text
stringlengths
0
4.5k
Nini mustakabali wa Zanzibar kwa miaka mitano ijayo?
Ni swali wanalojiuliza watu wengi, baada ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), kumtangaza Dk. Ali Mohamed Shein, kuwa mshindi wa nafasi ya urais kwenye uchaguzi wa marudio uliofanyika Jumapili iliyopita kwa kupata kura 299,982, sawa na asilimia 91.4.
Ushindi huo umeweka historia ya pekee kwa Zanzibar tangu kurejea kwa uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1995.
Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi huo wa marudio yaliyotangazwa na Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha, anayemfuata Dk. Shein ni Hamad Rashid Mohamed wa chama cha ADC, aliyepata kura 9,734 sawa na asilimia tatu, huku Maalim Seif Sharf Hamad wa CUF aliyetangaza kususia uchaguzi huo, akipata kura 6,076 sawa na asilimia 1.9.
Tangu mwaka 1995, CUF imekuwa mpinzani mkubwa wa CCM na karibu kila uchaguzi, imekuwa ikitangazwa na ZEC kupata zaidi ya asilimia 40 ya kura zilizopigwa.
Mwaka 1995, mgombea wa CCM, Dk. Salmin Amour Juma, alitangazwa kushinda kwa kupata kura 165,271 sawa na asilimia 50.2 huku Maalim Seif wa CUF akiwa na kura 163,706 sawa na asilimia 49.8 ya kura 328,977 zilizopigwa.
Kadhalika, mwaka 2005, Amani Abeid Karume wa CCM alishinda kwa kura 239,832 sawa na asilimia 53.2, huku Maalim Seif akifuatia kwa kura 207,733 sawa na asilimia 46.1. Kura halali zilikuwa 450,968.
Kabla ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa mwaka 2010, hali ya kisiasa ya Zanzibar ilikuwa tete, hasa kutokana na viongozi wa CUF na wanachama wake kuamini kwamba kwa miaka yote wamekuwa wakishinda, lakini huibiwa kura.
Hali hiyo ilijitokeza dhairi Januari, 2001, baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, kwa kuibuka vurugu na watu kadhaa kupoteza maisha huku wengine wakikimbilia Shimoni, Mombasa nchini Kenya walikokaa kama wakimbizi.
Baada ya uhasama wa muda mrefu, mwaka 2010 ilipoundwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), hali ya kisiasa ya visiwa hivyo ilitulia.
Miaka mitano baadaye sasa, CUF imesusia uchaguzi wa marudio ikitaka mshindi wa uchaguzi wa Oktoba 2015 atangazwe, jambo linaloibua maswali mengi juu ya mustakabali wa visiwa hivyo.
Kwa muda mrefu Wazanzibar wamekuwa wakilalamikia mfumo wa Muungano, hali iliyofanya wakati wa mchakato wa Katiba Mpya wengi kupendekeza kuwa na Muungano wa Mkataba.
Hata hivyo, Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ilitokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba, ilipendekeza kuwa na Muungano wa Serikali Tatu ambazo zilionekana kuungwa mkono na Wazanzibari, waliokuwa wanataka mfumo wa mkataba. Lakini suala hilo liliota mbawa, baada ya Katiba Inayopendekezwa kulitupilia mbali. Swali, ni je, baada ya uchaguzi huu, hali itakuwaje?
Hoja ya Zanzibar yenye mamlaka kamili, imekuwa pia ikishinikizwa kwa muda mrefu na chama hicho cha upinzani, ambacho kwa mujibu wa matokeo hayo ya ZEC kwenye uchaguzi uliopita, yanaonyesha kimekuwa kikiungwa mkono na zaidi ya asilimia 40 ya watu wanaopiga kura.
Chama hicho kutokuwa na mwakilishi hata mmoja kwenye baraza la wawakilishi wala kiongozi serikalini, kunaweza pia kufanya hoja hiyo sasa ikashika kasi, kutokana na kuamini kwamba kurudiwa kwa uchaguzi huo kumetokana na shinikizo la Tanzania Bara.
Waziri wa Fedha wa SMZ, Omary Yusuph Mzee, akizungumza na Nipashe mapama wiki hii, ofisini kwake eneo la Vuga, Zanzibar, alisema lengo la serikali ni kuhakikisha inaondokana na utegemezi wa wafadhili.
Mzee alisema Zanzibar inategemea asilimia 20 ya misaada kwa ajili ya kukamilisha bajeti yake kila mwaka pamoja na mikopo kutoka taasisi za fedha, zikiwamo benki za nje.
Pia bajeti ya Serikali ya Zanzibar inategemea asilimia 20 ya mikopo kutoka nje, jambo ambalo litaweza kuathiri maendeleo ya visiwa hivyo, endapo nchi wahisani zitaweka mgomo kwa sababu ya uchaguzi huo.
Kauli hiyo ya Mzee inaibua swali la kwamba baada ya wahisani kuonyesha kutoridhishwa na uchaguzi ulivyokuwa, nini hatma ya visiwa hivyo endapo wakisusia kuchangia bajeti yake?
Alisema bajeti ya Zanzibar inategemea asilimia 26 hadi 28 ya mapato yanayotokana na sekta ya utalii wa ndani na nje na kwamba bado kunahitajika mikakati ili kupanua wigo wa kupata fedha.
Kwa mujibu wa Mzee, Zanzibar inapokea watalii kati ya 300,000 na 400,000 kwa mwaka na kwamba wanatarajia wataongezeka baada ya kufungua ofisi za kuhamasisha utalii wa nje.
Licha ya takwimu hizo kuonekana ziko juu, hali ya sasa ya takriban asilimia 50 ya Wazanzbiar ambao wanaunga mkono CUF kususia uchaguzi wa marudio, je hakutaathiri sekta ya utalii haswa ikitegemeana na historia ya miaka ya nyuma kabla ya muafaka kufikiwa?
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jijini Dar es Salaam, Prof. Haji Semboja wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), alisema utawala wa Zanzibar haukuwa halali kushikiliwa na CCM, kutokana na mwitikio mkubwa wa ushindi ulioonyeshwa na CUF.
“Rekodi ya uchaguzi uliopita inaonyesha vyama vya upinzani vilistahili ushindi kwa Tanzania Bara na Visiwani tofauti na awali, kwa sababu kama vimeweza kutoka asilimia 10 za ushindi na kuingia nafasi ya kinyang’anyiro, kisiasa vilistahili kushika madaraka kama dhamira ya serikali ni kuwa na vyama vingi,” alisema Prof. Semboja.
Alisema ingawa mfumo wa kiuchumi hautayumba kwa serikali hizo mbili kutokana na madaraka hayo kushikiliwa na CCM, bado mfumo wa kidemokrasia utaathiri vyama vinavyothubutu kushiriki uchaguzi, kwa sababu wananchi wanataka mabadiliko.
Katika hilo, alimshauri Dk. Shein, kufanya majadiliano na vyama vya upinzani ili kuwapo na Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
“Kwa sasa washirikiane wakae meza moja na kupanga maendeleo ya serikali yao, lakini CCM wawe wapole na CUF wawe wastaarabu kwa maridhiano ya pamoja kwa sababu nchi yetu ni moja, tujenge umoja wetu,” alisema Semboja.
Naye Prof. Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT), alisema kama jitihada za haraka hazitafanywa na viongozi wa ngazi za juu, akiwamo Maalim Seif, kuunganisha umoja wa wananchi, hali ya mauaji inaweza kujitokeza.
Alisema uchaguzi si tendo la kuhesabu kura na kushinda, bali ni tendo la kisiasa ambalo ndani yake linaunganisha muungano wa wananchi, hivyo uchaguzi ukiwagawa wananchi katika matabaka, inamaanisha uchaguzi huo ni batili kwa sababu haujaunganisha lengo moja.
Alisema uchaguzi wa marudio, uliofanywa Zanzibar Machi 20, mwaka huu, na kwa mara nyingine Dk. Shein kushinda urais kupitia CCM, umewapa ubumbuazi na kuwapiga ganzi Wanzanzibar wengi, kwa sababu tatizo kubwa ni uhalali wa rais aliyeshinda kwa wananchi.
“Ukifuatilia uchaguzi wa Oktoba, mwaka jana, mshindi hakutangazwa, na baadaye uchaguzi huu baadhi ya vyama vimejiondoa.
Kutakuwapo na hali ya kutoelewana kwa sababu uchaguzi huo, kulisababisha mtafaruku kwa Wazanzibari tangu awali, hivyo mgogoro ni jambo lisilozuilika kwa sasa Zanzibar,” alisema.
Aliongeza kuwa: “Mawasiliano ni jambo la busara kwa nchi yoyote yenye kupenda amani na taifa lake. Ushauri wangu serikali ya Zanzibar itafute njia ya kukaa na vyama vya siasa ili kuingilia kati hali ya mvutano unaoendelea kwa sababu wakipuuza jambo dogo waelewe hali ya uvunjivu wa amani inaweza kujitokeza na mauaji yataendelea,” alisema.
Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Paul Kuwenga, alisema suala la Zanzibar linahitaji kuangaliwa upya kwa sababu liko katika kipindi cha mpito wa vyama vingi.
Alisema kinachotakiwa ni ushirikishwaji kwa sababu jamii inayoishi humo ni mchanganyiko na kila moja ina uhuru wa kufanya uamuzi wake katika jambo fulani, badala ya kushinikizwa wakubaliane kwa sababu nchi iko katika utawala wa demokrasia.
Jana Zanzibar iliweka historia nyingine kwa wananchi wake kushuhudia Rais wa awamu ya saba, Dk. Shein akila kiapo cha kuongoza visiwa hivyo.
Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othuman Makungu, alimwapisha Dk. Shein saa tano asubuhi, ikifuatiwa na tendo la kupigiwa mizinga 21.
Dk. Shein ambaye aliingia uwanjani hapo akiwa na msafara wa magari 10 na pikipiki 13, kabla ya kula kiapo, alikagua gwaride maalum la majeshi ya ulinzi na usalama.
Rais huyo wa Zanzibar akizungumza baada ya kuapishwa, aliahidi kuongoza kwa haki na bila kumwonea mtu yeyote.
Pia aliahidi kuunda serikali makini ambayo itawasaidia Wazanzibari kujiletea maendeleo ya haraka, huku akisema afanya hivyo kwa kuangalia Ilani ya CCM ya mwaka 2015.
Dk. Shein alisema Zanzibar ina matatizo mengi na kwamba serikali makini itasaidia kutatua matatizo ya wananchi wake.
Dk. Shein alimwahidi Rais John Magufuli kwamba atashirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusimamia misingi ya uwajibikaji na kuhakiksha watumishi wa umma wanakuwa na nidhamu.
Kabla ya kula kiapo, Dk. Shein aliombewa dua na viongozi wa dini, akiwamo Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Khamis Haji Khamisi na Askofu wa Kanisa Katoliki Zanzibar, Augstine Shao na Askofu wa Kanisa la Anglikana, Michael Hafidh.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo Mawaziri, Makatibu Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais Magufuli, baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, Marais wastaafu na wananchi wa kawaida.
Viongozi wa chama kikuu cha upinzani cha CUF pamoja na wafuasi wao hawakuhudhuria sherehe hizo.
RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMUAPISHA MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU, KATIBU MKUU WA WIZARA YA AFYA PAMOJA NA BALOZI MMOJA IKULU YA CHAMWINO JIJINI DODOMA.SEPTEMBA 12,2018.
Iringa ni ngome ya CCM. Jana jioni Dr Slaa alitua Iringa na kuvuta umati mkubwa wa watu. Nilikuwapo pale Viwanja vya Mwembetogwa. Nini aliongea na kina nini ndani yake, nitachambua hapa kwa ufupi;
Nilifika viwanja vya Mwembetogwa saa kumi na robo jioni. Tayari Dr Slaa alishatua. Watu walikuwa wengi sana. Pamoja na uzoefu wangu wote wa kujipenyeza kwenye kundi la watu nikiwa na kamera, bado kwangu safari hii ilishindikana. Niliishia kutafuta sehemu ya juu kidogo nyuma ili walau nipate picha ya Dr Slaa akihutubia. (Picha ya kwanza hapo juu blogiini imepigwa na Francis Godwin.)
Nimekaa Iringa tangu mwaka 2004 na nimeudhuria mikutano yote ya kampeni za Urais kuanzia Jakaya Kikwete, Mbowe, Lipumba hadi Mrema, lakini niweke wazi. Mkutano wa jana pale viwanja vya Mwembetogwa umevunja rekodi zote katika kujaza watu kwa mujibu wa kumbukumbu zangu za tangu 2004. Katika chaguzi ziliopita kuna watumishi wa Serikali waliokuwa wakienda kwenye mikutano ya vyama vya upinzani kwa kunyata. Walikuwa na hofu ya kuonekana wanaunga mkono upinzani na kuonekana kwao kwenye mikutano ya akina Mbowe, Zitto na Lipumba ingetafsiriwa kuwa hawaipigii kura CCM. Jana kulikuwa na watu wa aina zote, hata makada wa CCM walifika pia.
Kwenye hotuba yake ya takribani dakika 43 Dr Slaa alijikita katika maeneo makubwa matatu;
Uchaguzi wenyewe; alianza kwa shambulizi dhidi ya Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ( JWTZ) na Polisi kwa tamko lao juu ya uchaguzi. Dr Slaa naye akasema ametoa tamko lake akiwa Njombe kushutumu hatua hiyo ya jeshi na polisi akisema kuwa ni kuwatisha wapiga kura.
Dr Slaa akagusia pia masuala ya elimu akisisitiza azma ya Chadema kutoka elimu bure kuanzia chekechea. Katika eneo hili Dr Slaa alifanikiwa pia ( kisiasa) kukwepa kutoa ufafanuzi wa ni kwa namna gani. Kuna mahali alifanikiwa sana alipojaribu kulinganisha na wakati wake alipokuwa shuleni na hali ilivyo sasa.
Hapo Dr Slaa aliweza kupenya kwenye kero na matatizo ya kila siku ya wapiga kura. Na ni mambo haya ambayo wapiga kura wanayaelewa zaidi kuliko kashfa za EPA, IPTL, Deep Green na nyinginezo ambazo akina Dr Slaa na wanasiasa wengine wameshindwa kuziweka katika lugha nyepesi ikamfanya mpiga kura wa Kihesa awaelewe. Mpiga kura ambaye bado anaumiza kichwa kila siku kutafuta senti za kununulia mafuta ya taa na michango ya madawati ya watoto wake.
Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kumsikiliza Dr Slaa akihutubia ' live'.
Nguvu zake:
- Anaongea kwa staili ya kimahubiri. Ana uzoefu katika hilo. Kuna wakati anayaacha matokeo ya anachoongea kwa Mungu na watu.
- Dr Slaa mara kwa mara anatumia nafsi ya tatu; " Wanasema Dr Slaa…." Anayesema hayo ni Dr Slaa.
- Wakati mwingine anaonyesha jazba kidogo. Maneno kama ; " Kama Kikwete mwanamme…" Anatakiwa ayaepuke. Yanaweza kutafsiriwa vibaya na katika nchi nyingine wanaharakati wa jinsia wanaweza kumjia juu.
Tatizo la CHADEMA na vyama vingi vingine vya upinzani linabaki pale pale; oganaizesheni. Wengi katika umati ule uliokusanyika pale Mwembetogwa hawajui zilipo ofisi za CHADEMA mjini. Hawawajui makada wa Chadema. Mkutano kama ule ilikuwa ni fura kwa Chadema kuwatambulisha makada wa Chadema na wapi wapenzi wa Chadema waende kupata taarifa za chama chao.
Badala yake, wengi wa waliokwenda pale Mwembetogwa kumsikiliza Dr Slaa wamerudi majumbani kwao. Na atakayewatembelea tena kuzungumzia uchaguzi ni Balozi wao wa nyumba kumi.
Naam. Demokrasia yetu bado changa. Na ishara za jamii inayotaka mabadiliko inaonekana. Tuwe na ujasiri wa kutoa maoni yetu kwa kutanguliza MASLAHI YA TANZANIA KWANZA. Hata Roma haikujengwa kwa Siku Moja.
Tunakushukuru kwa kukiri kuwa haijawahi kutokea tangu uhuru watu wengi hivyo kwenda kwenye mkutano wa kampeni. Kumbuka kuwa watanzania wa leo sio wa enzi zile wanajua wanachokifanya na hata wanachokitaka
Je kulikuwa na ugumu gani kufanya utafiti wa haraka tu, kujua kama watu waliofika waliridhika na hotuba ya Slaa? Na matarajio yao yalikuwa nini?
Je kwa nini hawakuja na T-shirts kwenye mkutano huo? mana T-shirts kazi yake ni kutangaza na tunatangaza kwa watu wasiojua.
Uwe makini na Chambuzi zako, wewe sio kila kitu ni vyema ungeweka maoni ya watu waliohudhuria mana hao ndio wapiga kura, wewe hata ukimpigia Kikwete wao wanajua nani wa kumpigia. Japo tunathamini mawazo yako lakini usitake kutupotosha.
Unaandika usichokijua. Sasa hilo ni tatizo lako. Kama unahitaji msaada wa kujuzwa, omba.
Amini usiamini hiyo ama kweli Mwenyeezi Mungu kampa Mwanadamu akili.
Chama Cha Demokrasia na Maedeleo (Chadema) kiko hatarini wagombea wake wa ubunge na udiwani kuenguliwa katika Jimbo la Maswa Magharibi katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumapili kutokana na kuhusishwa na vurugu zilizotokea wiki iliyopita na kusababisha kifo cha mtu mmoja.
Tishio la wagombea wa Chadema kuenguliwa linatokana na Kamati ya Maadili ya Uchaguzi ya Jimbo la Maswa Magharibi kupendekeza wagombea wa Chadema waenguliwe kwa madai ya kuwa chanzo cha vurugu hizo.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya ya Maswa, Magharibi Elizabeth Kitundu, alisema jana kuwa kamati hiyo ilikutana Jumamosi iliyopita kujadili hoja ya kuwaengua wagombea wa Chadema kushiriki katika uchaguzi.
Kitundu alisema kuwa tume hiyo imepeleka mapendekezo hayo kwa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi ya Tume ya taifa ya uchaguzi (NEC).
Aliongeza kuwa Chadema nao tayari wamepeleka barua ya kujitetea kupinga kuenguliwa katika uchaguzi huo. Hatua ya kamati hiyo inadaiwa kuchukuliwa kufuatia vurugu zilizotokea Oktoba 21 na kusababisha kifo cha mfuasi mmoja wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Kwilasa, ambaye alipigwa jiwe na kuchomwa na kitu chenye ncha kali na kufariki papo hapo katika vurugu zilizotokea katika kijiji cha Kizungu wakati mgombea ubunge wa Jimbo la Maswa Magharibi kupitia Chadema, John Shibuda, alipokuwa akijinadi mbele ya wananchi wa kijiji hicho.
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Lewis Makame, alipoulizwa kama NEC imepokea mapendekezo ya kuwaengua wagombea wa Chadema, alisema kuwa asingeweza kulizungumzia suala hilo kwa kuwa alikuwa katika kikao.
Katika hatua nyingine, Jeshi la polisi limemwachia Shibuda aliyekuwa anashikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na vurugu zilizosababisha kifo cha mfuasi wa CCM.
Shibuda aliwekwa mahabusu tangu Oktoba 21, baada ya kutokea vurugu baina ya wafuasi wa Chadema na CCM iliyotokea katika kijiji cha Kizungu Kata ya Buchambi wilaya ya Maswa.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, alisema upelelezi wa kina uliofanywa na jeshi hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama nchini umebaini kuwa Shibuda hakuhusika na tukio hilo.
Alisema kwa mujibu wa upelelezi huo wakati tukio hilo likitokea, Shibuda alikuwa akifanya mkutano wa hadhara umbali wa mita 200 kutoka eneo la tukio na kuwa upelelezi huo pia hauonyeshi kuhusika kwake namna yoyote ya uchochezi wa vurugu hizo.
Manumba aliwaambia waandishi wa habari mjini Maswa kuwa Shibuda aliachiwa huru juzi majira ya saa 1:45 usiku ili aendelee na kampeni.
Hata hivyo Kamishna Manumba alisema kuwa upelelezi unaendelea na iwapo utapatikana ushahidi wa kutosha kwamba alihusika, atapaswa kuunganishwa katika tuhuma za mauaji hayo inayowakabili watu 11 ambao ni wafuasi wa Chadema.
"Kwa kuwa upelelezi haufanyiki kwa kipindi kifupi na kwisha yawezekana baadaye Shibuda pia akakamatwa na kuunganishwa kwenye kesi hiyo ya tuhuma ya mauaji, lakini kwa sasa tumejiridhisha kabisa kuwa hana kosa na ndiyo maana tumemwachia huru," alisema.
Kuhusu tuhuma za mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Robert Kisenha, kumpiga Mkuu wa Polisi Wilaya ya Maswa, Peter Ndunguru, DCI Manumba alisema mtuhumiwa huyo tayari amekamatwa lakini kwa sasa yuko nje kwa dhamana.
"Pamoja na kuwa mtuhumiwa huyu wa kumshambulia OCD yuko nje kwa dhamana, tuhuma zake tunazipeleleza kujua kama kweli alifanya hivyo na tukipata ushahidi wa kutosha basi sheria itafuata mkondo wake," alisema Manumba.
Kutokana na tukio hilo, watuhumiwa hao 11 jana walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Maswa na kusomewa shitaka la mauaji ambapo hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.
Watuhumiwa hao walisomewa shtaka hilo mbele ya Hakimu mkazi wa wilaya hiyo, Thomson Mtani, ambapo kesi hiyo imepangwa kutajwa tena Novemba 8, mwaka huu. Watuhumiwa wa kesi hiyo ya mauaji ni pamoja na Mohammed Juma (30), Constantine Zengo (20), Raphael Deusi (20), Juvent William (30), Frank Gogadi (22) na Emmanuel Bundala (22).
Kwa hiyo Wasimamizi wote wa uchaguzi hawana loyalty kwa Makame na timu yake, bali kwa serikali ya CCM iliyowateua katika nyadhifa ambazo hatimaye wanakuwa wasimamizi wa uchaguzi. Maamuzi yao yanukuwa pro-CCM tu! Inawezekana kamati hiyo ya NEC ilipata agizo kutoka kwa Makamba kufanya hivyo.
Lakini habari nilizopata, yaani zilizovuja kutoka sehemu hiyo ni kwamba kamati hiyo ya NEC iligawanyika, yaani haikuwa unanymous katika pendekezo hilo. habari zinasema baadhi ya wajumbe walinunuliwa kwa fedha zilizotoka kwa mfanyabiashara mmoja maarufu wa sehemu hiyo ya nchi na ambaye amekuwa anabebea tuhuma nzito za ufisadi.
Mtoa habari wangu anasema mfanyabiashara huyo alitoa msukumo kwa kamati hiyo ya NEC kukaa haraka haraka baada ya kuona Shibuda ataachiliwa na polisi kwa sababu kwamba hana kosa.
Yesu sasa akawaagiza wale watu kumi na mbili ambao walikuwa wamesikiliza azimio lake kuhusu ufalme kupiga magoti kumzunguka. Akaweka mikono yake juu ya kichwa cha kila mtume,kuanzia Judas Iscariot na kuishia kwa Andrew. Baada ya kuwabariki akanyoosha mikono yake na kusali;
'' Baba yangu,sasa nawaleta kwako hawa watu[these men],taarishi wangu kutoka miongoni mwa watoto wetu duniani nimewachagua hawa kumi na mbili waende kuniwakilisha kama mimi nilivyofika kukuwakilisha. Wapende na uwe pamoja nao kama ulivyonipenda na kuwa pamoja nami. Na sasa,Baba yangu,wape hawa watu hekima ninapoweka shughuli zote za ufalme utakaokuja,mikononi mwao.Na ningependa,kama itakuwa utashi wako,nikae kidogo duniani kuwasaidia katika kazi zao za ufalme. Na tena,Baba yangu,nakushukuru kwa hawa watu,na ninawakabidhi kwakouwaweke ninapoendelea kumaliza kazi uliyonipa kufanya.''
Yesu alipomaliza kusali,mitume walibaki wameinama wote kwa dakika nyingi,na Peter ndiye aliyekuwa wa kwanza aliyethubutu kuinua macho na kumtazama Yesu. Mmoja baada ya mwingine wakamkumbatia Yesu,lakini hakuna aliyesema chochote. Kulikuwa na kimya kabisa katika sehemu hii,na viumbe wengi mbinguni walitazama chini kwa makini kinachoendelea,jinsi Yesu alipokaribia kuzikabidhi kazi za undugu wa kitakatifu ziwe chini ya uongozi wa akili za wanadamu.
Hotuba ya kusimika.
'' Nawatuma kutangaza uhuru kwa watumwa wa kiroho,furaha kwa wale ambao wapo katika minyororo ya woga;na kuwatibu wagonjwa kufuatana na utashi wa Baba yangu mbinguni. Mkiwakuta watoto wako katika adha,zungumzeni kuwapa moyo,na kuwaambia;
''Heri walio maskini wa roho,wanyenyekevu,maana utajiri wa mbinguni ni wao,
Heri wenye njaa na kiu ya haki,maana watashibishwa,
Heri wenye moyo safi,maana watamuona Mungu.
''Na hivyo hivyo zungumzeni kwa watoto wangu maneno haya zaidi ya kuwafariji kiroho na kuwaahidi.