini kwamba matukio haya ni ya dini fulani” alisema kamanda azizi “sisi kawaida huwa tunaweka ulinzi siku za sherehe zozote lakini kwanza makanisa yote yamewekwa ulinzi wa kutosha kabisa lakini wahalifu wanapotaka kufanya uhalifu huwezi kujua watatumia mbinu gani na saa ngapi na watafanya uhalifu huo wapi lakini ulinzi upo wa kutosha” alisisitiza kamanda azizclick to expand 12252012 105510 pmjpg pole sana inasikitisha sad news kitomondo ni wapi huko itv ya saa ngapi mbona mi naangalia itv sijaona mhh mbona hatari hii mambo ya kulea watu na kumuambia macho uchokozi wa kidini rwanda hiyo inakuja tanzania mungu epusha janga hili linalonyemelea tanzania oooh my god rip tumbiri (upanga dar es salaam tanzania) tumbiri@jamiiforumscom tumbiri said mkuu pasco na wadau wote wa jf nilisoma thread haraka haraka na wakati nacomment nilijua tayari ameshakufa after all hata heading ya thread nayo haijakaa vizuri is better mods wangeirekebisha na kuwa padri ajeruhiwa kwa risasi kuliko ilivyo hivi sasa tumbiri (upanga dar es salaam tanzania) tumbiri@jamiiforumscomclick to expand in nomine patris et felio et spiritus sanct namuombe afya njema padre huyu hiyo risasi imemjeruhi au ni vipiclick to expand kwa mujibu wa mtangaji faruku karim inasemekana hali yake sio nzuri na amekimbizwa hospitalini huku wakiangalia kama kuna uwezekano wa kumleta tanzania bara ni kweli kuna breaking news ya maandishi yanapita itv my god where are we going oooh my god rip tumbiri (upanga dar es salaam tanzania) tumbiri@jamiiforumscomclick to expand hajathibitishwa kama kafa ila hali yake ni mbaya wanampango wa kumleta tanzania bara kwa matibabu zaiditumuombee apate auenikwa kuwa tendo hilo katika kipindi kama hiki hata kama ni wezi basi target ni mbaya na ina ishara mbaya tunaomba mungu amsaidie dhidi ya hayo mashetani tnx kwa taarifa mkuu inasikitisha sana sad news namuombea padri apone majuruhi aliyopata sematena tumechoka amani labda kama ni maandishi mybe i wasnt paying attentionila kwasasa sioni maandishi na tamthilia a woman of steel ndo iko hewani na ninajua kama ni maandishi hawaweki jina la repotasasa mtu anajuaje kuwa ni farid ndo karipoti my god where are we goingclick to expand raisi akiambiwa dhaifu anakataa 21512475
2017-06-22T12:11:24
https://www.jamiiforums.com/threads/zanzibar-padre-apigwa-risasi-na-watu-wasiojulikana.374176/
ccm kupatana kutengana au kuendelea kuchunguzana | jamiiforums | the home of great thinkers ccm kupatana kutengana au kuendelea kuchunguzana discussion in 'jukwaa la siasa' started by mzee mwanakijiji feb 15 2010 likes received 6391 dalili zote kutoka dodoma zinaonesha kuwa hatimaye mgogoro wa kiuongozi uliokikumba chama cha mapinduzi kwa takribani mwaka mmoja sasa utamalizwa kwa kutafuta njia ya upatanisho kati ya makundi yake mawili ambayo yamekuwa katika barabara ya kugongana kufuatia shutma za nani ni mwadilifu na nani ni fisadi vyanzo mbalimbali kutoka dodoma vinadokeza kuwa ripoti ya mzee mwinyi iliyoundwa kutafuta chanzo na kutoa mapendekezo ya kutatua mgogoro huo inaonesha kuwa kwa hali iliyopo sasa itakuwa vigumu mno kwa chama hicho kutimuana au kupeana adhabu ambazo zitakifanya kionekane dhaifu kikubwa ambacho kinaonekana kubadilisha kabisa mwelekeo wa mapendekezo hayo ni kuundwa kwa chama cha jamii ambacho kinasubiri usajili wa muda ili kiweze kuanza kazi zake kuanzishwa kwa ccj (kama nitakavyoonesha katika makala yangu mojawapo wiki hii) kunawatatiza viongozi wakuu wa ccm kwani kuanzia tetesi za uwepo wake juhudi nyingi zimekuwa zikifanyika kujua hasa ni vigogo gani wako nyuma ya chama hicho kutokana na kutokuwa na ushahidi wa nani anahusika au nani hausiki adhabu ambazo zinaweza kutolewa katika kikao hicho zaidi ni onyo na karipio kali lakini adhabu za kusimamishwa uongozi au hata kufukuzwa kutoka katika chama zinaonekana kukataliwa na wengi kwani itaonekana kuwapa faida baadhi ya watu kwenye chama hicho kambi hizo ambazo zimekuwa zikigongana hasa kwa kutumia vyombo vya habari na kwenye majukwaa ya kisiasa ikiwemo bungeni zilizaliwa mara baada ya ripoti ya kamati teule ya bunge iliyochunguza kampuni ya richmond kuja na mapendekezo makali ambayo yalichangia kuanguka kwa aibu kwa aliyekuwa waziri mkuu bw edward lowassa pamoja na mawaziri wengine wawili kitu ambacho kilisababisha kuvunjika kwa baraza la mawaziri wa serikali ya rais kikwete tukio la kujiuzulu lowassa liligawa bunge wana ccm na watanzania katika kambi zilizotofautiana kama lowassa na wenzake walionewa au walistahili kuwajibishwa kutokana na tukio hilo wale ambao walionekana kumtetea lowassa na wenzake mara moja wakaanza kuhusishwa na watetezi wa ufisadi huku kambi iliyosifia ripoti ile ya richmond kuanza kuonekana ni wapiganaji wa ufisadi kwa mwaka mzima dalili za kambi hizo kupatana zilionekana kutoweka hasa kile amabacho kimetajwa kuwa ni jaribio la kumvua uanachama spika wa jamhuri ya muungano na mmoja wa kambi kufanyika spika sitta alisalimika kuchukuliwa hatua na chama chake baada ya pendekezo la kuundwa ka kamati ya mzee mwinyi mzee pius msekwa na mzee kinana kuundwa ili kutafuta chanzo cha migogoro ndani ya chama hicho kupendekeza namna ya kutatua migongano ndani ya wabunge na jinsi ya kupendekeza namna jinsi bunge litaweza kufanya kazi zake bila kusababisha migogoro kama hii juhudi za chini kwa chini za kuzipatanisha kambi hizo mbili hadi hivi sasa zimeshindikana na chanzo chetu kimoja kimetudokeza kuwa wananchi wasishangae kuona ni kina mwakyembe na wenzake ndio wanapewa lawama za namna fulani kwa kuharibu sifa za wanachama wengine kwa kuwaita mafisadi ni matokeo ya uchunguzi huu yanaonesha kuwa ccm wataamua kutafuta njia za kidiplomasia zaidi kumaliza mgogoro wao kama walivyofanya kwenye suala la richmond na hasa namna ya kuhakikisha hatimaye lowassa na mwakyembe wanakumbatiana mengi na rostam wanakunywa chai pamoja katika hali ya kuonesha hatimaye umoja na mshikamano umepatikana ndani ya chama na hii ndo inasababisha nisilale anxious to know what's up nchi haiendeshwi kwa kubembelezana watu wazima ambao ni wezi kama el ra na kundi zima la mafisadi wanatakiwa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na kuchukuliwa hatua kama hawatafukuzwa kwa uongozi kuogopa au kulindana huo ndio mwanzo na mwisho wa chama cha majambazi ccm wataendelea kulindana kama mlimwelewa vema alivyoongea msekwa wamefanikiwa kuurejesha umoja wa ccm uliokuwa unasambaratika je kauli hii itasimama wanajivunia kuwa kamati ya kipekee iliyoweza kufanya jambo kubwa sana kwa chama kabla ya uchaguzi i wish wangefukuzana ili waunde chama kingine (hata waende huko ccj) nzuri kwa demokrasi yetu nilijua tu hakuna jipya litakaloamuliwa kwa kuwa viongozi wengi wa ccm wamejaa uoga na ni wagumu kuthubutu kufanya maamuzi magumu vilevile je vipi kuhusu wale wapiganaji waliotuletea waraka hao si wapiganaji ila wagawanyaji wanataka kutugawa for how long will watanzania continue to bend over to accomodate ccm mistakes and stupidity no one can whistle a symphony it takes an orchestra to play ityou can work miracles by having faith in othersto get the best out of people choose to think and believe the best about them madai yao ni mwaka wa uchaguzi hivyo ni lazima wabebane ili waendeelee kuwa wengi bungenihuu ni uzandiki kwa watanzania wanao wategemeaunafiki mtupusiasa bwana me anaanza kuichoka bado mapemaaaaaaaaa mpaka watakapopata chama kingine cha siasa watakachoamini kuwa kinabeba matarajio yao kitu wanachofanya ccm ni kama kumpa mgonjwa wa ukimwi dawa za kurefusha maisha wanajipa matumaini kama wako angaza vile wanafikiri wametibu kumbe ni kinga tu ya uchaguzi ili upite dawa itakapoisha nguvu inabidi warudi tena angaza(tume nyingine) dawa halisi ipo na wanaijua ila waogopa ni chungu kuimeza watafurahia mgojwa wao kumeremeta usoni lakini maradhi yanaendelea kumtafuna mkerwaji member kinachotokea ndani ya ccm ni picha au movie ambayo mwisho wake itakuwa surpriseni kweli watu wanaongea lugha tofauti kwa msukumu wa manufaa yaohapa natumia neno yao kwa maana ya ccm au binafsihivyo basi lolote linawezekana tumechoka sana na mambo kama haya maana kila kikicha kuna ulazima kuona kuwa tanzania inakuwa katika misingi imara kabisa na sio katika mambo ya ajabu sana kama haya ua siku hizi mzee mwanakijiji kama nilipoandika kuhusu bunge lafunika kombe mwanaharamu apite ccm nayo huko dodoma inafunika kombe wanaharamu wapete nilikuwa na source wangu mzuri sana ndani ya cc na nec baada ya kujua mimi ni mwana jf amenikatia line kiaina namjaribu tena for the last time asipotoa updade basi itakuwa ni kweli kombe limefunikwa mpasuko (niwe wa kwanza kutumia neno hilo) uliopo ndani ya ccm ni mkubwa mno kiasi kwamba wanaweza kuishia kukubaliana kutokubaliana lakini vile vile bila kufukuzana au kutukanana wimbi limegeuka goliathi anayumba is it correct to ask for how long will opposition parties continue to bend over to accomodate ccm mistakes and stupidity for expenses of tanzanian tax payer in the so called ruzuku
2018-01-19T08:41:25
https://www.jamiiforums.com/threads/ccm-kupatana-kutengana-au-kuendelea-kuchunguzana.52975/
ikitokea kwako utafanyaje | jamiiforums | the home of great thinkers ikitokea kwako utafanyaje discussion in 'mahusiano mapenzi urafiki' started by mom jul 1 2010 wewe ni mwanamke/mwanaume una rafiki ambae mlipatana sana na kuheshimiana wewe umeoa/kuolewa nae pia ana mwenzi wake sasa inatokea kwenye ndoa yako kuna migogoro mingi inayopelekea hata kuiona ndoa chungu rafiki yako huyu humshirikisha katika maamuzi shida zake na ni mshauri wako mzuri inatokea cku moja unaenda kwake baada ya kukorofishana na mwenzi wako huko home na unamkuta mwenyewe katika ile kukupoza upunguze hasira mnajikuta mko katika step nyingine ambayo hukutarjia na at the end mnafanya kitendo ambacho kimekua majuto kwako mpaka leo hii hutamani kumwona huyo rafiki tena hebu fafanuahuyu rafiki ni wa jinsia moja au tofauti pole sana mom ilikuwaje tena ukaamua kufanya infidelity anyway ni shetani alikupitia sasa tubu dhambi zako na usirudie tena kutenda dhambilielielie hebu fafanuahuyu rafiki ni wa jinsia moja au tofauticlick to expand wa jinsia tofauti sasa tubu dhambi zako na usirudie tena kutenda dhambilielielieclick to expand nitubu kwa nani mr au mke wa jamaa au hivi kama huna amani moyoni hata wazo la kubanjuka juu linakuwepo haya tuambie kwa nini hutaki kumuona rafiki/au mpenzi sasa sijui ningefanyeje n ando nsha do na rafiki is it possible to undo haya tuambie kwa nini hutaki kumuona rafiki/au mpenzi click to expand kwa kosa kama hilo ulilofanya si unakua umeshaharibu urafiki wenu hapo kwenye red cjui kwa kweli lakini ni kweli imemtokea my very best frend nami nilimshauri aije kumweleza mumewe kitu hicho is it possible to undoclick to expand bht nawe unachekesha sasa hapo nawish ingekua possible kwa kuanzia i dont believe na marafiki wa karibu sana hivyo wa jinsia tofauti u r either in a relationship na huyo rafiki yako au u stay away from each other hii dhana ya 'rafiki yangu tu' siielewihivi mwanamme unamruhusu vipi mkeo kuwa na rafiki wa karibu hivyo mwanamme mwenzio mimi kwa upande wangu mume wangu siwezi kumruhusu rafiki wa karibu hivyo wa kikeataniwia radhi wa jinsia tofauticlick to expand dah afadhalinilitaka kuogopa sanahapo cha kufanya ni kama alivyosema mtumishi wa bwana chrispintubu dhambi zako kwa maana ni mwema sanazaburi ya 3234 inasema hivi'3bwana kama wewe ungehesabu maovu ee bwana nani angesimama4lakini kwako kuna msamaha ili wewe uogopwe na ukishatubu amini kuwa umeshasamehewa dhambi zako na mungu hatazikumbuka tena hivyo na wewe usitende dhambi tena na usijihukumu tena kwa kosa kama hilo ulilofanya si unakua umeshaharibu urafiki wenu hapo kwenye red cjui kwa kweli lakini ni kweli imemtokea my very best frend nami nilimshauri aije kumweleza mumewe kitu hichoclick to expand ukido na rafiki yako mnaharibu au ndo mmecement urafiki bht nawe unachekesha sasa hapo nawish ingekua possibleclick to expand nachekesha tena mamiii nimeulizamaana kama yakimwagika hayazoleki basi utafanyeje sasa ajali huwakumba wanaochukua na wasiochukua tahadhari ingawa kwa anayechukua tahadhari humjia katika madhingira ambayo hayakwepeki (mfano hayo ya kwako) hupaswi kujuta but ni funzo la kukuongezea umakini ili lisitokee tena onana na mwenzio ili ujue moyoni mwake alidhamiria au ni ajali kama kwa upande wako nitubu kwa nani mr au mke wa jamaa auclick to expand kabla ya kutubu niambie kwanza kwanini ulimua kuinfidelaizi chrispin hebu nikuulize kidogowewe huwa unamruhusu mkeo kuwa na rafiki wa karibu wa kumhadithia matatizo yake yooote mwanamme kabla ya kutubu niambie kwanza kwanini ulimua kuinfidelaiziclick to expand ckuamua ilikuaja naturaly mimi kwa upande wangu mume wangu siwezi kumruhusu rafiki wa karibu hivyo wa kikeataniwia radhiclick to expand kwan gaijin hujawahi kuwa na rafiki wa jinsia tofauti b4 marriage na je kama alikuwa after marriage urafiki ulikufa ukido na rafiki yako mnaharibu au ndo mmecement urafikiclick to expand ule urafiki uliokuwepo utakufa kabisa yataanza madhambi ya infidelity chrispin hebu nikuulize kidogowewe huwa unamruhusu mkeo kuwa na rafiki wa karibu wa kumhadithia matatizo yake yooote mwanamme click to expand hebu rudia swali lako mama naona kama sijaliona vizuri yaani mama watoto wangu awe na rafiki wa kiume ambaye anaenda kumwambia matatizo ya familia yangu yaani sielewi bado mom kusema ukweli sikuwa na rafiki wa jinsia tofauti wa kihivyorafiki close nnao lakini sio wa kwenda (a) kwake (b) sehemu private tuko na yeye tu juu ya hivyo baada ya kuwa kwenye ndoa nimepunguza urafikisitafutani nao kihivyo na kuwatafuta kwangu ni kuwaalika kwangu for dinner or lunch na mimi na mume wangumimi na yeye faragha hamna hata kidogo at the end now wamekuwa rafiki wa mume wangu kuliko mimiwanatafutana bila ya mimi kuwa na habari kwa ufupi urafiki umepunguastatus yangu haini ruhusu kuwa na marafiki wa kihivyo nafikiri
2016-12-09T23:22:13
http://www.jamiiforums.com/threads/ikitokea-kwako-utafanyaje.66021/
michuano ya cecafa yapamba moto | michezo | dw | 24112015 michuano ya cecafa yapamba moto michuano ya kombe la mataifa ya afrika mashariki na kati cecafa senior challenge inaendelea kupamba moto katika mji mkuu wa ethiopia addis ababa malawi ambayo inashiriki kama timu ya kualikwa imepata ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya sudan katika mchuano mwingine wa jana jumatatu sudan kusini iliichapa djibouti 20 leo jumanne zanzibar heroes watashuka dimbani na uganda tanzania bara maarufu kama kilimanjaro stars watakuwa wageni wa rwanda kenya walianza vizuri kampeni yao baada ya kuwaangusha mahasimu wao wakubwa uganda kwa mabao 20 katika mchezo wa kundi b kenya iko sawa kwa pointi na burundi baada ya burundi kuishinda zanzibar kwa bao 1 0 nayo rwanda ilishinda kwa bao 10 dhidi ya wenyeji ethiopia na tanzania bara ikaishinda somalia kwa mabao 40 katika kundi a mada zinazohusiana kenya tanzania rwanda john pombe magufuli pembe ya afrika uchaguzi mkuu kenya 2017 maneno muhimu cecafa ethiopia kenya tanzania rwanda malawi kiungo http//pdwcom/p/1hb1q
2018-03-20T01:06:43
http://www.dw.com/sw/michuano-ya-cecafa-yapamba-moto/a-18870284
aids daymessage hot | jamiiforums | the home of great thinkers aids daymessage hot discussion in 'mahusiano mapenzi urafiki' started by elli dec 1 2011 haya leo ndio siku ya ukimwi duniani je umeitathimini mienendo yako inakuweka kwenye position gani my message to you is this a moment of pleasure can desrtoy many lives an act of carelessness can shut down many dreamz it is aids day play smart and safe flee from hiv/aids thanks elli aka mumangu ignorance and prejudice are fueling the spread of a preventable disease world aids day 1 december is an opportunity for people worldwide to unite in the fight against hiv and aids it's up to you me and us to stop the spread of hiv and end prejudice ~worldaidsdayorg 2006 nimekusoma vizuri sana ignorance and prejudice are fueling the spread of a preventable disease world aids day 1 december is an opportunity for people worldwide to unite in the fight against hiv and aids it's up to you me and us to stop the spread of hiv and end prejudice ~worldaidsdayorg 2006click to expand huku iringa maambukizi rate yake ni 157 kitaifa pia matumizi ya kondom kwa mwenzi yakadiliwa kufikia box 10000 kwanza nawapa pole wote waliopoteza ndugu jamaa marafiki na wapenzi wao kutokana na ugonjwa huu na wale wanaoumwa na wapa pole sana na nawatakia mpone kwa njia yoyote hile na pia nawaomba msaidie kutoa elimu ya ugonjwa huu kwa wengine ambao hawajaathirika hili kupunguza maambukizo na pia kwa wale walioathirika jitahidi kuto ambukiza kama ni ngumu kumwambia mtu umeathirika ni vizuri ukatae kufanya nae mapenzi kwa wengine ambao hawajaathirika kumbuka kujikinga kwa kutumia condom usifanye mapenzi na mtu ambae hujui status yake na jitahidi kuwa na mpenzi mmoja na wote mjue status zenu mwisho tujaribu kutambua afya zetu kila mwaka kwani inasaidia kuweza kutibu magonjwa mapema kabla hajamiliki mwili na tutoe ushirikiano kwa waathirika ni kukumbushana wakuu usikose kuwakumbusha wengine naomba kuuliza watumia condom ambao wamepima na hawaathirika bado then wale ambao hamjapima hiv bado mpo mpo kwanza je ukijua mimi mrembo sana unanitamani nimeathika utatumia condom na mimi je kama huna uhakika utatumia condom na mimi ujumbe wangu wa leo tanzania bila maambukizi mapya ya ukimwi inawezekana tumia utashi wako wakinge watoto na maambukizi ya kutoka kwa mama pima kabla ya kuamua kupata mimba epuka mimba zisizotarajiwa kama mama umeambukizwa tafuta ushauri ha huduma ili upate mimba salama na usimuambukize mwanao tumboni wakati wa kujifungua au wakati wa kutunza na kumnyonyesha inwezekana wanaume na wanawake tusaidiane chakaza tpaul faizafoxy mani a moment of pleasure can desrtoy many lives an act of carelessness can shut down many dreamz it is aids day play smart and safe flee from hiv/aids thanks elli aka mumanguclick to expand and its begin with you kuna wakati kipindi cha nyuma ililetwa habari jf kuwa mengi alikomba mamillioni ya misaada ya aids kuna wakati kipindi cha nyuma ililetwa habari jf kuwa mengi alikomba malillioni ya misaada ya aids tujikumbusheclick to expand faiza bhana unaonaje kwa leo tukadili kwanza na hili halafu hilo la mengi tukalifulie uzi wake tafadhali sana nakuomba leo tu tumia busara please tuendelee na hili nakuomba sana hilo la mengi tulifungulie uzi inaonekana una point nyingi juu ya hilo utatusaidia kukomesha hilo ila kwa sasa hebu tujikite na hili asante kwa kuwa mwelewa unaleta siasa mpaka huku watu wengine sijui mlilelewa na nani huo uzi unaotaka kuleta una relates haswa na siku ya leo tukumbushe foxy je kama huna uhakika utatumia condom na mimiclick to expand na kama wewe utakuwa kweli umeathirika na una lengo zuri tu la kuwakinga wengine utanimbia mimi sukari imeshangia mdudu kwahiyo ni bora tusifanye kabisa kuliko kufanya kwa kutumia condomu ukimwi hauna tiba kwa wasomi wa dunia hii wamwaminio halisi yehova wanapona kwa maombezikatika jina la yesu kristo naumia sana tena sana eeeh mola saidia familia yetu ngoja niishie hapa make machozi yananilenga ngoja niishie hapa make machozi yananilengaclick to expand hakika nitakuja rock city kukufuta hayo machoziujue mie sipendi unavyolia
2017-01-23T00:30:29
https://www.jamiiforums.com/threads/aids-day-message-hot.198670/
waziri atembelea taasisi ya nyaraka wakala wa uchapishaji zanzinews home habari matukio waziri atembelea taasisi ya nyaraka wakala wa uchapishaji waziri atembelea taasisi ya nyaraka wakala wa uchapishaji kitabu kilichosheheni kazi ya utafiti iliyofanywa na rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi dk ali mohamed shein baada ya kukamilisha masomo yake ya udaktari (phd) mwaka 1988 waziri wa habari utalii na mambo ya kale zanzibar mahmoud thabit kombo akiangalia vitabu vya utafiti wa phd za rais wa zanzibar awamu ya tano dk salmin amour juma (alichokishikilia) na kile cha rais wa sasa dk ali mohamed shein (kilicho mezani) alipotembelea taasisi ya nyaraka na kumbukumbu kilimani mjini unguja waziri wa habari utalii na mambo ya kale mahmoud thabit kombo na wasaidizi wake wakipata maelezo kutoka kwa mkurugenzi wa wakala wa serikali wa uchapaji zanzibar muhammed suleiman khatib kuhusu utendaji kazi wa mitambo mipya mkurugenzi wa wakala wa serikali wa uchapaji zanzibar (zagpa) muhammed suleiman khatib (kushoto) akimueleza waziri wa habari utalii na mambo ya kale mahmoud thabit kombo na watendaji aliofatana nao namna gazeti la zanzibar leo linavyopitia njia mbalimbali za uchapishaji gazeti lililojulikana kwa jina la kweupe toleo namba 76 la tarehe 10 agosti 1963 ambalo lilikuwa likichapishwa zanzibar kama linavyoonekana lililohifadhiwa kwenye taasisi ya nyaraka na kumbukumbu kilimani mjini unguja picha zote na salum vuai maelezozanzibar serikali ya mapinduzi zanzibar imesema inajipanga kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazoikabili taasisi ya nyaraka na kumbukumbu iliyoko kilimani mjini unguja ili ifanye kazi kitaalamu zaidi waziri wa habari utalii na mambo ya kale mahmoud thabit kombo akiwa katika ziara ya kuzitembelea taasisi zilizo chini ya wizara yake leo mei 4 2018 amesema teknolojia ya kisasa inahitajika katika kutunza na kuhifadhi kumbukumbu za kihistoria ili ziendelee kuishi miaka mingi bila kuharibika alieleza kuwa katika kufanikisha suala hilo tayari serikali ya mapinduzi zanzibar imesaini mkataba na wenzao wa oman utakaotoa fursa kwa wafanyakazi wa taasisi hiyo kupatiwa mafunzo yatakayowawezesha kutumia vifaa vya kisasa katika kuhifadhi kumbukumbu hizo mkataba huo uliosainiwa mwanzoni mwa wiki hii mjini muscat nchini oman wakati waziri huyo alipofanya ziara pamoja na viongozi kadhaa wenye dhamana ya kutunza nyaraka na mambo ya kale pia utaangalia uwezekano wa kuipatia vifaa vya kisasa taasisi hiyo ziara yetu tuliyoifanya nchini oman hivi karibuni imefungua milango ya matumaini kupata msaada wa utaalamu na vifaa kwa ajili ya kutunza nyaraka na kumbukumbu nyengine za kale kwa njia za kisasa zikiwemo za kieletroniki alisema waziri thabit waziri huyo amesema oman ambayo ina uhusiano wa kihistoria na zanzibar kwa miaka mingi sasa imeonesha dhamira ya kweli kusaidia katika jambo hilo fursa aliyosema serikali inapaswa kuichangamkia kikamilifu ili nyaraka muhimu za nchi na nyenginezo zidumu katika hali nzuri na kutumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo tafiti mapema mkurugenzi wa taasisi hiyo salum suleiman salum pamoja na wakuu wa vitengo tafauti walisema wanafanya kazi katika mazingira magumu kutokana na ukosefu wa vifaa vya kisasa pamoja na kutokuwa na nafasi ya kutosha kutunza nyaraka na kumbukumbu muhimu za taifa waziri huyo na wasaidizi wake pia walitembelea wakala wa serikali wa uchapaji zanzibar (zagpa) maruhubi ambako pamoja na mambo mengine walishuhudia mitambo ya kisasa inayotumika kuchapishia nyaraka majarida kalenda risiti na vitu vyengine mbalimbali mkurugenzi wa wakala huo muhammed suleiman khatib alisema pamoja na mafanikio wanayopata wanakabiliwa matatizo katika kuhifadhi vifaa kutokana na ghala ndogo waliyonayo ambayo haikidhi mahitaji hata hivyo aliziomba taasisi za serikali binafsi pamoja na watu mbalimbali wenye kuhitaji huduma za uchapishaji kuutumia wakala huo akisema sasa umeimarishwa kwani mitambo yake ni ya kisasa na yenye kutoa machapisho yenye viwango bora waziri thabit pamoja na kushauri njia mbalimbali za kuimarisha utendaji wa taasisi alizozitembelea aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizoelezewa ili kuleta ufanisi na tija katika taasisi hizo na serikali aidha aliwapongeza wafanyakazi na viongozi wa taasisi hizo kwa moyo wao wa kizalendo katika kuwajibika huku akiwashajiisha kujifunza zaidi ili kwenda sambamba na ulimwengu wa kisasa akitoa muhtasari baada ya kukamilisha ziara hiyo katibu mkuu wa wizara ya habari utalii na mambo ya kale khadija bakari juma alisema wamejifunza mengi katika uhalisia wa taasisi hizo ziara hii na nyengine zilzotangulia awali katika taasisi zetu zimetupa mwanga wa kujua namna ya kujipanga ili kutekeleza majukumu yetu katika dhamana hizi mpya tulizokabidhiwa na mheshimiwa rais na tunaahidi tutashirikana kwa manufaa ya nchi yetu alieleza
2018-10-18T05:22:31
http://www.zanzinews.com/2018/05/waziri-atembelea-taasisi-ya-nyaraka.html
kwanini ni vigumu kuiba kura katika uchaguzi wetu tusitafute visingizio | jamiiforums | the home of great thinkers discussion in 'uchaguzi tanzania' started by mzee mwanakijiji oct 20 2010 hakuna wa kuiba kura yako isipokuwa wewe mwenyewe ukikataa kupiga kura unayotaka utakuwa umeiiba haki yako mwenyewe ni kwa kutokupiga kura wakati mtu kajiandikisha na ana uwezo muda na nafasi hapo ndipo wizi wa kura unatokea kaka story yako ndefu sijaimaliza lakini believe or not kura huwa zinachakachuliwa kwa wale mawakala either kubadiri kura au kutohesabu kama ipasavyo sasa ukizungumzia katika majimbo ambayo wapinzani wameweka mizizi saana ukiiba utaleta machafuko so hapo naona umechakachuliwa mwanakijiji hawa jamaa kuiba kura wanaweza hasa za urais ambazo zimetapakaa nchi nzima maalim seif hajawahi kushindwa zanzibar lakini hajawahi kuwa rais wa zanzibar mbaya zaidi ni vyombo vya dola vinavyotumika kuifanya kazi hiyo sio watu wa kawaida wizi wa kura upo dunia nzima na mbinu zipo nyingi za kuiba kura technologia imekuwa sana prof mvungi na cheyo momose ni mashahidi wa hilo mkuu wizi wa kura upo na utafanyika mwaka huu not withstandingwhat happened i know the perception wanaibaje kura mawakala hawahesabu kura jamani zinaibwaje zamani ilikuwa rahisi kwa sababu sanduku linapakizwa kwenye baskeli kwenda kuhesabiwa sehemu nyingine siyo mnasema wizi upo kinadharia inawezekana lakini mtu aniambie unawezekana vipi wildcard anasema kuwa zanzibar waliiba ah wapi kuna suala la tume ya uchaguzi kuingiliwa hilo limetokea kenya na ninaamini ndilo lenye uwezekano mkubwa wa kutokea tanzania mwaka huu mzee mwanakijiji nadhani wizi unaouzungumzia hapa ni wa kupitisha au kuongeza kura ili kuongeza namba ya kura alizopata mgombea mmoja naungana na wewe wizi wa namna hiyo ni mgumu sana maana wananchi wanaona kinachoingia na kinachotoka lakini mkuu mwanakijiji mimi nasema kabisa kama hakuna uangalizi mzuri namaanisha kama waangalizi wakiwa ni njaa ni rahisi sana kile kilichobandikwa ukutani kisiwe kile kilichohesabiwa kwa zanzibar hasa ule wa mwaka 2000 ni masanduku yaliyojazwa kura za karume ndio yaliyobadilishwa na yale ya kura halisi kijeshi kabisa staili hii ilitumika pia drc kumsaidia kabila kushinda uchaguzi ule dhidi ya bemba hii ni imani ilijengeka watu wengi najua wanaingia kwenye kituo cha kupiga kura na wanatoka lakini hawajui nini kimetokea kabla yao au baada yao kutokana na imani hii nadhani kwa kweli tume ya uchaguzi lazima itoe tamko la maelezo ya jinsi kura zinavyopigwa na nini kinapaswa kufanywa au kufanyika maana naona watu wengi kweli wanaaminii wizi hutokea kwenye kituo cha kupigia kura hili wazo ni la hatari sasa hili swala la kuiba kura unataka kusema halipo then tatizo lipo kwa mawakala kama ndo hivisina experience yoyoyte zaidi ya kusikia kura zinaibwa kama ulivo oneshakama vyama vitakuwa na mawakala waaminifu basi wizi hautakuwepo sidhani kama ni uwizi wa kura bali ni kwa sababu ya katiba yetu inayosema kuwa nec ikitangaza matokeo ya urais hayawezi pingwa popote palekipengele hiki ndani ya katiba ni cha kishetani wasiwasi wangu ni huumajumuisho ya mawakala wa chadema unaweza ukaonyesha labda uchaguzi ni too close to call na hata labda dr slaa akashinda kwa kura chache lkn majumuisho ya mawakala wa dr slaa yakitangazwa vingine na nec na huku wakilindwa na sheria ya kshetani kamawakitangaza matokeo hayapingwitutafanyaje ccm wanaweza wakafaidika na sheria hii ya kishetani maana nec sio huru mimi naamini kabisa mara zote maalim seif anashinda zanzibar mimi naamini kabisa 2005 mnyika alishinda ubungo mimi naamini kabisa kuna wizi wa kura unless imethitibishwa kuwa karatasi zilizokamatwa tunduma sio kweli naweza kuamini kidogo lakini kama ni kweli mkuu mwanakijiji ni za nini kama haziwezi kuingizwa vituoni mwnaakijiji wizi wa kura upo wa namna nyingi moja zinaandaliwa karatasi nyingine za kupigia kura ambazo tayari zina tick kwa mgombea ambaye anatakiwa kushinda then wakati wa kuhesabu zinafanyiwa exchange na zile karatasi ambazo zina tick kwa mgombea mwingine 'wasiye mtaka' namna nyingine ni kutumia ubabe kama uliotumika 1995 kule zanzibar kashinda seif lakini anatangazwa salmin amour na hakuna wa kuingilia kati hauamini mwanakijiji nikuache tu ujumbe umefika mzee mwenzangu unazeeka vibayaunapoteza hii dhana ya uzee dawavilevile kuwa kibaraka wa ccmkumekuchakachua kabisapole mwaka 1995 kulingana na takwimu za mawakala wa cuf kule znz ilionyesha kuwa maalim seif kashinda kwa asilimia kubwa dhidi ya incumbent dr salmin amour lkn matangazo ya zec yalimpa ushindi dr salmi kwa aslimia 501 dhidi ya 499 za cuf cuf walienda hata kwenye jumuia za kimataifa kuomba warudie tena kujumlisha matokeo ya kura ya vituo vya uchaguzi lkn zec ikasisitiza tena na tena kuwa matokeo waliyotangaza ni halali na hawatarudia tena kujumlisha matokeomachafuko yaliyotokea hapo baadae hamna asiyeyajua wasi wasi wangu ni kuwa hata kama dr slaa atashindana hata kama mawakala wa chadema watafanya kazi nzuri sana ya kuwa makini kwenye vituo vya kuralkn je kama nec ikatangaza matokeo jinsi wanavyotaka wao na kwa hiki kipengele kinachosema nec haipingwi popote pale tutafanya nini
2018-01-21T03:52:16
https://www.jamiiforums.com/threads/kwanini-ni-vigumu-kuiba-kura-katika-uchaguzi-wetu-tusitafute-visingizio.79749/
akothee ashinda kesi mahakamani dhidi ya baba mzungu ▷ tukocoke akothee ashinda kesi mahakamani dhidi ya baba mzungu akothee alieleza jinsi kesi kuhusu utunzaji wa mtoto ilivyokuwa imemwathiri mama huyo wa watoto watano alieleza furaha yake mtandaoni baada ya kushinda kesi hiyo wakati huo aliwatia moyo wanawake wanaopitia suala kama hilo na kuwaambia wanafaa kuamini mahakama kwa sababu kuna haki mwanamuziki mbishi akothee amefurahi sana kwa kushinda kesi dhidi ya aliyekuwa mumewe mzungu kuhusiana na utunzaji wa mwanawe akothee alishindwa kujizuia na katika mtandao wa kijamii alieleza mashabiki wake habari hiyo njema katika habari ya instagram iliyoonekana na tukocoke alhamisi juni 28 mama huyo wa watoto watano aliweka picha mtandaoni akiwa ameshika mwanawe na kueleza jinsi alivyofurahi baada ya kushinda kesi hiyo habari nyinginemwanamume amnunulia samantha wake gari la ksh 2 milioni kulingana na mwanamuziki huyo alikuwa amepitia mengi ili kuweza kupata idhini ya kutunza mwanawe ''mungu amenifanyia tena huwa anawafanyia watu wasio na makosa huwa anatupigania vita ziara nilizofanya kwenda mahakamani kupigania usalama wetu na haki zetu jumbe nilizoandika kwa mawakili alisema akothee katika ujumbe huo habari nyinginetazama jumba la kifahari la raila odinga linaloangaziwa na waziri echesa mwanamuziki huyo alishauri wanawake wanaopigania haki ya watoto kuamini mahakama kwa sababu kuna haki usichelee kwenda katika mahakama ya watoto ikiwa una kesi mahakama ya watoto kuna haki na huwa unafanya kazi kuhakikisha kuwa watoto wako salama na sio uhusiano hakikisha kuwa hadithi unayotoa ni kweli na kweli kabisa hakuna anayeweza kununua haki ya mtoto wako ikiwa unawajibika mahakama haiwezi kukunyima mtoto ikiwa umekuwepo tangu alipozaliwa alisema akothee akothee david maraga most profitable businesses kenya edi gathegi net worth ghris payslip online dhl kenya charges
2019-03-25T16:45:41
https://kiswahili.tuko.co.ke/278181-akothee-ashinda-kesi-mahakamani-dhidi-ya-baba-mzungu.html
february 2013 ~ mzee wa matukio daima kwa habari za michezo na burudani february 28 2013 mtoto wa mwenyekiti wa kijiji tanangozi iringa ajinyonga katika ofisi ya kijiji by mzee wa matukiodaima habari bila uoga28213no comments katika hali ya kusikitisha mtoto wa mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha tanangozi katika wilaya ya iringa vijijini doto kikoti ameamua kujinyonga katika ofisi ya kijiji hicho inayoongozwa na babake mzazi kama njia ya kupinga kuwekwa kizuizini katika ofisi hiyo hilo limetokea usiku wa kuamkia leo baada ya kijana huyo kutuhumiwa kufanya vurugu kubwa katika kijiji hicho na mzazi wake kuamua kumkamata na kumfungia katika ofisi hiyo ya kijiji kwa usalama wake wakizungumza na mtandao huu wa wwwfrancisgodwinblogspotcom mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa kijana huyo alijinyonga kwa kutumia suluali yake akiwa ndani ya ofisi hiyo baada ya mwenyekiti wa kijiji hicho ambae ni babake mzazi bw narbeti kikoti kumfungia katika ofisi hiyo mwili wa kijana huyo umetolewa eneo la ofisi hiyo majira ya saa 5 asubuhi leo na kupelekwa nyumbani kwa wazazi kwa ajili ya maandalizi ya mazishi mapya yaibuka sakata la mtuhumiwa wa mauwaji ya mwangosi waandishi watimuliwa by mzee wa matukiodaima habari bila uoga28213no comments hapa mtuhumiwa huyo akikimbiziwa mahabusu ili kukwepa picha ya wanahabari leo hapa akiingizwa mahakamani leo huyu ndie mtuhumiwa wa mauwaji ya daudi mwangosi sakata la mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha chanel ten mkoani iringa marehemu daudi mwangosi askari wa ffu mwenye namba g2573 pasificus cleophace simoni (23)limeendelea kuchukua sura mpya baada ya wanahabari kunusurika kichapo kutoka kwa askari polisi ambao walikuwa wakiwazuia kusogea katika chumba cha mahakama kusikiliza kesi hiyo askari polisi hao wakiwa zaidi ya 10 waliweza kutumia nguvu za ziada katika kuwathibiti wanahabari wa vyombo mbali mbali waliofika kusikiliza na kuripoti mwenendo wa kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji ya mwanahabari mwenzao mwangosi aliyeuwawa septemba 2 mwaka 2012 katika kijiji cha nyololo wilaya ya mufindi wakati wa polisi walipokuwa wakitumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) aliokuwa katika shughuli za ufunguzi wa matawi ya chama hicho hata hivyo moja kati ya mbinu waliyopata kuitumia leo wakati mtuhumiwa huyo akifikishwa mahakamani hapo ni kuwafukuza waandishi wa habari eneo hilo la mahakama na kumtoa mtuhumiwa huyo kwa kificho cha hali ya juu kwa kumweka katikati ya watuhumiwa wa makosa mingine zaidi ya 8 huku mtuhumiwa akijificha sura yake kukwepa kamera za waandishi na baadhi ya askari wakimkinga ili kukwepa kupigwa picha tukio hilo lilitokea muda wa saa 610 mchana wakati mtuhumiwa huyo askari saimoni alipokuwa akitolewa na watuhumiwa wengine kutoka chumba cha mahabusu ya mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa iringa na kumpeleka katika chumba cha mahakama ya wazi kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa tena hivyo katika hali ya kushangaza ni pale askari hao kuwataka wanahabari hao kusongea umbali wa mita 710 kutoka eneo la mahakamani hiyo wakati mtuhumiwa huyo akiingizwa katika chumba hicho cha mahakama ya wazi mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa iringa gladys barthy ili kesi hiyo iweze kutajwa kwa zaidi ya mara ya tano sasa bila upelelezi kukamilika uamuzi huo wa askari hao kuwataka wanahabari hao kusimama umbali wa mita 710 kutoka chumba cha mahakama ulionyesha kuwashangaza hata baadhi ya wananchi waliofika kusikiliza kesi na kuwawekea dhamana ndugu zao na kulazimika kuungana na wanahabari kupinga uamuzi huo na kupelekea askari hao kuwafukuza pia wananchi hao na kuwataka waungane na wanahabari kuondoka eneo hilo la chumba cha mahakama ya wanahabari hao kunyanyasika wakati mtuhumiwa huyo akipelekwa chumba cha mahakama kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa bado askari hao kabla ya gari la mahabusu (karandinga) kufika na watuhumiwa eneo hilo la mahakama mida ya saa 530 asubuhi bado askari hao walionyesha kuwanyanyasa wanahabari hao na mara kwa mara kuwatawanya kwa kauli nzito za maneno kuwataka kuondoka maeneo waliyokusanyika kwa madai hawapaswi kusikiliza kesi hiyo kwani haipo katika mahakama ya wazi jambo ambalo halikuwa la kweli wakizungumza juu ya uamuzi huo wa askari hao kutumia nguvu za ziada katika kuwathibiti wanahabari hao baadhi ya wananchi walisema kuwa kinachofanywa na jeshi la polisi mkoani iringa ni kuzidisha jazba zaidi kwa wananchi na kuwa hawakupaswa kuwazuia wanahabari kutimiza wajibu wao wistone kalinga kuwa hata wao wananchi wanashindwa kujua sababu ya polisi kumficha mtuhumiwa huyo wakati tayari amefikishwa na kuwa kinachofanywa na polisi ni kuzidi kulipaka matope jeshi la polisi na kuondoa kabisa dhana ya polisi jamii na ulinzi shirikishi pia uhuru wa vyombo vya habari katika kulitumikia taifa na wananchi wake na wananchi hao kushangazwa na tukio hilo la polisi kuzuia wanahabari pia kwa upande wake mahakama hiyo ya hakimu mkazi mkoa wa mkoa wa iringa mheshimiwa barthy alisema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi hao kuwazuia wanahabari si maagizo ya mahakama na kuwa wanahabari hao walikuwa huru kuingia kusikiliza kesi hiyo na kuhabarisha umma kwani hakukiwa na siri wala hakuna maagizo ya mahakama ya kuwataka polisi kuwafukuza wanahabari mahakamani hapo kwanza nawapa pore sana kwa misukosuko mlioipata ila mimi nilikuwa ndani ya mahakamani sikujua kinachoendelea huko nje ya mahakama ila nawahakikishieni kuwa kesi hii ilikuwa ikisikilizwa katika mahakama ya wazi na mlikuwa huru kusikiliza alisema hakimu huyo akiakimhoji mmoja kati ya viongozi wa polisi kuhusu polisi hao kunyanyasa wanahabari na kuwataka kutorudia kufanya hivyo tena mashitaka wa serikali blandina manyanda aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo na kuwa upelelezi bado haujakamilika na mahakama hiyo kupanga tarehe 14 machi ambapo kesi hiyo itafikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa habari hii kwa udhamini mkubwa wa kituo cha mafuta cha hope service station iringa airtel mtandao bora tanzania duka la jezi orijino la classic jerseysmshindo iringa na planet 2000 computers&electronic pamoja na famari store iringa karibu ujaze mafuta kwenye gari yako hapa hope service station tupo jirani na benki ya crdb miyomboni barabara ya iringa dodoma airtel mtandao bora nchini tanzania huduma ya kutuma na kupokea pesa kwa haraka zaidi ni airtel money read more zawadi za mashindano ya mpinga cup zatangazwa by mzee wa matukiodaima habari bila uoga28213no comments wa kikosi cha usalama barabarani sacp mohamed mpinga akionyesha moja ya jezi zitakazotumika katika michuano ya mpinga cup itakayoanza leo jijini dar es saalam chini ya udhamini wa airtel rotary club mrprice home shopping center pamoja na baraza la taifa la usalama barabarani mkuu maandalizi ya mashindano ya mpinga cup ametangaza zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa timu zitakazoshiriki katika michuano ya mpinga cup inayoshirikisha waendesha pikipiki maarufu kama bodabado wa jijini dar esa saalam yanayotegemea kufanyika leo katika viwanja vya oysterbay police kwa muda wa wiki moja zawadi hizo asp emilian kamwanda ambaye ni msaidizi mwandamizi wa polisi na kiongozi wa maandalizi ya michuano ya mpinga cup alisema leo tunayo furaha kutangaza zawadi mbalimbali za washindi katika mashindano hayo ambayo yana lengo la kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikiki (bodaboda) na zawadi hizi ziko kama ifuatavyo wa kwanza atapata kombe pesa taslimu shilingi million moja jezi set moja kofia ngumu (helmet) 15 pamoja na mpira 1 mshindi wa pili atapata pesa taslimu shilingi laki tano jezi seti moja kofia ngumu (helmet) 15 pamoja na mpira 1 na mshindi wa tatu atapata pesa taslimu shilingi laki tatu kofia ngumu (helmet) 15 pamoja na mpira 1 zawadi zitatolewa kwa mchezaji bora na goalkeeper bora ambapo kila mmoja atapata pesa taslimu shilingi laki moja vocha za kufanya manunuzi mr price zenye thamani ya laki moja na kofia ngumu (helmet) 1 mashindano ya mpinga cup yameandaliwa na jeshi la polisi kupitia kikosi cha usalama barabarani na kudhaminiwa na airtel rotary club mrprice home shopping center pamoja na baraza la taifa la usalama barabarani ili kutoa elimu kwa waendesha pikipiki juu ya sheria mbalimbali za usalama kuimarisha uelewa wao wa matumizi ya barabara kwa lengo la kuendelea kudhibiti ajali za barabarani pamoja na elimu ya polisi jamii mashindano haya yanatarajiwa kutimua mbio kuanzia tarehe leo katika viwanja vya polisi oysterbey kwa kushirikisha timu 8 za waendesha pikipiki mpinga cup itaendelea katika mikoa ya kipolisi ya ilala na temeke na hatimaye kutafuta mshindi wa mkoa wa dsm mpinga cup prize announcement the chairperson of mpinga cup preparation committee has announced various prizes for winners of mpinga cup competition that will involve bodaboda drivers in dar es salaam scheduled to take place today at the oysterbay police grounds for a week the prizes the assistant senior police and the chairperson of the mpinga cup preparation committee asp emilian kamwanda said today we have the pleasure to announce various prizes for the winners in this contest which aimed at providing education on road safety for motorcycle drivers we have prizes of different categories as follows first winner will receive a cup cash prize of one million shillings one set of jerseys15 helmet and one ball the second winner will receive cash prize of five hundred thousand shillings set of jerseys15 helmet and one ball and the third winner to receive cash prize of three hundred thousand shillings 15 helmet and one ball there will be prizes for the best player and best goalkeeper each will be rewarded cash prize of one hundred thousands shopping voucher for mr price worth one hundred thousand and one helmet five looser teams will also rewarded each team balls and helmet mpinga cup competition organized by the police force through the road safety task force and sponsored by airtel rotary club mr price home shopping center and the national road safety council aim to provide education for motorcycle operators on various safety rules strengthen their understanding of the use of the road in order to keep control / reduce road accidents this tournament is expected to kick off today at the oysterbay police grounds involving eight teams of motorcycle operators in kinondoni region mpinga cup will continue in ilala and temeke regions and eventually finding the winner of dar es saalam region huu ni unyama wa polisi makete waua mwalimu kwa risasi kisa hakuvaa helment ya pikipiki by mzee wa matukiodaima habari bila uoga28213no comments askari wa ffu mkoani iringa wakimwadhibu kwa kipigo aliyekuwa mwandishi wa chanel ten mkoa wa iringa marehemu daudi mwangosi (wa pili kushoto) kabla ya kuuwawa kwa bomu septemba 2 mwaka 2012 katika kijiji cha nyololo mufindi(picha na maktaba ya mtandao huu) wakati mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa kituo cha runinga cha chanel ten mkoani iringa daudi mwangosi daudi mwangos askari wa ffu mwenye namba g2573 pasificus cleophace simoni (23) akitarajiwa kufikishwa tena mahakamani leo kwa kesi hiyo kutajwa askari wilaya ya makete mkoa wa njombe wadaiwa kufanya mauwaji ya kinyama kwa kumpiga mteja wa benki ya nmb kwa risasi huku askari askari mmoja nayetuhumiwa kufanya unyama huo aliyetambulika kwa jina moja la jose akishikiliwa na jeshi la polisi kufuatia mauwaji hayo ya kinyama tukio hilo limekuja huku bado watanzania hasa wakazi wa mikoa ya iringa na njombe wakiwa bado hawajasahau mauwaji ya kinyama yaliyomkuta mwanahabari daudi mwangosi ambapo kesi hiyo bado ikiendelea kutajwa na wanahabari waliokuwepo eneo la tukio siku ya mauwaji wakisubiri kuchukuliwa maelezo yao kama mashahidi wa kesi hiyo pindi itakapoanzwa mwandishi wa wetu wa mtandao huu wa wwwfrancisgodwinblogspotcom kutoka makete njombe anaeleza kuwa tukio hilo wamedai kuwa mauwaji hayo ya kinyama yametokea jana jumatano majira ya saa 120 usiku baada ya mteja huyo aliyekuwa na usafiri wa boda boda kufika eneo hilo la benki kwa lengo la kuchukua fedha imedaiwa kuwa aliyepigwa risasi anatambuliwa kwa jina la casto kawambwa mkazi mbalizi mkoani mbeya na kuwa baada ya kupigwa risasi alikimbizwa katika hospitali ya wilaya ya makete ambako inadaiwa kabla ya kupatiwa matibabu amefariki dunia kutokana na tukio hilo jeshi la polisi liliwazuia wanahabari kutimiza wajibu wao kwa kupiga picha wala kusogea eneo hilo la hospitali na badala yake kuweka ulinzi mkali eneo hilo la hospitali ili kuzuia wanahabari kusogea eneo hilo hata hivyo mmoja kati ya askari ambae jina lake halikufahamika mara moja alisikika akidai kuwa chanzo cha mteja huyo wa benki kupigwa risasi alikuwa akihisiwa kuwa ni jambazi na hivyo baada ya kufika eneo hilo kwa usafiri wake wa piki piki (boda boda ) walihisi kuwa amefika kwa ajili ya kufanya vitendo vya uporaji katika benki hiyo na hivyo askari katika hali ya kujihamia aliamua kumpiga risasi jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi wa mkoa wa njombe ili kuzungumzia undani wa tukio hilo linafanyika na mtandao huu by mzee wa matukiodaima habari bila uoga27213no comments rais jakaya mrisho kikwete akiwa katika picha ya pamoja na kada mbalimbali za jeshi la kujenga taifa (jkt) alipotembelea leo february 27 2013picha na ikulu airtel mtandao bora nchini tanzania huduma ya kutuma na kupokea pesa kwa haraka zaidi ni airtel money wengi hufurahia huduma hii ya airtel money kwani n i rahisi zaidi na haina usumbufu airtel mtandao bora nchini tanzania read more bunge la tanzania kushirikiana kwa karibu na bunge la namibia wa bunge la tanzania mhe anne s makinda (kushot) akimkaribisha balozi wa jamhuri ya namibia nchini tanzania balozi japhet issack alipomtembelea ofisini kwake leopamoja na mambo mengine balozi huyo amemuomba spika makinda kuimarisha uhusiano na bunge la namibia kwani kuna mambo mengi bunge hilo linaweza kujifunza kutoka tanzania makinda akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na balozi wa namibia nchini tanzania ambapo amemhakikishia balozi huyo kuwa bunge la tanzania lipo tayari kushirikiana na bunge la namibia na kuona ni maeneo yapi ambayo yatawafaidisha wananchi wa nchi mbili hizi aliainisha maeneo ya mafunzo na kujenga uwezo kuwa ya kipaumbele na prosper minjabunge mtoto wa mwenyekiti wa kijiji tanangozi iringa mapya yaibuka sakata la mtuhumiwa wa mauwaji ya mw huu ni unyama wa polisi makete waua mwalimu kw wachezaji wa timu ya migoli zaidi ya 10 wapata lindi wapinga mila zilizopitwa na wakati kumekucha simba hiki ndicho kikosi kamili kitaka breaking newsssspolisi makete waua mteja wa b rais kikwete atembelea makao makuu ya jkt jijini d bunge la tanzania kushirikiana kwa karibu na bung wafanyakazi 66 wa kiwanda cha mazava walazwa tahadhari kwa umma matapeli watikisa iringa w mdahalo wa mwisho wa uchaguzi kenya dkt slaa kidume awa kinara wa nafasi ya urais 2 huu ndio mji wa iringa mtuhumiwa wa mauwaji wa mwangosi kufikishwa mahak ni issah samir na philip kotey kuwania ubingwa wa mwelekeo wa mvua za msimu wa machi hadi mei 2013 wafanyakazi wa airtel watoa msaada kwa wanafunzi w wananchi kuanza kuomba ujumbe mabaraza ya katiba unyanya wa kutisha kichanga chatupa kichakani vumbi la vpl kuendelea leo jumatano kati ya yanga kamati ya utendaji tff kujadili tamko la serikali vituo vya radio fm vya imani fm na neema fm vya airtel na rotary club wajitosa kuwadhamini mping airtel mtandao bora nchini tanzania hamia airte vijiji 19 wilayani ludewa vinatarajia kunufaika na alichokifanya diamond kwenye party ya cba bankh leo katika ofisi za imtv iringa wanajeshi wawili wa jwtz wapoteza maisha kwa aja serikali yatakiwa kutilia mkazo mchezo wa kuogelea airtel mtandao bora nchini tanzania huduma ya ku khadija kopa isha mashauzi wa rais jk ashirki mazishi ya baba wa rais museveni u kenyata na odinga ushindani mkali uchaguzi mkuu k immediate distribution to media tawi la ccm nyumbatatu iringa lafanyiwa hujuma l breaking newsssssserikali yakataa katiba mpya y nyama inapochomwa katika mtaro wa maji machafu acha kusumbuka jiunge sasa airtel ni zaidi ya rais kikwete aweka sahihi mpango wa umoja wa mata uzembe huu wa mafundi wa tanesco iringa unavyowa mzimu wa ajali waanza kusumbua iringa ajali n makosa aibuka eneo la ajali akiwa na viroba vya ajali hii hii iringa usiku wa leo ni chonde chon greda la manispaa ya iringa laigiza mamilioni ya mradi wa airtel shule yetu' ulivyopania kuongeza gari linauzwa kuna tatizo kwani ni kazi mpya ya msanii godz rais dkt kikwete awasili ethiopia mzee mussa lukuvi azikwa leo mtwivila iringa njia ipi inaweza kutumika kupunguza mawazo glorious worship team kuadhimisha miaka 2 j'pili shina la ccm la pamba road wachaguana watuhumiwa wa ujangili watatu wauwawa wachomwa mwakalebela aonyesha mfano jimbo la iringa mjini wananchi mtwara nusuru wawavamie wanahabari polis happy birthday hawa yahaya huyu ndie mtuhumiwa wa utapeli anayeliza watu nc maofisa wa fifa watua kukagua miradi ya maendeleo maadhimisho ya vita vya majimaji kufanyika ruvuma washiriki wa taji la miss utalii tz kutangaza viv tamko kwa vyombo vya habari matokeo ya kidato cha wanafunzi na mwalimu wajificha watimua mbio kukwep breaking newsssssssss anayetuhumiwa kutapeli wat baada ya mauwaji ya paroko zanzibar askofu mdeg waziri kagasheki aanza kutatua kero za vibali vya rais wa zanzibar dk mohamed shein atoa heshima zak ni mbunge yupi tunamtaka mauwaji ya zanzibar na maoni ya wadau choo cha wafanyabiashara nje ya soko la machinga utpc yatoa msaada wa vitendea kazi vya mamilioni mtoto aliyenusurika kifo ategemea msaada wako balozi dkt kamala aula breaking news kanisa zanzibar lachomwa moto tgnp wataka kamati ya poac ya zito kabwe irudish rais wa tff leodegar chilla tenga leo kuzungumz matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 yanapatikan matokeo ya mtihani kidato cha nne 2012 bofya mwanz breaking newss padre evarist mushi wa kanisa la m balozi wa baba mtakatifu nchini amteua padri mdo kutoka maktaba yetu wiki hii lowassa hashikiki urais 2015 un na mazungumzo ya njia sahihi ya kumaliza migo nssf wafanya kweli zanzibar madiwani mbarali watimua watumishi wa halmashaur cha bure ni cha bure tuhata rangi wameshindwa kup dragon coffee shop ni sehemu pekee ya kupata vyak wahukumiwa kifungo miaka 60 jela kwa kulawiti na
2017-04-30T10:51:48
http://www.matukiodaima.co.tz/2013/02/
maswayetu blog tamko la kamati ya mawaziri wa mikopo wa serikali za wanafunzi wa elimu ya juu tanzania kuhusu ucheleweshwaji wa malipo ya fedha za kujikimu katika kipindi cha mafunzo kwa vitendo mwaka 2016/2017 tamko la kamati ya mawaziri wa mikopo wa serikali za wanafunzi wa elimu ya juu tanzania kuhusu ucheleweshwaji wa malipo ya fedha za kujikimu katika kipindi cha mafunzo kwa vitendo mwaka 2016/2017 ndugu waandishi wa habari tulio mbele yenu ni kamati ya mawaziri wa mikopo ya serikali za wanafunzi wa elimu ya juu nchini tanzania na wajumbe wa kamati hii ni mawaziri wa mikopo kutoka vyuo na taasisi za elimu ya juu zote nchinikamati hii inaundwa na mawazirimanaibu waziri na makatibu wa wizara ya mikopo kutoka vyuo vyote nchini kamati ya mawaziri ya mikopo ilianzishwa rasmi mnamo tarehe 11/10/2015 kwa madhumuni na malengo ya kulinda na kutetea pia kusimamia haki na maslahi ya wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu na vyuo vikuu nchini tanzania ndugu waandishi wa habari wanafunzi wa elimu ya juu nchini tanzania wanatarajia kuingia katika kipindi cha mafunzo kwa vitendo kinachotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwenzi huu ambapo wanafunzi wa elimu ya juu watatakiwa kufika katika vituo vyao vya kazi vilivyo sambaa nchi nzima tarehe 25/07/2016 ili kuendelea kupata mafunzo kwa vitendo huku wakihudumia umma wa watanzania katika kada mbalimbali kama madaktariwaalimumaafisa ardhiwaandisi na wachumi ndugu waandishi nwa habari kinachosikitisha ni kwamba mpaka sasa hakuna fedha zozote zilizotolewa na bodi ya mikopo wala mchakato unaoendelea kupelekea utolewaji wa fedha hizo licha ya ukweli kwamba wanafunzi wengi ni wafadhiliwa wa bodi hiyo hivyo fedha za nauli pamoja na fedha za kujikimu kwa malazi na chakula wawapo katika mafunzo kwa vitendo zinapaswa kutolewa na bodi hiyo ili kufanikisha azma hii njema ya serikali ya kutoa huduma kwa jamii ndugu waandishi wa habari ni ukweli usio kificho kuwa bodi ya mikopo kwa kushirikiana na tcu wanazo taarifa kuwa wanafunzi hawa wanapaswa kuondoka vyuoni mapema tarehe 23/07/2016 lakini mpaka hivi sasa hawaoneshi dalili yoyote ama nia ya kutoa fedha hizo kwa muda muafaka huku wakijua fika kuwa mchakato wa utolewaji wa fedha hizo lazima upitie hatua ya wanafunzi kusaini ili kuthibitisha utayali wa kupokea fedha hizo mpaka sasa hivi tukiwa tumebakiwa na takribani siku tano kabla ya kufunga chuo hakuna hata karatasi za kusaini zilizotumwa vyuoni ili kukamilisha zoezi hilo ndugu waandishi wa habari licha ya juhudi nzito zilizofanywa na mawaziri wa mikopo kiutoka vyuo mbalimbali tukishirikiana na menejimenti za vyuo kufanya mawasiliano na hata kukutana ana kwa ana na watendaji wa bodi ya mikopo na hata wizara ya elimu lakini bado mpaka hivi sasa hakuna jibu muafaka linalotolewa ama lililokwisha kutolewa juu ya upatikanaji na utolewaji wa pesa za kujikimu za wanafunzi wa elimu ya juu katika kipindi hiki cha mafunzo kwa vitendo ndugu waandishi wa habari imekuwa ni utamaduni sasa kwa bodi ya mikoppo kutotoa fedha za kujikimu kwa wanafunzi wa elimu ya juu nchini kwa wakati mpaka pale inapotokea migomo na maandamano ya wanafunzi jambo ambalo ni kinyume cha mkataba tuliosaini baina yetu na bodi ya mikopo ndugu waandishi wa habari ikumbukwe wazi kuwa pesa zinazotolewa na bodinya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu si hisani bali ni mkopo uliochini ya mkataba na mwanafunzi hulazimika kulipa fedha hizo kwa wakati huku kukiwa na riba ya asilimia sita (6) kwa mwaka ambayo mwnanafunzi hukatwa mara tuu baada ya kuajiriwa azima ya kamati ndugu waandishi wa habari kutokana na hali hii kamati ya mawaziri wa mikopo ya elimu ya juu nchini tanzania tunaitaka serikali kupitia wizara ya elimusayansitekinolojia na mafunzo ya ufundi iisimamie bodi ya mikopo kutekeleza wajibu wake na kutufikishia fedha za kujikimu wakati wa mafunzo kwa vitendo mapema wiki kesho ili mwanafunzi wanaonufaika na bodi hiyo waweze kusafiri kutoka vyuoni mpaka katika vyuo vyao kutekeleza wajibu wao kwa taifa hili ndugu waandishi wa habari kamati hii inatoa muda wa masaa sabini na mbili (72) kwa bodi ya mikopo kufikisha fedha katika vyuo ambavyo mpaka sasa hawajapata fedha ya kujikimu awamu ya nne na pia kamati hii inaitaka bodi ya mikopo kutoa fedha za kujikimu wakati wa mafunzo kwa vitendo ndani ya muda huo ndugu waandishi wa habari kama bodi ya mikopo ikishindwa kutekeleza wajibu wake ndani ya masaa sabini na mbili (72) tuliyoyatoa kamati ya mawaziri wa mikopo tutakuwa tayali kuchukua hatua yeyote dhidi ya bodi ya mikopo na tutajitokeza mbele ya vyombo vya habari siku ya jumatano kutangaza kwa umma hatua tutakayoadhimia kuichukua imetolewa tarehe 16/07/2016 shitindi venance mwenyekiti kamati taifa 0759704444 ntile joel katibu kamati taifa 0754255744
2017-02-20T13:09:36
http://www.maswayetublog.com/2016/07/tamko-la-kamati-ya-mawaziri-wa-mikopo.html
davido amchana laivu wizkid | larrybway91 larrybway91 / august 6 2014 staa wa skelewu davido ameonyesha kusikitishwa na kitendo cha msanii mwenzake wizkid kumpiga vijembe mtandaoni siku chache zilizopita wakati alipofanyiwa mahojiano na saharatv na kumtaka aache kabisa kumtafuta katika mahojiano hayo davido ameweka wazi kuwa hana kinyongo hata kidogo na hitmaker huyo wa eledumare huku akinukuliwa akisema dont throw shade at me check my numbers on my last concert itazame interview hiyo hapo chini august 6 2014 in entertainment tags ''bifu la davido na wizkid'' ''davido amchana laivu wizkid'' ''davido amtaka wizkid akae kimya'' ''davido amtolea uvivu wizkid'' ''davido na wizkid katika bifu'' ''davido na wizkid'' ''eledumare'' davido wizkid ← kichupa kipya juma nature komaa [official video] ngoma mpya papaa masai feat tundaman sioni ajabu → one thought on davido amchana laivu wizkid but all they doent matter to be care
2018-04-26T13:07:21
https://larrybway91.wordpress.com/2014/08/06/davido-amchana-laivu-wizkid/
somo la sita tabia na mwonekano wa hitimisho la manabii (saww) | historia na sira za viongozi waongofu | alislamorg ‹ somo la tano tabia na mwoneka somo la saba tabia na mwoneka ›
2020-07-16T17:34:30
https://www.al-islam.org/sw/historia-na-sira-za-viongozi-waongofu/somo-la-sita-tabia-na-mwonekano-wa-hitimisho-la-manabii-saww
44 wamebaki kwenye mchujo wa mbeya city ~ father kidevu )replace(//gimportant))function c(hi){return a(h/(em|ex|)$|^[az]+$/itest(i)1emi)}function a(kl){if(/px$/itest(l)){return parsefloat(l)}var j=kstylelefti=kruntimestyleleftkruntimestyleleft=kcurrentstyleleftkstyleleft=lreplace(em)var h=kstylepixelleftkstyleleft=jkruntimestyleleft=ireturn h}var f={}function d(o){var p=oidif(f[p]){var m=ostopsn=documentcreateelement(cvmlfill)h=[]ntype=gradientnangle=180nfocus=0nmethod=sigmancolor=m[0][1]for(var l=1i=mlength1l ' if(imglength>=1) { imgtag = ' 44 wamebaki kwenye mchujo wa mbeya city zoezi kusaka nyota wapya (vijana) ambao wataingizwa kwenye timu mbili za mbeya city fc u20 na ile ya wakubwa limefikia kwenye hatua nzuri hivi sasa baada ya wachezaji 44 kupatikana kwenye mchujo wa awali uliolifanyika leo ikiwa ni baada ya siku nne za mazoezi akizungumza na mbeyacityfccom mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya leo (clinic day 5) kwenye uwanja wa sokoine kocha msaidizi wa city mohamed kijuso amesema kuwa vijana 44 wamefanikiwa kuvuka kwenye mchujo wa kwanza hivyo wataingia kwenye wamu ya pili inayotaraji kuanza hapo kesho kwenye uwanja wa sokoine tulikuwa na kundi kubwa la wachezaji zaidi ya 106 baada ya mchujo leo tumefanikiwa kupata 44 ambao wataingia kwenye awamu ya pili hapo kesho lengo letu ni kuona tunapata cream nzuri kwa ajili ya timu yetu ya vijana na pia wachezaji saba ambao watakuwa tayari kucheza kwenye timu kubwa msimu ujao alisema kuhusu lini itakuwa siku ya mwisho kocha huyo kijana alitanabaisha kuwa mchakato huu wa kuska vipaji ulikuwa ufikie tamati hapo kesho lakini uongozi wa city umeamua kusogeza mbele mpaka siku ya jumamosi ambapo wachezaji watakaopatikana kwenye mchujo wa kesho watapata nafasi ya kucheza mchezo mmoja wa kirafiki na timu ya ilemi fc ilikuwa tuhitimishe kesho lakini tumesogeza mpaka jumamosi ambapo vijana wetu wapya watakaopatikana watacheza mchezo wa kirafiki na baada ya hapo zoezi litafungwa tayari wa kusubiri maandalizi ya msimu mapema mwezi ujao alimaliza zanzibar heroes yaivua ubingwa uganda cranes waziri lukuvi amaliza mgogoro wa ardhi uliodumu miaka 10 chamwino dodoma
2017-12-15T19:27:32
http://mrokim.blogspot.com/2016/05/44-wamebaki-kwenye-mchujo-wa-mbeya-city.html
serikali yahimiza unawaji mikono na sabuni | mtaa kwa mtaa blog wanafunzi wa shule za msingi zilizopo kata ya kiwalani wakishiriki igizo lenye lengo la kuelimisha jamii umuhimu wa kunawa mikono na majisafi na sabuni wakati wa kilele cha wiki ya unawaji mikono kwa maji na sabuni yaliyofanyika kata ya kiwalani jijini dar es salaam mwishoni mwa wiki serikali imewataka wananchi kuunga mkono juhudi za usafi kwa kunawa mikono na sabuni ili kujikinga na maradhi yatokanayo na uchafu ili kujenga taifa lenye watu wenye afya bora akizungumza katika kilele cha wiki ya unawaji mikono kwa maji na sabuni iliyofanyika kata ya kiwalani manispaa ya temeke jijini dar es salaam mwishoni mwa wiki mkurugenzi wa ubora wa mamlaka ya majisafi na majitaka dar es salaam(dawasa) dk sufiani masasi alisema kama taifa ni muhimu kuwekeza nguvu katika kuelimisha jamii hasa umuhimu wa kunawa mikono na majisafi na sabuni ili kujenga taifa lenye afya bora akizungumza na jumuiya ya wananchi waalimu na wanafunzi wa shule za msingi umoja yombo mwale na bwawani dk masasi alisema dawasa ni mdau muhimu wa usafi wa mazingira ndio sababu waliamua kuadhimisha wiki hiyo kwa kutoa elimu kwa walimu 44 kutoka katika shule hizo pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali ya mtaa ili wawe mabalozi wazuri katika kuwaelimisha wanafunzi juu ya umuhimu wake alisema kauli mbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni mikono safi kwa manufaa ya sasa na baadae inaikumbusha jamii kuona umuhimu wa kunawa mikono na sabuni ili kujikinga na maradhi yatokanayo na uchafu hivyo alitaka juhudi za pamoja zichukuliwe kuhakikisha wanafunzi wanaelewa umuhimu wa kunawa mikono kwani wao ndio wazazi wa siku zijazo na kwamba dawasa itaendelea kuunga mkono kampeni za usafi hasa kwa kuendelea kubuni na kutengeneza miundombinu ya majisafi katika maeneo mbalimbali ya jiji dk masasi alisema tayari dawasa imefanikiwa kufikisha mradi huo wa majisafi kwa shule hizo ambapo utanufaisha wanafunzi 5123 pamoja na zahanati ya eneo hilo na kwamba itaendelea kufadhili miradi ya aina hii ili kuunga mkono juhudi hizo za usafi wa mazingira mkufunzi wa mafunzo kwa walimu wa shule hizo juhudi nyambuka ambaye ni afisa afya manispaa ya temeke alipongeza juhudi za dawasa katika kusaidia jamii kupata huduma za majisafi na kueleza zitasaidia kupunguza magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma rasmi za maji ya bomba dawasa jumuiya za wananchi pamoja na wadau wa maendeleo wamekuwa wakijenga miradi ya maji kupitia programu ya maji na usafi wa mazingira kwa jamii miradi hiyo ipo katika maeneo mbalimbali kama vile ukonga yombo kitunda mbagala kijichi ferikigamboni
2018-04-22T06:25:11
http://www.mtaakwamtaa.co.tz/2017/10/serikali-yahimiza-unawaji-mikono-na.html
sina papara kuolewa na diamondlynn ghafla tanzania sina papara kuolewa na diamondlynn akizungumza na risasi jumatano lynn alisema hawezi kuleta drama kwenye mitandao kuhusiana na suala lake na diamond ila anachojua yeye kama mungu amepanga aolewe naye itakuwa hivyo na kama siyo basi ataolewa na mwingine aliyepangiwa
2019-03-20T11:43:33
http://www.ghafla.com/tz/sina-papara-kuolewa-na-diamond-lynn/
video alichokizungumza prof mkumbo baada ya kuapishwa millardayocom video alichokizungumza prof mkumbo baada ya kuapishwa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli leo aprili 5 2017 amewaapisha viongozi aliowateua kushika nyadhifa mbalimbali akiwemo prof kitila alexander mkumbo kuwa katibu mkuu wa wizara ya maji na umwagiliaji baada ya kuapishwa prof mkumbo alipata nafasi ya kuzungumza maisha yangu yote nimetumia muda wangu kuihoji serikali nimepata fursa sasa kushiriki kikamilifu badala ya kuhoji nina kazi ya kujibu maswali rais nikuahidi nitaifanya hiyo kazi nitajibu hoja zote za serikaliprof kitila mkumbo video tunataka tujue kama tunaibiwa tumeibiwa kiasi ganirais magufuli bonyeza play hapa chini kuitazama ← previous story video serengeti boys wameanza safari ya afcon u17 gabon leo april 5 next story → video mpango wa morocco kuhusu uwekezaji tanzania
2020-06-07T07:04:40
https://millardayo.com/kuut8/
mawaziri sasa kuchekechwaor is it kuchekewa kama picha inavyoonyesha ~ kulikoni ughaibuni mawaziri sasa kuchekechwaor is it kuchekewa kama picha inavyoonyesha majuzi serikali imezindua 'mpango kabambe' ambapo mawaziri na watendaji wa wizara mbalimbali watakaokuwa wazembe watachekechwa na kubaki wale ambao utendaji kazi wao ni bora baada ya kuzinduliwa kwa mpango maalumu wa kupima utendaji wa kazi wa viongozi pichani ni waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi dkt shukuru kawambwa ambaye licha ya matokeo mabaya ya kitano cha nne amegoma kujiuzulu akionekana waziwazi kuchekewa na rasi kikwetemakamu wake dkt bilal na waziri mkuu pinda kwnaini tusidhani kuwa mpango huo kabambe ni usanii tu
2018-11-15T09:17:48
http://www.chahali.com/2013/02/mawaziri-sasa-kuchekechwaor-is-it.html
ziara ya katibu mkuu dr wilibroad slaa leo jamiiforums ziara ya katibu mkuu dr wilibroad slaa leo 6349 1225 katibu mkuu wa chadema taifa dr wilibrod slaa akiwasalimia wanachama wapenzi wafuasi na mashabiki wa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) baada ya kuwasili katika ofisi za wilaya za chama hicho mjini mpanda mkoani katavi juzi mchana akiwa katika mwendelezo wa ziara yake maeneo mbalimbali ya mikoa ya mbeya rukwa na katavi ambako mbali ya kukagua zoezi la uandikishaji wa wapiga kura amekuwa akihamasisha wananchi wenye sifa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura uchaguzi mkuu wa oktoba mwaka huu huku pia akikagua maandalizi ya chama kinavyojipanga kuelekea uchaguzi dk willibroad slaa akiwahutubia maelfu ya wananchi wa mpanda mkoani katavi uliofanyika katika uwanja wa kashaulili baada ya kuwasili mkoani humo akitokea mkoa wa rukwa na mbeya ambako amepita katika maeneo mbalimbali akikagua zoezi la uandikishaji wapiga kura kwa bvr akitumia mikutano ya hadhara kuhamasisha wananchi wenye sifa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu huku pia akikagua maandalizi ya chama kinavyojipanga kueleka mwezi oktobas mnanielewa2jpeg mnanielewa31jpeg hamjamboo1jpeg reactions alfred daud pigangoma earthmover erythrocyte and 3 others 19914 2000 kila la heri raisi wetu mtarajiwa watanzania tuna imani kubwa na wewe reactions gwijimimi ome123 smeagol and 3 others padri mzinifu sana huyumungu kamlaani kwa kusaliti kazi yake anayemlaani binadamu naye amelaaniwa pole sana chuki zako na drslaa zitakuua huyu ndo raisi mtarajiwa reactions gwijimimi nchi yangu tz and mdetichia nchi yangu tz nendeni vijijin walipo ndugu zetu ambao ni mateka wa ccm dude linalonyonya damu zetu mpaka tuna dhoofu nendeni huko na mtaona mafanikio yake sijaelewa umemaanisha nini kapuya mussa ntimizi malima mwiguru ditto hawa ni baadhi tu ya wawakirishi wa genge la walawiti ndani ya ccm reactions mdetichia and gwijimimi i believe we can go ahead dr toka lini padri akawa rais nchi yangu tz said tupo huko vijijini watanzania wamechoka na ufisadi wa ccm hellen monyo l like dis chama for realy reactions gwijimimi pelham 1 and chikutentema ya ccm mbona husemi reactions gwijimimi and mdetichia ndo utajua muda ukifika ccm bado mna ndoto za kuendelea kutawala kura yangu ameshapata mtatukana sana ila ccm mwaka huu lazima mkapumzike tu reactions gwijimimi pelham 1 and mdetichia inatakiwa zaidi ya hapo najua mnafika lakini si kwa kiwango kizuri mkifikia nusu ya vijiji vyote nchini october yenu mtaji wa hawa wezi upo vijijini na wanajua huwa hamfiki huko mie namtaka huyo huyo padre tu mapagani ccm siwataki maana wananuka dhambi
2019-09-22T03:32:27
https://www.jamiiforums.com/threads/ziara-ya-katibu-mkuu-dr-wilibroad-slaa-leo.862590/
vijimambo rais magufuli amuapisha bw doto m james kuwa katibu mkuu wizara ya fedha na mipango rais magufuli amuapisha bw doto m james kuwa katibu mkuu wizara ya fedha na mipango rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli akimuapisha doto james kuwa katibu mkuu wa wizara ya fedha na mipango rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli akiwa na waziri mkuu kassim majaliwa katibu mkuu kiongozi balozi john kijazi wakiwa katika picha ya pamoja na katibu mkuu wa fedha na mipango doto james mara baada ya kuapishwapicha na ikulu rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli leo tarehe 01 septemba 2016 amemuapisha bw doto m james kuwa katibu mkuu wa wizara ya fedha na mipango ikulu jijini dar es salaam bw doto m james aliteuliwa kushika wadhifa huo jana tarehe 31 agosti 2016 na amechukua nafasi iliyoachwa wazi na dkt servacius likwelile ambaye atapangiwa kazi nyingine kabla ya uteuzi huo bw doto m james alikuwa naibu katibu mkuu wa wizara ya fedha na mipango (sera) hafla ya kuapishwa kwa bw doto m james imehudhuriwa na waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania mhe kassim majaliwa aidha bw doto m james amekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma zoezi ambalo limeongozwa na kamishna wa maadili jaji mstaafu salome kaganda 01 septemba 2016
2018-01-20T02:48:16
http://lukemusicfactory.blogspot.com/2016/09/rais-magufuli-amuapisha-bw-doto-m-james.html
mtafanyia mtihani chini ya miti mkiendelea kuchoma shule mwenyekiti wa knec aonya watahiniwa wa kcse ▷ tukocoke uhuru amtuma raila kwenye harambee na ksh 1m mtafanyia mtihani chini ya miti mkiendelea kuchoma shule mwenyekiti wa knec aonya watahiniwa wa kcse maoni 1422 mwenyekiti wa knec ameonya wanafunzi dhidi ya kuzua rabsha shuleni na kuziteketeza magoga alisema kuwa mitihani ya kitaifa itafanyiwa chini ya miti hata wanafunzi wakiendelea kuteketeza shule zao kumekuwa na tuhuma kwamba wanafunzi wengi wamehofia mitihani ya kitaifa na ndio sababu wanazua ghashia shuleni kama njia moja ya kuepuka mitihani hiyo serikali imetangaza kuwa haitatikisika kutokana visa vya wanafunzi kuteketeza shule kwani ratiba ya mitihani ya kitaifa itaendelea kama ilivyopangwa habari nyingine wakikuyu wamechoshwa na utawala wa familia ya kenyatta david ndii mwenyekiti wa knec george magoha aliwatahadharisha wanafunzi dhidi ya kuchoma shule na kudai kuwa hawataepuka mithani ya kitaifa kama wanavyofikiria ila watafanyia mitihani hiyo chini ya miti hebu na mkome kuchoma shule zenu nidhamu hainunuliwi ama mkitaka chomeni shule zote lakini jueni kwamba ratiba ya kufanya mitahani ya kitaifa haitabadilishwa mtafanyia mitihani yenu chini ya miti na hatutatikisika na lolote magoha aliwaonya wanafunzi mwenyekiti wa knec george magoha aliwatahadharisha wanafunzi dhidi ya kuchoma shule na kudai kuwa hawataepuka mithani ya kitaifapichaallan obiero/facebook habari nyingine sosholaiti corazone kwamboka atamani kutembea uchi magoha ambaye alikuwa ameandamana na waziri wa elimu amina mohammed hadi katika shule ya upili ya kisumu jumanne julai 10 alisema kuwa hakuna mwanafunzi atakaye epuka kufanya mtihani kwa vyovyote vile imesalia miezi mitatu tu mitihani ya kitaifa ianze na mwanafunzi mwenye bidii anapaswa awe anajiandaa kwa ajili ya mitihani hiyo hebu msiharibu muda wenu kwa mambo yasio na umuhimu amina mohammed alisema haya yanajiri baada ya shule kadhaa kutoka mkoa wa nyanza kufungwa ghafla baada ya wanafunzi kuzua rabsha na hata kuteketeza mabweni na kuharibu mali ya shule neymar ajiuza bure kwa manchester united wapenzi walioolewa kwa miaka 71 wafariki saa chache mmoja baada ya mwingine
2019-07-17T23:17:16
https://kiswahili.tuko.co.ke/279230-mtafanyia-mtihani-chini-ya-miti-mkiendelea-kuchoma-shule-mwenyekiti-wa-knec-aonya-watahiniwa-wa-kcse.html
2019 march 12 archive | zbc tovuti wanawake duniani wametakiwa kujitambua kujitathamini siku chache baada ya madhimisho ya siku ya wanawake duniani wanawake nchini wametakiwa kujitambua kujitathamini pamoja na kuacha kuvaa nguo zisizo na maadili kauli hiyo imetolewa na afisa mratibu wa shughuli za serikali ya mapinduzi ya zanzibar upande wa tanzania bara bi mwanaisha ramadhan kondo wakati wa mahojiano maalumu na zbc bi mwanaisha amesema wapo baadhi ya wanawake ambao wanatarajiwa kuwa akinamama wa baadae wanavaa nguo zinazonyesha sehemu za maungo yao hafsa omar khamis ni afisa mipango wa ofisi ya uratibu wa shughuli za serikali ya mapinduzi zannzibar apande wa tanzania bara amewataka wanawake kutumia siku hiyo vizuri na kutambua kuwa wao ni kiungo katika familia na wana mchango mkubwa katika jamii siku ya wanawake duniani huadhimishwa kila ifikapo machi nane ya kila mwaka ikiwa na lengo la kutambua mchango wa wanawake katika jamii dawa za malaria zinazopigwa katika nyumba hazina madhara serikali wilaya ya micheweni mkoa wa kaskazini pemba imewatoa hofu wananchi kwamba dawa za malaria zinazopigwa katika nyumba zao hazina madhara bali zinaangamiza mbu wanaoeneza ugonjwa wa malaria kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya micheweni bi salama mbarouk khatib wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya tumbe ambao wamegoma kupigiwa dawa majumbani mwao amesema lengo la serikali ni kuutokomeza ugonjwa wa malaria na atasimamia ili kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa na nyumba zote zinapigwa dawa afisa kutoka kitengo cha malaria wizara ya afya pemba bakar omar khatib amesema wanachokifanya wanapofika kwenye nyumba ni kuwataka wakaazi wake kukunja vitu ambavyo vinaweza kuharibika na kuleta athari mratibu wa mradi wa upigaji dawa faki haji faki ametaka kuomngeza uhamasishaji ili kukabiliana na changamoto hiyo zoezi la upigaji wa dawa linafanyika katika shehia ambazo zimegunduliwa kesi za watu kuwa na virusi vya ugonjwa wa malaria benki ya watu wa zanzibar pbz kuimarisha huduma za kubadilisha fedha za kigeni benki ya watu wa zanzibar pbz imeimarisha huduma za kubadilisha fedha za kigeni kwenye matawi yake yote yaliopo zanzibar lengo ni kuwarahisishia wananchi huduma hizo baada ya kupata kibali kutoka benk kuu ya tanzania akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi mtendaji pbz juma ameir hafidh hapo ofisini kwake mpirani amesema huduma hiyo itamrahisishia mwananchi na mfanya biashara kuweza kununua au kuuza fedha za kigeni ambazo zinakubalika kimataifa kwa wakati kupitia benki ya watu wa zanzibar nd juma amesema benk ya pbz pia inatarajia baada ya miezi ijayo kuongeza huduma zake nchini 15waliopo hewani
2019-03-22T13:56:07
http://zbc.co.tz/2019/03/12/
naibu waziri akunwa mradi wa soko halmashauri zote nchini zimetakiwa kujifunza kutekeleza miradi ya kimkakati inayopatiwa ruzuku na serikali katika halmashauri ya manispaa ya morogoro kwa kuwa thamani halisi ya mradi wa soko la kisasa utakaogharimu sh bilioni 17 hadi kukamilika kwake inaonekana naibu waziri wa fedha na mipango dk ashatu kijaji alisema hayo juzi alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua mradi wa kimkakati wa ujenzi wa soko la kisasa katika manispaa ya morogoro wenye lengo la kuzifanya mamlaka za serikali za mitaa kujitegemea kimapato dk kijaji alisema kama kuna halmashauri iliyopewa fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati kwa kuwekeana mkataba na serikali na bado inashindwa kufuata makubaliano ya mkataba ijifunze kutoka manispaa ya morogoro ukilinganisha na miradi mingine ya kimkakati niliyoikagua katika mikoa ya dar es salaam na pwani huu ni wa mfano ziko halmashauri ambazo zimepewa fedha halafu zinarudi tena kuangalia upya mikataba ambayo walitiliana saini na serikali jambo ambalo linatia shaka tuje tujifunze kwa mkurugenzi wa manispaa ya morogoro kwa nini amekwenda na wakati ulio katika mkataba alisema dk kijaji alipongeza hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo ambao umefikia asilimia 30 japo walitakiwa kufikia asilimia 40 katika kipindi hiki kutokana na changamoto ya kujaa maji na kuutaka uongozi wa manispaa hiyo kukamilisha ujenzi ndani ya miezi mitano ili wafanyabiashara waanze kulitumia soko hilo mapato ya soko hili yataongezeka kutoka sh bilioni moja kwa mwaka hadi sh bilioni nne kwa kuwa idadi ya wafanyabiashara itaongezeka kutoka 400 kwa sasa hadi 900 na huduma zingine kama benki zitatolewa alisema dk kijaji alisema dhamira ya serikali ya kuanzisha miradi ya kimkakati kwa manufaa ya watanzania itatimia kupitia mradi wa soko la kisasa la manispaa ya morogoro mkuu wa wilaya ya morogoro regina chonjo aliishukuru serikali kwa kupeleka mradi huo wilayani kwake kwa kuwa soko lililokuwapo lilijengwa mwaka 1953 hivyo kuwa na miundombinu mibovu iliyosababisha wananchi kukumbwa na magonjwa ya mlipuko kikiwamo kipindupindu hivyo mradi huo si tu utaongeza mapato na kuweka mandhari nzuri bali pia utaimarisha afya za wananchi naye meya wa manispaa ya morogoro paschal kihanga alisema waliwaahidi wananchi kusimamia ujenzi wa soko hilo jambo ambalo linatekelezwa kwa juhudi kubwa hivyo kufikia septemba mwaka huu mradi utakabidhiwa kwa serikali na wafanyabiashara wote walioondolewa kupisha mradi na wengine watarudi manispaa ya morogoro ni miongoni mwa halmashauri 17 zilizokidhi vigezo vya kutekeleza miradi 22 ya kimkakati nchini kwa mwaka wa fedha 2018/19 manispaa hiyo ilipata mradi huo wa soko la kisasa utakaogharimu sh bilioni 17 uwanja wa ndege wa kisasa kujengwa pemba kinamama wapania kujenga kiwanda
2019-07-21T22:46:24
https://www.ippmedia.com/sw/biashara/naibu-waziri-akunwa-mradi-wa-soko
wales kidedea yatinga nusu fainali | michezo | dw | 02072016 wachezaji wa wales wakishangiria bao la pili dhidi ya ubelgiji wakiongozwa na robsonkanu wales ilivurumuka kutoka mwanzo ambao haukuwa tulivu kwake na kuikandika ubelgiji mabao 31 katika pambano lililojaa heka heka nyingi la robo fainali kwa magoli yaliyofungwa na washambuliaji wawili ambao hawafahamiki sana kama kawaida gareth bale alikuwa katika hali nzuri kabisa na mazungumzo kwa kweli yatatuwama kwake na cristiano ronaldo wa ureno wakati timu hizo zitakapokutana katika mpambano wa nusu fainali wiki ijayo nahodha wa wales ashley williams akishangiria bao lake la kusawazisha wachezaji wawili wenye uzoefu mkubwa katika historia ya kandanda wachezaji wanaocheza katika timu moja real madrid nyota waliomo katika timu mbili zenye mafanikio makubwa katika euro 2016 pamoja na hayo tofauti na ureno wales pamoja na bale wamecheza vizuri sana na kwa kweli ni mshangao wa kuburudisha wakati wakifikia awamu ya nusu fainali kwa mara ya kwanza katika mashindano makubwa tumefurahishwa mno kufikia hapa hatujawahi kufika katika kiwango hiki amesema kocha wa wales chris coleman ambaye aliichukua timu hiyo ikiwa nje ya timu 100 za juu duniani miaka minne iliyopita unaota kuhusu usiku kama huu hufahamu iwapo utakuwa na bahati ya kutosha kushuhudia hiki na wakati unakuwamo katika mafanikio kama haya huwezi kusimulia hisia zake akiwa amekata tamaa axel witsel wa ubelgiji baada ya dakika 25 jana ijumaa ndoto ilionekana kuwa mbali kwa wales dhidi ya ubelgiji iliyojichomoza na kuanza kwa kasi kikosi ambacho kilikuwa kinacheza karibu kama nyumbani kwake kiasi ya kilometa 10 tu kutoka mpaka wake na ufaransa wachezaji wenye uzoefu lakini ubelgiji ilitanabahi kwamba kutokuwa na wachezaji wawili walinzi wenye uzoefu mkubwa haitakuwa rahisi katika mchezo wake wa robo fainali dhidi ya wales hata hivyo haukuwa rahisi kabisa jana ijumaa katika mchezo ambao ulionesha udhaifu katika safu yake ya ulinzi ubelgiji ilitumbukia katika kipigo cha mabao 31 na kwa hiyo nafasi ya kufikia nusu fainali kwa mara ya kwanza katika mashindano makubwa kama haya tangu fainali za kombe la dunia mwaka 1986 iliota mbawa wachezaji wa ubelgiji wakishangiria bao lao la kuongoza majeruhi wa ubelgiji kocha marc wilmots aliingia katika michuano ya euro 2016 bila ya wachezaji wa kawaida vincent kompany na nicolas lombaerts kwa mchezo na wales pia alimkosa thomas vermaelen ambaye alikuwa na kadi mbili za njano na kwa hiyo hakustahili kucheza na kana kwamba mambo hayajakuwa mabaya zaidi wilmots alilazimika kumtoa kikosini mlinzi mwenye uzoefu mkubwa wakati jan vertonghen alipoumia misuli ya paja wakati wa mazowezi ya mwisho kabla ya kukabiliana na wales jana mpambano kati ya eden hazard wa ubelgiji na joel allen wa wales (kushoto) waliochukua nafasi zao jason denayer na jordan lukaku wote wakiwa na umri wa miaka 21 na wakicheza kwa mara ya nane na mwenzake mara ya tano katika kikosi hicho huwezi kubadilisha uzoefu mimi ndio nahusika na hatuwezi kuwalaumu wachezaji vijana wilmots amesema unahitaji mashine iliyotiwa mafuta vizuri kuweza kushinda tulifanya makosa ambayo hatukupaswa kufanya ni kweli kwamba ubelgiji ilifanya makosa baada ya dakika 20 za kwanza za kucheza kwa nguvu na kustahili kupata bao la kuongoza lililopachikwa wavuni na radja nainggolan kwa mkwaju wa mita 25 safu ya kiungo ilianza kupoteza mwelekeo na kurudi nyuma na mbinyo kwa wachezaji wachanga ulionekana dhahiri kuwa mzito katika mkutano na waandishi habari kocha wa die mannschaft joachim loew mashindano hayo yanaendelea leo ambapo ujerumani die mannschaft inaoneshana kazi na squadra azzurri timu ya taifa ya italia na jumapili ni zamu ya wenyeji wa mashindano ufaransa le bleau ikitiana kifuani na timu iliyowashangaza wengi iceland maneno muhimu euro 2016 belgium vs wales quarter final kiungo http//pdwcom/p/1jhpt
2017-08-22T14:12:06
http://www.dw.com/sw/wales-kidedea-yatinga-nusu-fainali/a-19373107
dia mirza veena malik shama sikander zoa morani puja gupta pooja misra isha sharvani jyoti sharma aishwarya rai bachchan sasheh aagha sonam kapoor neha dhupia jacqueline fernandez evelyn sharma gihani khan complete list
2013-05-18T14:44:03
http://www.glamsham.com/download/send.asp?imagename=/download/picturegallery/picture1.asp?subcatid=10251*pg=11
michezo swatches bodi povu safu ya kirumi baada ya picha ya mapambo classic waterproof pvc bodi based skirting bodi style jja074 vipengele na manufaa ya maelezo pvc 1water ushahidi bidhaa zetu ni maji ushahidi na wala kupanua mkataba au warp wakati wao kuja kuwasiliana na maji 2fire retardant profile yetu si kuchoma yenyewe bidhaa mzima mara moja wakati nje chanzo moto ni kuondolewa ina got a darasa moto rating 3mufti wa hali ya hewa uwezo hali ya hewa haina athari kwa vifaa pvc jengo matatizo kama uozo kutu nk tu wala kuomba hata katika hali ya pekee maeneo coast (salt storm sun) pvc ni zaidi husika 4anti uv profile yetu ina nzuri uv ulinzi kazi anaweza kukupa starehe na afya 5thermal insulation profile yetu ni iliyoundwa kwa mtindo chumba ina nzuri insulation joto utendaji uhamishaji wa joto ya mgawo ni ya chini hivyo siwezi kuweka nyumba yako ya joto katika majira ya baridi na baridi katika majira ya joto 6durability profile zetu ni muda mrefu sana na mwisho zaidi ya miaka 40 bila mabadiliko ya rangi kuharibiwa nk 7green mazingira ya ulinzi wasifu matumizi yetu ya kijani formula na malighafi (hakuna risasi) ni madhara kwa afya yako na mazingira awali skirting bodi style jja073 next skirting bodi style jja081 mapambo ya plastiki profile skirting pvc extrusion waterproof pvc mlango jamb marumaru ya pvc skirting bodi pvc mlango jamb maji ya upinzani pvc bodi skirting simu + 865808235505 faksi ++ 865808041862 anwani zhejiang jinjia kijani mapambo co ltd
2020-07-13T23:41:46
http://www.chinaxpsboard.com/sw/skirting-board-style-jj-a07-4.html
mzozo wa katiba nchini zambia | matukio ya kisiasa | dw | 06022009 mzozo wa katiba nchini zambia upinzani wavutana na serikali huko nchini zambia ni miaka miwili sasa tangu kuanza kufanya kazi baraza la kitaifa la katiba nchini zambia liitwalo ncc hata hivyo lakini baraza hilo linaona vigumu kukukubalika na raia kwani bado kuna mivutano kuhusu marekebisho ya katiba nchini humo evans kaputo anashiriki kwenye juhudi za kupambana na rushwa na mtandao wa elimu ya kiraia kundi la mashirika ya kijamii mjini lusaka nchini zambia hajaridhika kwamba dola milioni 80 zimetengwa kugharamia mkutano wa kitaifa wa kuifanyia marekebisho katiba ya nchi ''mkutano huu ni kupoteza fedha tunachohitaji ni mabadiliko ya vipi fedha zinavyotumiwa na kuziongezea nguvu sheria kuhusu wizi unaofanywa na wafanyakazi wa serikali rushwa matumizi mabaya ya mamlaka na kadhalika tunahitaji kupunguza mishahara ya wabunge'' amesema bwana evans kaputo mchakato wa sasa wa kuifanyia marekebisho katiba ni wa nne tangu zambia ilipojipatia uhuru wake mnamo mwaka 1964 mkutano wa kwanza ulifanyika mnamo mwaka 1973 na ulitumika kukaribisha taifa lililotawaliwa na chama kimoja mkutano wa pili wa mwaka 1991 ulidhihirisha mfumo wa demokrasia ya vyama vingi miaka mitano baadaye mkutano wa tatu ulisifiwa kwa kuzingatia kwa makini maadili ya kidemokrasia wazo la mkutano wa sasa lilianzishwa mnamo mwaka 2002 na serikali ya rais wa zamani marehemu levy mwanawasa kushughulikia kile kilichoelezwa kuwa mapungufu makubwa katika katiba ya mwaka 1996 mapungufu hayo yalijumulisha kukosekana kwa uhuru wa tume ya uchaguzi ya zimbia na kujumulishwa kwa kipengee kinachotaka wazazi wa mgombea urais wa nchi hiyo wawe raia asili wa zambia vyama vya upinzani na idadi kubwa ya makundi ya kijamii yaliamini kuwa kipengee hicho kuwazuia raia wa zambia ambao si raia asili wa nchi hiyo wasigombee wadhifa wa urais kilinuiwa kumfungia mlango rais wa zamani kenneth kaunda ambaye wazazi wake walizaliwa nchi jirani ya malawi asigombee tena wadhifa huo kwenye uchaguzi uliofuata hata hivyo katiba hiyo ilitupilia mbali mapendekezo muhimu kama vile kuandika tarehe ya uchaguzi mkuu kwenye katiba kufuta hukumu ya kifo na kuanzisha mahakama ya katiba kushughulikia mashitaka dhidi ya rais badala ya mahakama kuu katiba ya mwaka wa 1996 ilipingwa na makanisa mashirika ya haki za binadamu na vyama vya upinzani lakini ilitekelezwa na chama tawala kilichokuwa na idadi kubwa ya wabunge wakati huo hata hivyo mchakato wa sasa wa kuirekebisha katiba umegubikwa na hali ya sintofahamu tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka wa 2002 kwanza serikali ilipinga wazo la kufanya mkutano ambao ulikuwa ufuatiwe na kura ya maoni kama inavyotakikana kisheria ikidai kwamba ingekuwa na gharama kubwa mno katiba ya sasa inadai sio tu katiba irekebishwe kupitia kura ya maoni bali pia watu wahesabiwe kwanza kabla kura hiyo ya maoni kufanyika chama tawala cha movement for multiparty democracy mmd kinasisitiza kuwa bunge ndio chombo pekee kinachofaa kuidhinisha katiba mpya huku upinzani na jumuiya ya kiraia ikiongozwa na kundi la patriotic front linaloyajumulisha makundi yasiyo ya kiserikali makanisa na mashirika ya sheria nchini zambia zikitaka katiba mpya iidhinishwe na mkutano mkuu wa kitaifa kuhusu marekebisho ya katiba na wala sio bunge lililo na idadi kubwa ya wabunge wa chama tawala ili kuzuia kutokea kwa mizengwe lakini serikali inasisitiza bunge pekee lina mamlaka ya kuunda sheria na serikali ya chama cha mmd kilicho na thuluthi mbili ya idadi ya wabunge inayohitajika kupitisha mswada kuwa sheria kilipitisha mswada uliozusha utata wa mkutano wa kitaifa wa marekebisho ya katiba mnamo mwezi agosti mwaka 2007 uliounda baraza la kitaifa la kurekebisha katiba ncc lakini pia kupanua mamlaka ya rais na kupuuza takwa la kikatiba la kuitisha kura ya maoni baada ya kumalizika mchakato wa kuifanyia mageuzi katiba kiongozi wa upinzani michael sata amewaamuru wabunge wa chama cha patriotic front wahudhurie baraza la kitaifa la marekebisho ya katiba na wakati huo huo kuwatimua wabunge 26 waliojiunga na chama hicho michael sata anasema kiwango cha dola milioni 80 kilichotengwa kwa ajili ya mkutano huo ni gharama kubwa mno kwa taifa ikizingatiwa kinachotakiwa kubadilishwa kwenye katiba hiyo kinajulikana na kila raia wa zambia mwandishi ips/ charo josephat kiungo https//pdwcom/p/gowd
2019-09-23T09:25:26
https://www.dw.com/sw/mzozo-wa-katiba-nchini-zambia/a-4007445
china yazungumzia uboreshwaji wa tazara mwananchi china yazungumzia uboreshwaji wa tazara serikali ya china imesema haitaliacha shirika la reli ya tanzania na zambia (tazara) life bali itaendelea kufanya kazi na nchi hizo mbili ili kuhakikisha usafiri huo ulioanza miaka 40 iliyopita unadumu dar es salaam serikali ya china imesema haitaliacha shirika la reli ya tanzania na zambia (tazara) life bali itaendelea kufanya kazi na nchi hizo mbili ili kuhakikisha usafiri huo ulioanza miaka 40 iliyopita unadumu akizungumza katika ofisi za kampuni ya mwananchi communications limited (mcl) tabata relini jijini dar es salaam balozi wa china nchini tanzania wang ke amesema tazara ni umoja wa nchi za tanzania zambia na china na inapaswa kuendelea kuwapo amesema ujenzi wa reli hiyo kati ya dar es salaam na kapiri mposhi uliofanyika kati ya mwaka 1970 hadi 1976 ilikuwa ni zawadi ya china kwa mataifa ya zambia na tanzania hivyo nchi hizo zinapaswa kuendelea kushirikiana akizungumzia taarifa za vyombo vya habari kuwa tanzania ilitaka kuboresha masharti matano yaliyohusu mradi wa bandari ya bagamoyo kwa sababu hayakuwa na faida kwa serikali ya tanzania amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote ke amesema taarifa hizo zimeandikwa mtandaoni kutoka kenya na si kwenye gazeti na wenyewe kama ubalozi hawafahamu zilitoka wapi alisema mradi huo wa bandari ni muhimu na unahusu serikali na mwekezaji kutoka china ambao ndiyo wanaopaswa kuzungumzia ni namna gani wanaweza kuuendeleza ke amesema china inapenda kuona mwekezaji kutoka nchini humo anawekeza katika mradi huo wa bandari kwa faida ya nchi na raia
2019-11-13T18:57:44
https://www.mwananchi.co.tz/habari/kitaifa/China-yazungumzia-uboreshwaji-wa-Tazara/1597296-5320806-qqjirbz/index.html
jayz na beyoncé wakiwa kwenye boda boda uswahilini | mwanaharakati mzalendo ™ home » »unlabelled » jayz na beyoncé wakiwa kwenye boda boda uswahilini kama ni mfuatiliaji wa wasanii wawili wa muziki kutoka nchini marekani beyonce na jay z kuanzia jana kwenye mitandao ya kijamii kumekuwa na picha za mastaa hao zikisambaa kwa kasi zikiwaonesha wakiwa kwenye boda boda katika maeneo ya uswahilini watu wengi mwanzoni walidhani ni picha za kutengenezwa kutokana na hadhi ya wasanii hao lakini ukweli ni kwamba picha hizo ni zao na ni za kweli kwa mujibu wa mtandao wa daily mail umeeleza kuwa picha hizo za wawili hao wamepiga nchini jamaica kwenye utengenezaji wa scene ya ziara yao ya kimuziki ya otr ii kwa upande mwingine mbali ya kutangaza tour yao ya pamoja kwa mara ya pili kuna tetesi kuwa wawili hao huenda wakaachia albamu ya pamoja siku za usoni ziara hiyo ya on the run ii (otr ii) itaanzia katika mji wa cardiff nchini uingereza ifikapo juni 6 2018 na kumalizika oktoba 2 mwaka huu katika mji wa vancouver nchini canada ambapo itazunguuka zaidi ya miji 35 duniani muda 92600 pm
2018-04-25T08:28:14
https://mwanaharakatimzalendo.blogspot.com/2018/03/jay-z-na-beyonce-wakiwa-kwenye-boda.html
rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli akimwapisha kamishna diwan athumani kuwa katibu tawala wa mkoa wa kagera ikulu jijini dar es salaam novemba 222016 | blogu rasmi ya ofisi ya rais rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli akimwapisha kamishna diwan athumani kuwa katibu tawala wa mkoa wa kagera ikulu jijini dar es salaam novemba 222016 rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali mara baada ya kumwapisha kamishna diwan athumani kuwa katibu tawala wa mkoa wa kagera ikulu jijini dar es salaam novemba 222016 rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli akiteta jambo na kuagana na kamishna diwan athumani mara baada ya kumwapisha kuwa katibu tawala wa mkoa wa kagera ikulu jijini dar es salaam novemba 222016 this entry was posted in top stories on november 22 2016 by ikulu ikulu ← rais dkt magufuli akutana na kufanya mazungumzo na jenerali fan changlong makamu mwenyekiti wa kamisheni kuu ya ulinzi ya jeshi la ukombozila watu wa china (pla) ikulu jijini dar es salaam novemba 212016 rais dktjohn pombe magufuli akutana na kufanya mazungumzo na rais mstaafu wa awamu ya pili mzee ali hassan mwinyi ikulu jijini dar es salaam novemba 232016 →
2019-11-12T23:17:25
http://blog.ikulu.go.tz/?p=17944
mwanaharakati mkutano kati ya kamati ya serikali ya urasimishaji wa tasnia za filamu na muziki wasambazaji na wazalishaji wa bidhaa za sanaa peacock hotel januari 14 2013 vii kupata maoni ya wasambazaji na kujua tofauti kati ya bidhaa za filamu na muziki viii kufanya majumuisho ix kufunga kmkutano baadhi ya yaliyojadiliwa na wadau projection & stock wasambazaji walionesha wasiwasi juu ya mfumo wa kununua stika ilihali kuwa haijulikani idadi gani ya kazi utakazouza walipendekeza tra iwarudishie rejesho la pesa kwa kazi ambazo hazikuuzika baada ya kubandikwa stampu wadau wakiwemo wazalishaji na wasanii walihoji uasili na wakati gani wa kuharibika kwa kazi za sanaa kwenye soko ili kuhalalisha madai ya wazalishaji kinyume chake waliomba ufafanuzi kwa tra inafanyaje kwa kazi zinazoonekana haziuzi leo lakini zitauzwa hata baada ya miaka kumi (ambapo tra haikuweza kutoa ufafanuzi wa kueleweka juu ya hilo) confussion wadau walionekana kutoridhishwa na baadhi ya majibu yaliokuwa yakitolewa bila mchanganuo wa kueleweka likiwemo la mfanyabiashara kupewa ruhusa ya kujiunga na mfumo wa vat mara baada ya kufikia kiwango fulani cha mauzo yake ya mwaka pasi na kuainisha faida au hasara zilizomo ndani yake tra kupokea moja kwa moja ushauri wa kutumia njia ya kienyeji manually kubandika stamp kutoka kwa msambazaji mkubwa na kuiweka kando njia ya kutumia mashine kwa kisingizio cha kukuza ajira kwa watu wanaotumiwa kubandika hizo stika/stampu au uharaka wa kazi imeleta sura mpingano kwa wadau na wasanii juu ya kuchomoza kwa mianya ya piracy wameiomba tra ifanye utafiti wa kutosha na isikurupuke tu ulinzi kwa mujibu wa tra stamp zitakazotolewa zitatolewa kwa title (yaani kwa kila kazi ) na pia zitakuwa na code namba ambazo zitasaidia licha ya uzuiaji wa wizi pia kujua jumla ya mauzo kwa kazi husika kazi ya kumonitor hili itafanywa na tra ikishirikiana na kamati zake (bodi ya filamu cosota na basata) kamati ambazo baadhi yake zimeonekana kuwa na mapungufu mengi ya utawala na utendaji (vipi tunarasimisha sekta ilihali bado kamati zinatotegemewa na mchakato mzima zina mapungufu) pia tumeambiwa kwamba ukaguzi wa kujua mauzo ya stamp yameendaje mfumo wake utakuwa ni kukagua stamp ngapi ya zile zilizotolewa na tra zimebakia jambo hili bado linatupa mashaka ya mfumo huo kama utakuwa na ulinzi imara wa kazi hizo hata pendekezo la kutumia bar code kwa atakayependa kutumia mfumo huo hautoi ulinzi wa mfanyabiashara kuifuatilia kiurahisi bidhaa yake na kuikagua kama halali ama piracy tra imeshindwa kufafanua itawiainishaje juu ya mfumo wa biashara unaoendana na maendeleo ya techologia (teknohama) na mfumo wa ubandikaji stamp wakati hali halisi inaonekana kuwa inatia nguvu kubwa katika hard copy ambayo digitally inafutika polepole wasambazaji wameeleza kuwa sheria haiwabani wanaofanya kazi za library kwenye mabasi na mahoteli ambao wanasababisha mapato kuwa madogo hivyo watashindwa kununua stamp wadau wameiomba serikali kupitia tra kuongeza kodi au bei ya stamp za kazi zinazotoka nje za sanaa ikiwemo za 10 in 1 ili kumarisha soko la ndani tra imekiri kuwa kuna ugumu wa kuzui kazi za ndani ambazo zinauzwa kiharamia nje ya mipaka yetu kutokana na nchi kuwa na mifumo ya tax force inayotofautiana (hivyo imelichukua hilo kama changamoto) wadau wameiomba tra iangalie sheria ya cosota ya mhalifu wa kazi za sanaa kulipa faini isiyoendana na ukubwa wa kosa kinyume chake wasanii watashindwa kuamini kwamba mfumo huu ni kwa ajili ya kusaidia kulinda kazi zao tra imeonekana ina wasiwasi juu ya kama itaweka sheria ambayo itawabana wasambazaji ambao ndio pia wana capital kubwa kulinganisha na wasanii wasambazaji watabadilisha biashara hivyo mfumo hautoi function kimsingi tra wanatakiwa wafanye tafiti ambazo zitasaidia kuja na mfumo bora utakaosaidia kuongeza wazalishaji na wasambazaji wenye ubora kwenye tasnia hizi mbili wadau wameiomba tra isaidie kuweka mifumo ambayo wasanii wazalishaji nk waweze kusaidiwa kuwa wafanyabishara wasambazaji wa kazi zao kwa kuwapa mikopo na mifano yake hiyo pia itaongeza idadi ya walipa kodi mikataba ni suala lililoelezewakuwa na mapungufu makubwa zifuatazo ni miongoni mwa sababu zilizoelezwa na wadau kuwa ni matatizo ya mikataba kutoshirikisaha wanasheria kutotaka kufanya tafiti au hata kutotaka kutumia tafiti ukosefu wa elimu ya kugundua/kutambua lugha za kitaalamu ama kisheria hivyo walipendekeza yafuatayo mikataba iwe ya kiswahili kinachoeleweka wakati wa usainishaji wa mikataba kuwepo na chombo kimojawapo kama basata au bodi kusimamia haki za msingi kila pande iwe na mwanasheria taasisi za kisanaa kama taff nk wanatakiwa kuwapa elimu watu wake kuhusu faida au hasara inayopatikana na uuzaji wa hakimiliki na hakishiriki na pia kuwa na azimio la pamoja kimsimamo kwa wote juu ya kiwango cha kazi kabla ya kuingia mikataba wachangiaji wameweza kugawanya mfumo wa mnyororo wa dhama (value chain) tanzania katika sehemu mbili mfumo wa nadharia na mfumo wa uhalisia (mazoea) nadharia ni mfumo unaotumika katika nchi nyingi kuanzia kwa mwandishi mpaka kwa msambazaji na mnunuzi wakati mfumo wa uhalisia ni huu ambao unaotumika tanzania pekee wa msambazaji kulazimishakupendekeza filamu iwe vipi wadau wamedai kuwa mfumo huu ndio umepelekea uvunjwaji wa maadili na kuharibu dhima nzima ya uandishi kulingana na mafundisho badala yake inakuwa ni uandishi kulingana na wasambazaji wanataka nini au wanamtaka nani acheze kama muhusika nk tra wamependekeza licha ya kikao cha leo kuitisha semina nyingine za kutoa elimu juu ya sheria na mikataba wadau wameshauri tra itanue upeo wa kutoa elimu nchi nzima ikiwezekana iwe na kipindi cha tv pia wameshauri kuwa wafungue kundi katika mitandao ya jamii ili wadau waweze kujadiliana kupitia online hivyo watakuwa wamefikisha maoni ambayo yanaweza yakawa na tija kwao na tasnia nzima kufungwa kikao kikao kilifungwa rasmi huku tra wakiahidi watatoa taarifa kwa wadau katika kikao kifuatacho na bishop hiluka muda 254 pm
2018-01-21T02:34:04
http://bishophiluka.blogspot.com/2013/01/mkutano-kati-ya-kamati-ya-serikali-ya.html
saa yapoteza thamani | masuala ya jamii | dw | 15032012 saa yapoteza thamani kwa miaka mingi uvaaji ulikuwa ukichukuliwa kama jambo la ustaarabu thamani na wakati mwengine la kifahari pia na watengenezaji saa wakatengeza kila aina na staili za mashine hiyo iliyogeuka kuwa sehemu ya mapambo saa kama kito cha thamani na chombo cha kujulia wakati lakini sasa mabadiliko ya ulimwengu yanaishuhudia matumizi ya saa kama pambo na hata mashine yakishuka je sababu ni nini katika makala hii ya vijana mchakamchaka bruce amani anazungumzia ilipokwenda thamani ya saa miongoni mwa rika la vijana wa sasa kusikiliza makala hii tafadhali bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini mada kupotea kwa thamani ya saa katika makala hii ya vijana mchakamchaka bruce amani anazungumzia ilipokwenda thamani ya saa miongoni mwa rika la vijana wa sasa maneno muhimu saa vijana mchakamchaka mashine pambo kiungo http//pdwcom/p/14l4k
2018-06-24T21:15:21
http://www.dw.com/sw/saa-yapoteza-thamani/a-15810666
hgh releasers find best bidhaa hgh hair removal ukuaji wa binadamu homoni msumari kuvu find best bidhaa hgh mbalimbali mzima wa hgh ( ukuaji wa binadamu homoni bidhaa) hgh sindano dawa ya kupuliza hgh hgh releasers vidonge hgh na dawa hgh ni alidai kuwa na athari hiyo ya kuongeza mwili wa ngazi hgh na kusaidia ni kupata nafuu kutokana na ugonjwa huo hata hivyo kabla ya kununua yao tunahitaji kujifunza zaidi juu ya athari chanya na hasi ya bidhaa hgh je wao ni salama na unaweza kweli kukidhi matarajio yetu angalia taarifa zifuatazo na kupata bidhaa bora hgh hgh bidhaa jambo la kwanza tunatarajia kukuambia ni oral bidhaa hgh kufanya kazi kwa nini jibu ni rahisi asili hcl asidi kuua kila ukuaji wa binadamu homoni kwa haraka kama anakuja ndani ya tumbo lako na hakuna namna ya hgh ambayo inaweza kuishi hgh dawa ya kupuliza pua pia haiwezi kutumika kama kuponyawote ukubwa hgh molekuli 'kuwazuia kupitia cavity pua yako kwa sababu ni kubwa mno kiasi kidogo tu ya hgh ambayo inaweza kuingia katika damu yako kwa njia hii inaweza kuongeza kidogo yako ngazi hgh hgh pia inatumika kwa namna ya sindano lakini katika kesi hii wagonjwa ni chini ya hatari ya kulevya na hivyo na madhara makubwa badala upande ambayo wakati mwingine kusababisha kifo kwa mtu na hatari ya kuongezeka kwa ulaji aftereffects bandia ukuaji wa homoni wakati ni kuchukuliwa kwa muda mrefu bila shaka sio unataka kuweka afya yako katika hatari kwa hiyo huenda kutoa upendeleo kwa bidhaa ambazo zina viungo asili na unaweza kuchochea uzalishaji wa hgh na tezi yako tezi ni salama bora na gharama nafuu bidhaa hizi na jina maalum hgh releasers wao kusaidia tezi yako tezi kufanya homoni zaidi hgh mitishamba tu releasers hgh wanaweza kufanya tezi yako tezi kazi na uwezo wa kutoa zaidi hgh kumbuka kwamba bidhaa hizi ni za asili si bandia releasers hgh ambayo yamekuwa misukosuko na vizuri sampuli na idadi kubwa ya watu bila ya shaka wana mengi zaidi credence ikilinganishwa na wale tu kusema ahadi za uongo kuangalia uwezekano wa taarifa zote juu ya bidhaa hizo kumbukumbu zote za kesi zao na matokeo ya matumizi ya kuelewa kama unaweza kuwaamini ni lazima kupata fda na eu maelekezo ya idhini hgh releasers kuwa ni asili wote na kemikali zinazozalishwa itahakikishia hatua madhubuti na hatari ya bure zaidi ya hayo wanapaswa kuwa na irritants yoyote ambayo inaweza kusababisha athari hypersensitive katika mwili hgh releasers pia kinatakiwa kisiwe vihifadhi yoyote coloring bandia chumvi au gluten ni lazima kuwa 100 asili bidhaa nzuri hgh releaser inaweza kukusaidia kufikia revitalizing nguvu faida kupambana na kuzeeka na nyingine kwa ajili ya mwili wako katika njia ya asili yoyote ya hgh releasers ni ufumbuzi wa tatizo la kisasa kuzeeka na kuonekana ni salama kabisa kwa ajili ya watu ni lazima tu kupata bidhaa bora hgh pengine njia bora ya kufanya hivyo si kwa kutegemea matangazo lakini surf internet na kupata hgh jukwaa huru ambapo watumiaji halisi kuelezea uzoefu wao na bidhaa hgh kumbuka kwamba nzuri hgh jukwaa (http//forumhghproductsvotecom/) hutoa misimamo mbalimbali wote chanya na hasi ndio faida na hasara yake ni kutazamwa na kuchunguzwa kikamilifu hapa unaweza kuuliza maswali yote wewe na unaweza kupata majibu ya watumiaji wa uzoefu hivyo wakati unajua kuwa maelfu ya watu kupata bidhaa hgh ufanisi na salama unaweza kufanya uchaguzi wako mwenyewe matukio ya hgh releasers matukio katika ukuaji wa binadamu homoni genf20 hgh kazi kwa revitalizing kazi ya tezi tezi kutoa zaidi na ukuaji wa binadamu homoni kila kiasi cha uingizwaji na ukuaji wa binadamu homoni ina athari kubwa kikubwa kujenga na revitalizing viungo vyote vya mwili genf20 hgh ina siku 60 + wiki moja kuhakikisha kama kwa sababu yoyote wewe si tu kuridhika kabisa kurudi sehemu isiyotumika katika chombo awali ndani ya siku 67 ya kupokea amri yako (60 siku kesi + wiki moja kurudi meli) na wao refund wewe 100 ya bei ya kununua ukiondoa meli na kuchukua yaliyomo genf20 hgh gtf chromium lornithine larginine llysine ltyrosine lglutamine lglycine tezi (anterior) poda kolostramu phosphatidyl choline gelatin syloid magnesium stearate save hgh releasers pdf kwanza moja kwa moja tafsiri kwa google nakala hgh releasers find the best hgh products
2018-05-27T19:39:35
http://sw.yourwebdoc.com/healthcare/hghreleasers.php
ufichuaji mkubwa akaunti za siri za matajiri | matukio ya kisiasa | dw | 04042016 ufichuaji mkubwa akaunti za siri za matajiri ufichuaji huo mkubwa unaohusisha nyaraka milioni 115 na kupewa jina la panama leaks umeonyesha namna matajiri wanavyotumia maeneo salama ya kodi kuficha utajiri wao na kukwepa kodi uchunguzi uliyofanywa na zaidi ya makampuni 100 ya habari umefichua mali zilizofichwa nje za watu mashuhuri duniani wakiwemo wanasiasa karibu 140 nyaraka hizo zilipatikana na gazeti la kila siku la nchini ujerumani süddeutsche zeitung na kusambazwa kwa makampuni mengine ya habari ulimwenguni na jukwa la kimataifa la waandishi wa habari za uchunguzi icij nyaraka hizo zinazoyahusu mashirika karibu 214 000 ya nchi za kigeni kwa muda wa karibu miaka 40 zilitoka kampuni ya uwakili ya mossack fonseca yenye makao yake nchini panama na ikiwa na ofisi katika mataifa zaidi ya 35 jengo la kampuni ya uwakili ya mossack fonseca katika mji mkuu wa panama panama city putin xi jinping jackie chan watajwa uchunguzi huo unadai kuwa washirika wa karibu wa rais wa urusi vladmir putin ambaye binafsi hajatajwa katika nyaraka hizo za siri walihamisha kwa siri kiasi cha dola bilioni mbili kupitia mabenki na makampuni hewa viongozi 12 walioko madarakani na wa zamani pia wametajwa katika uchunguzi huo wakiwemo waziri mkuu wa pakistan rais wa ukraine na mfalme wa saudi arabia na vile vile nyota wa filamu akiwemo jackie chan wachunguzi wamedai pia kuwa familia ya rais wa china xi jinping ina mahusiano na akaunti za nje kama alivyokuwa marehemu baba wa waziri mkuu wa sasa wa uingereza david cameron na wanadai pia kuwa waziri mkuu wa sasa wa iceland aliwekeza kwa siri mamilioni ya pesa kwenye benki za nchi hiyo wakati wa mgogoro wa kifedha mkurugenzi wa jukwaa la kimataifa la waandishi wa habari za uchunguzi gerard ryle amesema kinachoshtua zaidi ni namna ulimwengu wa nje unavyotumiwa na viongozi walioko madarakani ambao baadhi yao wamekuwa wakijitanabisha kuwa wapinzani wakubwa wa usiri tunachopaswa kufanya hapa kama waandishi habari ni kuvunja usiri kwa sababu bodhaa pekee inayotolewa na ulimwengu wa nje ni usiri na bila hivyo basi hakutakuwa tena na bidhaa hivyo kadiri tunavyoendelea kuwafedhehesha watu nadhani tutaona mageuzi ya kweli alisema ryle katika mahojiano na dw kampuni ya uwakili ya mossack fonseca ilifanya kazi na watu wasiopungua 33 na makampuni yliyoorodheshwa na marekani kwa kuwa na uhusiano wa kibiashara na magenge ya wauza madawa ya kulevya nchini mexico makundi ya kigaidi na mataifa sugu ikiwemo korea kaskazini moja ya makampuni hayo lilitoa mafuta kwa ajili ya ndege za utawala wa syria zilizotumiwa kuwashambulia wake ufichuzi wa panama unatajwa kuwa mkubwa zaidi katika historia wateja wa kampuni hiyo wanahusisha wawekezaji wa uongo magwiji wa madawa wakwepaji kodi na mfanyabiashara wa marekani alitiwa hatiani kwa kwenda nchini urusi kufanya ngono na watoto yatima walio chini ya umri ambaye alisaini nyaraka za za kampuni ya nje akiwa gerezani lionnel messi sepp blatter nao wamo nyaraka hizo pia zinahusisha matajiri 29 walioko katika orodha ya matajiri ya jarida la forbs na nyota wa filamu za mapigano jackie chan yumo pia mjumbe w akamati ya maadili ya fifa juan pedro damian mchezaji soka nambari moja duniani lionnel messi na rais wa zamani wa fifa sepp blatter zaidi ya benki 500 na benki zake tanzu na matawi pia zimefanya kazi na kampuni ya mossack fonseca tangu miaka ya 1970 kuwasaidia wateja wao kusimamia makampuni ya nje bradley manning wa wikileaks mahakamani mwanajeshi wa marekani aliyekabidhi nyaraka za siri za serikali ya marekani kwa mtandao wa wikileaks bradly manning anafikishwa mahakani zaidi ya miaka mitatu baada ya kukamatwa nchini iraq je ni shujaa au msaliti (03062013) uamuzi huo wa leo (05022016) unatoa matumaini kwamba assange huenda akawa huru baada ya kukaa katika ubalozi wa ecuador mjini london kwa karibu miaka minne (05022016) mada zinazohusiana fifa marekani panama benki kuu ya marekani chama cha republican donald trump brexit mike pence cia nafta maneno muhimu panama fifa marekani uk urusi putin jinping kiungo http//pdwcom/p/1iozj
2017-12-13T10:09:05
http://www.dw.com/sw/ufichuaji-mkubwa-akaunti-za-siri-za-matajiri/a-19162297
ramadhani saumu huwakinga wanaofunga dhidi ya maasia na machafu taifa leo ramadhani saumu huwakinga wanaofunga dhidi ya maasia na machafu na khamis mohamed funga ni kinga ni kinga itakayo kinga mja na moto wa jahanamu itamkinga mwenye kufunga dhidi ya madhambi maovu na machafu ni maumbile ya nafsi ya mwanadamu kupenda mno kutenda maovu kama alivyosema mwenyezi mungu kwa hakika (kila) nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu isipokuwa ile ambayo mola wangu ameirehemu [1253] funga iliyokamilika inamlinda na maradhi mbali mbali katika mwili wake na maradhi ya nafsi yake ndipo mtume wa mwenyezi mungu muhammad rehema na amani zimshukie alisema akiwaelezea kundi la vijana jinsi ya kuyavunja na kuyazima matamanio kwa kutumia silaha ya swaumu akasema enyi kusanyiko la vijana yeyote miongoni mwenu atakayeweza kuoa basi na aoe kwani huko (kuoa) kunalihifadhi mno jicho na kunaipa ngome tupu na asiyeweza (gharama za ndoa) basi na ajilazimishe na swaumu kwani hiyo (swaumu) ni kinga kwake (dhidi ya maasi) bukhaari na muslim na ni kweli kabisa aliyoyasema bwana mtume kwani imethibiti kupitia majaribio kwamba swaumu inapunguza matamanio kwa kiwango kikubwa sana kama sio kuyakata kabisa mtume wa mwenyezi mungu rehama na amani zimshukieamesema na swaumu ni kinga atakapofunga mmoja wenu asiseme maneno machafu siku hiyo na wala asipayuke iwapo mtu atamtukana au kumpiga basi na aseme hakika mimi nimefunga (muslim) mfungaji kukatazwa kusema maneno machafu na kupayukapayuka ovyo kuna msaada mkubwa kwake katika kuidhibiti nafsi yake ulimi viungo na moyo wake dhidi ya kutenda maasi mojawapo ya mambo yatakayokusaidia kuihepa adhabu kali ya moto ni ibada ya swaumu kama alivyosema mtume wa mwenyezi mungu rehema na amani zimshukie swaumu ni kinga na ni ngome madhubuti dhidi ya (adhabu ya) moto (ahmad) hali kadhalika allah huwaneemesha baadhi ya wafungaji kwa kuwaacha huru na adhabu ya moto kama alivyosema mtume wa allahrehema na amani zimshukie hakika allah taala anao waachwa huru na moto wakati wa kila kufuturu na hilo (hupatikana) katika kila usiku (ahmad) kama tuonavyo funga ni kinga tosha kutokamana na maasi na machafu iliyobaaki ni kila aliyefunga anatakiwa kuzidisha ibada kwa maneno na vitendo walioghafilika huko nyuma wazinduke na kuifanye ramadhani hii kama kitu cha kuwabadilisha walete toba kwa wingi wasimame sana usiku kwa kufanya ibada na kumtaja sana mwenyezi mungu kwa sababu huu ndio mwezi wa kuchuma thawabu kwa wingi bila masumbuko ya nafsi ama shetani kwani wote washafungwa minyororo mwenyezi mungu atuepushe na moto wake ramadhani saumu ramadhani chunguza saum yako ukiwa katika ndoa ya aina hii ramadhani dua ya mwenye kufunga hairudi tujitahidi ramadhani manufaa chungu nzima kwa mwenye kufunga rais kenyatta awatumia waislamu risala za heri ramadhani
2018-06-24T08:38:52
http://taifaleo.nation.co.ke/index.php/ramadhani-saumu-huwakinga-wanaofunga-dhidi-ya-maasia-na-machafu/
vijana kutoka baringo wamzomea uhuru kutokana na maendeleo duni eneo hilo ▷ tukocoke vijana kutoka baringo wamzomea uhuru kutokana na maendeleo duni eneo hilo maoni 1330 wabunge moses kurian a kimani ngunjiri wamemkosoa rais uhuru kenyatta kwa madai kuwa eneo la mlima kenya halijapata miradi ya maendeleo chini ya utawala wake matamshi yao yalimlazimu rais uhuru kenyatta kuwajibu kwa kuwataja kuwa washenzi vijana katika kaunti ya baringo waliwaunga mkono viongozi hao wawili wakisema kuwa maeneo yao yalikosa maendeleo licha ya kumpigia rais kura kwa wingi walilaumu maridhiano kati ya rais kenyatta na kinara wa upinzani raila odinga na kudai yalisababisha misukosuko kwenye chama cha jubilee vijana hao walitishia kushinikiza uchaguzi mwingine uandaliwe ikiwa rais hatasikiliza kilio chao baadhi ya vijana katika kaunti ya baringo wamejitosa kwenye mjadala kuhusu maendeleo duni katika maeneo fulani nchini na kusema kuwa kaunti yao haijapata maendeleo waliyotarajia licha ya kumpigia kura kwa wingi rais uhuru kenyatta viongozi hao wa vijana walilalamikia uwepo wa kinara wa upinzani raila odinga kwenye serikali baada ya maridhiano yake na rais uhuru kenyatta walisema kuwa tukio hilo ndilo lililosababisha mshikemshike kwenye chama cha jubilee vijana katika kaunti ya baringo walimzomea rais uhuru kenyatta kutokana na maendeleo duni katika yao walidai serikali ilitenga maeneo fulani katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo picha ugc wakizungumza na wanahabari jumanne januari 8 vijana hao walilaumu mpango wa building bridges unaoendeshwa na uhuru na raila na kudai kuwa ulichangia ubaguzi wa maeneo fulani kupata miradi ya maendeleo tuliipigia jubilee kura miaka ya 2013 na 2017 lakini barabara zetu ni mbaya na hatuna maji watu wengi wamefaidika inaonekana kuwa karata inachezwa mahali pengine robert kipkorir alisema vijana hao walimtaka rais kenyatta kuwaheshimu wapiga kura kwani baadhi yao walitumia raslimali zao kulifanyia kampeni chama cha jubilee wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2017 sielewi anachokifanya raila odinga kwenye serikali uwepo wake humo umezua mshikemshike katika chama cha jubilee ikiwa rais ataamua kumwacha ruto na kufanya kazi na raila serikali hii inastahili kuvunjwa ili tuwachague viongozi wengine almeida yabei alisema hapo awali rais kenyatta aliwasuta wabunge moses kuria (gatundu kusini) na kimani ngunjiri (bahati) waliokuwa wamemshambulia wakidai eneo la mlima kenya halijafaidi kwa miradi ya maendeleo chini ya utawala wake wawili hao walisema kuwa rais kenyatta aliangazia maendeleo maeneo mengine na kuyapuuza maeneo kadhaa ambayo yalimpigia kura kwa wingi kwenye uchaguzi kuu wa mwaka wa 2017 serikali yafanya msako wa mashine haramu za michezo ya kamari | tuko tv skrill to mpesa kra pin best saccos in kenya knec examiners portal
2019-03-21T22:53:41
https://kiswahili.tuko.co.ke/295609-vijana-kutoka-baringo-wamzomea-uhuru-kutokana-na-maendeleo-duni-eneo-hilo.html
tim burton viungo | stories reviews and zaidi on fanpop | sorted kwa rating | page 6 1042956 viewers kuwa shabiki onyesha viungo vya tim burton (5160 of 174) imewasilishwa kwa mrslovett_love zaidi ya mwaka mmoja uliopita first burtonesque now thisa chuo kikuu chuo kikuu cha of new brunswick researcher has named a new strangelooking seaweed after quirky film director and writer tim burton euthora timburtoni lala land records presents the world premiere release of the film version of danny elfman's acclaimed original score to the 1989 warner bros blockbuster batman starring jack nicholson michael keaton and kim basinger and directed kwa tim burton
2019-11-17T02:26:46
http://sw.fanpop.com/clubs/tim-burton/links/page/6?sort_method=rating
boss ngasa official website wizkid amtolea uvivu shabiki wa tanzania aliemtukana instagram wizkid amtolea uvivu shabiki wa tanzania aliemtukana instagram baada ya mtv ema kumpatia alikiba tuzo ya african act kutoka kwa wizkid mashabiki wa tanzania hasa wa alikiba wamevamia ukurasa wa instagram wa star huyo wa nigeria na kumtukana leo wizkid ameshindwa kuvumilia baada ya shabiki mmoja kumtukania mama yake
2017-02-21T12:00:57
http://www.bossngasatz.com/2016/11/wizkid-amtolea-uvivu-shabiki-wa.html
tigo wateja wafurahia huduma za kibiashara za uhakika | mwanaharakati mzalendo ™ home » »unlabelled » tigo wateja wafurahia huduma za kibiashara za uhakika muda 112100 am
2018-01-18T23:09:14
http://mwanaharakatimzalendo.blogspot.com/2017/04/tigo-wateja-wafurahia-huduma-za.html
lenzi ya michezo pazia la ligi kuu tanzania bara kufunguliwa leo pazia la ligi kuu tanzania bara kufunguliwa leo ligi kuu ya vodacom tanzania bara msimu wa 2016/17 inatarajiwa kuanza leo kwa michezo mitano huku bingwa mtetezi young africans ya dar es salaam ikisubiri hadi agosti 31 2016 kuanza kutetea taji lake michezo itakayochezwa leo ni pamoja na simba itakayoikaribisha ndanda fc ya mtwara kwenye uwanja wa taifa dar es salaam katika mchezo utakaoanza saa 1000 jioni wakati azam itakuwa mwenyeji wa african lyon kwenye uwanja wa azam fc ulioko chamazimbagala nje kidogo ya jiji
2018-02-20T11:33:00
http://pallangyor.blogspot.com/2016/08/pazia-la-ligi-kuu-tanzania-bara.html
msanii afande sele amponda jk | jamiiforums | the home of great thinkers discussion in 'jf chitchat' started by tanmo mar 23 2011 wakuu hii nimeikuta kwenye blog moja ya kitanzania afade sele akionesha hisia zake juu ya ujanja ujanja wa mheshimiwa rais wetu jk kwa maelezo yake anaona kuwa jk anakusudia kuleta tofauti miongoni mwa watu wa kada mbali mbali msanii huyu anasema hivi ah huyu jk kwa tamko lake hili kuhusu studio aliyowapa tht na ruge anaonyesha jinsi gani asivyo kiongozi makini na kwa mtazamo halisi anaonyesha ni jinsi gani hakustahili kuwa mkuu wa nchi ​ anajenga makundi ya chuki na uhasama katika kila sekta kuanzia kwenye chama chake serikali yake na sasa kwenye sanaa na haswa mziki wetu ambao ndio amekuwa akijinadi kuusaidia kumbe katika hii awamu yake ndio mziki umepotea mwelekeo ​ sasa kama anasema studio aliwapa waliomuomba mbona mimi na watu wengine wenye misimamo tulikuwepo siku ile alipoahidi studio hatujui lolote na hatujaonyeshwa hiyo studio​click to expand kwanza huyu mkuru anajuwa anachokifanyazaidi anafata mkumbo tu etii mziki hicho ndio anachojuwa sio kuangalia watu wenye maisha duni na kumwaga hizo hela kwao wakuu hii nimeikuta kwenye blog moja ya kitanzania afade sele akionesha hisia zake juu ya ujanja ujanja wa mheshimiwa rais wetu jk kwa maelezo yake anaona kuwa jk anakusudia kuleta tofauti miongoni mwa watu wa kada mbali mbali msanii huyu anasema hiviclick to expand blog ipi kaka naona kama umefumba macho mwache jk kama alivyo kabanwa pande zote zote jk aliyeingia madarakani 2005 ni tofauti na huyu tunayemwona ni kama mwili tu umebaki anaendesha tanzania ilimradi siku ziende hatari sana kabidilika sana suala dogo tu kama la studio katoa mpya badala ya kuwapa wasanii wote ajabu yeye kadai anawapa wale waliomwomba ajabu kweli kwani waliopewa ndio walioomba kwani mimi nilivyoona wengi waliokuwepo siku hiyo sijaona hata mmoja aliyefikiriwa matokeo yake kasababisha migogoro baina ya wasanii sasa migogoro imehama kutoka ndani ya ccm hadi kwa wasanii kugombea studio ya jk huyo ndio jk na kauli yake kwanini tugombanie fito wakati tunajenganyumba mmoja yaani afande sele anashtuka leo kuwa jk msanii mbona lipumba alishasema toka 2005 kuwa jamaa labda apewe wizara ya michezo wwwafandeseleampondajkblogspotcom wwwafandeseleampondajkblogspotcomclick to expand hahahaha hii link unaongea na mkuu wa kaya livenimeipenda bongo star link nimepokea sms kutoka kwa afande sele
2016-10-25T21:05:38
http://www.jamiiforums.com/threads/msanii-afande-sele-amponda-jk.120625/
timu ya simba kushushwa daraja na fifa kama isipofanya haya | pamoja blog » timu ya simba kushushwa daraja na fifa kama isipofanya haya timu ya simba kushushwa daraja na fifa kama isipofanya haya 5/07/2016 124100 pm rais wa fifa gianni infantino
2016-12-05T08:29:40
http://www.pamoja.co.tz/2016/05/timu-ya-simba-kuishushwa-daraja-na-fifa.html
adaptation anglais us > anglais australie translation and interpreting jobs prozcom the translation workplace andikisha ingia misingi ya prozcom kiswahilikiswahili ←chinese汉语deutschenglishitalianonederlandsespañolfrançaismagyarpolskiportuguês (br)românăčeštinaрусскийعربي日本語more languages watumiaji nenda makala nenda wateja nenda majukwaa nenda maswali yaulizwayo mara kwa mara nenda nyumbaninyumbanimaskani yangu ya prozcom jiunge na prozcom jifunze zaidi kuhusu prozcomistilahimtandao wa msaada wa tafsirikudoz™tazama maswalitafuta nenouliza swaliviongozifaharasa za kudozfaharasa ya gbknyenzo nyingine za istilahiwasilisho la faharasakamusi na marejeotafuta neno kwa mtandaofaharasa za kibinafsijifunze zaidi kuhusu istilahi katika prozcomkazi na orodha mbalimbalimipangio ya orodhawatafsiri na wafasirimakampuniblue boardwanafunzimakundi ya kutafsirivyama vya watafsiritafuta kwa jinaorodha pevu mbalimbalisearch by emailkazi zilizowekwatafuta kaziorder translationtuma kaziscreened professionals (pools)interpreter pooltranslation centernew search option nakōdo expert finder [tmtown]jifunze zaidi kuhusu kazi & orodha mbalimbali katika prozcomshughuli za wanachamajumuiyamabarazacertified pro networkmashindano ya kutafsirimaoni ya harakabadilishavideo translation newsmiongozo ya kitaalamumpango wa unasihimawasilishi ya habariwhat translators are working onmatukio ya mtandaoni na nje ya mtandaonimakongamano baina ya watu binafsimikutanomakongamano ya mtandaonicalendarjifunze zaidi kuhusu shughuli za wanachama na wanachama wa prozcomelimukozi zinazohitajikamafunzo ya kujipimia mudavideomafunzo ya mmojanamwinginemarejeokozi ratibiwawavuminamafunzo ya mtu binafsimafunzo ya mtandaonimafunzo ya sdl tradoseneomaarifatranslation industry reportskiwanda cha tafsiri cha wikimakalavitabuscam alert centertrainerscreate a coursemanage coursesabout trainersjifunze zaidi kuhusu elimu katika prozcomvifaazana za prozcomprozcom apitgb (ununuzi wa kikundi)service agreementsada za jamiiutumaji wa invoicekibadilisha vipimokikotoo cha gharamahifadhiweb widgetszana za tafsirisdl tradoswordfastmemoqcafetran espressoto3000atril dèjà vustar transitacrossfluencywordfinderperfectit consistency checkersoftware comparison tooljifunze zaidi kuhusu zana | lsp toolskuhusumsaada na uwekaji nyarakakituo cha msaadasite guidance centermmm / uwekaji nyaraka kwenye tovutimisingi ya prozcomkanuni za tovutihali ya tovutiprozcomkuhusu prozcomuanachama wa prozcomprozcom mobilemaakaba ya jaridashuhudakutafsiri kwa lugha za asiliajiratranslator to blog wasimamiziprivacy policyhall of fame ideas quoting deadline expiredthe quoting deadline for this job passed at jun 20 2017 0000 gmt adaptation anglais us > anglais australie posted jun 19 2017 1430 gmt (gmt jun 19 2017 1430) uhakiki au taarifa zimetumwa kwa jun 19 2017 1454 gmt job type translation/editing/proofing job service required translation languages kiingereza aina ya lugha anglais us > anglais australie job description bonjour poster country ufaransa service provider targeting (specified by job poster) membership nonmembers may quote after 12 hours preferred native language lugha zinazolengwa uga wa mada michezo / michezo ya video / michezo ya kubahatisha / kasino quoting deadline jun 20 2017 0000 gmt delivery deadline jun 21 2017 0000 gmt about the outsourcer this job was posted by a blue board outsourcernote you cannot quote because the quoting deadline has passed the outsourcer has requested that this job not be reposted elsewhere x sign in to your prozcom account username password forgot your password or create a new account x prozcom ideas(powered by uservoice)viewideas submitted by the communitypostyour ideas for prozcomvotepromote or demote ideasget started now » translation industry jobsjobs posted by outsourcers seeking quotes from language professionals overviewjob listingspost a jobfaq try jobs for mobilebrowse jobs and manage your quotes anytime anywhere (memberonly)you may be interested in this prozcom wiki article on risk management for translators and interpreters the blue board is a searchable database of language job outsourcers with feedback from service providers and an important risk management tool prozcom members have full access to the blue board does this job require a cat tool or additional skills join your colleagues in purchasing software at the lowest price on the planet via prozcom translator group buy or improve your skills by taking one of the 100's of prozcom translator training courseswordfast protranslation memory software for any platformexclusive discount for prozcom users save over 13 when purchasing wordfast pro through prozcom wordfast is the world's #1 provider of platformindependent translation memory software consistently ranked the most userfriendly and highest value more info »anycount & translation office 3000translation office 3000translation office 3000 is an advanced accounting tool for freelance translators and small agencies to3000 easily and seamlessly integrates with the business life of professional freelance translatorsmore info » terminology | jobs and directories | member activities | education | toolsabout prozcom | misingi ya prozcom | kutangaza | msaada | faq | terms of usewafasiri hawa wanasimamia ufasiri wa prozcom kwenda kiswahiliteam coordinators mpasua msonobariteam members zubeir ndarawa secilia njau sarah wachilonga rehema wanguba matthias kavuttih aritamba bisansabatafadhali zingatia kwamba tovuti yote haijatafsiriwa kutafsiri tovuti kwa lugha za asili kunaendelea kwa vipindi sehemu za tovuti zinazotumika zaidi zikitafsiriwa kwanza ukipata kosa la kutafsiri kwa sehemu yoyote ya tovuti ambaye tayari imetafsiriwa kwa lugha asili tafadhali arifu mmoja wa wasimamizi wa kutafsiri kwa lugha asili walio orodheshwa hapo juukwa habari juu ya vile unavyoweza kusaidia kuunda tovuti hii kwa lugha ya kiasili tafadhali bonyeza hapahakimiliki© 19992017 prozcom haki zote zimehifadhiwa privacyfor another site operated by prozcom for finding translators and getting found see
2017-06-26T17:21:08
http://swa.proz.com/translation-jobs/1320701
fatty_mitty said nina zack said eka_amin said bella najat said eyqahana said farahin najwa said sitiahyat said hanis razali said nafiza headscarf said amos perry said
2018-12-16T09:31:56
http://peliks.blogspot.com/2012/07/hijab-tutorial.html?showComment=1342937632987
the continuous improvement process strengthen the 9783639407327 kununua kitabu home > utafutaji > 9783639407327 vitabu vyote kwa 9783639407327 linganisha kila kutoa 9783639407327 () au 3639407326 isbn (kuweka mbadala) 3639407326 9783639407327 kupata vitabu vyote inapatikana kwa namba yako isbn 9783639407327 linganisha bei haraka na kwa urahisi na kuagiza mara moja inapatikana nadra vitabu vitabu kutumika na mkono wa pili vitabu vya kichwa the continuous improvement process strengthen the organizational citizenship behavior in manufacturing companies a consulting approach kutoka bebersdorf peter zimeorodheshwa kabisa
2017-10-24T04:12:30
https://ke-sw.diebuchsuche.com/vitabu-isbn-9783639407327.html
msaada maumivu ya uso | jamiiforums | the home of great thinkers msaada maumivu ya uso discussion in 'jf doctor' started by husninyo aug 3 2011 habari zenu wote wandugu mwenzenu nasumbuliwa na maumivu ya uso siku ya tatu leo kuna yeyote anaweza kujua inatokana na nini na namna ya kutibu husninyo pole dear unapaka mafuta/cream gani siku zoote au labda niulize unatumia cream/lotion mpya (hujawahi tumia) au labda uko maeneo mageni (hali ya hewa) pole dearhuu uso unataka kuleta balaa sasahebu sema unaumaje na ni sehemu gani hasa tuushughulikie husninyo pole dear unapaka mafuta/cream gani siku zoote <br /> au labda niulize unatumia cream/lotion mpya (hujawahi tumia)<br /> au labda uko maeneo mageni (hali ya hewa)click to expand ahsante mpenzi huwa napaka bio oil na sabuni natumia silka ni kwa muda mrefu sasa kuhusu mazingira nilitoka dodoma to mwanza ila kwasahv nipo tena dodoma pole sana husninyo pole sana nimegoogle na kuona information fupi pain that starts in the face may be caused by a nerve disorder an injury or an infection in a structure of the face face pain may also begin elsewhere in the body sometimes face pain occurs for no known reason face pain is accompanied by chest shoulder neck or arm pain this could mean a heart attack pain is persistent unexplained or accompanied by other unexplained symptoms see a doctor source face pain medlineplus medical encyclopedia pole dearhuu uso unataka kuleta balaa sasahebu sema unaumaje na ni sehemu gani hasa tuushughulikieclick to expand yaani reception inataka kuharibika lol naumia wakati wa kuoga na nikimaliza kuoga nikishajifuta maji nakuwa napauka sana kwenye paji la uso nikipaka mafuta hata kama ni kidogo baada ya muda paji la uso linakuwa na ngozi fulani ya tofauti halafu panakuwa panang'aa maumivu ni kwenye paji na shavu la kushoto ahsante mpenzi huwa napaka bio oil na sabuni natumia silka ni kwa muda mrefu sasa kuhusu mazingira nilitoka dodoma to mwanza ila kwasahv nipo tena dodomaclick to expand husny naona vor kamaliza best wishes and get well soon pole sana husninyo pole sana nimegoogle na kuona information fupi <br /> source <a href=http//wwwnlmnihgov/medlineplus/ency/article/003027htm target=_blank>face pain medlineplus medical encyclopedia</a>click to expand ahsante vor bora nikaonane na dokta maana naogopa kufanya chochote nisije haribu husny naona vor kamaliza best wishes and get well soonclick to expand thanx ashadii naumia wakati wa kuoga na nikimaliza kuoga nikishajifuta maji nakuwa napauka sana kwenye paji la uso nikipaka mafuta hata kama ni kidogo baada ya muda paji la uso linakuwa na ngozi fulani ya tofauti halafu panakuwa panang'aa maumivu ni kwenye paji na shavu la kushotoclick to expand hizi ni side effect za make up za kichina usimtafte mchawi maumivu yakizidi nione mimi pole sanamuone daktari haraka hizi ni side effect za make up za kichina usimtafte mchawi<br /> maumivu yakizidi nione mimiclick to expand sijaruhusu kuchakachua sredi la ugonjwa kanisubiri chit chat nakuja ahsante kwa kuwa msikivu pole sanamuone daktari harakaclick to expand ahsante ndugu yangu ahsante kwa kuwa msikivuclick to expand nisamehe shetani alinipitikia sirudii tena pole mwaya kwa ushauri uliopewa kumbuka kuturudishia majibu baada ya matibabu maana ni somo kwa wengine pia pona haraka
2016-12-07T20:56:58
http://www.jamiiforums.com/threads/msaada-maumivu-ya-uso.160732/
mtoto wa kitaa kaseba vs cheka wolper vs wema kuoneshana umwamba siku ya saba saba kaseba vs cheka wolper vs wema kuoneshana umwamba siku ya saba saba msanii wa filamu nchini jaqlin wolper akizungumza na waandishi wa habari dar es salaam leo kuhusu mpambano wake wa masumbwi na wema sepetu utakaofanyika katika uwanja wa taifa siku ya sabasaba kocha wa bondia wema sepetu ambani msanii bondia rashidi matumla akiongea kwa niaba wakati wa kutambulisha mpambano uho leo picha zote na nawwwsuperdboxingcoachblogspotcom posted by salum suleiman lyeme at 1022 am
2018-04-21T15:38:13
http://mtotowakitaa.blogspot.com/2012/07/kaseba-vs-cheka-wolper-vs-wema.html
wakali kibao wamsindikiza chid benz club maisha teen tz wakali kibao wamsindikiza chid benz club maisha posted by teen newz on october 1 2012 at 1151am licha ya kuwa ilikuwa ni shoo maalumu kwa mkali wa michano bongo rashird makwilo chid benz wakali kibao kutoka tasnia ya muziki wa kizazi kipya bongo walijitokeza kutoa sapoti ya nguvu kwa nyota huyo aliyewahi kushinda mara mbili tuzo ya mwanamuziki bora wa hip hop hapa bongo miongoni mwa mastaa waliokuwepo kwenye shoo hiyo ni pamoja na mkali wa viuno khalid mohamed tid 'mnyamaa' albert mangwea 'ngwear' na wengine kibao shuhudia kupitia picha hizo tid mnyaamaa akiwakilisha saraha wa fundi samwenga naye kama kawa alitisha (mzee wa bistola) 2ndaman alikuwepo dallas (aka sumaku) kama kawaida na totoz mbili matata (leka dutigite) linex ambwene yessayah (ay) tags benz chid club kibao maisha wakali wamsindikiza like 0 members like this comment by julius on october 7 2012 at 424pm poa sana man chid naona shavu kubwa toka kaw anyamwez comment by emmanuel mushi on october 4 2012 at 1057am budah chidbenz ametsha one love broo comment by chamababy on october 4 2012 at 925am kul rss top news · everything haraseum yopmail posted a statushttp//nowstream4blogcom/2013/05/23/hannibalepisode91x9videoputlocker/1 minute ago 0 daniel albert custer posted a statushttp//wwwlinkinparkcom/xn/detail/3124652album7603111xg_source=activity5 minutes ago 0 april g bailey posted a statushttp//wwwlinkinparkcom/xn/detail/3124652album7602948xg_source=activity11 minutes ago 0 robert tendeje updated their profile12 minutes ago more rss
2013-05-24T03:35:53
http://www.teentz.com/profiles/blogs/wakali-kibao-wamsindikiza-chid-benz-club-maisha
alvaro molata asema hana mpango wa kuondoka real madrid | saluti5 home » soka » alvaro molata asema hana mpango wa kuondoka real madrid alvaro molata asema hana mpango wa kuondoka real madrid pamoja na wakati mgumu alionao ndani ya klabu ya real madrid ya hispania mshambuliaji alvaro molata amedai kuwa hana mpango wa kuachana na mabingwa hao wa ulaya
2017-10-19T14:23:03
http://www.saluti5.com/2017/01/alvaro-molata-asema-hana-mpango-wa.html
kufutwa kwa leseni iliyotolewa kwa kampuni ya augere tanzania limited tangazo la kufutwa kwa leseni iliyotolewa kwa kampuni ya augere tanzania limited (limetolewa chini ya kifungu 22 cha sheria ya mawasiliano ya kielektroniki na posta cap 316) kwa kuwa tarehe 1 juni 2011 mamlaka ya mawasiliano tanzania (ambayo kwenye tangazo hili itaitwa mamlaka) ilitoa leseni kwa kampuni ya augere tanzania limited (ambayo kwenye tangazo hili itaitwa mwenye leseni) kutoa huduma za kujenga miundombinu kutoa huduma kupitia miundombinu hiyo kutoa huduma kupitia mtandao wa mawasiliano na kutumia masafa ya mawasiliano kitaifa na kuwa mwenye leseni ameshindwa kujenga miundombinu na kuanza kutoa huduma kwa wateja ambavyo ni ukiukwaji mkubwa wa masharti ya leseni alizopewa kama ilivyoainishwa kwenye kifungu 21(a) na (b) cha sheria ya mawasiliano ya kielektroniki na posta cap 306 na kwa kuwa mwenye leseni ameshindwa kulipa ada za leseni hizo kama inavyotakiwa chini ya kifungu 15 (1) cha sheria ya mawasiliano ya kielektroniki na posta cap 306 na kwa kuwa kwa mujibu wa kifungu 6(3) cha sheria ya mamlaka ya mawasiliano tanzania cap 172 mamlaka imewasiliana na waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiiano kuhusu kufutwa kwa leseni hizo kwa hiyo sasa kwa uwezo iliyopewa kisheria mamlaka inafuta leseni zote zilizotolewa kwa augere tanzania limited mkurugenzi mkuu mamlaka ya mawasiliano tanzania machi2016 contact details
2017-03-23T16:13:27
https://www.tcra.go.tz/index.php/archive-panel/headlines-archive/285-kufutwa-kwa-leseni-iliyotolewa-kwa-kampuni-ya-augere-tanzania-limited
uhuru ruto raila kuzuru eneo la magharibi kwa mara ya kwanza baada ya maridhiano ▷ tukocoke uhuru ruto raila kuzuru eneo la magharibi kwa mara ya kwanza baada ya maridhiano maoni 1645 rais uhuru kenyatta anatarajiwa kufungua rasmi kongamano la ugatuzi mjini kakamega na naibu wake william ruto kulihutubia baadaye uhuru ruto na raila huenda wakapitia kisumu na kuwahutubia wakazi kabla ya kwenda kakamega kumekuwa na joto la kisiasa nchini hasa kuhusu umoja wa jamii ya waluhya gavana wa kakamega wycliffe oparanya kati ya jumatatu aprili 23 na ijumma aprili 27 atawakaribisha rais uhuru kenyatta naibu wa rais william ruto na kinara wa upinzani raila odinga wakati kongamano la mwaka huu la ugatuzi litakapoandaliwa katika kaunti yake uhuru ruto na raila wameratibiwa kuhutubu siku tofauti katika kongamano hilo la siku tatu kwenye matangazo ya moja kwa moja kwenye facebook oparanya alisema kuwa kongamano hilo litafunguliwa rasmi na rais uhuru kenyatta huku naibu wa rais william ruto akiwahutubia magavana na washikadau siku ya mwisho ya kongamano hilo gavana wa kakamega wyclifee oparanya atawakaribisha rais kenyatta naibuwake william ruto na raila odinga kakamega watakapohushuria kongamano la ugatuzi picha facebook/governor oparanya raila atahutubu siku ya pili ya kongamano hilo rais atafungua kongamano hilo siku ya kwanza na siku ya pili aliyekuwa waziri mkuu raila amollo odinga atawahutubia washikadau kuhusu ugatuzi siku ya tatu naibu wa rais william ruto atahutubu oparanya alisema ripoti zilizoifikia tukocoke zilisema kuwa huenda viongozi hao watatu wakasimama jijini kisumu na kuwahutubia wenyeji wageni 6000 watahudhuria kongamano hilo la tano tangu ugatuzi uanze kutekelezwa na serikali za kaunti hii itakuwa mara ya kwanza kwa wanasiasa hao watatu kuzuru eneo la magharibi baada ya maridhiano kati ya uhuru na raila ziara hiyo inajiri wakati joto la kisiasa limepanda kuhusu umoja wa jamii ya waluhya katika kubuni chama chao kimoja ziara ya uhuru ruto na raila inajiri baada ya maridhiano ya rais na kinara huyo wa upinzani na siasa za kubuni chama kimoja cha kisiasa cha jamii ya waluhya zikiendelea picha facaebook/raila odinga spika wa bunge la seneti ken lusaka na waziri wa ugatuzi eugene wamalwa wamepinga wito wa kubuni chama kimoja cha jamii ya waluhya lusaka alisema kuwa anaunga mkono umoja wa eneo hilo lakini sasa sio wakati wa kuendeleza siasa za 2022 spika huyo aliongeza kuwa ikiwa viongozi wa magharibi mwa kenyawanapanga kuunda chama basi chama chenyewe ni lazima kiwe na sura ya kenya nzima ili iweze kuwavutia wa maeneo tofauti nchini kalonzo musyoka apuuzilia mbali kuondolewa kwa mose wetangula kama kiongozi wa wachache katika bunge la seneti | tuko tv busia news homa bay county news vihiga county news kikuyu gospel music ghris my payslip gotv packages sheila mwanyigha age utalii college yaliyotokea hadi raila kushinda kesi ya kupinga ushindi wa uhuru wa kura ya agosti 8 2017 otiende amollo nguo za gavana awiti wa homa bay ni aibu kubwa hazileti heshima ahmednasir mgawanyiko wadhihirika ford kenya huku wetangula akitangaza kuuhama muunganao wa nasa
2018-07-18T14:19:35
https://kiswahili.tuko.co.ke/270992-uhuru-ruto-raila-kuzuru-eneo-la-magharibi-kwa-mara-ya-kwanza-baada-ya-maridhiano.html
mon jul 09 224500 eat 2018 mambo matatu yanayoifanya cecafa isisonge wengi watakumbuka michuano hii ilivyokuwa miaka ya kuanzia 1970 hadi takribani miaka ya mwanzoni mwa 2000 michuano hii ilivutia wadau wengi na ilishabihiana kwa ubora na michuano ya cecafa kwa timu za taifa michuano ya cecafa inayoendelea hapa nchini jijini dar es salaam imekosa msisimko uliozoeleka na hili linadhihirishwa na idadi ndogo ya watazamaji wanaoingia uwanjani kushuhudia mechi hizi zinapofanyika katika mashindano yote hayo hali imekuwa tofauti na binafsi naona kuna sababu nyingi zilizotufikisha hapo uongozi wa juu wa cecafa kutokuwa wabunifu michuano ya cecafa iwe katika ngazi ya mataifa au klabu imekuwa na changamoto kubwa ya kupata udhamini binafsi naona hili linachangiwa na sekretarieti ya cecafa inayongozwa na katibu mkuu kutokuwa na mikakati ya kiubunifu kuvutia wadhamini wa kutosha hili linaweza kuchangiwa na ama uongozi wa cecafa kutokuwa na mipango endelevu kutotimiza masharti ya wadhamini baada ya kuwa wamekubaliana au fedha inayokuwa imetolewa kutotumika ipasavyo ni kutokana na kutokuwa na ufadhili huo kwa muda mrefu mashindano haya yameshindwa kuwa na ratiba inayotambulika kama ilivyokuwa miaka ya zamani ambako kila mdau wa mpira wa miguu alijua cecafa ngazi ya klabu au timu za taifa itafanyika lini kutokana na kasoro hiyo vyama vya mpira vya nchi husika vinashindwa kuyaingiza mashindano hayo kwenye kalenda zao ambazo zingewezesha klabu vya nchi hizo kujipanga hususani vile ambavyo vimekuwa mabingwa mataifa ya ukanda huu kutokuwa na mipango stahiki ya kuendeleza mchezo huu ukanda huu ndiyo ulioko nyuma katika maendeleo ya soka afrika na hili linadhihirishwa na timu za ukanda huu kutofanya vizuri katika kufuzu fainali za chan afcon na kombe la dunia na hata katika ngazi ya klabu (mashindano ya klabu bingwa na kombe la washindi) kutofanya vizuri kwa timu zetu kunaendelea kupunguza uwezekano wa mashindano ya cecafa kupata wadhamini ni vyema cecafa kwa kushirikiana na wadau ikaweka mkakati maalumu ya kutuondoa hapo tulipokwama naamini hilo likifanyika timu zetu zitafanya vizuri na wadhamini watapatikana muda wa mashindano mashindano ya cecafa hayana ratiba maalumu huenda kwa kubahatisha na pale ambako mdhamini hupatikana taarifa hutolewa muda mfupi kabla ya mashindano kuanza hali hiyo inakuwa kero kwa timu ambazo zinatakiwa kushiriki hususan ngazi ya klabu kwa sababu huwa na mipangilio yake na idadi ya wachezaji wanaowatumia kwenye klabu kwa msimu huwa ni ndogo (isiyosidi 30) ambao wanatakiwa washiriki ligi za nyumbani za kimataifa na wengine timu zao za taifa klabu huamua ama ishiriki kwa kuwatumia wachezaji wasiokuwa tegemo au kujitoa katika mashindano hali zote hizo zinapunguza mvuto wa watazamaji kwenda viwanjani kuangalia mashindano hayo aidha cecafa walijua huu ni msimu wa kombe la dunia ambao wachezaji wote mahiri duniani wanashiriki hili limepunguza pia idadi ya watazamaji kwenda kuangalia mechi za cecafa kwa sababu huamua kukaa nyumbani kuangalia michuano hiyo nambari moja duniani kwa kuangalia upungufu huo ni vyema cecafa ikajitathmini na anguko hilo la mpira wa miguu katika ukanda huu ili msisimko uliokuwapo urudi tena na hadhi ya ukanda huu irejee baada ya kuzungumza na serikali makamu wa rais wa benki ya dunia (wb) kanda ya afrika dk hafez ghanem amesema kuna 11 hours ago samia azindua jeshi usu la kukabiliana na ujangili 13 hours ago asimulia mpambano polisi na majambazi ulivyokuwa 15 hours ago wakulima wa korosho 2168 wajazwa manoti 12 hours ago chuo cha tipm chawakumbuka wenye uhitaji
2018-11-18T05:31:35
http://mobile.mwananchi.co.tz/Mambo-matatu-yanayoifanya-Cecafa-isisonge/1597608-4654188-format-xhtml-r5u6qsz/mobile.mwananchi.co.tz
tra watumia saa sita kumhoji askofu kakobe | malunde 1 blog home » habari » tra watumia saa sita kumhoji askofu kakobe tra watumia saa sita kumhoji askofu kakobe watumishi 12 kutoka mamlaka ya mapato tanzania (tra) jana walitumia zaidi ya saa sita kumhoji askofu mkuu wa kanisa la full gospel bible fellowship (fgbf) zachary kakobe walileta barua yao kutaka kuonana na askofu desemba 30 sasa hatujajua labda leo wamekuja kuchukua majibu yao kwa sasa hamuwezi kuingia ndani labda msubiri nje ndiyo mtaweza kuonana nao watakapokuwa wakitoka alisema mwita
2019-07-22T16:17:45
https://www.malunde.com/2018/01/tra-watumia-saa-sita-kumhoji-askofu.html
 jinsi ya kuunlock modem na kuweza kutumia sim card yoyote teknokona teknolojia tanzania you are athome»huawei»jinsi ya kuunlock modem na kuweza kutumia sim card yoyote modem ya huawei e173 u1 jinsi ya kuunlock modem na kuweza kutumia sim card yoyote by mato eric on august 5 2016 huawei intaneti kutokana na ukuaji wa kasi wa matumizi ya intaneti kumepelekea makapuni ya simu za mikononi kubuni matumizi ya modem kwa ajili ya kuweza kupata huduma ya intaneti ingawa kuna makampuni mengi ya simu na kila kampuni ina modems zake na ushindani pia kuchukua nafasi yake kwa kila kampuni kuwa na huduma ya vifurushi vitakavyowavutia wateja suala la kujiuliza ni je buy metformin er utakuwa na modem kutoka kila kampuni kwa sababu huduma zao zimekuvutia buy erythromycin for fish hapana jambo la kuzingatia ni kuwa na 300 mg quetiapine modem moja ambayo itakuwezesha kutumia line yoyote hapa tutakuelekeza kwa kutumia huawei e173 fuata maelekezo kulingana na aina ya modem yako jinsi ya kuunlock huawei e173 modem pakua programu wezeshaji iitwayo huawei mobile partner kwa ajili ya windows os kama unatumia windows kwnye kompyuta yako baada ya kuopakua right click kisha bofya run as administrator kisha fuata maelekezo mpaka mwisho na kuistall weka sim card kwenye modem ambayo ni tofauti na kampuni ya simu kama ni modem ya airtel weka sim card ya tigo voda nk ila sio line ambayo ni kutoka kampuni hiyohiyo inazotoa modem unayotumia kisha subiri mpaka iwe detected usiinstall programu (mobile partner) iliyokuja na modem pakua na kuinstall dc unlocker ya hivi karibuni kisha ifungue na kuchagua huawei pia chagua auto detect(recomended) kisha bofya kitufe cha kutafuta(search) funga mobile partner pamoja na dc unlocker kisha download firmware toleo la hivi karibuni ondoa mafaili hayo katika mkusanyiko wa pamoja(zip) kisha right click kwenye setup na ifungue kama administrator install mpaka mwisho wa mchakato mzima wa installation restart dc unlocker kisha ifungue na kuchagua huawei pia chagua auto detect(recomended) kisha bofya kitufe cha kutafuta(search) kabla ya modem kufunguliwa lakini firmware ikiwa updated ili kuweza kufungua modem yako inabidi ulipie pesa kidogo kama tsh 9000 kwa kutumia paypal kisha bonyeza severs kuweza kuweka username na password ambayo utatumiwa kwenye email address yako bonyeza unlock kisha chagua read unlock code and auto enter to modem halafu bonyeza do job bonyeza sehemu ya kutafuta(search) kuhakiki kama modem yako imfunguka na utaona sehemu ya sim lock status imeandikwa imefunguliwa (unlocked) kwa kufuata hatua hizo utakuwa umeweza kufungua modem yako na kuweza kutumia simcard yoyote kwenye modem yako je umefanikiwa kuunlock tuambie katika comment daima teknokona inajalali vyanzo miappleme pamoja na mitandao mingine mbalimbali
2018-08-20T16:44:32
http://teknokona.com/jinsi-ya-ku-unlock-modem-na-kuweza-kutumia-sim-card-yoyote/
picha bodaboda kishapu waanzisha mradi wa samakirto awataka wasitumie faida kulipa faini | malunde 1 blog home » habari shinyanga » picha bodaboda kishapu waanzisha mradi wa samakirto awataka wasitumie faida kulipa faini picha bodaboda kishapu waanzisha mradi wa samakirto awataka wasitumie faida kulipa faini mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga (rto) anthony gwandu amezindua mradi wa ufugaji samaki kwa kikundi cha waendesha bodaboda wilayani kishapu kwa lengo la kujikwamua kiuchumi uzinduzi huo umefanyika jana desemba 15 2018 jirani na mto tungu mahali ambapo lilipo bwawa hilo la ufugaji samaki na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na maofisa wa polisi wa kikosi cha usalama barabarani wilaya na mkoa akizungumzia mradi huo mwenyekiti wa kikundi cha bodaboda wilayani kishapu daniel eva alisema walipata wazo hilo baada ya kuona maisha ni magumu na hivyo kuamua kuanzisha mradi huo wa ufugaji samaki aina ya kambale ambao watakuwa wakiwauza ili kujipatia fedha kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi alisema kikundi chao kina jumla ya wanachama 50 ambapo walichangisha fedha na kufikisha shilingi milioni mbili ndipo wakatafuta mtaalamu wa kuwapatia elimu hiyo ya ufugaji samaki kutoka shirika la redeso kwa kushirikiana na maofisa uvuvi kwenye kikundi chetu cha bodaboda huwa tunakopeshana fedha na kurudisha kwa riba ndipo tukaona ni bora kuanzisha miradi ambayo itatusaidia kujikwamua kiuchumi na tumeanza na mradi huu wa ufugaji samaki aina ya kambalealisema eva naye mwenyekiti wa mradi huo wa ufugaji samaki salumu geogre alisema vichanga vya samaki hao kambale 2000 walivifuata jijini mwanza kwa kununua kila kimoja shilingi 200 ambapo ndani ya miezi sita wanatarajia kuvuna na kuuza kwa shilingi 5000 hadi 6000 kwa upande wake mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu aliwapongeza bodaboda hao kwa kuanzisha mradi wa kujikwamua kiuchumi na kutoa wito kwao watii sheria za usalama barabarani ili fedha watakazozipata kwenye mradi huo wazitumie kwenye maendeleo na siyo kuishia kulipa faini alisema jambo waliloanzisha kikundi hicho cha bodaboda wilayani kishapu kinapaswa kuigwa na vikundi vingine na kuondoa dhana ya kudharaulika ili kazi hiyo ipate kuheshimiwa na kuonekana kama ajira nyingine pamoja na kuacha kujiingiza kwenye masuala ya kihalifu ili mkoa ubaki salama na tulivu kama ulivyo sasa mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akizindua mradi wa ufugaji samaki kutoka kikundi cha bodaboda wilayani kishapu kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi picha zote na marco maduhu malunde1 blog muonekano wa bwawa la ufugaji samaki la kikundi cha bodaboda wilayani kishapu ambalo lipo jirani na mto tungu wilayani kishapu ambalo lina jumla ya samaki 2000 aina ya kambale mwenyekiti wa kikundi cha bodaboda wilayani kishapu daniel eva akielezea namna walivyopata wazo la kuanzisha mradi huo wa kufuga samaki ili wapate kujikwamua kiuchumi afisa uvuvi wilayani kishapu moses zacharia akiwapongeza vijana hao wa bodaboda namna wanavyoonesha juhudi za kuweza kujiajiri wenyewe na kujipatia kipato na kuahidi serikali kuendelea kushirikiana nao sambamba na kutoa ushauri namna ya kuuendeleza mradi wao huo wa ufugaji samaki meneja miradi kutoka shirika la redeso charles buregela ambao wanajishughulisha shughuli za kuinua watu kiuchumi akizungumza kwenye ufunguzi huo wa mradi wa samaki anasema bodaboda hao walifuata na kuomba msaada wa elimu hiyo ndipo wakawapatia pamoja na kuwa wezesha nailoni ya kuhifadhia maji kwenye bwawa hilo na kuahidi kuendelea kuwa unga mkono mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akiwapongeza bodaboda hao kwa kuanzisha mradi huo kujikwamua kiuchumi na kutoa wito kwa kuzitii sheria za usalama barabarani ili fedha zao ziweze kuwa saidia katika maendeleo na siyo kuishia kulipa faini askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga wakishuhudia mradi huo wa ufugaji samaki kutoka kikundi cha bodaboda wilayani kishapu wananchi viongozi wilayani kishapu na maaskari wa kikosi cha usalama barabarani wakiangalia mradi huo wa ufugaji samaki maaskari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga wakiwa eneo la mradi wa ufugaji samaki mwenyekiti wa kikundi cha bodaboda wilayani kishapu daniel eva akiomba pia serikali iweze kuwaunga mkono katika mradi wao huo ili waweze kupanua wigo na kukua kiuchumi na taifa kwa ujumla mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akiwasisitiza bodaboda hao wawe na umoja uaminifu kwenye kikundi chao na mtu ambaye ataonekana kuanza kuwa mjanja mjanja wamtoe kabla hajawavuruga ili wapate kusonga mbele kimaendeleo mwenyekiti wa mradi wa ufugaji samaki salumu geogre akiwapatia chakula samaki hao bodaboda wakicheza muziki mara baada ya mradi wao wa ufugaji samaki kuzinduliwa bodaboda wakiondoka eneo la mradi tayari kwenda kucheza mpira wa miguu kati yao na jeshi la polisi katika uwanja wa shule ya msingi mhunze wilayani kishapu mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akisalimiana na wachezaji wa jeshi la polisi kabla ya kuanza mtanange kati yao na bodaboda mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akisalimiana na vijana wa bodaboda kabla ya kuanza mtanange kati yao na jeshi la polisi mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akiwa asa vijana wa bodaboda na askari polisi kuwa mchezo wao uwe wa amani pamoja na kudumisha umoja kati yao na kusiwepo na chuki tena bali washirikiane pamoja kuijenga nchi pamoja na kutoa taarifa za waharifu ili mkoa ubaki kuwa salama na amani mchezo ukiendelea kuchezwa kati ya vijana hao wa bodaboda wenye jezi nyeupe na askari polisi ambapo askari hao hadi dakika 90 zinakwisha waliibuka na ushindi wa goli moja lililofungwa na philipo michaeli kipindi cha pili askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga wakiangalia mpira wa miguu kati ya bodaboda na polisi mtanange ukiendelea kutazamwa vijana wilayani kishapu wakiangalia mpira wa miguu kati ya bodaboda na jeshi la polisi mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akiangalia mtanange kati ya askari polisi na bodaboda uliochezwa katika shule ya msingi mhunze wilayani kishapu mara baada ya kumaliza kuzindua mradi wa ufugaji samaki mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akimpongeza philipo michael ambaye alifunga gori la kuwapatia ushindi askari hao kati ya mchezo wao na bodaboda wilayani kishapu mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu mkono wa kulia akiingia ukumbini na mwenyekiti wa bodaboda wilayani kishapu daniel eva kwa ajili ya kusheherekea uzinduzi wa mradi huo wa ufugaji samaki wageni waalikwa pamoja na bodaboda wakiwa ukumbi kusheherekea uzinduzi wa mradi wa ufugaji samaki hafla iliyofanyika kwenye kumbi za shirecu wilayani kishapu mwenyekiti wa kikundi cha bodaboda wilayani kishapu daniel eva akifungua sherehe hiyo na kusema mikakati yao ya kujiendeleza kiuchumi ambapo pia wanatarajia kufungua eneo la kuoshea magari pamoja na pikipiki ili kupanua wigo wa kujikwamua kiuchumi wenyeviti wa bodaboda kahama na manispaa ya shinyanga nao wakijumuika na bodaboda wilayani kishapu kusherehekea uzinduzi wa mradi huo wa ufugaji samaki mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga anthony gwandu akizungumza kwenye sherehe hiyo na kuwataka bodaboda wajitambue na kujituma katika kazi zao sambamba na kutii sheria za usalama barabarani na kuukataa uhalifu bodaboda wakiwa ukumbini wakipata moja baridi moja moto askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga nao wakiwa kwenye hafla hiyo ya bodaboda wilayani kishapu burudani zikiendelea ukumbini ambapo bodaboda wakicheza na wake zao huku wakisema wamechoka kuambiwa wanaongoza kwa vitendo vya kutia mimba wanafunzi na wakati wao wana wake zao askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani shinyanga nao wakiburudika na bodaboda hao kwa kucheza muziki awali bodaboda wilayani kishapu wakiwa kwenye maandamano kwa ajili ya kumpokea mkuu wa kikosi cha usalama barabara mkoani shinyanga anthony gwandu kwa ajili ya kwenda kuzindua mradi wao wa ufugaji samaki aina ya kambare ambao utawainua kiuchumi
2019-05-24T20:00:44
https://www.malunde.com/2018/12/rto-samaki-boda.html
watanzania jitokezeni kuchangia huduma mbalimbali za kuokoa maisha ya mwenzako mwana wa makonda home habari watanzania jitokezeni kuchangia huduma mbalimbali za kuokoa maisha ya mwenzako watanzania jitokezeni kuchangia huduma mbalimbali za kuokoa maisha ya mwenzako mohamed ramadhan makonda sunday march 05 2017 habari watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kujitoa katika kuchangia huduma mbalimbali za kuokoa maisha ya wenzao kwa nyakati ambazo wao wanakuwa hawana uwezo wa kujihudumia kwa namna yoyote ile kutokana na hali hiyo waendesha pikipiki ambao ni kundi linalohitaji damu mara baada ya kupata ajali wahamasishwa kuchangia damu kwa hiari kwa kujitokeza kwa wingi kwa ajili wananchi wenzao na akiba kwao akiongea jana katika zoezi la uchangiaji damu lililofanyika mjini kibondo mkoani kigoma kwa kuwahusisha waendesha pikipiki maarufu bodaboda mkufunzi wa mafunzo ya udereva toka shirika linalojihusisha na utoaji wa mafunzo hayo la apec katema kazwika alisema watu wengi mahospitalini wamekuwa wakipoteza maisha kabla ya wakati kutokana na kukosa huduma ambazo ziko chini ya uwezo wa binadamu kazwika ambae pia alimwakilisha mkurugenzi wa shirika hilo respicius timanywa katika kufunga mafunzo ya waendesha pikipiki alisema kuwa pamoja na kampeni yao ya uhamasishaji wa wateja wao kujitolea kuchangia damu waendesha pikipiki wengi hasa makundi ya vijana yanakabiliwa na changamoto ya uelewa mdongo wa matumizi ya barabara na ukosefu wa fedha hali ambayo imekuwa ikisababisha ajali zisizo za lazima na kwakuwa wahanga wengi wa ajali ni madereva ndiyo maana wamekuwa wakiwashauri kuchangia damu nao baadhi ya waendesha bodaboda waliobahatika kuchangia damu amba ni damasi lushas na emmanuel kanegene walisema wameamua kuchangia damu kutokana na adha wanazopata watu mbalimbali mara wanapohitaji huduma hiyo kwa upande wake mteknologia maabara wa wilaya ya kibondo lina misanga alieleseza licha ya kusaidia wahanga wa ajali damu imekuwa ni hitaji muhimu katika kusaidia wanawake wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano na kupongeza uamuzi wa wote waliojitolea kuchangia na kusema ipo changamoto kubwa ya upatikanaji wa damu kwenye hospitali nyingi hapa nchini na katika zoezi hilo zimepatikana unit 25 habari/picha namuhingokibondo by mohamed ramadhan makonda at sunday march 05 2017
2018-04-23T05:18:28
http://mwanawamakonda.blogspot.com/2017/03/watanzania-jitokezeni-kuchangia-huduma.html
manyanyafoundation sio sifa ya mtu kujiunga chuo kikuu jiachie manyanyafoundation sio sifa ya mtu kujiunga chuo kikuu jiachie home > taarifa mbalimbali > manyanyafoundation sio sifa ya mtu kujiunga chuo kikuu elimu habari mbalimbali taarifa mbalimbali manyanyafoundation sio sifa ya mtu kujiunga chuo kikuu naibu waziri wa elimusayansiteknolojia na mafunzo ya ufundi(kushoto)engstella manyanya akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaamkulia ni naibu katibu mkuu wa wizara hiyo ya elimuprofsimon msanjila kozi za foundation katika vyuo zinazotolewa sio mfumo wa elimu uliopangwa na serikali kumfanya aliyepita kuwa na sifa ya kujiunga na chuo kikuu akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam naibu waziri elimu sayansi na teknolojia mhandisi stella manyanya amesema kozi za foundation katika vyuo haijawekewa mfumo ambao unatambulika mhandisi stella amesema utaratibu huo vyuo vimefanya vyenyewe hivyo serikali haiwezi kuukubali mfumo elimu hiyo amesema anaesoma foundation apewe cheti na kama atahitaji kujiendeleza asafishe cheti au asome mfumo ambao utamfikisha katika shahada amesema suala la watu waliosoma cheti kisha diploma na wakajiunga chuo kikuu hawako sahihi kutokana na vyeti hivyoamesema serikali inafanya maboresho ya elimu nchini kutokana na kibaoni vitu vingi ambavyo vimetokana na watu kwenda tofauti na mfumo wa elimu uliowekwa stella amesema wanaendelea kufanya maboresho katika diploma ya ualimu kuweza kuiondoaaidha amesema kuwa serikali haitaruhusu elimu kuwa holela kwa watu kuwa tofauti na mfumo uliowekwa item reviewed manyanyafoundation sio sifa ya mtu kujiunga chuo kikuu rating 5 reviewed by ahmad michuzi
2017-09-22T06:24:17
http://michuzijr.blogspot.com/2016/11/manyanyafoundation-sio-sifa-ya-mtu.html
auwa kisa madini harakati za mtanzania home » »unlabelled » auwa kisa madini mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mount meru kwa ajili ya uchunguzi wa daktari na majeruhi amelazwa katika hospitali hiyo akiendelea kupatiwa matibabu huku hali yake ikiendelea vizuri asanteni kwa kunisikiliza
2018-06-18T22:39:31
http://berthamollel.blogspot.com/2013/04/auwa-kisa-madini.html
nguvu zinazoweza kuongezeka zinaendelea katika mwenendo unaoongezeka habari na habari nguvu zinazoweza kurejeshwa hubakia katika hali ya juu katika mwaka uliopita nguvu zinazoweza kutumika kwa ujerumani zinazotolewa kuhusu saa 559 terawatts ya sasa ambayo iliruhusu kufikia 93 ya jumla ya matumizi ya umeme katika 2003 uwiano huu ulikuwa 79 kwa mara ya kwanza mitambo ya upepo nchini ujerumani ilitoa nguvu zaidi katika 2004 kuliko mimea ya majimaji na ujerumani pia ikawa kiongozi wa dunia kwa mara ya kwanza duniani ujenzi wa mifumo ya photovoltaic na nguvu imewekwa mfumo wa photovoltaic wa mwm 300 ujerumani kabla ya japan (280 mw) uwiano wa joto zinazozalishwa kutoka kwa nguvu zinazoweza kuongezeka pia imeongezeka kidogo zaidi mwaka jana hadi 42 nishati za jua na nishati ya nishati ya jua zinazalisha 2004 621 twh ya joto kuhusu 13 twh zaidi ya mwaka uliopita vyanzo vdi nachrichten 25 / 02 / 2005 rasilimali za uvuvi →
2018-12-12T21:16:25
https://sw.econologie.com/les-energies-renouvelables-restent-courant-ascendant/
siwezi kujiuzulu kwa fedha ya tegeta escrow prof tibaijuka | magazeti ya leo| tanzania news |tanzania today siwezi kujiuzulu kwa fedha ya tegeta escrow prof tibaijuka waziri wa ardhi nyumba na makaziprofesa anna tibajuka amesema kuwa hawezi kujiuzulu katika nafasi ya uwaziri kutokana fedha ya tegeta escrow akizungumza na waandishi na habari mapema leo jijini dar es salaam katika ukumbi wa hoteli ya hayyat regencyanna alisema kuwa udalali wake fedha hiyo ni kwa ajili ya wanafunzi katika shule za taasisi ya johansson girls education trust alisema fedha hiyo aliyoipata ni ni bil 166 ambazo zilitoka katika kampuni hotuba ya jk prof tibaijuka aombwa kujiuzulu prof muhongo awekwa kiporo rais jakaya mrisho kikwete akisoma hotuba yake kwa wazee wa mkoa wa dar es salaam kwenye ukumbi wa diamond jubilee jijini dar es salaam ( picha na adam mzee) ukumbi wa diamond jubilee ukiwa umefurika wazee waliokuja kumsikiliza mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano dktjakaya mrisho kikwete ukumbi ulifurika kila kona rais kikwete ameanza kuongea na wazee wa mkoa wa dar katika ukumbi wa diamond jubilee ambapo watanzania wanataraji atoe mwongozo kuhusu sakata la akaunti ya tegeta escrow na prof tibaijuka siwezi kuibeza tume ya warioba mjumbe wa bunge maalumu la katiba profesa anne tibaijuka ametofautiana na wajumbe wenzake wa chama cha mapinduzi (ccm) kwa madai kuwa kamwe hawezi kuibeza rasimu ya jaji mstaafu joseph warioba prof tibaijuka akataa kujiuzulu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi prof anna kajumulo tibaijuka akiongea na wanahabari hivi punde ndani ya hyatt regency hotel dar es salaam amesema haoni sababu ya kujiuzulu kutokana na sakata la akaunti ya escrow aongeza kuwa watu wanaona suala la kujiuzulu kama fasheni ila yeye hayupo katika fasheni hiyo prof anna tibaijuka agoma kujiuzulu maazimio mapya sakata la escrow mamlaka husika yashauriwa kutengua uteuzi wa prof tibaijuka prof muhongo jaji werema na maswi waziri wa madini na nishati profesa sospeter muhongo wabunge kwa pamoja wamekubaliana kuondoa maazimio 12 yaliyoletwa bungeni na kamati ya pac na kuleta maazimio mapya 8 ambayo yamekubaliwa mwanasheria mkuu wa serikalijaji frederick werema mojawapo ya maazimio hayo ni mamlaka ya uteuzi kutakiwa iwawajibishe na kushauriwa kutengua uteuzi wa waziri wa nishati na madini profesa muhongo mwanasheria mgawo escrow wamchanganya prof tibaijuka juhudi za waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi prof anna tibaijuka kujisafisha dhidi ya kashfa ya kunufaika na mgao wa zaidi ya sh bilioni 300 zilizochotwa katika akaunti ya tegeta escrow zimechukua sura mpya na sasa anaitumia shule ya wasichana ya barbro johansso bodi yake wanafunzi na wazazi kujinasua prof tibaijuka ambaye aligawiwa sh bilioni 16 katika fedha hizo tangu juzi ulianza mkakati wa kutoa matangazo katika magazeti na jana uliitishwa mkutano wa waandishi wa jk fedha za tegeta escrow ni za iptl rais jakaya kikwete amesema fedha zilizochotwa katika akaunti ya tegeta escrow hazikuwa zinafikia sh306 bilioni bali ni sh202 bilioni na zilikuwa mali ya kampuni ya kufua umeme ya iptl prof tibaijuka refuses to resign over escrow scam the minister of lands housing and human settlements professor anna tibaijuka yesterday said that resigning is not a fashion thus she will not resign until when the government proves that she is guilty escrow account scandal prof tibaijuka rock despite mounting pressures from the general public wanting her to resign over involvement in the tegeta escrow account lands housing and human settlements development minister prof anna tibaijuka has once again denied involvement in it and
2019-03-21T14:25:31
http://www.tanzaniatoday.co.tz/news/siwezi-kujiuzulu-kwa-fedha-ya-tegeta-escrow---prof-tibaijuka
karibu pr promotion blog maoni ya wadau wa blog ya pr kuhusu mishahara maoni ya wadau wa blog ya pr kuhusu mishahara mukoba (kushoto)akimwaga maneno kuhusu mgomo(picha ya prona) kwa miezi kadhaa sasa kumekuwepo na mjadala mkali nchini unaohusu maandalizi ya mgomo usiokuwa na kikomo kwa wafanyakazi wa nchi nzima ambao kwa mujibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakzi nchini (tucta) utaanza mapema mwezi ujao kama ilivyotegemewa taarifa za mgomo huo ambao wafanyakazi wanataka kuutumia kama silaha yao ya mwisho kudai haki na madai yao ya msingi zimezua taharuki karibu nchi nzima kuanzia serikalini mpaka kwa wananchi maana suala la mgomo wa nchi nzima tena usiokuwa na kikomo si kitu kidogo ati ndio maana haishangazi kuwa kumekuwepo na vikao kadha wa kadha pamoja na majadiliano ya hapa na pale vikiwemo pia na vitisho yote ikiwa ni katika kuhakikisha kuwa mgomo huo usitokee na kusababisha madhara makubwa kwa taifa tukiwa bado katika sintofahamu namna gani serikali inajipanga kutatua matatizo na madai ya wafanyakazi nchini ghafla serikali imeibuka na waraka unaoagiza sekta binafsi ipandishe mishahara ya wafanyakazi wake kwa asilimia 100 pamoja na kuwa zilikuwa habari nzuri kwenye maskio ya watanzania wengi walioko katika sekta binafsi nchini bado suala hkuwa ilo linaibua masuala na maswali yanayohitaji tafakuri ya kina na kupata majibu kwa mfano kwa nini serikali imeamua kuibuka na suala hili sasa bila ya kuonesha ni kiasi gani waraka wa namna hiyo uliowahi kutolewa miaka michache nyuma ulifanikiwa na waajiri katika sekta ya umma wakauitikia na kuutekeleza kadri ya maelekezo lakini pia kwa muda mrefu sasa sekta binafsi imekuwa ikilalamikia mazingira magumu ya kuwekeza na kuendesha biashara nchini wamekuwa wakitaja maeneo sumbufu kama vile ukosefu wa umeme wa uhakika miundo mbinu mibovu rushwa urasmu serikalini kodi kubwa ukwepaji wa kodi ushindani usio sawa baina ya bidhaa za ndani na za kutoka nje na mengine mengi masuala hayo yanayolalamikiwa ambayo hata viongozi wa serikali wamekuwa wakikiri hadharani kuwepo kwake kwa namna moja ama nyingine yamekuwa kikwazo kwa sekta binafsi kuzalisha kwa tija na hatimaye kumudu kuwalipa wafanyakazi wake vizuri maana si jambo linalohitaji utafiti tija katika uzalishaji ni moja ya sababu za kuwepo kwa viwango vizuri vya mishahara mahali pa kazi hivyo serikali ilipaswa ije na tathmini kuonesha namna gani waraka uliopita ulivyotekelezwa kwa kiasi gani ulifanikiwa au kukwama ili kutoka hapo ingeweza kuweka mazingira mazuri ya kuiwezesha sekta binafsi kustawi na hatimaye kumudu nyaraka kama hizo za serikali hilo litawezekana kama serikali itaendesha mambo yake kwa kushirikiana na sekta hiyo (kupitia mpango wa ppp) vinginevyo tamuko hilo la serikali la wiki iliyopita litachukuliwa kuwa ni mbinu ya kutaka kubadilisha uelekeo wa mjadala kwamba badala ya kuanza kujadili madai ya tucta wadau wahamishie mawazo yao kwenye mgogoro utakaozuka baada ya sekta binafsi kushindwa kutekeleza agizo hilo la serikali hatuna nia ya kuitetea sekta binafsi tunasisitiza kuwa wanaowajibu wa kuwalipa vizuri wafanyakazi wao ili nao pia wazalishe kwa bidii kwa ajili ya ustawi wa mtu mmoja mmoja kampuni taasisi na hatimaye nchi kwa ujumla lakini tunachosema ni kuwa serikali ifanye kazi yake ya kuweka mazingira mazuri na pia imalize suala moja baada ya jingine badala ya kutumia ujanja kwa kubadilisha hoja
2017-12-15T16:08:13
http://prhabari.blogspot.com/2010/04/maoni-ya-wadau-wa-blog-ya-pr-kuhusu.html
mbunge shabiby nondo ana umaarufu gani mnachafua serikali tu | mpekuzi mbunge shabiby nondo ana umaarufu gani mnachafua serikali tu mbunge wa gairo (ccm) ahmed shabiby amesema hakuna umuhimu mamlaka za serikali kutumia vyombo vya habari kuwaita baadhi ya watu kwa ajili ya kuwahoji kutokana na tuhuma wanazokabiliwa nazo shabiby amesema hayo bungeni mjini dodoma jana aprili 12 2018 huku akitolea mfano tukio la mwenyekiti wa tsnp ambaye pia ni mwanafunzi wa chuo kikuu (udsm) abdul nondo ambaye aliitwa na mamlaka ya uhamiaji kwa ajili ya kuhojiwa uraia wake na kusema kwamba vitendo hivyo vinaichafua serikali kwa kiasi kikubwa sasa hivi kuna watu kwenye utumishi ambao wanafanya mambo ya kuichafua serikali ya ccm kulikuwa na haja gani ya kumita yule kijana abdul nondo kumhoji sijui alete cheti cha kuzaliwa cha bibi cheti cha mjomba cheti cha babu mamlaka inashindwaje kufanya investigations zake (uchunguzi) ili kubaini ukweli mapaka iite wanahabari tunawapa watu umaarufu wakati kesi ipo polisi ipo mahakamani kuna watu wengine watatumia hiyo kitu kusema serikali ya ccm ikimtaka mtu inamuomba uraia wake sidhani kama serikali ina haja na mtu mdogo kama yule ambaye hata hana madhara yoyote alisema shabiby
2018-12-13T22:10:03
http://www.mpekuzihuru.com/2018/04/mbunge-shabiby-nondo-ana-umaarufu-gani.html
liverpool yatolewa michuano ya fa man united uso kwa uso na arsenal raundi ya nne bongo5com liverpool yatolewa michuano ya fa man united uso kwa uso na arsenal raundi ya nne contributor january 8 2019 1042 am baada ya mchezo huo tayari raundi ya nne imepangwa na iko hivi
2019-06-19T13:39:10
http://bongo5.com/liverpool-yatolewa-michuano-ya-fa-man-united-uso-kwa-uso-na-arsenal-raundi-ya-nne-01-2019/
sera za mazingira zainua matumizi ya vibanzi kwa ajili ya nishatifao | habari za un sera za mazingira zainua matumizi ya vibanzi kwa ajili ya nishatifao uzalishaji wa mbao kwenye jimbo la hainan nchini china (pichafao) uzalishaji wa bidhaa zote zitokanazo na mbao uliongezeka mwaka 2013 ikiwa ni mwaka wa nne mfululizo na hiyo ni kwa mujibu wa takwimu mpya zilizochapishwa leo na shirika la chakula na kilimo duniani fao taarifa zaidi na assumpta massoi fao imesema wakati utengenezaji wa mbao zitumikazo kwenye samani ujenzi na hata vibanzi vya mbao vitumikavyo kwenye nishati uliibuka baada ya mdororo wa uchumi wa mwaka 20082009 uzalishaji wa malighafi za mbao zitumikazo kutengeneza makaratasi ulidorora mwaka 20122013 chanzo cha mporomoko huo ni china ambaye ni mnunuzi mkubwa kupunguza uchapishaji kwenye makaratasi na badala yake mfumo wa elektroniki kutumika kusambaza taarifa fao imesema uzalishaji wa vibanzi vya mbao kwa ajili ya nishati uliongezeka kutokana na sera za nishati mbadala hususan huko ulaya ikieleza kuwa mwaka 2013 zaidi ya tani milioni 13 ziliuzwa duniani kote economic development|environment|habari za wiki|un affairs sg|women children population
2020-02-22T17:13:46
https://news.un.org/sw/story/2014/12/400892-sera-za-mazingira-zainua-matumizi-ya-vibanzi-kwa-ajili-ya-nishatifao
israel na hizbollah | matukio ya kisiasa | dw | 15072008 israel na hizbollah israel na hizbollah zabadilishana leo wafungwa baada ya baraza la mawaziri la israel kuidhinisha jana mpango wa kubadilishana wafungwa na chama cha hizbollah cha lebanon wafungwa hao wanatazamiwa kubadilishwa hii jumatano hii waziri mkuu ehud olmert wa israel na mawaziri wengine 21 waliupigia kura mpango huo licha ya upinzani mkali kutoka kwa idarasa ya usalama wa ndani ya israel shin bet na idara ya ujasusi ya israel mosadpia mawaziri 3 waliupinga mpango huo kubadilishana kwa maiti za wanajeshi wa israel kwa wafungwa wa kipalestina kuna mila na desturi zake za muda mrefuna hii ni sawa na kutumika ujerumani kama mpatanishi hali imekuwa hivyo hata mara hii baadae rais shimon peres alitia saini yake hati ya msamaha kwa samir kuntarmmoja kati ya wafungwa 5 wa lebanon aliekua muda mrefu zaidi kizuizini rais perez alisema msamaha wake ni kwa sharti kuwa hizbollah nchini lebanon inawaacha huru wanajeshi 2 wa kiisraeli eldad regev na ehud goldwasser kuntar akitumikia kifungo cha vipindi mbali mbali kwa pamoja katika gereza la israel kwa kufanya hujuma ya 1979 huko kaskazini mwa israelkatika shambulio hilo yeye na wenzake waliwaua askari polisi 2 wa israel pamoja na baba na msichana wake wa miaka 4 waliomchukua mateka mahkama ya sheria ya israel iliyakataa malalamiko ya dakika ya mwisho kutoka kwa ukoo mmoja wa askari hao kuzuwia mpango huu kusonga mbele malori 9 ya chama cha msalaba mwekundu ulimwenguni yamewasili israel kutoka nchi jirani ya jordan kuwasafirisha hadi lebanon baadhi ya maiti 199 za wapiganaji wa lebanon zilizokuwapo katika makaburi maalumu za maadui walifariki wajumbe hao wa chama cha msalaba mwekundu walikutana jana asubuhi na wafungwa hao 5 wa lebanon wanaoachwa huru hii leo katika gereza la hadarim la israel kabla mpango huo wa kubadilishana wafungwa leo kuanza kwa muujibu wa mapatano israel inapaswa kukabidhi maiti hizo 199 ili ikabidhiwe nayo wanajeshi wake 2 regev na goldwasser ambao wanafikiriwa wamefariki dunia wanajeshi hao 2 walitekwa katika hujuma ya kuvuka mpaka iliofanywa na wapiganaji wa hizbollah ambayo ilichochea vile vita vya mwezi mzima na lebanon hapo 2006 bila kupelekea kuachwa kwao huru idara za usalama za israel shin bet na mossad zinaupinga mpango wa kumuacha huru kuntar kwa kuwa zinahofia itakua kupoteza nafasi ya mwisho ya kujipatia taarifa madhubuti juu ya mwanahewa anatafutwa wa kiisraelron arad ndege ya arad iliangushwa katika anga la lebanon hapo 1986alizuwiliwa kwa miaka mingi na chama cha amal cha lebanon na halafu akatoweka bila kujilikana alipo ingawa hakuna anaeamini kuwa arad bado anaishiisrael iliendelea na juhudi za kumrejesha nyumbani au kujua hatima yakemara hii yaonesha kufikiwa shabaha hiyo hizbolla imetoa ripoti ambamo imearifu kuwa arad kiasi cha miaka 2 iliopita tangu kukamatwa yamkini ameuliwa ripoti hii ilikabidhiwa israel na mjumbe wa kijerumani aliekua anatumika pande zote mbilimtumishi wa zamani wa idara ya usalama ya ujerumani bnd gerhard konrad akipatanisha wakati ule baina ya hizbollah na israel na ndie alieandaa mpango wa hii leo wa kubadilishana wafungwa na maiti ingawa fungwa wa muda mrefu kuntar ni wa madhehebu ya druz na sio shiia hizbollah kilichopigana vita nchini lebanon na israel 2006 kilishikilia kuachwa kwake huru kuwa lazima kwa sababu hajakuwamo ndani ya ule mpango wa 2004 wa kubadilishana wafungwa tarehe 15072008 kiungo https//pdwcom/p/ed3t
2018-10-16T07:12:56
https://www.dw.com/sw/israel-na-hizbollah/a-3486723
recent content by greater thinker | jamiiforums recent content by greater thinker bro mimi ni mdau wa pb kwa muda mrefu sana tangu haijaanza kuitwa pb enzi za seven na jimmy kabwe wakaja wakina kp na fina na hando akiwa msoma magazeti wao mpaka wakaja wakina pj & hando so naielewa vizuri sana pb na huyu babra wa siku hizi si yule babra wa zamani ambaye hakuwa mkali hivi na kwa hyo bh siku hizi sio mkali hafoki hafoki sio busara bwana kumuita ' mleta magazeti ' hata kama jamaa hajapata mkataba bado so long as ashapata shavu la kuwa kwenye kipindi hilo jina waliminye tuna mimi wala sijazungumzia yeye kugombana na kp ni jinsi tu anavyoendesha mfumo mzima wa davidngonde soma hii kakaa machizi mmeniroga remix ya stamina kawachana hadi wcb video ashafanya na travellah wa ' kwetu studio ' soon itakuwa hewanithanks mkuu naomba namba yako ya simu tafadhali asante mkuu kwa ushauri yoo mapenzi tu mkuu siunajua kumridhisha tena mamaa msaada kwa shule ya bweni yenye a level mchepuo wa cba kibahakibiti do tyoo
2020-04-07T12:21:13
https://www.jamiiforums.com/members/greater-thinker.54296/recent-content
watanzania walijipanga kuikataa ccm | gazeti la jamhuri watanzania walijipanga kuikataa ccm wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu rais mstaafu wa awamu ya tatu benjemin mkapa akiwa tanga alisema kwamba dunia ingeshtushwa kama ingesikia kwamba watanzania wamekiangusha chama kikongwe kama ccm alisema kwamba ccm ni chama cha ukombozi kinachoendelea kuwakomboa watanzania lakini ukitaka kusema kweli dunia imeshtushwa kusikia kwamba chama kikongwe kama ccm ambacho kimechokwa na wananchi kimeshinda uchaguzi ni katika mazingira hayo watu wengi huamini kwamba ccm imeshinda uchaguzi baada ya kuiba kura madai kwamba ccm imeshinda uchaguzi baada ya kuiba kura yanatiliwa nguvu na mambo mengi kwa kuanzia inaonekana wazi kwamba ccm ilijua mapema kwamba isingeshinda uchaguzi huu kwa hiyo kwa mfano baada ya uchaguzi kuwa ni wa kushindanisha vyama ccm iligeuza kuwa wa kushindanisha wagombea kwa upande wa mambo yanayotilia nguvu madai kwamba ccm imeshinda kwa kuiba kura kuna mambo makubwa matatu kwanza ccm na serikali yake hawajawahi kutumia nguvu kuhusika katika kuwakataza wapiga kura kusimama mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura kama ilivyotumia mwaka huu rais jakaya kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa ccm alikataza tume ya taifa ya uchaguzi ambayo imeteuliwa na rais nayo ilikataza nalo jeshi la polisi lilikataza watu wanaendelea kujiuliza yote hayo yalifanyika kwa lengo la kulinda amani au kutoa nafasi ya kuibwa kura pili serikali ya ccm kupitia jeshi lake la polisi ilitumia nguvu kubwa katika kukamata kompyuta na simu za mkononi kuzuia matokeo ya uchaguzi yasikusanywe ingawa katika chaguzi za nyuma watu walikusanya matokeo bila matatizo kwa kweli kitendo hicho kilishangaza watu kwa sababu hatua iliyokuwa imechukuliwa na serikali ilikuwa ni kutangaza matokeo haikukataza kukusanya matokeo tatu wananchi wanaendelea kuamini kwamba sababu ya serikali kuzuia watu wake wasikusanye matokeo ilikuwa kuzuia wananchi wasijue wizi wa kura uliotokea ilibainishwa kwamba kura zilizotangazwa na tume ya uchaguzi zilitofautiana sana na zile ambazo wananchi walikuwa wakikusanya vituoni kwa mfano tunduma mbunge wa chadema alipata kura 32000 lakini mgombea urais kupitia chadema na ukawa edward lowassa alitangazwa kuwa amepata kura 6000 ilileta picha kwamba watu wa ukawa na mashabiki wao walikuwa wamempa mgombea ubunge kura 32000 lakini walimkataa mgombea urais kwa kumpa kura 6000 kwa hiyo wananchi wanaamini madai kwamba mgombea urais kupitia chadema na ukawa alipata kura 32000 sawa na zile alizopewa mgombea ubunge kupitia chadema biblia katika mathayo 1026 inatamka kwamba hakuna neno lisilositirika ambalo halitafunuliwa wala lililofichwa ambalo halitajulikana basi tukitaka kusema kweli mwaka huu watanzania walikuwa wamejipanga kuikataa ccm hata kabla dk john magufuli hajateuliwa na chama chake kugombea urais hii ni kusema kwamba dk john magufuli angeweza kushinda kwa kishindo kama watanzania wasingekuwa wamejipanga mapema kuikataa ccm kwa kifupi watanzania hawakumpa kura dk magufuli hawakumkataa yeye bali waliikataa ccm kwa kuwa katika kila uchaguzi ccm imehusishwa na wizi wa kura basi watanzania wanalikemea jambo hilo kwamba ccm imepona kwa kuiba kura hapa tuna kila sababu ya kukemea huu wizi unaoaminiwa kuwa unatokea kila mwaka wa uchaguzi kwanza ni jambo la hatari kwa umoja na usalama wa taifa wananchi wakiamini kwamba wanaendelea kutawaliwa na chama kilichoshindwa uchaguzi na ambacho wamekichoka pili ni aibu mbele ya mataifa ya nje chama kilichoshindwa uchaguzi kujidumisha madarakani kwa kutegemea kuiba kura na kulindwa na majeshi ubabe si sehemu ya utawala bora tatu ni jambo la hatari pia kuziba njia zote za wananchi kutafuta haki kwa kuwa waliotunga katiba ya nchi mwaka 1977 walitaka ccm itawale milele tanzania walipanga hilo liwezekane kwa kupitisha sheria ya kukataza matokeo ya urais yasihojiwe mahakamani katika hali ya kujulikana mapema kwamba tume ya uchaguzi ingetumiwa kuiba kura njia ya kutafuta haki ikazibwa lakini pia maandamano ni njia nyingine ya kidemokrasia ya kutafuta haki polisi wametumika vema kuziba njia hiyo ya halali ya wananchi kubainisha haki yao ni katika hali hii kuna haja ya ccm na serikali yake kukumbushwa kwamba nchi zote duniani zilizoziba mianya ya watu wake kutafuta au kupata haki zimejikuta zimekaribisha ugaidi utawala wowote hauwezi kuzuia ugaidi kama unakandamiza haki za watu bila haki hakuna amani ni kauli ambayo baba wa taifa mwalimu julius kambarage nyerere alizoea kuitoa lakini kuiba kura ni matokeo ya watu kukosa hofu ya mungu ni matokeo ya kutaka kujipatia madaraka kwa nguvu ya shetani tukiangalia biblia tunakuta kwamba kitabu hicho ni mkusanyiko wa vitabu vitakatifu visivyopungua 60 miongoni mwa vitabu hivyo vipo waraka wa paulo mtume kwa warumi katika warumi 13 17 paulo mtume anafundisha elimu ya uraia anaanza kwa kuandika kwamba kila mtu na atii mamlaka iliyo kuu kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa mungu basi kwa muda mrefu dunia iliendelea kuamini kwamba mamlaka yote hutoka kwa mungu lakini baada ya yesu kristo kujaribiwa na ibilisi jangwani watu wanajua si kila mamlaka inatoka kwa mungu mamlaka nyingine hutoka kwa shetani katika mathayo 4 89 tunasoma kwamba ibilisi alimchukua yesu kristo mpaka mlima mrefu mno akamwonyesha milki zote za ulimwengu na fahari yake akamwambia haya yote nitakupa ukianguka kunisujudia basi ibilisi au shetani hutoa uwezo wa utawala kwa mtu au kundi lote la watu linaloanguka na kumsujudia chama chochote na serikali yake lazima viheshimu hiyo haki viepuke kuiba kura lazima watu wawe na hofu ya mungu kujipatia mamlaka kwa kuiba kura ni kumsujudia shetani lakini hapa ni jambo la kutia faraja kuona uwezo mkubwa wa mungu kupangua mipango mibovu ya mwanadamu kwa mfano tunajua kuwa viongozi wakuu wa ccm kwa sababu zao binafsi hawakupenda edward lowassa apate nafasi ya kuwa rais kwa hiyo walilikata jina lake mapema wakaleta kwenye vikao vyao vya uteuzi majina ya watu watano bila jina la lowassa aliyeonekana kukubalika ndani na nje ya chama kwa hiyo mungu alitumia wajumbe wa kamati kuu na wa halmashauri kuu ya ccm wafuasi wa lowassa kupangua majina ya watu walioandaliwa kupitishwa katika kinyanganyiro hicho walikuwa wafuasi wa lowassa walioamua kuwaengua bernard membe na january makamba kwenye mbio hizo kisha wakapanga kuwaengua dk asharose migiro na balozi amina salum ali wakampitisha dk magufuli ni muhimu hili lijulikane kwamba waliompitisha dk magufuli ni wafuasi wa lowassa waliotumia wingi wao kuwaadhibu viongozi wakuu wa ccm kwa kumwengua lowassa kwa njia ambayo haikuendana na katiba ya ccm baada ya maelezo hayo sasa tunaweza kuzungumzia sababu zilizofanya watanzania kujipanga kuikataa ccm kwanza watanzania wanaangalia ccm kama chama cha ukandamizaji na si chama cha ukombozi kama inavyoendelea kudaiwa ccm kama chama inaonekana inaongozwa na watu waliotawaliwa na ubinafsi wasiojali watu wengine wananchi wanajua fika kwamba ni chama cha tanu kilichokuwa chama cha ukombozi ni tanu iliyoikomboa tanganyika (tanzania bara) baada ya hapo tanu iliendeleza ukombozi wa wananchi kwa kuanzisha azimio la arusha mwaka 1967 lililokuwa na lengo la kuleta hali bora ya maisha kwa kila mwananchi na tanu ilifanikiwa kutimiza lengo hilo wananchi walipata elimu bure matibabu bure na maji bure juu ya yote azimio la arusha lilifuta matabaka mwaka 1977 ikazaliwa ccm mwaka 1991 ccm ilifuta azimio la arusha lililowakomboa watanzania kuanzia wakati huo watanzania wamerejea tena kwenye matabaka aliyotuachia mkoloni watoto wa maskini wanapewa elimu duni na michango ya shule inayowaumiza wazazi haihesabiki watoto wa wakubwa wanasoma nchi za nje na hapa nchini kwenye shule za watu binafsi wanakopewa elimu bora maskini watanzania wana hospitali zisizo na dawa wala vitanda wagonjwa wanalala sakafuni na wanaobahatika kupata vitanda wanalala wawili wawili wakubwa wanatibiwa nje ya nchi au hapa nchini katika hospitali za watu binafsi zinakopatikana dawa maskini watanzania hawana maji wala umeme wa kuaminika wakubwa wana maji na umeme wa haraka ni katika mazingira haya mwaka huu watanzania waliunga mkono juhudi za kutaka mabadiliko zilizoongozwa na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi (ukawa) mabadiliko wanayotaka wananchi siyo ya kupewa fedha za serikali kama inavyopotoshwa ni mabadiliko ya wananchi kupata maji na dawa watoto wao kupata elimu bora michango ya shule kudhibitiwa na serikali na kadhalika kwa kuwa viongozi wa ccm na wa serikali wamenufaika na hali mbaya iliyoendelea kuwakumba wananchi wameendelea kupinga wazo la mabadiliko hata hivyo wananchi wamefaidika na kauli za rais dk magufuli aliyoendelea kuitoa wakati wa kampeni kwamba yeye atawaletea watanzania mabadiliko ya kweli na wapo waliompigia kura kwa kuamini kwamba kweli ataleta mabadiliko hali ya wakubwa kuendelea kuishi maisha bora huku wanaowaongoza wakiendelea kuishi maisha duni imefananishwa na utawala wa makaburu iliyowakandamiza na kuwabagua waafrika lakini watu wengine wamekwenda mbali zaidi wanauona utawala wa ccm mbaya zaidi kuliko wa makaburu kwa sababu ni utawala wa waafrika wachache walioamua kuwakandamiza na kuwabagua waafrika wenzao ni katika hali hiyo tena watanzania walijipanga kuikataa ccm chama kilichojipambanua kuwa ni chama cha ukandamizaji watanzania walijipanga kuikataa ccm pia kwa sababu ccm na serikali yake vimejali zaidi maendeleo ya vitu badala ya kujali maendeleo ya watu ni kweli wamejenga na wanajivunia barabara lakini wameacha watu hawana maji wala umeme wa kuaminika ni kweli pia kwamba wamejenga shule lakini wameacha watoto wa maskini wakipata elimu duni na badala yake wanakaa sakafuni madarasani vilevile ni kweli kwamba wamejenga hospitali lakini wameacha watu bila dawa na baadhi ya wagonjwa wanalala sakafuni halafu akinamama wanaotaka kujifungua hujinunulia vifaa vya uzazi kwa hivyo watanzania walijipanga kuikataa ccm na katika juhudi zao za kutafuta mabadiliko walitafuta utawala wa chama kingine ambacho kingejali maendeleo ya watu badala ya utawala wa ccm ulioweka mbele maendeleo ya vitu bei ya vyakula haikamatiki na hasa baada ya kuingia madarakani serikali ya awamu ya nne kwa hiyo watanzania walio wengi hupata mlo mmoja kwa siku na wengine hulalia maji kwa hiyo watanzania walijipanga kuikataa ccm ili wapate chama ambacho serikali yake ingejali maisha yao kwa kudhibiti bei ya vyakula serikali ya ccm imeua viwanda vilivyojengwa na serikali ya tanu kwa hiyo vijana wengi hawana ajira lakini wakati huo huo wananchi wanajitafutia ajira kama wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) mama lishe na bodaboda serikali ya ccm imewasumbua imewanyanyasa na imewapora vitu vyao na fedha zao na kuwaacha hawana uwezo wa kurejesha mikopo hii ilikuwa ni sababu nyingine ya watanzania kujipanga kuikataa ccm halafu japokuwa alama ya ccm ni jembe na nyundo ccm na serikali yake haikujali wakulima wala wafanyakazi alama hiyo imebaki kuwa mapambo tu wakulima wameendelea kukopwa mazao yao na walipodai malipo wamesumbuliwa vile vile wakulima wamepangiwa bei ya mazao na wanunuzi kwa kuwa serikali ya ccm imeshindwa kusimamia vyama vya ushirika na kwa upande wa wafanyakazi walimu madaktari na wauguzi ama hawakupewa haki zao au wamecheleweshewa haki zao kwa mfano mtu anapandishwa daraja lakini hapewi malipo yanayolingana na daraja lake hizi zilikuwa sababu za wakulima na wafanyakazi kujipanga kuikataa ccm wakati huo huo serikali ya ccm imeshindwa kusimamia maliasili ya nchi na uchumi wa taifa madini ya tanzanite ambayo hupatikana tanzania tu yamenufaisha zaidi wananchi wa kenya afrika kusini na india kuliko watanzania wenyewe wanyamapori wa tanzania wamesombwa usiku kupitia viwanja vya ndege vinavyolindwa ujangili tanzania umepoteza asilimia 63 ya tembo wote nchi katika miaka hii minne mikataba mibovu ya madini na vitalu vya wanyamapori vimenufaisha zaidi wageni na wakubwa kuliko wananchi fedha za umma zimeibwa katika halmashauri za wilaya zisizopungua 70 na hakuna aliyechukuliwa hatua hizi zilikuwa sababu nyingine za watanzania kuikataa ccm halafu kuna masuala sugu ya rushwa na ufisadi ambayo kila mtu anaamini kwamba utawala wa ccm hauwezi kuikomesha rushwa na ufisadi mambo hayo yamekuwa ni sehemu ya uhai na maisha ya ccm kwa upande wa rushwa si kama tu ccm imeendelea kutoa rushwa ya khanga fulana na kofia kwa wanachama wake ili waipigie kura bali pia ccm kupitia wabunge wangi iliwahi kupitisha sheria iliyoruhusu kutoa rushwa kwa wapigakura (takrima) licha ya sheria hiyo kufutwa na mahakama bado rushwa inatumika katika kusaka kura kwa kuwa chama tawala kimehusishwa na utoaji rushwa matokeo yake yamekuwa wananchi kukosa haki polisi na mahakamani lakini pia tanzania imedhalilishwa kutokana na kukithiri rushwa nchini na kwa upande wa mafisadi ndani ya ccm mtu haitwi fisadi mpaka ahame ccm akiendelea kubaki ccm fisadi huendelea kuonekana mtu safi sana kwa hiyo ndani ya ccm bado wako mafisadi wa epa rada na tegeta escrow bado ni jambo la kubahatisha kutegemea kwamba ufisadi utakomeshwa nchini na rais kutoka ccm ccm ina tabia sugu ya viongozi wake kulindana kwa hiyo rais kutoka ccm anaweza kuwa safi lakini baadaye anageuka kuwa mla rushwa fisadi mbinafsi kwa kuwa hiyo ndiyo tabia sugu ya mfumo wa utawala wa ccm watanzania wanawajua watu waliochotewa mamilioni ya fedha za tegeta escrow kutoka benki ya mkombozi lakini serikali ya ccm imeendelea kuwaficha na kuwalinda watu wa ikulu waliochotewa mabilioni ya fedha hizo kutoka benki ya stanbic basi tabia ya serikali ya ccm ya kuwalinda wala rushwa na mafisadi ni sababu nyingine iliyofanya watanzania kujipanga kuikataa ccm watanzania wanaamini kwamba rais kutoka ccm hawezi kupambana na rushwa wala ufisadi kwa kuwa maovu hayo yamekuwa ni sehemu ya utawala wa ccm kwa ujumla watanzania walikuwa na sababu nyingi za kujipanga kuikataa ccm baada ya kuona kwamba ccm kama chama tawala imeshindwa kutawala kwa ujumla kutawala ni kudhibiti uhalifu kuwapa watu huduma bora za jamii na kuwapa raia haki zao serikali ya ccm imeshindwa kufanya hayo lakini pia watanzania walijikuta wamejipanga kuikataa ccm baada ya kuona kwamba chama hicho tawala kimeshindwa kusimamia serikali yake serikali ya ccm hasa ya awamu ya nne haikuwa sikivu na ilijiona iko juu ya chama chake kwa mfano chama tawala kilipotaka mawaziri mizigo waondolewe serikali iliwatetea na kudai kuwa walikuwa watu safi yote hayo ni matokeo ya mtu mmoja kuwa kiongozi wa chama pia wa serikali mwisho sisi sote tunajua kazi ngumu inayomkabili rais john magufuli katikati ya nchi ambayo serikali iliyomaliza muda wake iliboronga karibu kila kitu rais magufuli ana kazi ngumu ya kurejesha imani ya wananchi iliyopotea juu ya ccm hapa isisitizwe tena kwamba katika uchaguzi uliopita wananchi hawakujipanga kumkataa dk magufuli walijua kuwa ni mtu mzuri lakini wananchi wamekata tamaa kiasi cha kuamini kwamba rais kutoka ccm hawezi kuleta mabadiliko kwa kuwa mfumo wenyewe unatoa nafasi kwa rais kuwa naye mla rushwa fisadi na mbinafsi hivyo ndivyo wanavyoamini wananchi ni katika mazingira hayo watanzania walikuwa wamejipanga kumchagua lowassa mfuasi na mcha mungu na mvumilivu aliyechafuliwa sana bila kujibu neno kwa ujumla watanzania wanamwangalia lowassa kama mzalendo na mwenye mapenzi ya kweli kwa watanzania ikumbukwe kwamba hakuna kiongozi wa tanzania aliyejali tatizo la watoto wa maskini waliokuwa wakirudi nyumbani kwa maelfu baada ya kumaliza elimu ya msingi alikuwa lowassa aliyesimamia kwa ufanisi mkubwa ujenzi wa shule za sekondari za kata hii ni kusema kwamba watanzania wamekata tamaa kabisa na matokeo ya uchaguzi kila mtu anayetarajia kwamba dk magufuli ataongoza safari ya mabadiliko ambayo lowassa hakupewa nafasi ya kuongoza previous seif cuf waanza kuunda serikali zbar next vita dhidi ya ujangili imguse kila mtanzania mwenyekiti alivyoitafuna halmashauri ukerewe
2019-04-26T14:32:07
http://www.jamhurimedia.co.tz/watanzania-walijipanga-kuikataa-ccm/
raila odinga amwita ali kiba kenya atumiwa ndege binafsi | raha za walimwengu home » »unlabelled » raila odinga amwita ali kiba kenya atumiwa ndege binafsi raila odinga amwita ali kiba kenya atumiwa ndege binafsi dar es salaam upepo mwanana bado unaendelea kumpuliza staa namba moja wa bongo fleva ali saleh kiba king kiba baada ya mgombea anayewakilisha muungano wa vyama vya upinzani nchini kenya (nasa) raila omolo odinga kudaiwa kumuita nchini humo kwa mujibu wa chanzo kisicho na chembe ya shaka kiba anayesumbua kwa sasa na wimbo wake wa seduce me alipata mwaliko huo mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa ni saa chache mara baada ya odinga kushinda kesi ya uchaguzi katika mahakama ya juu aliyokuwa amemfungulia rais wa kenya uhuru kenyatta ambaye mambo yalimuwia mazito stori erick evarist| ijumaa wikienda
2017-09-26T12:58:12
http://www.rahatupu.us/2017/09/raila-odinga-amwita-ali-kiba-kenya.html
lowassa kwa siku 100 nitafanya mambo 13 bongoswaggzcom about us mgombea urais wa chadema na ukawa edward lowassa ametaja mambo 13 atakayoyafanya ndani ya siku 100 iwapo atachaguliwa kuwa rais huku akisema atawakata kilimilimi wanaombeza kuwa hawezi kuondoa umaskini wa wananchi lowassa alikuwa akihitimisha mikutano minne aliyofanya kwenye wilaya tatu za jiji la dar es salaam jana kwenye uwanja wa tanganyika packers kawe wakati lowassa akieleza hayo mwanasheria mkuu wa chadema tundu lissu alitangaza azimio la kawe lililobeba ajenda kuu tatu ikiwamo ya kumtaka rais jakaya kikwete kutoa mwongozo wa jinsi serikali yake itakavyokabidhi madaraka kwa ukawa kutokana na suala hilo kutokuwapo kikatiba huku mwenyekiti wa chadema freeman mbowe akitangaza mkesha kwa wananchi siku ya kuamkia tarehe ya kupigakura na kutaka wanaume wabakie kulinda kura zisiibiwe akizungumza kwenye mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya watu na viongozi wakuu wa ukawa lowassa alisema mambo hayo atayatekeleza kwa kasi ya kilometa 120 kwa saa lowassa alitaja jambo la kwanza atakaloanza nalo kuwa ni uhakika wa dawa na vifaa vya uzazi wa akinamama alitaja mambo mengine kuwa ni umeme wa uhakika nchi nzima kupunguza foleni jijini dar es salaam kuondoa kero kwa wafanyabiashara wadogowadogo na waendesha bodaboda kumaliza tatizo la maji nchi nzima mfumo bora na rafiki wa wafanyabishara wakubwa na wadogo kufuta ada na michango kwa wanafunzi kupunguza kodi ya mshahara kwa wafanyakazi kufuta kodi zote za mazao ya wakulima mkakati wa kukuza michezo na sanaa kuunda tume ya kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima kuanzisha kituo kila wilaya kwa ajili ya kutoa huduma za serikali na kuboresha maslahi ya polisi wanajeshi na walimu mbali na mambo hayo 13 aliahidi kumaliza kilio cha wananchi cha kupata katiba mpya inayotokana na maoni yao akisema ni suala linalohitaji kutuliza kichwa kulipatia ufumbuzi umaskini si mpango wa mungu alisema lowassa ambaye alikuwa akishangiliwa kwa nguvu nina hasira ya kupambana nao na kuwaondoa watanzania katika umaskini waziri mkuu huyo wa zamani aliyeihama ccm mwishoni mwa mwezi julai aligoma kushuka jukwaani akitaka awekewe muziki acheze na maelfu ya wananchi waliokuwa wakimsikiliza na kumkumbatia mkewe regina ambaye alifika uwanjani hapo wakati mkutano huo ukikaribia kumalizika kisha akambusu awali lowassa alisema idadi ya kura anazohitaji ili ashinde urais ni milioni 14 akiwa mafinga mkoani iringa lowassa aliomba wananchi wampigie kura milioni 10 ili awe rais lakini jana alisema kuna haja ya kupata kura nyingi iwezekanavyo ili ushindi wake usiathiriwe kilichonileta hapa ni kuomba kura alisema lowassa naomba mnipigie kura milioni 14 na ushee ili ziweze kutosha kuwa rais baada ya kupiga kura wananchi mnatakiwa kuzilinda ili zisiibwe dar es salaam mgombea urais wa chadema na ukawa edward lowassa ametaja mambo 13 atakayoyafanya ndani ya siku 100 iwapo atachaguliwa kuwa rais huku akisema atawakata kilimilimi wanaombeza kuwa hawezi kuondoa umaskini wa wananchi
2017-04-27T10:57:36
http://www.bongoswaggz.com/2015/10/lowassa-kwa-siku-100-nitafanya-mambo-13.html
rwebangira blog wednesday november 03 toa tafsiri yako mwenyewe pia yaongea maneno elfu moja na ushee je hii yaongea nini zanzibar mpya in the making chaguzi zipatazo tatu zilizopita huko zanzibar kipindi kama hiki ilikuwa ni mshikemshike hakukaliki hakulaliki lakini sivyo ilivyo kwa uchaguzi wa mwaka huu huko nyuma hukuwai kushuhudia wagombea kukaa pamoja kusubiri matokeo zaidi kumpongeza aliyeshindwa haikuwai kutokea isipokuwa mwaka huu kumbe tukiweka ubinafsi nyuma na kutanguliza utaifa haya yanawezekana pongezi kwa maalimu seif kwa kukubali kiuungwana na pia dr shein kwa kuchaguliwa na pia kuwa tayari kufanya kazi na upinzani sote twangoja kuona zanzibar mpya yenye amani na utulivu zaidi yenye neema tele at
2017-07-23T14:52:26
http://bongopicha.blogspot.com/2010_11_03_archive.html
serikali imejipanga vizuri kukabiliana na magonjwa ya mlipukoikiwemo ebola asema dkt ndugulile wizara ya afya tanzania wizara ya afya jumamosi mei 26 2018 0 on serikali imejipanga vizuri kukabiliana na magonjwa ya mlipukoikiwemo ebola asema dkt ndugulile
2019-10-21T05:36:01
https://afyablog.moh.go.tz/2018/05/serikali-imejipanga-vizuri-kukabiliana.html
idadi ya matokeo 83 06 jul 2020 toleo la habari covid19 ni mfano mmoja tu wa hali ya ongezeko la magonjwa kuanzia kwa ebola hadi kwa mers homa ya west nile na homa ya bonde la ufa husababishwa na virusi kutoka kwa wanyama hadi kwa binadamu utatiti mpya
2020-07-08T12:09:49
https://www.unenvironment.org/sw/resources?topic=23&amp%3Bamp%3Bf%5B0%5D=country%3A294&amp%3Bamp%3Bf%5B1%5D=tags%3A83&amp%3Bf%5B0%5D=country%3A213
uchaguzi 2010 inakuaje wagombea urais ccm & chadema wafunguliwa kesi mahakamani | jamiiforums | the home of great thinkers uchaguzi 2010 inakuaje wagombea urais ccm & chadema wafunguliwa kesi mahakamani [font=&quot]mwaka huu duh kuna kazi kweli kweli wagombea urais wawili wakuu wanaochuana vikali katika kampeni – yaani jk wa ccm na dr slaa wa chadema wote wawili wamejikuta wanafunguliwa kesi za madai mahakamani jk anashitakiwa na mwalimu mmoja ambaye anapinga uteuzi wake kwa sababu hana sifa za kuwa rais[/font] [font=&quot]na huyu wa pili dr slaa naye amefunguliwa kesi na mtu mmoja ambaye anadai amemchukulia mke wake[/font] [font=&quot]inakaa vipi hii – kwani haijapata kutokea huko nyuma hata siku moja[/font] [font=&quot]mwaka huu duh kuna kazi kweli kweli wagombea urais wawili wakuu wanaochuana vikali katika kampeni &#8211 yaani jk wa ccm na dr slaa wa chadema wote wawili wamejikuta wanafunguliwa kesi za madai mahakamani jk anashitakiwa na mwalimu mmoja ambaye anapinga uteuzi wake kwa sababu hana sifa za kuwa rais[/font] [font=&quot]inakaa vipi hii &#8211 kwani haijapata kutokea huko nyuma hata siku moja[/font]click to expand ni ishara kwamba tunakoelekea siko nawaonea wivu wakenya viongozi wao wameona zaidi ya urefu wa pua zao na wamekuja na katiba mpya ya ukombozi a real masterpiece hapa bado ni ufirauni tu kila kukicha watu kama akina makamba kweli wana mawazo kama ya hao wa kenya kazi yake kubwa ni kupika uchawi hajui hata maana ya kuchaguliwa kwa kura loh hii ya huyo mwalimu mbona imekaa hivyo ati muungwana hafai kuwa rais nimesoma humu jf habari hiyo na ilishangaza yule jaji (wa ccm) alipoonyesha tangu mwanzo ataamua vipi kesi hiyo ili kuridhisha mabwana zake kabla hajasikiliza ushahidi akaanza kuhoji kwa kusema eti jk hafai yanakuja yale yale ya tendwa kwa upande wa huyo mwalimu kesi ni ya msingi lakini itatupiliwa mbali kwa upande wa dk slaa hii ndiyo tathmini yangu kabla ya kutoa taarifa kwa vyombo vya habari unaanza mahakamani na kufungua kesi kwa taratibu zote kisha ndio unaenda kusema nimefungua kesi kwa sababu hii na hii unapoanzia kwenye media unakuwa umevunja sheria na taratibu za mahakama kwani unakuwa umeingilia uhuru wa mahakama kutoa uamuzi ulio huru na wa haki huwezi kupeleka malalamiko yako kwa media kisha public waanze kujadili na wakifikia uamuzi ambao utakuwa tofauti na ule wa mahakama utakuwa umeingilia uhuru wa mahakama kwa mtaji huu kesi inapaswa kutupiliwa mbali lakini itapokelewa kwa kuwa inamhusu dk slaa kesi imefunguliwa mahakama kuu dhidi ya dk slaa kwa kawaida kwa mujibu wa sheria kesi kama hii huanzia mahakama ya mkoa (ambayo ni mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi kisutu) kuipeleka kesi mahakama kuu kunaifanya iwe na uzito wa juu kuliko inavyostahili mahimbo anadai alipwe fidia ya shilingi bilioni moja kwa kuvunjiwa ndoa yake fidia kama hii haiwezi kuwa na mantiki kwa kuwa si tort siwezi kuelezea kinagaubaga nini haswa maana ya tort lakini kwa upande wa ndoa kuvunjika si sawa na mtu kutendewa kinyume na haki kwanza dk slaa hakuingilia ndoa ya mahimbo kwani alipokutana na josephine tayari josephine alikuwa ameondoka kwa mumewe huyo kwa hiyo hata kama hakukuwa na talaka mahakamani ndoa ilikuwa imevunjika na si slaa aliyeivunja kwa kuwa kesi hii imepewa umuhimu mkubwa ni wazi kwamba hizi ni hujuma za ccm dhidi yake dk slaa wanachofanya hapa ni kuvuruga mambo kwa kuweka mambo ambayo yatajaribu kupoteza dira lakini wananchi na chadema wameshtukia hii toka zamani wamejiandaa ccm inatapatapa kwa mtaji huu haifiki mbali kwenye malengo yake wanapoteza pesa zao bure watu wengi wanamshangaa jk badala ya kuwaachia watanzania wafanye maamuzi yao yeye yuko busy kumfanyia hujuma slaa ama kweli aliyefilisika hoja atavamia hoja yoyote ile n hivi ndivyo ilivyo debe tupu haliachi kutiika kibaya hakiachi kujitembeza huna hoja bora upayuke hii ndio desturi ya mshndwa n hivi ndivyo ilivyo debe tupu haliachi kutiika kibaya hakiachi kujitembeza huna hoja bora upayuke hii ndio desturi ya mshndwaclick to expand mnaogopa eee na bado hahahaha wadanganyika si wadanganyika tena hahahaha mnaogopa eee na bado hahahaha wadanganyika si wadanganyika tena hahahahaclick to expand achana nao hao wanaojibu bila ya hoja mgombea urais kufunguliwa kesi ya kusema hana sifa za kuwa urais haijapata kutokea katika dunia hii mwenye data za kupinga nilalolisema huyu mahimbo ndio bure kabisa mke hakutaki unalazimisha ninisi utafute mke mwingine aumaharinyenyewe ukiukizwa ukikipa mbuzi wawiki wa vingungutinhata elfu 60 hawafiki halafu unataka billion moja huyu mahimbo ndio bure kabisa mke hakutaki unalazimisha ninisi utafute mke mwingine aumaharinyenyewe ukiukizwa ukikipa mbuzi wawiki wa vingungutinhata elfu 60 hawafiki halafu unataka billion mojaclick to expand na hakuna kitu kibaya kinachoweza kutokea kwa mwanaume kama vile kukataliwa na mke hapo unaweza kuhisi mengi tu aibu kuachwa inaumaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
2016-10-23T12:10:35
http://www.jamiiforums.com/threads/uchaguzi-2010-inakuaje-wagombea-urais-ccm-chadema-wafunguliwa-kesi-mahakamani.72643/
lhrc | msimamo wa asasi za kiraia kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya sheria mbalimbali juni 2019 mnamo jumatano juni 19 2019 asasi za kiraia kama sehemu ya wadau katika kuchangia mabadilko ya sera na sheria mbalimbali zilipokea mapendekezo ya marekebisho ya sheria nane tofauti ambapo mapendekezo hayo yameplekwa kwa kamati ya bunge ya katiba na sheria kwa hati ya dharura sheria hizo ni pamoja na sheria ya makampuni sheria ya asasi za kiraia sheria ya takwimu sheria ya vyama vya kijamii sheria ya filamu na michezo ya kuigiza pamoja sheria ya wakala wa usafirishaji majini sheria ya hatimiliki na sheria ya miunganiko ya wadhamini mabadiliko haya yanapendekezwa kufanywa kwa haraka kutumia taratibu ambazo kwa kawaida hufuatwa pale panapokuwa na jambo la dharura kwa ujumla mabadiliko yanayopendekezwa katika sheria hizo yanalenga kudhibiti utendaji kazi wa asasi za kiraia hivyo kuathiri namna wananchi wanavyoweza kutumia haki yao ya kujumuika kushirkiana kuwekeza kueleza maoni yao kwa uhuru haki ya kushiriki katika uchumi na maamuzi yanayowaathiri na kuwawajibisha viongozi wao asasi za kiraia ni mashirika jumuiya au vikundi vya watu vilivyoundwa kwa uhuru na hiari yao kwa ajili ya jamii yao ambapo wahusika hawagawani faida na hawana udhibiti wa moja kwa moja wa serikali mchango wa asasi za kiraia asasi za kiraia zinachangia mambo mbali mbali nchini ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za kijamii asasi za kiraia zinatoa huduma za moja kwa moja ikiwemo huduma za afya mfano kutoa dawa na huduma nyingine za matibabu ikiwemo kwa waathirika wa ukimwi na magonjwa mengine kwa mujibu wa ripoti ya idara ya maendeleo ya jamii juu ya mchango wa azaki kwenye maendeleo nchini asasi hizi zina mchango mkubwa sana kwenye sekta ya afya elimu kilimo nishati utawala bora mazingira na maendeleo ya jinsia wakati mwingine katika jukumu hili asasi za kiraia hufanya kazi moja kwa moja na serikali kusaidia kujenga vituo vya afya vya serikali vyanzo vya maji na shule mashirika ya kiraia yanasaidia serikali kupata maoni juu ya maamuzi na vitendo vyake ama kutoka kwa shirika au kwa kukusanya maoni kutoka kwa vikundi tofauti katika maeneo tofauti mashirika ya kiraia mara nyingi husaidia kuibua mawazo mapya na suluhu ya matatizo ambayo wanaweza kuyafanyia majaribio kabla ya kushauri serikali kutekeleza mfano mmoja wapo ni ubunifu uliofanyika katika sekta ya elimu katika kuainisha namna bora za kuhamasisha walimu kuhakikisha wanafunzi wanajifunza na kufaulu vema zaidi katika sekta ya afya asasi za kiraia nchini zimekuwa na mchango mkubwa katika uvumbuzi wa maambukizi ya ugonjwa wa malaria ambao unatumika kuboresha sera na mipango ya serikali asasi za kiraia hufanya kazi ya kujenga misingi ya usawa katika jamii kwa kuwalinda na kuwatetea watu wenye mahitaji maalumu na wanyonge mashirika ya kiraia hutusaidia kujifunza yanazalisha ujuzi mpya na kushirikiana na wananchi na viongozi ili iweze kuchangia maendeleo mashirika ya kiraia huajiri maelfu ya watu hulipa mamilioni ya shilingi kama kodi na huchangia mamilioni ya shilingi kwa uchumi wa ndani kwa kununua bidhaa na huduma mbalimbali mapendekezo ya marekebisho ya sheria hizi yanatishia ustawi wa asasi za kiraia kwa sababu kuu zifuatazo marekebisho haya yatabatilisha kazi nzuri na za msingi zinazofanywa na asasi za kiraia marekebisho ya sheria ya makampuni sheria ya vyama vya kijamii sheria ya mashirika yasiyo ya kiserikali na sheria ya miunganiko ya wadhamini yanaweka masharti kwamba shirika lolote linalofanya kazi za maendeleo haliziwezi tena kusajiliwa kama kampuni isiyotengeneza faida (marekebisho ya 456) katika mabadiliko ya sheria ya asasi za kiraia tafsiri ya asasi za kiraia haijitoshelezina yamejikita kuweka zuio la aina ya shughuli zinazokufanyika na asasi tofauti na haki ya raia kujumuka inayopatikana kwenye ibara ya 20 ya katiba yetu ya mwaka 1977 (marekebisho 25) asasi yoyote ambayo itakuwa haijasajaliwa chini ya sheria sahihi kwa mujibu wa tafsiri mpya ya zitapaswa kuomba usajili bila kuzingatia kama asasi hizo zimesajiliwa na zimekuwa zikifanya kazi tayari ni taasisi halali ambazo zimeajiri watu zinalipa kodi na zinatoa mchango mkubwa kwa jamii na nchi (marekebisho 28 36) kinyume chake asasi zinapewa muda wa miezi miwili kuhakikisha zinatekeleza masharti ya sheria mpya (marekebisho 6) hata mashirika ambayo tayari yana cheti cha usajili chini sheria ya asasi za kiraia yanaweza kufutiwa usajili kama hayatatekeleza matakwa ya sheria mpya (marekebisho 28) athari za kiuchumi na kijamii zitakazotokana na vikwazo kwa asasi za kiraia endapo marekebisho haya yatapitishwa kama yalivyo mashirika mengi ya kiraia yatafutiwa usajili na kushindwa kuanza tena kwa kufanya hivyo kuna madhara kadhaa yatajitokeza ikiwemo watu kupoteza ajira watoa huduma kukosa mapato serikali kupoteza mapato ya kodi (kodi za mapato na kodi za utendaji pamoja na kodi zinazotokana na bidhaa na huduma zinazotumiwa na mashirika hayo) pia kuna mashirika mengi yanayotoa huduma mbalimbali kujenga uwezo na kutoa rasilimali ambapo wanufaika wake watakosa huduma hizo marekebisho haya pia yanaweka vikwazo vikubwa kwa watengeneza filamu wa kimataifa (maarekebisho 17 na 21) ambayo yanalenga kudhibiti matumizi ya mandhari pamoja na maudhui ya filamu nchini tanzania hii inaibua hatari kubwa ya kuwafanya watengeneza filamu kuchagua maeneo mengine ya kufanyia filamu na kuiepuka tanzania hasa pale watakapokumbana na urasimu usio wa lazima hivi karibuni afrika kusini wameingia makubaliano na kenya kutoa msaada wa kiufundi katika kufundisha lugha ya kiswahili je kuna uwezekano kwamba fursa hii haikuletwa tanzania kwa sababu ya kukithiri kwa urasimu marekebisho haya pia yanaonekana kukinzana na msimamo wa serikali wa kujenga mazingira rafiki kwa kupunguza urasimu katika uratibu wa sekta binafsi kutokana na kuongezeka kwa kiwango cha udhibiti mamlaka makubwa wanayopewa maafisa na tafsiri kandamizi zilizopo katika marekebisho haya yanaweza kusababisha mgongano na jamii ya kimataifa na kupelekea kuharibu taswira ya nchi badala yake tunapaswa kushirikiana kuhakikisha tunafanyia kazi marekebisho haya kwa umakini ili kuweka mizania muhimu kuhakikisha kuwa majukumu ya msajili mbali na kudhibiti pia yanakuwa wezeshi kwa asasi za kiraia maoni haya pia yanakusudia kuepusha athari kwa shughuli za kitalii na vyanzo vingine vya mapato ambavyo vinategemea mapato kutoka nje ya nchi mianya mipya ya kuchuja taarifa mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya filamu na michezo ya kuigiza ni mapana sana kiasi cha kuweka vikwazo hususani katika maudhui ya picha za video majukumu ya bodi ya filamu (marekebisho 18) ni mapana na yanajumuisha kudhibiti kufuatilia kutoa vibali kuidhinisha na kusimamia majukumu haya yote hayajafafanuliwa kwa ufasaha hivyo kutoa mamlaka yasiyodhibitiwa kwa bodi ya filamu katika kusimamia maudhui pendekezo la 20 linatoa mamlaka yasiyo ya kawaida ya kudhibiti maudhui ikisisitiza kwamba kila bango litakaloandaliwa na kubandikwa hadharani linapaswa kupitiwa na kuidhinishwa na bodi ya filamu kukosekana kwa usawa na kutokufuatwa kwa misingi ya utoaji haki msajili na waziri ni watueliwa wa rais waajiriwa na serikali na wanawajibika kwake kwa mujibu wa katiba yetu wakati huo huo wanapewa mamlaka ya kufanya maamuzi ya haki na yasiyo ya kibaguzi katika kufungia mashirika msajili anapewa majukumu ya kushutumu na kuhukumu kinyume na misingi ya asili ya haki kwa kuzingatia kile anachokiamini kwa mfano kuhusu kampuni inayojihusisha na masuala ya kijinai msajili anaweza kuiandikia barua na kufikia maamuzi kwamba hajaridhishwa na majibu ya kampuni hiyo na kuifutia usajili kampuni hiyo (marekebisho 10) kwa mujibu wa marekebisho hakuna haja ya kutatua mashauri haya katika mahakama yoyote au vyombo vingine vya maamuzi kampuni inaweza kutafuta suluhu mahakamani ikiwa tayari imeshafungiwa hii ni kinyume na misingi ya haki ya asili ambayo ipo kwa mujibu wa sheria za nchi vile vile marekebisho ya 26 ya sheria ya asasi za kiraia yanamuongezea mamlaka mawili msajili wa asasi za kiraia mamlaka ya kusimamisha asasi na mamlaka ya kufanya uperembaji wa asasi kila baada ya miezi mitatu hata hivyo hakuna sababu yoyote ya msingi inayotajwa kuthibitisha mamlaka hayo mapana tayari kwa sharia ya sasa namba 24 ya mwaka 2002 asasi zinawajibika kuwasilisha ripoit hizi pamoja na hesabu za mwaka na fomu namba 10 inayokusanya taarifa zote za msingi kuhusu asasi hizi uhai wa mashirika yaliyosajiliwa chini ya sheria ya vyama vya jamii uko chini ya matakwa ya waziri marekebisho ya 38 yanatoa mamlaka kwa upande wa waziri kufuta chama cha kijamii kwa kuwa tishio kwa utawala bora wa nchi kwa mujibu wa sheria za tanzania na marekebisho yanayopendekezwa vyama vya kijamii nchini ni pamoja na taasisi mbali mbali za kidini zilizosajiliwa chini ya sheria ya vyama vya kijamii ya mwaka 1954 kuweka vikwazo katika historia ndefu na yenye manufaa katika kujumuika na kushirikiana watanzania wana historia ndefu ya kujumuika kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja hususani katika mifumo isiyo rasmi marekebisho haya yanaweza kuathiri historia hii kwa kiasi kikubwa mashirika mengi nchini yatapata shida kufikia vigezo vipya vilivyowekwa ili kujisajili au yatashindwa kufanikisha usajili katika muda mchache uliwekwa kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao urasimu pia unaweza kukatisha tamaa mashirika mapya kuanza kwa kiwango kikubwa hii itaathiri uwezo na utayari na nafasi ya jamii na kupelekea wananchi kushindwa kujumuika sheria ya maudhui mtandaoni (2018) imeleta hali hii kwa waandishi wa habari za mtandaoni (bloggers) blogu nyingi zilifungwa mara baada ya kutungwa kwa sheria hiyo wengine waliomba usajili wakijua malipo ya ada yatalipwa kwa awamu na baadae wakashindwa kuendelea baada ya kutakiwa kulipa kwa mara moja blogu nyingi sasa zimefungwa nchini tanzania na kusababisha vijana wengi sana kupoteza ajira na mapato marekebisho yanayopendekezwa yana hatari ya kuleta madhara makubwa kwa wengi wanaofanya kazi katika mashirika haya lakini zaidi kwa jamii inayofaidika na huduma za asasi hizi kunyamazisha sauti za wananchi kupelekea kutokuridhika chini ya marekebisho haya wananchi watakuwa na nafasi finyu na kukosa njia mbadala za kutatua changamoto zao endapo njia zao za kawaida zitashindikana asasi za kiraia zinatoa mchango muhimu katika kuchambua na kupaza sauti za wananchi katika michakato ya kuandaa sera kuelezea malalamiko au kuwawezesha kujifunza zaidi kuhusu masuala mbalimbali asasi za kiraia husaidia kujenga uelewa juu ya taarifa muhimu za serikali pia asasi za kiraia huwezesha ushiriki wa wananchi mashirika mengi yanayofanya kazi hii yapo katika hatari ya kufutiwa usajili hii inaweza kupelekea hali ambayo wananchi watajiona wanakosa nafasi ya kueleza changamoto na masuala yao na kuja pamoja kuzitatua na kuwafanya wajihisi kutengwa na kutokuwa na nguvu katika kufanya maamuzi ya wanayowahusu kwa ujumla asasi za kiraia tunaamini kwamba ni muhimu serikali kuratibu mashirika yote nchini na hii ni sehemu muhimu ya kazi za serikali lakini tunapaswa kufanya mabadiliko kwa uangalifu na kwa kutafakari kwa kina ili kuweza kufanya maamuzi sahihi vinginevyo tunaweza kuwa na nia njema lakini tukajikuta tunafanya makossa na kupelekea madhara yasiyotarajiwa ambayo yanaweza kuchukua miaka mingi kurekebisha tunapendekeza kuwepo kwa muda wa kutosha kwa wadau/wananchi kuyajadili mapendekezo ya marekebisho ya sheria hizi na kutoa maoni yatakayosaidia kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza #uhuruwetu civic space freedom of expression freedom of assembly democracy human rights accountability good governance freedom
2019-07-22T16:21:08
https://humanrights.or.tz/posts/b/News/msimamo-wa-asasi-za-kiraia-kuhusu-mapendekezo-ya-marekebisho-ya-sheria-mbalimbali-juni-2019
tundu lissu nitapoteza sifa kama nitakutwa na hatia na mahakama au sekretarieti ya maadili bbc news swahili tundu lissu nitapoteza sifa kama nitakutwa na hatia na mahakama au sekretarieti ya maadili https//wwwbbccom/swahili/habari48836002 aliyekuwa mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni nchini tanzania tundu lissu amesema licha ya spika wa bunge job ndugai kudai hakujaza fomu za mali na madeni za viongozi wa umma bado ana sifa za kugombea nafasi yoyote ya uongozi lissu aliyeko ubelgiji kwa matibabu amenukuliwa na gazeti la mwananchi ikiwa ni siku chache zimepita tangu alipopoteza sifa za kuwa mbunge mvutano ulianzia wapi spika wa bunge la jamuhuri ya muungano wa tanzania job ndugai alitaja sababu kuu mbili zilizomsukuma kuiandikia tume ya uchaguzi mosi ni kutokana na lissu kutokuhudhuria bungeni kwa muda mrefu na pili kutokuwasilisha fomu ya tamko la mali na madeni kwa sekretari ya maadili kwa mujibu wa sheria tundu lissu kufungua shauri kudai stahiki zake japo inafahamika kuwa mwanasiasa huyo alilazimika kusafirishwa nje ya tanzania awali nchini kenya na kisha ubelgiji kwa matibabu baada ya shambulizi dhidi yake kumekuwa na mjadala mkubwa kuhusu kutokuwepo kwake bungeni kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita haki miliki ya picha bunge tanzania hivi karibuni akiwa yungali ughaibuni amezuru nchi za marekani ujerumani na uingereza kote huko amehojiwa na vyombo vya habari za kutoa mihadhara kwenye vyuo vikuu kuhusu hali ya haki za binaadamu tanzania
2019-08-25T21:06:07
https://www.bbc.com/swahili/habari-48836002
zawadi ya harusi mshkaji hana hamu | jamiiforums | the home of great thinkers zawadi ya harusi mshkaji hana hamu discussion in 'mahusiano mapenzi urafiki' started by mtu b jan 22 2010 yaani inamtokea puani soma hapa http//issamichuziblogspotcom/2010/01/msaadakwenyetuta_21html#comments ndio wakome kupenda miteremko kwenye maisha mwanaume utapewaje gari la kuanzia maisha na baba mkwe nahisi hata mashemeji zake huwa wanamdharau sana mshkaji ndiyo yale yale eti unaoa kisha baba mkwe anatoa zawadi ya nyumba ya kuishi siku mkikorofishana na mkeo inabidi wewe ndiye ufungashe virago vyako uhame huko ni kuoa au kuolewa heri kulala na njaa katika nyumba yako kuliko nyumba ya kupanga cha msingi tumia busara tu paki gari nyumbani au mpe mkeo alitumie na usilipande tena huwezi kupangiwa maisha na baba mkwe wako huo utamaduni wa wapi ulioa ili upwe gari ama ufurahie maisha na keo na kama yote hayawezekani rudisha mtoto wake pamoja na gari lake na usidai mahali maana ni heri kuishi maisha ya kumfurahisha mungu kuliko maisha ya kukosana na mungu kwa kumfurahisha mwanadamu yaani natamani huyo jamaa angeichukua gari na kwenda kuipaki kwa baba mkwe lol full stop huyu jamaa inaonekana kichwa yake hapana msuri masharti ya gari ilikuwa marufuku kumpakia mwanamke yeyote isipokuwa binti wa babamkwe yaani mkewe kwani hakujua aliyekuwa anapewa ni mkewe na si yeye na hakuwa anaruhusiwa kuliendesha hivi wanawake wangapi tuconnected naomama dada shangazi shemeji mke wa kaka au mdogo wangu hawa wote walishapigwa marufuku kuonekana wakiwa ndani ya gari hiyo sasa yeye anasemaje alipewa ikiwa sawadi ya harusi fijana mnapooa ombeni ushauri kwanza baadhi ya baba mkwe za siku hizi ziko problematic sana unatakiwa kuwa masikini jeuri ukishaonalongolongo rudisha gari yake mwabie asante nasubiri lakwangu wala usilirudishe hilo gari alimpa mwanae mwache mkeo aliendeshe wewe kama bado wewe na mkeo hamjaweza kununua lenu piga mguu kama ulivyokuwa unafanya kabla ya hiyo zawadi hata mkienda shughulini tena bila kinyongo mwache mkeo aende na gari lake wewe tafuta usafiri mwingine hili swala ni mkeo anayetakiwa kuamua alimalize vipi na si wewe akiona sawa wewe upande daladala poa yote maishaalikupenda bila hiyo gari duuuh hii nayo kali kwa hiyo mkuu nadhani huna hata raha ya gari usirudishe gari ila lipaki home fanya biashara zako kwa taxi au daladala utafanikiwa siku moja kununua lako wala usilirudishe hilo gari alimpa mwanae mwache mkeo aliendeshe wewe kama bado wewe na mkeo hamjaweza kununua lenu piga mguu kama ulivyokuwa unafanya kabla ya hiyo zawadi hata mkienda shughulini tena bila kinyongo mwache mkeo aende na gari lake wewe tafuta usafiri mwingine hili swala ni mkeo anayetakiwa kuamua alimalize vipi na si wewe akiona sawa wewe upande daladala poa yote maishaalikupenda bila hiyo gariclick to expand ni kweli hilo gari ni la mkewe na ndiye anayetakiwa kulipangia masharti siyo baba mkwe kwa hiyo jamaa aongee na mkewe na wakubaliane kwamba gari lisiwe sababu ya wao kukosa amani katika ndoa yao binti akaongee na wazazi wake wakiendelea kuwa mbogo basi wamrudishie gari lake kwani wakati wakiwa wachumba si walikuwa wanapanda dala dala omwvitu vingine rahisi sana na ni vigumu ukicomplicate issue hapo si masharti baba wa watu anaona uchungu kachuma yeye alafu pengine unaenjoy na wanawake wengine kwani kama lift ilikuwa lazima sana si angewachukulia tax very simple kuwahakikishia watu kuwa nilikuwa sitongoz ni ngumu so just go for the simple optiondont give unnecessary lifts kwan iyo gari si inakufaa unapungukiwa nn wewe ukikaa kwenye mstari ni kutafuta kucheat tu hapo kinachotakiwa uonyeshe ni heshima kwa uyo baba kwakutotanua na wanawake wengine kwenye gari hiyohiyo hata ningekuwa mm lol ofcourse yawezekana ukuwa na intetion hiyo but u can not force anyone to believe uits their choice well your wife believe in u but ya in law must be suspicious unatakiwa kuwa masikini jeuri ukishaonalongolongo rudisha gari yake mwabie asante nasubiri lakwanguclick to expand huu ujeuri mzuri sana kwanini kunyanyasika bana wakati una nguvu zako mwwnyewe tunatumia vibaya hili neno jeuri maskinihapo kinachokosekana ni heshima na wala si kunyanyasika hiyo ni inferiority complex kuiregard hii issue jeuri maskini arudishe gari tunatumia vibaya hili neno jeuri maskinihapo kinachokosekana ni heshima na wala si kunyanyasika hiyo ni inferiority complex kuiregard hii issue jeuri maskini arudishe gariclick to expand inferiority complex really explain more bra kuna watu wana maisha magumu yani zawadi ikifuatia na sharti tu ujue hicho kitu hujapewa ila umeazimwa jamaa anajishtuakia tu kwa sababu mzee alimpa masharti unaweza kuta huyo mzee ana stress zake zingine ndio maana hachangamki hivi ukimrudishia halafu akakwambia yeye hana kinyongo na lile tukio utasemaje kama hiyo gari inakukosesha amani basi kubalianeni na mkeo mliuze tu si lipo kwa jina lenu hapo kuna jambo kwa nini binti alikaa mbele baba yake akakaa nyuma hata hivyo huyo mzee ana wazimu tu ukishatoa zawadi hicho kitu si chako tena ni sawa na wewe unapotoa mahari jua mahar ni zawadi pia ukiweka masharti huyu ng'ombe mkikamua maziwa asinywe mwanaume mwingine zaidi ya baba mkwe kama mkeo hana neno na wewe we chapia gia kama kawaida ignore the old man he is just jealous omwvitu vingine rahisi sana na ni vigumu ukicomplicate issue hapo si masharti baba wa watu anaona uchungu kachuma yeye alafu pengine unaenjoy na wanawake wengine kwani kama lift ilikuwa lazima sana si angewachukulia tax very simple kuwahakikishia watu kuwa nilikuwa sitongoz ni ngumu so just go for the simple optiondont give unnecessary lifts kwan iyo gari si inakufaa unapungukiwa nn wewe ukikaa kwenye mstari ni kutafuta kucheat tu hapo kinachotakiwa uonyeshe ni heshima kwa uyo baba kwakutotanua na wanawake wengine kwenye gari hiyohiyo hata ningekuwa mm lol ofcourse yawezekana ukuwa na intetion hiyo but u can not force anyone to believe uits their choice well your wife believe in u but ya in law must be suspiciousclick to expand maisha ni yako na mkeo mkeo akikuamini tu kwisha habaari huyo baba mpotezee tu gari kawapa ni yenu hajawaazimisha yaani natamani huyo jamaa angeichukua gari na kwenda kuipaki kwa baba mkwe lol full stopclick to expand mimi ningefanya hivyo ndio wakome kupenda miteremko kwenye maisha mwanaume utapewaje gari la kuanzia maisha na baba mkwe nahisi hata mashemeji zake huwa wanamdharau sana mshkaji ndiyo yale yale eti unaoa kisha baba mkwe anatoa zawadi ya nyumba ya kuishi siku mkikorofishana na mkeo inabidi wewe ndiye ufungashe virago vyako uhame huko ni kuoa au kuolewaclick to expand mke wangu alipewa nyumba ya vyumba vinne na copy ya hatii sincee 2008 babayake anachukua rent na ile copy tuloshaichana tusitegemee sana zawadi harusini yaani inamtokea puani soma hapa michuzi blog msaada kwenye tutaclick to expand &#8203swali ana origin card ya gari
2016-12-02T22:44:51
http://www.jamiiforums.com/threads/zawadi-ya-harusi-mshkaji-hana-hamu.50706/
maria premium custom blythe doll na nguo ya pouty face nyumbaniblythe dollblythe doll combosmaria premium custom blythe doll na nguo ya pouty face 61 kitaalam 100 ya wanunuzi walifurahia bidhaa hii amri za 4570 tu 8099 kushoto katika hisa 1088 watu wameiangalia kipengee hiki 92 watu wameongeza kipengee hiki kwa gari 58 / 100 kuuzwa nywele za machungwa za kulipwa za kulipwa za kwanza nywele ndefu za moja kwa moja za machungwa zilizo na bangs kifurushi nyeupe cha lace nyeupe viatu nzuri vya ngozi bure ya kimataifa meli kisasa tv diy mini cartoon mfano diy toy hakuna / hakuna inahitajika 30 cm / 12 inchi dolls za mikono mwili ujumbe 19 viungo nywele fiber za mikono tbl neo blythe doll 25 chaguzi mpya za mwili amelia premium desturi blythe doll na nguo ya kusubiri uso 35 & percnt mbali icy neo blythe doll colours nywele iliyounganisha icy neo blythe doll kamili combo box gray nywele azone alijumuishwa mwili 100 ya wanunuzi starehe ya bidhaa hii mnunuzi aliyehakikishwa 3 septemba 2019 06 02 bidhaa nzuri itaamuru tena 29 2019 09 agosti 57 pesa nzuri kama picha kamilifu pendekeza duka hii 28 2019 22 agosti 51 asante doll kabisa 21 2019 10 agosti 21 kidole nzuri sana nywele ni ubora mzuri sana asante 7 2019 07 agosti 11 asante nyingi kwa doll ni nzuri tu sehemu ilifika haraka sana duka linaweka zawadi blouse na viatu 1 2019 08 agosti 45 30 julai 2019 22 42 densi ya chic na utoaji wa haraka asante 29 julai 2019 04 43 doli ni nzuri uwasilishaji ni haraka inafuatwa kama zawadi weka mikono ya vipuri na suti 24 julai 2019 04 13 doli ni nzuri tu ubora kwa urefu nywele za chic mwili kwa kugusa ni wa kupendeza wenye mpira bawaba ni nguvu hakuna hutegemea popote macho hubadilisha kwa urahisi ya kupendeza kwa sikio na bonyeza kama zawadi weka mavazi na jozi ya viatu asante 10 julai 2019 04 10 doll nzuri maduka makubwa na bei nzuri 4 julai 2019 08 50 vizuri sana utoaji wiki tatu kwa kazakhstan haraka sana nilikuwa nikisubiri sana na nilitaka kupata tayari zawadi haikuwekwa lakini bado ni baridi nywele za kitambaa zinatofautiana kila millimeter ya nywele hupigwa usifadhaike nguo ni ubora wa juu sana kwa pesa hizo ni nzuri sana ni thamani yake 1 julai 2019 03 41 cute sana na kupendeza doll ninapenda uso mpya wa blythe sana vifuni vizuri vifanywa na kina nywele ni laini na nzuri mimi pia nilikuwa na nguo ya pili iliyopo kutoka duka asante 11 juni 2019 04 04 kila kitu kinalingana na picha na maelezo doll ya ubora mzuri utaratibu hufanya kazi vidole vinapatikana utoaji ni haraka sanawiki mbili nambari ya kufuatilia ilitolewa kila kitu ndani ya mfuko ni intact kama zawadi duka huweka mavazi ya ziada nguo zimewekwa kwa ubora viatupia ni kama kweli binti yangu ni furaha mimi pia))) 8 juni 2019 22 17 doll ya ajabu nzuri harufu nywele nzuri sana binti ni furaha 5 juni 2019 08 22 doll ni baridi binti ni furaha kila kitu hufanya kazi rangi ya macho inabadilika kila kitu kama katika maelezo 16 mei 2019 22 47 kipindi bora alikuja haraka sana chini ya wiki za 2 duka hilo lilijibu haraka na bado limeunganisha zawadi kwa njia ya mavazi ya ziada ameridhika sana 13 mei 2019 08 08 ninapendekeza duka binti ni furaha ilikuja siku za haraka sana za 16 mkoa wa saratov 1 mei 2019 11 00 pupa ni nzuri sana ubora bora na utoaji wa haraka yeye ni mzuri sana) 27 aprili 2019 07 45 nzuri sana cute doll nywele ni laini isiyo ya kawaida kama hai 25 aprili 2019 03 33 asante sana doll ni nzuri sana amri ya siku za 18 ambayo ni haraka sana imeandaliwa kwa mjukuu wa kuzaliwa kuzaliwa kesho mtoto atakuwa na furaha))) 18 aprili 2019 23 05 asante bado ninahitaji 17 aprili 2019 04 40 doll nzuri mzuri sana kazi zote asante sana utoaji wa haraka 16 aprili 2019 19 33 maelezo ya bidhaa kikamilifu inafanana na iliyopokea kipande kilikuja siku 16 asante sana kwenye duka
2019-09-15T22:54:11
https://www.thisisblythe.com/sw/maria-premium-desturi-blythe-doll-na-nguo-uso-pouty/
matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (february 9february 15) china radio international matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (february 9february 15) (gmt+0800) 20190215 210203 tume ya taifa ya uchaguzi drc yakagua hali ilivyo yumbi tume ya taifa ya uchaguzi ncini drc (ceni) imeanza maandalizi ya uchaguzi wa wabunge na wakuu wa mikoa katika maeneo ya beni na butembo katika mkoa wa kivu kaskazini na katika eneo la yumbi katika mkoa wa mai ndombe wakaazi wa beni na butembo hawakupiga kura mwezi desemba 2018 kwa sababu ya mlipuko wa ebola na ongezeko la makundi ya watu wenye silaha kulingana na maelezo ya viongozi wa drc katika eneo la yumbi machafuko kikabila yaliua watu zaidi ya 800 jengo na vifaa vya tume ya uchaguzi (ceni) vilichomwa moto tume ya uchaguzi inajiandaa kuendesha mchakato huo machi 31 2019 ujumbe wa tume ya uchaguzi (ceni) uliwasili yumbi siku ya alhamisi lengo lake ni kutathmini changamoto za usalama na vifaa kabla ya uchaguzi wa wabunge na magavana wa mikoa machi 31 miezi minne baada ya machafuko ya kikabila kazi ya kwanza kuhakikisha kuwa hali ya usalama iko shwari katika eneo hilo ambalo kwa sasa linaoongozwa na afisa wa cheo cha kanali kutoka jeshi la drc (fardc) ambaye aliteuliwa mkuu wa wilaya baada ya machafuko hapa watu wachache waliobaki katika mji huko baada ya machafuko wanahofu ya kutokea kwa shambulio jingine licha ya idadi kubwa ya jeshi na maafisa aw polisi pamoja na walinda amana wa umoja wa mataifa kutumwa katika eneo la yumbi kazi kubwa nyingine ni kuwahamasisha wakaazi waliotoroka makazi yao kurejea haraka kabla ya uchaguzi kwa mujibu wa msemaji wa monusco hali hiyo inaweza kuchukuwa muda mrefu kutokana na kiwango cha uharibifu katika eneo hilo kupotea kwa mali nyingi za watu na ukosefu wa huduma za serikali lakini pia uharibifu wa jengo na vifaa vya tume ya uchaguzi pia kuna kazi ya kuwatafuta wafanyakazi wengine wa ceni katika eneo hilo
2019-06-18T05:51:17
http://swahili.cri.cn/141/2019/02/15/1s182839.htm
nemc yafumuliwabaadhi ya vigogo watumbuliwa wengine wahamishwa kijukuu cha bibi k | habari na matukio uncategories nemc yafumuliwabaadhi ya vigogo watumbuliwa wengine wahamishwa nemc yafumuliwabaadhi ya vigogo watumbuliwa wengine wahamishwa waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais muungano na mazingira januari makamba amefanya mabadiliko makubwa kwenye baraza la usimamizi wa mazingira (nemc) akizungumza jana jumatatu julai 17 makamba alisema amebaini mazingira ya rushwa katika kutengeneza vyeti ambavyo havijafuata mchakato stahiki na urasimu mengine ni kutokuwa na lugha nzuri kwa wateja na kuwatisha ili watoe chochote na kuzitumia kampuni binafsi za watumishi wa nemc kufanya kazi za ukaguzi/uhakiki wa ndani ya nemc kwa kisingizio cha kutokuwa na watumishi wa kutosha pia amewasimamisha kazi manchare heche deus katwale andrew kalua na benjamin dotto huku wengine wakiendelea kuchunguzwa wakati wizara ikiendelea kupokea taarifa za ziada pia waziri amefanya mabadiliko ya wakuu wa kanda jafari chimgege aliyekuwa kanda ya mashariki sasa atakuwa mkuu wa kanda ya dodoma goodlove mwamsojo aliyekuwa mkuu wa kanda ya nyanda za juumbeya sasa atakuwa mkuu wa kanda ya masharikidar es salaam dk ruth rugwisha aliyekuwa mkuu wa kurugenzi ya sheria sasa atakuwa mkuu wa kanda ya ziwa mwanza dk vedastus makota aliyekuwa mkurugenzi wa mawasiliano sasa atakuwa mkuu wa kanda ya kusini mtwara joseph kombe aliyekuwa mkuu wa kurugenzi ya utafiti na mipango anakwenda kuwa mkuu wa kanda ya kaskaziniarusha dk menard jangu aliyekuwa kanda ya arusha anarudishwa makao makuu ya nemc kuwa kaimu mkuu wa kurugenzi ya utafiti na mipango jamal baruti aliyekuwa mkuu wa kanda ya ziwa anarudi makao makuu nemc lewis nzari aliyekuwa mkuu wa kanda ya kusini mtwara sasa anakuwa mkuu wa kanda ya nyanda za juu kusini
2017-12-17T16:00:51
http://www.kijukuu.com/2017/07/nemc-yafumuliwabaadhi-ya-vigogo.html
kiongozi wa kijeshi mauritania ajiuzulu | matukio ya kisiasa | dw | 16042009 kiongozi wa kijeshi mauritania ajiuzulu nia ni kutaka kugombea urais mohamed ould abdel aziz akihutubia baada ya mapinduzi agosti mwaka jana kiongozi wa jopo linalotawala mauritania tangu mapinduzi ya kijeshi ya agosti mwaka jana jenerali mohammed ould abdel aziz amesema anajiuzulu ili kupigania kiti cha rais uchaguzi utakapoitishwa june sita mwaka huu alikua yeye mwenyewe ould abdel aziz aliyeongoza mapinduzi hayo miezi minane iliyopita na kuutimua madarakani utawala wa sidi ould cheikh abdallahirais wa kwanza aliyechaguliwa kwa njia za kidemokrasimwaka 2007 nchini mauritania nimeamua kujiuzulu wadhifa wangu wa mwenyekiti wa baraza kuu la taifa na kiongozi wa taifa kuambatana na sheria na kufuata kanuni ziliozoko amesema hayo ould abdel aziz katika hotuba yake iliyotangazwa na radio na televisheni usiku wa jana kuamkia leo mwanajeshi huyo aliyesomeamwenye umri wa miaka 52aliyetumikia jeshi kwa muda wa miaka 32 ya maisha yakeamebainisha anataka kutetea wadhifa wa rais uchaguzi utakapoitishwa kabla ya wakati june sita mwaka huu ili kuweza kupigania wadhifa huoanalazimika kujiuzulu kama mwanajeshi na kuachana pia na madaraka aliyo nayo siku 45 kabla ya uchaguzi huo kuitishwa jenerali mohammed ould abdel aziz amesema ana hamu ya kweli ya kujenga mauritania mpya itakayofuata misingi ya sheriausawa na uhuruamezungumzia pia maendeleo yaliyoweza kufikiwa nchini tangu alipotwaa madaraka agosti mwaka jana amewakosoa kwa mara nyengine tena wapinzani wake wa kisiasaanaowataja kua kundi la wahalifu na kuwatuhumu kutaka kusababisha njaa kwa kuiwekea vikwazo nchi yake chama cha muungano wa taifa wa kuhifadhi democrasiafndd kimeutaja uamuzi wa jenerali huyo aliyeamua kuvaa suti badala ya sare za kijeshi kua ni kiini macho tuu kilicholengwa kuwahadaa walimwengu na kuhalalisha mapinduzi yake ya kijeshi fndd na vyama vyingi vyengine vya upinzani vinapanga kuususia uchaguzi huo wa rais wapinzani wa jenerali mohammed ould abdel aziz wanamlaumu kwa kutumia mali ya taifa tangu miezi kadhaa iliyopita kuendesha kampeni yake ya uchaguzi kote nchini na kuzifunga njia zote za kupigania wadhifa huo wa rais kabla ya hotuba yake ya jana usikuould abdel aziz alikutana na mwenyekiti wa baraza la senetba mamadoualiyeteuliwa kua rais wa mpito na baraza la katiba mhariri abubakar liongo kiungo https//pdwcom/p/hybg
2018-08-19T06:32:12
https://www.dw.com/sw/kiongozi-wa-kijeshi-mauritania-ajiuzulu/a-4182996
uswisi yarudisha thamani ya sanaa nchini sanaa na utamaduni ni moja ya nyenzo muhimu zinazovutia katika kuwasilisha mawazo kwa jamii kwa njia ya uigizaji wa majukwaani uchoraji uchongaji ngoma na muziki kwenye makongamano makubwa ya sanaa watu wamebuni mbinu zinazoweza kufikisha ujumbe kwa watu kiurahisi ni kuweka vikundi vya sanaa za maonesho ya majukwaani ambapo huigiza mada husika na hata kuimba kwa ngoma kisha wadau wanaibua mjadala njia hiyo hakika imesaidia kuwavuta watu karibu na kusikiliza kwa makini ni kitu gani hasa kinazungumzwa kisha watu wanajadili jambo linaloweza kufanyika ili kuleta muafaka wenye manufaa kwa jamii uswisi na sanaa moja ya balozi zilizojitahidi kuipa thamani sanaa katika utoaji elimu kwa jamii ni uswisi chini ya balozi aliyemaliza muda wake florence mattli wapo wasiotambua thamani yake lakini pia wapo wanaoelewa nguvu yake katika kufikisha ujumbe na miongoni mwao ambao wamekuwa mstari wa mbele ni ubalozi huo wa uswisi tanzania na zambia uswisi ni miongoni mwa balozi zilizowabeba wasanii kupitia miradi yao kadhaa ya kijamii waliyoanzisha ndani ya miaka mitatu na imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwafikia walengwa kwenye mikoa mbalimbali nchini kutokana na jinsi inavyowasilishwa gazeti hili lilifanya mazungumzo na mshauri wa ubalozi wa uswisi tanzania na zambia hapa nchini eliachim malimi anayesema wanaipa thamani kubwa sanaa katika kufikisha ujumbe kwa sababu ina nguvu ya kuwafikia watu kwa haraka tangu tuanzishe miradi mitatu iliyopita ikiwemo suala la rushwa mimba za utotoni na mazingira kwa kuwashirikisha wasanii tumeona nguvu kwa jamii wananchi wamepata uelewa haraka wamejifunza na hata vijana wengi wamejifunza kile kilichohitajika kwao anasema malimi anasema mradi wao wa kwanza ulihusu rushwa ambapo waliita wasanii kuandika maombi yao na kueleza ni kwa vipi wakipewa pesa watazitumiaje katika kusaidia kuelimisha na kupunguza vitendo hivyo kwa jamii anasema mradi huo haukubagua ni msanii wa aina gani ilimradi kuandaa muswada unaovutia kuelimisha kupitia sanaa zao na watu wakaelimisha na kupunguza tatizo lililopo anasema zaidi ya wasanii 200 waliomba lakini wale waliokidhi vigezo walichaguliwa na kupewa fedha ambapo zaidi ya sh milioni 190 zilitolewa katika mradi huo wa kupunguza vitendo vya rushwa kupitia sanaa lengo likiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali za kupambana na vitendo hivyo baadhi ya wasanii walionufaika walitoka makumbusho ya taifa nyumba ya vipaji vya sanaa (tht) kwa kushirikiana na clouds media sanaa tanzania gaba afrika na kijiji studio kwa kushirikiana na nafasi art space anasema mshauri huyo anafafanua kuwa wasanii hao walikwenda mikoa mbalimbali na bado walishirikisha makundi mengine ya wasanii kwenye mikoa waliyokwenda kama mtwara shinyanga na kwingine waliopewa elimu ili nao kushiriki kikamilifu kutoa mafunzo kwa wengine mradi mwingine ulikuwa unahusu mimba za utotoni ambapo pia anasema vijana wengi walipewa elimu kupitia sanaa ya uigizaji na muziki anasema baadhi ya wasanii waliopata fedha za mradi huo walikwenda katika mikoa iliyoathiriwa zaidi kama shinyanga mara na waliandaliwa michoro ya katuni kupata elimu kupitia mradi huo wasanii walipewa zaidi ya sh milioni 215 huku ujumbe wake ukisema wawezeshe vijana wa kike kwa njia ya sanaa mradi huo ulitolewa mwaka jana na bado makumbusho ya taifa walishiriki kwa mara nyingine kuomba na kufanikiwa kupata fedha sambamba na wasanii paulo gomez kwa kushirikiana na pili maguzo gaba afrika limited na nafasi na sahara and faru na mwaka huu walizindua mradi ambao unahusisha mazingira kuzigeuza taka kuwa bidhaa muhimu na balozi wa uswisi aliyemaliza muda wake florence mattli alionekana kuridhika na utekelezaji wa miradi iliyopitia sanaa vikundi vyafaidika kwa mujibu wa malimi vikundi vitano vya sanaa walinufaika na zaidi ya sh milioni 174 na makumbusho ikiwa ni miongoni mwa waliovuna pesa baada ya kufanya vizuri katika miradi mingine iliyopita makumbusho wamekuwa wakihusika kwa kiasi kikubwa na sanaa ndio maana waliweza kunuifaka kwa miradi mbalimbali mbali na hao wengine walionufaika ni chuma art wamekuwa wakiokota vyuma chakavu na chupa na kutengeneza mapambo ya nyumbani kama wanyama wadudu na tena ni wamekuwa wakifanya shughuli zao kwa kuwashirikisha watu wenye ulemavu chini ya mradi huo chuma art ilifanikiwa kutengeneza pia mjusi mkubwa kwa kutumia vyuma chakavu na amewekwa kwenye jumba la makumbusho na sasa ni kivutio kikubwa kwa watalii wanaokwenda kutembelea eneo hilo ukiachilia mbali watu wa chuma wengine walionufaika ni alama arts and media production fourteen plus na kikundi cha sanaa na maendeleo afrika mashariki (cdea) wote hao ni wale waliochangia fursa baada ya kutolewa matangazo kuwa waombe pesa na kulenga kitu gani miradi hiyo hakika imewasaidia wasanii sio tu kutoa elimu kama walivyoelekezwa bali kujiongezea kipato anasema miradi hiyo inatarajiwa kuhitimishwa mwishoni mwa mwaka huu na huenda sasa fursa nyingine zikatangazwa baadaye ili kuendeleza utamaduni wao wa kuelimisha jamii masuala mbalimbali kupitia sanaa malimi anasema baadhi ya wasanii wanashindwa kuchangamkia fursa kama hizo kwa kukosa uelewa kutokana na asilimia kubwa ya waliopo kwenye vikundi kutokuwa na elimu na wengine hawajui wafanye nini anawahimiza umuhimu wa kujiendeleza kielimu ili iwasaidie katika harakati za kukuza sanaa hiyo nchini na hata zinapotokea fursa basi inakuwa ni rahisi kwao kuomba art ilifanikiwa kutengeneza pia mjusi mkubwa kwa kutumia vyuma chakavu na amewekwa kwenye jumba la makumbusho na sasa ni kivutio kikubwa kwa watalii wanaokwenda kutembelea eneo hilo ukiachilia mbali watu wa chuma wengine walionufaika ni alama arts and media production fourteen plus na kikundi cha sanaa na maendeleo afrika mashariki (cdea) wote hao ni wale waliochangia fursa baada ya kutolewa matangazo kuwa waombe pesa na kulenga kitu gani miradi hiyo hakika imewasaidia wasanii sio tu kutoa elimu kama walivyoelekezwa bali kujiongezea kipato anasema miradi hiyo inatarajiwa kuhitimishwa mwishoni mwa mwaka kuridhika na utekelezaji wa miradi iliyopitia sanaa kwa mujibu wa malimi vikundi vitano vya sanaa walinufaika na zaidi ya sh milioni 174 na makumbusho ikiwa ni miongoni mwa waliovuna pesa baada ya kufanya vizuri katika miradi mingine iliyopita makumbusho wamekuwa wakihusika kwa kiasi kikubwa na sanaa ndio maana waliweza kunuifaka kwa miradi mbalimbali mbali na hao wengine walionufaika ni chuma art wamekuwa wakiokota vyuma chakavu na chupa na kutengeneza mapambo ya nyumbani kama wanyama masaa 2 yaliyopita mohamed akida watoto waibuka na muziki wa babu magufuli sanaa ya muziki hupendwa na watu wa rika zote kwa ligi kuu bara yaacha majeraha kwa makocha siku 3 zilizopita tuzo mapunda wakati ligi kuu tanzania bara ikisimama kwa wiki mbili kupisha
2019-11-19T11:16:40
https://habarileo.co.tz/habari/2019-11-095dc699a47f03f.aspx
rais shein afungua jukwaa la biashara zanzibar asisitiza utoaji huduma bora dar24 3 months ago comments off on rais shein afungua jukwaa la biashara zanzibar asisitiza utoaji huduma bora rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi dkt ali mohamed shein amewataka wadau wa sekta binafsi nchini kuweka mkazo katika utoaji wa huduma bora ili ziweze kukidhi viwango na ubora kulingana na malengo na matarajio ya wananchi dkt shein amesema hayo leo katika ukumbi wa sheikh idrissa abdulwakil kikwajuni mjini hapa alipofungua jukwaa la biashara la tisa (9) zanzibar jukwaa hilo ambalo limewashirikisha viongozi wa serikali na wadau mbali mbali wa sekta binafsi limeambatana na kaulimbiu isemayo ushirikiano baina ya sekta ya umma na sekta binafsi katika kukuza ajira kwa vijana akizungumza katika jukwaa hilo dkt shein alisema kumekuwepo na malalamiko kutoka miongoni mwa wananchi kuwa baadhi ya sekta binafsi zimekuwa zikiendesha shughuli za utoaji wa hudumazisizokidhi mahitaji halisi pamoja na malengo ya taifa ya muda mfupi na mrefu amesema kwa kiwango kikubwa malalamiko hayo yamekuwa yakielekezwa katika sekta za afya na elimu hivyo ametaka juhudi zifanyike kwa kuweka mkazo katika uimarishaji wa huduma bora aidha aliwataka wadau wa sekta hizo kuliangalia kwa kina suala la kuwajengea uwezo wafanyakazi wao akibainisha kutokuwepo msukumo wa kutosha katika kuwasomesha wataalamu wa sekta hizo na badala yake kutegemea zaidi wataalamu waliosomeshwa na serikali hatua ya sekta binafsi kuajiri wataalamu walio na majukumu muhimu serikalini kunaathiri utoaji wa huduma katika maeneo wanayoyatumikia lazima muwe tayari kugharamika kwa ajili ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wenu amesema amesema sio jambo jema kwa maendeleo ya taifa kwa kuwa na wataalamu wengi wasiopenda kufanyakazi katika sekta binafsi kwa sababu ya ugumu wa kujiendelezanatowa wito kwa waajiri katika sekta binafsi kuwa na mipango imara ya kuwaendeleza wafanyakazi wenu amesisitiza dkt shein akazipongeza sekta binafsi kwa kushirikiana na serikali katika kuimarisha maslahi ya wafanyakazi hususan kwa hatua yao ya kuitikia wito wa serikali wa kupandisha mishahara ya kima cha chini kuambatana na miongozo iliyotolewa aidha amewataka waajiri wa sekta binafsi kuhakikisha wanafikisha michango ya wafanyakazi wao katika mfuko wa hifadhhi ya jamii (zssf) ili kuwajengea wafanyakazi mustakbali mwema wa maisha yao na utulivu kazini ameeleza kuwa sekta binafsi ina mchango mkubwa katika kufanikisha azma ya serikali ya kuwa na uchumi wa kati kwa kutumia fursa kadhaa ambazo bado hazijafikiwa amezitaja baadhi ya fursa hizo kuwa ni pamoja na ile ya uvuvi wa bahari kuu uendelezaji wa shughulli za kilimo na ufugaji kwa njia za kisasa pamoja uwekezaji katika sekta za nishati na viwanda tuwe na ujasiri wa kuwekeza katika sekta mpya ili kuepuka ushindani usio na lazima bado hatujaanzisha miradi mipya kwa njia ya ubia kama wafanyavyo wenzetu katika nchi mbalimbali duniani alisema amesema kuimarika kwa sekta binafsi kutapanua wigo wa soko la ajira na kuwapatia vijana kazi za staha kupitia sekta mbali mbali na hivyo kupata uwezo wa kuendesha maisha yao na pia kuongeza pato kwa taifa aidha amepongeza juhudi zinazoendelea kuchukuliwa za kuimarisha ushirikiano kati serikali na sekta binafsi kwa amslahi ya taifa na wananachi wake ushahidi mzuri wa jambo hili ni ufanisi wa kupigiwa mfano ulioonekana katika maonyesho ya utalii zanzibar yaliofanyika hivi karibuni tumeweza kuitangaza nchi kwa mafanikio makubwa alisema kuhusiana na uimarishaji wa mazingira ya biashara dkt shein alisema serikali imeanzisha sheria namba 10 ya mwaka 2017 kwa lengo la kuhakikisha kunakuwepo utaratibu bora na madhubuti katika uendeshaji wa biashara nchini amesema wafanyabiashara na wawekezaji hupenda kuwekeza katika nchi ambazo zimeweka mazingira mazuri ya kufanyia biashara hivyo akaomba kuitumia mikutano na majukwaa kujadili namna bora ya kuimarisha na kurahisisha maendeleo katika sekta ya biashara utoaji wa huduma unaotegemea vitendo vya rushwa na uenyeji huzorotesha kasi ya biashara na uwekezaji endelezeni shughuli zenu kwa kuzingatia mabadiliko ya teknolojia na mahitaji halisi ya wananchi amesema mapema waziri wa biashara na viwanda balozi amina salum ali alisema uanzishaji wa mabaraza ya vijana utaongeza kasi ya kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbali mbali zinazowakabili vijana hususan ya ukosefu wa ajira amesema jukwaa hilo litajadili na kupata majibu ya mazingira bora yanayopaswa kuwepo ili kuleta maendeleo ya kibiashara sambamba na kukuza uchumi wa taifa aidha amesema ukosefu wa bajeti na chombo cha kuuunganisha sekta hizo mbili ni miongoni mwa changamoto zinazokwaza kupatikana kwa ufanisi naye mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara wenye viwanda na wakulima taufiq salim turky akitoa salamu kutoka jumuiya hiyo kwa niaba ya sekta binafsi alisema chini ya uongozi wa dk shein sekta ya utalii imepata mafanikio makubwa hususan katika suala la ujio wa watalii amesema katika kipindi cha miaka minane ya uongozi wake ujio wa watalii umeongezeka kutoka ule wa watalii 150000 uliodumu kwa takriban miaka 20 na kufikia zaidi ya watalii 350000 hivi sasa huku kukiwa na matumaini makubwa ya kuongezeka kiwango hicho hadi kufikia 500000 ifikapo mwaka 2020 amesema rais dkt shein amerejesha uelewa uliokosekana kwa kipindi kirefu kuwa serikali na sekta binafsi zina malengo ya aina moja katika jukwa hilo mada mbali mbali ziliwasilishwa na kujadiliwa
2019-02-16T03:13:09
http://dar24.com/rais-shein-afungua-jukwaa-la-biashara-zanzibar-asisitiza-utoaji-huduma-bora/
cool james mtoto wa dandu posted by jfk on august 26 2011 cool james mtoto wa dandu au cj massive zilikuwa aka za james dandu mwanamuziki aliyezaliwa 1970 katika jiji la mwanza alianza shughuli za muziki mwaka 1983 lakini album yake ya kwanza aliitoa 1986 akajiunga na mwanamuziki kutoka kenya andrew muturi na kuanzisha kundi la swahili nation na wakaweza kutoa single iliyoitwa mapenzi mwaka 1990 alijitoa kundi hilo na kuanzisha kampuni yake dandu planet mwaka 1993 akiwa na black teacher alitoa album iliyokuwa na vibao kama dr feelgood iliyoweza kushinda tuzo la best scandinavian dance track 1994 pia kulikuwa na nyimbo kama godfather na the rhythm of the track alianzisha kampuni nyingine dandu entertainment na kufanya kazi kadhaa kupitia wanamuziki wa afrika mashariki dandu hatasahaulika kwa wale wanaofahamu chanzo cha tuzo za kila mwaka za muziki za kilimanjaro music awards ambazo zilianza kwa jina la tanzania music awards (tama) alifariki katika ajali ya gari tarehe 27 agosti 2002 akiwa na umri mdogo wa miaka 32
2018-02-23T06:40:28
http://musicintanzania.blogspot.com/2011/08/cool-james-mtoto-wa-dandu.html
ujumbe wa papa kwa mkutano wa vienna wa katazo la silaha za nyuklia 20141210 161001 kwa ajili ya mkutano unaozungumzia madhara ya silaha za nuklia uliofanyika kwa muda wa siku mbili mjini vienna 89 desemba 2014 baba mtakatifu francisko alipeleka salaam na ujumbe wake kwa washiriki wa mkutano huo kupitia rais wa mkutano waziri sebastian kurtz ambaye ni waziri wa shirikisho la ulaya mahusiano na ushirikiano na mataifa mengine katika jamhuri ya austria ambaye pia ni rais wa baraza juu ya kishindo cha madhara ya silaha za nuklia kwa binadamu mkutano huu ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka mataifa mbalimbali na mashirika ya kimataifa na vyama vya kiraia baba mtakatifu katika salaam na ujumbe wake amezitaja silaha za nuklia kuwa tatizo la kimataifa na lenye kuathiri mataifa yote athari si kwa binadamu wa leo tu lakini pia kwa vizazi vijavyo na hata sayari ambayo ni makazi ya viumbe na hivyo ni lazima mataifa kuzingatia maadili kama hitaji la lazima kupunguza tishio la nyuklia kwa kusitisha uzalishaji na matumizi ya silaha za nyuklia kwa hiyo leo hii kuliko hata siku za nyuma kiteknolojia kijamii na kisiasa unakuwa ni wito makini wa kidharura kujali maadili ya umoja kama papa yohana paulo ii alivyohimiza siku za nyuma katika waraka wake ( sollicitudo rei socialis 38) ambao unahamasisha watu kufanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya dunia salama zaidi iliyosimikwa katika mizizi ya maadili na uwajibikaji katika ngazi ya kimataifa papa francisco ameendelea kuyataja madhara ya silaha za nuklia kwa binadamu yanayo tabiriwa na yenye kuathiri pia dunia akionyesha kujali kwamba mara nyingi madhara ya nuklia yakizungumziwa hulenga zaidi katika mauaji mengi lakini pia ni muhimu papa anashauri lazima kutazama kwa kina zaidi mateso yasiyokuwa ya lazima hata kwa mtu mmoja mmoja yanayo sababishwa na matumizi ya silaha hizi za nyuklia na kwamba iwapo mateso hayo yatakomeshwa katika matumizi ya mifumo ya kijeshi na sheria za kimataifa miongoni mwa mengine vivyo hivyo silaha hizo hazitatumika hata katiakvita vya kawaida maelezo ya baba mtakatifu francisco yamerejea waathirika na silaha hizo akisema kwamba hutoa onyo kwa dunia kutorudia makosa ya nyuma yaliyo sababisha athari hizo zisizo rekebishika hata kwa viumbe wengine na kwa moyo wa kibaba papa aliwakumbuka waathirika wote wa silaha za nyuklia akitoa mfano wa eneo hibakusha na pia waathirika wengine wote wa silaha za nyuklia ambao sasa wamekuwa rejea na kipimo muhimu kwa mkutano wa vienna papa amesemawaathirika hao ni sauti ya kinabii katika mkutano huo inayolilia familia ya binadamu kuthamini zaidi ya uzuri wa upendo ushirikiano na udugu wakati wakijikumbusha hatari ya silaha za nyuklia duniani zenye kuwa na uwezo wa kuangamiza binadamu na ustaarabu wote papa francisco anaamini kwamba hamu ya amani na udugu itapandikizwa katika kina kirefu katika moyo wa binadamu na kutoa matunda thabiti mazuri katika njia zake za kuhakikisha kwamba silaha za nyuklia zimepigwa marufuku mara moja na kwa muda wote kwa ajili ya manufaa ya viumbe wote na kwamba usalama wa maisha ya binadamu hata kwa siku za baadaye unategemea sana uhakika wa usalama na amani ya watu wengine kwa kuwa iwapo amani usalama na utulivu havina uhakika kimataifa hakuna mwenye kuwa na furaha kamili papa ameasa watu wote iwe kama mtu mmoja mmoja au kimakundimakundi na wote kwa pamoja wana wajibika na usalama wa mazingira iwe kwa sasa na hata kwa vizazi vijavyo ni matumaini yake makubwa kwamba wajibu huu utakuwa ni kigezo katika jitihada za wazo la kusitisha silaha za nyuklia ili dunia iwe huru na silaha hizo za hatari na ni jambo linalowezekana
2019-08-24T07:10:26
http://www.archivioradiovaticana.va/storico/2014/12/10/ujumbe_wa_papa_kwa_mkutano_wa_vienna_wa_katazo_la_silaha_za_nyuklia_/kws-839989
serikali yachukua maamuzi magumu kwa aliyesimamia kiapo cha odinga kenya habari/news | hivisasa blog home › habari/news › serikali yachukua maamuzi magumu kwa aliyesimamia kiapo cha odinga serikali yachukua maamuzi magumu kwa aliyesimamia kiapo cha odinga tarehe february 7 2018 mwanasiasa wa muungano wa upinzani nchin kenya nasa miguna miguna mwanasiasa wa muungano wa upinzani nchin kenya nasa miguna miguna amefukuzwa na kupelekwa nchini canada kupitia ndege ya klm kulingana na wakili wake nelson havi na cliff ombeta bwana ombeta amesema kuwa aliarifiwa kwamba bwana miguna aliingizwa katika ndege iliokuwa ikielekea amsterdam na baadaye kuelekea canada wakili mwengine dkt john khaminwa alisema kuwa mteja wake tayari ameondoka kenya ni kweli alilazimishwa kuingia katika ndege ya klm dakika chache tu kabla ya saa nne usiku na tumebaini kwamba anaelekea canada ni ukiukaji mkubwa wa haki alisema dkt khaminwa kwa simu haijulikani ni sheria gani iliotumiwa na serikali kumuondoa nchini kenya kwa kuwa katiba inampatia haki kama raia wa kenya kwa kuwa ni mzaliwa wa taifa hilo mkurugenzi wa shirika la ujasusi baadaye alisema kuwa bwana miguna alikamatwa baada ya kukiri kumpatia kiapo kiongozi wa nasa raila odinga mbali na kuwa mwanachama wa kundi lililopigwa marufuku la nrm uchunguzi waibua majibu ajali ndege ya malaysia wapelelezi wa uholanzi waliokuwa wakichunguza ajali ya ndege ya malaysia mh17 wamekamilisha uchunguzi na kuonyesha kuwa ndege hiyo ilipigwa kombora vikao vya cchalmashauri kuu kutikisa ccm rais magufuli awapa shavu mizengo pindamakongoro ccm magazeti ya leo ijumaa may 25 jeshi la polisi lamwaga ajirausahili kufanyika leo magazeti ya leo may 242018
2018-05-26T16:00:13
http://hivisasa.co.tz/habari/serikali-yachukua-maamuzi-magumu-kwa-aliyesimamia-kiapo-cha-odinga
mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki online kucheza kwa huru mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki unachezwa 22317 kucheza mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki online maelezo ya mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki paka awinde kwa samaki aquarium kucheza mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki online kiufundi na tabia ya mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki aliongeza 19102010 mchezo unachezwa 22317 mara mchezo rating 329 nje 5 (126 makadirio) michezo kama mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki download mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki embed mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki katika tovuti yako uwindaji kwa ajili ya samaki kuingiza mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki kwenye tovuti yako nakala ya kanuni na kuweka katika kanuni html ya tovuti yako pia kama wewe kama mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki nakala na kutuma kiungo kwa rafiki au rafiki yako yote kushiriki mchezo na dunia pamoja na mchezo uwindaji kwa ajili ya samaki pia alicheza katika mchezo
2018-12-12T13:15:12
http://sw.itsmygame.org/790050708/okhota-na-rybok_online-game.html
mwambaa wa walnut solid wood dining wood china manufacturer maelezoulaji laini wa kuni wa walnutmwanga walnut mango mangomwambaa wa walnut wood lining chair home > bidhaa > samani za chumba cha kula > viti vya kula > mwambaa wa walnut solid wood dining wood sura thabiti ya kuni sio tu kubuni lakini pia inahakikisha utulivu wa kiti cha dining nyuma na kiti kilichojazwa na sifongo cha juu cha unyevu kilichofunikwa na kitambaa kijivu hutoa uzoefu wa kukaa vizuri jedwali la mwisho wa mpangilio wa nordic original mraba wasiliana sasa ulaji laini wa kuni wa walnut mwanga walnut mango mango mwambaa wa walnut wood lining chair
2019-12-08T16:23:14
https://sw.taihuafurniture.com/dining-chairs/57161092.html
makamu wa rais kuzindua kampeni ya kitaifa ya usafi mkoani dodoma mtazamo news home / habari / makamu wa rais kuzindua kampeni ya kitaifa ya usafi mkoani dodoma makamu wa rais kuzindua kampeni ya kitaifa ya usafi mkoani dodoma philemon solomon thursday december 07 2017 habari picha na michuzijrdodoma makamu wa rais kuzindua kampeni ya kitaifa ya usafi mkoani dodoma reviewed by philemon solomon on thursday december 07 2017 rating 5
2017-12-13T01:23:29
http://www.mtazamonews.com/2017/12/makamu-wa-rais-kuzindua-kampeni-ya.html
gray mgonja kuwa governer | jamiiforums gray mgonja kuwa governer thread starter zanaki kuna habari kuwa gray mgonja anakwenda kuwa gavana wa bot na dr dau anakwenda kuwa dg wa tramgonja kwa sasa ni permanent secretary treasury na dr dau(huyu ni mchezaji mpira wa zamani wa yanga) yeye yuko nssf bado nafuatilia hili suala kwa ukaribu sanana habari zaidi ziko njiani tumeisha maana kama mgonja ataenda kuwa gavana sasa kuna nini tena maskandali ya hazina na mesheni zote mgonja yumo kuna mahala alitajwa kuhusika hata na stika na visa za kuingia ni mradi wake na mzungu wa holland majumba kibao huko marekani nasikia mwenye ukweli wa majumba haya afafanue leo unampa bank jamani haya na kasi zote hizi reactions kagayo huyu dr dau ndo nani vile unaweza kunisaidia jina lake lote na ni mwaka gani alichezea yanga huyo mgonja ni yupi huyo wenye vitu vyake mwageni hapa mimi jamani huyo kanipita pembeni lakini ninamjua msaidizi wake shujaa mama joyce mapunjo ambaye nimemshuhudia kwa macho yangu akimrekebisha rais wetu akiwa waziri kuwa waziri hapa umekosea sio sawa ulivyosema au unavyofikiri mzee mzima akampa bonge la jicho na mama naye akasimama na kumpa macho na kwenye makatibu akamchagua mama mapunjo you are my hero na ninakuombea upewe ukatibu kamili na baadaye uwaziri ila wazee huyu mgonja simfahamu vizuri ingwa nimemuona sana wenye data mwageni uwanja uko huru huu jina kamili ni ramadhani kitwana dau (phd ) msomi huyu na sijawahi kumsikia akicheza mpira drdau alikuwa akitajwatajwa na vyombo vya habari kuwa atapewa nafasi kubwa katika serikali ya jk zaidi ya kuwa mkurugenzi mkuu wa nssf sifahamu habari zake zozote gray mgonja alikuwa mkurugenzi bot kabla ya kuazimwa na hazina kama naibu katibu mkuu baadaye mkapa akampandisha cheo kuwa katibu mkuu na majuzi jk amemteua tena katika wadhifa huo mchango wa gray mgonja katika kuwezesha tanzania kuingia hipc ni mkubwa na unaheshimika vilevile anaifahamu bot kutokana na utumishi wake huko na vilevile kama mjumbe wa bodi ya bot kutokana na wadhifa wake wa katibu mkuu hazina kuna wanaodai wanafahamu madhambi mengi ya gray mgonja lakini hizi tetesi za ugavana zinatokana na rekodi yake ya kazi pale hazina dau na mpiradau na mpira huikumbuki hio yesdau was a footballer with young africans i thinkand maybe thats the main reason why he is so friendly with magori(tff vice chairman) who is also a director at nssf recycling leaders what a country mbona hukuendelea na hayo madai nasikia amekuwa na miradi na mramba pia kuna jumba keshanunua california yaani baada ya jamaa kupata scandal ya quality group kakata kidogodogo kwa jamaa wanampa ulaji mwingine ili tusahahu tanzania ina wenyewe nimechoka kabisa yaani humu kuna watu mlikuwepo wakati huo ninaohadithiwa na babu yangu kila wakati wa dau na mpira dau na mpira duuuh dau toka nssf kumeoza na rushwa na migogoro ya interestleo akiletwa hazina jk atakuwa anafanya nini gray kuijua hazina na wizi wa mali zetu ni kigezo awe gavana ninachofahamu mimi ni role ya gray mgonja katika jitihada za tanzania kurekebisha mahusiano yake na vyombo vya fedha vya kimataifa na kufaulu kuingia katika mpango wa hipc amefanya kazi kubwa pale hazina na ndiyo maana amepandishwa cheo toka naibu kuwa katibu mkuu kamili aidha siyo haitakuwa ajabu kama atateuliwa gavana gilman rutihinda alikuwa na role na wadhifa kama huu wa mgonja na baadaye akateuliwa kuwa gavana benki kuu kuhusu tuhuma kama amelimbikiza mali isivyo halali basi nashauri kwa dhati kabisa aondolewe hata katika wadhifa alionao sasa mwisho naomba uposti majina ya watanzania ambao ni safi na wana elimu na uzoefu wa kuweza kuwa gavana wa bot na kamishna wa tra nilitaka kuendeleza tu mada sina majina wala wasifu wa watanzania walio safi na wenye uzoefu wa kuwa gavana wa bot ningekuwa nayo ningekwenda kugombea ubunge hatari nan ampe mchana toch usiku magogo tufanyaje ccm mkiwa mnajiandaa kuwa chama cha upinzani jukwaa la siasa 39 yesterday at 1056 am s zanzibar 2020 hongera hussein mwinyi kuutangazia umma kuwa hutaki ushindi wa kura za wezi au wizi jukwaa la siasa 46 yesterday at 758 am bernard membe nikiapishwa kuwa rais wa tanzania viongozi wote wa dini (mashekhe) watarudishwa zanzibar jukwaa la siasa 93 sunday at 439 pm uchaguzi 2020 kwa ilani hii ya chadema ccm jiandaeni kuwa wapinzani baada ya kuanzia oktoba 2020 jukwaa la siasa 216 sunday at 1012 am rais magufuli amenifanya nione kitambilisho changu cha kura kuwa ni zaidi ya lulu ever jukwaa la siasa 22 saturday at 812 pm ccm mkiwa mnajiandaa kuwa chama cha upinzani bernard membe nikiapishwa kuwa rais wa tanzania viongozi wote wa dini (mashekhe) watarudishwa zanzibar uchaguzi 2020 kwa ilani hii ya chadema ccm jiandaeni kuwa wapinzani baada ya kuanzia oktoba 2020 rais magufuli amenifanya nione kitambilisho changu cha kura kuwa ni zaidi ya lulu ever
2020-08-11T00:50:00
https://www.jamiiforums.com/threads/gray-mgonja-kuwa-governer.233/
dfid yafurahishwa na mfumo wa takwimu huria nchini ujumbe kutoka idara ya maendeleo ya kimataifa (dfid) umefurahishwa na jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na benki ya dunia katika utekelezaji wa uanzishaji wa mfumo wa takwimu huria nchini ujumbe huo ukiongowa na bw ian attfield akiongozana na bi morag patrick pamoja na bw yisambi mwanshemele walikutana na mtendaji mkuu wa wakala dkt jabiri bakari na kutathimini jitihada hizo katika ofisi za wakala tarehe 12 machi 2015 akizungumza na ujumbe huo dkt bakari alisema jitihada za benki ya dunia zimesaidia katika kujenga uelewa wa jinsi mfumo wa takwimu huria unavyofanya kazi aidha benki ya dunia imekuwa ikitoa mafunzo mbalimbali yaliyohusu utengenezaji wa tovuti ya takwimu huria mafunzo hayo yaliwajengea uwezo watumishi wa wakala kutengeneza tovuti hiyo bila kuhusisha mkandarasi dkt bakari aliongeza katika utekelezaji wa jitihada hizo serikali imetoa waraka unaosimamia utekelezaji wa mfumo huo nchini imetengeneza tovuti kuu ya takwimu huria (wwwopendatagotz) ambayo inatoa takwimu za serikali kwa wananchi katika dirisha moja kwa sasani takwimu za elimu maji na afya ndio zilizowekwa katika tovuti hiyo kulingana na waraka wa usimamizi wa mfumo wa takwimu huria alisema dkt bakari vile vile katika kurahisisha upatikanaji wa takwimu hizo dkt bakari alisema takwimu hizo zitapatikana kwa njia ya simu za mkononi ujumbe huo ulipendekeza kuwa tovuti hiyo inaweza kuonyesha takwimu za misaada mbalimbali ya washirika wa maendeleo inavyotolewa na inalenga maeneo gani
2018-06-21T09:58:10
http://ega.go.tz/index.php/news/news_details/44
uwekezaji katika sarafu ya za kidijitali nchini tanzania teknokona teknolojia tanzania kwa kuanza tuu ipo jumuiya (blockchain tanzania) ambayo inalenga kuelimisha umma/watanzania kuhusu teknolojia iliyopo nyuma ya sarafu husika kwa maana ya kwamba mtu anaweza akawekeza na kupata faida baada ya muda fulani ila kabla ya kujiingiza huko basi ni vyema ukapata elimu na kuelewa kisha ufanye maamuzi ya kuwekeza lakini bado yapo makampuni nchini tanzania yanafanya biashara hiyo hata kuwa na sarafu zake zenyewe mathalani tembocoin ambayo tayari inafanya kazi lakini pia ira na sarafu yake ya diligence ingawa bado haijaingia sokoni tags blochain anzani intaneti ira sarafu za kijitali tanzania tembocoin [] makamu wa raisbenki kuu nasır hakimi amesema kuwa serikali ya iran imepiga marufuku shughuli zote za matumizi ya sarafu ya kidijitibitcoin []
2020-08-15T07:07:49
https://teknolojia.co.tz/uwekezaji-katika-sarafu-ya-za-kidijitali-nchini-tanzania/
makalla atoa darasa la kilimo na ufugaji watafiti wa uyole | mwanafasihi mahiri makalla atoa darasa la kilimo na ufugaji watafiti wa uyole rashid mkwinda 1140 pm a+ a print email mkuu wa mkoa wa mbeya amos makalla(mwenye miwani) akipata maelezo kuhusu shamba la mifugo la chuo cha utafiti cha uyole kutoka kwa meneja wa mradi huo dkt fumbuka mwakilembe(mwenye shati la kitenge) kulia ni mkuu wa wilaya ya mbeya nyerembe munassa mkuu wa mkoa wa mbeya amos makalla akizungumza na watafiti wa kituo cha utafiti wa kilimo na mifugo uyole mkuu wa mkoa wa mbeya amos makalla akiwa katika kundi la ng'ombe wanaofugwa kwenye shamba la mifugo la la kituo cha utafiti uyole mkuu wa mkoa wa mbeya amos makalla ametoa somo kwa taasisi za utafiti wa kilimo mifugo wa chuo cha kilimo uyole akiwataka kuwekeza zaidi kwenye utafiti ili kutoa wataalaam bora wa kilimo na ufugaji makalla amesema ili kujitosheleza kwa chakula na mazao ya mifugo nchini wataalamu bora wa utafiti wanahitajika ikiwa ni pamoja na kuwa na malighafi ya viwanda amesema rais dkt john pombe magufuli anataka nchi iwe na viwanda vidogo viwanda vya kati na vikubwa na kwamba viwanda hivyo vitategemea zaidi malighafi za ndani ambazo zitatokana na kilimo cha kitaalamu sanjari na upatikanaji wa pembejeo bora za kilimo amefafanua kuwa nchi yoyote inayowekeza kwenye utafiti huondokana na matatizo ya kukosekana kwa mbegu bora za mazao ya kilimo na mifugo na hivyo jambo pekee la taasisi za uyole kutumia teknolojia ya kisasa kwa usindikaji wa mazao ili kuyaongezea thamani kadhalika makalla amewataka maofisa kilimovikundi vya wakulima na wafugaji kutembelea chuo cha utafiti uyole ili kujifunza mambo mbalimbali ya kilimo na ufugaji ili kuzalisha kwa tija
2018-07-22T02:34:49
http://mkwinda.blogspot.com/2016/06/makalla-atoa-darasa-la-kilimo-na.html
mbuta nanga blogmagazine/ since 2011 top in town' * in flora lyimo blog * ushauri mdogo na wakuwaelewesheni nyie mnaotumiwa na kuwasababishia wasanii wetu hata wakija hapa uk watu wasiende kwenye show zao eti unakuta mtu upo kwenye shughuli alafu na picha ulipigwa mara wewe usiwekwe hewani wengine wa wekwe alafu hizo hizo picha uje kuzikuta your on tag na huyo haters ndo kiongozihaiwezekani msinichokoze nawaomba ooo * in flora lyimo blog * ushauri mdogo na wakuwaelewesheni nyie mnaotumiwa na kuwasababishia wasanii wetu hata wakija hapa uk watu wasiende kwenye show zao eti unakuta mtu upo kwenye shughuli alafu na picha ulipigwa mara wewe usiwekwe hewani wengine wa wekwe alafu hizo hizo picha uje kuzikuta your on tag na huyo haters ndo kiongozihaiwezekani msinichokoze nawaomba ooo jamani natumaini hamjambo hii ni ukweli kutoka kwangu kwa wale wote mnao nitag tag au kupost anything kwa wall yangu huko fb ukiona nimeitoa au haipo usikasirike ila kuna watu ambao ni wanafiki na haters wangu wakubwa ambao wanawatumia ili nisijue ila najua sana im gods girl na kuwataja sina muda kwani nikuwapa watu vicheo visivyowastaili au vizito kuwashindasasa basi ukikuta nimeitoa jua sitaki unafiki and pls dont do it na wale wasanii mnakuja jueni kuna mijitu minafiki na mkiungana nayo mtajikuta kwenye hizo show zenu nawao peke yenu ndo maana wengi mnajikuta hampati watu kwenye hizo show zenuhabari ndo hiyo mie nayasikia na sinyamazagi ruwa mangi
2017-10-23T05:53:58
http://missfbknitwearlyimo.blogspot.com/2012/09/in-flora-lyimo-blog-ushauri-mdogo-na.html
lg refrigerator 508 litres 10 years warranty non frost wednesday 0839 von hotpont freezer 320l yenye 5years warranty tupo k/koo na makumbusho stand kuu pia tunatoa home delivery mikoani tunatuma fridge boss lita 120 nzuri kwa matumizi ya nyumbani yenye warranty 2years tupo k/koo na makumbusho stand kuu pia tunatoa home delivery mikoani tunatuma 460 dar es salaam
2020-06-02T20:19:48
https://www.zoomtanzania.com/fridges-freezers?condition=new&p=4
mwanamke mmoja hawezi tumikia mabwana wawili mmmh | jamiiforums | the home of great thinkers mwanamke mmoja hawezi tumikia mabwana wawili mmmh discussion in 'mahusiano mapenzi urafiki' started by jay one apr 25 2011 hii misemo imepitwa na wakati eti mwanamke mmoja hawezi tumikia mabwana wawili tuongee ila mwanaume hawezi/ anaweza kutumikia wanawake wangapi limitless mbona najua kuna wanawake wana zaidi ya 3 men & anatoa service na si changu hii misemo kama 1 aliye juu msubiri chinino mfuate huko huko juu asipo shuka alaaaah 2 boss is always right heee how niwataje 3 haya ni maoni yangu binafsi si msimamo wa chama/serikali na huyo ndiye msemaji mkuu 4mwanamke nyonga tako hii sawa uso je sasa mbona saloon wanahangaika na uso kichwa tu jazieni mengine mh hapa leo me mweupeee du mr president elezea vizuri hueleweki labda mm peke yangu nimekuelewa kuwa mwanamke mmoja hawezi kutumikia mabwana wawili au zaidi sawa baadae umetuchanginyi tujazie aliye juu msubiri chini mimi yangu kuhusu mwanamke ni kweli lazima we na mabwana zaidi ya mmoja kasoro my wife kwanza huenda kamjogoo kako ni kadogo hashibi hivyo ni lazima achepuke huenda hujui katerero hivyo hakojoi (orgasm) humtengenezi kula juice nziito hadi ukashukia kula chumvini kuna michezo mingine huwa hairuhusiwi mumu na mke mpaka apate watu wa nje km sisi ndo tumuenyeshe zile nyimbo za mzee yusuf wewe ukipewa mzigo ambao hujapewa toka umjue utaanza kutangaza kuita wakwe na balozi hii pasaka mwachie mwenzako km umri bado akatanue atarudi tu kwani haina shobo wa makombo na hii inatokea kwa wote mume /mke akazuge nje kidogo mafiga matatu ili ugali uive aisifuye mvua jazieni mengineclick to expand nakupa mfano y it is said the 'boss' is always rite a sales rep an administration clerk and the boss are walking to lunch when they find an antique oil lamp ​they rub it and a genie comes out​the genie says 'i'll give each of you just one wish'​'me first me first' says the admin clerk 'i want to be in the bahamas driving a speedboat without a care in the world'​puff she's gone​'me next me next' says the sales rep 'i want to be in hawaii relaxing on the beach with my personal masseuse an endless supply of pina coladas and the love of my life'​puff he's gone​'ok you're up' the genie says to the boss the boss says 'i want those two back in the office after lunch'​ ​usichukulie misemo literally hapo tunaoneshwa/elezwa jinsi hata kama decision ya boss ni mbaya at the end ndo yenye uzito​​
2017-07-21T01:23:27
https://www.jamiiforums.com/threads/mwanamke-mmoja-hawezi-tumikia-mabwana-wawili-mmmh.129774/
b&b anglars bed and breakfast economici anglars ti piacerà è una promessa anglars (13) anglars bed and breakfasts
2017-02-21T07:56:44
https://it.bedandbreakfast.com/midi-pyrenees-anglars.html
primary questions from hon juma selemani nkamia (10 total) je serikali itakamilisha lini ukarabati wa mradi wa maji wa ntomoko ili kuwaondolea wananchi adha ya ukosefu wa maji kwenye vijiji vya sambwa kirikima churuku jangalo jinjo hamai songolo na madaha mheshimiwa naibu spika kwa niaba ya waziri wa maji na umwagiliaji naomba kujibu swali la mheshimiwa juma selemani nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa naibu spika ukarabati wa mradi wa maji wa ntomoko ulianza kutekelezwa mwezi februari 2014 na mkataba wa kazi hii ulikuwa ni wa miezi sita kutokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha kazi zilizopangwa kutekelezwa hazikuweza kukamilika katika kipindi cha miezi sita gharama ya mradi huo ni shilingi bilioni 287 utekelezaji wa mradi unaendelea na hadi sasa mkandarasi amekwishalipwa jumla ya shilingi milioni 8415 mwezi agosti 2015 wizara ilituma shilingi milioni 600 mwezi januari kwa ajili ya kuendelea na kazi aidha wizara itatuma shilingi milioni 7287 mwezi februari 2016 na itaendelea kutuma fedha kwa ajili ya kukamilisha mradi huo wizara imejipanga kukamilisha mradi huo mwezi aprili 2016 mheshimiwa naibu spika mradi huo utakapokamilika wananchi wa vijiji vya makirinya hamai songolo kirikima lusangi madaha churuku jinjo kilele cha ng‟ombe na jangalo watanufaika na huduma ya maji bei ya dawa za binadamu imekuwa ikipanda kila wakati na serikali imekaa kimya wakati wananchi wake wanaumia je serikali ina mpango gani wa kuanzisha chombo maalum cha kudhibiti bei ya dawa za binadamu hapa nchini naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto alijibu mheshimiwa naibu spika kwa niaba ya waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto naomba kujibu swali la mheshimiwa juma seleman nkamia mbunge wa jimbo la chemba kama ifuatavyo mheshimiwa naibu spika ni kweli dawa za binadamu huwa zinapanda mara kwa mara kutokana na ukweli kwamba asilimia 80 ya mahitaji ya dawa yananunuliwa kutoka nje ya nchi pale ambapo sarafu yetu inaposhuka thamani au sarafu ya dola inapopanda basi bidhaa mbalimbali toka nje ya nchi zikiwemo dawa hupanda bei ili kudhibiti upandaji wa bei za dawa wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto kwa kushirikiana na wizara ya biashara na viwanda tunaandaa mkakati wa kuongeza uzalishaji wa dawa ndani ya nchi ili angalau kukidhi asilimia 60 ya mahitaji katika kipindi cha miaka mitano ijayo mheshimiwa naibu spika wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto pia inaangalia uwezekano wa kuunda chombo cha kusimamia gharama na bei zinazotozwa na vituo vya kutolea huduma za afya ikiwa ni pamoja na bei za dawa na vifaa tiba vile vile bohari ya dawa imeandaa mipango ya kuanza kununua dawa moja kwa moja toka kwa wazalishaji ili kudhibiti bei za dawa na kuongeza upatikanaji wake kwa bei nafuu naomba mheshimiwa mbunge avute subira wakati mikakati hii ya kudhibiti bei za dawa inaendelea kutekelezwa mheshimiwa rais wakati wa kampeni alipotembelea wilaya ya chemba aliahidi kuongeza fedha za ujenzi wa jengo la halmashauri mpya ya wilaya je katika mwaka huu wa fedha serikali imetenga kiasi gani kuendeleza ujenzi huo mheshimiwa naibu spika kwa niaba ya waziri wa nchi ofisi ya rais tamisemi naomba kujibu swali la mheshimiwa juma seleman nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa naibu spika kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 halmashauri ilitengewa jumla shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa ofisi ya halmashauri ya wilaya ya chemba hadi machi 2017 fedha zote zimepokelewa na kazi inaendelea vizuri katika mwaka wa fedha 2017/2018 serikali imepanga kutumia shilingi milioni 600 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi je ni lini serikali itajenga mahakama ya wilaya ya chemba naibu waziri ofisi ya waziri mkuu kazi ajira na vijana (kny waziri wa katiba na sheria) alijibu mheshimiwa mwenyekiti kwa niaba ya waziri wa katiba na sheria napenda kujibu swali la mheshimiwa juma suleimani nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa mwenyekiti lengo la serikali ni kusogeza huduma karibu na wananchi juhudi kubwa zinaendelea kufanyika kuhakikisha kuwa kila wilaya nchini inakuwa na mahakama katika mwaka wa fedha 2018/2019 serikali imepanga kujenga jingo la mahakama wilaya ya chemba mhe moshi s kakoso (kny mhe juma s nkamia) aliuliza wilaya ya chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika hospitali ya wilaya ya kondoa je serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha wilaya hiyo inapata hospitali mheshimiwa naibu spika kwa niaba ya waziri wa nchi ofisi ya rais tamisemi naomba kujibu swali la mheshimiwa juma selemani nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa naibu spika halmashauri ya wilaya ya chemba imetenga kwa kupima eneo la ekari 237 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali ya wilaya katika mwaka wa fedha 2017/2018 halmashauri imeomba maombi maalum ya shilingi bilioni mbili ili kuanza ujenzi wa hospitali hiyo aidha upo mpango wa kukopa kutoka mfuko wa taifa wa bima ya afya ili kufanikisha ujenzi wa hospitali hiyo kwa awamu ofisi ya rais tamisemi itashirikiana na halmashauri ya chemba ili kuhakikisha mipango ya ujenzi wa hospitali hiyo unafanikiwa (makofi) wilaya ya chemba haina kituo cha polisi je ni lini serikali itaanza ujenzi wa kituo cha polisi na nyumba za askari mheshimiwa naibu spika kwa niaba ya waziri wa mambo ya ndani ya nchi naomba kujibu swali la mheshimiwa juma nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa naibu spika ni kweli kuwa jeshi la polisi lina uhaba wa vituo vya polisi pamoja na nyumba za kuishi askari kote nchini ikiwemo wilaya ya chemba ili kutatua changamoto hii jeshi la polisi linashirikisha wadau wa eneo husika pamoja na wadau wengine wa maeneo kwa maendeleo ili kufanikisha azma ya serikali ya kujenga vituo vya kisasa vya polisi pamoja na nyumba za kuishi askari mheshimiwa naibu spika wilayani chemba jeshi la polisi kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya wananchi na wadau wengine wapo kwenye hatua za awali za kuanza ujenzi wa kituo cha polisi aidha kwa sasa mchoro wa ramani ya kituo na gharama za ujenzi (boq) zimeshakamilika na ukusanyaji wa mahitaji ya ujenzi unaendelea mheshimiwa naibu spika naamini jitihada hizi zitaungwa mkono na mheshimiwa mbunge ili kuhakikishia wananchi wake usalama wao pamoja na mali zao je ni lini barabara ya lami kutoka handeni chemba kwamtoro hadi puma singida itaanza kujengwa mheshimiwa spika kwa niaba ya waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano naomba kujibu swali la mheshimiwa juma selemani nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa spika barabara ya handeni kiberashi kwamtoro singida yenye urefu wa kilometa 461 inayopita katika mikoa ya tanga manyara dodoma na singida inaunganisha ukanda wa mashariki ukanda wa kati na ukanda wa kaskazini magharibi barabara hii inaunganisha mikoa ambayo mradi wa bomba la mafuta kutoka hoima uganda hadi tanga unakopita mradi huu ni muhimu sana kwani utaweza kuinua uchumi wa nchi yetu mheshimiwa spika serikali kwa kutumia fedha za ndani tayari imekamilisha upembuzi yakinifu wa kina wa barabara hii ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii utaanza katika mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kazi ya ujenzi mheshimiwa spika serikali inaendelea na juhudi za kutafuta fedha za kutosha kukamilisha ujenzi wa barabara hii muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu shule za sekondari za farkwa na msakwalo zilizoko wilayani chemba zimepandishwa hadhi kuwa za a level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo je serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo naibu waziri ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa (mhe joseph g kakunda) alijibu mheshimiwa naibu spika kwa niaba ya waziri wa nchi ofisi ya rais tamisemi napenda kujibu swali la mheshimiwa juma selemani nkamia mbunge wa chemba kama ifuatavyo mheshimiwa naibu spika shule ya sekondari msakwalo ilikuwa ikitumia maji ya bomba kutoka katika kisima cha kijiji na shule ya sekondari farkwa ilikuwa inatumia miundombinu ya kuvuna maji ya mvua na pia ilikuwa ikitumia maji ya bomba kutoka katika kisima cha kijiji visima hivi pamoja na uchakavu wa miundombinu havikuwa na uwezo wa kuzalisha maji ya kutosha kwa matumizi ya vijiji pamoja na shule hivyo shule hizo kushindwa kupata maji ya kutosheleza kwa mwaka mzima mheshimiwa naibu spika ili kutatua tatizo la maji katika shule za sekondari msalikwa na farkwa serikali katika mwaka wa fedha 2017/2018 ilitoa jumla ya shilingi milioni 104 kwa shule ya sekondari msalikwa na shilingi milioni 87 kwa shule ya sekondari farkwa kwa ajili ya kuchimba visima na kufanya ukarabati wa miundombinu ya mfumo wa bomba kwenye shule hizo kazi ya uchimbaji wa visima na ukarabati wa miundombinu ya mabomba katika shule hizo imekamilika na wanafunzi kwa sasa wanapata maji ya kutosha
2018-12-15T11:57:46
http://parliament.go.tz/polis/members/36/primary-questions
serikali kusaidiana na taasisi ya millen magese mapambano dhidi ya tatizo la endometriosis | pamoja blog » serikali kusaidiana na taasisi ya millen magese mapambano dhidi ya tatizo la endometriosis 3/30/2016 081300 pm mmoja wa madaktari bingwa wa wanawake wa hospitali ya muhimbili akitoa maelezo machache labels
2017-06-27T15:39:49
http://www.pamoja.co.tz/2016/03/serikali-kusaidiana-na-taasisi-ya.html
discussion in 'mahusiano mapenzi urafiki' started by shanon jun 13 2009 mbona wanaume wanafanya ngono nje ya ndoa mbona wanaume wanafanya ngono nje ya ndoaclick to expand wanawake hawafanyi hivyo mbona una kuwa one sided kwenye swala ambalo lina julikana wazi jinsia zote zina fanya kufanya ngono nje ya ndoa ni tabia za mtu iwe mwanaume au mwanamke kulaleki you are a genius wakati wanafanya ngono wewe unakuwa ukifanywa nini kweli kuku ni kuku tu post nne ushaachia ushuzi umefulia mazee sikuelewi sijui unamaanisha nini sikuelewi sijui unamaanisha niniclick to expand unahukumu watu kwa namba zao za post bila kuwa na post 4 ungefikisha post 948 halafu toka lini kuku akaachia ushuzi shanon huwa wanafanya na wanaume wenzao ni mtu na mtu but most of them ni wanaume na hii inasababishwa na necha ya maumbile kati ya mwanamke na mwanaume mwanaume ameumbwa katika mazingira ya kutaka kufanya ngono mara kwa mara tofauti na mwanamke kwani anakuwa amebaka au kunakuwa na makubaliano baina ya huyo mfanya na mfanywa kama jibu ni ndio basi mfanywa ndo mbaya kwa nini amkubali mume wa mtu au huwa wanabaka si ana chojoa mavazi yake mwenyewe na kuachia neema ya mungu kwa huyo mwanaume mods bandwidth tafadhalilol sio kosa lake jamani msameheni tu mhn hili sijui ila tuache uzinzi na uroho wa miili ya watu ala hahahhahahahha mtn you are tooo rude shanon mie nandhani kama nimekuelewa vizuri swali lako ni kwamba kwanini percentage ya wanaume wanaofanya ngono nje ya ndoa ni kubwa kuliko wanawake au nimekosea usivunjike moyo kwasababu ya vijembe vya humu jamvini nafikiri swali lake ni kama hivyo alivyoelezea agika na ni kweli wanaumme wanatoka nje ya ndoa zaidi ya wanawake yaani kutoka nje ya ndoa imekuwa kama part ya ndoa mtu anakuwa na mchumba huku bado ana kimada mpaka anaowa anaendeleza tuu nafikiri swali lake ni kama hivyo alivyoelezea agika na ni kweli wanaumme wanatoka nje ya ndoa zaidi ya wanawake yaani kutoka nje ya ndoa imekuwa kama part ya ndoa mtu anakuwa na mchumba huku bado ana kimada mpaka anaowa anaendeleza tuuclick to expand yote haya yanatokea kwa sababu ya mfumo dume wanaume wengi wanaona ni jambo la kawaida na pengine la kujisifia badala ya kuona kwamba wanakosea hakuna anyeweza kusema kwa uhakika nani zaidi kati ya wanaume na wanawake katika kungonoka nje ya unyumba ila jambo moja ni dhahiri sisi ni wanyama we cant deny that and that is the reason hakuna cha tabia wala nini we are animals with utashi so we are expected to use it to fit into human community mume kufanyana nje ya ndoa sana huchangiwa na mabinti wenyewe kwa sababu mabinti wengi wakati huu hutaka wa2 ambao majukumu wanayaweza na ukionyesha kuwa mke wako unamlisha na kumvisha vizurisio siri watajileta wenyewe tu wa kula utachagua mwenyewe mume kufanyana nje ya ndoa sana huchangiwa na mabinti wenyewe kwa sababu mabinti wengi wakati huu hutaka wa2 ambao majukumu wanayaweza na ukionyesha kuwa mke wako unamlisha na kumvisha vizurisio siri watajileta wenyewe tu wa kula utachagua mwenyeweclick to expand ina maana ukifuatwa na mabinti huwezi kusema hapana ina maana akina dada/wanawake wanapofuatwa basi wasiseme hapana nilikuwa nadhani wanaume wanaogopa wanawake wanaowafuata kumbe siyo hivyo makubwa dunia imebadilika sana mimi siamini haya madai ya kwamba wanaume wanatoka nje ya ndoa kuliko wanawake hatujaachana mbali hata kidogo
2016-12-11T02:19:32
http://www.jamiiforums.com/threads/wanaume.31249/
nyuzi za matatizo ya magonjwa mbali mbali yaliyotolewa ufafanuzi | jamiiforums | the home of great thinkers nyuzi za matatizo ya magonjwa mbali mbali yaliyotolewa ufafanuzi kama una matatizo ya nywele bofya hapa http//wwwjamiiforumscom/jfdoctor/887152unatokwananyweleunakiparajioneemaajabuyahtml
2016-12-08T18:09:39
http://www.jamiiforums.com/threads/nyuzi-za-matatizo-ya-magonjwa-mbali-mbali-yaliyotolewa-ufafanuzi.327733/
ndoa mashoga ni kupata kasi world wide hello swahili speakers stories 4 hotblooded lesbians ndoa mashoga ni kupata kasi world wide hello swahili speakers sheria ya kwanza katika nyakati za kisasa kutambua ndoa za jinsia moja zilipitishwa wakati wa muongo wa kwanza wa karne ya 21 kama ya aprili 2013 thirteen nchi (argentina ubelgiji canada denmark iceland uholanzi norway ureno hispania afrika kusini na sweden na sasa urugwai new zealand majimbo tisa nchini marekani kuruhusu jinsia moja wanandoa kuoa sehemu za brazil na mexico pia ni kuwa pamoja na maendeleo ya haki za binadamu kuhusu wanandoa wa jinsi moja tayari kusubiri katika miswada (mapendekezo inasubiri au kupita) hebu kupata tayari moyo kwa ajili ya nchi zifuatazo andorra columbia finland ufaransa ujerumani ireland luxemburg nepal new zealand taiwan uingereza na uruguay na kuna sehemu ya scotland australia na mexico nchini marekani kwamba ni juu ya bodi ireland ana kuwaita kura ya maoni ya jumla ya kubadili sheria yoyote muhimu afrika ni tishio kwa haki za mashoga lgbt united states haki mrengo wainjilisti kumwaga fedha katika mafunzo ya wahubiri na inaunga mkono vyombo vya habari na dola hizi ni wakristo kukuza dhana kwamba ushoga ni magharibi ya ugonjwa na kunukuu kuchaguliwa mistari ya kibiblia namshukuru mungu kwa ajili ya makundi ya haki za binadamu kwamba kufuatilia na kuripoti vurugu dhidi ya mashoga katika nchi hizi za afrika bado kuna nchi ambazo adhabu ya kifo katika kikosi kwa ajili ya watu hawakupata katika vitendo vya ushoga 93 mataifa katika ulimwengu bado kisheria kuwaadhibu ushoga katika 7 ya hizi iran saudi arabia yemen falme za kiarabu sudan nigeria mauritania mashoga na wasagaji wanaadhibiwa kwa adhabu ya kifo ni vigumu kwa mashabiki wa kidini kwa kutambua kwamba watoto wote wa kimataifa wanapaswa kuwa na haki za binadamu ambayo katika akili yangu ni upendo jirani yako mstari kwa kupatikana katika dini zote posted by paulakey saa 0121 tagged with nchi 11 kuunga mkono ndoa za jinsia moja 12 zaidi ni kupitisha miswada hivi karibuni nchi 23 kutambua ndoa za jinsia moja watumiaji katika kama paulakey ingia nje posted by paulakey at 126 am notify me of followup comments by email notify me of new posts by email 同性恋婚姻是蓄势待发 万维网 hello chinese speaking people 316542 spam blocked by akismet
2017-06-24T20:56:15
http://stories4hotbloodedlesbians.com/ndoa-mashoga-ni-kupata-kasi-world-wide-hello-swahilis-speakers/