text
stringlengths 43
182k
| timestamp
timestamp[s] | url
stringlengths 16
3.37k
|
---|---|---|
mbona mnazidi kutubana | simbadeo2000
mbona mnazidi kutubana
watoto wakikipiga cha mchangani viwanja vya michezo kwa watoto linazidi kuwa tatizo kubwa hapa ni katika moja ya mitaa iliyo temeke ili tuingie kwenye ramani ya dunia ya soka hatuna budi kutenga maeneo maalumu kwa michezo siyo kwa soka tu bali hata kwa michezo mingine
kila la kheri serikali mpya katika awamu ya nne kazi
« baraza jipya katika serikali ya awamu ya nne
ujio wa bush tanzania na kwingineko barani afrika » | 2018-03-17T23:44:14 | https://simbadeo.wordpress.com/2008/02/13/mbona-mnazidi-kutubana/ |
raia mwema waziri matatani
habari sakata la upanuzi bandari waziri matatani mwandishi wetu toleo la 235 18 apr 2012 wabunge wataka angoke nyaraka zaanikwa atofautiana na naibu na katibu mkuu wake alitaka kuwazunguka mkulo na dk kawambwa waziri wa uchukuzi omar nundu sasa anasubiri huruma ya rais jakaya kikwete kuendelea na uwaziri baada ya kamati ya kudumu ya bunge ya miundombinu kupendekeza avuliwe nafasi hiyo imefahamika
taarifa za suala hilo zinasema kamati ilitaka maelezo kuhusiana na taarifa za kwamba nundu amethubutu hata kukejeli maamuzi yaliyofanywa na serikali kupitia wizara ya fedha yakimhusisha waziri wa fedha mustafa mkulo na watendaji wengine wa wizara ya uchukuzi nundu aliingia katika kikao na laptop yake bila ya kuwa na nyaraka zozote wakati wabunge walikuwa na nyaraka na walipomhoji hakuwa na maelezo ya kuridhisha walimtaka aeleze ni kwa nini amefanya maamuzi kupingana na maamuzi yaliyokwisha kufanywa na wizara yake na wizara ya fedha na pia walitaka kujua safari alizokwenda nje ya nchi zilikuwa na maslahi gani kwa nchi anasema mbunge mmoja aliyehudhuria kikao hicho katika kikao hicho mbunge mmoja ambaye amewahi kuwa waziri mwandamizi alitoa mifano hai ya jinsi serikali ilivyofanikisha miradi yake katika mtindo ambao nundu anapingana nao na akamuasa mheshimiwa waziri unapaswa kuangalia maslahi ya nchi kwanza awali katika kikao chao na wabunge bodi na menejimenti ya tpa ilitofautiana waziwazi na waziri nundu ikiorodhesha sababu nne za kumpinga waziri nundu pamoja na viambatanisho vinavyothibitisha sababu hizo gazeti hili limefanikiwa kuona nakala za nyaraka mbalimbali ikiwamo viambatanisho kadhaa kuhusu mvutano huo ambao unaonyesha kuwa waziri nundu ametofautiana hata na naibu wake dk athumani mfutakamba na katibu mkuu wake omar chambo kiini cha mvutano huo inaelezwa kuwa baada ya kuteuliwa kuwa waziri ni kama amekuwa akivuruga mipango ya kimaendeleo iliyowekwa na waziri aliyemtangulia dk shukuru kawambwa kuhusu upanuzi wa bandari akiwa waziri wa uchukuzi dk kawambwa kwa kushirikiana na mamlaka ya bandari walitafuta mkopo kutoka serikali ya china kupitia benki ya exim ya china iliyoridhia kutoa mkopo wa dola za marekani takriban 524 ili zisaidie upanuzi wa gati namba 13 na 14 katika bandari ya dar es salaam kinachogomba katika mvutano huo ni uamuzi wa waziri nundu kumkataa mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo ambaye benki ya exim imependekeza ndiye awe mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo mkandarasi aliyependekezwa na benki ya exim ya china ili itoe mabilioni hayo kama mkopo ni kampuni ya huko huko china inayoitwa china communications construction company (cccc) taarifa zinadai kwamba waziri nundu anadaiwa kuwa na mkandarasi wake mfukoni ambaye ni kampuni nyingine ya china inayoitwa china merchants ambayo aliamua kuingia nayo mkataba wa makubaliano (mou) bila kuwahusisha watendaji wake na tpa wasaidizi wake wote waligoma kushirikiana naye na akalazimika kumfukuza mmoja wa wakurugenzi wake ambaye sasa amehamia wizara ya ujenzi waziri kwanza ameingia mou na kampuni hiyo katika kipindi ambacho tayari serikali imekwishakamilisha mchakato wa kupata fedha na kuanza kwa mradi cha kushangaza waziri alipoulizwa alisema kampuni hiyo ilikuja dar es salaam na baadaye yeye kuwafuata china lakini akashindwa kutoa maelezo ya kuhalalisha maamuzi yake anasema mbunge mwingine wa kamati hiyo kutokana na nguvu za kampuni hiyo inayopiganiwa dhidi ya cccc imeelezwa kuwa serikali inaweza kukosa mkopo huo unaotajwa kuwa wa riba nafuu ili kampuni mpya iendeshe si ujenzi wa mradi tu lakini baada ya mradi iendelee kumiliki utoaji huduma bandarini kwa kushirikiana na wadau wengine kwa mkataba wa miaka 45 hali ilivyokuwa kabla ujio wa nundu
mipango inadaiwa kuwa safi wakati wa waziri shukuru kawambwa ni wakati huo ambao tpa iliandikia wizara ya uchukuzi (wakati huo wizara ya miundombinu) kuelezea mapendekezo ya kupanua bandari wizara iliafiki mapendekezo ya tpa na kuchukua hatua ambazo ni kuiandikia wizara ya fedha barua zenye zenye kumbukumbu namba cb 230/364/01/62 ya aprili 14 2010 na ccb 364/505/01/54 ya julai 9 mwaka juzi (2010) ili ipate kibali cha kuomba mkopo kutoka serikali ya watu wa china wizara ya fedha iliunga mkono kuendeleza mchakato huo kwa kuomba mkopo benki ya exim ya china kupitia barua yenye kumbukumbu namba tyc/450/2/02 ya februari 22 mwaka jana na nyingine yenye kumbukumbu namba tyc/e/450/2/130 ya novemba 9 mwaka jana pamoja na barua ya januari 24 mwaka huu yenye kumbukumbu namba tyc/e/450/2/02 baada ya hapo wizara ya fedha ilitaarifu wizara ya uchukuzi kupitia barua yake yenye kumbukumbu namba tyc/e450/2/02 ya agosti 22 2011 kuhusu kuridhia kupatikana kwa mkopo na kushauri kuwa tpa iendelee na mchakato wa kupata mkopo husika kutokana na kibali hicho kutoka wizara ya fedha wizara ya uchukuzi ilitaarifu tpa kuendelea na mchakato wake wa kuomba mkopo kutoka benki ya exim sababu za kuomba mkopo sababu za kuomba mkopo kwa ajili ya upanuzi huo wa gati za bandari ya dar es salaam ni kwanza mkopo utatolewa kwa serikali ya tanzania kwa masharti nafuu ukiwa ni mkopo wa miaka 15 kwa riba ya asilimia mbili na kipindi cha mpito (grace period) ya miaka mitatu mkopo huo unatajwa kuwa nafuu kutokana na ukweli kwamba mikopo kutoka vyanzo vingine ina riba isiyopungua asilimia 55 na muda wake wa kurejesha ni mfupi ukiwa kati ya miaka mitano hadi 10 sababu ya pili ni kwamba mkopo kutoka serikali ya china una masharti nafuu na mradi utakuwa na faida kwa maelezo kwamba gharama za ujenzi zimekadiriwa kurejeshwa katika kipindi cha miaka 12 baada ya mradi kukamilika na hivyo faida yote kubakia kwa mamlaka ya bandari sababu ya tatu ya kungangania mkopo huo inatajwa kuwa ni serikali baada ya ujenzi wa mradi itaweza kukodisha shughuli za biashara na kupata faida zaidi kutokana na tpa kuwa na uwezo wa kupanda kodi ya pango na mrabaha sababu hiyo ya tatu inapingana na matakwa ya waziri nundu ambaye anataka ujenzi uendeshwe na kampuni nyingine ambayo pia baada ya ujenzi kukamilika itaendesha biashara na kujifidia gharama za ujenzi kwa miaka zaidi ya 45 kama mradi huu utatekelezwa na kampuni binafsi mwekezaji atahitaji kutumia gati kwa zaidi ya miaka 40 kabla ya kurejesha mikononi mwa serikali kwa mfano kampuni ya china merchants imependekeza kujenga kumiliki kuendesha gati namba 13 na 14 kwa miaka 45 tpa yamuumbua waziri mbele ya wabunge
katika hali isiyokuwa ya kawaida menejimenti ya bandari imewasilisha waraka kwa wabunge ambao ni wajumbe wa kamati ya bunge ya miundombinu ikieleza kutoridhishwa na waziri nundu kuhusu usimamizi wake katika mradi huo waraka huo unaeleza menejimenti imetathmini hoja za waziri wa uchukuzi na haikubaliani nazo zote kwa ujumla wake wanabainisha sababu za kutokukubaliana kuwa ni pamoja na kampuni ya cccc ilikuja kama mwekezaji wala si kama washauri (tofauti na anavyoeleza waziri) na ilifanya upembuzi yakinifu kwa gharama zake na mradi huu unatakiwa kutekelezwa chini ya utaratibu wa engineering procurement and construction (epc) ambapo mwekezaji anatakiwa kufanya upembuzi yakinifu usanifu (design) na kujenga wanaeleza pia kuwa sababu nyingine kuwa ni kampuni zinazopiganiwa na waziri nundu kwamba zitatekeleza mradi kwa gharama nafuu hazijathibitisha gharama halisi za mradi kwa sababu hazijafanya upembuzi yakinifu na kwamba gharama wanazotaja kuwa ni nafuu ni makisio tu wanaendelea kueleza kuwa kinyume cha kauli ya waziri nundu kwamba waziri wa biashara wa china anaunga mkono uamuzi wake (nundu) menejimenti haina ushahidi wa hilo na kwamba ushahidi uliopo kuhusu kampuni ya china merchants holdings anayoipigania nundu waliwahi kutaka kujitoa katika mradi baada ya kubaini tayari serikali ilianza mchakato na kampuni ya cccc kwa kutumia fedha za exim pamoja na hayo sheria ya manunuzi ya umma namba 21 ya mwaka 2004 inaelekeza chini ya kifungu cha 4 (1) cha sheria hiyo kukubaliana na masharti ya utekelezaji wa mkataba pale serikali zinapokubaliana jinsi ya utekelezaji wa manunuzi ya mradi husika hivyo kukubaliana na masharti ya mkopo ulioombwa kutoka exim hakukiuki sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 unaeleza waraka huo mdau mmoja wa sekta ya bandari alisema waziri nundu anapaswa kumpeleka mwekezaji anayemtaka kujenga bandari ya mbegani badala ya kulazimisha kumuingiza katika eneo la mradi ambalo tayari serikali imekwisha kamilisha mchakato wake kwa miezi kadhaa sasa raia mwema limekuwa likiandika utata katika upanuzi wa bandari ya dar es salaam suala ambalo waziri nundu amekuwa akilitolea ufafanuzi kwa jazba hadi kufikia kutoa matangazo ya kutetea uamuzi wake huo na kukejeli taarifa zinazopingana naye soma zaidi kuhusu
nundu tufuatilie mtandaoni
waziri nundu aepusha vurugu kampuni iliyomngoa waziri yapigwa stop ni kejeli rais zanzibar kuwa waziri bila wizara bandari wamzunguka waziri mwakyembe maoni ya wasomaji
lazima tutambue kuwa mwalimu
permalink submitted by joseph chengula (not verified) on thu 20120419 1130 lazima tutambue kuwa mwalimu aliamini kuwasisi bado wachanga kiakilikwa hiyo hatuna budi kutocheza ngoma tusizozijua
sioni haja ya kumwadabisha
permalink submitted by davishermans (not verified) on mon 20120423 0852 sioni haja ya kumwadabisha waziri kutokana na vyombo vya habari uangaliwe ukweli upo wapi utumike kwenye kikao cha bunge tumeona waziri akijitetea kutokana na utetezi wake mimi naona kuna kundi ambalo may be ndio liloweka taarifa hii kwenye gazeti naona hili kundi lina maslahi binafsi sio ya kitaifa nashukuru mbunge mnyika kwa kuona kuwa ujanja umejificha ambao unaweza kuingiza taifa hili kwenye janga au hasara haiji akilini mtu akufanyie upembuzi yakinifu halafu umpe yeye hiyo kazi kazi ya kufanya upembuzi ibakie ni ya serikali baada ya hapo ndio tenda itangazwe mshindi apatikane kwa vigezo hili la mshindi apatikane kwa vigezo ndio wanalolikataa watoa habari ambalo waziri anakubaliana nalo sasa waziri ana kosa gani asifuate taratibu huu si ungwana hatakidogo raisi kikwete usifuate maneno ya watu angalia ukweli
huyu waziri kwa nini ni
permalink submitted by walter samuel mairo (not verified) on mon 20120423 1222 huyu waziri kwa nini ni mbinafsi kwanini haweki wazi unafuu wa hiyo kampuni anayoitetean a kwa nini anatakata wachina wake wajenge na kisha watumikie miaka 45 kama sehemu ya klipa deni hii ndio ile mikataba miboccu go to hell nundu
mtazamo wangu kuusu mwelekeo
permalink submitted by tiga (not verified) on wed 20120425 1752 mtazamo wangu kuusu mwelekeo wa taifa sasa ni giza naamin mwanga upo na naamini tutauona swali la kujiuliza ni njia zipi zitakazo tumika ili tuweze kuuona mwanga huo hofu yangu ni kwamba tusije tukalazimika kubadili bendera ya taifa yenye rangi nzuri za amani kwa kuweka rangi nyekundu ya kumwaga damu
naifananisha nchiyetu kama meli inayo safiri alafu ikiwa safalini baahari ikachafuka na kwa kawaida bahari inapochafuka huku meri ikiwa safarini hapo ndipo ufundi wa naodha unapoonekana lakini hatakama naodha meri imemshinda kuipeka pwani basi bahari yenyewe huchukuwa jukumu la naodha kuifikisha pwani kwani bahari inatabia ya kujisafisha yenyewe ndio maana hata ukitupa mfuko katikati ya bahari ni lazima tu utaukuta pwani
raisi ndio naodha wa meri yetu tunamuomba ajitaidi kuifikisha pwani kabla bahari haijachukua jukumu hilo | 2013-05-22T22:19:43 | http://raiamwema.co.tz/waziri-matatani |
picha rais mstaafu kikwete waziri mwakyembe wakiwa msibani kwa ephraim kibonde | mpekuzi
picha rais mstaafu kikwete waziri mwakyembe wakiwa msibani kwa ephraim kibonde
rais mstaafu wa awamu ya nne wa jamhuri ya muungano wa tanzania dk jakaya mrisho kikwete leo jumamosi amewaongoza mamia ya wananchi kuaga mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa clouds media group ephraim kibonde nyumbani kwa wazazi wake mbezi africana jijini dar es salaam
viongozi wengine waliofika kuaga mwili wa kibonde ni mkuu wa mkoa wa dar es salaam paul makonda dk harrison mwakyembe (waziri wa habari utamaduni sanaa na michezo) dotto biteko (waziri wa madini) william lukuvi (waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi) na nape nnauye (mbunge wa mtama)
wengine ni manaibu mawaziri katibu mkuu wizara ya habari wabunge na wakuu wa wilaya
ephraim kibonde alifariki machi 6 2019 asubuhi saa kumi na mbili na nusu katika hospitali ya uhuru jijini mwanza mazishi yanatarajiwa kufanyika leo jumamosi saa kumi jioni katika makaburi ya kinondoni | 2019-09-19T08:47:59 | http://www.mpekuzihuru.com/2019/03/picha-rais-mstaafu-kikwete-waziri.html |
jinsi ya kumjua mungu wa vitendo | injili ya kushuka kwa ufalme
1 je unapaswa kujua nini kuhusu mungu wa vitendo mungu wa vitendo mwenyewe anajumuisha roho nafsi na neno na hii ndiyo maana ya kweli ya mungu wa utendaji mwenyewe ufahamu wa mungu wa vitendo unajumuisha kujua na kuyapitia maneno yake na kuelewa sheria na kanuni za kazi ya roho mtakatifu na jinsi roho wa mungu anavyofanya kazi katika mwili kwa hivyo pia inajumuisha kujua kwamba kila tendo la mungu katika mwili linaongozwa na roho na kwamba maneno anenayo ni maonyesho ya moja kwa moja ya roho hivyo ukitaka kumjua mungu wa vitendo lazima kimsingi ujue jinsi ambavyo mungu hufanya kazi katika ubinadamu na katika uungu hili wakati ule ule linahusu maonyesho ya roho ambayo watu wote hujihusisha nayo
2 ni nini kilichomo katika maonyesho ya roho wakati mwingine mungu hufanya kazi miongoni mwa ubinadamu na wakati mwingine katika uungulakini kwa jumla roho anatawala katika pande zote mbili lakini kuna pande mbili za uelekezaji wake kwa roho upande mmoja ni kazi yake kwa ubinadamu na upande mwingine ni kupitia uungu unafaa kujua haya wazi wazi kazi ya roho hubadilika kulingana na matukio wakati kazi yake ya binadamu inahitajika roho anaielekeza kazi hii ya binadamu na wakati kazi ya uungu inahitajika uungu hujitokeza moja kwa moja kuifanya kwa sababu mungu hufanya kazi katika mwili na kujionyesha katika mwili anafanya kazi katika ubinadamu na katika uungu
3 kuonekana kwa mungu katika mwili kunamaanisha kuwa kazi yote na maneno ya roho wa mungu yanafanywa katika ubinadamu wake wa kawaida na kupitia mwili wake uliopatikana kwa maneno mengine roho wa mungu huelekeza kazi yake ya ubinadamu na hutekeleza kazi yake ya uungu katika mwili na katika mungu kupata mwili unaweza kuona kazi ya mungu katika ubinadamu na kazi kamili ya uungu huu ndio umuhimu wa utendaji hata zaidi wa kuonekana kwa mungu wa vitendo katika mwili maana ya mungu wa vitendo ni kuwa kazi yake ya ubinadamu na kazi yake ya uungu kama inavyoelekezwa na roho inaonyeshwa kupitia mwili wake ili watu waone kuwa yeye ni wazi na mwenye kufanana na kiumbe chenye uhai na ni halisi na wa hakika
iliyotangulia:watu wanamchukulia kristo kama mwanadamu wa kawaida
inayofuata:mbinu na kanuni ya kazi ya mungu kwa wanadamu | 2020-02-23T19:33:36 | https://sw.kingdomsalvation.org/how-to-know-practical-God-lyrics.html |
habari radio maria tanzania
mapadre mapadri watatu wa jimbo katoliki same ambao vifo vyao vilipishana kwa siku moja moja yamefanyika katika seminari ndogo ya chanjare jimboni same mkoani kilimanjaro mapadre hao ni padri michael kiraghanja aliyefariki dunia aprili 11 akiwa kwenye mafungo huko maua moshi padre arobogasti mndeme wa parokia ya kirangare alifariki aprili 12 katika hospitali ya rufaa []
leo kanisa linamkumbuka mtakatifu marselino wa embrunaskofu mtakatifu marselinoanaheshimika kama askofu wa kwanza wa embrun (ufaransa)alikuwa mzaliwa wa afrika ya kaskazini yeye na wenzake wawiliwatakatifu vinsenti na damianowalijitosa katika kuihubiri injili huko ufaransa walitua huko nice (ufaransa) kisha waliendelea kusafiri mpaka milimani eusebi wa verseli aliyekuwa amefukuzwa huko alimweka marselino wakfu na kumsimika awe askofu []
baba mtakatifu francisko amekubali na kuridhia ombi lililowasilishwa kwake na askofu damian kyaruzi wa jimbo katoliki sumbawanga tanzania la kungatuka kutoka madarakani wakati huo huo baba mtakatifu amemteua mheshimiwa padre beatus christian urassa wa shirika la kazi ya roho mtakatifu (alcp / oss) kuwa askofu mpya wa jimbo katoliki la sumbawanga askofu mteule beatus christian []
aba mtakatifu francisko katika waraka wake wa kitume laudato si yaani sifa iwe kwako juu ya utunzaji wa nyumba ya wote anatoa mwelekeo wa ustaarabu mpya wa maisha unaojikita katika mafundisho jamii ya kanisa kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa mwenyezi mungu muumba wa mbingu na nchi binadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa mungu mazingira na []
baba mtakatifu francisko ametoa wosia wa kitume gaudete et exsultate yaani furahini na kushangilia wito wa utakatifu katika ulimwengu mamboleo (mt 512) umezinduliwa jumatatu tarehe 9 aprili 2018 kumbu kumbu ya bikira maria kupashwa habari kuwa atakuwa ni mama wa mungu kristo yesu anawaalika wote wanaoteseka au kudhulumiwa kwa ajili yake kufurahi na kushangilia kwani yeye ni []
mwenyezi mungu mwingi wa huruma na mapendo daima amekuwa akiwasindikiza waja wake hata katika njia ngumu za maisha yao zinazosheheni mavumbi na matope anatambua fika kiu ya upendo iliyoko ndani mwao na hivyo anawaita kushiriki furaha yake hiki ndicho kiini cha ujumbe wa baba mtakatifu francisko kwa siku ya 55 ya kuombea miito duniani inayoadhimishwa na mama []
leo aprili 17 kanisa linamkumbuka mtakatifu stefano harding abate mtakatifu stefano harding alizaliwa uingereza akasoma katika chuo cha monasteri ya sherbo (uingereza) alisafiri na rafiki yake mmoja kwenda roma wakati wa kurudi wakaona njiani vibanda duni kadhaa huko walikaa mamonaki waliokuwa wakiishi maisha ya ufukara nusu ya muda wao walitumia katika kusali nusu nyingine kwa []
sakramenti zote na hasa zile za kuingizwa katika ukristo zina kama lengo pasaka ya mwisho ya mtoto wa mungu ile ambayo kwa kifo inamwingiza katika uzima wa ufalme wa mungu sasa kinatimilizika kile alichokisadiki katika imani na matumaini nangojea ufufko wa wafu na uzima wa ulimwengu ujao maana ya kikristo ya kifo imefunuliwa katika mwanga []
waamini wanapaswa kumwachia mwenyezi mungu uhuru kamili ili aweze kutenda ndani mwao kadiri anavyotaka kama ilivyokuwa kwa farisayo aliyejulikana kama gamalieli mwalimu wa torati aliyekuwa anaheshimiwa sana aliyesimamia kidete ukweli kuhusu mafundisho ya mitume wengine walioshuhudia uhuru wa kweli ni petro mtume na yohane mwanafunzi aliyependwa zaidi na kristo yesu hawa wanaweza kuwa ni mashuhuda []
leo aprili 13 kanisa linamkumbuka mtakatifu martino wa kwanza papa na mfiadini martino alizaliwa todi (italia) alichaguliwa kuwa papa mwaka 649 zamani zile wamonoteliti wafitini wa diniwalijaribu kutangaza kokote mafundisho yao kwamba yesu kristu hakuwa na utashi wa kibinadamu katika mtaguso wa laterani ilithibitishwa kwamba kristu alikuwa na tashi mbiliutashi wa kibinadamu na utashi wa [] | 2018-04-23T03:52:28 | http://www.radiomaria.co.tz/category/habari/ |
uchambuzi fid q propaganda (i) | vijana fm
uchambuzi fid q propaganda (i)
vijana fm > audio > uchambuzi fid q propaganda (i)
so now betelgeuse is to explode not so fast
posted by sn on january 22 2011 in audio swahili text
na bahati mabala na steven nyabero
sikiliza wimbo kwa makini pia unaweza ukasoma kile fid q anachosema fid q propaganda lyrics
propaganda ni aina ya mawasiliano ambayo lengo lake hasa ni kubadilisha au kufanya watu kwenye jamii kuwa na itikadi msimamo au mtazamo fulani kuhusu jambo husika lakini kwenye aina hii ya mawasiliano vitu au mambo kadhaa tu huchaguliwa na mtoa propaganda na kuwasilishwa kwa hadhira kinyume na kuwapa watu taarifa na hoja sahihi kikamilifu na kuwaacha wafanye maamuzi yao wenyewe
kwa kutumia mfano na lugha nyepesi wewe unajua kuwa binti fulani mtaani ana virusi vya ukimwi na labda aliambukizwa wakati anafanya biashara ya ngono ili kukidhi mahitaji yake na mtoto wake kwa sababu wewe unataka jamii inayomzunguka imnyanyapae yule binti basi kama mtoa propaganda utawaambia watu yule changu ana ngoma utaficha ukweli kwa makusudi kuwa kuna uwezekano alipata ukimwi kwa njia nyingine na wala hautagusia vitu vilivyomsukuma yule binti awe changudoa
propaganda hutumiwa sana wakati wa vita
propaganda ambazo huhusishwa na siasa zaidi mara nyingi hudhamiria kuamsha hisia za watu hivyo kutoupa nafasi ujengaji wa hoja matokeo yake wapokeaji propaganda hushindwa kufanya maamuzi sahihi au kwa matakwa yao kama wangepewa au wangejenga hoja sahihi kikamilifu vita ya kwanza ya dunia ni mfano mzuri wa jinsi propaganda zinavyotumiwa na wanasiasa na watu wenye mamlaka kwenye jamii
nyimbo kama juhudi za wasiojiweza nyota ya mchezo hey lord mwanamalundi tema noleji utaua gemu nilipotoka na propaganda zinazopatikana kwenye albamu propaganda zinakupa picha kamili ya uanaharakati wa fareed kubanda kama msanii wa hip hop na raia wa tanzania kwa wale wavivu kusikiliza tungo kwa makini kufikiria wenyewe na kujenga hoja kwa kifupi albamu propaganda ni juhudi za dhati kabisa kutenganisha ukweli na uongo kwenye bongo hip hop na jamii ya watanzania kwa ujumla
na wimbo propaganda hubeba mantiki thabiti ya albamu nzima hasa nyimbo zilizotajwa awali tungo zinabeba na kuwasilisha ukweli kuhusu sanaa ya muziki siasa na maisha kwa ujumla ili hadhira iweze kupambanua kama walichokuwa wakiamini kabla ni uongo yaani propaganda tu (kwa mtazamo wa fid q)
wimbo propaganda unaanza kwa midundo yenye utulivu ambao unamlazimisha msikilizaji kusikiliza kile ambacho fid q anaghani wengi watakubali kuwa fid q anaghani vizuri na sambamba na midundo iliyoundwa na marco chali
badala ya kuanza kwa kughani ubeti wa kwanza moja kwa moja fid q anaamua kuweka msingi wa ushairi wake kwenye kiitikio
yule ni last king of scotland sio idi amin wa uganda
mambo anayosema na kuhoji kwenye mistari minne ya kwanza tu yanaamsha fikra ukifiria kwa makini utagundua kuwa anaanza na propaganda polisi wanasapoti gangsta rap ili uhalifu uongezeke' kisha inafuatiwa na kitu ambacho anajipa fursa ya kuhoji wabana pua kuimba mapenzi je ifatafanya ukimwi usepe' kwa hiyo mstari wa pili sio propaganda ila anahoji jinsi jamii yetu inavyozipa kipaumbele nyimbo za watu ambao hawana vipaji vya kweli na zinazochochea anasa huku tukitegemea matokeo tofauti kabisa je unadhani watoto na vijana wakiendelea kusikiliza mambo ya anasa na nyimbo zisizo na nasaha za kujilinda na magonjwa ya zinaa tutegemee janga kama la ukimwi kutoweka hamfungi mawazo msikilizaji bali anahoji
lakini msikilizaji anaweza akadhani anayosema kwenye mstari wa kwanza labda yana ukweli uhalifu mwingi humaanisha kazi nyingi kwa polisi kwanza tanzania hakuna gangsta rap pili baadhi ya wamarekani ndio walianzisha hizo propaganda ili kuchafua muziki wa hip hop ambao mara nyingi huusishwa na uhalifu (matumizi wa madawa ya kulevya mauaji kwa kutumia silaha vitendo vya ngono na anasa kwa ujumla) kinyume na kuchukulia kinachoimbwa na wasanii kama ukweli wa mambo yanayotokea kwenye mitaa yao kama umekuwa unafuatilia mauaji ya halaiki mashuleni nchini marekani mara kwa mara vyombo vya habari vimekuwa vikisema watuhumiwa walikuwa wanasikiliza nyimbo za wasanii wa hip hop gangsta rap hivyo bila shaka kinachoimbwa kwenye tungo za wasanii husika kimechangia mauaji ya halaiki
kama ilivyojadiliwa mwanzoni mtoa propaganda hudhamiria kukufunga kimawazo kwa kutokupa nafasi ya kuhoji kutoa majibu rahisi kwa maswali magumu watu wengine huweza kuita tabia hii determinism kwasababu wanashindwa au hawataki kuzipa nafasi hoja mbadala
anarudi tena kwenye propaganda media zinapromoti beef wanadai zinakuza muziki' kawaulize hao madj kama wanawajua wasanii wowote ambao ni ushahidi thabiti kwamba viwango vyao vya kuandika tungo bora ubunifu uwasilishaji wa kazi zao nk viliongezeka baada ya kuingia kwenye malumbano na wasanii wengine ukiacha ushabiki na umbea wa malumbano kuna lolote la maana kwanini hatuwabani wahusika wanapotupa upuuzi kama huu ni kama tunameza chochote kile madj wanachotuambia hiyo ndio jamii yetu
baada ya hapo anaamua kuhoji kitu kingine kwenye sanaa ya muziki tanzania wadau wana wasanii wabovu nyie wakali mtatoka vipi' ndio ni swali gumu kwa wasanii wenye vipaji kwani hawapewi kipaumbele na walioshika usukani wa gari moshi la muziki kama hili halitoshi wanajamii nao wanaamini chochote kile kinachotoka kwenye midomo ya wadau wa muziki halafu kama tunavyowapa vipaumbele wabana pua tunategemea matokeo tofauti ukimwi usepe na sanaa ikue kwani kila siku tunalalamika muziki wa tanzania unakufa kifo cha mende
baada ya kusema na kuhoji hayo yote hasa kuhusu sanaa anakwambia hizi ni propaganda usiyatilie maanani aliyosema na haupewi nafasi ya kuuliza maswali na kujenga hoja zako binafsi wakoloni wetu wa mwisho wanaita hii kitu sarcasm anatucheka
wasanii wabunifu wa hip hop hupata sifa na kuheshimika kutokana na punchlines tafsiri nyepesi inaweza ikawa ni [kama] mistari inayojumuisha aliyosema kwenye mistari kadhaa iliyopita kwa kutumia fumbo au kucheza na maneno na kuweka msisitizo kwa maneno mengine anakupa vidokezo vya mambo aliyokuwa anazungumzia
na fid q anatumia punchline ifuatayo utaibiwa ukicheza blanda yule ni last king of scotland sio idi amin wa uganda'
hapa unahitaji hisabati na utundu utakuwa umefanya makosa (makubwa sana) kama ukidhani last king of scotland ni idi amin wa uganda
kuna idi amin mmoja tu wa ukweli
[the] last king of scotland ni filamu iliyoandikwa na giles foden ni hadithi ya kutunga alichofanya mwandishi wa filamu hii ni kutumia wasifu wa mhusika wa kubuni dr nicholas garrigan kujenga wasifu wa idi amin dada kilichofanyika ni kuchagua matukio machache tu kutoka kwenye historia ya uganda/idi amin na kuyapachika kwenye filamu
ukiacha hayo kuna uongo wa hapa na pale kwa mfano mke wa amin kay amin alipewa mimba na dr garrigan lakini ukweli ni kuwa bi kay alipewa mimba na mpenzi wake dr mbalu mukasa pia kadri filamu inavyoendelea mambo yanayotokea kwenye filamu yanazidi kutengana na mambo halisi yaliyotokea kwenye historia ya uganda
haya tafuta kikokotozi na visoda kama umesahau kuhesabu
mstari wa kwanza na wa tatu kwenye kiitikio ni last king of scotland propaganda
mstari wa pili na wa nne (ambayo inahoji na kuruhusu ukweli kujulikana) ni idi amin wa uganda na usishangae ukikutana na waganda wanaomchukulia idi amin kama mzalendo
bado unaamini last king of scotland ni idi amin dada
sehemu ya pili ambayo itachambua ubeti wa pili wiki ijayo makala nyingine
one the incredible (see msangis comments)
tagsart education music politics youth
1 about sn
steven was born and raised in dar es salaam and moved to germany for his studies he graduated with a bsc in physics (jacobs university bremen) and then a msc in engineering physics (technische universität münchen) steven is currently pursuing a phd in physics (growth of coatings/multilayers for next generation lithography reflective optics) in the netherlands hes thinking about starting his own business in a few years something hightech related at vijana fm steven discusses issues critical to youths in tanzania music sport and a host of other angles hes also helping vijana fm with a swahili translation project 21 comments
sinza09 6 years ago reply kwa maoni yangu naona mstari wa pili wa kiitikiowabana pua kuimba mapenzi je ifatafanya ukimwi usepe unamaana zaidi ya moja au wanavyosema huko ughaibuni ni double/triple entendre ukiufatilia huu wimbo unatambua fiddy anatukanya kuyaangalia maswala ya kijamii kwa juu juu tu kwa hiyo kama ziada ya jinsi bahati na steve walivyochambua mi naona tunakanywa kutafuta uhusiano wa moja kwa moja (correlation) kati ya sanaa (hasa ya bongo flava) na maovu ya jamii yani hata kama wabana pua wasipo imba ukimwi utaendelea kuua waafrika kama hatutabadilisha tabia zetu mziki unaweza kuonya au kukanya lakini mabadiliko yanaletwa na watu binafsi mwisho ningependa kuwapongeza sana kwa kazi yenu nzuri nasubiria kwa hamu sehemu ya pili
sn 6 years ago reply ndio maana ya kuchambua fasihi na michango kama hii ndio inahitajika hii ni fasihi na kila mtu anaruhusiwa kutafsiri jinsi anavyoelewa nimekusoma mkuu kwa hiyo huo mstari ni propaganda au kumbuka anahoji 🙂 ndio maana ukaweza kujenga hiyo hoja tutaingia kwenye falsafa hata hivyo nyimbo zinaweza kutumiwa kama chombo cha kuelimisha wanajamii
kuna kitu kingine tulitaka kujadili (na inafanana na hayo uliyosema) polisi wanasapoti gangsta rap ili uhalifu uongezeke ni propaganda lakini nadhani ingekuwa vizuri zaidi kama fid q angegusia ile ishu ya muziki wa kufokafoka unakuza uhuni sidhani wengi wanamuelewa vizuri anavyotaja gangsta rap ukiacha hayo kama ulivyosema kutoa majibu rahisi kwa maswali mazito na kukwepa kujiangalia wenyewe kama jamii kwa ujumla najua fid q atapita hapa kuangalia tunachojadili tafadhali tunakuomba usichangie lolote hadi tutapomaliza mjadala/uchambuzi wa mwisho shukrani
sinza09 6 years ago reply @sn sijui huo ujumbe wa kuchangia ni wa watu wote au fid q tu lakini nitajizuia hadi mmalize kuchambua
sn 6 years ago reply ujumbe ni kwa fid q tu akianza kuchangia hapa hatatutendea haki kwenye uchambuzi na mjadala kwa hiyo tafadhali endelea (endeleeni) kuchangia
denis munene 6 years ago reply fid q im a kenyan in kampala and married to a tanzanian mama so that means ive rubbed shoulders with all east african music artistes for this i wanna tell you are one in a million your songs are good to the ears touches the soul and there are very educative and even though people will not turn to you in large to tell you you are a great artist just know they feel you inside you are so hard to hate thumbs up bro keep up tha gud work hope to meet you someday
jumah 6 years ago reply yap ma bro uko correct kwa kila idara izo puch na all gd shity zko deep sana
eustace landelin 6 years ago reply fid q propaganda ni wembo ambao msikilizaji ili awaze kuelewa nini unamaanisha lazima akae kitako kuusikiliza kwa makinpunch ya last king of scotland sio idi amin wa ugandainavutia lakini watu wengi walikuwa hawajui nini unaanisha kwani wengi wetu hatuja icheck hiyo movie but kwa sasa nafurahi nimeelewa vyakutosha kaka
ally waziri 6 years ago reply ndani ya propadanda punch ya last king of scotland inasema kweli sababu ile movie sehemu kubwa ni ya kumzalilisha idi amini tu
bahati m 6 years ago reply kwenye huo mstari wa idi amin na hiyo movie ya last king of scotland nadhani ni kweli mtunzi anataka kuweka sawa maana ya propaganda kwa kutoa huo mfano
lakini swali langu ni hili je hiyo movie pamoja na mapungufu yake tunaweza kusema vyote kuhusu character ya amin ni propaganda sasa uwiano kati ya huo mstari na nia ya mtunzi kuutumia je fid q anataka tuchambue ipi ni propaganda na yapi ni ukweli kwani sidhani kila kitu ni propaganda kwani hata stereotypes zimejengwa kwenye msingi ya ukweli fulani sema sasa watu wanakuwa wanazidisha chumvi na sukari hapa na pale au exaggerate inamaana tunakubali kuwa yule sio idi amin kwenye movie bali ni last king of scotland yaani character aliyeundwa na mtunzi wa hadithi ya filamu hii au hapo fid q anafanya tu wordplay ambayo inamaana iliyojificha
labda unachotakiwa kujiuliza kwani propaganda zote ni uongo 100 kwani utakuja kugundua kuna a lot of kejeli/ sarcasm nyingi kwenye hii nyimbo ni kama mtu asema yule wa kampeni ya 2005 alikuwa chaguo la mungu kwetu sote bali sio huyu kiongozi wa leohihihihi nimemaliza
sn 6 years ago reply kama ile mantiki ya propaganda (yenye negative tone) ikiangaliwa kwa makini basi kwa uelewa wangu mdogo nadhani ule wasifu uliojengwa na mwandishi ni propaganda 1 amechagua matukio anayotaka yeye binafsi yanayoendana na anachotaka kusema kuhusu idi amin 2 je alikuwa na lengo la kuwaambia watu ukweli kwa nini aongezee vitu/visa vya kutunga wakati ukweli upo hadithi za ukweli hazivutii sana au hazikukaa vizuri kwenye mtitiriko wake (ambao bila shaka ulikusudia kuamsha hisia)*
3 watu wengi hasa wa nchi za magharibi hawajawahi hata kusoma vitabu na historia ya uganda na idi amin unadhani watakuwa na mawazo au mtazamo gani baada ya kuiona ile filamu
4 baada ya kuangalia ile filamu na documentary hii kuhusu maisha yake (idi amin) unadhani utakuwa na mtazamo ule ule lipi limeongezeka kwenye hiyo documentary (hiyo documentary inaweza kuchukuliwa kama propaganda pia kama unajua zaidi ya yaliyooneshwa humo ndani)
bahati najua unaelewa lying by omission
5 kuhusu suala la wordplay unadhani fid q alishindwa kutumia nyingine yaani katika metaphors zoooote kwanini alichagua hiyo ya last king of scotland nadhani hilo ndilo swali unalouliza kumbuka propaganda humfunga mtu mawazo na hivyo hadhira hupata hisia kama ilivyodhamiriwa na mtoa propaganda hakupi nafasi ya kujenga hoja yako binafsi na kufanya mambo/maamuzi kwa matakwa yako mwenyewe (of course hapa tunazungumzia ile hadhira ambayo haijui kinachoendelea tutaelewa vizuri baada ya kuzama kwenye zile beti mbili nzito)
kwenye vita ya pili ya dunia mojawapo za propaganda ilikuwa ni kuwa wayahudi wameshikilia vyombo vinavyoendesha uchumi wa ujerumani na dunia nzima kwa ujumla kwa sababu chungu mbovu unadhani kama watu wangeambiwa kuwa elimu na misingi ya kusaidiana kwenye kueneza ujuzi ndio umechangia mafanikio yao kwa kiasi kikubwa je matokeo yangekuwa tofauti nini kilichokuwa kinasemwa dhidi ya waromani walemavu na mashoga yalikuwa yana ukweli labda kiasi tu yaani baada ya kupewa ukweli na hali halisi kama ilivyo unadhani watu wangeshika mtutu * kama mchangiaji wa kwanza na bahati wanavyodai labda tunapaswa kujiangalia sisi wenyewe hatupendi ukweli na tunajali mambo yanayoamsha hisia zaidi hivyo kushindwa kujinufaisha na kujiendeleza sakura 6 years ago reply sijawahi sikia mtunzi akaandika msatari mmoja fact mstari mmoja uongo kisha wimbo ukaitwa jina lenye utata mwandishi akiandika kimtindo huo lazima wasikilizaji wasielewe kwa hiyo sioni mantiki kwenye uandishi wa aina hiyo (na kwa vile hakuna mantiki basi haikuwa hivyo )) yaliyoandikwa yote ni facts au tuseme ukweli japo unaweza ukawa sio the whole truth polisi wana sapoti gangstar rap ili uhalifu uongezeke
wabana pua kuimba mapenzi kutafanya ukwimwi usepe
media zinapromoti beef wanadai zinakuza mziki
wadau wana wasanii wabovu nyie wakali mtatoka vipi hapo juu mkuu bahati hakuna propaganda wote ukweli mtupu gangstar rap ni hiphop inayo promote violance wewe utasema hakuna gangstar rap but kwenye dictionary la polisi na watu wa kawaida zipo
bahati m 6 years ago reply @sakura asante kwa mchango wako mimi ningeomba utoe mfano hai wa gangsta rap inayo promote violence ukianza kwa kuelezea gangstar rap maana yake ni nini
pili tanzania hakuna gangstar rap sasa hapo jiulize kwanini fid q ameamua kuzungumzia hiyo kwenye hii nyimbo yake wewe unadhani ni kwanini ningependa kujua fact ya hilo suala tatu nitakuquote sijawahi sikia mtunzi akaandika msatari mmoja fact mstari mmoja uongo kisha wimbo ukaitwa jina lenye utata sasa ukiniuliza mimi nitasema hiyo ndio propaganda yenyewe au wewe unasemajepropaganda siku zote huwa na utata kwasababu sio ukweli japokuwa kuna kuwaga na ukweli kiasi fulanihuo ni mtazamo wangu lakini cha msingi ningependa mfano wako wa gangsta rap inayo promote violence na maana ya gangsta rap ni nini na je tanzania ipo kweli
sakura 6 years ago reply actually huo ubeti rahisi kuuelewa ukiuchukua kaa ulivyo
polisi badala ya kuzuwia uhalifu wanapendelea vitu vinavyouchochea
waimbaji badala ya kusaidia jamii kupambana na ukimwi wanaimba nyimbo zinazochochea media badala ya kusaidia kukuza vipaji vya wambaji kwa kutafuta ushirikiano zinachochea mifarakano
wadau badala ya kupokea wasanii wakali tayari weshazongwa na wasanii wabovu
gangsta rap (kwa mujibu wa official media) ni hiphop iliyoanza east coast marekani ambayo ina promote violence profanity drug abuse sex vandalism and other whatnots (japokuwa waimbaji wenyewe husema kuwa wanaakisi tu maisha ya vijana waliowazunguka na sio kama wanakubaliana na vitendo hivyo)
kwa hiyo lazima tukubali kuwa gangster rap ipo na nyimbo zinazozungumzia kwa mfano wa kusifia vitu hivyo zipo tele kwa mujibu wa international media
jee gangster rappers wapo tanzania suala gumu kwangu kwa kuwa simsikilizaji wa muziki wa kufokafoka as a hobby but kuna mheshimiwa mmoja alisikika akijinadi i want to kill right now sijui wengine
hata hivyo hata ikiwa hao gangsta rappers hawapo haimzuwii muandishi kutumia mfano huo hata for a want of a better parody tu (besides ametumia mfano wa iddi amini with no relation to tanzania either)
akitaka kuonyesha kuwa polisi hawafanyi kazi yao inavyotakiwa na wakipata chance ya kuchochea uvunjaji wa sheria watafanya hivyo ili kujiomgezea chances za kula nafikiri ni mfano mwepesi kueleweka
sn 6 years ago reply sakura unasema yaliyoandikwa yote ni facts au tuseme ukweli japo unaweza ukawa sio the whole truth narudia facts au ukweli japokuwa zinaweza zikawa sio the whole truth halafu hapo juu mkuu bahati hakuna propaganda wote ukweli mtupu google neno propaganda au kaangalie kwenye vitabu maktaba kama hukubaliani na maelezo na mifano iliyotolewa kwenye makala ingawa kwa upande mwingine wewe mwenyewe umeshadefine propaganda ila kwa kijichanganya kidogo facts au ukweli japokuwa zinaweza zikawa sio the whole truth no one can refute facts facts are facts usiulize ni nani ni yupi saa ngapi ilikuwaje na nani ili iweje nadhani wewe ndio unachofanya kumbuka fid q ni mwanahip hop mbona hizo media hazisemi chochote kuhusu rock music kina eric harris and dylan klebold si wanadai walikuwa influenced by marilyn mansons music (kasome kuhusu columbine massacre) si polisi walikuta tapes za dmx na eminem pia vipi mbona gangsta rap tu ndio imejaa kwenye vinywa vya waandishi wa habari
wao walianza na hip hop waliokuja kuichafua wakaanza kuiita gangsta rap kuna wimbo mmoja wa common unaitwa i used to love her nadhani labda utaongeza mwanga kidogo
kwa kumalizia tu kama mpenzi wa gangsta rap au hip hop akifanya uhalifu ina maana hicho tu ndio kimemsukuma (kufanya uhalifu) yaani matatizo yote ya kiakili kiafya kifamilia nk yanapigwa pingu nakushauri umsikilize ti kwa makini sana kwenye hii clip http//wwwyoutubecom/watchv=ygoeuhojazs ndio yale yale mtu anadai ataandika katiba mpya ndani ya siku 100 na sisi hata hatusumbuki kuhoji
bahati m 6 years ago reply @sakura umetoa maelezo mazuri ni kweli ukiangalia hiyo mistari na kuisoma kama ilivyo sio migumu kuielewa lakini sasa mashairi kama kazi ya fasihi itakuwa ni sahihi tukisema fikra za mwandishi hapo zilikuwa tu ni black and white au alikuwa anabeba ujumbe uliojificha kama kazi za fasihi zilivyo kawaida yake hapo sasa mimi sina uhakika lakini tutasaidiana hivyo hivyo mpaka kujua nia hasa ya fid q pili gangsta rap haikuanzia east coast hiyo source imekosea juu ya chimbuko halisi la gangsta rap ukiangalia gang violence marekani ilianzia na kushamiri west coast au pwani ya magharibi huko ndio kitovu cha bloods & crips lakini si muda mrefu sana ndio wakaanza kuspread katika vitongoji vingine hadi kutapakaa east coast pia
nwa walikuwa wanaogopwa sana kwa mashairi yao ambayo nadhani yalikuwa makali kama hotuba za malcolm x ambaye aliogopwa sana na kuwa labelled kama mtu anayechochea uhasama na fujo lakini sikiliza hotuba zake na interviews utachoka mwenyewe jinsi anavyovunjavunja hizo hoja dhidi yake kuhusiana na kuwa violent sasa basi kama crips & bloods chimbuko lao kuu lilikuwa west coast na mwanzo wa gangsta rap ulitokea huko unadhani all that is just a coincidence mimi binafsi sidhani kama tunakubaliana na afande sele kuwa sanaa ni kioo cha jamii hivyo tutakubali ya kuwa wasanii wa hip hop kutoka west coast wasingeweza kuzungumzia kitu kingine chochote zaidi ya mambo yaliyowazunguka na hilo ni gang violence iliyotapakaa katika mitaa yao tupac alisema hivi nitatafsiri na kuparaphrase wao kama wasanii wataendelea kutengeneza music videos ambazo zina images za kusisimua kuhusu gang violence mpaka watu washtuke na kuanza to do something about it yeye akatoa mfano wa jinsi media ilivyosaidia kufanikisha vita ya vietnam kusitishwa kwani wamarekani wlaipoanza kuona picha za vita ya huko na jinsi wanajeshi wao walivyokuwa wakitesekana na kufa kwa wingi protests zinachachamaa marekani kila kona dhidi ya vita hiyo sasa ni vipi mimi ninayekaa uswazi kurap kuhusu mambo ya masaki kama kila wiki naona mwizi akichomwa moto unadhani ni nini nitazungumzia kwenye nyimbo yangu si lingine bali hilo inashangaza kuwa ni sawa watu kuishi kwenye extreme conditions lakini we get offended hizo extreme conditions zinapozunguzwa na kuonyeshwa hadharani mfano mzuri kipindi cha hurricane katrina marekani didnt like the images zilizokuwa zinatoka huko maanake iliacha wengi wakijiuliza hii sio marekani tunayoijua siyo ile ya mtv tunayoishobokea kila kukicha pia umesema fid q alitumia mfano wa idd amin pasipo na uhusiano wowote na tanzania hilo ni kweli tukiangalia kijuujuu lakini unadhani alifanya hivyo by accident ukiniuliza mimi nitasema hapana nadhani alifanya hivyo makusudi kutumia huo mfano kujaribu kuelezea zaidi maana ya neno propaganda na hapo hapo kuacha watu wakijadili hiyo filamu kama je ilimtendea haki idd amin au ilijawa na propaganda dhidi yake kama fid q anavyoonekana kusuggest sasa hapo ndipo ninapomsifu fid q kwani anagusia halafu anaacha hadhira ijitafutie jibu kuliko ile style ya kutafuniwa na kumezewa mwisho nadhani hapo juu umegusia nyimbo ya sugu katika mixtape yake ya anti virus hiyo line ya i want to kill right now sina uhakika inaingia vipi kwenye kuwa gansta rap kwani kama khadija kopa kipindi kile taarab ilikuwa taarab angesema maneno hayo dhidi ya wapinzani wake tungesema taarab ghafla imekuwa gangsta rap nadhani kuna nyimbo ya hasheem inaitwa saa za kazi nadhani tukipata muda tutabidi tuujadili huo halafu tuone kama ni gangsta rap kwa kuwa watu wanaweza kusema kuwa anachochea maovu kama ile bendi waliotupa nyimbo ya masikini mtaji wake ni nguvu zake mwenyewe ambao ulikuwa ukiimbwa na majambazi wanapokuwa katika kazi hapo sasa sijui tuilaumu bendi kwa kutunga hiyo nyimbo au majambazi kwa kuigeuza kuwa soundtrack to their action movie hah
sakura 6 years ago reply vijana mbona mnataka kuwa na double standards tunakataa kuwa gangster rap hazipromote violence wakati tunakubali kuwa wabana pua kuimba mapenzi wanapromote ngono and consequently ukimwi
mnataka kunirudisha kwenye the theory of cause and actions naona hivi nyimbo ikisifia violence haimuathiri msikilizaji kweli why do we say msanii ana jukumu la kuelimisha jamii iwapo kumbe kazi zake hazisababishi actions kwa hadhira
papo kwa papo kamba hukata jiwe ukiimbiwa uchukue sheria mkononi kila siku mwisho utafuata tu @bahati khadijah koppa akiimba anataka kuuwa mtu tutamtafutia jina linalokwenda na sifa hiyo (since haimbi hip hop hatakuwa gangsta rapper) kama sasa kwa wajuzi wa taarab walivyomwita malkia wa mipasho (and i believe not in a good way)
hatusemi wala hatutaki wa manzese kuimba kama wa masaki lkn akiimba usihofu kuchomwa moto pora japo mtoto tutasema ana promote violence na sio ana reflect maisha ya vibaka anaowaona
@bahati my bad zilianza west coast you are very right
hebu twende logically tu na huo mstari wa kwanza polisi wana sapoti gangsta rap ili uhalifu uongezeke
if this sentence is a propaganda then it means
polisi wanasapoti gangsta rap lakini sio kwa sababu ya kutaka kuongeza uhalifu
polisi hawasapoti gangsta rap wanazuliwa tu kuambiwa wanasapoti ili kuendeleza uhalifu
tukisema mwandishi anataka kusema kuwa gangsta rap is just a propaganda haimake sense logically kwenye sentensi hiyo and the whole sentence collapses nitakupa mfano huu
wanawake wa pwani wanapenda kujipamba kwa hinna ili kuburudisha waume zao
nikiambiwa hiyo ni propaganda basi nitaangalia sentensi as a whole na sio kumega vipande niseme hapa ndo kuna propaganda
ama wanawake wa pwani hujipamba kwa sababu nyengine na sio kupendezeshea waume zao au wanawake hao hawapendi kujipamba kwa hinna sentensi hainipi mimi nafasi ya kuanza kuhoji uhalisia kuhusu hinna
sn 6 years ago reply tunakataa kuwa gangster rap hazipromote violence wakati tunakubali kuwa wabana pua kuimba mapenzi wanapromote ngono and consequently ukimwi
wapi tumesema hivyo sakura kilichoandikwa ni hiki anahoji jinsi jamii yetu inavyozipa kipaumbele nyimbo za watu ambao hawana vipaji vya kweli na inayochochea anasa huku tukitegemea matokeo tofauti kabisa je unadhani watoto na vijana wakiendelea kusikiliza mambo ya anasa na nyimbo zisizo na nasaha za kujilinda na magonjwa ya zinaa tutegemee janga kama la ukimwi kutoweka hamfungi mawazo msikilizaji bali anahoji
kwa mantiki hiyo wewe msikilizaji unaruhusiwa kujenga hoja yako kwa matakwa yako na kuamua upi uwe mtazamo wako tofauti na lugha inayotumiwa kwenye propaganda
kitakachoimbwa kiwe kibaya au kizuri hakimaanishi lazima msikilizaji atakifuata unachosikia kwenye kazi ya sanaa ni sehemu ndogo sana ya vitu vinavyokupa mwongozo wa maisha yako wewe binafsi nilihoji pale juu lakini hakuna mtu aliyejibu labda kwasababu huo mjadala upo kwenye positive tone
kama ingekuwa hivyo mbona maisha yangekuwa marahisi just buying a couple of cds from some informative smart artist who talks about positive things then the parents/societys job is done
mjadala na hoja nzuri @ sakura lakini ulivyomalizia ndio imenifanya niumize kichwa zaidi
huoni labda hapo ndipo kwenye tatizo kwenye jamii yetu kwani watoa propaganda hawapachiki vitu yaani kama wahutu walivyoanzisha propaganda dhidi ya watutsi na kuwaita cockroaches kurefute hizo propaganda kwa kusema tu watutsi sio mende (au) kwasababu mende sio watutsi inatosha kureverse the effects of propaganda unadhani wakielewa mantiki hasa ya kutumia neno cockroaches dhidi ya ndugu zao na kupembua kwa kina tofauti za ubinadamu na unyama au wadudu (mende) labda inaweza ikaleta matunda mazuri zaidi mfano mwingine kwenye makala umerefute kuwa [the] last king of scotland ni idi amin wa uganda kwa kuonesha kuwa kuna vitu vilivyopachikwa ambavyo ni vya kubuni je mimi binafsi kama nikitaka kujua ile hadithi ni ya kweli au uongo/propaganda sina nafasi ya kuhoji uhalisia wa yaliyomo kwenye hiyo filamu kuna formula ya kurefute propaganda
kama mtu akiambiwa filamu last king of scotland ni propaganda ataanzia wapi kama hapewi nafasi ya kuhoji uhalisia wa mambo
tuache mifano ya kubuni ambayo ni rahisi kupinga au kuelezea unavyotaka wewe au ninavyotaka mimi ukipata muda soma hii makala ni juhudi za kueleweshana hoja za pande mbili zinazosigishana halafu amua hiyo ya kumtumia einstein ilikuwa ni propaganda au la
sakura unaona sisemi ipi ni sahihi ila nahoji tu utaamua mwenyewe kutokana na mtazamamo wako sidhani ni jambo la busara kuchukulia lugha au aina za mawasiliano kama hisabati au logic labda makala ya tatu ya huu uchambuzi itakupa jibu litakaloridhisha fikra zako bahati m 6 years ago reply @sakurahahaha nimependa mfano wako wa hinna hao mabinti lazima watakuwa wanapaka ili wapendeze na sababu kuu ya kupendeza mara nyingi huwa either kuvutia wanaume (kama wao ni single) au kuvutia waume zao si unajua tena mpango wa nje unaweza ukakukuta mwanamke kama hujiweki mrembo mara kwa marahahmtazamo tu
polisi wana sapoti gangsta rap ili uhalifu uongezeke hapa mimi mwenyewe sina uhakika kama ni propaganda au la hasa tukiiweka kwenye context ya tanzania hili halitaleta maana sana tukisoma huo mstari kama ulivyo ndio maana mimi nikasema ninahisi mwandishi anaweza akawa ametumia hiyo kama metaphor kuzungumzia kitu kingine au maana hiyo hiyo lakini akituficha kitu hapo sasa ndipo itabidi tusaidiane kuweza kuelewa mimi nimependa hii tunakataa kuwa gangster rap hazipromote violence wakati tunakubali kuwa wabana pua kuimba mapenzi wanapromote ngono and consequently ukimwi hili ni swali zuri kabisa nadhani double standard uliyoisema ndio inaingia hapa nadhani ndio maana makala ilichofanya ni kuuliza swali na sio kudraw conclusion kwenye hilo suala i guess tunaweza kuangalia tafiti za wanasosholojia na kuona takwimu kama wapo watu waliofanya maovu kwa kusukumwa na nyimbo au kufanya zinaa kwasababu ya nyimbo lakini hapo hapo zipo nyimbo zinazo hamasisha watu kuvaa mipira je zimefanikiwa au ni hadithi tu baada ya habari mimi sina jibu la moja kwa moja hapo sijui nyinyi
au je inawezekana tunaangalia yasiyopo yaani tumengangania kusoma polisi kama polisi bila kuhoji hao polisi ni akina nani ni polisi wenye magwanda au hilo neno polisi limetumika tu kuzungumzia authority na wala sio polisi kama tunavyofikiria kama kikwete atatumia wanabongo flava kwenye kampeni zake ina maana he cares for the youth yaani anataka kuonesha kuwa anasupport muziki huu wa hip hop na hapo hapo na yeye ni kijana kwa kuwa anafungamana na vijana ili mwisho wa siku tukiwaangalia hivyo basi vijana na sisi tutoke kwa makundi kwenda kumpigia kura yeye kwani tayari tumeshamwona kama kijana mwenzetu kwani anazungukwa na vijana wenzetu na anasikiliza nyimbo tunazozisikiliza sijui kama nimefanikiwa kuonyesha connection ya mfano huu na kilichosemwa na mwandishi wa shairi
jack d 6 years ago reply propaganda seems to be something we are all engaged with in some way or another in presenting ourselves at a job interview for example we leave out things that would harm the chances of landing a gig isnt this propaganda lest on a different level
so im with fid q on instigating the habit of asking questions ni yupi saa ngapi ilikwaje etc but i would humbly extend this further than what we hear/watch on commercial media and into our daily lives in other words i think fid qs lyrics especially the hook/chorus tell us (everyone young and old) to stop taking things for granted baas
@rams 5 years ago reply ill get the most qeution when clear 2 explean dat
juvenal makevel 3 years ago reply kaka pole na safari nzito ya kuikomboa jamii yetu nazidi kukufuatilia kiundani zaidi na pia naombea kazi njema yenye mafanikio kiufupi kaka propaganda mzigo nimeukubali sana man duh dude lipo salama kinoma | 2016-08-26T03:08:35 | http://www.vijana.fm/2011/01/22/uchambuzi-fid-q-propaganda-i/ |
rwebangira blog saturday september 19
wahenga walisema kizuri wala na nduguyo naam nami nimekutana na habari nzuri toka kwa mtumishi bayless conley nikaona ni vyema niwashirikishe wadau anasema yawezekana kushushwa kwako ni njia alioipanga mungu ili aweze kukuinua amini leo nawe utaona matokeo yake
the way up may be down
it is not unusual for gods promotion to look like a demotion at first to feel like you are going backward rather than forward
kauli ya makame yaichanganya zec
mkurugenzi wa tume ya uchaguzi ya zanzibar (zec) salum kassim amesema haamini kama mwenyekiti wa taifa jaji lewis makame anaweza kujitoa katika suala la zanzibar na kutaka jamii iilaumu zec kwa vurugu zinazoendelea kisiwani pemba
juzi jaji makame alisema mjini dodoma kuwa tume ya taifa ya uchaguzi (nec) haistahili kuhusishwa na vurugu zinazoendelea kisiwani pemba ambako wananchi wanagomea zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura wakipinga matumizi ya kitambulisho cha uzanzibari ukaazi kama kigezo kikuu
kama nec ingekuwa msimamizi wa uandikishaji kwa ajili ya chaguzi hizo (za zanzibar) ingestahili kubeba lawama lakini zanzibar kuna tume huru zec ambayo inasimamia taratibu zote katika daftari hilo ndiyo inapaswa kulaumiwaalisema jaji makame juzi | 2017-08-17T03:47:30 | http://bongopicha.blogspot.com/2009_09_19_archive.html |
jeshi | simbadeo2000
waza mpaka basi (think to no end)com weblog note views or opinions expressed in this blog do not in any way represent those of any organisation community association company circle of friends religious or ethnic group to which i am associated with jeshi
nani mwenye uwezo wa kulimiliki jeshi hili je tunao ubavu wa kudhibiti biashara za mkononi je hali itakuwaje miaka mitano kumi au zaidi ijayo
ama kwa hakika hapa tunapaswa kufikiri kwa bidii hapa sadaka kubwa inahitajika kiongozi shupavu tu ndiye atakayeweza kumaliza changamoto hii ya umachinga uchumi serious haupaswi kuwa na biashara aina hii kwa kiwango tulicho nacho
tukiwa na viongozi walio visionary committed and courageous tutaweza mungu ibariki tanzania
ni kibaha maili moja jumamosi 4 oktoba 2008
written by simbadeo october 8 2008 at 944 pm
« atown ndani ya nyumba
kopitan reprographic rights organisation » | 2017-07-28T14:47:22 | https://simbadeo.wordpress.com/2008/10/08/jeshi/ |
ikulu yalijibu gazeti la dira ya mtanzania yataka watoe majibu au wachukuliwe hatua | jamiiforums | the home of great thinkers
ikulu yalijibu gazeti la dira ya mtanzania yataka watoe majibu au wachukuliwe hatua
discussion in 'jukwaa la siasa' started by mwana mpotevu may 7 2012
ikulu imetoa taarifa kukanusha kuhusika kwao kwenye biashara na home shopping centre taarifa kwa vyombo vya habari
gazeti la kila wiki la dira ya mtanzania toleo la leo jumatatu mei 7 mwaka huu 2012 limechapisha habari yenye kichwa cha habari familia ya jk yachafuliwa katika habari hiyo gazeti hili linadai kuwa familia ya rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania mheshimiwa jakaya mrisho kikwete inafanya biashara na kampuni ya home shopping centre (hsc) ya dar es salaam
aidha gazeti hili linadai kuwa mkurugenzi wa kampuni hiyo bwana said saad ndiye msimamizi wa biashara za familia hiyo ya mheshimiwa raistunapenda kuujulisha umma habari hizo si za kweli ni uongo unaolenga kuupotosha umma na kuchafua jina la mheshimiwa rais kikwete na familia yake na au vinginevyo unalenga kuchafua jina la kampuni ya home shopping centre kama nia ni kufanya hivyo tafadhali msilitumie jina la familia ya rais
ni imani yetu kuwa gazeti hili litatoa majibu ya masuala haya muhimu katika toleo lake lijalo vinginevyo familia ya mheshimiwa rais itakuwa na haki ya kuchukua hatua stahiki za kisheria ……mwisho…
my take hivi kurugenzi ya mawasiliano ni msemaji wa ikulu ama msemaji wa familia ya jk
kumbe hawa taarifa wanazipata kila siku kamateni mafisadi basi na wanaosafirisha wanyama wetu au
ni wasemaji wa familia ya jk na riz
teheeeeeekaaazi kwelikweli
kumbe hawa taarifa wanazipata kila siku kamateni mafisadi basi na wanaosafirisha wanyama wetu auclick to expand
interejensia yao ni kuangalia cdm wako wapi na nani anamfatilia rais lakin si mambo ya umma
wakiona ina maslahi kwao wanakuwa wepesi kujitokeza kujibu na kujitetea
gazeti la kila wiki la dira ya mtanzania toleo la leo jumatatu mei 7 mwaka huu 2012 limechapisha habari yenye kichwa cha habari familia ya jk yachafuliwa katika habari hiyo gazeti hili linadai kuwa familia ya rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania mheshimiwa jakaya mrisho kikwete inafanya biashara na kampuni ya home shopping centre (hsc) ya dar es salaam
ni imani yetu kuwa gazeti hili litatoa majibu ya masuala haya muhimu katika toleo lake lijalo vinginevyo familia ya mheshimiwa rais itakuwa na haki ya kuchukua hatua stahiki za kisheria
mwisho
my take hivi kurugenzi ya mawasiliano ni msemaji wa ikulu ama msemaji wa familia ya jkclick to expand
hii ni taarifa kutoka familia ya rais au kutoka ikulu au kutoka ofisi binafsi ya rais (obr) du haya 2 people likes
inamaana hata biashara za riz1 wanazikanusha
mheshimiwa rais kikwete haendeshi hajawahi kuendesha na wala hana mpango wa kuendesha biashara iwe ni yeye binafsi au na familia yake ni vema gazeti likaeleza namna gani au likamtaja ni nani ndani ya familia ya mhe rais kikwete anaendesha biashara kwa kushirikiana na kampuni ya home shopping centre click to expand
ukisoma hizo sentence mbili ni wazi kuwa kurugenzi ya mawasiliano hawana uhakika na wanachosema sentence ya kwanza wanakanusha kuwa raia na familia yake hawahusiki lakini sentence ya pili wanataka gazeti limtaje mwanafamilia anayehusika pengine wao kurugenzi wangejiridhisha hakuna mtu anayehusika na hivyo watoe kanusho la ama yes au no 6 people likes
si ndio hapo magazeti yakiandika na kulalamikia ufisadi wanakaa kimyarais akiandikwa anafanya biashara wanatoa statement kwani kufanya biashara ni kosa ikulu watuambie kukiwa kuna ushahidi kua bosi wao anapiga madili na hsc atajiuzulu sio watu wanakuja na evidence afu bado anabakia tu pale anakenua
what a shame to the state department
hata kiwira ilikanwa hivi hivi yatajulikana tu we will leave no stone unturned
na pia dk slaa ashitakiwe au atoe ufafanuzi haraka ile issue ya r1 hatuwezi tukawa tunachafua majina namna hii
ha ha ha ha ha nimependa hiyo mh ni mkulima na mfugaji
yaani ikulu imepoteza credibility serikali yote ya tanzania imepoteza credibility hatari hii
inamaana hata biashara za riz1 wanazikanushaclick to expand
ndiyo maana yake mkuu
tetesi nilizosikia from a person who is close to the said guy ni kwamba in 2010 hsc ilitoa mil 500 kwa ajili ya kampeni za jamaa
kama kweli raisi wetu na familia yake hawafanyi biashara kabisa basi tuna raisi wa kipekee sana na wa kuigwa lakini kwani biashara ni dhambi
7 mei 2012click to expand
nimejaribu kuisoma tena bado najiuliza swali taarifa hii inatoka kwenye familia ya rais ikulu au ofisi binafsi ya rais (obr) nway lakini kwenye red hapo juu inaonesha inconsistency katika utumiaji wa aina ya maneno kiasi inachanganya wanataka kumuaddress nani hasa katika taarifa hii
paragraph yenye bluu ikichambuliwa vyema kuna ujumbe 'mtamu' katikati ya maneno hayo vipi jamaa wakiibuka na ushahidi tehe tehe tehe watoa taarifa wanaweka nini mezani kuahidi tehe tehe tehe
ukisoma hizo sentence mbili ni wazi kuwa kurugenzi ya mawasiliano hawana uhakika na wanachosema sentence ya kwanza wanakanusha kuwa raia na familia yake hawahusiki lakini sentence ya pili wanataka gazeti limtaje mwanafamilia anayehusika pengine wao kurugenzi wangejiridhisha hakuna mtu anayehusika na hivyo watoe kanusho la ama yes au no click to expand
mkuu unakuwa kama humfahamu salva
hajuu hata kukanusha | 2017-07-26T23:09:30 | https://www.jamiiforums.com/threads/ikulu-yalijibu-gazeti-la-dira-ya-mtanzania-yataka-watoe-majibu-au-wachukuliwe-hatua.263558/ |
kikao cha siku moja cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar zanzinews
home habari matukio kikao cha siku moja cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar
baadhi ya wajumbe kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar wakiimba wimbo wa chama kumkaribisha rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein (hayupo pichani) katika kikao cha siku moja kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi kuu ya ccm kisiwandui mjini unguja [picha na ikulu] 22/10/2017
rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein (katikati) na wajumbe kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar wakiimba wimbo wa chama kumkaribisha kabla ya kuanza kwa kikao cha siku moja kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi kuu ya ccm kisiwandui mjini unguja [picha na ikulu] 22/10/2017
naibu katibu mkuu wa ccm zanzibar dkjuma abdalla juma (mabodi) alipokuwa akimkaribisha rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein (katikati) kukifungua kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi kuu ya ccm kisiwandui mjini ungujawengine ni makamo wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania mama samia suluhu hassan (wa pili kushoto) na makamu wa pili wa rais wa zanzibar balozi seif ali iddi (kushoto)[picha na ikulu] 22/10/2017
wajumbe wa sekretarieti ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar wakiwa katika kikao cha siku moja cha kamati kuu ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar kilichofanyika leo katika ukumbi wa ccm kisiwandui mjini ungujachini ya mwenyekiti wake rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein(hayupo pichani) [picha na ikulu)22/10/2017
baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar wakifuatilia kwa makini taarifa zilizotolewa katika kikao hicho kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi kuu ya ccm kisiwandui mjini ungujachini ya mwenyekiti wake rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein (hayupo pichani)[picha na ikulu] 22/10/2017
rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein (katikati) alipokuwa akiendesha kikao cha siku moja cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi kuu ya ccm kisiwandui mjini unguja (kushoto) makamo wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania mama samia suluhu hassan na (kulia) naibu katibu mkuu wa ccm zanzibar dkjuma abdalla juma (mabodi) [picha na ikulu] 22/10/2017
rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi pia makamo mwenyekiti wa ccm zanzibar dkali mohamed shein(katikati) alipokuwa akizungumza na wajumbe wa kamati maalum ya halmashauri kuu ya ccm zanzibar katika kikao cha siku moja kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi kuu ya ccm kisiwandui mjini unguja[picha na ikulu] 22/10/2017 | 2018-04-22T12:02:27 | http://www.zanzinews.com/2017/10/kikao-cha-siku-moja-cha-kamati-maalum.html |
ponce de leon na chemchemi ya vijana
historia & utamaduni historia ya amerika ya kusini
explorer ya hadithi ya kutafuta chemchemi ya mythological
juan ponce de león (14741521) alikuwa mtafiti wa kihispania na mshindi wa vita alikuwa mmoja wa watu wa kwanza wa puerto rico na alikuwa mhispania wa kwanza kwenda rasmi (kutembelea florida) anakumbuka vizuri hata hivyo kwa kutafuta kwake fountain ya vijana ya hadithi je kweli aliutafuta na ikiwa ni hivyo aliiona
chemchemi ya vijana na hadithi nyingine
wakati wa uvumbuzi wanaume wengi walichukuliwa juu ya kutafuta maeneo ya hadithi
christopher columbus alikuwa mmoja alidai kuwa amepata bustani ya edeni kwenye safari yake ya tatu wanaume wengine walitumia miaka katika jangwa la amazon kutafuta mji uliopotea wa el dorado mtu wa golden wengine pia walitafuta giants nchi ya amazons na ufalme wa prester john hadithi hizi zilizidi sana na katika msisimko wa ugunduzi na uchunguzi wa dunia mpya haikuonekana kuwa haiwezekani kwa watu wa ponce de leon kupata maeneo hayo
juan ponce de león alizaliwa nchini hispania mwaka wa 1474 lakini alikuja ulimwengu mpya bila zaidi ya 1502 kwa 1504 alikuwa anajulikana kama askari mwenye ujuzi na alikuwa ameona hatua nyingi kupigana na wenyeji wa hispaniola alipewa ardhi kubwa na hivi karibuni akawa mpandaji na tajiri wakati huo huo alikuwa akijaribu kuchunguza kisiwa cha karibu cha puerto rico (ambacho kinachojulikana kama san juan bautista) alipewa haki za kukaa kisiwa hicho na alifanya hivyo lakini baadaye alipoteza kisiwa kwa diego columbus (mwana wa christopher) kufuatia hukumu ya kisheria nchini hispania
ponce de leon na florida
ponce de león alijua kwamba alikuwa na kuanza juu na kufuata uvumi wa ardhi tajiri kwa kaskazini magharibi ya puerto rico alichukua safari yake ya kwanza kwenda florida mwaka wa 1513 ilikuwa safari hiyo kwamba nchi ilikuwa jina lake florida na ponce mwenyewe kwa sababu ya maua huko na ukweli kwamba ilikuwa karibu na pasaka wakati yeye na wafungwa wake kwanza waliiona
ponce de león ilipewa haki za kukaa florida alirudi mnamo mwaka wa 1521 na kikundi cha wakazi lakini walifukuzwa na wenyeji wenye hasira na ponce de león walijeruhiwa na mshale wenye sumu alikufa muda mfupi baadaye
rekodi yoyote ambazo ponce de león zimeendelea safari zake mbili zimekuwa za muda mrefu tangu zimepotea historia taarifa bora juu ya safari zake huja kwetu kutoka kwa maandishi ya antonio de herrera y tordesillas aliyechaguliwa mhistoria mkuu wa indies mwaka 1596 miongo baada ya safari ya ponce de leon maelezo ya herrera ilikuwa uwezekano wa tatu kwa mkono anasema maji ya vijana kwa kutaja safari ya kwanza ya ponce huko florida mwaka wa 1513 hivi ndivyo herrera alivyosema kuhusu ponce de león na fountain of youth
juan ponce alisahau meli zake na ingawa alionekana kuwa alikuwa amefanya kazi kwa bidii aliamua kutuma meli ili kutambua isla de bimini hata ingawa hakutaka kwa maana alitaka kufanya hivyo mwenyewe akaunti ya utajiri wa kisiwa hiki (bimini) na hasa chemchemi ya pekee ambayo wahindi waliyasema ambayo iliwageuza wanaume kutoka kwa wazee kuwa wavulanahakuweza kupata hiyo kwa sababu ya shoals na mito na hali ya hewa kinyume basi juan pérez de ortubia akiwa nahodha wa meli na antón de alaminos kama jaribiowakawachukua wahindi wawili kuwaongoza juu ya viatu bahari nyingine (iliyoachwa kutafuta bimini na fountain) iliwasili na ikaeleza kuwa bimini (zaidi ya uwezekano wa kisiwa cha andros) imepatikana lakini si chemchemi
utafutaji wa ponce kwa chemchemi ya vijana
ikiwa akaunti ya herrera inapaswa kuaminika basi ponce iliwaokoa wachache wa wanaume kutafuta kisiwa cha bimini na kuangalia karibu kwa chemchemi ya fabled wakati walipokuwa legends ya chemchemi ya kichawi ambayo inaweza kurejesha vijana ilikuwa karibu kwa karne nyingi na ponce de león hakuwa na shaka kuwasikia pengine aliposikia uvumi wa eneo kama hilo huko florida ambalo haliwezi kushangaza kuna mengi ya chemchem ya mafuta na mamia ya maziwa na mabwawa huko
lakini alikuwa kweli akiutafuta haiwezekani ponce de león alikuwa mtu mgumu mwenye manufaa ambaye alitaka kupata bahati yake huko florida lakini si kwa kupata chemchemi ya kichawi katika tukio lolote ponce de leon mwenyewe alianza kupitia mabwawa na misitu ya florida kutafuta kwa makusudi chemchemi ya vijana
hata hivyo wazo la mshambuliaji wa kihispania na mshindi wa vita kutafuta chemchemi ya hadithi alitekwa mawazo ya umma na jina la ponce de leon litakuwa limefungwa kwa fountain ya vijana na florida hadi leo spas za florida chemchem za moto na hata wasaafu wa plastiki wanajishughulisha wenyewe na chemchemi ya vijana
fuson robert h juan ponce de leon na uvumbuzi wa hispania wa puerto rico na florida blacksburg mcdonald na woodward 2000
juan domingo peron na wanazi wa argentina
matukio 10 muhimu zaidi katika historia ya amerika ya kusini
historia ya amerika ya kusini vita vya kiraia na mapinduzi
meli maarufu za maharamia
mapinduzi ya mexican vita ya celaya
vita ya boyaca
wasifu wa francisco de miranda
umri wa dhahabu
juu villains kumi ya historia ya amerika ya kusini
mapinduzi ya mexican
wasifu wa simon bolivar
nguvu kundi la grittiest girl group
sabbeta ya baseball acronyms na ufafanuzi
faida za comptia a + vyeti
vidokezo 7 vya kuchagua mipango yanayofaa kwa nyumba yako ya ndoto
maswali ya saikolojia ya michezo kwa wanaoogelea yaliyomo
lebo ya rekodi ya kikristo kumbukumbu za sparrow
kalenda ya hindu inafananaje na gregorian
stcw viwango vya mafunzo vyeti na ufuatiliaji
jinsi astronomy ya rayray inafanya kazi
chuo kikuu cha michiganadmissions dearborn
sanaa za uhuru
kabla ya kujifunza biblia
ambaye alikuwa mshindi wa mwisho wa mashindano ya british open golf
hadithi za slave za kawaida
shtreimel ni nini
albamu 10 bora za kwanza za rap
hernandez jina la jina na mwanzo
hyena ya pango (crocuta crocuta spelaea)
dudou nguo za kale za kichina
mwaka mpya wa kichina taa ya taa
albamu bora za slayer
watetezi wa kisiasa na dini katika siasa
juniata chuo cha gpa sat na act takwimu
puyi mfalme wa mwisho wa china
nini cha kutarajia katika kipindi cha reflexology
utaniko wa uhamiaji
3 compasses iliyochaguliwa na misitu | 2020-07-16T14:22:30 | https://sw.eferrit.com/ponce-de-leon-na-chemchemi-ya-vijana/ |
kuelekea mkutano wa jumuiya ya madola sri lanka yasema haina chakuficha kuhusu suala la haki za binadamu ulaya rfi
canada david cameron india mahinda rajapakse mauritius jumuiya ya madola sri lanka uingereza
imechapishwa 14112013 • imehaririwa 14112013 saa 1354 | 2019-11-13T02:34:36 | http://m.sw.rfi.fr/generali/20131114-kuelekea-mkutano-wa-jumuiya-ya-madola-sri-lanka-yasema-haina-chakuficha-kuhusu-sua |
tanzanian blog awards vipengele vingine tutaviweka leo mchana
vipengele vingine tutaviweka leo mchana
bado tunamalizia kukagua vipengele vilivyobakia tutaviweka mchana huu na kuna blogs ambazo tumeziona zilipendekezwa kwa kutumia email account ya nomination@bloggerassociationoftananiacom niliiondoa mapema sana baada ya kuona kuwa watu watatuma kwa email accounts zote wakiwa wanapendekeza blogs zao kumbe mapema haikuwa mapema enough na kuna waliotumia email ile tu na nilikua sijaiforward kwa hawa vijana waliokua wanakusanya hizi blogs jana kuna mtu aliniambia amewapa watu email account hiyo wapendekeze blog yake na haioni katika blogs zilizopendekezwa ndio nikakumbuka na kuingia kuangalia
nimeona blog kadhaa zilipendekezwa kwa kupitia huko hivyo hizo blogs mnazoziona zimeengezwa ni kuwa zitukuzipata wakati nilipoletewa haya majina hapo mwanzoni hizo ilipendekezwa kwa kupitia hiyo email account nyingine | 2018-12-13T17:51:28 | http://tanzanianblogawards.blogspot.com/2013/09/vipengele-vingine-tutaviweka-leo-mchana.html |
aliyemuua mama yake ufoo saro na kujiua aagwa dsm kuzikwa kesho moshi tulonge
aliyemuua mama yake ufoo saro na kujiua aagwa dsm kuzikwa kesho moshi
posted by tulonge on october 17 2013 at 2300
waombolezaji wakipita kuaga mwili wa aliyekuwa mzazi mwenzake mwandishi wa habari wa itv/radio one ufoo saro marehemu anthery mushi wakati wa ibada fupi ya kuaga mwili wake iliyofanyika hospitali ya taifa ya muhimbili dar es salaam
comment by sharifa mkumbaru on october 19 2013 at 936
pole kwa wafiwa wote mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu walichokuwa nacho
comment by david edson mayanga on october 18 2013 at 1954
rip bro ila nimamuzi magumu sana lakini siri alikuwanayo yeye na mpenzi wake mh yetu macho ila mungu wasimamie
comment by cha the optimist on october 18 2013 at 1842
comment by mgao siaminip on october 18 2013 at 936
ilibidi amalize wote waliokula njamahasa huyo jamaa anaesemekana alitaka kumuoa ufosaro wakati hajajiridhisha kama mzazi mwenzie kamuacha au la maana inasemekana alikamilisha taratibu zote za kitamaduni ilibaki ndoa halafu hatujui mapenzi yao wametoka nayo wapi uckute wamesomeshana na shule wanawake kuweni waminifu
comment by habiba mustafa mlawa on october 18 2013 at 857
ni maamuzi magumu sana rip bro | 2020-05-29T08:32:34 | http://tulonge.ning.com/profiles/blogs/aliyemuua-mama-yake-ufoo-saro-na-kujiua-aagwa-dsm-kuzikwa-kesho-m?xg_source=activity |
bbc swahili habari mkuu wa majeshi drc afutwa kazi
imebadilishwa 23 novemba 2012 saa 1011 gmt
generali amisi
mkuu wa majeshi nchini jamuhuri ya kidemokrasia ya congo amesimamishwa kazi huku uchunguzi ukiendelea kufuatia madai kuwa aliwauzia silaha makundi ya waasi yanaopambana na serikali ya nchi hiyo
ripoti moja ya umoja wa mataifa imemtuhumu generali gabriel amisi kwa kuendesha mtandao wa kusambaza silaha kwa wawindaji haramu na makundi ya waasi likiwemo kundi la mai mai raia mutomboki
msemaji wa serikali ya nchi hiyo amesema maafisa kadhaa wa jeshi pia wanachunguzwa
serikali ya rais kabila imemfuta kazi mkuu huyo wa majeshi siku chache baada ya waasi wa m23 kuuteka mji wa goma mashariki mwa nchi hiyo
waasi hao mpia wameutekja mji wa sake lakini msemaji wa serikali lambert mende amesema wanajeshi wa serikali wamefanikiwa kuumboa tena mji huo mdogo
waasi hao ambao wanaaminika kuungwa mkono na serikali za rwanda na uganda wametishia kuendeleza mapigano hayo hadi mji mkuu wa kinshasa ikiwa rais joseph kabila hatabuli kuanzisha mazungumzo ya amani
uganda inaandaa mkutano wa marais wa rwanda na uganda hii leo na kuna ripoti kuwa baadhi ya viongozi wa kundi hilo la waasi wa m23 wamesafiri mjini kampala kushiriki katika mazungumzo hayo
ripoti iliyoandikiwa umoja wa mataifa na kundi moja wa wataalamu huru imesema kuwa generali amisi anaendesha mtandao wa kusambaza silaha kwa makundi ya kihalifu na waasi wanaohudumu mashariki mwa congo eneo ambao bado kuna idadi kubwa ya wapiganaji wa waasi
hata hivyo kundi hilo la m23 halikuwa miongoni mwa makundi yaliyotajwa kwenye ripoti hiyo lakini kundi la raia mutomboki moja ya makundi kadhaa yanayojumuisha wapiganaji wa mai mai inaaminika kuwa na uhusiano wa karibu na kundi hilo la m23
ripoti hiyo ya umoja wa mataifa imenadi kuwa generali amisi aliagiza bundi 300 aina ya ak47 kukabithiwa kundi moja linalohudumu katika eneo hilo la mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya congo lijulikanalo kama nyatura
ripoti hiyo imeongeza kusema kuwa waasi hao wananunua risasi kutoka kwa nchi jirani ya congo na kusafirisha kupitia kinshasa hado mashariki mwa nchi hiyo na mtandao unaoendeshwa na washirika wa generali amisi wakiwemo baadhi ya jamaa ya familia yake | 2017-12-16T13:53:07 | http://www.bbc.com/swahili/habari/2012/11/121123_waasicongo |
kwa wote wasiwasi live kutoka lockdown 3703
on desemba 5 2014 mimi ilikuwa imefungwa chini kwa 212 group maandamano 196 matumizi haramu ya barua pepe na 106 kuchochea ghasia all inayotokana na sehemu ya mwisho ya hotuba nilitoa katika usp victorville haki matrix on desemba 31 2014 baada ya saa tatu majaribio kusikia mimi nilikuwa huru wa mashtaka yote
baada ya miaka kumi na saba mimi hatimaye got kipande kidogo ya haki wewe kuchimba
gangster je gangsta si
stateville correctional center mashairi mahabusu locator tewhan butler inmate search mitaani magenge smu kuongeza up media molekulikufungwa jela wafungwa maalum management unit kuongeza up chicago shirikisho gerezani uhalifu new jersey live kutoka lockdown kubadilisha lockdown confinement faragha mahabusu lookup usp lewisburg mahabusu gangsta illinois bloods live from penitentiary magenge gereza | 2017-08-24T08:53:26 | http://www.livefromlockdown.com/sw/to-all-concerned/ |
michuzi blog dkt arnold kashembe katibu mkuu mpya wa simba ' if(imglength>=1) { imgtag = '
dkt arnold kashembe katibu mkuu mpya wa simba
friday july 14 2017 ~ copyright michuzi blog michezo ~ mtumie rafiki yako maoni 0 | 2017-09-22T22:29:57 | https://issamichuzi.blogspot.com/2017/07/dkt-arnold-kashembe-katibu-mkuu-mpya-wa.html |
download audio nikki mbishi ft slim sal nataka kutoka ngombozi media con =
home nikki mbishi download audio nikki mbishi ft slim sal nataka kutoka
download audio nikki mbishi ft slim sal nataka kutoka
nikki mbishi ft slim sal nataka kutoka
tags nikki mbishi | 2020-04-06T11:52:07 | https://www.ngombozi.com/2019/08/blog-post24_37.html |
sababu kwanini wanaume waliofanya punyeto kwa muda mrefu huwa na maumbile madogo na yaliyo sinyaa | mpekuzi
sababu kwanini wanaume waliofanya punyeto kwa muda mrefu huwa na maumbile madogo na yaliyo sinyaa
wanaume wengi waliofanya mchezo wa kujichua kwa muda mrefu hupatwa na side effect ya kuwa na kusinyaa na kudumaa kwa maumbile yao ya kiume ambayo huenda pamoja na tatizo a ukosefu na ama upungufu wa nguvu za kiume
nini husababisha hali hii
kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kitaalamu zifuatazo ndio sababu kuu kwanini wanaume walio jihusisha na tabia ya kujichua kwa muda mrefu hupatwa na tatizo la kusinyaa na kudumaa kwa maumbile ya kiume
kwa mujibu wa tafiti za kitaalamutendo la kujichua kwa mwanaume linapofanyika kwa kipindi kirefu huathiri na uharibu mishipa na misuli ya uume na hivyo kusababisha kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ateri jambo hili husababisha makuu mawili
1 huzuia mishipa ya ateri kupanuka na kuongezeka jambo linalotajwa na wanasayansi kama jambo muhimu sana katika kukua kwa uume
2 huzuika kutirika kwa damu kuingia kwenye misuli ya uume
mambo hayo mawili huathiri sana ukuaji wa uume kwa sababu yanapo tokea huathiri uzalishaji wa homoni muhimu zinazo husika na ukuaji wa misuli ya uume na matokeo yake husababisha uume wa mhusika kudumaa kusinyaakunywea na kurudi ndani kiasi cha kuufanya uonekane kama uume wa mtoto
homoni hujulikana kitaalamu kama hgh na huzalishwa kwenye ini
sababu nyingine inayo tajwa na wataalamu ni kwamba mwanaume anae fanya punyeto hutumia akili nguvu na nishati nyingi sana jambo ambalo huathiri utendaji wa wa ogani nyingine muhimu katika mwili likiwemo ini ikumbukwe katika ini ndimo huzalishwa homoni zijulikanazo kama hgh ambazo ndizo zinazo husika na kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume
upigaji punyeto pamoja na mambo mengine huathiri pia utendaji kazi wa ini na moja kati ya kazi za ini ni pamoja na kuzalisha homoni hizo zijulikanazo kama hgh ambazo huusika na kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume
na kwa mujibu wa maelezo ya wanasayansi kinacho fanya ini lishindwe kuzalisha homoni za hgh kwa mwanaume anaejihusisha na upigaji punyeto ni kwa sababu ya kukosa nishati ya kutosha inayo hitajika katika uzalishaji wa homoni hizo
nishati hii hupotea katika tendo la upigaji punyeto kwa sababu mtu anepiga punyeto hutumia nguvu akili nguvu na nishati nyingi sana nishati inayo potea wakati wa tendo la upigaji punyeto huathiri utendaji wa ogani nyingine mwilini likiwamo ini
kibaya zaidi ni kwamba waathirika wengi wa punyeto huanza kujihusisha na punyeto katika umri wa balehe
na kwa mujibu wa tafiti za kitaalamu ni katika kipindi hiki hiki cha balehe ndio kipindi ambacho homoni za hgh ambazo huhusika na kuchochea ukuaji wa sehemu mbalimbali mwilini yakiwemo maumbile ya kiume ndio huzalishwa kwa wingi
matokeo yake ni kwamba maumbile ya kijana husika yanashindwa kuendelea kukua kwa sababu upigaji punyeto huzuia ama kupunguza uzalishwaji wa homoni hizo
1kama bado unaendelea kujihusisha na punyeto basi jitahidi uache tabia hiyo mara moja kwani inakuharibu inaweza isiwe rahisi sana kuacha mara moja lakini ukiweka nia thabiti basi unaweza kuacha kabisa kama walivyofanikiwa kuacha wengine ambao walikuwa wametopea kwenye tabia hiyo lakini wakajitahidi kujilazimisha na hatimaye wakafanikiwa kuachana kabisa na tabia hiyo
kama utaona kuna ugumu wa kuacha tabia hiyo unaweza kubonyeza link hii hapa chini ili uone namna unavyo weza kutumia mbinu ya asili kuweza kuachana na tabia hiyo mbinu hiyo haikufanyi uache punyeto moja kwa moja isipokuwa inasaidia kukulazimisha kuacha punyeto
ina saidia ku incapacitate uwezo wa wewe kufanya punyeto mbinu hii inahitaji ushirikiano wako wa dhati kabisa kwa sababu wewe mwenyewe ndio utakae amua kuendelea kuitumia mbinu hiyo kila siku ili usiweze kufanya punyeto
kusoma mbinu hiyo bofya hapa https//neemaherbalistblogspotcom/2013/03/tibayaasiliyakuachapunyetokwahtml
2 tumia tiba maalumu kwa ajili ya kutibu athari zilizo tokana na tabia ya kujichua pamoja na kurejesha maumbile yako katika hali yake ya kawaida
kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa simu namba 0693 005 189 au 0766 538384 tunapatikana ubungo jijini dar es salaam nyuma ya jengo la ubungo plaza jirani na shule ya msingi ubungo national housing
na kwa makala zaidi tutembelee kila siku kupitia blogu yetu | 2019-09-18T14:18:11 | http://www.mpekuzihuru.com/2019/04/sababu-kwanini-wanaume-waliofanya.html |
mzee wa mshitu pumzika wa amani marehemu anneth christian kajura
pumzika wa amani marehemu anneth christian kajura
mume wa marehemu akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mke wake anneth christian mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwa marehemu mbezi beach salasala jijini dar es salaam na baadae maziko yalifanyika makaburi ya kondo bahari beach
mmoja ya wanandugu akitoa heshima ya mwisho
mume wa marehemu anneth christian akiweka mchanga katika kaburi la mke wake katika makaburi ya kondo bahari beach
mama wa marehemu akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mwanae anneth christian mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwa marehemu mbezi beach salasala jijini dar es salaam na baadae maziko yalifanyika makaburi ya kondo bahari beach
mume wa marehemu akiweka shahada la ua katika kaburi la mke wake katika makaburi ya kondo bahari beach
mtoto wa marehemu akiweka mchanga katika kaburi la mama yake
mama wa marehem akiweka mchanga katika kaburi la mwanae
wanafamilia wakiweka maua katika kaburi la anneth christian
mwili wa marehemu anneth christian ukiingizwa nyumbani kwake mbezi beach salasala jijini dar es salaam na baadae maziko yalifanyika makaburi ya kondo bahari beach
yasome hapa magazeti ya leo jumapili agosti 20 2017 | 2017-08-20T07:55:31 | http://charaz.blogspot.com/2015/11/pumzika-wa-amani-marehemu-anneth.html |
psychiatric disorders and criminality | jama | jama network
jama 1974227(6)641642 doi101001/jama197403230190033008
guze sb woodruff ra clayton pj psychiatric disorders and criminality jama 1974227(6)641642 doi101001/jama197403230190033008 | 2018-05-22T12:06:40 | https://jamanetwork.com/journals/jama/article-abstract/352879?redirect=true |
unapomtaja guardiola umkumbuke na conte bingwa
nyumbani maoni unapomtaja guardiola umkumbuke na conte
pep guardiola ni kama ameshamaliza kazi aliyopanga kuifanya pale manchester city na kizuri zaidi ameifanya man city icheze kama wale wamiliki wa kiarabu walivyotamani kwa miaka kadhaa sasa
nani anayeweza kukaa bila kumuwaza guardiola kwa sasa
katika wakati huu unaosoma andiko hili nikukumbushe vitu viwili ambavyo vina kiki sana nanihii kukaza pamoja na simba kuendelea kushikilia usukani wa vpl halafu cha tatu ambacho kipo mawazoni mwa wadau wengi wa soka nchini hasa wale wanaofuatilia soka la majuu ni pep guardiola
guardiola anatajwa sana halafu anayefuata kwa karibu ni jose mourinho na man united yake kwa ujumla
antonio conte yeye amepotea kabisa kwenye fikra na midomo ya wengi si mbaya sana kwa sasa angalau anapumua kwa amani ni mwanamume pekee aliyefanikiwa kupata utulivu wa nafsi na akili wakati muhimu katikati ya mawimbi mazito pale chelsea
kazi anayoifanya pale stamford bridge kwa sasa inaridhisha nazungumzia katika msimu wa pili baada ya kuchukua ubingwa wa premier league ni tofauti na ilivyokuwa kwa kocha aliyemtangulia darajani mourinho
mourinho kwa sasa anahangaika kuirudisha manchester united kwenye reli conte amefanikiwa kutulia na kuifanya chelsea ikae sawa kwenye reli ambayo mourinho aliwahi kupita kwa misukosuko miaka miwili iliyopita
nani amesahau kilichomuondoa mourinho pale chelsea si kitu kigeni sana na ambacho kilikaribia kumfukuzisha kazi conte darajani msimu huu
mourinho aliondoka kwa aibu chelsea baada ya kuipa ubingwa msimu mmoja kabla kilichomtoa pale ni baada ya kuifanya timu hiyo kumaliza katika nafasi mbovu mno ikiwa kama bingwa mtetezi
miezi saba tu baada ya kuchukua ubingwa wa premier mourinho alisimamishwa kazi huku chelsea akiiacha katika nafasi ya 16 tena ikiwa kwenye hatari kubwa mno ya kushuka daraja kuliko kutetea ubingwa
hiyo ikaongezwa kwenye historia ya makocha waliotimuliwa chelsea halafu jina la conte nalo likaandaliwa kuingizwa humo hasa baada ya kulumbana na mshambuliaji mahiri aliyeisaidia sana chelsea diego costa kumkosa romelu lukaku katika vita ya kumwania dhidi ya manchester united
na kingine kikubwa zaidi ni kumuuza kiungo mkabaji nemanja matic kwenda man united
kitendo cha nyota hao wawili lukaku na matic kuanza vizuri united kilisababisha maisha ya conte yawe magumu chelsea
kwanini sababu ni licha ya kubakiwa na akina eden hazard pedro willian sambamba na kusajili watu kama tiemoue bakayoko na danny drinkwater ambao waliangaziwa kama jeshi litakalomsaidia conte kutetea ubingwa bado alionekana kama kocha mwingine atakayefeli tu katika msimu wa pili
maneno mengi yalisemwa wengi walimcheka na kumtabiria anguko msimu huu
presha ikawa kubwa hata yeye mwenyewe alikaribia kuanguka kwenye kibarua chake kazi ilitaka kumshinda
nimeamini soka ni mchezo wa wazi na kila kinachotokea kwenye mchezo huu si maigizo sikuamini kama chelsea itatulia hivi baada ya kuchukua ubingwa msimu uliopita baada ya changamoto za usajili
sikuamini kama conte angefika mbali na chelsea hii hasa kutokana na kutoelewana na watu kama michael emenalo ambaye alikuwa mkurugenzi wa ufundi akisimamia sajili za wachezaji na mwanamama mkurugenzi mwingine wa klabu maria granovska
lakini baada ya kutokea hayo yote hadi kupelekea emenalo kuondoka chelsea conte aliamua kubaki na kutuliza akili yake kwenye mawimbi mazito ili kuilinda heshima yake kama kocha mwenye mafanikio italia na england pamoja na kuilinda hadhi ya chelsea kwa ujumla
ukizitaja timu zenye presha sana england man united inaongoza ikifuatiwa na chelsea inahitaji kocha mwenye busara sana kuzisimamia hizi timu conte amedhihirisha kuwa yeye ni jabali mwamba jembe anayeweza kuishi katika vipindi tofauti vya soka
guardiola kazi yake ishamalizika ana nini kipya cha kuzungumziwa zaidi ya rekodi atakazoendelea kuzivunja
kwa sasa hebu tumwangalie conte na jeshi lake la chelsea jeshi lililotulia na linaloelekea katika njia sahihi
makala ya awalimwaka huu uwe wa mafanikio katika michezo
makala ijayohii hapafirst elevenkali epl 2017 | 2018-07-19T19:14:17 | http://bingwa.co.tz/unapomtaja-guardiola-umkumbuke-na-conte/ |
tamasha la fiesta latamatika jijini dar es salaam rfi
imetangazwa tarehe 01122017 imehaririwa 21122017 saa 1026
wapenzi wa muziki wa bongo fleva wakishangilia moja miongoni mwa tamasha la fiesta 2017 msafimediacom | 2018-10-15T13:57:55 | http://sw.rfi.fr/afrika/20171201-tamasha-la-fiesta-latamatika-jijini-dar-es-salaam |
kura uako utaipeleka kwa nani hapa | spoti na starehe
homehabari za afya ya uzazijunekweli koffi olomide kakopa kwa jb mpiana dola 30000 magari yanauzwamaoni yakomaywerrason kafungua mradi wa kuuza madiniwerrason na jb mpiana wampongeza papa wemba kutokana na ndoa yake ya kanisani
kura uako utaipeleka kwa nani hapa
msikilize mtaalamu heritier watanabe mzee wa masauti hapa
hapa kuna nyimbo mbili ambazo zinafanana kimiondoko kwa maana zote zimepigwa taratibu ni nyimbo ambazo kiukweli ndio zinapendwa zaidi katika ulimwengu wa wazungumza lingala nyimbo hizi ni 3éme doigt ya ferre gola ambae nadhani kila mtu anafahamu kwamba hizi ndio njia zake ukitaka kumjua sawasawa basi ni kwenye hizi rhumba za kicongo lakini pia tuna wimbo remise et reprise wakwake heritier wata plus akimshirikisha de la forret werrason zitazame na kuzisikiliza vizuri then kama unachochote kiseme la huna cha kusema basi pata burudani kimya kimya tu
this entry was posted on sunday march 31st 2013 at 626 am and is filed under michezo you can follow any responses to this entry through the rss 20 feed
one response to kura uako utaipeleka kwa nani hapa
glady says september 10 2013 at 556 pm ndio watanabe anaimba ila ferre yuko juu sauti ya ajabu
2116114 hits
r i p mama anene instagramcom/p/bh1tgtfbhjsn 4 months ago
rip my sister kipenzi edwina pius mikongoti tulikupenda sana mama instagramcom/p/bhx8pl6btra2 4 months ago
huawei p8 huawei p8 4g octa core 3gb 64gb limited edition instagramcom/p/bhq8toohwyeg 4 months ago
mwanagenzi rais mstaafu mzee ali hassan mwinyi alifurahi sana instagramcom/p/bhpng0ybckyj 4 months ago
mheshimiwa aliniomba tupige picha nisingeweza kumkatalia kwakweli instagramcom/p/bho_hknhuhci 4 months ago
picha za mwili wa kanumba ukiingizwa chumba cha maiti muhimbili magari yanauzwa habari za afya ya uzazi simulizi ya kweli ya kifo cha aliyekuwa mkuu wa mkoa wa iringa 1971 dr kleruu tafsiri ya wimbo selfie ekotite wa nguli koffi olomide for sale subaru impreza wrx turbo 6000 usd to dar es salaam amida shatur vs sylvie mampata koffi apata ruhusa kuimba nyimbo za franco ally mayai tembele mrs col maganga alipokamata nondo yake wadhamini
liverpool left stunned december 5 2016 big wins for bournemouth and chelsea left liverpool and man city in despair the reds proved you can score three goals and still lose if you concede four while pep guardiola&aposs men lost the plot and the game iain macintosh » trending mourinho defends marouane fellaini klopp denies mental collapse december 5 2016 here are the latest stories for monday espn staffalexis sanchez cesc fabregas lead team of the weekend with diego costa december 4 2016 after each round of premier league fixtures espn fc brings you its team of the weekend our panel of experts carefully selects 11 star tom sweetmantransfer rater mesut ozil to real madrid manolo gabbiadini to everton december 5 2016 things change in the blink of an eye in football the danny lee footballwhisperscristiano ronaldo and jose mourinho were warned over tax affairs report december 5 2016 the representatives of cristiano ronaldo and jose mourinho were warned that the structure of the their tax affairs was potentially risky dermot corriganarsenal midfielder mesut ozil paid ¬2m in spanish backtaxes report december 5 2016 germany international mesut ozil paid more than €2 stephan uersfeldmario balotelli had behaviour clause in liverpool contract report december 5 2016 mario balotelli was entitled to a bonus payment of £1 million from liverpool if he was not sent off on three occasions each season for espn staffman united boss jose mourinho defends bringing on marouane fellaini december 5 2016 manchester united manager jose mourinho was unhappy with questions about his decision to bring on marouane fellaini as a late substitute in pa sportman united's marcos rojo deserved red card vs everton former top refs december 5 2016 marcos rojo&aposs challenge on idrissa gueye has been described as reckless and serious by former referees who feel the manchester united arindam rej man united correspondentman united's paul pogba unhappy with distorted juventus 'holiday' stories december 5 2016 manchester united midfielder paul pogba has hit out at distorted claims from the media who he accused of twisting his espn staffjurgen klopp defends loris karius after jamie carragher criticism december 5 2016 liverpool manager jurgen klopp was quick to shrug off criticism of goalkeeper loris karius after liverpool&aposs 43 defeat at bournemouth on espn staffinform diego costa now 'showing maturity' at chelsea gary cahill december 5 2016 chelsea captain gary cahill believes diego costa is now a smarter player after he helped fire the club clear at the top of the premier espn staff
anton's mathewa mwas on kolonia santita riwaya ya kisvanesa mush on picha za mwili wa kanumba ukiianonymous on sandra lina mcheza show wa wenanonymous on yanga yaongoza kwa kipato timu0977013892 on picha za mwili wa kanumba ukii twitter updates
spotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordprspotistarehefileswordpryoutubecom/watchv=5zequ | 2016-12-05T12:34:37 | https://spotistarehe.wordpress.com/2013/03/31/kura-uako-utaipeleka-kwa-nani-hapa/ |
migongo 1950 ikulu yamjibu godbless lema
ikulu yamjibu godbless lema
kauli hii ya bwana lema ni upuuzi siyo mheshimiwa rais kikwete wala ikulu imeingilia kati kesi yake kwa namna yoyote ile iwe ni kwa kupiga simu ama kuzungumza na mheshimiwa jaji rwakibalirakwa hakika haijapata kutokea
mheshimiwa kikwete tokea alipoingia madarakani desemba 21 2005 akaingilia kwa namna yoyote ile mwenendo wa kesi yoyote ile katika mahakama yoyote na ya ngazi yoyote katika tanzania na wala hakusudii kufanya hivyo wakati wote wa muda wake uliobakia wa uongozi siyo kazi ya rais kutoa hukumu ama kuelekeza namna ya kutoa hukumu katika kesi zilizoko mahakamani rais hana madaraka wala mamlaka hayo
bwana lema asitafute visingizio kwa yaliyomfika kwa sababu hakuna mtu mwingine wa kumbebea msalaba huubadala ya kutafuta mchawi asiyekuwepo ni vyema bwana lema angekaa chini na kuangalia ni sababu zipi za kisheria zilizomfanya ashindwe na kama ameridhika kuwa hakutendewa haki akate rufani kwa mujibu wa sheria na taratibu
tunaomba wananchi wampuuze ameshindwa kesi kwa makosa yake aliyofanya hana mtu wa kumlaumu bali ajilaumu mwenyewe
posted by elia migongo at 1021 pm | 2018-07-16T12:44:44 | http://eliamigongo.blogspot.com/2012/04/ikulu-yamjibu-godbless-lema.html |
ruhagoyacucom perezida magufuri yohereje ubutumwa bwakababaro yatewe nurupfu rwumufana wa yanga
yanditswe kuya 22062017 saa 0932' na philbert hagengimana
perezida john pombe magufuri wa tanzania yagaragaje akababaro atewe nurupfu rwa ali mohamed bakundaga kwita ali yanga umufana wa yanga africans wahitanywe nimpanuka yimodoka
mu itangazo rigenewe abanyamakuru ryashyizwe ahagaragara nibiro byumukuru wigihugu cya tanzania perezida magufuri yoherereje ubutumwa bwakababaro umuryango wa ali yanga abayoboke bishyaka ccm (chama cha mapinduzi) ubuyobozi bwikipe ya yanga africans ndetse nabandi bakunda umupira wamaguru muri rusange
ali yanga yapfuye kuwa 20 kamena azize impanuka yimodoka yakoreye ahitwa chipogoro mu karere ka mpwapwa ho mu ntara ya dodoma
ali yanga yabaga ameze nkaho umutima wenda guhagarara iyo yanga yabaga irimo yotswa igitutu
perezida magufuri yagaragaje ko atazibagirwa uburyo ali yanga yakundaga igihugu akabigaragaza haba imbere mu gihugu ndetse no mu mahanga ndetse nuburyo yakundaga imikino byumwihariko
perezida magufuri yagize ati mbabajwe cyane nurupfu rwa ali yanga nari kumwe na we mu gihe cyo kwiyamamaza mu matora ya 2015 aho yagize uruhare runini mu gushishikariza abanyagihugu gushyigikira ishyaka ryanjye ccm anabifatanya no kuyobora abandi bafana mu gushyigikira yanga ndetse nikipe yigihugu ya tanzania kandi atananirwa yari umuhanga mu bufana bwe
perezida wa tanzania john pombe magufuri ntazibagirwa akamaro ka ali yanga muri ccm
yakomeje agira ati nihanganishije cyane umuryango we abayobozi bikipe ya yanga abakunda imikino bose abarwanashyaka ba ccm nabandi mwese mwababajwe nurupfu rwa ali yanga nkanamusabira ku mana ngo roho ye iruhukire mu mahoro amina
ally yanga umufana ukomeye wikipe ya yanga africans wari uzwi cyane i dar es salaam nahandi hose ikipe ye yajyaga gukina yaba mu gihugu cyangwa hanze ubuyobozi bwikipe ya yanga africans bwemeje ko yamaze kwitaba imana
imodoka ali yanga yarashwanyaguritse ku buryo kuyirokoka byari kuba ari igitangaza
nkuko yanga africans itazamwibagirwa ali yanga ntazava mu mitwe yabakeba bayo kubera ukuntu yabazengerezaga
mbere yo kuza i kigali uganda cranes yagereye kcca mu gatebo kamwe namavubi
issa hayatou yamaganye ibyavuzwe nuwamusimbuye ku buyobozi bwa caf | 2017-08-21T16:05:46 | http://ruhagoyacu.com/afurika/amakuru-ashyushye/article/tanzania-perezida-magufuri-yohereje-ubutumwa-bw-akababaro-yatewe-n-urupfu-rw |
uhuru anaelekezwa kwenye mtego kutokana na sakata za ufisadi mutahi ngunyi ▷ tukocoke
uhuru anaelekezwa kwenye mtego kutokana na sakata za ufisadi mutahi ngunyi
maoni 1084
ngunyi amekiri ufisadi upo lakini hali hiyo imekusudiwa kuzua hasira na kuonyesha uhuru hana ujuzi wa kuongoza na hafanyi bidii
amesema kuwa ingawa uhuru alirithi mfumo wa serikali uliokuwa na ufisadi inaaminika ana uwezo kukabiliana na jinamizi hilo kama mkuu anayewateuwa maafisa serikalini
mwanasayansi huyo wa siasa alimtaka rais kufanya mabadiliko kwenye idara ya wafanyikazi wa umma ikiwa anataka kushinda vita dhidi ya ufisadi
mwanasayansi wa siasa mutahi ngunyi ameonya kuwa rais uhutu kenyatta anaelekezwa kwenye mtego wa kisiasa kutokana na sakata za ufisadi zinazoendelea kuchipuka
ngunyi alisema serikali ilikuwa uchi na mbinu ya kukabiliana na ufisadi ilikuwa ya hali ya chini alisema hali hiyo ilipelekea kuangaziwa sana kwa sakata za ufisadi kwenye mwaka wa kwanza wa muhula wa pili wa uongozi wa uhuru
ngunyi alionya kuwa sakata za ufisadi zinakusudiwa kusababisha hasira miongoni mwa raia na kupelekea uhuru kuondolewa ofisini kwa kura ya kutokuwa na imani naye
mwanasayansi wa siasa mutahi ngunyi amedai kuwa rais uhuru kenyatta yuko kwenye hatari ya kuondolewa ofisini kwa kura ya kutokuwa na imani naye kutokana na sakata za ufisadi picha you tube
miezi sita ndani ya muhula wa pili wa uongozi wa uhuru ufisadi umesambaa sana na hautaisha ufisadi umezishinda ajenda nne kuu za uhuru
kwa maoni yetu sakata hizo ni mradi uliopangwa kuzua hasira na kumfanya uhuru aonekane kama rais ambaye hana ujuzi wa kuongoza na unaonekana kufanya kazi mutahi alisema kwenye kipindi chake cha mtandaoni cha fifth estate jumatatu mei 28
ngunyi alionya kuwa sakata za ufisadi zitamfanya rais uhuru apingwe vikali hali ambayo itaharibiwa zaidi na maridhiano yake ya kisiasa
hata wakikuyu waliomuunga mkono wataanza kumuona kama mtu ambaye hana ujuzi hali hii itakuwa imepangwa kutoa sababu ya kumwondoa ofisini kwa kura ya kutokuwa na imani naye
tunamuonya uhuru kuna mtego mbele yake ikiwa hutadhibiti siasa siasa itamdhibiti na uamuzi wa maraga bado ni kumbukumbu yenye uchungu mutahi aliongeza akizungumzia kufutwa kwa uchaguzi wa uhuru kwenye uchaguzi mkuu wa urais wa agosti 8 2017
ngunyi alisema kuwa licha ya uhuru kuurithi mfumo wa serikali wenye ufisadi alikuwa na mamlaka ya kusitisha uporaji wa mali ya umma unaoendelea
hatuwachagui mkurugenzi wa nys mkurugenzi wa ncpb au mkurugenzi wa kpc tulimchagua uhuru kenyatta pesa za umma zikiibwa rais ndiye anawajibika na sio wale aliowachagua ngunyi aliongeza
ngunyi alidai kuwa rais alimrushia lawama mkuu wa huduma kwa umma joseph kinyua afisa ambaye yeye alimchagua na anafanya kazi chini ya uongozi wake
ikiwa serikali ya uhuru iko uchi basi idara ya huduma kwa umma imemfanya afeli ni rahisi hivyo
kwa maoni yangu ni mapema sana kuzungumzia kura ya kutokuwa na imani lakini rais hastahili kuacha nafasi kwa wazo hilo kuwepo kutokana na kufeli kwa idara ya huduma kwa umma anahitaji kufanya mabadiliko kwenye idara hiyo ili kuangamiza ufisadi ngunyi alimshauri rais
knec examiners portal kikuyu proverbs huduma centre birth certificate replacement prediction sites mpesa charges 2018 | 2018-12-12T22:03:24 | https://kiswahili.tuko.co.ke/275145-uhuru-anaelekezwa-kwenye-mtego-kutokana-na-sakata-za-ufisadi-mutahi-ngunyi.html |
the superstars tz diamond aweka wazi kuhusu yeye kumuowa zari
diamond aweka wazi kuhusu yeye kumuowa zari
staa wa bongo fleva nasibu abdul diamond platnumz akiwa na mwandani wake zarinah hassan zari the boss lady katika pozi
kiki wikiendi iliyopita gumzo kubwa katika mitandao ya kijamii lilikuwa ni kuhusu stori ya staa wa bongo fleva nasibu abdul diamond platnumz kufunga ndoa na mwandani wake zarinah hassan zari the boss lady lakini ijumaa wikiendalimezungumza na mwanamuziki huyo na kupata ukweli wake
hizo ziliibuka katika mtandao wa instagram mara baada ya diamond kuweka
picha iliyomuonesha akiwa na zari ambaye alivaa shela huku diamond akiwa na suti kuashiria kuwa wawili hao wamefunga ndoa kutokana na ujumbe uliosindikiza picha hiyo
aliandika wakati mwingine usiri una baraka zaidialhamdullah (sometimes privacy has more blessingsthank you so much god)
baada ya ujumbe huo ndipo mashabiki wao walipoanza kusambaziana ujumbe kuwa diamond amemuoa zari
ya kuenea kwa ubuyu huo mwanahabari wetu alimvutia waya diamond na kumtaka aeleze ukweli wa habari hiyo ambapo alifunguka
ijumaa wikienda ebwana vipi hii ishu ya ndoa ni kweli umeoa
diamond suala la ndoa lipo tu kwani wewe hujui mtoto zari ana familia yangu nikikamilisha mchakato naweka wazi kila kitu
ijumaa wikienda kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania kwamba umeshamuoa zari au bado
taratibu za awali nyingi tumeshakamilisha lakini zaidi kuna kitu kikubwa natarajia kukifanya pale mlimani city (dar) na hiki kitathibitisha ukweli wa unachokiuliza
ijumaa wikienda umesema nisubiri sawa hiyo mlimani city ni tarehe ngapi
diamond usijali ni mei mosi mwaka huu
ijumaa wikienda poa kila la kheri tutajumuika pamoja siku hiyo
mara kadhaa diamond amekuwa akionesha nia ya kumuoa zari hivyo mashabiki wengi wanaamini kuwa safari hii yupo siriaz zaidi
inasemekana huyu ndiye mwigizaji mwenye demu mkali | 2017-03-29T20:58:24 | http://thesuperstarstz.blogspot.com/2015/04/diamond-aweka-wazi-kuhusu-yeye-kumuowa.html |
makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania mhe samia suluhu aongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha wauguzi wakunga zanzinews
home habari matukio makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania mhe samia suluhu aongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha wauguzi wakunga
makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania mhe samia suluhu aongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha wauguzi wakunga
makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania mhe samia suluhu hassan akiwa ameshika bendera ya taifa kabla ya kuaza kwa matembezi hayo akiwa na waziri wa afya mhe ummy mwalimu
makamu wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania mhe samia ssuluhu hassan leo ameongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha wauguzi wakunga matembezi hayo ya kilometa 45 yalianzia kwenye viwanja vya green grounds oysterbay jijini dar es salaam
makamu wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania mhe samia ssuluhu hassan leo ameongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha wauguzi wakunga matembezi hayo ya kilometa 45 yalianzia kwenye viwanja vya green grounds oysterbay jijini dar es salaam (picha na ofisi ya makamu wa rais)
makamu wa rais wa jamhuri ya muungani wa tanzania mheshimiwa samia suluhu hassan leo ameshiriki katika matembezi ya hisani ya kilomita nne na nusu yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga
akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza katika viwanja vya green ground oysterbay mara baada ya matembezi hayo makamu wa rais alisema takwimu za vifo vya kina mama zimeongezeka hivyo wazo la kusaida kuongeza idadi ya wakunga ambao watasaidia kupunguza vifo hivyo ni zuri sana
makamu wa rais alisema nimefarijika kusikia kuwa mwaka 2016 matembezi haya ya hisani yalikusanya wastani wa shilingi milioni 290 pesa ambayo iliwekwa
katika fungu la kusomesha wauguzi wakunga wapya 75 katika mafunzo ya ngazi ya cheti makamu wa rais alionesha kufurahishwa na malengo yaliyowekwa kwa miaka miwili ijayo ya kukusanya kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya kusomesha wakunga wauguzi 400 katika ngazi ya cheti na diploma kwas njia ya masafa
makamu wa rais alisisitiza kuwa moja ya chanzo cha vifo vya kina mama na watoto wakati wa kujifungua ni ukosefu wa wataalam wa kuwahudumia takwimu za tanzania zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya akina mama hawaendi kujifungua katika vituo vyetu vya kutolea huduma kutokana na kukosekana kwa wataalam wa kuwahudumia akina mama hao
makamu wa rais aliwahakikishia wadau wote wa sekta ya afya kwamba serikali ipo nao bega kwa bega katika kuhakikisha wanaotaka kuwekeza katika sekta hii wanafanikisha malengo yao aidha alisema serikali inaendeleza juhudi za kuinua uchumi kwa kuongeza idadi ya viwanda ikiwa ni pamoja na viwanda vya kutengeneza dawa na vifaa tiba ili kuongeza upatikanaji na uboreshaji wa huduma muhimu za afya kwa binadamu
makamu wa rais aliiagiza wizara ya afya iusimamie kikamilifu mwongozo unaotaka kila kifo cha mama na mtoto kinachotokana na matatizo ya uzazi kijadiliwe ndani ya saa 24 katika kituo au hospitali husika kwa lengo la kubaini chimbuko la kifo hicho na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kuboresha zaidi huduma zinazotolewa katika kituo husika
makamu wa rais aliwashukuru wadau wahisani na wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye matembezi hayo na kuwaomba kuendelea kushiriki na kuchangia fedha kwa ajili ya kusomesha wakunga wauguzi | 2018-10-15T17:32:55 | http://www.zanzinews.com/2017/11/makamu-wa-rais-wa-jamuhuri-ya-muungano.html |
njaa kikwazo cha elimu shule za msingi mbeya mwananchi
njaa kikwazo cha elimu shule za msingi mbeya
inakaribia majira ya saa saba mchana katika shule ya msingi madaraka iliyopo tukuyu wilaya ya rungwe mbeya mwalimu ezron kyejo anamuuliza mmoja wa wanafunzi wa darasa la nne tatu mara tatu ni ngapi mwanafunzi hajibu chochote anakaa kimya
by sauli giliard mwananchi
muda huo wanafunzi wanaonekana kutokuwa na umakini katika somo la hisabati wanaonekana kudhoofika na kuchoka hasa ikizingatiwa kuwa hawajaweka chochote tumboni tangu asubuhi
kwa mujibu wa ratiba ya shule muda huo wanafunzi wanapaswa kurudi nyumbani kwa ajili ya kupata chakula cha mchana kabla ya kurudi shuleni saa nane mchana kwa ajili ya kuendelea na masomo lakini leo mwalimu kyejo alichelewa kidogo kuwaruhusu
baada ya kubaini hali hiyo mwalimu huyo anawaruhusu wanafunzi waende kujitafutia chochote kwa ajili ya kuupa mwili nguvu baadhi ya wanafunzi waliondoka wengine walibaki katika maeneo ya shuleni ili kuwasubiri wenzao kwa ajili ya vipindi vya mchana
samuel festo ni miongoni mwa wanafunzi wa darasa la saba ambao hawakwenda nyumbani kwa ajili ya kupata chakula cha mchana anasema nyumbani kwetu ni mbali siwezi kwenda na kurudi hapa kuendelea na masomo
iwapo festo angeweza kwenda nyumbani angepata chochote cha kula kwa wengine hali ni tofauti
hata nikienda nyumbani nitapata nini kule sipati kitu ni bora nibaki hapa (shuleni) hadi jioni anasema isaya peter mwanafunzi mwingine
wengine wanaomudu kufika majumbani mwao siyo kana wote kwamba wanakuta chakula kipo mezani ili wale na kuwahi kurudi shuleni kuendelea na masomo wanapaswa kuingia jikoni na kujipikia japokuwa muda ni mfupi
yuster oden ni miongoni mwa wanafunzi wanaoweza kufika nyumbani mapema shukrani kwa makazi yao kuwa karibu na shule anasema kwa kuwa wazazi wanakuwa shambani sokoni ama kwenye shughuli nyingine za kujipatia kipato wanafunzi hulazimika kujipikia mara warudipo nyumbani mchana
athari ya chakula katika taaluma
kutokuwapo kwa huduma ya chakula cha mchana katika shule za msingi mkoani mbeya ni miongoni mwa sababu zinazochangia mkoa huo kushindwa kufikia lengo la taifa la ufaulu wa asilimia 80
wanafunzi wanapokuwa na njaa hawajifunzi sawasawa na hii hali ipo kila mahali ambapo wanafunzi hawapati chakula cha mchana
tunapowaruhusu wanafunzi hawa waende nyumbani kula kwa mujibu wa ratiba ya shule na kurudi saa nane wengi wanashindwa kufanya hivyo na hata uwepo wao kiakili unakuwa mdogo anasema mwalimu kyejo ambaye amefundisha kwa takribani miaka 28
mwaka 2016 shule ya madaraka ilifaulisha kwa wastani wa b na kuwa ya sita katika wilaya ya rungwe kitaifa madaraka imekuwa ya 1769 kati ya shule 8109 ambazo zilikuwa na wanafunzi zaidi ya 40 juhudi kubwa inatoka kwa walimu kwa kukubali kufundisha muda wa ziada hasa kwa madarasa ambayo yanakabiliwa na mitihani ya kitaifa
walimu katika shule hii wanasema kuwa iwapo kungekuwapo na utaratibu wa kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi shuleni hapo wanafunzi wa madaraka wangefanya vema kama ilivyo kwa shule ya msingi nuru iliyopo nje kidogo ya mji wa tukuyu inayotoa uji saa nne asubuhi na chakula cha mchana
shule ya msingi nuru
kwa mujibu wa ratiba ya shule ya nuru ifikapo saa nne asubuhi wanafunzi hunywa uji uliochanganywa na maziwa na sukari na saa saba hupata chakula cha mchana shukrani kwa utaratibu wa uchangiaji wa ada
shule hii ambayo lugha ya ufundishaji ni kiingereza ni miongoni mwa shule chache za msingi tanzania ambazo zimeruhusiwa kuendelea kutoza ada
mwalimu mkuu herbert mwambipile anasema kiasi cha fedha kinachokusanywa kinatumika kwa ajili ya uendeshaji wa shule pamoja na kugharimia chakula cha wanafunzi wakiwa shuleni
anasema kuwa siri pekee ya shule yake kufaulisha wanafunzi kwa asilimia 100 katika mtihani wa kuhitimu darasa la saba mwaka jana ni uwapo wa uji na chakula cha mchana pamoja na kuwa na walimu wanaowajibika
mbali na mafanikio hayo nuru iliongoza kwa shule za serikali kwa kuwa kuwa ya kwanza kiwilaya na mkoa wa mbeya kitaifa imekuwa ya 302 kati ya shule 8241 zenye wanafunzi chini ya 40
njaa shule za mbeya
kwa mujibu wa ofisi ya elimu ya mkoa wa mbeya shule za serikali zinazotoa chakula kwa sasa ni 32 pekee na nyingi ni za wilaya ya mbarali
hadi machi mwaka jana takwimu kwa umma (open data) zinaonyesha mkoa huu kinara katika uzalishaji wa chakula ulikuwa na shule za serikali 756
baadhi ya maofisa wa wilaya na elimu ambao hawakutaka kuweka majina yao bayana wanasema kuwa kushuka kwa idadi ya shule zitoazo chakula kumeanza mara baada ya serikali kuanza kutekeleza sera ya elimu bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari
baadhi ya walimu nao wanasema wazazi na wananchi wengi kwa ujumla hawakuelewa lengo hilo na wanajiona hawawajibiki kwa watoto wao ikiwamo kuchangia chakula shuleni
shule zetu nyingi hazitoi chakula cha mchana kwa kuwa wazazi hawachangii wanafanya hivyo tu ikiwa ni wakati wa mitihani ya kitaifa na wakati wa chanjo anathibitisha mkazi aitwaye mama hadija na kuongeza
tangu kuanza sera ya elimu bure wengi tuliamini kila kitu ikiwamo chakula lakini wazazi wengi hawana imani na walimu kwa kuhisi watachukua fedha na chakula tutakachochangia shuleni
mkoa wa mbeya bado uko nyuma ya malengo ya kitaifa wa kufaulisha kwa asilimia 80 katika ngazi ya elimu ya msingi kwa miaka mitatu mfululizo mkoa huu umeshindwa kufikia lengo jambo linalosababisha hii kuwa ajenda muhimu katika vikao vya maendeleo ya mbeya
mwaka 2014 lengo la kitaifa lilikuwa ni asilimia 70 lakini mkoa (mbeya) ulifanikiwa kufaulisha kwa asilimia 488 pekee
mwaka 2015 lengo la taifa lilikuwa ni asilimia 80 mkoa ulifaulisha asilimia 5709 na mwaka jana mbeya iliweza kufaulisha asilimia 6073 chini ya kiwango cha taifa inasomeka sehemu ya ripoti ya kamati ya ushauri ya mkoa (rcc) ya mwaka jana
japokuwa ripoti hiyo haihitaji kukosekana kwa chakula kama moja ya sababu zinazochangia kuanguka kwa elimu ya msingi mkoani mbeya mwalimu katika shule ya nuru brown kisinga anasema wataalamu katika serikali za mitaa wanapaswa kutoa elimu kwa wazazi ili kujua uhusiano kati ya kukosa chakula shuleni na matokeo mabaya
anaeleza mkoa huu una vyakula mbalimbali suala hapa ni kuwaunganisha wazazi ili wachangie chakula ikiwa tunataka watoto wetu wafanye vema katika mitihani ya darasa la nne na la saba
akizungumza na idhaa ya kiswahili ya bbc hivi karibuni waziri wa tawala za mikoa na serikali za mitaa (tamisemi) george simbachawene anasema serikali hutoa fedha za chakula kwa ajili ya shule za msingi za bweni hususani za wanafunzi wa mahitaji maalum
kuhusu shule nyingine za msingi simbachawene anasema kwa wale wanaosoma shule za kutwa za msingi na sekondari ni jukumu la mzazi kuchangia
sauligiliard@gmailcom | 2018-09-21T12:54:26 | http://www.mwananchi.co.tz/habari/Makala/Njaa-kikwazo-cha-elimu-shule-za-msingi-Mbeya/1597592-3893916-view-asAMP-8s40mvz/index.html |
home > shahidi kwa ajili ya ubinadamu > sura ya 43 matokeo yenye mafunzo > mafundisho ya kimaadili na ya kijamii ambayo yaweza kupatikana kutokana na masaibu ya karbala
ingekuwa ni kuufanyia ukatili mtazamo wa uislamu na ufahamu wake kwamba matokeo ya mhanga wa husein uonekane umefungika pekee kwenye kundi lolote lile maalum la jamii ya binadamu faida inayotiririka kutokana na mhanga wake wanaweza wakaishirikiana wale wote ambao watapenda kujifunza kutokana nayo juu ya namna wanavyoweza kujichunga katika maisha yao faida ambazo zinaongezeka kwenye dini ubinadamu na uislamu kutokana na matukio ya karbala zimetajwa hapa kwa ufupi
uyakinifu na hali ya kiroho siku zote vimekuwa katika vita baina ya vyenyewe kwa vyenyewe dini inashikilia imani ya kiroho hata sasa ingawaje imani ya kiroho haiko katika mtindo katika ulimwengu wa leo vita vya karbala vilikuwa ni vita vya dini dhidi ya uyakinifu (maslahi ya kidunia) mbali na nguvu zake kubwa mno jeshi la yazid halikuweza kukipata kwa kutumia nguvu kile kiapo walichokitamani sana kutoka kwa husein cha utii kwa ajili ya mtawala wake katika majumuisho ya mwisho ilikuwa ni husein ambaye ingawa aliuawa na kushindwa kwa muonekano wa nje ndiye aliibuka mshindi na pamoja naye ilishinda imani ya kiroho
alama moja muhimu ya ukweli wa dini ni ile subira ya kijabari na umad hubuti ambao kwamba waanzilishi wake hukabiliana na shida na dhiki na wanangangania kwenye misingi yao mpaka mwisho wa siku zao msaada uliotolewa kwenye dini yao na wafuasi wake wa kawaida wakikabiliana na dhiki kubwa kishujaa na wakijitoa mhanga maisha yao wenyewe usingeweza kuthibitisha kwa uhakika ukweli wa imani (dini) yao kwani pengine wangeweza kuwa wamedanganywa au walikuwa pengine hawau tambui ukweli wenyewe lakini kama mwanzilishi wa dini wasiri wake na watu wa familia yake ambao ni wajuzi wa ndani wa siri za maisha yake binafsi na kwa undani wa karibu sana wameizoea hali ya maadili yake na sifa zake nyingine wanakubali kukabiliana na mitihani katika kuunga mkono kanuni na misingi yake na kama ni lazima kuyatoa maisha yao (kufa) katika kuthibitisha uhalali wa kanuni za dini yake ukweli wa misingi yake bila shaka yeyote utakuwa umethibitika
pamoja na alhusein wapenzi na wafuasi wake wote na pia ndugu zake walijitoa mhanga maisha yao baada ya kupata mateso makali sana na ukandamizwaji
mhanga wa husein haukumpata kwa kimya kimya aliendelea taratibu kuwalingania watu kwenye uislamu wa kweli na halisi katika tarehe 9 ya muharram wakati adui aliposonga mbele dhidi ya husein wakati wa jioni bila ya kutanguliwa tangazo kabla aliomba kusimamishwa mapigano kwa usiku mmoja ili kwa usiku mmoja ili utumike tu katika maombi yake mwisho na sala kwa mwenyezi mungu husein na wafuasi wake waliutenga usiku wote kwa lengo ambalo mapatano ya kusimamishwa vita yalikuwa yamekusudiwa katika kufanya hivyo walionyesha na kuthibitisha kwamba katika hali za mitihani mikali sana kanuni na misingi ya dini lazima izingatiwe na kwamba nguvu za kiroho ni bora kuliko nguvu zote za kilimwengu
bado hali ngumu zaidi ya mazingira ilikuwepo wakati siku ya tarehe 10 ya muharram husein alipoongoza sala za mchana ndani ya uwanja wa vita katika mfululizo wa mishale baada ya watu wengi wa kundi lake dogo walipokwishauawa
haya yalikuwa maonyesho dhahiri ya ukweli wa mafundisho ya kiislam ambayo yaliujaza ulimwengu kwa wito wa uzinduzi wa haki uliamsha dhamira ya waislamu na kufichua ukatili wa yazid na uadui wake kwa uislamu
kila mtu wa kundi la husein alikuwa kama mhubiri mashindano ya burayr na yazid bin maqil na kuomba laana za mwenyezi mungu ishuke juu ya yeyote yule kati yao aliyesema uwongo na khutuba za zuhayr bin alqayn zinaweza kutolewa kutoka miongoni mwa idadi kubwa sana ya mifano ambayo ndani yake wapenzi wa husein walizifafanua sababu ambazo zilimshawishi husein kuchukua mwenendo ambao aliuchukua haina umuhimu kwamba jitihada hizi hazikuleta mafanikio ya haraka kwani kazi ya mhubiri inahusu tu kuwaita watu kwenye kweli ya ujumbe wake hata katika mazingira yenye kuvunja moyo kabisa
sawia pamoja na kuwa ni yenye kusikitisha kupita kiasi matukio ya karbala si yenye kuleta maomboleza pekee yanaelekeza na kubadilisha ili kuupandisha uhai wa binaadamu katika daraja za juu sana za rehema na uchamungu baadhi ya mafundisho makuu ya matukio ya karbala yametajwa na kuelezewa kwa ufupi chini ya vichwa vya habari vifuatavyo
uhuru uhuru maana yake ni kuwa huru wa kutenda kwa mujibu wa inavyoamua dhamira ya mtu bila ya kizuizi chochote kile miongoni mwa vizuizi kwenye uhuru wa kutenda ni mapenzi ya mtu juu ya starehe na vitu ambavyo starehe zinazoendelea umehatarishwa kwa kufuata maamuru ya dhamira ya mtu ukombozi kutokana na tamaa unakataa katakata nguvu zote za kidunia za kumfanya mtu mtumwa kwa kutenda kwa mujibu wa mwongozo wa dhamira yake husein alionyesha kujikomboa kwake kutokana na matamanio katika hali za taabu na dhiki zenye kutisha mno
kwa mujibu wa umuhimu ambao jitihada ya husein zilitoa kwenye uhuru raia wa nchi huru kwa kweli ni watumwa kama watafuata mambo maovu kwa upande mwingine raia wa nchi iliyofanywa utumwa wako huru kama mbali na kuteseka kwa ukandamizaji wanafuata haki na kumwabudu mwenyezi mungu
uimara ni uimara kama tu katika kufuata njia ngumu na ya hatari katika vitendo mtu kamwe hatasita wala kukwepa na atadumisha utulivu wake na ushwari katika kuzimiliki sifa hizi mashahidi wa karbala wanachukua nafasi ya mbele kabisa
husein alikuwa amekataa kuapa kiapo cha utii kwa yazid baada ya kuchunguza undani wa roho yake na baada ya kupima katika sehemu ya ndani kabisa ya akili yake zile hatari za hali hiyo na baada ya kujiridhisha mwenyewe kwamba kwa ukubwa wowote ule wa makali ya mateso yake utakaoweza kutokeza umadhubuti wa uamuzi wake usingetikisika wasaidizi wote wa husein hapo karbala pamoja na watoto walisimama imara katika kuupa athari upinzani uliodhamiriwa na husein kwa yazid
katika safari ya husein kwenda kufa alhurr alikuwa amekutana naye na akiyatabiri mauaji ya husein kama akishikilia kufuata mwelekeo wake wa kwenda kufa alimwomba ajionee huruma mwenyewe na auache mpango wake husein alijibu kwamba kifo kilikuwa si kitu kama mtu atakuwa amesimama katika haki hivi ndivyo ali alakbar bin husein alivyowahi kueleza
maadui wa husein waliijua nguvu ya azma yake mnamo siku ya tarehe 9 ya muharram umar bin sad alipokea barua ya ibn ziyad ikimuelekeza kwamba ni lazima apate kutoka kwa husein kiapo cha utii kwa yazid bila ya masharti au ampige vita umar bin sad mara moja akasema husein kamwe hawezi kukubali kwa namna hii roho ya baba yake inadunda ndani ya kifua chake na kila mtu aliona kwamba husein kama ukingo wa uimara na umadhubuti alihimili gharika za mateso na maumivu ambayo yalikuwa yamemzunguka katika medani ya vitaku | 2015-11-25T21:39:35 | http://www.al-islam.org/sw/print/book/export/html/25363 |
lago di garda (tischkalender 2018 din a5 quer) 9783665725785 kununua kitabu
home > utafutaji > 9783665725785
vitabu vyote kwa 9783665725785 linganisha kila kutoa
9783665725785 () au 366572578x
isbn (kuweka mbadala) 366572578x 9783665725785
kupata vitabu vyote inapatikana kwa namba yako isbn 9783665725785 linganisha bei haraka na kwa urahisi na kuagiza mara moja
inapatikana nadra vitabu vitabu kutumika na mkono wa pili vitabu vya kichwa lago di garda (tischkalender 2018 din a5 quer) gardasee im august 2011 (monatskalender 14 seiten ) kutoka konrad diebler zimeorodheshwa kabisa | 2017-10-22T13:43:22 | https://ke-sw.diebuchsuche.com/vitabu-isbn-9783665725785.html |
wasomi watoa maoni kuhusu epa ministry of foreign affairs and east african cooperation
dodoma 12 aprili 2019
tanzania imeshauriwa kufanya tathmini ya kina kuhusu faida na hasara za kusaini mkataba wa ubia wa kiuchumi kati ya jumuiya ya afrika mashariki (eac) na umoja wa ulaya (eu) unaojulikana kwa kifupi epaushauri huo umetolewa na mbobezi wa masuala ya uchumi na mtangamano wa kikanda kutoka ujerumani prof helmut asche alipokuwa anatoa muhadhara kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha dodoma (udom) kuhusu changamoto za kutekeleza mkataba wa epa muhadhara huo umeratibiwa kwa ushirikiano kati ya wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa afrika mashariki na udom ulifanyika tarehe 12 aprili 2019 | 2019-06-26T23:07:09 | http://www.foreign.go.tz/index.php/resources/view/wasomi-watoa-maoni-kuhusu-epa-1 |
ni somo gani kubwa maisha yamekufundisha ~ mwalimu makoba commented)if(n_rc==true){documentwrite( on +b)}documentwrite( )if(jlength)documentwrite(j)documentwrite(
ni somo gani kubwa maisha yamekufundisha
nilikuwa katika kiota cha burudani humo nilikwenda kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa rafiki yangu mmoja ambaye tumefahamiana kwa miaka dahari katika meza niliyokaa tulikaa wawili mimi na dada mmoja ambaye hatukuwahi kuonana kabla hata hivyo haikuchukua muda kufahamiana na kuanzisha mazungumzo
wakati sherehe ikiendelea dada aliniuliza swali mwalimu makoba ni somo gani kubwa maisha yamekufundisha
nilitafakari kidogo kisha nikajibu
nimejifunza kwamba hakuna njia ya mkato katika maisha
watu wenye miili mizuri isiyo na vitambi wala unene kupitiliza wanastahili siyo uchawi wamefanikiwa kwa maamuzi waliyofanya ikiwemo kupangilia mlo na kufanya mazoezi
watu wenye mafanikio wanastahili mafanikio hayaji kwa bahati tena hayatokei kwa usiku mmoja wamefanikiwa kwa sababu waliamua kufanikiwa
nilimaliza kuzungumza nikabaki kusikiliza mziki na kusukuma mafunda kadhaa ya kinywaji nilichopewa nilimsikia dada akirudia maneno niliyosema
hakuna njia ya mkato katika maisha | 2020-05-25T05:30:08 | https://www.mwalimumakoba.co.tz/2020/04/ni-somo-gani-kubwa-maisha-yamekufundisha.html |
mtwara kumekucha mbunge matatani adaiwa kukibaka kitoto cha miaka 16 na kukiambukiza vvu
mbunge matatani adaiwa kukibaka kitoto cha miaka 16 na kukiambukiza vvu
kutoka gazeti la tanzania daima
hata hivyo baada ya kuhisi kuwa watoto hao wamedhamiria kumchukulia hatua na wamewasiliana na taasisi mbalimbali za kiraia na serikali zenye uwezo wa kumtia adabu mbunge huyo alimtumia mtoto huyo ujumbe wa kuonyesha alikuwa anafikiria kunywa sumu
na kapuya aliwapigia simu kuwaarifu kuwa amempa zawadi ya gari kwa ajili ya matumizi ila yeye na dada yake wanaruhusiwa kuuza ili wapate pesa kwa ajili ya mahitaji yake siku zilizosalia kwani muda sio mrefu baada ya uchguzi mkuu 2015 kapuya atakuwa waziri mkuu hivyo itakuwa ngumu yeye kumtumia huyo binti pesa kama alivyoelekezwa na jeshi la polisi kituo cha oysterbay
posted by baraka mfunguo at thursday november 14 2013
january came in july
waziri lukuvi azindua rasmi bodi ya wakurugenzi ya shirika la nyumba la taifa jijini dodoma
benki ya maendeleo ya afrikaafdb kulig'arisha jiji la dodoma kwa barabara za kisasa huduma za jamii
ziara ya makamu wa pili wa rais zanzibar balozi seif yaja na neema kwa wakulima wa tumbaku kahama
fearless bachela mbili ft key (official video) mistari iliyoenda shule
master's scholarship in uk (chevening scholarship) deadline november 5 2019 (no toefl or ielts requirement at the time of application)
kwa nini ni vigumu sana kupata a katika vyuo vyetu tunawahujumu wanafunzi wetu
jiji la arusha lasaini mkataba mdogo na kampuni ya china mradi ujenzi wa barabara
miss tanzania kupatikana agosti 23 mwaka huu mwanukuzi atoa neno
kwaya ya injili family toka drc waendelea kuwepo nchini tanzania (+video)
mkuu wa wilaya kasesela asuluhisha mgogoro wa ardhi iringa | 2019-08-21T04:46:11 | http://mtwarakumekucha.blogspot.com/2013/11/mbunge-matatani-adaiwa-kukibaka-kitoto.html |
36 824 697
karibu ngasa tv ujipatie habari mpya kila siku za ukweli na uhakika
hakikisha ume subscribe kwenye channel hii
kauli ya kwanza ya rais magufuli kwa harmonize
bila uoga rc makonda avujisha siri mbele ya jpm
views 18114 hours ago
tundu lissu atajwa na rais magufuli kisa hiki hapa
views 92014 hours ago
tazama tukio hili wakati msafara wa rais magufuli ukiondoka
views 1k14 hours ago
mama samia afunguka rais wa afrika ya kusini alivyozomewa zimbabwe kwenye msiba wa mugabe
ukistaajabu ya musa utaona ya mbunge tajiri kuliko wote / naendaga kwake na baiskeli
mbunge tajiri asiyejulikana / nyumba ya nyasi baiskeli na daladala ndio usafiri wake
ben pol azungukwa na polisi dodoma afunguka haya
tamko la jukwaa la sera kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa 2019
kangi lugola ashindwa kuvumilia afanya tukio hili tena hakikisheni hakuna wizi
habari kubwa iliyotufikia jumapili ya leo ikimuhusu waziri mkuu
hii ni nzito rais ramaphosa azomewa zimbabweaomba msamaha
usiku huu alichokisema mkuu wa majeshi mbele ya rais magufuli
mbunge chikota aibana serikali bungeni kuhusu korosho
waziri mpango asikitishwa atoa maagizo mazito kwa benki zote ni hatari
cheki ulinzi wa waziri mkuu kwenye msafara wake ni hatari
kauli ya waziri mkuu bungeni baada ya will smith kuja tanzania
breakingwaziri ummy akanusha taarifa hizi zinasosambazwa kwenye mitandao kuhusu ugonjwa huu hatari
jumamosi ya leo hii ndi habari kubwa kuhusu mbunge huyu alichokifanya bungeni
views 9492 days ago
ajali za moto za muibua kangi lugola atema cheche kwa zimamotokushangaa shangaa tu
views 3263 days ago
sakata la ndege laibukia bungeniwaziri mkuu atoa neno
views 8303 days ago
kubwa kutoka kwa mbunge ngeleja kwenda kwa mwanasheria mkuu wa serikali
utani wa spika kwa wabunge baada ya waziri mkuu kusema 'yanga timu ya wananchi'
musukuma ajisifia mbele ya waziri kuandamana mpaka kuweka ndani
rais magufuli atoa maagizo mazito kwa wanajeshi hawa
inasikitisha sana ndoa ya mateso ilivyomtesa mama huyu wa dodoma
views 3934 days ago
kishindo mtihani darasa la saba/ wanafunzi wamshukuru mpina kwa hili
jioni hii taarifa nzito iliyotufikia kutoka takukuru
wanawake wafunguliwa macho / siku hizi hakuna kutoa rushwa fatma toufiq
views 3364 days ago
musiba apewa onyo kali na lugola / jeshi la polisi laagizwa
dk bashiru anena mazito anaweza kugombea hata urais
walinzi wa rais walivyokimbiza gari wakati rais analitest
kilichotokea baada ya mbunge vulu alivyosimama bungeni leo
naibu spika tulia unasababu gani kusema maneno ya ovyo
views 2574 days ago
cheche za mrithi wa lissu mbele ya spika ndugai /waziri atoa majibu
tccia waiangukia serikali ya rais magufuli watoa ombi zito
spika ''alivyomzuia'' waziri mkuu kujibu swali
views 8304 days ago
mbunge kiula amkaba koo waziri ataka kauli ya serikali
mbunge wa ccm amwambia naibu spika mimi mwenyewe nilikua mpinzani
views 3554 days ago
''nilimpigia magoti shabiby \ nilitaka kukatwa mguu '''
views 7094 days ago
ndoa ya mateso ''nilipigwa ngumi moja nikalazwa icu mwaka mzima''
cheche za balozi kagasheki unaweza ukashika mdomo / hujajiumba wewe
tazama alichokisema mbunge njeza baada ya kusimama bungeni
waziri mkuu atoa kauli kuhusu kilio cha wakulima wa pamba
spika atoa rasmi taarifa ya msiba huu /alikuwa na mchango mkubwa
mbunge fatma toufiq afunguka mambo muhimu mazito
tazama rais alivyokamatia stelingi ya gari la jeshi
mbunge shangazi asikitishwa sana amwambia waziri mkuulimetokea tatizo kubwa sana
spika atangaza taarifa mbaya bungeni / amejinyonga
brakingmbunge mwingine aibuka bungeni aomba msamaha serikali ya jpm
breaking news ikulu boss mpya wa usalama akiapishwa na rais
boda boda 20 waliofanya fujo kwa muroto sasa wanajutia fujo zao
views 9574 days ago
spika ndugai atoa kauli kuhusu nape nnauye /makamba na ngeleja
mchana huu taarifa nyingine kutoka ikulu rais magufuli kashafanya maamuzi
bungeniwaziri mkuu kikaangoni maswali ya papo kwa hapo
spika atema cheche bungeni amjia juu mbunge mtolea baada ya kumuuliza waziri mkuu swali hii
naibu waziri kijaji alivyotoa taarifa hii bungeni ''si jambo baya''
rc kagera marco gaguti ashukiwa na neema kubwa sana
hussein bashe azidi kwenda na kasi ya magufuli afanya tukio kubwa zaidi
musukuma avaana na kamwelwe bungeni ''leo ni mara ya tatu namwambia''
nabii ashika kichwa baada ya kubanwa kutoa password ya simu kimiujiza
sakata la mtoto aliyekatwa mkono kimbembe chaibuka /n waziri aliamsha dude
mkataba mzito wa tano umesainiwa na katibu mkuu wizara ya afya
views 1275 days ago
waziri lukuvi aibuka na habari njema / hii inafurahisha sana
usiku huu taarifa kutoka ikulu rais magufuli afanya maamuzi mengine
''nikijisikia najirekodi / kama ni ushamba makonda naye' prophet shillah
nape nnauye gumzo kila kona / chozi lake halijapotea bure
views 2195 days ago
gumzo laibuka siri nzito ya kifo cha mugabefamilia yafichua
bashe aleta balaa bungeni leo ni mwendo wa hesabu tu
ufafanuzi wa maana ya neno mabahari
views 7996 days ago
habari kubwa leo kuhusu rais magufuli baada ya kuibuka huku
tazama kilichowakuta wafanyabiashara 10 wahujumu uchumi
views 8096 days ago
mbunge acharuka kibabe bungeni / tunawafanya wakimbizi kwenye nchi yao
shujaa nape nnauye alivyosimama leo bungeni baada ya kutoka ikulu jana
tamko la viongozi wa dini kuhusu mtihani wa darasa la saba leo
views 2496 days ago
taarifa nzito iliyotufika kutoka kwa mkuu wa majeshi atangaza jambo hili
habari kubwa iliyotufikia asubuhi kutoka bungeni kwenye maswali na majibu
breakingbaada ya kumuomba msamaha rais nape afunguka ya moyoni
waziri aliyeteuliwa na magufuli alivyotinga bungeniaanza na hili
views 9166 days ago
rais baada ya kuibuka gafla kituo cha polisi kwa kushtukiza
usiku huu taarifa ikufikie kuhusu ajali nyingine ya moto
watu 9 wafukiwa na kifusi mmoja afarikikamanda afunguka
mbunge wa babati mjini pauline gekuli alivyosimama bungeni leo
jioni hii tumepokea taarifa nzito iliyotufikia kutoka necta
mbunge abood amkaba koo waziri bungeni ''tunataka kujua''
views 4626 days ago
breaking nape ajitosa atinga ikulu kuomba msamahajpm amsamehe
duuhhasira za hussein bashe bungenihili jambo haliwezekani
maagizo mazito ya katibu mkuu cwt kwa wasimamizi wa mitihani darasa la 7
views 3346 days ago
kimenukaumaamuzi ya waziri kugola kwa baa zinazokesha kupiga muziki usiku mzima
mbunge alivyoangua kilio baada ya kufanyiwa tukio hili la kushangaza
taarifa kubwa iliyotufikia muda huu kutoka takwimu kuhusu mfumuko wa bei
views 1097 days ago
spika ndugai alivyompa somo mbunge wa uinzani bungeni leo
mbunge wa zanzibar aliavyoliamsha bunge leo usipime
views 3357 days ago
moto wa mbunge mlinga bungeni hauzimi ni balaa tupu/ataka kauli ya serikali
views 8177 days ago
spika ndugai '' hata mtambike vipi hamwezi kumfikia huyu mzee''
baada ya rais magufuli kupendekeza jina mbunge kiruswa atia neno
breakingbaada ya maamuzi ya mahakama kesi ya lissu spika atia nenoujeuri tu
waziri kigwangala afunguka kuhusu azimio la ubadilishaji pori la selous
mbunge mabula haipendezi na wala haifuraishi ucheleweshaji huu
mauaji yanayoendelea afrika kusini spika ndugai akasirishwa atoa neno
sakata la ndege laibukia bungenimbunge mlinga aibua mazito amtaja zitto kabwe
mangson samson 9 minutes ago
namuomba mungu amuongezee rais wetu hekima na busara naona kapungukiwa kwa kilichompata lissu huwez kusema aliterekeza jumbo hata kidogo hata kama yangempata yy angeenda nje kutibiwa je na yy angekuwa ameterekeza nchi
mangson samson 14 minutes ago
wanyonge wanaotajwa ni wale wanaoendesha magar mazur na mishahara minono ya serikali kwa wale wasakatonge hakuna kitu
tumaini temu 18 minutes ago
bugumba deus 48 minutes ago
kuna tukio gan sasa hapomnamalza mb za bure
lameck mtaka hour ago
kwa kauli kama hizi tunaamini shambulio la lisu serikali ina husika 100
utukufu eliya hour ago
huyu jamaa amewahi kumiliki meli ziwa victoria aseme yote
saidi kabuta 3 hours ago
chedema mulipitushwa na makamba musingeweza
witness msigwa 3 hours ago
nakumbuka 2012
lameck mtaka 3 hours ago
mkipata rais akiwa wakala wa wa shetani taifa lina yumba
jumanne said 3 hours ago
wanyoge tumekoma daa juwa hadi mfukoni kwer wanyong
bernard ndemba hour ago
kafanye kazi kuwa mbunifu utapata pesa
michael malima 2 hours ago
fanya kazi utapata pesa
gigo tz 4 hours ago
huyo dda hatanawa wki nzima
simon prosperity 4 hours ago
hamjambohatujambo duhhata 1 wa kumpa heshima yake kakosa hata we mama
frank minja 4 hours ago
wahuni nyie
joseph ndaki 4 hours ago
dawa bure mmh am not sure
juma igoti 4 hours ago
vizuri sana msahau kwao ni mtumwa
hanlack shabani 4 hours ago
hakuna mwana siasa wakweli na mtetezi wa wanyoonge kama zitto luyagwa
godfrey kirway 4 hours ago
great ramaphosa shouldn't say bad things too much on his safrican's candidatesbcoz he needs more times of presidency in his country
anuary ally 5 hours ago
mama samia ondoka na siketi ndefu vibuga vya nini mamaa nakuomba mamaa
fatuma nditi 6 hours ago
wadodoma wote piga keleleeeeee nakukubali ben p
simon hussle6 7 hours ago
ongela san
luinda mchwa kanigee 8 hours ago
nimekuelewa mzee
mtahima mussa 8 hours ago
mheshimiwa uko vzr
simon thedon 8 hours ago
ameni impress hapo
onesmo akwilini 8 hours ago
pumba zote
peter martin 9 hours ago
look who is talking aliyeitafuna tanzania na kuiacha mifupa mitupu ni nani aliyejiuzia mgodi ni nani tukisema makosa waliyoyafanya oh munawadhalilisha wastaafu makosa waliyoyafanya yasinyamaziwe lazima yakumbushwe ili yasijirudie tena nchi za kiafrika zinadharirika kwa uongozi mbaya selfish leaders that is what we have wakiuguwa ulaya watoto wao kusoma ulaya pesa za wote zinakuwa zikitumiwa na watu wachache rais magufuli ameleta mapinduzi makubwa na watanzania wanayaona
shaban mohamed 3 hours ago
kama nakuelewaavileee
said njukute 10 hours ago
uko pouh ben
tecno kitkat 17 hours ago
pambambana na msiba hon
maneno clais 17 hours ago
hii channel ya kifala sana hapo wapi sasa au mnajua kuandika caption tu
muba hassan 18 hours ago
unatafuta kiki kwa kupitia musiba
getaro magaiwa 18 hours ago
wewe ndie waziri yule mwingine ni mdori
masukuzi bakari 18 hours ago
steven mdoe 19 hours ago
watu wanaomba serikal kwakuwa ndio inayokusanya kodi
captenn dunga 20 hours ago
kwanza unatakiwa ujue maana ya mwanaharakati bila kulijua hilo utafeli huyo rais alokupa hiyo kazi mwenyewe ni mwanaharakati kwahiyo ujue kutofautisha harakati na siasa we ni mwanasiasa usingeweza kumsamehe hata nape
prisca mbwambo 20 hours ago
hana jipya mnafki mkubwa kajisemesha hana uwezo wa kuwa kiongozi kama akina michael jakison wir the walold wir the childrn bob marle akaimba one love one heart let as get together and feel alright lucky dube akaimba different colour one people na akakemea sana mtu anaeleta ubaguzi nyimbo zote zilikuwa zinaukemea ubaguzi wa rangi leo hii mwafrika na mwafrika ngozi moja wanauana wanawaitavwengine foreigner hawa niliowataja wangekuwa hai wangekuwa na hasira sana na nchi ya southi afrika ujumbe kwa ramaphosa you have to teech your jungpeople your histori you have to tell them and they have to know who their period
keneth japhet 20 hours ago
sawa nimekuelewa mzalendo wetu ben pol
saimon matonya 20 hours ago
nahene wawaha
mama chris 20 hours ago
pandidha key kidogo huyo mama ana key ya juu
adam liundi 20 hours ago
halehaleeeeee
yuzo matinted 20 hours ago
baho nelowa havaha mno
shawwali kingungo 21 hour ago
yani inashangaza sana ht makampuni binafsi yanahuluma na wanainchi wanaofia bahresa ansafilisha mait nawasindikizaji 2 bule kuna baazi ya benk zinawasamee madeni watu waliokufa
juma kapesa 21 hour ago
safi sana mh spika kwa ushauri na mafunzo mh sugu zingatia
polo alawi 22 hours ago
shida yake ni kutishia au tutafuta njia nyingine maelezo yake siyo mabaya lakini siyo kutishia maneno
suleiman bakar 22 hours ago
hanna lolote
kwetu huku tandahimba ni asilimia 40
nasser alhabsi day ago
wengi tulifikiri kuna mwana siasa kajinyonga 😣
edward msongelwa day ago
kama nimekuelewa hali mashauri kukusanya nguvu ni kodi mbali mbali ambazo zilikua zikiliwa bila muangalizi na watu kuto jali hata kuwakilisha pesa hizo serikari ni mlishidwa kusimamia katiba mpya kwa nini hmkuitilia mkazo kwenye vipindi vyenu mliogopa mini sasa mko nnje mnaipigia debe hameleweki mimi nakubaliana na jpm nyinyi mliamini kila mliempa jukumu mlifikiri atalifanya bila kufatiliwa ni koda kubwa mlituongoza kwa rimot hamkutujalu nchi yetu ika didimia kuibia serikari ikawa ni rukusa rushwa waziwazi madawa hakuna ni taabu tupu nyinyi mpo acheni kujaribu kumdhofisha jpm muacheni amalize aweke record sawa sawa atakae kuna atapata mtelemko hii katiba abayo hawa wanao ililia ipi mifano ya wazi wanao waonyesha watanzania kwa katiba hiyo tinge fanya mengi kwani mamolioni wana pesa na serikari instead wana shindana kula hizo pesa kama walivyo zoea muacheni jpm we don't see no need of a new construction for now till further notice
rama mtetu day ago
zomea zomea afrika inasikitisha kuona tunauana kwa kugombea ugali na maharagwe cha kusikitisha ni wageni wenye rangi nyeusi tu ndio wanaopata hii shida ila mungu awasamehe wa south africa nasi tuwasamehe pia
cherily david day ago
point ni nini hapa kuhusu mwanafunzi kujinyonga mmeonya waalimu na kutoa kodi za pedi vinginevyo haieleweki sababu ya kuzungumzia hichi kisa bungeni
cherily david 18 hours ago
@makongoro wassira ni mpaka mtoto ajinyonge kwani hiyo elimu haikuwepo basi ni negligence ya hali ya juu mno wabunge wako wangapi ina maana hawana watoto wakike sijamsikia akitamka kutoa kodi ya pedi
makongoro wassira 19 hours ago
cherily david sikiliza vizuri ndugu yangu kaongea vizuri kuwa kwe na elimu mashuleni kuhusiana na hilo swala la watoto kike kufikia hedhi
j fk day ago
hilo la kutokujituma kukusanya nguvu ni changamoto kubwa tunapenda kuomba sana
teresea masawe day ago
magufuli oyeeeeeeeeeeeeee
gervasi njawi day ago
kangi ametumia cheo chake kujilinda kisiasa kwenye jimbo lake zidi ya msiba sisi tunamuelewa msiba kazi anayo fanya ni ya kizalendo
lugola kazi ya uwazi imekushinda kabisamagufuli rais wetu mtumbue huyu lugola hatufai ni mchochezi
justine chacha day ago
waandishi uchwara headings zingine vituko
hercules the power day ago
nyiye always mnashtuka ktk hali mbaya hili jambo limeongelewa sana bungeni na ktk mitandaoni lkn sijui kama mlitilia mahanani kwa kutaka kuongeza kodi sasa imetokea msichana kujinyonga ndiyo mnakuja kwa sauti ya huruma kabisa
hercules the power hata swala sio kodi unaweza kupunguza kodi na bei ikawa juu tu cha muhimu ni kuhakikisha watoto wa kike wanapewa au wanawezeshwa kumudu upatikanaji wa hizo pedi unaweza punguzq kodi na wafanyabiashara ndo wakanufaika tu kwenye mchakato mzima hivyo ni bora hata ikiwezekana wapewe hizo pedi directly au wapewe hela za ununuzi wake
mama yangu day ago
naam ✔️ ✔️ ✔️
juma igoti day ago
wewe sio kiongozi achia ngazi au tukuazime magufuri akunyoshee hiyo nchi yako ni wiki watakuwa wamenyooka au huna jeshi
groun green day ago
julius lubega day ago
sasa hapo makofi ya nini taarifa ya kujinyonga mnapiga makofi kweli🙆🙆🙆🙆
happy msaki 12 hours ago
sophie kido day ago
makofi ya pongezi kwa sugu kuoa
faida masegeng'he day ago
asituzuge sisi siyo watoto ataziludisha roho za watu walio kufa huko kwake
beatus rwegoshora day ago
i'm stranded☺☺
di gates mwanafunzi day ago
hata jinsi anavyo toa kauli zake unamuona kama ni mtu asie kua na msimamo ameshindwa kamata wanao muujumu na kuzoofisha rais anamvamia musiba kazi ya musiba imeonekana ila lugola yuko hovyo sana hovyo sana wewe lugola ndege imekamatwa hukufanya chochote rais katukanwa hujafanya lolote tundu kapigwa lisasi hujafanya lolote watanzania wameungua hujafanya lolote wa piga dili wanazidizi kujigamba huku wakisumbua wana nchi hufanyi lolote mo katekwa hujafanya lolote bora sirro kuliko wewe haujamsaidia rais lolote kwatarifaa yako 2020 kazima utumbulie usimtumie musiba ili ufute makosa yako wa tzania siwajinga
jacob makono day ago
lugola you'd just kept quiet mimi binafsi nilijua musiba anatumiwa na serikalisasa kama leo unathibitisha musiba hatumwi na serikali then musiba is right
dennis stafford day ago
ziara wapi kwenu mtwara two terms umeenda mara mbili mtu anayewafikia wananchi ni jpm pekee
mussa abdalla day ago
tupalaiki zamana
deogratius timoth day ago
nakuona mh rais mstaaf
polo alawi day ago
sawa kabisa lakini kuwa na tozo ambayo serikali hipange siyo wao wanafanya huwamuzi kiasi gani watoze nchi za west serikali zoo ndo zina panga asilimia ngapi siyo private in canada anything you buy ni 13 percent on top of price and banks they charge up 19 percent or less hill hupate customer
erick chitumbi day ago
kweli raisi alisema hataki siasa kwenye maisha ya watzsasa bado hajaeleweka
martine sizya day ago
ww unataka kufukua makaburi ya watu utakspomkamata musiba itabidi apelekwe mahakamani sasa unategemea nini musiba akileta full document za hao mafisadi unaowakumbatia unafikiri watatoka hao inaonekana ww unafurahia rais anavotukanwa na kukashifiwa umemshindwa mwanamke mange utamuweza wp mwanamume musiba nadhani jpm aangalie upya hili nalo ni jipu aka timu membe
unaweza ukasoma ukakosa maalifa lugola jipange upya umebugi hapo
amoni mbise day ago
musiba hajawai kusema kama anatumwa na mtu ili la kutumwa hii kauli ya kusema anatumwa mheshimiwa umelitoa kutoka wapi
jafari bori day ago
kuvuka mipaka ni kutukana na kuvunja sheria je nikipengelekipi musiba kakenguka
anthony kilosa day ago
jeshi raha sana
mariam mstapha mariam mstapha day ago
saf sana mkuu
theresia ngunda day ago
safi sana jpm
zakia zakia day ago
wa kwanza kukomenti
suleiman bakar day ago
ujinga tu hanna binge hanna kitu
isaya merickiory wille day ago
mh unafaa sana kuitwa mh
ester jimmy day ago
heading na taarifa iliyopo ni different 🤔🤔
ulinzi gani mbona ulinzi wa kawaida tu huo
gaspar lubaga day ago
uko sawa mheshimiwa waziri
c mchezo
john katindasa day ago
ushauri wangu waziri lugola amwombe radhi musiba na watanzania aliotufadhaisha kwa kauli yake ya kumshambulia kipenzi chetu musiba mzalendo anayetetea maslahi ya nchi yetu
lolo samuel 2 days ago
ndio maana riba ni kharamu mungu anaichukia sana riba
anafi suleimani 2 days ago
waangalie au unawaamulisha na kuwapa kikomo cha riba kwa kauli hiyo hakuna jipya hapo
goodluck edson 2 days ago
kamera yako inanenepesha kishenzi ina vitamin gan
ibrahim hamza 2 days ago
kwani makusudio ya uchaguzi wa raisi kila baada ya miaka mitano ni nini naona gharama za uchaguzi 2020 zitumike kwa ajili ya maji vijijini
imma mlowe 2 days ago
leo hii watanzania wakipiga kura kati ya musiba na lugola mmoja aache kazi watanzania wengi watasema musiba abaki lugola aache kazi maana atasema mwingine
lugola umejishushia heshima yako kwakumingilia musiba tulikupenda sana watanzania lakini ili tuendelee kuwa na wewe au kukuamini lazima ufue kauli yako kuhusu musiba yakumtaka anyamaze ukiwa achia wanaomtukana raisi waendelee
rahima aaaa 2 days ago
kiukweli period inatesa sana
jowa kani 2 days ago
mkuu hizi lorry zamafuta zinaangunga kila wiki isiwekua wanachakachua mafuta nakupindua gari hili ni tatizo mkuu linahitaji ufumbuzieither madreva wapewe mafunzo rasmi yakuendesha tank zenye liquidsau lorry zote zitiwe kick valves ambazo hufunguliwa tu kutoka kwenye dashbody na dereva mwenyewe kwa umeme au pedomatic (hewa)engine ikizima hazifunguki lorry inaweza kuanguka namafuta yasimwagikenikupitisha tu sheria ya lorry zamafuta
mungu atawaongezea uwezo zaidi tz sababu mnaelekeza katika haki talanta ndogo mliyopewasoon mtavumbua mlima wa dhahabu somewhere kimuugiza tu
mathayo wilson 2 days ago
la mhe nadhani wewe ndo unajua leo msiba ameanza kipindi kumbe police hawakuwa wanajua kazi ya msiba
anthony njombo 2 days ago
japhet mwamlenga 2 days ago
ndomaana polic hawatimizi matamko yako unakulupuka sana kwahiyo wanaomtukana rais umewapa unyo gani
simeon mutashobya 2 days ago
nilichokiona hapo ni kuwa wewe ni jasiri afu umetajasheria nyingine ya ovyohujasakamwa hata kwa kuvunja kanuni hongera kijana
osten mwakasita 2 days ago
kakimya auna ya kuongea ww ndio unasababisha wapiga dili wandelee kupiga dili
dna of god tv 2 days ago
hapana ubishi mwanamme hakai chini tunamwona big up
miraji juma 2 days ago
hii nimichezo tuu watu wasio nafikra wanachezewa picha la kihindilugola why now na musiba alianza mda na kama niuharibifu keshaufanyahii inanikumbusha mbez walibomolewa watu walilia mno zaid ya week mbili bila kusikia chochote kutoka kwa viongozwatu washaumia ndio mkuu wamkoa anajidai analaanitunajiuliza mambo yanavyoanza huwa hamsikii au hiz nijanja janja tuu | 2019-09-16T14:09:49 | https://ruclip.com/channel/UCuZoQN16S-otkbGH-90gkgA |
picha za ujenzi uingereza (januariagosti 2015) | jworg
awamu ya 1 ya picha za ujenzi uingereza (januari hadi agosti 2015)
mashahidi wa yehova wanahamisha ofisi yao ya tawi kutoka mill hill london kwenda eneo lililopo kilometa 70 hivi kuelekea mashariki karibu na jiji la chelmsford essex kati ya mwezi wa januari na agosti 2015 wajenzi waliandaa makazi ya muda ili kuwa tayari kuanza kazi ya kujenga
januari 23 2015eneo la ujenzi la ofisi ya tawi
wakiwa na kibali kutoka kwenye mamlaka za eneo hilo wafanyakazi walikata miti kwa ajili ya kuanza ujenzi walijitahidi kufanya hivyo kwa bidii ili wamalize mapema kabla kipindi cha ndege kutengeneza viota na kutaga mayai kuanza mabaki ya mbao yanatumika kutengenezea njia salama za wanaotembea kwa miguu na mbao zinahifadhiwa kwa ajili ya kutumiwa katika ujenzi
januari 30 2015chumba cha muda cha kulia chakula
fundi wa umeme akiweka soketi kwa ajili ya skrini za video kwenye jengo lililokuwa hoteli zamani sasa jengo hilo litatumiwa kupikia na kulia chakula skrini hizo zitatumiwa kutazama programu za kiroho kama vile ibada ya asubuhi na funzo la mnara wa mlinzi la familia ya betheli
februari 23 2015eneo la ujenzi wa ofisi ya tawi
wafanyakazi wakizungushia ua eneo kubwa la ujenzi kwa kuwa eneo liko nje ya mji hatua zinachukuliwa ili kuhakikisha kwamba ujenzi huo hauathiri sana wanyama wanaoishi eneo hilo kwa mfano upande wa chini ya ua nafasi yenye urefu wa sentimeta 20 imeachwa kuruhusu melesi wanaotafuta chakula usiku kuendelea na shughuli zao
wafanyakazi wakijenga barabara ya muda inayounganisha eneo la makazi ya muda na eneo maalumu la ujenzi
machi 5 2015eneo la ujenzi wa ofisi ya tawi
mwonekano wa barabara ya muda iliyokamilika kutoka upande wa mashariki kama inavyoonekana upande wa juu kulia barabara hiyo inatoka kwenye makazi ya muda hadi kwenye eneo maalumu la ujenzi majengo yanayoonekana upande wa chini kushoto sasa yanatumika kama nyumba za wajenzi mjengo ya makazi ya muda yatawekwa kwenye maeneo yaliyo karibu na majengo hayo
aprili 20 2015eneo la makazi ya muda
mshiriki wa baraza linaloongoza la mashahidi wa yehova na mwakilishi mwingine wa makao makuu walikitembelea kikosi cha ujenzi baadaye katika juma hilo mkutano wa pekee ulifanywa na majumba yote ya ufalme nchini uingereza na ireland yaliunganishwa kupitia intaneti kwa ajili ya programu hiyo ikatangazwa kuwa katika jioni iliyotangulia halmashauri ya jiji la chelmsford ilitoa kibali cha awali cha kuendelea na ujenzi
mei 13 2015eneo la kutegemeza ujenzi
wafanya kazi wakiweka vifaa vya kuilinda mizizi katikati ya mialoni miwili njia hii inaunganisha eneo maalumu la makazi ya muda na eneo maalumu la ujenzi hivyo vifaa hivyo vinaweza kusaidia kulinda mizizi isiharibiwe vyombo vizito vinapopita
mei 21 2015eneo la makazi ya muda
wafanyakazi wakichimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba na nyaya za makazi ya muda nyuma kuna majengo 50 yaliyokamilika watakayokuwa wakiishi wafanyakazi katika kipindi cha ujenzi
juni 16 2015 eneo la makazi ya muda
fundi wa mabomba akiweka mabomba ya maji kwenye majengo ya makazi ya muda
juni 16 2015eneo la makazi ya muda
mwonekano wa nyumba za muda kutoka upande wa mashariki mbele ni maeneo yanayoandaliwa kwa ajili ya kuweka nyumba zaidi upande wa kushoto kuna majengo mengine yanayotia ndani chumba cha kulia chakula ofisi ya tawi itajengwa katika eneo linaloonekana katikati ya picha kwa nyuma
mtaalamu akiunganisha nyaya katika chumba cha vyombo vya mawasiliano mfumo wa kompyuta na intaneti ilihitajika mapema katika mradi huo ili kushughulikia shughuli zote za ujenzi kuwasiliana na ofisi za tawi nyingine na kuwasiliana na makao makuu ya ulimwenguni pote
julai 6 2015eneo la ujenzi wa ofisi ya tawi
mwanakandarasi akipima maeneo yenye mashimo ya kufanyia uchunguzi kwa kutumia kifaa cha kupokea habari kutoka kwenye setilaiti (gps) mashimo hayo yanawasaidia wanaakiolojia kutathmini eneo kabla ya ujenzi kuanza ingawa waroma waliishi eneo la karibu la chelmsford katika mashimo 107 yaliyochimbwa kwenye awamu ya kwanza ya tathmini hizo hakuna vitu vyenye thamani vya kale vilivyovumbuliwa
julai 6 2015eneo la kutegemeza ujenzi
mfanyakazi akikata fremu ya mlango katika urefu unaofaa baadhi ya majengo katika eneo la kutegemeza ujenzi yalirekebishwa ili yawe karakana ofisi za muda na utendaji mwingine wa kutegemeza kazi utapatikana hapo
julai 6 2015eneo maalumu la makazi ya muda
mfanya kazi akijaza udongo kwenye lori ili kujaza maeneo yaliyo na mashimo
julai 7 2015eneo la ujenzi la ofisi ya tawi
mandhari kutoka upande wa kusini wa eneo la ujenzi lenye ekari 34 inayoonyesha mashamba ya jirani barabara kuu iliyo jirani (haijaonyeshwa) inafika kwenye bandari viwanja vya ndege na kwenye jiji la london
julai 23 2015eneo la ujenzi la ofisi ya tawi
wanakandarasi wakibomoa majengo yaliyokuwapo kwenye eneo linalotarajiwa kujengwa ofisi ya tawi mpya
agosti 20 2015eneo la kutegemeza ujenzi
kreni yenye uwezo wa kubeba uzito wa tani 60 ikiweka sehemu ya chini ya kibanda kwenye mahali pake sehemu ya mbele ya picha inaonyesha misingi kwa ajili ya kuweka vibanda vingine vibanda hivi ni kwa ajili ya ofisi za kuratibu mradi wa ujenzi
https//wwwjworg/finderdocid=502016514&wtlocale=sw&srcid=share
mailtobody=awamu ya 1 ya picha za ujenzi uingereza (januari hadi agosti 2015)0a0ahttps3a2f2fwwwjworg2ffinder3fdocid3d50201651426wtlocale3dsw26srcid=share⊂ject=awamu ya 1 ya picha za ujenzi uingereza (januari hadi agosti 2015)
kuhubiri katika lugha za asili za ireland na uingereza
mashahidi wa yehovakujenga bila mipaka
wanaomba kazi lakini si malipo | 2017-03-23T01:41:14 | https://www.jw.org/sw/mashahidi-wa-yehova/utendaji/ujenzi/picha-za-uingereza-jan-ago-2015/ |
cardiff city archives tanzania sports
23rd march 2019 last update at 1234 pm
arsenal left it late to stay top of the english premier league title race as niklas bendtner and theo walcott scored in the last two minutes at the emirates wednesday to beat cardiff city 20
arsenal ndio manchester united mpya
* man u wamechacha kama liverpool ya 1990 *lukaku aliyeitwa garasa anathibitisha ubora *krismasi kuwa chungu kwa baadhi ya timu kwa miaka 20 iliyopita ilikuwa kawaida kuona timu zikipepesuka nyuma y
*wawapiga southampton chelsea nao wazuri *man city wawapiga tottenham hotspur 60 *man united wabanwa liverpool everton sare ligi kuu ya england imeingia raundi ya 12 kwa matokeo mch | 2019-03-25T08:28:11 | https://www.tanzaniasports.com/tag/cardiff-city/ |
semalt jinsi usalama wa usalama unaathiri data yako
je trafiki ya uhamisho ni nini kwa nini ni muhimu naam jack miller meneja mfanikio wa mteja mkubwa wa semalt anaelezea kuwa trafiki ya rufaa ni sehemu ya trafiki inayoweka kwenye tovuti yako kupitia chanzo kingine chanzo inaweza kuwa kiungo kutoka kwenye uwanja mwingine google analytics mara moja anajua wapi trafiki ya wavuti ilikuwa kabla ya kutua kwenye tovuti yako online prom dress shops uk kwa hiyo (google analytics) itaonyesha majina ya uwanja wa tovuti hizi kama chanzo cha trafiki ya rufaa katika ripoti zake
data yako imeathirikaje wakati unapoondoa trafiki ya uhamisho
ni kwa chaguomsingi kwamba wahamisho hujitokeza moja kwa moja vikao vipya hata hivyo wakati unapochagua kuwatenga chanzo chochote cha uhamisho basi trafiki ya wavuti kutoka kwa vikoa visivyochapishwa haitoi vikao vipya kama ni dhahiri kama unataka trafiki ya rufaa ili kusababisha vikao vipya basi haipaswi kuingiza domains katika orodha hii ya kutengwa
kutoka kwa hali hiyo hapo juu unaweza kuona kuwa tangu ruhusa husababisha vikao vipya ukiondoa uhamisho kisha unaashiria kwamba inathiri jinsi vikao vyako vinavyohesabiwa mwingiliano huu unaweza kuhesabiwa kama vikao vya umoja au vingi kulingana na jinsi unavyoweza kushughulikia kwa mfano mtumiaji kwenye mysitecom anatembelea tovuti yako yakoitecom kisha inarudi kwenye mysitecom ikiwa haujaondoa tovuti yako (yakoitecom) basi vikao vyote viwili vinahesabiwa mara moja kila wakati yeye / yeye anapata ardhi kwenye mysitecom ikiwa kwa upande mwingine umetenga yakoitecom basi kikao kimoja kilitokea hiyo ni jinsi gani ukiondoa trafiki ya rufaa inathiri jinsi vikao vyako vinavyohesabiwa
matumizi ya kawaida ya msamaha wa rufaa
kwa usindikaji wa malipo ya chama cha tatu
kufuatilia uwanja wa kikoa
orodha ya kutengwa
unapaswa kuwa na ufahamu wa ukweli kwamba trafiki ya mtandao tu kutoka kwenye uwanja na mada ndogo yake yanaweza kutengwa trafiki kutoka kwenye uwanja unao na mechi ya kamba ndogo sio
kwa mfano ikiwa huondoa trafiki ya rufaa kutoka websitecom basi trafiki ya wavuti kutoka tovuti ya domaincom na ndogo ya uwanja mwinginewebsitecom imechukuliwa usafiri wa wavuti kutoka kwa mwinginewebsitecom haujachukuliwa
jinsi ya kuunda orodha ya uhamisho wa rufaa
kuanza kwa kuingia kwenye akaunti yako ya google analytics
bonyeza 'admin'
ukitumia orodha ya kushuka mahali fulani kwenye safu ya safu yako chagua mali ungependa kuifanya
bonyeza infotracking
bofya rufaakuondolewaorodha
kuongeza jina la kikoa kisha uunda orodha yako
ihifadhi mabadiliko na wewe ni mzuri kwenda
jinsi ya kuondoa uwanja kutoka orodha ya kutengwa
ikiwa kwa sababu fulani unajulikana kwako kuchunguza tena kuondosha kikoa kutoka kwa orodha ya kutengwa basi unaweza kufanya hivyo kwa urahisi tumia hatua za juu ila kwa maelezo mafupi badala ya kuongeza rufaa uondoe ondoa mbali kwa kubonyeza kufuta domain kisha uhifadhi mabadiliko
mtihani maji
hakikisha orodha yako ya kutengwa inafanya kazi kwa kupima wataalamu wanakupendekeza kutumia google recording msaidizi wa tag itakuambia nini kinachotengwa na kile ambacho sio
kuna mara ambazo trafiki zimeondolewa bado zinaonekana katika ripoti yako inaweza kutokea kwa sababu
watumiaji walitembelea tovuti yako kabla ya kuunda orodha ya kutengwa
wanaweza kutumia alama | 2018-05-25T03:28:24 | http://halftheink.com/semalt-jinsi-usalama-wa-usalama-unaathiri-data-yako |
mauaji arusha yakoroga bunge | jamiiforums | the home of great thinkers
mauaji arusha yakoroga bunge
discussion in 'jukwaa la siasa' started by candid scope feb 11 2011
kauli ya pinda yaamsha mapya
mbunge lema awekwa mtegoni
spika makinda awaka asema�
waziri mkuu mizengo pinda (aliyesimama) akijibu maswali ya wabunge katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo bungeni mjini dodoma jana (pichatryphone mweji)
[font=arialmt sansserif]kishindo cha mauaji ya watu watatu yaliyofanywa na polisi mkoani arusha januari 5 mwaka huu jana kilifunika bunge kwa staili ya aina yake na mwishowe kumfikisha mbunge wa arusha mjini (chadema) godbless lema kujikuta katika mtego wa kikanuni[/font]
[font=arialmt sansserif]lema akiomba mwongozo wa spika juu ya hatua anazoweza kuchukua mbunge iwapo atagundua kwamba kiongozi mkubwa wa serikali kama waziri mkuu amelidanganya bunge alimfanya spika anne makinda kuwa mkali akikemea kwamba kauli ya mbunge huyo ililenga kumdhalilisha waziri mkuu mizengo pinda[/font]
[font=arialmt sansserif]bunge letu hili lazima liwe na adabu inayostahili maana kama tunafanya sasa unataka kusema waziri mkuu kwa ahadi aliyoiweka bungeni anadanganya alisema makinda kwa kuhamaki[/font]
[font=arialmt sansserif]baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika spika alilizungumzia kwa mara nyingine jambo hilo[/font]
[font=arialmt sansserif]sasa bunge hili linataka kukosa hata adabu napenda nitumie kifungu kinachohusika kwa maelezo naomba wote mnisikilize alisema[/font]
[font=arialmt sansserif]alisimamia kifungu cha 63(1) cha kanuni ambacho kinasema bila kuathiri masharti ya ibara ya 100 ya katiba yanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika bunge ni marufuku kabisa kusema uongo bungeni na kwa sababu hiyo mbunge yeyote anapokuwa akisema bungeni anawajibika kuhakikisha kuwa anatoa kauli maelezo na suala ambalo anaamini kuwa ni la kweli na sio jambo la kubuni au la kubahatisha tu[/font]
[font=arialmt sansserif]alinukuu pia kifungu cha 63 (2) mbunge yeyote anapokuwa akisema bungeni hatachukuliwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu jambo fulani lilotangazwa au lililoandikwa na vyombo vya habari[/font]
[font=arialmt sansserif]aliendelea kunukuu kifungu cha 63 (3) ambacho kinasema mbunge mwingine yeyote yule anaweza kusimama mahali pake na kutamka kuhusu utaratibu kama alivyofanya lema[/font]
[font=arialmt sansserif]alisema baada ya kuruhusiwa na spika kuongea na kudai kuwa mbunge aliyekuwa anasema kabla yake alikuwa anatoa maelezo ya uongo kuhusu suala au jambo alilokuwa analisemea bungeni[/font]
[font=arialmt sansserif]baada ya kusema hayo makinda alimpa lema hadi februari 14 mwaka huu (siku tano) awe amewasilisha ushahidi wa maandishi utakaoonyesha kuwa waziri mkuu mizengo alisema uongo bungeni[/font]
[font=arialmt sansserif]sakata hilo lilianza baada ya kipindi cha maswali na majibu kuisha ambapo lema alisimama na kuomba mwongozo wa spika hasa akilenga majibu ya pinda juu ya mauaji ya arusha[/font]
[font=arialmt sansserif]alimtaka lema kuandika vizuri maelezo kama pinda amedanganya halafu watamweleza atafanya nini kwa mujibu wa kanuni hiyo kama mbunge atashindwa kuthibitisha kauli yake ana mawili moja kuomba radhi na kufuta usemi wake au ang'ang'ane nao na kupewa adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya bunge[/font]
[font=arialmt sansserif]kabla ya kufikiwa kwa maamuzi ya spika makinda wakati wa kipindi cha maswali na majibu alisimama mbunge wa kibakwe (ccm) george simbachawene na kuomba mwogozo wa spika[/font]
[font=arialmt sansserif]aliomba mwongozo kwa spika mtu kama lema ambaye ametoa kauli anayemkashifu kiongozi wa juu na kanuni zinasemaje na adhabu gani atachukuliwa[/font]
[font=arialmt sansserif]hata hivyo spika alimtaka mbunge huyo kukaa chini kwa kuwa alipoomba mwongozo si mahali husika[/font]
[font=arialmt sansserif]mtafaruku huo uliibuka baada ya kiongozi wa upinzani bungeni ambaye pia ni mbunge wa hai (chadema) freeman mbowe kumbana waziri mkuu mizengo pinda wakati wa maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu juu ya mauaji yaliyofanywa na polisi jijini arusha dhidi ya raia[/font]
[font=arialmt sansserif]mbowe alimtaka pinda aeleze kama serikali ina nia ya kuunda tume kuchunguza mauaji hayo[/font]
[font=arialmt sansserif]mbowe aliuliza kwa kuwa serikali ilipewa taarifa na polisi bila kupata taarifa za upande wa pili ni lini itaunda tume ya uchunguzi wa kimahakama (judicial commission of inquiry) ili kupata waliohusika[/font]
[font=arialmt sansserif]katika majibu yake pinda alisema serikali haiko tayari kuunda tume ya kimahakama ya uchunguzi kwa ajili ya kuchunguza na kuwabaini waliohusika na vifo hivyo[/font]
[font=arialmt sansserif]pinda alisema kama mbowe ana dhamira asingesubiri kumuuliza swali hilo bungeni badala ya kuwasilisha taarifa serikalini kwanza ili izifanyie kazi[/font]
[font=arialmt sansserif]pinda ambaye alionekana kukerwa na swali hilo alisema kuwa serikali lazima iridhike kuwa zipo sababu za kutosha ili ianzishe uchunguzi huo[/font]
[font=arialmt sansserif]katika swali la msingi mbowe alimuuliza pinda kuwa pamejitokeza matukio mengi ya askari kuwapiga risasi raia na kupoteza maisha na kwamba kwa kuwa serikali haijawahi kutoa taarifa je inaweza kutoa tamko kwa vifo vya arusha ikiwemo kujiuzulu kwa mkuu wa jeshi la polisi (igp) na waziri wa mambo ya ndani ya nchi[/font]
[font=arialmt sansserif]pinda alisema serikali hii ni makini sana ukiona jambo limetokea kama la arusha usikimbilie kusema serikali bali nani amesababisha hayo[/font]
[font=arialmt sansserif]alisema chadema kilikutana na kujadiliana na kushauriana na polisi kuwa maandamamo yao yatumie ruti moja ya barabara kutokana na ufinyu wa barabara za jiji la arusha lakini chama hicho kilikaidi[/font]
[font=arialmt sansserif]alisema kuwa baada ya chadema kukataa ushauri huo serikali iliamua kuzuia maandamano hayo na badala yake ilielekeza kuwa ufanyike mkutano peke yake lakini chadema waliendelea na maandamano[/font]
[font=arialmt sansserif]baadhi yenu mlikamatwa na pale kwenye mkutano matamshi yenu hayakuendana na chama cha siasa alisema pinda[/font]
[font=arialmt sansserif]alisema kilichosababisha watu hao kupigwa risasi ni kutokana na hatua ya wafuasi wa chama hicho kwenda kuwakomboa wenzao katika kituo cha polisi na kukisogelea umbali wa mita 50 na kwamba polisi hawakuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutumia nguvu na watu kupigwa risasi[/font]
[font=arialmt sansserif]mngefuata ushauri haya yote yasingetokea alisema bila kuzungumzia suala la igp na waziri wa mambo ya ndani ya nchi kutakiwa kujiuzulu[/font]
[font=arialmt sansserif]akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya bunge lema alisema atawasilisha ushahidi huo kama alivyotakiwa na spika[/font]
[font=arialmt sansserif]alisema yeye ni mtu mzima na haogopi chochote[/font]
[font=arialmt sansserif]januari 5 mwaka huu chadema waliandaa maandamano makubwa katika jiji la arusha pamoja na mkutano wa hadhara kwa nia ya kulaani mchakato wa kumpata meya wa jiji hilo ambaye inadaiwa alipatikana kwa njia ambazo hazikubaliki kwa kuwa wapo madiwani waliopiga kura kinyume cha kanuni[/font]
[font=arialmt sansserif]katika maandamano hayo ambayo awali yalikuwa yamekubaliwa na polisi yalibatilishwa na igp mwema jioni kabla ya siku ya maandamano lakini chadema waliendelea nayo hali iliyosababisha mapambano baina ya wafuasi wa chama hicho na polisi[/font]
[font=arialmt sansserif]polisi walitumia nguvu kupita kiasi kwa mabomu ya kutoa machozi maji ya kuwasha risasi za moto na kuua watu watatu[/font]
[font=arialmt sansserif]siku hiyo pia viongozi wakuu wa chadema akiwamo mbowe katibu mkuu wa chadema ambaye pia alikuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu uliopita dk willibrod slaa mbunge wa moshi mjini philemon ndesamburo mbunge wa rombo joseph selasini lema na viongozi wengine kadhaa walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kuandamana bila kibali[/font]
[font=arialmt sansserif]kesi hiyo bado inaendelea kutajwa katika mahakama ya mkoa arusha
busara ya kujibu swali ni muhimu zaidi kuliko kutumia tu mbinu za kujitetea mheshimiwa pinda hakutumia busara zaidi katika kujibu swali na papo hapo spika makinda ndio karuka jivu na kukanyaga moto moto utakaolipuka sasa baada ya kumruhusu lema kuwasilisha vielele vya maafa ya arusha makinda kafanya bila kukusudia na huenda atakuja kujutia mambo yatakapofumuka upya
moto utakaolipuka sasa baada ya kumruhusu lema kuwasilisha vielele vya maafa ya arusha makinda kafanya bila kukusudia na huenda atakuja kujutia mambo yatakapofumuka upyaclick to expand
bila ushabiki nitasema kwa haki huyu mtu kama mnategemea anything than rubish mtakuwa mmekufa jamaa hana akili busara wala adabu yeye peke yake amefanikiwa kuitukanisha cdm kwa wananchi na mataifa mengine mara nyingi zaidi kuliko mtu yeyote ndani ya cdm tena amevunja rekodi kwa kuyafanya haya kwa muda mfupi kuliko mwanasiasa yeyote(hata mrema)
ni busara waziri mkuu kusema hayo
spika wa bunge kuombwa mwongozo kwake maana yake ni matusi
bila ushabiki nitasema kwa haki huyu mtu kama mnategemea anything than rubish mtakuwa mmekufa jamaa hana akili busara wala adabu yeye peke yake amefanikiwa kuitukanisha cdm kwa wananchi na mataifa mengine mara nyingi zaidi kuliko mtu yeyote ndani ya cdm tena amevunja rekodi kwa kuyafanya haya kwa muda mfupi kuliko mwanasiasa yeyote(hata mrema)click to expand
ametukanisha chadema how ulitaka asemeje akubaliane na maneno ya waziri mkuu heri yeye ambaye hana akili busaraadabu ya kuitetea ccm lakini ana baraka za kila mtanzania anayeililia na kuipenda tz na heri kwako wewe unayetetea mafisadi nadhani huu ni uwiano sawia kabisa ni sawa na 1+1=11 na si vinginevyo
huna jipya ndio upeo wako
je waliouawa walipigwa risasi umbali wa mita 50 toka kituo cha polisi
raia wa kenya pia alikuwa amekwenda kuvamia kituo cha polisi kuwatoa viongozi wa cdm waliokuwa mahabusu
majibu ya maswali hayo ndiyo yatakayobainisha muongo ni nani kati ya pinda na lema
nasema muhimu kutumia busara katika kujibu badala ya kujibu kisiasa vielelezo vikiletwa kwamba waliouawa walikuwa nje na mbali ya kituo cha polisi arusha waziri mkuu ataelewekaje
halafu unadhalilisha wajapan kwa kujipachika nick 'mjepu' hawana akili fupi kama weweotherwise wangekuwa mamefutika katika ramani ya dunia siku nyingi
yaani hawa hawaogop ya misri
tunajua huko kazini lakini wakati mwingine uwe unaona aibu kidogo
lema atakapoleta uthibitisho wa mkenya aliyeuawa mbali kabisa na kituo cha polisi atasemaje kitakapoletwa kithibitisho cha polisi kuingia mpaka makanisani kuwasaka watu kama walipoingia mpaka nyumba ya masisi karibu na kanisa la mt theresia atasima kuna kituo cha polisi pale
pamoja na mapangufu yoteunayoyaona bado ukweli utakuwa wazi mjepu | 2017-05-01T07:06:42 | https://www.jamiiforums.com/threads/mauaji-arusha-yakoroga-bunge.109975/ |
china yapiga hatua katika juhudi za kuondoa umaskini kwenye sehemu zenye umaskini uliokithiri china radio international
china yapiga hatua katika juhudi za kuondoa umaskini kwenye sehemu zenye umaskini uliokithiri
(gmt+0800) 20190626 170748
ofisa mwandamizi wa ofisi ya kuwasaidia watu maskini iliyo chini ya baraza la serikali la china bw ou qingping amesema china imeongeza nguvu katika kuondoa umaskini kwenye sehemu zenye umaskini uliokithiri na hatua ijayo itakuwa ni kuhamasisha matumizi kuwa njia muhimu ya kuondoa umaskini
kwa mujibu wa mpango wa kuondoa umaskini uliowekwa na serikali ya china hadi kufikia mwaka 2020 china itawaondoa watu wote vijijini katika umaskini na kuondoa umaskini uliokithiri kwenye wilaya zote naibu mkurungezi wa ofisi ya kuwasaidia watu kuondokana na umaskini iliyo chini ya baraza la serikali la china bw ou qingping amesema sehemu zenye umaskini uliokithiri ni changamoto kubwa zaidi kwa juhudi ya kuondoa umaskini nchini china ameeleza kuwa mwaka 2017 china iliorodhesha wilaya 334 zenye umaskini uliokithiri haswa katika mikoa mitano ya tibet xinjiang sichuan yunnan na gansu
takwimu zinaonesha kuwa kati ya mwaka 2018 hadi 2020 china imetenga zaidi ya dola bilioni 31 za kimarekani kwa ajili ya sehemu zenye umaskini uliokithiri na nusu ya fedha hizo imetumiwa katika mikoa hiyo mitano bw ou amesema juhudi za kuondoa umaskini katika sehemu hizo zimepata ufanisi akisema
mwaka jana tumewasaidia watu milioni 48 kuondokana na umaskini katika wilaya 334 zenye umaskini uliokithiri ambao ni asilimia 38 ya watu wote walioondokana na umaskini nchini china mwaka huo hali hii inaonesha kuwa sera yetu inafanya kazi
hata hivyo bw ou amesema juhudi za kuondoa umaskini bado zinakabiliwa na changamoto kubwa kwa mfano katika mikoa mitano yenye umaskini zaidi bado kuna watu milioni 172 wanaoishi kwenye umaskini uliokithiri na kuwasaidia kuondokana na umaskini ni kazi ngumu
alipozungumzia vigezo vya kuondokana na umaskini bw ou amesisitiza kuwa mstari wa mwisho ni hakuna shida ya kupata chakula mavazi elimu ya kimsingi matibabu na makazi anaona kuwa kuwahamasisha watu maskini kuwa na hamu ya kuondokana na umaskini ni njia muhimu ya kupambana na janga hili
hadi kufikia mwaka 2020 endapo tutafanikiwa kuwasaidia watu wengi kuondokana na umaskini huku watu wengi wakirejea kuwa maskini hatuwezi kusema tumetimiza lengo letu ni lazima tuzingatie kazi ya kuimarisha matokeo ya kuondoa umaskini njia muhimu ni kuendeleza sekta za uchumi na kuhimiza ajira
aidha bw ou amesema china itaongeza nguvu zaidi katika kupambana na umaskini katika siku zijazo | 2020-04-01T21:21:51 | http://swahili.cri.cn/141/2019/06/26/1s186762.htm |
tume inapitisha mawasiliano juu ya misaada ya serikali kwa ajili ya sinema mwandishi wa eu mwandishi wa eu
tume antar mawasiliano juu ya hali ya misaada kwa ajili ya sinema
on 14 novemba tume ya ulaya itakuwa kupitisha communication mpya juu ya hali ya misaada kwa ajili ya filamu na kazi nyingine audiovisuella
communication ina vigezo kina kwamba kufafanua jinsi nchi wanachama wanaweza msaada wa fedha kwa uzalishaji na usambazaji wa filamu kwa kuzingatia kanuni misaada ya eu serikali ni nafasi vigezo ambayo wamekuwa kutumika tangu 2001 na akasuluhisha yao
lengo la communication ni kuhamasisha viumbe na utamaduni kila mahali katika umoja wa ulaya na kuweka masharti ya mafanikio ulaya sekta ya audiovisuella ambapo uzalishaji wa mpakani inaweza kuweka juu kwa urahisi
nchi wanachama kutoa inakadiriwa € 3 bilioni kwa mwaka katika msaada filamu € 2bn katika misaada na mikopo laini kama vile € 1bn katika motisha ya kodi karibu 80 ya hii ni kwa ajili ya uzalishaji wa filamu
msaada wa fedha ni muhimu ili kuhakikisha kuendelea na ya maana ulaya uzalishaji wa filamu katika 2001 tume ya kuchapishwa kwa sheria mara ya kwanza juu ya matumizi ya sheria hali ya misaada na misaada kwa ajili ya uzalishaji filamu (cinema communication) sheria hizi muda wake mwishoni mwa 2012
kwa hivyo tume ilianza mchakato wa mapitio katika 2011 ambayo imesababisha mashauriano tatu umma wa nchi wanachama na wadau
kwa ajili ya mapitio ubora wa filamu kwenda picturenosecom
tags sinema cinema communication hali sheria za eu misaada filamu ruzuku mikopo
jamii frontpage burudani tume ya ulaya
« kwanza eumyanmar kikosi kazi mkutano katika yangon na nay pyi taw
tume antar ukandamizaji kila mwezi mfuko » | 2020-02-24T05:50:39 | https://sw.eureporter.co/frontpage/2013/11/08/commission-adopts-communication-on-state-aid-for-cinema-2/ |
idadi yawaliopoteza maisha kufuatia kimbunga idai yaongezeka afrika rfi
msumbiji zimbabwe majanga ya asili
imechapishwa 20032019 • imehaririwa 20032019 saa 0827
picha ya mji wa beira iliyopigwa mnamo machi 18 baada ya kimbunga kupiga nchini msumbiji © ifrc
takwimu za hivi karibuni zinaeleza kuwa watu 300 ndio wamehesabiwa kupoteza maisha kufuatia kimbunga idai kilichopiga eneo la ukanda wa afrika kusini wakati huu mchakato wa kuwaokoa watu waliokimbilia juu ya miti na juu ya paa za majumba
nchini msumbuji nchi ilioguswa zaidi na kimbunga hicho inaelezwa kuwa mpaka sasa ni watu 200 ndio waliopoteza maisha kulingana na taarifa ya rais wa nchi hiyo filipe nyusi ambae ametangaza maombolezo ya siku tatu
nchini zimbabwe zaidi ya watu 100 ndio wanaodaiwa kupoteza maisha lakini kwa mujibu wa waziri wa serikali za mikoa july moyo idadi hiyo inaweza kuongezeka mara tatu kwani kuna miili ya watu inayoelea juu ya maji kuelekea nchini msumbiji
wito wa misaada ya kimataifa umetolewa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi waliokimbia kutokana na mafuriko hayoyatokanayo na kimbunga idai debora guyene ni mkurugenzi kwenye shirika la msaada wa chakula la umoja wa mataifa pam
upande wake serikali ya tanzania imetowa msaada wa chakula na dawa kwa ajili ya wananchi wamataifa hayo yalioathirika na kumbunga hicho kama anavyoelea hapa waziri wa mambo ya nnje wa tanzania paramagamba kabudi
tayari shughuli za mazishi zimeanza nchini zimbabwe ambapo rais wa nchi hiyo emerson mnangagwa anatarajiwa kuwasili katika eneo la manikalan eneo lililoguswa zaidi na kimbunga hicho wakati huu shirika la kimataifa la haki za binadamu amnesty international likitoa wito kwa jumuiya kimataifa kuhamasisha utoaji msaada ili kukabiliana na hali hiyo | 2019-09-16T14:33:55 | http://m.sw.rfi.fr/afrika/20190320-idadi-yawaliopoteza-maisha-kufuatia-kimbunga-idai-yaongezeka |
ziara ya vyombo vya habari nchini leo ofisi za azam media bin zubeiry sports online ziara ya vyombo vya habari nchini leo ofisi za azam media bin zubeiry sports online
mwanzo > untagged ziara ya vyombo vya habari nchini leo ofisi za azam media
ziara ya vyombo vya habari nchini leo ofisi za azam media
mtendaji mkuu wa azam media rhys torrington akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa ziara ya vyombo vya habari nchini katika ofisi za azam tv mchana wa leo barabara ya nyerere dar es salaam
torrington akiwahutubia waandishi wa habari
torrington akionyesha king'amuzi na rimoti ya azam tv ambavyo vitaanza kuuzwa mwezi ujao kwa bei ya sh 95000 pamoja na dishi lake na huduma za kufungiwa wakati malipo ya mwezi yatakuwa ni sh 12500
bei moja chaneli kibao babu kubwa burudani maisha habari na michezo mbalimbali
torrington akizungumza na mtendaji mkuu wa bin zubeiry blog mahmoud zubeiry kushoto
azam tv imenunua haki za kuonyesha ligi kuu ya bara
ofisa mwendeshaji mkuu wa azam tv eric caste akifafanua jambo kwa waandishi
waandishi wa habari wakielekezwa mambo na meneja huduma kwa wateja loth mziray katika ofisi ya huduma kwa wateja ya azam tv
mziray aliwapa maelezo ya kutosha waandishi
mziray akijibu swali la mhariri wa michezo wa gazeti la habari leo mgaya kingoba kulia
waandishi pia waliingias kwenye gari la kurushia matangazo ya mpira moja kwa moja kujionea
ndani ya gari hilo wakielekezwa mambo na mtaalamu meb
mmoja wa wakurugenzi wa azam media yussuf bakhresa akizungumza na waandishi wa habari
yussuf akifafanua jambo kwa waandishi wa habari
item reviewed ziara ya vyombo vya habari nchini leo ofisi za azam media rating 5 reviewed by mahmoud bin zubeiry | 2020-08-04T12:01:23 | http://www.binzubeiry.co.tz/2013/10/ziara-ya-vyombo-vya-habari-nchini-leo.html |
mwiseneza josiane yavuze ku banya canada baherutse kumusura nurwenya aherutse gutera miss rwanda 2019
imyidagaduro yanditswe na dusingizimana remy 17 february 2019 yasuwe 7058
mwiseneza josiane wigaruriye imitima ya benshi yatangaje ko abanya canada baherutse kumugenderera batari baje kumutera inkunga yamafaranga nkuko benshi babitekereje ahubwo bari bazanywe no kumugira inama yuko yakora neza umushinga we ndetse ashimangira ko avugana cyane na miss rwanda 2019nimwiza meghanndetse bajya bananyuzamo bagatebya
mwiseneza yatangarije ikinyamakuru ukwezi dukesha iyi nkuru ko abanya canada baherutse kuza kumureba batari baje kumuha inkunga yamafarangaahubwo bamugiriye inama yamufasha gukora neza umushinga we
yagize ati bariya banya canada bari baje kuntera ingabo mu bitugu ndetse no kungira inama ku mushinga wanjyenta nkunga irenze bampaye ahubwo bai baje kunganiriza banyereka ibyo nakora ngo ugende nezandamutse nkoze umushinga ukagira akamaro neza bantera inkunga
mwiseneza josiane yatangaje ko kuwa gatatu taliki ya 20 gashyantare uyu mwakaaribwo azatangira gushyira mu bikorwa umushinga weahereye mu karere ka rwamaganaaho azaba ari kumwe nabanyarwenya batandukanye barimo njugasamusure na clapton kibonke baherutse kwifotoza bari kumwe mu mafoto yaciye ibintu ku mbuga nkoranyambaga
yagize ati ntabwo nteganya kujya muri sinema ahubwo bariya bakinnyi twifotozanyije biyemeje kumfasha muri kiriya gikorwa cyo kuwa gatatundifuza ko abantu bazaza ari benshibakanshyigikiranabifashishije kubera ko ikinamico ikurura abantu ndetse ituma abantu babasha kumva ubutumwa neza kurusha kuvuga amagambo gusa
mwiseneza yabwiye ukwezi ko umubano we na nyampinga wu rwandanimwiza meghan ari nta makemwahari byinshi bifuza gukorana ndetse ngo banyuzamo bakanatera urwenya ku mbuga nkoranyambaga
yagize ati dukunda gusererezanya ku mbuga nkoranyambaga bitewe ahanini nibyo abafana bavuzehari ukuntu dusubiramo ukuntu byari bimeze muri miss rwandatukibaza uko byari kugenda iyo ntaza kuba miss popularity kuko benshi bari bamaje kubyakirayarambwiye ati iyo baza kuba barampaye ririya kamba rya miss popularityabantu bari kuntera amabuyenamusubije nti uretse nabo nanjye nari kuba umwe mu batera amabuye
mwiseneza yavuze ko umubano we na meghan ari nta makemwa ndetse bari gutegurira hamwe umushinga ukomeye
chat_bubble ndayambaje emmanwul
misirwa ndamusigikiye kumushingawe
17 april 2019 yasuwe 3574 0
17 april 2019 yasuwe 4753 1
16 april 2019 yasuwe 5356 0
16 april 2019 yasuwe 3086 0
cardi b yatunguranye avuga ko adakumbuye umugabo we offset ahubwo avuga
umuraperikazi ukunzwe muri iyi minsi muri amerika cardi b avuga ko mu
16 april 2019 yasuwe 3547 0
abantu batandukanye babonye amashusho ya kimenyi yves yambaye ubusa bagiriye inama umukunzi we
rutahizamu wa rayon sports sarpong yeruye ahishura ibyurukundo ruvugwa hagati ye na asinah era | 2019-04-18T10:26:15 | http://umuryango.rw/imyidagaduro/article/mwiseneza-josiane-yavuze-ku-banya-canada-baherutse-kuganira-n-urwenya-aherutse |
global voices in swahili · habari za uandishi wa kiraia kuhusu western sahara
kumbukumbu za mwezi wa western sahara agosti 2008 · 1 ujumbe
kiungo cha rss kwa western sahara habari mpya kuhusu western sahara
arabeyes rais wa mauritania aliyepinduliwa katika mapinduzi ya kijeshi imeandikwa na jillian c york · imetafsiriwa na charahani · algeria makamanda wa jeshi wamemuondoa madarakani rais sidi ould cheikh abdallahi rais wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa jumatano iliyopita baada ya mtafaruku · soma » gv summit 2012
photos video christian bwaya199 jumbe | 2013-05-22T05:28:25 | http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/middle-east-north-africa/western-sahara/ |
nyumba hii inauzwa jamiiforums
thread starter akiri
1456 1225
nyumba ya vyumba 4 kimoja master
ina sitting room public toilet jiko stoo juu imewekwa gypsum chini tiles
umeme upo maji ya kisima maji ya bomba yapo nyumba ya jirani ni suala la kuunga
kiwanja ni kikubwa kina sqm 1300 na kimepimwa kina hati
nyumba ipo mbagara maji matitu ni km 2 kutoka barabara iendayo chamazi
inauzwa tsh 85m ( inasungumzika )
tuwasiliane 0657 145555 & 0755 099 291
sababu za kuuza nyumba ni nin mkuu
sababu yakuuza nyumba hiyo ninini mkuu akiri maana si haba tupe ukweli ili tujipange
mtugani wa wapi huyo
tupia ramani yake pia
nakukubali sana akiri kwenye sector hizo ila madali wanapiga hela sana nakumbuka kuna dalali m1 alimtafutia kiwanja mzungualichofanya dalali alienda yeye kwanza akawakusanya wakazi wa maeneo yale akawlipa hela yake ya mfukoni ambayo kama mil150 hivi kesho yake akaja na mzungu akavuta mil450nawakunali sana madalali achana na hawa njaa kwenda hata kuangalia shamba anakuchaji hela ya mafuta madalali wa kisasa ananunua yeye issue halafu anaiuza
reactions akiri
wewe sababu ya kutaka kuinunua nini watu wengine bwana do your homework kama una hela fungua biashara sio kukebehi watu humu kama huna cha kuandika sio lazima upost hapa
nb umeshawahi kusikia property developers that is business
uchumi umeyumba kiongozi kama utaangalia vema hizo picha utaona jamaa kashindwa kufanya finishing ya uhakika jamaa anayumba ingine ipo chamazi anataka ahamie huko halafu hiyo ifanye mambo mengine ( kuna watu nawafahamu huwa hawakopi pesa benk wanajenga kisha wanauza < ondoa shaka njoo mezani tufanye biashara
reactions altaaf
view attachment 74311 view attachment 74312 view attachment 74313 view attachment 74314 view attachment 74315
asante sana akiri naona leo umekuja na tangazo zuri na umeliboresha kidogo maji matitu ni kilometre ngapi hadi dar city centre (yaani mjini) maana nyumba yenyewe tena ni kilometre 2 toka barabara ya chamazi hiyo bei mbona ni kubwa sana kwa maeneo hayo akiri nikiangalia nyumba sijui finishing yake ni namna gani sana (ubora wa materials etc) kwa hiyo bei inaua japo umesema maongezi yapo kuna maeneo ukijenga nyumba kama ni nzuri sana huwezi kupata bei kubwa na maeneo mengine gofu tu ni bei ya kuua mtu kwa maji matitu mmmmmmmmmmmmmmmmmmmmh kama una za karibu kidog sema
mimi ni mtu wa kati na mmiliki wa nyumba yupo ukiwa tayari njoo ukaone nyumba useme bei gani utatoa kutoka maji matitu mpaka posta mpya labda ni 18km nyumba za karibu zipo mkuu sasa sijui karibu wapi
katika maeneo haya watu wengi wanajenga nyumba na kuziuza sasa unaweza pata nyumba kuanzia 30m mpaka 100m na nyumba hizo ni mpya na zina kila kitu
biaashara wengi wanajenga na kuziuza akipata pesa anatafuta sehemu ingine anajenga atauza tena shaka ondoa
asante mkuu kwa maji matitu hapana ila maeneo kama kijichi au mbagala kuu ile ya ustaarabuni vipi
mtoni kijichi zipo na mbagara kuu zipo naomba niambie budget yako na ni lini unahitaji maana kijichi zipo nyumba kama 4 hv 2 ni za beach hizi 2 zingine ziko maeneo ambayo sio beach naomba niamba niambie budget yako na aina ya nyumba uitakayo kisha nitakujibu au ni pm
mkuu najua utakuwa unafahamu bei ya hizi ulizosema hapa hebu taja bei kwa kila moja kuanzia hizo za beach na nyinginezo
hizi za beach 500 350 na hizo zingnia 300 200
mbagara kuu kuna ya 150 inashuka mpaka 120 hv na ingine inauzwa 70 lakini gari haifiki hapo
ina majini usiku ukiingia utatamani mwenyewe ukalale makaburini kuliko humo ndani
na humo ndani ukilala usiku ukiamka unajikuta uko juu ya mti | 2019-04-22T02:19:14 | https://www.jamiiforums.com/threads/nyumba-hii-inauzwa.366065/ |
waziri biteko aitaka halmashauri ya uvinza kuratibu uanzishwaji soko la chumvi ministry of minerals
waziri biteko aitaka halmashauri ya uvinza kuratibu uanzishwaji soko la chumvi
waziri wa madini doto biteko ameuagiza uongozi wa halmashauri ya uvinza ukishirikiana na kiwanda cha chumvi cha uvinza pamoja na ofisi ya madini mkoani kigoma kujadili namna ya kuanzisha soko la chumvi katika halmashauri hiyo
maelekezo hayo yametolewa kufuatia maombi ya wananchi wa halmashauri hiyo ya uvinza kulalamikia ukosefu wa soko la kuuzia bidhaa hiyo na kuiomba serikali kufanya utaratibu wa kufungua soko ili kuwawezesha kufanya biashara yao mahali salama
waziri wa madini doto biteko akitembelea shughuli za uzalishaji wa madini ya chumvi wilayani uvinza
agizo hilo limetolewa tarehe 29 july 2019 katika ofisi za kiwanda cha chumvi cha uvinza mara baada ya waziri biteko na ujumbe alioambatana nao kuwasili kwa lengo la kuzungumza na uongozi wa kiwanda hicho ili kuweka sawa mambo mbalimbali yaliyowasilishwa na wananchi wakati wa mkutano baina ya waziri biteko na wachimbaji wadogo pamoja na wananchi wa uvinza
moja kati ya malalamiko yaliyomfikia waziri biteko ni malipo duni ya ujira kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho ambapo aliutaka uongozi wa kiwanda hicho kujadili na kufikia maamuzi ya kuongeza ujira kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho waliodai kulipwa ujira mdogo
aidha biteko aliutaka uongozi wa kiwanda hicho kufanya marekebisho hayo mpaka ifikapo tarehe mosi mwezi agosti 2019 mara baada ya kiwanda kufanya mahesabu na kujiridhisha juu ya kiasi kinachobaki baada ya kutoa gharama za uwekezaji kiongezwe katika malipo hayo ya ujira
akijibu hoja ya baadhi ya wananchi wa uvinza waliolalamikia uongozi wa kiwanda hicho kuuza chumvi inayozalishwa kiwandani hapo hiyo bei kubwa inayowafanya walanguzi hao kupata faida kidogo biteko aliutaka uongozi wa kiwanda hicho na wachimbaji wengine wa chumvi wilayani humo kupunguza bei hiyo ili kuiwezesha jamii inayowazunguka kunufaika na uwepo wa chumvi katika mji wao
biteko aliutaka uongozi wa kiwanda cha chumvi kuwapa wananchi sababu ya kuwapenda kwa kuwatendea mema aliendelea kwa kusema mtu mwenye kurekebisha bei ya chumvi kwa manufaa ya wafanyabiashara wadogo ni mwekezaji mkubwa ifanye jamii hii iugue siku ukiwa haupo ifanye jamii ikukumbuke kwa mema yako biteko alisisitiza
pamoja na hayo waziri biteko aliutaka uongozi wa halmashauri ya uvinza ofisi ya madini ya mkoa wa kigoma pamoja na uongozi wa kiwanda kukutana na kujadili namna na mahali patakapofaa kwa ajili ya kuanzisha soko la madini ili kuwaondolea adha ya soko la chumvi wananchi wa uvinza
kufuatia malalamiko ya wananchi wa uvinza ya kutozwa kiasi cha tzs 500 ya ushuru kwa kila kilo 25 za chumvi waziri biteko aliiagiza halmashauri ya uvinza kufuta tozo hiyo na kueleza kuwa tozo hiyo haipo chini ya mamlaka yake na hivyo haitambui
matukio mbalimbali wakati wa ziara ya waziri wilayani uvinza
akijibu kero ya mwananchi wa uvinza aliyejulikana kwa jina la yona william gwagula kwa niaba ya wanakikundi wa twikome salt kinyo chakuru juu ya watu waliokuwa wakiwatoza kodi kwa madai kuwa leseni iliyokuwa ikichimbwa na wanakikundi hao ni ya kwao jambo lililobainika kuwa si kweli waziri biteko alimtaka afisa madini mkazi wa mkoa wa kigoma david william ndosi kuifuta leseni hiyo mara moja na kuwapa wachimbaji hao wadogo ili waweze kuendeleza shughuli zao
kwa upande wake katibu wa wachimbaji wadogo wa wilaya ya uvinza hamisa omari kambi akiwasilisha changamoto wanazokumbana nazo alisema ni pamoja na maeneo yao kuvamiwa ukosefu wa vitendea kazi halmashauri kutowapa kipaumbele wamiliki wa leseni kwenye tenda za serikali pamoja na kuomba kurahisishwa kwa utolewaji wa vibali vya kusafirisha madini nje ya nchi ambapo changamoto zote zimepatiwa ufumbuzi
waziri biteko atakuwepo mkoani kigoma kwa ziara ya siku mbili ambapo atafanya majadiliano na ofisi ya mkoa wakishirikiana na ofisi ya tume ya madini ili kujadili namna bora ya kuimarisha soko la madini litakalowezesha kuweka mazingira rafiki na salama kwa ajili ya nchi jirani ya kongo kutokana na kuonesha nia ya kushirikiana na tanzania katika biashara ya madini kupitia masoko yaliyoanzishwa hususani mkoani kigoma
total 236029 | 2019-08-23T01:44:14 | https://www.madini.go.tz/waziri-biteko-aitaka-halmashauri-ya-uvinza-kuratibu-uanzishwaji-soko-la-chumvi/ |
kesi 457 dhidi ya jamiiforums upande wa jamhuri wafunga ushahidi mahakama kutoa uamuzi mei 3 mwaka huu | fikrapevu
hatimaye upande wa jamhuri katika kesi inayoikabili jamiiforums imekamilisha kutoa ushahidi wake na kuipa nafasi mahakama ya hakimu mkazi kisutu kuamua kama kuna kesi ya kujibu au la
katika kesi hiyo namba 457 jamiiforums inashitakiwa na kampuni ya cusna investment na oceanic link ambayo ilidaiwa kufoji nyaraka bandarini kukwepa kodi na kuwatesa wafanyakazi wazalendo na kupendelea wageni toka nje ya nchi
uamuzi huo umefikiwa leo mbele ya hakimu godfrey mwambapa ambaye anasikiliza kesi hiyo upande wa jamhuri ukiongozwa na wakili nassoro katuga kufunga ushahidi na kuiachia mahakama jukumu la kupitia ushahidi walioutoa ili kubaini kama upande wa washatakiwa wana kesi ya kujibu
ikumbukwe kuwa kesi hiyo ilianza kusikilizwa mwaka 2016 na mpaka leo upande wa jamhuri ulifanikiwa kuwaleta mahakamani mashahidi wa tano kutoka jeshi la polisi wakala wa kusajili biashara na leseni na kampuni ya cusna investment na oceanic link kutoa ushahidi wao
shahidi wa kwanza alikuwa inspekta monica pambe kutokana jeshi la polisi kitengo cha makosa ya mtandao mwingine ni asp fadhiri bakari ambaye ni mkuu wa kitengo cha uhalifu wa fedha kanda maalumu ya dar es salaa ambaye alitoa ushahidi wake desemba 5 2017
wengine ni msajili msaidizi mkuu wa makampuni rehema kitambi kutoka brela ambaye alitoa ushahidi wake juu ya kusajiliwa kwa kampuni ya jamiiforums shahidi wa nne alikuwa jonas wilson mcharo kutoka cusna investment and oceanic link ambapo aliwasilisha kielelezo kinachodaiwa kuwa ni andiko lenye maudhui ya kuichafua kampuni yao linalodaiwa kuwekwa kwenye mtandao wa jamiiforums lakini mahakama ilikataa kupokea kielelezo hicho kwasababu hakikudhi matakwa ya kisheria
shahidi wa tano na wa mwisho alikuwa ni loy mhando naibu msajili wa alama na huduma kutoka brela ambapo leo upande wa jamhuri umeamua kufunga ushahidi wao ili kutoa nafasi kwa mahakama kutoa uamuzi kama kuna kesi ya kujibu au la
baada ya wakili katuga kumaliza kutoa maelezo yake na kufunga ushahidi hakimu mwambapa uliugeukia upande wa utetezi ambao ulikuwa ukiongozwa na wakili jeremiah mtobesya ambaye aliiomba mahakama iwapatie muda wa kupitia ushahidi ili kutoa utetezi wao kabla ya mahakama hiyo haijatoa uamuzi wa kesi
hakimu mwambapa alikubali ombi hilo la upande wa utetezi ambapo aliwataka hadi aprili 9 mwaka huo wawe wamewasilisha ombi lao la kujitetea dhidi ya ushahidi uliotolewa na jamhuri kwa upande mwingine jamhuri wametakiwa hadi kwa aprili 23 2018 kujibu hoja za upande wa utetezi (counterreply)
hata hivyo hakimu mwambapa amebainisha kuwa mahakama itatoa uamuzi kama kuna kesi ya kujibu au la siku ya 3 mei 2018 ambapo watakutana tena mahakamani hapo
kesi ilikotoka
katika kesi hii polisi walitaka jamiiforums iwapatie taarifa za mwanzisha mada na mchangiaji mmoja ili waweze kuwakamata na kuwahoji wakidai kuwa kampuni ya cusna investment na oceanic link ilichafuliwa
jamiiforums inadaiwa ilikataa kutoa taarifa binafsi za wanachama wake kwa kuamini kuwa chanzo hicho cha taarifa kilikuwa na nia njema hivyo kutaka kwanza iwepo hati ya mahakama inayoridhia kukamatwa kwa wahusika na kuelezwa kosa lililofanywa na wahusika
kutokana na msimamo huo wa jamiiforums maxence melo alikamatwa disemba 13 2016 na kufikishwa mahakamani disemba 16 2016 akishtakiwa kwa makosa 3 ikiwemo kuendesha mtandao wa jamiiforums bila kutumia kikoa cha tz ambacho kina usajili wa tanzania
shtaka lingine ni lile lilofunguliwa na kampuni ya oilcom ambayo inadai ilichafuliwa na jamiiforums kutokana taarifa iliyowekwa kwenye mtandao huo kuwa kampuni hiyo inakwepa kodi na kuchakuchua mafuta bandarini
kufuatilia mlolongo wa yale ambayo yamekuwa yakijiri katika kesi hizo 3 fuatilia hapa kinachojiri mahakama ya kisutu kesi ya jamhuri dhidi ya jamiiforums | 2019-09-16T00:57:00 | http://www.fikrapevu.com/kesi-457-dhidi-ya-jamiiforums-upande-wa-jamhuri-wafunga-ushahidi-mahakama-kutoa-uamuzi-mei-3-mwaka-huu/ |
mtazamo wangu (mac temba jr) editor contact email is mactemba@hotmailcom a moment with my md in share n care
a moment with my md in share n care
hapo ilikuwa siku ya uzinduzi wa kampeni ya kusaidia watoto yatima share & carepichani md wa vodacom dietlof mare akipozi na mdau wa blog hii mac temba jrhapo kati ni mkuu wa kitengo cha hr wa vodacom mama stella kiwango
posted by the editor edwin mac temba at 543 am | 2017-08-18T10:59:25 | http://mactemba.blogspot.com/2010/01/moment-with-my-md-in-share-n-care.html |
(showing articles 11861 to 11880 of 37912)
07/25/151330 _rais jakaya kikwete
07/26/150629 _madaktari diaspora
07/26/150717 _chama cha ukombozi
07/26/150726 _mahojiano na charle
07/27/150049 _bonny mwaitege kuzi
07/27/150104 _phidesia mbunge vit
07/27/150134 _makundi 5 yang'ara
07/27/150142 _the rise of the blo
07/27/150349 _unesco kuendelea ku
07/27/150420 _mdau yahya kiyabo a
07/27/150554 _chuo cha taifa cha
07/27/150616 _benki m yaadhimisha
07/27/150648 _mbunge chiku abwao
07/27/150651 _wadau wa utamaduni
07/27/150726 _mamlaka ya chakula
07/27/150750 _unesco kuendelea ku
older | 1 | | 592 | 593 | (page 594) | 595 | 596 | | 1896 | newer
07/25/151330 rais jakaya kikwete aongoza watanzania kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa
rais jakaya kikwete akiwaaga baadhi ya mashujaa waliopigana vita kuikomboa tanzania
rais akiweka mkuki na ngao kwenye mnara wa uhuru
mkuu wa majeshi jenerali davis mwamunyange akirejea kwenye sehemu yake baada ya kuweka sime kwenye mnara
makamu wa rais dkt bilal makamu wa pili wa rais wa zanzibar balozi iddi na spika wa bunge anne makinda wakiondoka kwenye viwanja vya mnazi mmoja
baadhi ya askari wa jwtz waliopigana vita ya kuikomboa tanzania
brass bendi ya jeshi ikiingia kwenye viwanja vya mnazi mmoja kuanza maadhimishopicha zote na hussein makamemaelezo
mnadhimu mkuu wa jeshi la ulinzi la wananchi wa (jwtz) luteni jenerali samweli ndomba akisalimiana na waziri wa ujenzi dkt john magufuli baada ya kuwasili viwanja vya mnazi mmoja
spika wa baraza la wawakilishi pandu ameir kificho akiwasili
spika wa bunge la jamhuri anne makinda akiwasili
makamu wa pili wa rais wa zanzibar balozi seif ally idd
makamu wa rais wa serikali ya jamhuri dkt mohamed gharib bilal akiwasili
rais jakaya kikwete akiwasili
rais jakaya kikwete akiwaongoza viongozi mbalimbali na wananchi kuimba wimbo wa taifa
kiongozi wa mabalozi akiweka shada la amaua
mstahiki meya wa jiji la dar es salaam dkt didas masaburi akiwa ameweka upinde na mshale kwenye mnara
mwenyekiti wa tanzania legion akiweka shoka kwenye mnara
baadhi ya wazee walioipigania tanzania viongozi wa dini na wageni waalikwa waliohudhuria
sheikh wa mkoa wa dar es salaam sheikh alhad musa salum akisoma dua
mchungaji theophil bolampete wa kanisa katoliki akiomba
mchungaji john komoyo akiomba
rais jakaya kikwete akiongoza viongozi mbalimbali kuimba wimbo wa taifa baada ya maadhimisho kukamilika
baadhi ya wananchi waliofika nje ya viwanja vya mnazi mmoja kushuhudia maadhimisho
07/26/150629 madaktari diaspora kutoka marekani watowa huduma ya elimu kwa wanafunzi wa chuo cha eilimu ya afya
mkurugenzi wa idara ya ushirikiano wa kimataifa diaspora zanzibar ndg adila hilal vuai akiutambulisha ujumbe wa madaktari diaspora kutoka washington walioletwa na jumuiya ya watanzania wanaoishi washington wakali walipofika katika chuo cha elimu ya afya zanzibar walipofika hapo kutowa elimu ya afya ya saratani ya matiti na mano wakiwa zanzibar kwa uwenyeji wa idara ya ushirikiano wa kimataifa diaspora na benki ya watu wa zanzibar (pbz)
rais wa jumuiya ya watanzania washinton ndg iddi sandaly akiutambulisha ujumbe wa madaktari 17 diaspora waliofika zanzibar kutoa tiba ya maradhi ya saratani ya matiti kisukari na meno akitowa maelezo wakati walipofika katik chuo cha elimu ya afya mombasa zanzibar na kutowa elimu ya kutambua saratani ya matiti kwa kinamama na kutowa huduma ya uchunguzi wa meno
rais wa jumuiya ya wanawake afrika washington (africa womens cancer awereness association ) dr ify anne nwabukwu akiutambulisha ujumbe wa madaktari wa maradhi mbalimbali waliowasili zanzibar kwa ajili ya kutowa huduma kwa wananchi wa zanzibar ikiwa ni kusaidia wafrika wenzao walioko afrika
wanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar wakimsikiliza dr ify akitowa maelezo na kuwatambulisha madaktari diaspora aliofuatana nao
dr ify anne nwabukwu akitowa elimu ya tambua viashiria vya saratani ya matiti kwa wanafunzi hao wa chuo cha elimu ya afya zanzibar
dr ify akitowa mada kuhusiana na saratani ya matiti kwa wanafunzi wa chuo hicho hutoa elimu ya udaktari wa aima mbalimbali chuoni hapo
dr ify akionesha mashine ya kupimia saratani ya matiti ya kisasa inayoitwa mamagram hutumika kucunguza viashiria vya saratani ya matiti kwa wanachuo hao wakati akitowa elimu ya saratani ya matiti jinsi ya kumgundua mwanamke mwenye matatizo hayo
wanafunzi wa chuo hicho wamepata fursa ya kuuliza mswali wakati wa mafunzo hayo
mmoja wa madaktari hayo akitowa mfano hai kutokana na matatizo ya saratani ya matiti kwa wanachuo hao
daktari wa meno bi queenate ibeto akitowa elimu ya kutunza meno na kinga ya mane kwa wanafunzi hao jinsi ya kuyatunza meno wakati walipofika chuoni hapo kutowa elimu kwa wanachuo hicho
daktari wa meno venessal quitero akionesha moja ya tiba ya kunusuru meno kwa wanafunzi hao wakati wakitowa elimu ya utunzaji wa meno na tiba yake
mwanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar akionesha mafunzo ya utunzaji wa meno kwa vitendo jinsi ya kupiga msuwaki inavyotakiwa kuweza kuimarisha meno kuwa imara
dr queenate ibeto akionesha mfano ya vitendo kwa mmoja wa mnafunzi wa chuo hichi jinsi ya utumiaji wa msuaki katika kupiga kwa wanafunzi hao wakati walipofika kutoa elimu ya afya kwa wanafunzi wa chuo hicho mombasa zanzibar
profesa hailu na dr quintero wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwakilishwa kuhusiana na saratani ya matiti na tiba ya meno kwa wanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar mombasa wakati walipofika katika chuo hicho wakiwa zanzibar kwa ajili ya kutoa tiba ya saratani ya matiti ugonjwa wa kisukari na meno
dr quintero ni mtaalamu ya magonjwa ya meno akifafanua moja ya swali lililoulizwa na wanafunzi wa chuo hicho
mwanafunzi wa chuo hicho akiuliza swali kuhusiana na baadhi ya wananchi meno yao huwa na ukungu mweusi kwa wataalam hao
madaktari wa diaspora wakigawa misuwaki na dawa za meno kwa wanafunzi hao baada ya kutowa elimu chuoni hapo
dr silvia dasi akitowa maelezo kwa wanafunzi hau jinsi ya kumgundua mwanamke mwenye matatiti ya saratani ya matiti wakati wakifanya mafunzo hayo kwa wanafunzi hao wanaochukua elimu ya afya ya binadamu
dr ify akitowa elimu ya vitendo kugundua viashiria vya saratani ya matiti kwa mwanamke akitowa mafunzo hayo ya mmoja wa mwanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar
dr ify akitowa elimu ya vitendo kugundua viashiria vya saratani ya matiti kwa mwanamke akitowa mafunzo hayo ya mmoja wa mwanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar kulia mkurugenzi wa ushirikiano wa kimataifa diaspora zanzibar ndg adila hilal vuai
madaktari diaspora wakiwa katika picha ya kumbukumbu na wanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar baada ya kutoa elimu kwao
dr queenate ibote akimfanyia uchunguzi wa meno mmoja wa wanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar wakati walipofika chuoni hapo kutowa elimu kwa wanachuo hicho
madaktari wa diaspora wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa chuo cha elimu ya afya zanzibar wakiwa nje ya jengo la chuo hicho katika skuli ya sekondari ya shaa mombasa zanzibar picha na othmanmaparablog zanzinewscom
07/26/150717 chama cha ukombozi wa umma (chaumma) chamtangaza mgombea kiti cha urais wa zanzibar kupitia chama hicho
naibu katibu mkuu wa chama cha ukombozi wa umma zanzibar (chaumma) faki salum abdalla akitoa salamu za chama hicho wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) wa kumtambulisha mgombea urais wa zanzibar kupitia chama hicho katika ukumbi wa umoja wa watu wenye ulemavu kikwajuni mjini zabnzibar
picha no 2152 baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza mgombea nafasi ya rais wa zanzibar kupitia chaumma katika ukumbi wa umoja wa watu wenye ulemavu kikwajuni mjini zanzibar
baadhi ya wanahabari waliohudhuria mkutano huo
katibu mkuu wa chaumma ali omar juma akitowa wasfu wa mgombea nafasi ya rais wa zanzibar kupitia chama hicho katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ukumbi wa umoja wa watu wenye ulemavu kikwajuni mjini zanzibar
mgombea kiti cha rais wa zanzibar kupitia chama cha ukombozi wa umma (chaumma) mohd masoud rashid akijitambulisha na kueleza sera zake mbele ya waandishi wa habari katika ukumbi wa umoja wa watu wenye ulemavu kikwajuni mjini zanzibar (kulia) mgombea mwenza wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania kupitia chama hicho issa abass na (kushoto) katibu mkuu ali omar juma picha na makame mshengamaelezo znz
07/26/150726 mahojiano na charles magali ndani ya washington dmv
charles magali akiwa ndani ya kilimanjaro studio zinazomilikiwa na vijimambo radio kwanza production na nesiwangu media
ijumaa ya julai 24 2015 mwigizaji na mwimbaji wa muziki nchini tanzania charles magali alipata fursa ya kutembelea studio zetu zilizopo beltsville maryland hapo akazungumza nasi kwa ufupikaribu umsikilize akihojiwa na mbunifu na mtayarishaji wa kipindi hiki dj luke joe na mubelwa bandio
07/27/150049 bonny mwaitege kuzindua albamu tatu kwa mpigo agosti 2 jijini dar
mkurugenzi wa msama promotions alex msama amewaita maaskofu na viongozi wengine wa dini katika uzinduzi wa albamu tatu za mwimbaji nguli bonny mwaitege zinazotarajia kuzinduliwa agosti 2 kwenye ukumbi wa diamond jubilee jijini dar es salaam
kwa mujibu wa msama ambaye ni mdhamini wa uzinduzi huo maaskofu watafikisha ujumbe wa neno la mungu kwa karibu zaidi baada ya waimbaji kumaliza kazi yao jukwaani
msama alisema uzinduzi huo unatarajia kusindikizwa na waimbaji mbalimbali wa tanzania na nje lengo likiwa ni kufanikisha uzinduzi mahiri wa albamu hizo msama alisema pamoja na uzinduzi huo kusindikizwa na waimbaji mahiri pia waimbaji chipukizi watamsindikiza mwaitege ambaye hivi sasa anaendelea na mazoezi kuelekea uzinduzi huo
aidha msama alisema hivi sasa muimbaji huyo pia anamalizia kurekodi baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hizo katika majiji ya mwanza arusha mbeya na nairobi msama alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa mashabiki wa muziki wa injili kujiandaa na uzinduzi huo ambao utakuwa ni wa aina yake
maandalizi makubwa kuelekea uzinduzi wa mwaitege yameshafanyika kilicho mbele ni uzinduzi wa hali ya juu mashabiki wakae mkao wa kula alisema msama na kuongeza uzinduzi wa mwaitege utakuwa ni wa aina yake kwa sababu maandalizi yake kwa sababu yamefanywa kwa ustadi mkubwa mashabiki watarajie kazi bora zaidi kutoka kwa muimbaji huyo alisema
bonny mwaitege anatamba na nyimbo mbalimbali kama mama ni mama mke mwema wakusamehe fungua moyo wako njoo uombewe na yesu yupo
07/27/150104 phidesia mbunge viti maalum awataka wananchi wasirubuniwe
kada maarufu wa chama cha mapinduzi ambaye pia ni mfanyabiashara wa madini jijini arusha justine nyari anayeomba ridhaa ya ccm katika nafasi ya ubunge akiteta jambo na mbunge viti maalum wazazi phidesia mwakitalima ambaye pia ni afisa masoko wa triple a na mkurugenzi wa phide entertainment kabla ya mkutano wao wa kujinadi kuanza
mbunge viti maalum wazazi phidesia mwakitalima ambaye pia ni afisa masoko wa triple ana mkurugenzi wa phide entertainment akibadilishana mawazo na wakili msomi edimond ngemela anayeomba ridhaa ya ccm katika nafasi ya ubunge
mbunge viti maalum wazazi phidesia mwakitalima ambaye pia ni afisa masoko wa triple a na mkurugenzi wa phide entertainment akiwa katika picha ya pamoja na watia nia nafasi ya ubunge kupitia chama cha mapinduzi ccm
mbunge viti maalum wazazi phidesia mwakitalima ambaye pia ni afisa masoko wa triple ana mkurugenzi wa phide entertainment akisalimiana na mtia nia nafasi ya ubunge kupitia chama cha mapinduzi ccm thomas munisi ambapo mwakitalima aliibuka mshindi katika kura za maoni za kutafuta wabunge wa viti maalum mkoa wa arusha kupitia jumuiya ya wazazi wa chama cha mapinduzi ( ccm )
mbunge viti maalum wazazi phidesia mwakitalima ambaye pia ni afisa masoko wa triple a akisalimiana na wadau ambao ni watia nia ubunge na udiwanikushoto ni simba salum anayeomba chama cha mapinduzi kumpitisha kuwania nafasi ya udiwani mtaa wa kati bondeni na kulia wakili msomi edimond ngemela anayeomba ridhaa ya ccm katika nafasi ya ubunge
07/27/150112 benki ya exim yaendesha droo ya kwanza kampeni ya akaunti ya malengo
the smart boy galaxy ikanda akiwa maejipanga fresh kwa ujio wake mpya alielezea sababu zinazompelekea kutumia muda wake mwingi kujipanga na sio kukurupuka muziki umekuwa na ushindani mkubwa sana kiasi inampelekea msanii makini kuongeza umakini na ubunifu kwenye utendaji otherwise unaweza kujikuta kila siku umesimama sehemu moja huendi mbele kitu ambacho sikitarajii kulingana na jitihada nilizonazo
07/27/150134 makundi 5 yang'ara ndani ya temeke kwenye usaili wa kwanza dance 100 2015 temeke
pichani juu kati ya makundi matano yaliyopita kwenye usaili wa kwanza wa dance 100 (2015) temeke kundi linaitwa 'the best boys kaka zao'
shabiki wa kundi la 'noma sana' akiwa anajitayarisha kushangilia timu yake kwenye usaili wa kwanza temeke kwenye dance 100 (2015)
washiriki wa kundi la 'noma sana' mwaka huu kwenye dance 100 wakiwa wanafanya yao viwanja vya tcc changombe
watangazaji rasmi wa dance 100 tbway 360 na maggie vampire wakiwa wanasherehesha kikamilifu huku burudani mbalimbali zikijiri tcc changombe
07/27/150142 the rise of the blog entrepreneur krantz mwantepele
dedicated professional eager to succeed innovative and passionate are just some of the words used to describe krantz charles mwantepele he realized there was a deficiency and opportunity in internet marketing but did not wait for changes he made them happen with no it background just a passion for news reporting he has successfully
who prompted you to start your blog
i have always been interested in media and news reporting from my early stages throughout my ordinary and advanced level studies i have been involved with the school magazine and the school newsletter in my school days i would go to the library read on current issues and report it to my peers of course on the journey to starting mwanaharakati mzalendo i drew inspiration from bloggers like michuzi and haki ngowi
i am sure you write with a purpose and a particular segment of the society tell me who is a mwanaharakati mzalendo
anybody and everybody is mwanaharakati mzalendo so to speak earlier on during my school days in seminary school i realized that many youth were not interested in current global affairs so i set out my blog to capture the young person since i already had the content for the more mature section of society now there is something for everybody the student the working man/woman the entrepreneur for me and for you we are all mwanaharakati mzalendo
we are more and more of an interest in many people on the internet and in blogging i am curious with all these blogs around what gives mwanaharakati mzalendo that edge above the competition
key aspect is originality i come up with my own content as opposed to taking it down and pasting in to my space i have a friendly approach to the readers giving out my contact information so they can give comments feedback or stories they would like us to follow up on recently i opened up an application with google play by the name of my blog look it up we are objective and never post content that makes someone target to ridicule or hatred of any kind we believe in hard hitting news that benefits our readers we also give previews and references on our sites for more understanding
discipline to post interesting topics frequently is often cited as one of the requirements to a successful blog what other factors in your opinion can make a blog successful
forming relationships with the readers interactive posts tips on various subjects like love and life i also have
great communication with some other bloggers the key is realizing that it is not about competition its about bettering yourself and accepting that you do not know everything every once in a while someone will beat you to that story i do post the news to my readers but make sure to give them their due credit
is it possible for someone to have a blog as his full time income generating business or are blogs simply side projects that can earn people some extra income
yes it is very possible it has to be your passion and profession like with kenyans and nigerians i blog on my own free time and i recently have hired two more individuals to assist me with marketing and it
these two have degrees in their respective fields and earn incomes from the work they do on mwanaharakati mzalendo like all jobs it needs commitment to blogging all day and being on media as much as possible you do not want to miss a
thing in this business mwanaharakati mzalendo has been known for breaking the news first thats how you do it
you have reputable companies advertising with your blog how long did it take you to get the first company to advertise with you
two years it was after winning the tanzania blog award for best political blog and first runner up for best news
blog in 2012 it was a uk based company called serengeti clearers and forwarders in the beginning i offered them
the space for free as a trial run but after a month i started to receive commissions from them they were impressed with the response
to be recognized beyond national borders as an international blog and it has already started with the nomination i received this year for the best educational and political blog from the african blog awards 2014 it takes me and this blog to another level i am ecstatic
what advice do you give to anyone who would like to start a blog that generates income
content give people what they want with someone you are proud of professionalism know what you are about
and stick to it set goals as to what your blog is about and what it is for keep it fresh and always try to give it new looks every now and then love what you do and last but not least creativity matters
you can visit wwwmwanaharakatimzalendoblogspotcom
wwwharakati360blogspotcom
wwwmzalendotimesblogspotcom
credit http//wwwmanmagazinecotz
07/27/150349 unesco kuendelea kusaidiana na tanzania kuinua elimu
alisema unesco ipo tayari kuhakikisha kwamba tanzania inazalisha wanafunzi ambao watakuwa na uwezo mkubwa katika tehama ambao utaibua maendeleo endelevusi kutoa walimu wazuri tu bali kuwezesha jamii wanafunzi na waliopitia mafunzo hayo kuwa na namna mpya ya kufikiri na kuvumbua vitu vipya vya kujiendelea na kuendeleza taifa alisema yusuph
alisema kimsingi elimu inatoa asilimia 5 lakini maisha yanatoa asilimia zilizobaki kama mtu atatumia vyema msingi wa maarifa aliyopewa
naye mratibu wa kitaifa wa mradi wa cfit kutoka unesco faith shayo alisema kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya mafunzo na matumizi ya maabara katika vyuo vya monduli na tabora katika kufunza tehama ili kuboresha mafunzo na ufundishaji
leo tuko hapa bagamoyo kwa ajili ya wadau kudiscuss ict draft document (kujadili hati hii yenye draft ya mafunzo) ambayo ilipitiwa na watu watano kabla ya kuikabidhi kwa wizara ya elimu alisema faith
alifafanua kwamba mradi huo ambao awali ulifadhiliwa na benki ya dunia na kukamilika mwaka 2011 haukuridhiwa kutumika hadi mwaka jana ulipokuja mradi wa cfit ambao uliingizia upitiaji upya wa mradi huo na kuwezesha kuridhiwa kwa matumizi
naye kiongozi wa timu iliyopitia awali katika mradi huo wa cfit profesa ralph masenge amesema wataalamu waliohusika na upitiaji huo kabla ya kongamano walitoka chuo cha ualimu tabora na kile cha mondulichuo kikuu huria tanzania na chuo kikuu cha dar es salaamalisema awali walipitia kuona mahitaji maalumu ya walimu kisha wakaja na mapendekezo ambayo sasa yanafanyiwa kazi
alisema matatizo mengi ya elimu tanzania yanatokana na uhaba wa vifaa vya elimu na ubora wa walimualisema mradi huo utasaidia kutoa elimu bora kwa kuwa na walimu bora na vifaa bora kupitia tehama alisema mradi huo utasaidia kuwezesha tehama kutumiwa kama chombo cha kutumia wanafunzi hasa pale panapokosekanaprofesa masenge alisema hatua waliyofikia ni hatua ya matayarisho na kwamba ni matarajio yao kwamba wakishafikisha hati hiyo kwa wizara masuala ya matumizi ya maabara yatakuwa yamekamilika
pichani juu na chini ni washiriki wakiwasilisha mawazo yao wakati kongamano likiendelea kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha waraka huo
washiriki wa kongamano hilo wakifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikiwasilishwa
07/27/150420 mdau yahya kiyabo achukua jiko
maharausi wakikata keki kuashilia upendo katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa danken housemikocheni jijini dar es salaam
bwanaharusi yahaya kiyabo akimlisha keki biharusiaisha kirapo katika hafla iliyfanyofanyika katika ukumbi wa danken housemikocheni jijini dar es salaam
biharusiaisha kirapo akimlisha keki bwanaharusi yahya kiyabo katika hafla iliyfanyofanyika katika ukumbi wa danken mikocheni jijini dar es salaam
bwanaharusi yahya kiyabo akiwakabidhi baadhi ya wafanyakazi wenzake wa benki ya crdb keki katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa dunken housemikochenijijini dar es salaam
baadhi wa washiriki katika hafla hiyo wakisubiri keki katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa danken housemikocheni jijini dar es salaam
mama mzazi wa bwanaharusi wakifurahia jambo kwa pamoja
maharusi wakipeleka keki kwa wakwe hawapo pichani katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa dakanmikocheni jijini dar es salaam
07/27/150554 chuo cha taifa cha utalii wazindua kiota cha burudani
mkurugenzi mtendaji wa chuo cha taifa cha utalii rosada musoma akizindua kwa kukata utepe kiota cha burudani cha goldbar and restaurant katika chuo cha taifa cha utalii kampasi ya dar es salaam mwishoni mwa wiki
mkurugenzi kitengo cha biashara wa chuo cha taifa cha utalii (nct)neema chololo kusiga akizungumza mara baada ya uzinduzi wa kiota cha burudani cha goldbar and restaurant kilichopo katika chuo cha taifa cha utalii kampasi ya dar es salaam mwishoni mwa wiki
mkurugenzi mtendaji wa chuo cha taifa cha utalii rosada musoma akizungumza mara baada ya kuzindua goldbar and restaurant katika chuo hicho mwishoni mwa wiki jijini dar es salaam katika ukumbi wa chuo cha taifa cha utalii kampasi ya bustani
picha ya pamoja ya wafanyakazi wa chuo cha taifa cha utalii kampasi ya bustani mara baada ya kuzindua goldbar and restaurant katika chuo hicho uzinduzi uliofanyika katika jijini dar es salaam mwishoni mwa wiki
wana kamati ya maandalizi wakiwa katika picha ya pamoja wakiongozwa na afisa masoko wa chuo cha taifa cha utalii waheeda mohamed
vitu vipatikanavyo katika chuo cha taifa cha utalii kampasi ya bustani jijini dar es salaam
bendi kitumbuiza katika uzinduzi wa
goldbar and restaurant katika chuo cha taifa cha utalii uzinduzi uliofanyika katika jijini dar es salaam mwishoni mwa wiki
mkurugenzi kitengo cha biashara wa chuo cha taifa cha utalii (nct)neema chololo kusigaakiwa na mfanyakazi wa chuo hicho
afisa manunuzi mkuu wa masoko wa chuo cha taifa cha utaliielizabeth kasawara akiwa katika pozi mara baada ya
kiota cha burudani cha goldbar and restaurant katika chuo cha taifa cha utalii kampasi ya dar es salaam mwishoni mwa wiki
mkurugenzi mtendaji wa chuo cha taifa cha utalii rosada musoma akiwa na wafanyakazi wa chuo cha taifa
07/27/150616 benki m yaadhimisha miaka 8 toka ilipoanzishwa
benki m yaadhimisha miaka 8 toka ilipoanzishwa pichani ni naibu mkurugenzi mkuu wa benki m bi jaqueline woiso katika mkutano na waandishi wa habari wikiendi hii katika ukumbi wa hoteli ya hyatt regency kuelezea mafanikio waliyopata katika kipindi hicho cha miaka 8 kulia ni mkurugenzi wa mawasiliano wa benki hiyo bw allan msalilwa
bank m tanzania plc leo inatimiza miaka 8 toka ilipoanzishwa july 27 2007 akiongea na waandishi wa habari naibu mkurugenzi mkuu wa benki hiyo bi jacqueline woiso alisema wanaadhimisha miaka minane yenye mafanikio makubwa mwaka 2007 tulifunga mwaka tukiwa na rasilimali zenye thamani ya tzs 32 billioni tu na sasa tumefikia kiasi cha tzs 800 billioni tumekuwa tukifanya vizuri katika masoko kwa muda mrefu na tulifanikiwa kuanza kupata faida ndani ya miaka miwili (2) tu toka kuanzishwa kwa benki yetu kwa mwaka huu hadi kufikia june 2015 tumepata faida ya tzs 115 billioni
alisema kuwa benki hiyo ilianza na kiasi kidogo sana cha tzs 16 billioni hadi kufikia tzs 630 billioni huku mtaji ukiwa pia umeongezeka kutoka tzs 65billioni hadi kufikia tzs 84 billioni kwa sasa huku idadi ya wafanyakazi pia imeongezeka kutoka 40 hadi 236 kwa uwiano wa asilimia 50 kati ya wanaume na wanawake
kwa upande wa huduma kwa wateja bi woiso alisema kuwa benki m imekuwa ni benki ya kwanza kutoa huduma masaa 12 kila siku kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa mbili usiku siku 7 za wiki yaani jumapili hadi jumapili pia tunatoa garantii endapo tutazidisha muda tuliokubaliana kufanikisha miamala ya wateja huduma hii inajulikana kama ssg (service standard guarantee) aliongeza
benki hiyo pia imekuwa ikishiriki kwa kiasi kikubwa katika kusaidia jamii ikiwa ni moja ya sera kubwa za benki hiyo ambayo huiita money@heart alisema woiso tunashirikiana na taasisi mbalimbali katika kufanikisha miradi mingi kwenye jamii katika sekta ya afya elimu maji utunzaji wa mazingirana pia kuwainua wajasiriamali na wasanii wa michoro ya asili nchini
pia alisema kuwa wamefanikiwa kupata tuzo mbalimbali za kimataifa ikiwemo tuzo ya benki bora ya biashara kwa mwaka 2015 iliyotolewa katika soko la hisa la london benki bora katika sekta ya biashara za makampuni afrika mashariki na benki bora inayoshiriki katika maendeleo ya jamii afrika mashariki zilitolewa na banker africa
hatimaye tumefanikiwa kuwa chaguo bora katika benki zinazotoa huduma kwa makampuni nchini (preffered bank) alimalizia bi woiso
07/27/150648 mbunge chiku abwao wa chadema amfuata zitto kabwe actwazalendo
wanahabari wakichukua taarifa hiyo (imeandaliwa na mtandao wa www habari za jamiicom
07/27/150651 wadau wa utamaduni wazungumzia jinsi unavyochangia uchumi hapa nchini
mgeni rasmi dk salim ahamed salim akizungumza katika ufunguzi wa semina iliyoandaliwa na chuo cha waislam morogoro kuhusiana utamaduni na mirathi ya utamaduni iliyopo hapa nchini semina hiyo iliyohusisha viongozi mbalimbali na wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam (udsm) iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano katika hoteli ya lamada jijini dar es salaam leo kushoto ni mkurugenzi wa taasisi ya utamaduni wa chuo cha kiislam morogoro abdalla bujra
dk salim ahamed salim akizungumza na mkurugenzi wa taasisi ya utamaduni wa chuo cha kiislam morogoro abdalla bujra mara baada ya kumalizika kwa semina inayozungumzia masuala ya utamaduni iliyofanyika katika hotel ya lamada jijini dar es salaam leo
mwenyekiti wa kigoda cha mwalimu nyerere profesa issa shivji kichangia maada kuhusiana na mambo ya utamaduni na mambo ya kale jinsi yanavyochangia katika uchumi wa hapa nchini katika semina iliyoandaliwa na chuo cha waislam morogoro iliyofanyika katika hotel ya lamada jijini dar es salaam leo
wadau wa mambo ya utamaduni wakimsikiliza dk salim ahamed salim
katika semina iliyoandaliwa na chuo cha waislam morogoro iliyofanyika katika hotel ya lamada jijini dar es salaam leo
baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam wanaosoma kozi ya utamaduni ( culture) waliohudhuria katika semina iliyoandaliwa na chuo cha waislam morogoro iliyofanyika katika hotel ya lamada jijini dar es salaam leo
baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika semina iliyoandaliwa na chuo cha waislam morogoro iliyofanyika katika hotel ya lamada jijini dar es salaam leo
mwenyekiti wa kigoda cha mwalimu nyerere profesa issa shivji akizungumza na profesa abdul shariff kabla ya kuanza semina iliyoandaliwa na chuo cha waislam morogoro iliyofanyika katika hotel ya lamada jijini dar es salaam leo
07/27/150726 mamlaka ya chakula na dawa yaipiga jeki manispaa ya ilala
mkurugenzi wa manispaa ya ilala isaya mngurumi akipokea madebe maalum la kuhifadhia takatakakatika ni mkurungenzi wa usalama wa chakula kutoka mamlaka ya chakula na dawa (tfda) raymond wigeng iliyofanyika katika eneo la wazi la posta ya zamani leo jiji dar es salaam
mkurungenzi wa manispaa ya ilala isaya mngurumi akitoa shukrani kwa uongozi mzima wa mamlaka ya chakula na dawa (tfda) kwa kupokea msaada wa madebe ya kuhifadhia takataka ili zisizagae hovyo msaada huo umetolewa katika eneo la wazi posta ya zamani leo jiji dar es salaam
baadhi ya waandishi wa habari waliohudhulia katika kikao hicho kutoka mamlaka ya chakula na dawa (tfda) iliyofanyika katika eneo la wazi posta ya zamani leo jiji dar es salaam
07/27/150750 unesco kuendelea kusaidiana na tanzania kuinua elimu
si kutoa walimu wazuri tu bali kuwezesha jamii wanafunzi na waliopitia mafunzo hayo kuwa na namna mpya ya kufikiri na kuvumbua vitu vipya vya kujiendelea na kuendeleza taifa alisema yusuph
jaco du toit kutoka ofisi za unesco kanda ya nairobi akiendesha majadiliano ya maboresho ya vipengele mbalimbali vya waraka wa mafunzo ya tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimuunesco ict competency framework for teachers in tanzania wakati wa kongamano hilo lililomalizika mwishoni mwa juma mjini bagamoyo
naye kiongozi wa timu iliyopitia awali katika mradi huo wa cfit profesa ralph masenge amesema wataalamu waliohusika na upitiaji huo kabla ya kongamano walitoka chuo cha ualimu tabora na kile cha mondulichuo kikuu huria tanzania na chuo kikuu cha dar es salaam
alisema awali walipitia kuona mahitaji maalumu ya walimu kisha wakaja na mapendekezo ambayo sasa yanafanyiwa kazi
alisema matatizo mengi ya elimu tanzania yanatokana na uhaba wa vifaa vya elimu na ubora wa walimu
alisema mradi huo utasaidia kutoa elimu bora kwa kuwa na walimu bora na vifaa bora kupitia tehama
alisema mradi huo utasaidia kuwezesha tehama kutumiwa kama chombo cha kutumia wanafunzi hasa pale panapokosekana
profesa masenge alisema hatua waliyofikia ni hatua ya matayarisho na kwamba ni matarajio yao kwamba wakishafikisha hati hiyo kwa wizara masuala ya matumizi ya maabara yatakuwa yamekamilika | 2019-12-05T18:30:51 | http://jiachie1.rssing.com/chan-7007640/all_p594.html |
wabunge viti maalumu
ccm 65 chadema 23 na cuf 8
tume ya taifa ya uchaguzi imekamilisha kazi ya kuwateua wabunge wa awali wa viti maalumu na kuwasilisha orodha ya wateule hao katika vyama husika vya siasa
habari za uhakika ambazo tanzania daima jumatano imezipata kutoka ndani ya nec na miongoni mwa viongozi wa juu wa vyama vitatu vya siasa vyenye wabunge wa viti maalumu wamethibitisha kupokea majina ya wabunge hao
kwa mujibu wa habari hizo chama cha mapinduzi (ccm) kimepata wabunge 65 wa viti maalumu kikifuatiwa na chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) kilichopata viti 23 na chama cha wananchi (cuf) kikapata viti vinane
hata hivyo habari zaidi zinasema kuwa idadi hiyo ya viti maalum ambavyo jumla yake ni 96 itaongezeka kwa kila chama baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi ulioahirishwa wa wabunge katika majimbo saba
chama cha nccr mageuzi kilichopata viti vinne vya wabunge tlp na udp kimoja havikupata kiti hata kimoja cha wabunge wa viti maalumu kutokana na kukosa sifa ya kufikisha asilimia tano ya kura za wabunge wote kwa mujibu wa sheria
wabunge wa viti maalumu wa chadema ambao majina yao yamepitishwa na mikoa wanayotoka kwenye mabano ni pamoja na lucy owenya (kilimanjaro) esther matiko (mara) mhonga luhanywa (kigoma) anna mallac (katavi) paulina gekul (manyara) na conchesta rwalumulaza (kagera)
wengine ni suzan kiwanga (morogoro) grace kiwelu (kilimanjaro) suzan lyimo (kilimanjaro) regia mtema (morogoro) christowaja mtinda (singida) anna komu (dar es salaam) mwanamrisho abama (zanzibar) joyce mukya (arusha) leticia mageni nyerere (mwanza) na naomi kaihula (dar es salaam)
majina mengine ya wateule hao ni chiku abwao (iringa) rose kamili (manyara) christina lissu (singida) raya ibrahim khamis (zanzibar) philipa mturano (dar es salaam) mariam msabaha (zanzibar) na rachel mashishanga (dar es salaam)
wabunge hao ambao wanatarajia kusafiri kwenda mjini dodoma kuungana na wenzao wanafanya idadi ya wabunge wote wa chadema hadi sasa kufikia 45
kwa mujibu wa habari hizo idadi hiyo inakifanya chama hicho kiwe na sifa ya kuunda kambi ya upinzani bila kutegemea wabunge wa kutoka vyama vingine vya upinzani
kwa upande wa chama cha mapinduzi (ccm) ambacho hata hivyo majina ya washindi hayakuweza kupatikana kimepata idadi ndogo ya viti tofauti ilivyotarajiwa
endelea kusoma habari hii posted by
even with a c
jana rais jakaya
wabunge
prince william kufunga ndoa mwakani
mjukuu wa m
eid al adha the festival of sacrifice
what is e
waziri mkuu ni mizengo kayanza peter pinda
mambo ya kobe bryant
igp mwema apangua makamanda
amng'oa kamishina nzow
samsung galaxy tab new information
sugu asiachwe yatima asaidiwe kuleta mapinduzi
mh anne makinda spika wa bunge la tanzania
fifa yamuongozea pesa obilale wa togomlinda mlango
mbio za uspika kamati kuu yamuengua sita
kamati
ccm 65 chadema 23 na cuf 8
aliyekuwa r
michael jacksons two
mziray aliondoka tanga na african sports yetu
mkakati waundwa kummaliza sitta
kundi
hotuba ya rais jk baada ya kuapishwa
hotuba ya l
jk aapishwa kuwa rais wa tanzania
rais jakaya kiwe
jk ateuliwa kuwa rais wa jamuhuri ya muungano wa t
bungeni hapatoshi bunge la 10 la jamhuri ya muung
asema limesheheni wa
ccm yapata pigo katika ubunge tanzaniavia voa news
dk shein atangazwa rais zanzibartume ya uchaguzi | 2017-05-01T04:25:12 | http://habariyaleo.blogspot.com/2010/11/wabunge-viti-maalumu.html |
zoezi la upigaji kura laendelea kwa utulivu na amani visiwani zanzibar | magazeti ya leo| tanzania news |tanzania today
zoezi za upigaji kura laanza na kuendelea kwa utulivu na amani jijini dar es salaam
wapiga kura kituo cha mnazi mmoja jijini dar es salaam wakiwajibika kwa utulivu na amani asubuhi hii utulivu na amani watawala kituo cha mnazi mmoja jijini dar es salaam nidhamu utulivu uvumilivu na amani vyatawala kila sehemu hapa ni kibaha machinjioni mkoa wa pwani hapa ni kibaha machinjioni mkoa wa pwani kituo cha afisa mtendaji wa kata ya olorieni jijini arusha
kituo cha dispensary ya kata ya olorieni arusha
picha kwa hisani ya blogger seria
zoezi la upigaji kura laenda kwa utulivu dar
hatimaye zoezi la upigaji kura nchi nzima limeanza leo huku kukiwa na hali ya utulivu katika vituo vingi
zoezi la kuhesabu kura linaendelea visiwani zanzibar
maafisa wa tume ya uchaguzi zanzibar wakiendelea na zoezi la kuhesabu kura katika vituo vilivyopo katika shule ya sekondari ya ben bella jimbo la mji mkongwe mkoa wa mjini magharibi
zoezi la upigaji kura lafunguliwa rasmi kwa ajili ya kumpigia kura mrembo
kama inavyojulikana kuwa mrembo wa miss universe tanzania 2016 jihan dimack aliyetwaa taji la miss universe tanzania mapema mwezi wa kumi na moja mwaka 2016 aliondoka nchini tangu tarehe 11 januari kuelekea manilla nchini philipines kwa ajili ya kushiriki mashindano ya miss universe kwa ngazi ya kimataifa
jihan dimack akiungana na wenzake kutoka nchi mbalimbali ulimwenguni yupo nchini phillipines kwa muda wa wiki mbili sasa akiiwakilisha vyema tanzania katika kuwania taji | 2019-01-16T23:01:16 | http://www.tanzaniatoday.co.tz/news/zoezi-la-upigaji-kura-laendelea-kwa-utulivu-na-amani-visiwani-zanzibar |
tume ya mawasiliano uganda yazfungia redio 23 kwa kushabikia uchawi habari na matukio
home habari na matukio tume ya mawasiliano uganda yazfungia redio 23 kwa kushabikia uchawi
tume ya mawasiliano uganda yazfungia redio 23 kwa kushabikia uchawi
kajunason at march 28 2018 habari na matukio
na kibena kindibwa uganda
redio 23 hazitakuwa hewani uganda tume ya mawasiliano ya uganda (ucc) imesitisha leseni za vituo 23 vya redio kwa tuhuma za kushabikia na kueneza uchawi
kwa mujibu wa msemaji wa tume hiyo bi pamela ankunda redio hizo zimekuwa zikihusika katika kukuza uchawi kwa njia ya kutoa matangazo (witchcraft content) ya uchawi redio hizo ni metro fm nile fm kagadi broadcasting services emambya fm village club fm radio kitara packwach fm na tropical fm
kifungu cha 41 (1 a &b) cha sheria ya mawasiliano uganda ya mwaka 2013 kinatoa jukumu kwa tume hiyo kusitisha au kufuta leseni ya chombo chochote cha habari nchini humo ambacho kinakiuka masharti ya leseni husika
bi ankunda amesema vituo hivyo vya redio viwahi kuonywa kuhusu mwenendo wao kabla ya hatua hiyo ya kuvifungia
anasema walivionya vituo hivyo kwa kukiuka matakwa ya utangazaji yaliyowekwa na ucc
alisema redio hizo zitaruhusiwa kurejea hewani kama wahusika wataahidi kwa maandishi kufuata masharti ya leseni zao na kamwe hawatangaza masuala ya uchawi au kujihusisha na shughuli zozote ambazo kwa namna moja au nyingine zitahusiana na ufisadi wa kieletroniki
amezishauri redio hizo kuwapa mafunzo watangazaji wake kuhusu mambo gani yanaruhusiwa na mambo gani hayaruhusiwi wakati wa kutangaza ili kujiepusha na makosa kama hayo siku za baadaye | 2018-07-23T04:18:44 | http://www.kajunason.com/2018/03/tume-ya-mawasiliano-uganda-yazfungia.html |
japan rushwa rank
sasa maadili data ya kihistoria utabiri takwimu chati na kalenda ya kiuchumi japan rushwa rank
<iframe src='https//tradingeconomicscom/embed/s=japancorran&v=202008142300v20200716&lang=all&h=300&w=600&ref=/japan/corruptionrank' height='300' width='600' frameborder='0' scrolling='no'></iframe><br />source <a href='https//tradingeconomicscom/japan/corruptionrank'>tradingeconomicscom</a>
viwanda pmi 4520 4010 5620 2960 pointi [+]
huduma pmi 4540 4500 5530 2150 pointi [+]
viwanda uzalishaji 1770 2630 3000 3720 asilimia [+]
viwanda uzalishaji (mwezi) 270 890 680 1650 asilimia [+]
viwanda uzalishaji 1770 2630 2930 3720 asilimia [+]
uwezo wa matumizi 7060 7990 13610 6860 pointi [+]
mabadiliko katika inventories 53700 78640 766230 656620 jpy bilioni [+]
kisadfa index 7640 7290 10730 6940 [+]
uchumi walinzi survey 4110 3880 5760 790 [+]
gari uzalishaji wa 25138400 35940300 96199400 24977200 vitengo [+]
gari sajili 20747300 18212800 58544900 8304400 [+]
uongozi index uchumi 8500 7840 10860 7270 pointi [+]
uwekezaji wa kibinafsi 010 350 1280 2533 asilimia [+]
mining uzalishaji 570 1130 1620 1610 asilimia [+]
maagizo ya chombo cha machine 6978400 6719000 18286000 1903700 jpy milioni [+]
sekta ya juu ya viwanda 9390 8700 10720 7320 pointi [+]
steel uzalishaji 559791 591634 1077500 117700 elfu tani [+]
reuters tankan index 4400 4600 3900 7800 pointi [+]
cement uzalishaji 452100 430000 936800 421800 maelfu ya tani [+]
orodha ya shughuli zote za sekta 8900 9220 10870 8900 pointi [+]
composite pmi 4490 4080 5410 2580 pointi [+] | 2020-08-14T23:44:42 | https://sw.tradingeconomics.com/japan/corruption-rank |
klopp awafanyia kauzibe napoli kwa beki wake alberto moreno atupiliambali ofa yao ya pauni mil 11 | saluti5
home » soka » klopp awafanyia kauzibe napoli kwa beki wake alberto moreno atupiliambali ofa yao ya pauni mil 11
klopp awafanyia kauzibe napoli kwa beki wake alberto moreno atupiliambali ofa yao ya pauni mil 11
liverpool wameitupilia mbali ofa ya pauni mil 11 kutoka kwa napoli wanaomtaka beki alberto moreno mtandao wa times umedai
licha ya kutaka kuifanyia marekebisho makubwa safu ya ulinzi bado kocha jurgen klopp haonyeshi kumchoka moreno
at monday july 03 2017 | 2017-09-24T17:37:25 | http://www.saluti5.com/2017/07/klopp-awafanyia-kauzibe-napoli-kwa-beki.html |
kesi dhidi ya lema (mb) ya uchochezi chuoni yaahirishwa hadi oktoba 1 2013 ocd makamu mkuu wa chuo mashahidi muhimu | politiksi kurunzini
home habari politiksi kesi dhidi ya lema (mb) ya uchochezi chuoni yaahirishwa hadi oktoba 1 2013 ocd makamu mkuu wa chuo mashahidi muhimu
kesi dhidi ya lema (mb) ya uchochezi chuoni yaahirishwa hadi oktoba 1 2013 ocd makamu mkuu wa chuo mashahidi muhimu
mahakama ya hakimu mkazi arusha imeahirisha shauri la kesi inayomkabili mbunge wa jimbo la arusha mjini mh godbless lema (chadema) kwa tuhuma za kuchochea vurugu katika chuo cha uhasibu arusha (iaa) hadi octoba 1 2013 ambapo mashahidi wa upande wa mashitaka wataanza kutoa ushahidi wao kwa siku mbili mfululizo
akitoa uamuzi huo mapema leo asubuhi hakimu mkazi hawa mguruta alisema kwamba ameridhia ombi la wakili wa mh lema aliyeomba shauri hilo liahirishwe kutokana na mteja wake kuwa mgonjwa hakimu msofe aliwataka mashahidi wote kama walivyohuduria leo kufika mahakamani hapo siku ya jumanne na jumatano ya oktoba 1 na 2 kwa ajili ya kuanza kutoa ushahidi wao zoezi ambalo lilipangwa kuanza leo kama kuningekuwa na udhuru wa kuahirisha shauri hilo
mashahidi wa upande wa jamhuri waliofika mahakamani hapo ni pamoja na ocd wa wilaya ya arusha mjini giresi muroto na mlezi wa wananfunzi chuoni hapo bw john joseph nanyaro
wengine ni maofisa wa polisi bernad nyambalya na jane chibuga na makamu mkuu wa chuo cha iaa bw faraj kasidi
awali wakili kimomongoro anayemwakilisha lema wakisaidiana na wakili humrefy mtui aliwasilisha ombi la kuiomba mahakama iahirishe shauri hilo hadi tarehe nyingine kwa kile alichoeleza kuwa ni kutokana na mh lema kuwa katika hali ya kuumwa na kwamba ni jana tu aliruhusiwa kutoka hospitali ya aicc alikokuwa amelazwa tangia agosti 14 akiendelea kutumikia siku 10 alizopewa na daktari za mapumziko ya kitandani
wakili kimomongoro alimkabidhi mwanasheria wa jamhuri nakala ya discharge summary kutoka hospitali ya aicc nae akaipitia na kuridhia shauri hilo kuahirishwa kutokana na sababu hiyo ya ugonjwa
mashahidi wa kesi hiyo ya uchochezi dhidi ya lema wakiondoka katika viwanja vya mahakama leo hii asubuhi kwa nyuma anaonekana dean of students akizungumza na inspekta bernad
mashahidi upande wa mashitaka anaeongea na simu ni makamu mkuu wa chuo cha iaa bw faraj kasidi na anaemtazama ni jane chibuga
ocd giresi muroto akisalimiana na dereva wa gari ya mbunge lema huku wakili mtui akishuhudia nje ya viwanja vya mahakama kuu arusha
inspekta bernad nyambalya akisalimiana na mawakili wa mh lema mara baada ya kesi hiyo kuahirishwa kulia kabisa ni mwanasheria glory kaaya picha zote na seria jr | 2017-08-17T23:28:56 | https://arusha255.blogspot.com/2013/08/kesi-dhidi-ya-lema-mb-ya-uchochezi.html |
walemavu wa kutosikia mkoani ruvuma watoa maoni ya katiba mpya waomba kero zao ziwekwe bayana ndani ya katiba mpya | songeayetublogspotcom
home » unlabelled » walemavu wa kutosikia mkoani ruvuma watoa maoni ya katiba mpya waomba kero zao ziwekwe bayana ndani ya katiba mpya
walemavu wa kutosikia mkoani ruvuma watoa maoni ya katiba mpya waomba kero zao ziwekwe bayana ndani ya katiba mpya
watu wenye ulemavu wa kuto sikia mkoani ruvuma wametoa mapendekezo yao kuwa katiba mpya ni vyema iweke bayana lugha kwa watu wenye ulemavu wa
kuto sikia na wamependekeza uwepo mgawanyo wa madaraka mfano wabunge wasiteuliwe kuwa mawaziri na wakuu wa mikoa wasichaguliwe kuwa wabunge kwani jamhuri ya muungano wa tanzania ina wasomi wengi
yamesemwa jana kwenye semina ya chama cha viziwi tanzania (
chavita) mkoani ruvuma ya kuwajengea uwezo wa namna ya kutoa maoni ya katiba mpya iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chama cha ushirika wa kuweka na kukopa cha halmashauri ya wafanyakazi wa manispaa ya songea
semina hiyo iliyofadhiliwa na the foundation of civil society organization ya jijini dar es salaam hery chaima mjumbe wa chama cha viziwi tanzania mkoa wa ruvuma alisema kuwa anapendekeza kuwa katiba mpya ni vyema rais apunguziwe madaraka kwani sio lazima wakurugenzi wa halmashauri za wilaya miji manispaa na majiji wateuliwe na rais na badala yake uteuzi ufanywe na waziri mkuu
chaima alisema kuwa kufanya hivyo rais kutampunguzia kazi zake za kila siku na ameiomba katiba mpya iweke bayana lugha kwa watu wenye ulemavu wa kuto sikia na kwamba makundi maalumu serikali yatambue kama ni makundi yanayo hitaji kutoa maoni kama watu wengine na iyasamini na kuyajali kama wao ni binadamu kama wengine
upande wake mtaalamu wa lugha alama mery haule alisema kuwa walemavu wasiosikia wanahitaji kupata msaada mkubwa kwa jamii hivyo katiba mpya ni vyema iwatambue pale wanapopata matatizo ya ugonjwa hospitalini waweze kusaidiwa kwa uraisi vilevile wanapopatwa na
matatizo kwenye vituo vya polisi
mahakamani na sehemu zingine wanatakiwa wawepo wataalamu wa lugha alama wa kuwasaidia kwani kwa hivi sasa wamekuwa wakipata
shida pale matatizo yanapotokea
abdul homera mkalimani wa lugha alama tanzania
ameiomba serikali ione umuhimu wa kutoa upendeleo kwa walemavu wasiosikia na walemavu wengine kwa kuwapa ajira kwani hali zao kimaisha ni ngumu
zaidi kuwa wakalimani wa l ugha alama vile vile watambulike ndani ya katiba mpya nalugha ya alama itambulike kama lugha rasmi ya taifa na mkalimani wa lugha alama kwanza ni vyema alipwe au ahajiliwe na serikali kama wanataaluma wengine wanavyopatiwa ajira na serikali
homera aliiomba serikali hichukue hatua za
makusudi za kujengwa kwa vyuo vya lugha alama maana hapa nchini hakuna hata chuo kimoja ambacho kinafundisha taaluma hiyo
wa chama cha viziwi tanzania (chavita) mkoa wa ruvuma kelvin vicent amesema kwenye katiba mpya ni nyema mgombea binafsi wakati wa kumchagua raisi awepo ili kuweka bayana demokrasia kwani kuna baadhi ya watanzania si wanachama wa vyama vya aina yoyote vya siasa na ameitaka katiba mpya iweke bayana mikataba ya nchi kwa uwazi zaidi kwa wananchi mfano mgogoro uliojitokeza mtwara wa gesi ambao umeonekana haukuwa wazi kwa wakazi wa mtwara na ardhi iwe mali ya wananchi na sio serikali ambayo kwa sasa hivi meonekana kuwepo na migogoro mingi hasa pale wanapogundua chini ya ardhi kuna madini
vyombo vya habari kwenye katiba mpya lazima viwe huru na
sio kuingiliwa na serikkali hata ikizingatiwa kuwa waandishi wa habari ni kioo cha jamii na si vinginevyo wakusanye habari bila kuwepo bugudha na kama wanahitaji kupata taarifa kutoka serikalini wasinyimwe | 2017-04-25T10:36:10 | http://songeayetu.blogspot.com/2013/02/walemavu-wa-kutosikia-mkoani-ruvuma.html |
habari online casino codes bonus
chanzo wako kwa kuvunja casino habari kupata latest mpya ya maendeleo casino uchumi sheria na zaidi
wakati wa kuamua kujiunga na mkondoni mkondoni waendeshaji wengi watakushukuru na bonasi inayokaribishwa lakini unaweza kuchagua chaguo sio kuchukua bonasi hakuna sheria ambazo unapojiunga lazima uchukue nje na utumie ziada wakati mwingi mwendeshaji atafuatilia baada ya usajili wako na []
je ni kweli kwamba unatafuta maendeleo makubwa ya kuratibu mtazamo wako kutathmini haziwezi kulinganishwa codes zote za bonasi za uingereza wanahakikisha kufikisha kwenye matakwa yaliyoinuliwa zaidi yanayofanya mtu yeyote arudi kwa nyongeza hatua hii imeamua jinsi ya kusonga mbele kwa kuwapa wageni wake kile wanachohitaji []
kutafuta vilabu vya uchezaji vya bure vya wahindi ambavyo vinapatikana india ambapo unaweza kucheza michezo ya bure ya pesa ya 100 bure katika nafasi ya mbali kwamba umeenda mahali sahihi utagundua usajili ulioshinizwa na huria wa india hakuna duka (bure ya mkopo / zamu za bure) unazoweza kutumia kucheza ubora wa juu []
kupata thawabu bora ya kucheza kamari kwenye mkondoni inaweza kuwa mtihani ndio sababu tumefanya bidii kwako kwako hapa utagundua mwongozo ukifafanua wapi upate thawabu bora na bora ya kamari ya kamari karibu ili uweze kufahamu maendeleo ya karibu ya ukaribishaji wakati wa kujiandikisha hadi []
kuna aina tatu ya australia hakuna duka la kamari la duka la kucheza hakuna duka la ziada ya rehani (pesa) hakuna duka huru ya zamu na hakuna duka huru la bure na hakuna mahitaji ya betting tofauti na sifa za kila huonyeshwa chini nambari ya bonus ya amana ya australia hakuna sifa za ziada zinapatikana tu kwa wachezaji ambao []
kutoa kwa mtandao huko amerika kunazidi kuwa kweli zaidi na majimbo mengi yanayoelekea kufungua shughuli hii ya burudani ya ajabu kuna vilabu vingi vya kucheza kamari mtandaoni ambavyo vinapatikana kwa wachezaji wa amerika na wanatoa maneno mazuri tuzo na picha za juu endelea kusisitiza kusoma ubuni wa wavuti huko usa wauzaji wa programu inayoshughulikia amerika []
kuhusu biashara ya kupeana na maendeleo ya hivi karibuni katika uvumbuzi tasnia ya uuzaji wa wavuti imeendelea pia kwa kuongezea kwa sababu ya uwasilishaji wa uvumbuzi wa html5 wachezaji kwa sasa wanauwezo wa kuthamini vitu vya kupendeza kwenye vifaa vyote vya portable na vya eneo la kazi maendeleo ya ulimwengu huu wa michezo ya kubahatisha yanaweza kuzingatiwa kwa ufanisi kupitia []
utaftaji wa eucasino ulioburudisha mara kwa mara wa michezo ya kujihusisha na upeo mkubwa wa fidia ya maendeleo kweli huweka ukurasa huu wa wavuti ya kamari ya mkondoni iliyotengwa na wengine inadhibitiwa na skillonnet bidhaa ya eucasino inapatikana katika lahaja tofauti unaweza kuhifadhi na kucheza katika uamuzi wako wa fomu za kifedha za 9 na msaada wa lugha nyingi pia unapatikana na kuifanya []
kuenda ujerumani kwa muda mrefu imekuwa na halali lakini sio halali kabisa nchini ujerumani kwa muda mrefu mahali pengine katika anuwai ya 2008 na 2012 betting ilitangazwa kweli na serikali ya kitaifa kwa bahati nzuri kwa kilabu kinachowathamini watu wa ujerumani ambao wanathamini kuwachana na uwezekano hii sio kweli tena hivi sasa wachezaji wanaweza []
katika tukio ambalo unatafuta kilabu za kamari za mkondoni za uswidi wakati huo uko katika eneo sahihi hapa unaweza kuona na kutumia uchunguzi bora kwa vilabu vya kamari mtandaoni kutoka uswidi kuweka nchini uswidi ni kujua kutoka saa za waviking kuna hadithi hata juu ya kutatua maswali ya eneo na []
posted juu ya septemba 19 2019 septemba 19 2019 mwandishi maoni off juu ya mafao ya casino ya uswidi
licha ya ukweli kwamba serikali ya merika ni umbali mrefu kutoka kwa kuidhinisha na kudhibiti utapeli wa wavuti kwa kiwango cha ukiritimba wakaazi wa merika bado ni kutafuta na kucheza michezo ya kufurahisha na ya kweli ya pesa kwenye mengi makubwa zaidi duniani na unafuu mzuri wa kilabu mkondoni hizi 'usa []
posted juu ya agosti 19 2019 agosti 19 2019 mwandishi maoni off kuhusu kuhusu usa hakuna nambari za bonasi za amana
unibet kasino ni kasino yenye sifa ya mkondoni ambayo inaruhusu wachezaji wa amerika kwa furaha ni katika tasnia yote kwa muda mrefu wa kutosha kuamua sifa kali na kuwa takwimu kwenye soko la kamari la mtandao wacheza wanathamini aina ya majina ya mchezo na vile vile usalama na usawa kasino fulani []
kiwango cha kasino 80 / 100 slotocash usa casino slotocash casino ilizinduliwa katika 2007 150 + michezo ya kasino ofa muuzaji wa moja kwa moja & wacheza michezo wa simu kutoka urusi kukubaliwa kucheza katika slotocash casino kwenye simu ya rununu kibaomac au pc ukurasa huu ni kujitolea kwa mkongwe katika uwanja wa kamari mashuhuri kasino bitcoin huko usa shujaa wa leo ni slotocash ambayo ni []
posted juu ya juni 12 2019 juni 12 2019 mwandishi maoni off kwenye sloto cash usa casino
salamu mchezaji mwenzako na mnakaribishwa kwenye orodha yetu ya kasinon zinazokubaliwa mtandaoni ambapo utapata mafao ya juu ya kila aina lakini kwanza kabisa asante kwa kuwa hapa na kwa kuweka tumaini lako kwetu tunafahamu vyema ukweli kwamba hakuna tovuti nyingi huko zinalenga zaidi []
mashabiki wa kasino wana kasinon zaidi ya 50 kuchagua fomu huko us wameenea kote nchini miji mikubwa zaidi ya amerika ina kasino moja walakini kasinon nyingi za amerika ziko katika hoteli na miji ya spa iliyoonyeshwa na neno mbaya (umwagaji spa) mwanzoni mwa majina yao kama kasino maarufu []
teknolojia inakua haraka na inapokuja kwenye kamari na kasino mkondoni hadithi hiyo ni sawa sekta ya uchezaji ya mkondoni imeshuhudia kuongezeka kwa kipekee katika miaka michache iliyopita shukrani zote za kupatikana kwa programu za kamari za kijamii na kamari kwa kuongezea kasino mkondoni hutegemea tu teknolojia na maendeleo ya hivi karibuni []
kutafuta toleo bora nenda na mojawapo ya bonasi zetu za kasino zilizo na viwango vya juu zaidi ya haya yanapeanwa kwa kipekee kwa casinoground na jamii yake tunapima kasinon kabisa tunajua ni nani atakayewapatia wachezaji wetu mafao bora ya mkaribishaji wa mkopo na muhimu zaidi ambayo kasinon itatoa jukwaa salama la kamari wakati []
bonasi za kasino za juu $ 2875 hakuna nambari ya bonasi ya amana pesa ya bure ya 55 spins za bure za 215 hakuna amana $ 455 chip chip € 4650 hakuna amana euro 2795 hakuna bonus au bonus tikiti ya bure ya casino ya eur 585 € 180 online casino mashindano £ 845 online mashindano ya casino $ 745 mashindano ya bure ya casino 110 free spins spins za bure za 77 € 295 online casino []
posted juu ya novemba 15 2018 novemba 15 2018 mwandishi maoni off juu ya mafao ya juu ya kasino
mashtaka ya mchezo wa mwisho yalibadilishwa katika taifa yalikuwa katika 1998 wakati walipanda kutoka 22 hadi 25 kwa hivyo utaftaji wa miaka xxumx hauwezekani kuwa hivyo upanuzi wowote kwa bahati mbaya ambayo inakuja hautakuwa suala la chini ya kilabu kimoja cha kamari katika taifa kama []
posted juu ya novemba 15 2018 mwandishi maoni off kwa viongozi wa malaysia walionyesha wiki iliyopita labda kuleta mashtaka na lengo la mwisho la kugeuza kiunga cha serikali cha mikataba
kasino za mtandaoni ambazo zinakubali wachezaji wa vilabu vya kamari kutoka uturuki wanaishia kujulikana zaidi kwa miundo yao kusimamia vyema akaunti na matangazo kwa kila shark wa kadi anayeishi uturuki na anayetafuta faragha katika vilabu vya kamari tumefanya uamuzi wa zote bora zaidi ya kituruki kuna idadi kubwa kama hii []
kasino za mtandaoni ambazo zinakubali wachezaji wa vilabu vya kamari kutoka uhispania wanazidi kujulikana kwa vielelezo vyao kutunza pesa vizuri na kukuza kwa kila mchezaji anayeishi nchini uhispania na anayetafuta siri katika kilabu tumefanya uchaguzi wa vilabu bora kabisa vya kamari za uhispania kuna idadi kubwa kama ya wauzaji wa programu []
kwa kweli hata na tovuti kadhaa za wavuti za uchezaji za wavuti zinazopatikana ulimwenguni kote kupata kilabu bora cha kucheza kamari mtandaoni kwa watendaji wa michezo huko norway sio jambo rahisi katika nakala hii tumekusanya chanjo ya kilabu bora kabisa ambayo unapaswa kuangalia kwa bahati mbaya kuwa wewe ni mchezaji wa michezo []
uchekeshaji unadhibitiwa vikali huko japani na imekuwa tangu karne ya ishirini kwa kweli betting inaruhusiwa tu kwenye tafrija za michezo zilizochaguliwa na uwezo pamoja na pachinko ya burudani ya mtindo ni nini zaidi kwa upande wa wavuti za wavuti wakati baadhi ya vilabu nje ya mkondoni wanafurahi kukubali wachezaji wa japan huko japan yenyewe kutangaza wavuti kwenye wavuti []
venice casino klabu ya kwanza ulimwenguni iliona mwangaza wa siku huko venice italia ilikuwa 1638 na mji mkali wa venice mwishowe ulichukua jicho la ulimwengu kinachofanya kilabu ya venice kuwa ya kushangaza ni njia ambayo kilabu cha kamari kinasambazwa kila mahali katika jiji kwa sababu za wazi []
kusanya ni maarufu sana nchini ujerumani na watu wengi kama sasa hucheza kwenye clubhouse mkondoni na kwenye tovuti za kuchekesha michezo inaweza pia kuwa njia ya kushangaza kuwa na tani ya kufurahisha na kupata pesa za ziada kwa watu wanaoishi ujerumani kuna sehemu nyingi za wavuti za betting zinazopatikana kila moja ya hizo []
kuchukua fursa ya kucheza kamari ya mkondoni kwenye mtandao inaweza kuwa njia kubwa ya kutatanisha kwa chaguo sahihi ni ikiwa kurasa za wavuti zinapatikana katika kifini hoja kati ya vitu vinavyo gumu sana mchezaji wa kifini anaweza kuhusika na kilabu cha kucheza kamari mtandaoni ni kutofaulu kwa kurasa za wavuti kupatikana katika kifini []
pata tuzo bora zaidi ya duka inayopatikana uholanzi sasa kwa msaada wa nodepositreward tunakupa maarifa ndani ya kilabu bora cha uholanzi mkondoni inayopatikana ambao hutoa tuzo bora za duka nodepositreward inaundwa na kundi la wachambuzi wa kujitolea walio na uzoefu wa muda mrefu ndani ya biashara ya uuzaji katika uwezo huo []
hakuna mataifa yote kwenye sayari ambamo betting halali ni halali bado jamhuri ya czech ni moja wapo wacheza czech wanafurahi kuwa na tasnia ya biashara iliyodhibitiwa na wazi ya kuwawekea ambayo inawawezesha kuchagua miongoni mwa biashara nyingi za kilabu za kamari zilizowekwa mtandaoni pamoja na bora zaidi []
posted juu ya novemba 13 2018 mwandishi maoni off juu ya czech hakuna bonasi ya amana ya amana
clubhouse mkondoni ambayo husaidia lahaja ya kiarabu sio nyingi kwa kuongezea hata kidogo ni wale wanaokubali wachezaji kutoka mataifa ya kiislamu sababu ni moja kwa moja dini la kiisilamu linakataza betting kwa ukamilifu wa miundo yake sisi kwa mistari hii tunaamini kuwa sehemu hii ni ya msaada kwa watu wa lahaja ya kiarabu kote ulimwenguni []
blogi yetu ya clubhouse ya mtandaoni ina hadithi za kupendeza zaidi zinazohusika na zenye kuelimisha kutoka kwa ulimwengu wa uwasilishaji wa wavuti uliowekwa kwa kupendeza kwako na faida yako aina anuwai ya mada za blogi za kasino kikundi cha askgambler kinachounda kikundi hufanya bidii kugundua mada zinazojumuisha kutoka kwa biashara ya igaming na kukupa na mchanganyiko wa siri na vidokezo vilivyokusudiwa []
hakuna tuzo za duka ni tuzo za bure ambazo vilabu vya kamari za mkondoni kama sheria zinawakaribisha wachezaji wao mpya na kuwa hivyo inaweza kuwa tuzo kwa wachezaji wenye msimamo zaidi kwa njia yoyote ni msimamo kati ya vitu huria zaidi ambavyo vilabu vya kamari vinaweza kutoa kwa wachezaji wao kwa hivyo []
burudani ya wavu inaonyesha na utaftaji wake mpya kwamba haachi kupanua mashine za nafasi za bure katika ubora pamoja na upendeleo wa nafasi ya mkondoni ya mungu ambayo imekuwa kama ya kusambazwa marehemu kwenye slotsup utahakikisha kwa njia ya kukumbukwa tunakutia moyo kufahamiana na michache ya mambo hila kwa kweli inategemea []
posted juu ya novemba 2 2018 mwandishi maoni off kwenye zawadi ya bonasi ya bahati ya kiungu
vilabu vya kamari za ufalme zilizojumuishwa kwenye mtandao ni vingi na hautakuwa na suala la kugundua clubhouse ambayo ni desturi ya kutoshea matakwa ya wachezaji wa uingereza kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka karibu utaalam maalum kwa lengo la mwisho ili kupendeza mataifa fulani au idadi ya jumla ndani ya []
posted juu ya novemba 1 2018 mwandishi maoni off kwenye kadi za bonasi za mkondoni bora zaidi kwa kamari za uingereza
romania clubhouse mtandaoni ni mingi na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimehifadhiwa kwa mahitaji ya wachezaji wa romania kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka vituo maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani ya zile []
posted juu ya novemba 1 2018 mwandishi maoni off kwenye nambari za bonasi za mkondoni bora zaidi ya mkondoni kwa kamari za romania
uholanzi clubhouse mtandaoni ni nyingi na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimetekelezwa kwa mahitaji ya wachezaji wa uholanzi kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka katikati maalum maalum kwa lengo la mwisho ili kupendeza mataifa fulani au idadi ya jumla ndani ya mataifa hayo []
vilabu vya kamari mtandaoni vya italia ni vingi na hautakuwa na suala la kugundua clubhouse ambayo imeundwa kwa mahitaji ya wachezaji wa italia kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka vituo maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani ya zile []
vilabu vya kamari mtandaoni vya ujerumani ni vya kutosha na hautakuwa na suala la kugundua clubhouse ambayo imetengenezwa kwa mahitaji ya wachezaji wa ujerumani kama wewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka katikati maalum maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya jumla ndani ya mataifa hayo []
posted juu ya novemba 1 2018 mwandishi maoni off kwenye kadi za bonasi za mkondoni bora zaidi kwa kamari za ujerumani
klabu ya mkondoni ya estonia ni ya kutosha na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimefungwa kwa mahitaji ya wachezaji wa estonia kama wewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka vituo maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani ya zile []
vilabu vya uchezaji mkondoni vya uhispania ni vya kutosha na hautakuwa na suala la kugundua clubhouse ambayo imeundwa kwa mahitaji ya wachezaji wa uhispania kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka vituo maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani ya zile []
posted juu ya novemba 1 2018 mwandishi maoni off kwenye nambari za bonasi za mkondoni bora zaidi ya mkondoni kwa kamari za uhispania
klabu ya mkondoni ya ureno imejaa na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimeboreshwa kwa mahitaji ya wachezaji wa ureno kama wewe mwenyewe nambari za bonasi za mkondoni bora zaidi kwa kamari za ureno kwa sababu ya upinzani kati ya vilabu vya kamari jaribu kuweka katikati utaalam maalum kwa lengo la mwisho la kushirikisha []
vilabu vya kamari mtandaoni vya malta ni vya kutosha na hautakuwa na suala la kugundua clubhouse ambayo imetengenezwa kwa mahitaji ya wachezaji wa malta kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka vituo maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani ya zile []
klabu ya mkondoni ya ufaransa ni kubwa na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimehifadhiwa kwa mahitaji ya wachezaji wa ufaransa kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya vilabu vya kamari jaribu kuweka karibu utaalam maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani []
klabu ya mkondoni ya denmark ni ya kutosha na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimehifadhiwa kwa mahitaji ya wachezaji wa denmark kama vile wewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka vituo maalum kwa lengo la mwisho kuzungumza na mataifa maalum au idadi ya watu ndani ya zile []
posted juu ya novemba 1 2018 mwandishi maoni off kwenye kadi za bonasi za mkondoni bora zaidi kwa kamari za denmark
clubhouse ya austria mkondoni ni mingi na hautakuwa na suala la kugundua vilabu vya kamari ambavyo vimetengenezwa kwa matakwa ya wachezaji wa austria kama wewe mwenyewe kwa sababu ya upinzani kati ya kilabu jaribu kuweka katikati maalum maalum kwa lengo la mwisho ili kupendeza mataifa fulani au idadi ya jumla ndani ya mataifa hayo wao []
posted juu ya novemba 1 2018 mwandishi maoni off kwenye nambari za bonasi za mkondoni bora zaidi kwa kamari za austria | 2019-11-18T23:01:45 | https://sw.usa-casino-online.com/jamii/habari/ |
nyumbani2013mart21 (alhamisi)
siku 21 machi 2013
meneja mkuu wa tcdd süleyman karaman huko eurasiarail fair rayhaber walitembelea kibanda (video)
meneja mkuu wa tcdd süleyman karaman huko eurasiarail fair rayhaber meneja mkuu wa reli ya tcdd ya 3eurasia süleyman karaman alitembelea reli ya 2013 reli ya taa miundombinu na haki za vifaa [zaidi ]
6 wengi high speed train set na 1 simulator ununuzi 7 kila mwaka matengenezo na huduma ya ukarabati
ugavi wa 6 seti ya kasi kubwa ya treni na simulizi ya 1 na idhini inayotarajiwa ya 7 ya matengenezo ya mwaka na huduma za matengenezo ya tc state (tcdd) [zaidi ]
mradi wa tram line ya manispaa ya karacabey itaanza maandalizi ya specifikationer zabuni katika siku zijazo
mradi wa tram line wa manispaa ya karacabey utaanza matayarisho ya zabuni maalum katika siku zijazo za kubadilishana kwa daraja ya bursa i̇zmir taşlık yolu tram ujenzi wa barabara kwa siku zijazo [zaidi ]
manispaa ya metropolitan kayseri 2 na 3 mradi wa usafirishaji wa usafiri wa reli ya kudumu ili kukamilishwa oktoba
kayseri metropolitan municipality 2 na 3 mradi wa mifumo ya usafirishaji wa usafirishaji wa awamu ya kukamilika utakamilika ifikapo oktoba mstari umepangwa kukamilika na kutumika kwa oktoba 14 magari yatanunuliwa ikiwa inahitajika [zaidi ]
aygm maendeleo mapya katika uturuki georgia tbilisi kars reli project kuokolewa
aygm uturuki georgia tbilisi kars project reli maendeleo mapya walikuwa kumbukumbu katika gcc comsa ufunguzi sezai alikataa rufaa yake kwa ajili ya matokeo ya zabuni ya ubia itakuwa tiril ukurugenzi mkuu wa uwekezaji wa miundombinu gerçekleş [zaidi ]
maendeleo mapya katika tcdd ankara sivas high speed train mradi wa miundombinu ya ujenzi wa zabuni ilikuwa kumbukumbu
mabadiliko mapya yameandikwa katika tcdd ankara sivas high speed treni ya ujenzi wa miundombinu ya ujenzi wa yertaş sty i̇nşaat ubia uliowasilishwa kwa tcdd kwa matokeo ya zabuni ya ujenzi wa miundombinu kati ya kayaş kırıkkale (sehemu ya i) [zaidi ]
tcdd konya karaman line line mradi ununuzi wa zabuni
zabuni ya ujenzi wa zabuni ya treni ya tcdd konya karaman ilikusanya kurugenzi kuu ya reli ya jimbo la uturuki (tcdd) kosa kubadilisha ubadilishaji wa mstari uliopo kati ya vituo vya konyakaraman [zaidi ]
tender kwa ufungaji wa automatic transit wa kiwango cha kuvuka kwenye boğazköprüulukışla line saa km 61 + 500
2012 / 168905 zabuni ya no no mkoa wa boğazköprüulukışla line km 61 + 500 level kuvuka mkataba wa ufungaji wa zabuni imekamilika medmeti̇şltemi̇şl [zaidi ]
mradi wa garage ya tcdd bilecik na bozuyuk unatarajiwa kuchapishwa
zabuni ya ujenzi wa tcdd bilecik na mradi wa kituo cha bozüyük unatarajiwa kuchapishwa tender ile bilecik na bozüyük ujenzi wa kituo cha treni [zaidi ]
arifiye ya tcdd pamukova 2 mradi wa umeme wa mradi wa kuashiria na mawasiliano ya televisheni umeidhinishwa na tender
tcdd arifiye pamukova 2 hat elektrifikasyon sinyalizasyon ve telekomünikasyon tesisi projesi i̇haleye çıkılabilmesi için beklenen yönetim kurulu onayı alındı tc devlet demiryolları (tcdd) genel müdürlüğü tesisler dairesi başkanlığı tarafından [zaidi ]
maendeleo mapya yalifanywa katika zabuni ya mradi wa badikentray ya tcdd mpya
maendeleo mapya yameandikwa katika zabuni ya tcdd new başkentray project gülermak aş ujenzi wa kolin na makyol kampuni ya ujenzi wa cengiz ilikataa tcdd kwa matokeo ya zabuni wakati comsa [zaidi ]
mkataba wa upyaji wa manispaa ya metropolitan ya izmir cable vifaa vya huduma mkataba uliosainiwa na stm sistem iliyoshinda zabuni
i̇zmir büyükşehir belediyesi teleferik tesislerinin yenilenmesi i̇halesi i̇haleyi kazanan stm sistem firması ile sözleşme imzalandı i̇zmir büyükşehir belediyesi balçova teleferik tesislerinin yenilenmesi yapım ihalesi ile ilgili yeni gelişmeler kaydedildi yatırımlar [zaidi ]
matumizi ya kabla ya kuchaguliwa kwa zabuni ya ujenzi wa aksaray municipality
maombi ya kabla ya kuchaguliwa kwa zabuni ya ujenzi wa manispaa ya aksaray [zaidi ]
mapendekezo ya zabuni za ujenzi wa vituo vya ujenzi wa kituo cha metrobus ya istanbul metropolitan zilikusanywa
zabuni ya zabuni ya ujenzi wa vituo vya ujenzi wa vituo vya metropolitan manispaa ya istanbul ilikusanywa zabuni ya zabuni ya kazi za ujenzi wa ukarabati wa vituo vya metrobus inayotekelezwa na manispaa ya metropolitan ilikusanywa mnamo 12 machi 2013 uwekezaji [zaidi ] | 2019-12-14T02:18:56 | https://sw.rayhaber.com/2013/03/21/ |
tamasha la olimpiki kufunguliwa london | michezo | dw | 23072012
tamasha la olimpiki kufunguliwa london
miaka saba ya kuandaliwa kugharimu pauni bilioni 93 na kuwahusisha wanariadha 10490 michezo ya olimpiki inafunguliwa rasmi ijumaa hii huku kukiwa na medali za dhahabu 302 za kushindaniwa
marokko 1500m lauf el aouzari
uwanja wa michezo wa olimpic na kituo cha vidimbwi vya kuogolea katiaka upande wa mashariki mwa london vitakuwa mwenyeji wa mashujaa wa beijing usain bolt na michael phelps ambao walirarua vitabu vya kumbukumbu katika mashindano ya mwaka wa 2008
katika upande mwingine wa mji roger federer novak jokovic na serena williams watagonga vichwa vya habari wakati wimbledon ikiwakaribisha miamba hao wa mchezo wa tennis aidha kutakuwa na voliboli ambayo maarufu huchezewa ufukweni lakini sasa italetwa katikati ya london huku uwanja wa wembley ukiandaa fainali ya kandanda
medali zitakazopeanwa kwa washindi wa mwaka wa 2012
katika uwanja wa riadha bolt ambaye ni bingwa mara tatu wa dhahbu katika michezo ya olimpiki kwenye mbio za mita 100 200 na 100 za wachezaji wanne wa kupokezana vijiti anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa mwenzake wa jamaica yohan blake katika fainali ya mbio za mita 100 mnamo tarehe 5 agosti bolt anashikilia rekodi ya ulimwengu ya sekunde 958 lakini blake ni bingwa wa ulimwengu na ambaye ana muda wa kasi zaidi msimu huu kutokana na majaribio ya mwezi jana nchini jamaica
nyota wengine wa riadha ni pamoja na mkenya david rudisha wa mbio za mita 800 kenenisa bekele ambaye alikuwa bingwa wa mbo za mita 5000 na 10000 mjini beijing mjini london hali ya usalama imeimarishwa jinsi anavyoeleza waziri wa mambo ya ndani wa uingereza james brokenshire
kumbukumbu ya mashambulizi ya munich
mkuu wa kamati ya kimataifa ya olimpiki jacques rogge leo ameongoza hafla ya kusalia kimya kwa dakika moja kama kumbukumbu ya miaka 40 ya mashambulio mabaya dhidi ya wanariadha wa israel katika mashindano ya olimpiki ya mwaka 1972 mjini munich rogge ambaye alisema hakutakuwa na dakika moja ya kusalia kimya katika sherehe za ufunguzi siku ya ijumaa ameiongoza hafla hiyo kuwakumbuka wanariadha 11 wa israel walioshambuliwa na wanamgambo wa palestina wakati alipozuru eneo la makaazi ya wanariadha alisema ana matumaini makubwa kwamba usalama mjini london umekwekwa katika hali ya juu
katika habari nyingine za olimpiki ni kuwa kamati ya kimataifa ya olimpiki ioc imempa kibali mwanariadha wa mbio za marathon mzaliwa wa sudan kusini ashiriki michezo hiyo chini ya bendera ya olimpiki katika mashindano hayo ya london
guor marial ambaye ana makao yake nchini marekani ambaye ni mkimbiaji wa zamani kushiriki kama mwanariadha huru marial aliliambia shirika la habari la ap kuwa sauti ya sudan kusini hatimaye imesikika alisema hata ingawaje hatabeba bendera ya nchi hiyo katika michezo ya olimpiki nchi yenyewe imewakilishwa marial hana paspoti na hawakilishwi na kamati ya kitaifa ya olimpiki sudan kusini ilitangaza uhuru wake kutoka kwa sudan na bado haitambuliwi na kamati ya olimpiki ya kimataifa
aboutrika kutegemewa na misri
mohamed aboutrika huenda anaendelea na mazoezi yake ya michezo ya olimpikilakini jana alifunga bao katika dakika za mwisho na kuisaidia al ahly kuwabwaga mahasimu wake wakali zamalek bao moja kwa sifuri katika mchuano wa ligi ya mabingwa afrika
kiungo huyo nyota aboutrika ambaye ni mmoja wa wachezaji watatu wenye umri mkubwa waliojiunga na timu ya misri ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 23 katika michezo ya olimpiki mjini london alirejea mjini cairo kutoka ulaya kwa mchuano huo wa siku ya pili mchuano huo ulichezewa katika uwanja wa kijeshi wa cairo ambao haukuwa na mashabiki kwa mara ya kwanza katika uhasimu uliodumu miaka 101
maneno muhimu london olimpiki olympics
kiungo http//pdwcom/p/15dcc
mashindano ya olimpiki ya rio yamalizika rasmi 22082016
mashindano ya olimpiki ya rio yafikia tamati katika sherehe kubwa ya kufunga mashindano hayo katika uwanja maarufu wa maracana wakati mji wa tokyo unapokea kijiti kwa ajili ya mashindano ya 2020 | 2017-08-23T11:06:24 | http://www.dw.com/sw/tamasha-la-olimpiki-kufunguliwa-london/a-16120260 |
kazimoto aitakia heri simba ligi kuunaye canavaro afagilia kurejea kwa ngassa kesho adai wanaanza kazi rasmi mdimu's blog
home / michezo / video / kazimoto aitakia heri simba ligi kuunaye canavaro afagilia kurejea kwa ngassa kesho adai wanaanza kazi rasmi
kazimoto aitakia heri simba ligi kuunaye canavaro afagilia kurejea kwa ngassa kesho adai wanaanza kazi rasmi
na baraka mpenja wa fullshangwe mbeya
kiungo wa zamani wa klabu ya simba na timu ya taifa ya tanzania taifa stars aliyetoroka kambini mwezi julai mwaka huu wakati stars ikijiandaa na mechi ya kuwania kufuzu kombe la dunia dhidi ya uganda `the cranes` katika uwanja wa namboole kampala mwinyi kazimoto mwitula ametuma salamu za shukurani kwa mashabiki wa simba viongozi na watanzania wote waliokuwa wanamuunga mkono
ujumbe ambao kazimoto ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook maarufu kwa jina la fb amesomeka kama ifuatavyo
najua sikupata muda wa kuwashukuru watanzania wote waliokua wananiunga mkono kwa support yao siku zote kwanza haswa haswa wapenzi wa simbaviongoziwanachama kwa kunivumilia kwa mabaya na mazuri yotenawatakia simba mafanikio mema kwenye ligipamoja sana
jembe la kazi kazimoto alitoroka kambi ya timu ya taifa taifa stars akiwa jijini mwanza kujiandaa na mchezo dhidi ya uganda lakini aliomba radhi na yakaisha sasa anag`ara huko qatar
ikumbukwe kuwa kitendo alichokifanya nyota huyu kutoroka katika kambi ya taifa kilitafsiriwa kuwa ni kukosa uzalendo kwani stars ilikuwa inakabiliwa na mchezo mgumu zaidi
kocha wa taifa stars kim poulsen alisikitishwa sana na kitendo alichofanyiwa na kiungo wake tegemeo katika kikosi chake lakini baadaye zilitoka taarifa kuwa ametimkia qatar kwenda kucheza soka la kulipwa na kim kubariki mafanikio ya nyota wake
mkali wa kumiliki gozi na kupiga pasi za uhakika mwinyi kazimoto enza zake akiwa simba kuonesha maujuzi ya hali ya juu
baadaye kazimoto alijitokeza na kuandika barua ya wazi akiwaomba radhi watanzania shirikisho la soka tanzania tff uongozi wa simba kwa kitendo alichofanya
kazimoto alieleza kuwa siku zote alikuwa ana ndoto ya kucheza soka la kulipwa hivyo baada ya kupata timu qatar alishawishika kutoroka kwani nafasi ilikuwa adimu na ya haraka kwake lakini baadaye kuna taarifa zilitoka kuwa alitoroka kwasababu kuna baadhi ya watu walimkera
kazimoto ambaye kabla ya kujiunga na simba alikuwa anakipiga kwa maafande wa jeshi la kujenga taifa jkt ruvu kutoka mwaka 20072011 na akajiunga na wekundu wa msimbazi simba mwaka 2011 na kuwa kiungo tegemeo mpaka anaondoka mwaka katikati ya mwaka huu
kijana huyo anawavutia wapenzi wengi wa soka kwa uwezo wake wa kupiga mashuti na kufunga mabao ya mbali lakini pia kumiliki mpira na kupiga pasi za uhakika
kwa sasa nyota huyo mzaliwa wa mwaka 1988 mjini dodoma anakipiga huko nchini qatar katika klabu ya al markhiya
wakati huo huo nahodha wa mabingwa watetezo wa ligi kuu soka tanzania bara nadir haroub `canavaro` amefurahishwa na kitendo cha uongozi wa timu yake chini ya mwenyekiti yusuf manji kumaliza sakata la mrisho ngassa kwa kukubali kulipa deni la milioni 45 kwa klabu ya simba sc na kutoa kauli kuwa sasa kesho ndio wanaanza ligi dhidi ya ruvu shooting
canavaro ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook ambao mara nyingi huwa anautumia kutoa kauli tofauti kwa mashabiki wake kuwa
habari mwenyekiti kayamalizakesho tunaanza kazi
ujumbe huu hauko moja kwa moja lakini kutokana na sakata la ngassa kuwa habari ya mjini kwa sasa na uongozi kukubali kulipa deni lake na kusema kuwa nyota huyo atacheza kesho inatosha kujiridhisha kuwa canavaro anamaanisha urejeo wa nyota huyo baada ya kifungo cha mechi 6
wakati hayo yakijiri naye kocha msaidizi wa yanga fred ferlix minziro amekaririrwa na vyombo vya habari akisema kuwa kesho ngassa atakuwa miongoni mwa wachezaji 11 watakaoanza katika kikosi cha kocha ernie brandts dhidi ya ruvu shooting katika dimba la taifa jijini dar es salaam | 2018-01-16T09:54:24 | http://www.mdimuz.com/2013/09/kazimoto-aitakia-heri-simba-ligi.html |
karen blixen wikipedia kamusi elezo huru
karen christence blixenfinecke (jina la kiuandishi alilotumia kwenye nchi zinazozungumza kiingereza isak dinesen) (rungsted/ denmark 17 aprili 1885 7 septemba 1962) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya denmark alitumia pia majina ya tania blixen kwenye nchi zinazozungumza kijerumani osceola na pierre andrézel
aliishi kenya wakati ule afrika ya mashariki ya kiingereza kati ya 1913 hadi 1931 akiongoza shamba la kahawa karibu na mji wa nairobi eneo la shamba lake la zamani hadi leo laitwa karen ni kitongoji cha nairobi
aliandika kumbukumbu ya maisha yake kenya na kitabu hiki kikawa msingi wa filamu out of africa huko denmark alijulikana sana kwa kazi yake iitwayo seven gothic tales
karen blixen na kaka yake thomas kwenye shamba la familia huko kenya kwenye miaka ya 1920
karen dinesen alizaliwa rungstedlund kaskazini mwa copenhagen baba yake wilhelm dinesen (18451895) alikuwa ni mwandishi na ofisa wa kijeshi toka familia ya wamiliki wa mashamba ya jutland yenye uhusiano wa karibu na ufalme kanisa na siasa za mrengo wa kulia mama yake ingeborg westenholz (18561939) alitoka kwenye familia tajiri inayofanya biashara karen dinesen alikuwa ni mtoto wa pili kati ya watoto watatu wa kike na wawili wa kiume mdodo wake wa kiume thomas dinesen alipata tuzo ya victoria cross wakati wa vita kuu ya kwanza ya dunia[1] dinesen was known to her friends as tanne
eneboerne (the hermits) agosti 1907 kilichapishwa kwa jina la tilskueren kwa jina lake la uandishi osceola
pløjeren (the ploughman) oktoba 1907 kwa jina la gads danske magasinakitumia jina la osceola
familien de cats (the de cats family) januari 1909 kwa jina la tilskueren akitumia jina la osceola
sandhedens hævn en marionetkomedie mei 1926 akitumia jina la karen blixenfinecke
seven gothic tales (1934 nchini marekani 1935 nchini denmark)[2]
out of africa (1937 denmark na uingereza 1938 nchini marekani)
winter's tales (1942)[3]
the angelic avengers (1946)[4]
last tales (1957)[5]
anecdotes of destiny (1958) (pamoja na babette's feast)
shadows on the grass (1960 uingereza na denmark 1961 marekani)[6]
ehrengard (baada ya kufa 1963 marekani)[7]
carnival entertainments and posthumous tales (baada ya kufa 1977 marekani)[8]
daguerreotypes and other essays (baada ya kufa 1979 marekani)[9]
on modern marriage and other observations (baada ya kufa 1986 marekani)[10]
letters from africa 19141931 (baada ya kufa 1981 marekani)[11]
karen blixen in danmark breve 19311962 (baada ya kufa1996 denmark)
karen blixen i afrika en brevsamling 191431 i iv bind (baada ya kufa 2013 denmark)[12]
↑ fall john updike john updike's new novel roger's version will be published in the 'seven gothic tales' the divine swank of isak dinesen the new york times 23 february 1986
↑ spurling hilary book choice winter's tales telegraphcouk (en)
↑ the angelic avengers by isak dinesen | kirkus reviews (in enus)
↑ last tales by isak dinesen | penguinrandomhousecom (in enus)
↑ shadows on the grass by isak dinesen (en)
↑ ehrengard | karen blixen adelphi edizioni (itit)
↑ (1986) summary/reviews on modern marriage and other observations / (in en) st martin's press isbn 9780312584436
↑ the british empire imperialism colonialism colonies
↑ karen blixen i afrika en brevsamling 191431 karen blixen | bibliotekdk (da)
tovuti ya karen blixen isak dinesen
wasifu mfupi wa isak dinesen/karen blixen
karen blixen's kenya
jumba la makumbusho la karen blixen denmark
jumba la makumbusho la karen blixen kenya
je unajua kitu kuhusu karen blixen kama wasifu wake habari za maisha au kazi yake
rudishwa kutoka https//swwikipediaorg/w/indexphptitle=karen_blixen&oldid=1069841
last edited on 2 julai 2019 at 1415
ukurasa huu umebadilishwa kwa mara ya mwisho tarehe 2 julai 2019 saa 1415 | 2020-08-07T16:24:29 | https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Karen_Blixen |
rais wa uturuki recep tayyip erdogan ataka uchunguzi ufanyike ndani ya ubalozi wa saudia jijini istanbul kuhusu kupotea kwa mwandishi bongo5com
rais wa uturuki recep tayyip erdogan ataka uchunguzi ufanyike ndani ya ubalozi wa saudia jijini istanbul kuhusu kupotea kwa mwandishi
contributor october 9 2018 934 am
rais wa uturuki recep tayyip erdogan ameitaka saudia kutoa ushahidi kuhusiana na mwandishi wa habari aliyepotea kwamba alitoka nje ya majengo ya ubalozi wao mjini istanbul | 2018-12-09T22:29:03 | http://bongo5.com/rais-wa-uturuki-recep-tayyip-erdogan-ataka-uchunguzi-ufanyike-ndani-ya-ubalozi-wa-saudia-jijini-istanbul-kuhusu-kupotea-kwa-mwandishi-10-2018/ |
michuzi blog mazishi ya sir george kahama kufanyika kesho spika mstaafu anne makinda atoa pole kwa wafiwa
kesho mwili wa marehemu utaondolewa nyumbani kwake kuelekea ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa julius nyerere (jnicc) kuanzia saa mbili kamili kwa ajili ya viongozi mbalimbali na wananchi kutoa heshima zao za mwisho kabla ya kuelekea kanisa la mtakatifu petro ( st peters) oysterbay dar es salaam saa tano na nusu 530 asubuhi kwa ibada | 2017-03-29T11:16:03 | https://issamichuzi.blogspot.com/2017/03/mazishi-ya-sir-george-kahama-kufanyika.html |
samira bawumia 2nd lady kutoka ghana ni fashion goals | afroswagga
samira bawumia 2nd lady kutoka ghana ni fashion goals
wakati wengi tukiangalia au tukiwaangalia first ladies kutoka nchi za nje la bara la africa na kupenda wanavyo vaa tunasahau wa kwetu kutoka africa well miaka iliyo pita michelle obama alikuwa ana make headlines sana kutokana na kuslay kwake as a first lady lakini pia melania trump ameonekana kutokuwa nyuma nae baada na kabla ya kuingia white house amekuwa akimake fashion statement
well africa wapo pia japo nabii huwa akubaliki kwao lakini wapo na wanapendeza mno mfano mzuri ni 2nd lady kutoka ghana bi samira bawumia amekuwa akipendeza kila unapo muona kizuri tulicho kipenda kutoka kwake ni kwamba anatumia local designers na materials mara nyingi anavaa vitenge au kente kutoka ghana ambapo anawakilisha vizuri bara letu la africa
anavaa sana viremba na anaemfunga ana mpatia mno
well anavaa na mavazi mengine pia apo hit red carpet harusini au hafla yoyote ambayo ana attend
je kuna umuhimu wa 1st ladies wetu kutoka africa kujaribu kuwa na mionekano tofauti mizuri
zamaradi mketema serving us classic look
5 fashion tips kwa wanawake wenye matiti madogo | 2018-07-20T05:11:05 | http://afroswagga.com/mitindo/samira-bawumia-2nd-lady-kutoka-ghana-ni-fashion-goals/ |
russell hobbs steam iron in tanzania | zoomtanzania
russel hobbs steam glide ni pas za kisasa kutoka uk ambazo unatumia kunyooshea nguo zkanyooka kama znatoka drycleanerkama utatumia kupigia surual za kitambaa mashat suti hua unaeka maji ili zinyooke vizur zaid kwa mvukounaweza kutumia bila maji pia kupigia jeans tshirt nk | 2017-11-22T07:27:16 | https://www.zoomtanzania.com/home-appliances/russell-hobbs-steam-iron-839493 |
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu mhemhagama aweka jiwe la msingi ujenzi wa kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi ipogolo zanzinews
home habari matukio waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu mhemhagama aweka jiwe la msingi ujenzi wa kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi ipogolo
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu mhemhagama aweka jiwe la msingi ujenzi wa kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi ipogolo
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama akiweka jiwe la msingi katika jengo la kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi linalojengwa kwa lengo la uboreshaji wa vituo 20 vya huduma ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi katika kituo cha afya cha ipogolo mkoani iringa novemba 22 2019wa kwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya hiyo mhe richard kasesela
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama akisalimiana na mkurugenzi mtendaji wa tacaids dkt leonard maboko mara baada ya kuwasili katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa iringa alipofika kwa ajili ya zoezi la uwekaji wa jiwe la msingi katika kituo cha afya cha ipogolo kwa ajili ya utoaji huduma za ukimwi kituoni hapo
mkuu wa wilaya ya iringa mhe richard kasesela akitoa taarifa hali ya ukimwi katika mkoa huo kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo mhe ally hapi kwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama alipotembea mkoani hapo
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama akisalimia na baadhi ya wagonjwa wanaosubiri kupewa huduma katika kituo cha afya cha ipogolo mkoani iringa alipotembelea kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la kuhudumia watu wanaoishi na vvu
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama akimfurahi mtoto aliyezaliwa katika kituo cha afya cha ipogolo na kupewa lake (jenista) alipotembelea kituo hicho
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama akimjulia hali mzee marko mveyange aliyelazwa katika kituo cha afya cha ipogolo kwa ajili ya matibabu
msimamizi mkuu wa huduma za matibabu na matunzo kwa watu wanaoishi na vvu (ctc) dkt onesmo ngande akitoa maelezo kwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama kuhusu jengo linaloendelea kujengwa kwa ajili ya utoaji wa huduma za ukimwi alipotembelea na kuweka jiwe la msingi ujenzi huo katika kituo cha afya cha ipogolo iringa
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama akihutubia wananchi wa ipogolo walioshiriki wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika jengo la kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi linaloendelea kujengwa katika kituo cha afya cha ipogolo mkoani iringa
mkurugenzi mtendaji wa tume ya kudhibiti ukimwi tanzania (tacaids) dkt leonard maboko akizungumza wananchi wa ipogolo (hawapo pichani) walioshiriki wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika jengo la kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi linaloendelea kujengwa katika kituo cha afya cha ipogolo mkoani iringa
baadhi ya washiriki waliohudhurika katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika jengo la kituo cha utoaji wa huduma za ukimwi lililopo katika kituo cha afya cha ipogolo iringa wakimsikiliza waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana ajira na wenye ulemavu mhe jenista mhagama (hayupo pichani)
mwenyekiti wa nacopha leticia kapela akitoa salamu wakati wa hafla hiyo
mwakilishi wa kamati ya kudumu ya bunge ya masuala ya ukimwi na dawa za kulevya mheomari badwel (mb) wa bahi akitoa salamu za kamati hiyo wakati wa hafla hiyo
mkuu wa wilaya ya iringa mhe richard kasele akitoa salamu za mkoa kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo wakati wa hafla hiyo | 2020-07-08T14:54:07 | http://www.zanzinews.com/2019/11/waziri-wa-nchi-ofisi-ya-waziri-mkuu.html |
fighters of life tazama picha zikionesha jinsi video queen jack cliff (mtanzania) alivyonaswa na dawa za kulevya china anatia huruma niaje big brother
tazama picha zikionesha jinsi video queen jack cliff (mtanzania) alivyonaswa na dawa za kulevya china anatia huruma niaje pichani ni mwanamke huyo wa kitanzania (akiwa amefunikwa uso) aliyekamatwa na kilo 11 za heroin huko macau hapo amepigwa picha na vidonge vyake kwenye press conference huko macau disemba 19 2013
wa kitanzania mwenye umri wa miaka 28 amekamatwa na kilo 11 za dawa za
kulevya aina ya heroin huko macao dawa hizo zilikutwa tumboni mwake baada ya kushtukiwa na kufanyiwa xray ambapo alikutwa na jumla ya vidonge 66 vyenye thamani ya dola za kimarekani 137720 mwanamke huyo alikuwa akisafiri kutoka thailand akielekea macao jumanne iliyopita aliwaambia polisi kuwa alikuwa anaelekea guangzhou ambao ni mji wa jimbo la guangdong huko china
polisi wakichunguza vidonge ambavyo huyu mrembo alikuwa amevimeza ok kwa wale walokuwa wakilalamika 'habari nusu nusu' huyo binti anaitwa jackie cliff appeared in diamondz nataka kulewa was a runners up or something kwenye miss tz huko nyuma
waandishi wa habari wakipiga picha vidonge vya heroin alivyokamatwa navyo mremboi huyu wa kitanzania jackie cliff ambaye ni video queen wa bongo anadaiwa kukamatwa na dawa za kulevya nchini china star mmoja nchini aliyekataa
kutajwa jina lake aliutonya mtandao wa swahiliworldplanet bila kufafanua zaidi kwa kusema
kuwa jackie amekamatwa na madawa ya kulevya china
jackie cliff amekamatwa na unga china alisema star huyo huku akitutumia na picha za
mwanamke aliyefungwa kitambaa usoni baada ya kukamatwa na dawa hizo na mwanamke huyo anadaiwa ni jackie cliff angalia picha hizo hapo chini
hata hivyo baadhi ya mitandao jana iliweka habari za mwanamke mmoja wa kitanzania kukamatwa na dawa za kulevya huko china lakini bado habari hizo hazikubainisha mwanamke huyo ni nani na usiku huu ndiyo ikasemekana
ni jackie cliff habari hiyo inasomek kama ifuatavyo mwanamke wa kitanzania mwenye umri wa miaka 28 amekamatwa na kilo 11 za
dawa za kulevya aina ya heroin huko macao dawa hizo zilikutwa tumboni mwake baada ya kushtukiwa na kufanyiwa xray ambapo alikutwa na jumla ya
vidonge 66 vyenye thamani ya dola za kimarekani 137720
pichani ni mwanamke huyo wa kitanzania (akiwa amefunikwa uso) aliyekamatwa na kilo 11 za heroin huko macau hapo amepigwa picha na vidonge vyake kwenye press conference huko macau disemba 19 2013 | 2017-07-23T04:33:59 | http://folclassic.blogspot.com/2013/12/tazama-picha-zikionesha-jinsi-video.html |
serikali yaahidi kupeleka gari ya wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya manyoni wizara ya afya tanzania
wizara ya afya tuesday october 30 2018
naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto dkt faustine ndugulile akikagua cheti cha mgonjwa katika wodi ya akina mama wakati alipotembelea hospitali ya wilaya ya manyoni kuona hali ya utoaji huduma za afya
naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto dkt faustine ndugulile (kushoto) akikagua madaftari ya wagonjwa waliolazwa katika wodi ya akina mama wakati alipotembelea hospitali ya wilaya ya manyoni kuona hali ya utoaji huduma za afya kulia ni mkuu wa wilaya hiyo bi rahabu solomon
naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto dkt faustine ndugulile (kulia) akifafanua jambo wakati alipotembelea kitengo cha kuzalisha chakula cha lishe kwa mama wajawazito na watoto katika hospitali ya mtakatifu gasper kushoto ni mkurugenzi mtendaji wa hospitali hiyo fr seraphine lesiriam
naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto dkt faustine ndugulile akiongea na wananchi waliokuwa wakisubiri huduma hospitali ya rufaa ya mkoa wa singida wakati alipofanya ziara hospitalini hapo kuona hali ya utoaji wa huduma za afya
na wamjwsingida
serikali imetangaza neema ya kupeleka gari ya wagonjwa (ambulance) katika hospitali ya wilaya ya manyoni ili kutatua tatizo linaloikabidi wilaya hiyo hususan ya vifo vitokanavyo na uzazi
ahadi hiyo imetolewa jana na naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto dkt faustine ndugulile wakati alipoitembelea hospitali hiyo kwa lengo la kutazama utoaji wa huduma za afya ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu katika mkoa wa singida
dkt ndugulile amefikia uamuzi huo baada ya kusikiliza kero kutoka kwa wananchi wanaotumia hospitali hiyo ambapo wengi walisema kungekuwepo na gari ya wagonjwa kungeepusha vifo vya akina mama wajawazito na watoto pamoja na wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura
naomba niwaahidi wananchi wa manyoni serikali imeagiza magari ya kubebea wagonjwa ambayk yanaweza kufika mwezi disemba mwaka huuhivyo nitahakikisha katika mgao wa magari hayo basi na hospitali hii ya wilaya inapata gari moja kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wa hapa alisema dkt ndugulile
aidha dktndugulile aliahidi kuwatafutia wataalam wa afya watakaoweza kwenda kupunguza uhaba wa watumishi wanaokabiliana nayo hospitali hiyo
naye mganga mfawidhi wa hospitali hiyo dkt atupele mohamed alisema hospitali hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa majengo ikiwemo chumba cha huduma za uzazi ambapo uwezo wake kwa mwezi ni kuzalisha akina mama 90 lakini kwa sasa huzalisha wastani wa akina mama 400
aidha dkt atupele alisema hospitali hiyo ina upungufu mkubwa wa watumishi wenye sifa ambapo ina jumla ya watumishi 107 sawa na asilimia 53 ya watumishi wanaohitajika
dkt atupele alitaja uhaba mkubwa wa watumishi hao ni madaktari wauguzi wataalamu wa mionzi na wataalamu wa kutoa huduma za usingizi
katika wilaya hiyo naibu waziri huyo aliweza kutembelea kutembelea kituo cha kulea wazee na wasiojiweza cha sukamahela pamoja na hospitali ya rufaa ya mtakatifu gasper iliyopo itigi na kuridhika na hali ya utoaji wa huduma za afya katika hospitali hiyo
0 on serikali yaahidi kupeleka gari ya wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya manyoni | 2019-05-24T05:49:32 | http://afyablog.moh.go.tz/2018/10/serikali-yaahidi-kupeleka-gari-ya.html |
waziri mkuu aunga mkono juhudi za makonda za kupambana na dawa za kulevya | ishi kistaa
home news waziri mkuu aunga mkono juhudi za makonda za kupambana na dawa za
waziri mkuu aunga mkono juhudi za makonda za kupambana na dawa za kulevya
waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania kassimu majaliwa amesema kuwa serikali itapambana na janga la madawa ya kulevya kwa dhati bila kumuonea mtu yoyote na kuzingatia misingi sheria na haki
kauli hiyo ameitoa jana bungeni wakati akitoa hoja ya kuhairisha mkutano wa sita bunge la 11 mkoani dodoma
waziri mkuu amesema kuwa lengo la serikali ni kuwasaidia waathirika wa dawa za kulevya na kuwachukulia hatua kali wale warioathiri ambao ni wauzaji na wasambazaji wa dawa hizo hapa nchini
waziri mkuu amesema kuwa takwimu za jumla zinaonesha kuwa watanzania waliokamatwa ni 515 na wamefungwa katika magereza ya nchi mbali mbali kutokana na makosa hayo ya uuzaji wa dawa za kulevya
pia waziri mkuu amezitaja nchi ambazo watanzania wamefungwa kutokana na biashara hiyo ni china ambapo wapo watanzania 200 brazil wamefungwa 12 iran wapo 63 ethiopia wapo saba na afrika kusini wapo watanzania 296
waziri mkuu ameunga harakati za kupambana na madawa ya kuelvya zilizoanzishwa na mkuu wa mkoa wa dar es salaam paul makonda baada ya kuwataja wahusika wa biashara hiyo hapa nchini
previous articleshirika la nyumba visiwani zanzibar linahitaji bilioni 5 kwa ukarabati
next articlembaroni kwa kukutwa na shehena za dawa za kulevya chumbani kwake mkoani mwanza
waziri mkuu asema rubada itaangaliwa upya
mdee atiwa mbaroni kwa amri ya mkuu wa wilaya ya kinondoni | 2020-01-27T11:56:40 | http://www.ishikistaa.com/waziri-mkuu-aunga-mkono-juhudi-za-makonda-za-kupambana-na-dawa-za-kulevya/ |
thea afunguka kuhusu kufunga ndoa mwaka huu | raha za walimwengu
home » »unlabelled » thea afunguka kuhusu kufunga ndoa mwaka huu
thea afunguka kuhusu kufunga ndoa mwaka huu
staa wa filamu za kibongo salome urassa thea ameweka wazi kuwa baada ya kutengana na mumewe mike sangu na kukaa kimya muda mrefu sasa anatangaza rasmi kwamba mwaka huu ndio mwaka wake wa kuingia kwenye ndoa nyingine iwapo mungu atamjalia
thea alisema kuwa anavyoona yeye kwa mipango ya mungu mwaka huu atapata ndoa nyingine kwani ni mwaka wa baraka kwake
nitaolewa mwaka huu ni mwaka wa baraka na ninaamini mungu atanijaalia kama ninavyomuomba ili mambo na mipango niliyoipanga isiende tofauti alisema thea | 2018-01-20T11:03:22 | http://www.rahatupu.us/2018/01/thea-afunguka-kuhusu-kufunga-ndoa-mwaka.html |
chezea twanga wewe | spoti na starehe
chezea twanga wewe
sale sale sale saletaarifa kwa wenye mabendi african stars band inapenda kuwatangazia wamiliki wa bendi hapa nchini kuwa inauza wacheza show wake wanne1 asha sharapova aka cristiano ronaldo tsh mil 20/= 2 fasha aka lionel messi tsh mil 20/=3 mary kimwana aka van persie tsh mil 10/=4 mariam kiduku aka mario balotelli tsh 10/=
hahahaha nilifurahishwa na huu utani wa kuwanadi ma dancer wao kwenye mtandao wa kijamii bendi ya twanga pepeta inajikusanya upya baada ya kuondokewa na wanamuziki wake lakini hivi karibuni kiongozi wa bendi hiyo asha baraka alipokuwa akihojiwa na kipindi cha mkasi cha salama jabri alisema kuwa twanga ni kama chuo kila kukicha kuna watu wapya wana graduate na kwa mashabiki wa twanga wanasema kuwa haiwasumbui mtu kutoka kwani anatoa pengo kwa mwingine mpya kuonekana
this entry was posted on sunday march 11th 2012 at 343 am and is filed under michezo you can follow any responses to this entry through the rss 20 feed | 2017-04-25T00:49:36 | https://spotistarehe.wordpress.com/2012/03/11/chezea-twanga-wewe/ |
tanzanian community in romeitaly( comunita' tanzaniana a roma) tangazo maalum kwa watanzania italy
tangazo maalum kwa watanzania italy
tangazo kwa watanzania nchini italia
jumuiya ya watanzania italia na jumuiya ya watanzania roma zinawafahamisha kuwa mwili wa marehemu ally kijuu juma utaagwa siku ya jumatatu tarehe 20 januari mjini roma kwenye camera mortuaria ospedale policlinico tor vergata iliyopo kwenye mtaa wa viale oxford 81 kuanzia saa nne asubuhi tunaombwa tufike mapema na kwa wingi ili tuweze kuuaga mwili wa mtanzania mwenzetu kabla ya kusafirishwa kwenda tanzania kwa mazishi mwili utaondoka policlinico saa sita kamili mchana
hapo kwa chini kuna ramani ya sehemu tutakapo uaga mwili wa marehemu kwa usafiri wa kizalendo mnaweza kuchukua metro linea a kwa mfano tokea termini mpaka anagnigna mkishuka anagnina chukueni bus namba 20 direction cambellotti then shukeni baada ya vituo 10 kwenye kituo kinachoitwa heidelberg baada ya hapo ni mguu kwa mita 500
vile tunapenda kuwafahamisha kwamba kesho mjini napoli mwili wa marehemu abdalla maulid hamid utaagwa mida ya saa tano asubuhi tunawaomba watanzania popole pale mlipo nchini italy mfike kwa wingi tuweze kuuaga mwili wa marehemu abdallah
rip ally kijuu juma na abdalla maulid hamid
katibu wa jumuiya ya watanzania roma
posted by andrew chole mhella at 20700 pm | 2017-08-19T16:53:34 | http://watanzania-roma.blogspot.com/2014/01/tangazo-maalum-kwa-watanzania-italy.html |
tanzania one hatimaye tundaman aamsha akinamama tandale dar
msanii wa muziki wa bongo fleva ambaye pia ni balozi wa kampeni ya amsha mama 2016 tundaman (kulia) akiongea jambo na mama rishe sophia amri au maarufu kwa jina la mama dayna muda mfupi baada ya kumkabidhi kiasi cha shilingi laki moja ikiwa ni njia mojawapo ya kutekeleza kampeni ya amsha mama 2016 aliyoanza kutekeleza majuku yake mapema leo katika soko la tandale jijini dar es salaam anayeshuhudia zoezi hilo kushoto kwake ni mkurugenzi wa kampeni hiyo joe kariuki
balozi wa kampeni ya amsha mama 2016 tundaman (katikati) akimkabidhi kiasi cha shilingi laki moja antonia msomboki ambaye ni mfanya biashara wa matunda katika soko la tandale jijini dar mapema leo
balozi wa kampeni ya amsha mama 2016 tundamani akikatiza kwenye mitaa ya tandale na baadhi ya wanahabari waliojitokeza kushuhudia tukio hilo
tundaman aamsha akinamama tandale
kariuki alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha akina mama katika tamasha litakalowakutanisha na akinamama wengine kutoka nchi mbalimbali afrika kwa lengo la kujifunza na kupewa utaalam na jinsi kukuza biashara zao | 2017-11-22T09:12:40 | http://mateja20.blogspot.com/2016/02/hatimaye-tundaman-aamsha-akinamama.html |
pagale na eneo sqm 378 dodoma mjini in tanzania | zoomtanzania
pagale na eneo sqm 378 dodoma mjini
804526
4 sep 1145
dodoma mjini dodoma mbanga(mtaa unaofuata baada ya nkuhungu)
nauza pagale lipo mbwanga(mtaa unaofuata baada ya nkuhungu)
2lina ukubwa wa karibu mita 21 kwa 18
3maji na umeme vipo
4lina hati ya mtaa pamoja na risiti za kulipia jengo
5umbali toka barabara kuu ya lami iendayo singida/mwanza/tabora ni kama mita 400/500
6umbali toka katikati ya mji ni kama kilomita 7
8ni eneo zuri sana kwa makazi mana nyumba zimejengwa kisasa na pana mandhari nzuri sana
9pagale na eneo ni milioni 5 tu
10eneo bila pagale ni milioni 3
pungufu tutaongea
steven masaka
member since 30 dec '15 9 active ads active ads 14 published ads
+255767833496 | 2017-11-22T01:52:54 | https://www.zoomtanzania.com/land-for-sale/pagale-na-eneo-milioni-5-dodoma-mjini-0767833496-804526 |
kuhusu sisi amka mtanzania
kuhusu amka mtanzania
karibu sana kwenye mtandao wetu wa amka mtanzania
amka mtanzania ni mtandao ambao umejikita katika kutoa makala za mafunzo na hamasa kwa watu wote ambao wanapenda kupiga hatua kwenye maisha yao
mtandao huu ni nyumbani kwa wale wote ambao wanapenda kufanikiwa zaidi kwenye maisha yao kwenye kila eneo la maisha kuanzia fedha kazi biashara mahusiano familia na afya
kupitia mtandao huu kila siku unapata makala zenye mafunzo na hamasa ya kupiga hatua zaidi ili kuweza kufanikiwa
kupitia amka mtanzania pia utapata mafunzo na ushauri wa kina kuhusu biashara fedha uwekezaji na mafanikio
kupitia amka mtanzania utajijengea uwezo wa kujiamini na kuepuka kukata tamaa hata pale unapokutana na changamoto au hali ngumu
huduma zetu
pamoja na mafunzo mazuri unayopata kupitia makala zilizopo kwenye mtandao huu unaweza kupata huduma nyingine nzuri zaidi kupitia mtandao huu
zifuatazo ni huduma nzuri unazoweza kupata kwenye amka mtanzania ambazo zitakuwezesha kufanikiwa zaidi
vitabu vya biashara na mafanikio
hapa unaweza kupata vitabu vizuri vya biashara na mafanikio kwa ujumla vitabu hivi vipo kwenye mfumo wa nakala tete (softcopy) na nakala ngumu (hardcopy)
kupata utaratibu wa vitabu bonyeza maandishi haya
kundi maalumu la mafunzo
lipo kundi maalumu la mafunzo ambalo unaweza kujiunga na kuendelea kujifunza zaidi kila siku kundi hili lipo kwenye mitandao ya wasap na telegram ili uweze kuingia kwenye kundi hili unapaswa kujiunga na kisima cha maarifa
kujiunga na kisima cha maarifa bonyeza maandishi haya ili kupata maelekezo
ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa kocha makirita amani
unaweza kupata ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa kocha makirita amani kwa njia ya makala au moja kwa moja kusoma makala za ushauri bonyeza maandishi haya
kupata ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa kocha makirita bonyeza hapa kupata utaratibu kamili
kupata blog na kutengeneza kipato kwenye mtandao
kupitia mtandao huu unaweza kujifunza na kupata blog ambayo utaweza kuitumia kutengeneza kipato kwenye mtandao wa intaneti
kuweza kupata huduma hii bonyeza maandishi haya
kupokea makala na mafunzo moja kwa moja kwenye email yako
kuna makala na mafunzo ambayo yanatumwa moja kwa moja kwenye email yako kupata huduma hii ambayo ni bure kabisa bonyeza maandishi haya
kwa mawasiliano zaidi kuhusiana na chochote kwenye mtandao huu unaweza kutumia njia zifuatazo
namba za simu +255 717 396 253 au +255 755 953 887
email maarifa@kisimachamaarifacotz au amakirita@gmailcom
karibu sana tufanye kazi pamoja kwa mafanikio yako
3 thoughts on kuhusu sisi
mbaruku mickdad says
nimekusoma ndugu vyote hivyo kunielekeza mpaka nikafahamu utaratibu wake ukoje nimeonna umuhimu wa mwalimu ndugu yangu na kwa hili naomba uwe mwalimu wangu wa masomo haya nami napenda kuwa bloger mzuli na mkubwa
habari mbaruku
karibu sana niko tayari kuwa mwalimu wako nafikiri nilishakutumia maelezo ya mentorship program tunaweza kuanzia hapo na ukajifunza mengi sana
chatguestcom says
habari mtaalamu mimi nakubali kazi yako ya kuelisha jamii sasa nina zawadi kwa ajiri ya amkamtanzania zawadi yenyewe ni hii copy kisha search http//youtube/v6esyingcm0 nitafurahi ukiipokea sina kingine kikubwa cha kukupa amkamtanzania | 2019-07-20T09:36:16 | https://amkamtanzania.com/huduma/comment-page-1/ |
ppf wakabidhiwa rasmi jengo jipya la kisasa walilojenga jijini arusha lenye thamani ya bilioni 325 zanzinews home | 2017-01-23T08:22:59 | http://www.zanzinews.com/2016/02/ppf-wakabidhiwa-rasmi-jengo-jipya-la.html |
dustless blasting machine china qingdao antai heavy viwanda
dustless blasting mashine ni kutumika kwa kila filed katika dunia kama vile automative marine reginery fleet magari graffiti kuondolewa stripe removal vifaa vya nzito uso kusafisha poda mipako offshore mbao marejesho asbestos abaement
wetu mashine dustless blasting hasa iliyoundwa na kuunganishwa na mbalimbali ya nozzles mvua attachments mlipuko ndani ya vifaa bomba kusafisha vumbi bure ulipuaji vichwa abrasive kudhibiti kifaa
dustless blasting inatambua mahitaji ya sekta na mashine yetu inatoa makala yote kwamba matumizi ya kitaalamu inahitaji mashine zote inaweza zimefungwa pamoja iliyoundwa na kuthibitika moja kipande kijijini kudhibiti kufa mtu kubadili na silencer ambayo kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za kazi kuboresha ufanisi wa abrasive utendaji na usalama
mashine ni kujengwa kwa kiwango cha juu 150 psi shinikizo kazi nyumatiki abrasive kijijini kudhibiti valve wanaweza kufikia watoa kuacha au kuanza
ufundi paramete
ulipuaji mode
hewa ndege
1cubic mguu
2cubic mguu
5cubic mguu
8cubic mguu
15cubic mguu
30cubic mguu
mlipuko huo
~ dakika 30
~ masaa 23
~ saa 46
kilo 120
uendeshaji shinikizo
ulipuaji urefu hose
mita 15
(2) mahitaji kwa ajili ya kujazia hewa
(3) ni pamoja na
a blast hose (inner mduara ni 32mm)
b deadman valve activator
c tungsten carbide pua (mduara ni 10mm)
d jaza faneli
e lifetime udhamini juu ya mlipuko sufuria
(4) za matumizi
kutu kiviza
1high quality uso kuonekana
2high ufanisi tija
gharama 3low
4environmental kirafiki
5lower matumizi abrasive
6safe hakuna kuzua
7less uchafuzi
8not muhimu kuacha kazi jirani
9removes kuongeza kwa rangi tayari juu ya ardhi
10 matoleo tu nafasi ya maegesho
11 je si kukunja chuma
12 majani primertayari uso
13 easy kusafisha
14 huzuia kutu kwa saa 72
dustless blasting mashine mchakato uchoraji
dustless blasting mashine ya kusafisha uso ufanisi
dustless ulipuaji mchakato wa kujifungua
dustless blasting mashine maelezo picha db150 & db225 & db500 & db800
australia wateja alitembelea kiwanda yetu checked blaster dustless
awali mchanga blasting machine
next mchanga ulipuaji kibanda
air blast vyumba
moja kwa moja blast machine
blast magurudumu
ulipuaji abrasive
ulipuaji kusafisha chumba
ulipuaji mashine
ulipuaji mashine chuma
ulipuaji uchoraji
ulipuaji pot machine
ulipuaji turbine
akitoa viwanda shot blasting machine
vumbi free blasting machine
vumbifree sandblasting machine
dustless blast baraza la mawaziri
dustless blasting gharama
dustless blasting vifaa kwa sale
dustless blasting machine kwa sale
dustless blasting machine bei
dustless blasting mkono
nje ya bomba blasting machine
kiwanda moja kwa moja ya kuuza blast pot
grit blasting baraza la mawaziri
high pressure blaster water
high quality ulipuaji vifaa
mabomba blasting machine
mabomba ya nje blasting machine
mabomba ya ndani blasting machine
shinikizo ulipuaji pot kwa sale
rotary indexing aina blasting machine
chuma grit blasting equipment
uso machine blast
kutumika water blasting vifaa kwa sale
kutumika wet blasting equipment
wet blasting baraza la mawaziri | 2019-10-23T00:54:34 | https://www.antaigroup-china.com/sw/dustless-blasting.html |
msiba mwingine jimbo la ilemela ~ g sengo
msiba mwingine jimbo la ilemela
wednesday june 27 2018 bango no comments
mbunge wa jimbo la ilemela ambae pia ni naibu waziri wa wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi mhe dkt angeline s lubala mabula amepokea kwa mshtuko mkubwa na masikito taarifa za kifo cha aliyekuwa diwani wa viti maalum manispaa ya ilemela kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) mhe dotto ponsian balilemwa wa kata ya nyamanoro
aidha mhe mbunge anawapa pole ndugu jamaa marafiki wananchi wote viongozi wa chama na serikali walioguswa na msiba huo huku akiwataka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao
' bwana ametoa bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe ' | 2018-11-21T04:21:25 | https://gsengo.blogspot.com/2018/06/msiba-mwingine-jimbo-la-ilemela.html |
serikali yajipanga 'kutangaza tenda' kubinafsisha treni ya mwakyembe shommi b 'if(findexof(imgyoutubecom)=1){w=' '}z=w+''+titlex+'
home » »unlabelled » serikali yajipanga 'kutangaza tenda' kubinafsisha treni ya mwakyembe
serikali yajipanga 'kutangaza tenda' kubinafsisha treni ya mwakyembe
baada ya serikali kubuni na kufanikiwa kuanzisha na kuendesha usafiri wa treni jijini dar es salaam sasa inajipanga kubinafsisha usafiri huo unaosaidia kupunguza msongamano waziri wa uchukuzi dk harrison mwakyembe alisema hayo bungeni jana wakati akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2013/2014
alisema serikali inakamilisha mchakato wa kumpata mwekezaji na mwendeshaji wa huduma hiyo jijini humo
kwa mujibu wa dk mwakyembe kampuni hodhi ya rasilimali za reli tanzania (rahco) ndiyo itakayokamilisha mchakato wa kumpata mwekezaji na mwendeshaji wa huduma hiyo atakayetumia miundombinu ya reli iliyopo na vichwa vya treni na mabehewa maalumu ya usafiri katika miji
dk mwakyembe alisema mwitikio wa wananchi kutumia huduma ya treni ya abiria umekuwa mkubwa ikilinganishwa na uwezo wa kutoa huduma yenyewe hususan nyakati za mahitaji makubwa ya usafiri
wingi wa abiria kwa sasa kwa mujibu wa dk mwakyembe treni hiyo ya jijini dar es salaam inabeba watu 14000 kwa kila siku sawa na zaidi ya daladala 467 zenye uwezo wa kubeba abiria 30 kila siku
kwa upande wa tazara wastani wa idadi ya abiria wanaosafiri kwa treni kwa siku umefikia 9000 baada ya kukamilika kwa ukarabati wa mabehewa mengine saba na kichwa kimoja cha treni na kuanza kutumika rasmi mei 9 2013
aidha kwa upande wa trl wastani wa abiria wanaosafiri kwa siku ni 5000 aliongeza dk mwakyembe akizungumzia usafiri huo ulioanza oktoba mwaka jana kati ya stesheni na ubungo maziwa na kati ya tazara na mwakanga
faida changamoto alisema kuanzishwa kwa usafiri huo wa treni jijini dar es salaam kumesaidia kumepunguza idadi ya magari barabarani
kuanza kwa usafiri huu kumeshawishi baadhi ya wananchi waliokuwa wanatumia magari binafsi kuja katikati ya jiji la dar es salaam kuanza kutumia usafiri wa treni alisema dk mwakyembe
alizitaja baadhi ya faida zingine zinazotokana na usafiri huo kuwa ni kupungua kwa matumizi ya mafuta muda unaotumika barabarani na hivyo kusaidia wananchi kufika kwa wakati katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii
alisema wizara inaendelea kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zilizojitokeza zikiwamo za kutokuwa na mfumo thabiti wa kukusanya mapato uchakavu wa miundombinu na uhaba wa injini na mabehewa
kuhusu kuongeza huduma za usafiri huo alisema wizara imeunda kamati maalumu chini ya uenyekiti wa naibu waziri wa uchukuzi dk charles tizeba ili kuchambua kuainisha na kushauri mipango na mikakati ya kuboresha na kupanua usafiri huo
ruti mpya pia wizara inaangalia uwezekano wa kuanzisha huduma maalumu ya treni kati ya stesheni ya dar es salaam na gongo la mboto kwa ajili ya kuhudumia abiria wanaopita kwenda kiwanja cha ndege cha kimataifa cha julius nyerere alisema dk mwakyembe
kwa upande wake kamati ya kudumu ya bunge ya miundombinu ilishauri kuwa ili mradi huo ufanye kazi kwa ufanisi na kuondokana na hasara serikali iharakishe kununua angalau treni mbili za kisasa na maalumu kwa safari fupi ambazo gharama yake ni sh bilioni 8 kila moja
chanzo sufianimafotoblog | 2017-08-17T17:17:37 | http://shommibinda.blogspot.com/2013/05/serikali-yajipanga-kutangaza-tenda.html |
niligonga mtu na gari usiku je nimueleze huu mkasa
ww ni binadam miongoni mwa binadam sent using jamii forums mobile app
brother umeuwa sent using jamii forums mobile app
k2206 hiyo ni kwa line za airtel na tigo pekee ndo majina yanaweza kubadilika kama ulisajili kwa majina mengine au kwa kutumia kitambulisho cha mtu mwingine lakini kwa mtandao wa vodacom lazima usajili kwa kitambulisho husika na taarifa zako za mwanzo laima ziendane na taarifa utakazotoa
nashukur sana mkuu kwa majib yako sent using jamii forums mobile app
asante mkuu kwa majib yako mazuri sent using jamii forums mobile app
sawa mkuu sent using jamii forums mobile app
mkuu bdo inazingua aiseee hv ndivyo inavyofanya hii ni android 60 sent using jamii forums mobile app
sorry mkuu nmekosea iko hv simu yng samsung galaxy s6 edge+ model number smg928a sent using jamii forums mobile app
nmetumia link hii hapa mkuu but cjui ni gcam ipi sent using jamii forums mobile app
mm najarib kuifungua gcam inazingua inaniambia unfortunately camera has stopped sent using jamii forums mobile app
hivi mnawezaje kuishi na watu wa namna hii
polee sana mkuu ukitambua kuwa binadam sis huwa haturidhiki utaish maisha yako pasipo kumwangalia mtu tambua kuwa hapo ulipo huna ajira bdo tu unasaka wapi utapata wanakusema je cku mungu akinyoosha mkono wake ukapata unadhani hautasemwa cha msingi hapo ww fuata mambo yako
mume wangu kaniacha kisa nimemtukania mama yake nataka kujiua nipeni ushauri
unasubir nn
siku zote ukweli huwa mchungu
binti fahamu hili
sauti kama ipo chini vile
wanaume mnapenda kutubebesha lawama
hakumsingizia bali alisema ukwel kutokana na kile ambacho alikifanya mwanamke
ni nyimbo gani kila ukiiskiliza inakukumbusha mbali
jim reeves album zake zote
ni chuo gani kinafundisha u operetta wa crein
sio cren ni crane | 2020-01-29T17:28:21 | https://www.jamiiforums.com/search/5538860/ |
kubeti rugby mitandaoni tanzania kubeti michezo mitandaoni tanzania parimatch
home > blog > kubeti rugbymitandaoni tanzania kubeti michezo mitandaoni tanzania parimatch
zinazobamba kwenye kubeti rugby
kubeti rugby ni kitu gani ufafanuzi wa kina
wakamalia hutengeneza beti zao kwa bookmakers waliokuwa wazuri na kubeti rugby ni miongoni mwa wanaowezesha
duniani kote au umaarufu wa kubeti rugby
kawaida michezo haina mipaka maslahi ya kawaida pamoja na kubeti rugby huwa inaunganisha watu unatumia muda wako kutazama timu unazozitegemea zaidi ni jambo zuri zaidi kwani linawafanya watu wawasiliane kupitia mashabiki wa michezo hiyo pamoja na wale wanaopenda kubeti soka kwa upande mwingine hii ina msaidia mtumiaji kupata marafiki wenye tabia kama zake pamoja na hayo pia ni dream job
unaweza kukusanya pamoja vile unavyovipenda na ukapata pesa hiyo ndio sababu betting inaendelea ikiwemo kubeti rugby ambayo imekuwa maarufu ulimwenguni kote
mamilioni ya mtandao wa michezo ya kubahatisha imeonyesha thamani ya kweli ya kubeti rugby hivyo basi unaweza ukachagua aina ya michezo na uangalie juu ya ujuzi ulionao katika kubashiri kwa mfano umepata ugumu kwenye kusuka mkeka katika michezo hii
sisi ni mabingwa au jamii ya kubeti rugby
tukizungumzia juu ya mwenendo wa kisasa wa michezo kubeti rugby ndio ya kwanza itatajwa ni rahisi kujisajili inavutia na ufanisi mkubwa masuala ya kubeti michezo hutoa faida nyingi jaribu hii | 2020-05-26T19:53:51 | https://thebeauty.co.tz/sw/betting-rugby |
ta rivala | xalamuka september 2012
eku sunguleni ka lembe ra 2011 a ku ri ni tiselfoni ta 54 wa tibiliyoni leti a tirhisiwa hi vanhu emisaveni hinkwayomagazini wa un chronicle wa le usa
eka malembe lama tlulaka khume lama hundzeke timhangu ti dlaye vanhu vo tlula 780 000 naswona lava endlaka kwalomu ka 60 wa tiphesente va dlayiwe hi ku tsekatseka ka misavaphephahungu ra the lancet ra le britain
eka malembe lama tlulaka 20 lama hundzeke vanhu va kwalomu ka 800 000 va le rhaxiya va tidlayilephephahungu ra rossiiskaya gazeta ra le rhaxiya
etikweni ra philippine laha ku dlaya vukati swi nga pfumeleriwiki nhlayo ya vavasati va 15 eka va 49 lava tshamaka ni vavanuna lava va nga catangiki na vona kumbe lava nga tekiwangiki hi nawu yi phindheke minkarhi leyi tlulaka yimbirhi exikarhi ka 1993 na 2008phephahungu ra the philippine star ra le philippine
le riphabliki ra georgia vaakatiko lava endlaka 792 wa tiphesente va khomiwe hi mavabyi lama vangiwaka hi ku hefemula musi wa fole edorobeni ra tbilisi leri nga ntsindza wa tiko rero vana lava endlaka tiphesente ta 877 va khomiwe hi mavabyi wolawomagazini wa tabula wa le georgia
vanhu va ya easia leswaku va ya tshunguriwa
vavabyi vo tala lava humaka ematikweni yo hambanahambana ya misava va ya easia leswaku va ya tshunguriwa naswona hakanyingi mali leyi va yi hakelaka kwalaho i yitsongo swinene loko yi pimanisiwa ni leyi a va ta yi hakela ematikweni ya ka vona phephahungu ra business world ri vika leswaku ku languteriwe vanhu lava ringanaka miliyoni leswaku va endzela tiko ra philippine hi 2015 leswaku va ya tshunguriwa naswona ku languteriwe nhlayo leyi fanaka leswaku yi ya tshunguriwa etikweni ra korea dzonga hi 2020 matiko manwana lawa vavabyi va rhandzaka ku ya tshunguriwa eka wona i india malaysia singapore na thailand a hi vanhu va le vupeladyambu ntsena lava lavaka ku tshunguriwa mavabyi yo tanihi ya mbilu ni ku lamala ka longo phephahungu rero ri tlhela ri vika leswaku machayina yo tala lawa ma ha ku fuwaka na wona ma ya eka madokodela lama endlaka vuhandzuri byo cinca xivumbeko xa munhu va ri ni swifaniso swa vanhu lava dumeke lava ma lavaka ku languteka ku fana na vona
nhwarimbirhi yinwe yi tshwa nkanga
thekinoloji hakanyingi yi sindzisa vatirhi ku endla mintirho yimbirhi kumbe yo tala leyi rharhanganeke hi nkarhi wunwe ni ku hlamula swivutiso hi ku hatlisa hambiswiritano clifford nass mukongomisi wa ndzawulo ya communication between humans and interactive media laboratory eyunivhesiti ya stanford le usa u ri vatirhi lava endlaka swilo swo tala hi nkarhi wunwe a va swi endli kahle ku vuriwa leswaku vanhu lava endlaka mintirho yo tala hi nkarhi wunwe hakanyingi va khomiwa hi ntshikilelo va kavanyetiwa hi ku olova hi swilo leswi nga riki swa nkoka a va dzikisi mianakanyo ya vona eka leswi va swi endlaka xisweswo va honisa vuxokoxoko bya nkoka nass u nyikele xiringanyeto lexi loko u sungula ntirho wo karhi tinyike timinete ta 20 leswaku u endla wona ntsena leswi swi ku dyondzisa ku dzikisa mianakanyo ya wena eka leswi u swi endlaka | 2019-12-06T21:57:06 | https://www.jw.org/ts/layiburari/timagazini/g201209/ta-rivala/ |
serikali kuu ya muungano siku 100 madarakani berlin | magazetini | dw | 26032014
serikali kuu ya muungano siku 100 madarakani berlin
siku 100 za serikali ya muungano wa vyama vikuu mjini berlinsheria mpya ya halmashauri kuu ya umoja wa ulaya kuhusu mazao ya bio na bayern munich kutawazwa mabingwa wa ligi kuu ya kandanda ya ujerumani magazetini
kikao cha baraza la mawaziri walipokuwa wanakula kiapo disemba 17 mwaka 2013
tunaanzia berlin kumulika siku mia moja tangu serikali ya muungano wa vyama vya kihafidhina vya christian democratic unioncduchrisian social union csu na wasocial democrats wa spd ilipoingia madarakanihawakuanza vibayahakuna malumbano hata kashfa ya edathy haikuwatia kishindo au washirika wadogo spd ndio wanaong'ara ni miongoni mwa vichwa vya habari habari magazetini gazeti la münchner mercur linaandikasiku mia moja za muungano wa vyama vikuu zinabainisha wasoshial democrat ndio walioshinda mashindano ya awamu hii ya kwanza madarakanihakuna aliyewapitanaiwe katika suala la malipo ya uzeenikiwango cha chini cha mshaharamalipo ziada kwa wazee au kuwekewa kikomo kodi za nyumbasote tunabidi tutambue kwamba tija ya uchaguzi wa leowatoto na wajukuu zetu ndio watakaotakiwa wailipie keshohapo serikali ina nafasi ya kurekebisha mambo sawa na vile inavyopaswa irekebishe katika suala la mageuzi ya nishati
mtaka cha mvunguni huinama
mbonga na mhuri wa bio
imani ya mnunuzi imepungua linapohusika suala la mazao ya bio au yale mazao ambayo tangu mwanzo mpaka mwisho hayatumiliwi mbolea za sumu na kadhalikaili kutuliza hofu za wanunuzi na kurejesha imanihalmashauri kuu ya umoja wa ulaya imetangaza sheria mpyagazeti la esslinger zeitung linaandika ni sawa kabisa kuiona halmashauri kuu ya umoja wa ulaya inawajibika na kutangaza viwango vya chini kabisa vya mabaki ya dawa ya kuuwa wadudu waharibifu katika mazao ya biokwamba baadae mazao hayo yanabidi yachunguzwesi suala la kuulizwa usalama wa wanunuzi hauwezekani bila ya urasimumtaka cha mvunguni huinamakila mmoja atabidi atambue akitaka bio atabidi alipie bio
bayern munich watawazwa kwa mara ya 24 mabingwa wa ligi kuu
watoto wa bayern munich wanyanyuwa taji la ubingwa wa ligi kuu
mada yetu ya mwisho magazetini inahusu kabumbujana usiku timu mashuhuri ya ujerumani bayern munich imevikwa taji la ubingwa wa ligi kuu bundesliga hata kabla ya michuano kumalizikagazeti la berliner morgenpost linaandika kama ilivyokuwa ikitarajiwawatoto wa fc bayern munich wamenyakuwa taji la mabingwa wa ligi kuukwa wengi wa mashabiki wake lakini taji hilo la 24 katika historia ya bayern munich lilitiwa ila kidogohata hivyo ni jambo la kawaida kwa kila kitu kutiwa ila humu nchinikuna wanaowamezea mate na wengine wanaowaonea kijicho
mada zinazohusiana jeshi la ujerumani bundeswehr bayern munich ujerumani bonn frankwalter steinmeier mkutano wa usalama munich helmut kohl bundeswehr giz shirika la ushirikiano wa kimataifa la ujerumani
maneno muhimu serikali kuu ujerumani bio bayern munich
kiungo http//pdwcom/p/1bvrz | 2018-03-18T14:18:08 | http://www.dw.com/sw/serikali-kuu-ya-muungano-siku-100-madarakani-berlin/a-17520429 |
riwaya mwanafunzi mchawi ( a wizard student ) sehemu ya pili | ubuyu
riwaya mwanafunzi mchawi ( a wizard student ) sehemu ya pili
ilipoishia sehemu ya kwanza ( kama hukuisoma bofya hapa)
wakati
wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao doreen alikuwa amejitenga peke yake nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na giza totoro alikuwa
uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe sehemu ya pili doreen aliendelea kuongea maneno aliyoyajua mwenyewe akiwa bado yupo uchi wa mnyama nyuma ya bweni alilokuwa anaishi ghafla kipande kidogo cha karatasi nyeupe kikashuka mikononi mwake bila kuonekana kilikotokea doreen alicheka kwa sauti kali ya kutisha sana kisha akalikazia macho karatasi lile matone ya damu yaliangukia kwenye karatasi lile kutoka kwenye macho yaliyotisha sana ya doreen kwani yalikuwa na rangi nyeusi halafu yakawa na umbile kama macho ya paka
wakati eddy na dorice wakiendelea kuzungumza maneno hayo doreen alikuwa nyuma ya mti waliosimama hivyo alisikia kila kitu roho ilimuuma sana kwani tangu alipohamia shuleni hapo alitokea kumpenda sana eddy na alitamani awe mpenzi wake kwani ndio chaguo la moyo wake lakini dorice alikuwa kikwazo
ilikuwa asubuhi tulivu sana majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi ambapo mwalimu dayana mbeshi aliwahi ofisini kwake kama ilivyokuwa kawaida yake majengo ya ofisi yalimkaribisha kwa shangwe naye akaitikia ukaribisho huo kwa kufungua ofisi yake kisha akasogeza mapazia ya dirishani ili kuruhusu mwangaza wa jua changa uweze kupenyeza vizuri baada ya kukamilisha yote hayo madam mbeshi akasogeza kiti chake karibu na meza kisha akaketi halafu akaanza kusogeza vitu vilivyokuwepo mezani pale lakini ghafla akakutana na karatasi chafuchafu mezani kwake lakini ilikuwa na maandishi akashtuka kidogo halafu akaichukua ili aisome vizuri mwalimu mbeshi hakutaka kuamini kile alichokiona akataharuki kwa hofu na mshangao | 2017-02-28T14:47:31 | http://www.ubuyublog.com/2016/06/riwayamwanafunzi-mchawi-wizard-student.html |
jumatatu 18 aprili 2016 1239
hali ya mambo nchini libya inatajwa kuwa ni tete licha ya kuanza kazi serikali ya umoja wa kitaifa iliyoungwa mkono na kukaribishwa na jamii ya kimataifa
mwakilishi wa umoja wa mataifa katika masuala ya libya martin kobler ametangaza kuwa wafanyakazi wa ofisi ya umoja huo wamerejea libya kwa ajili ya kuanza shughuli zao kobler amesema maafisa hao wanahitajia mawasiliano ya kudumu na pande zote za kisiasa na makundi ya jamii ya libya wafanyakazi wa umoja wa mataifa waliondoka libya katika vita vya msimu wa joto wa mwaka 2014 baada ya muungano wa makundi yenye silaha unaojiita fajr libya kudhibiti mji wa tripoli
wakati huo huo naibu waziri mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya libya ametangaza kuwa wizara za michezo na vijana masuala ya jamii nyumba na ya huduma za umma zitakabidhiwa kwa serikali ya maridhiano ya kitaifa hii leo jumatatu
libya ambayo ilitumbukia katika machafuko na ghasia baada ya kuondolewa madarakani utawala wa kanali muammar gaddafi hapo mwaka 2011 katika miezi ya hivi karibuni imekuwa kwenye hali tete kutokana na kushadidi hitilafu na mapigano ya ndani kwa upande mmoja na hujuma na mashambulizi ya makundi ya kigaidi hususan daesh katika upande mwingine kwa kuzingatia hali hyo makundi mbalimbali ya kisiasa hatimaye yamechukua uamuzi wa kutia saini makubaliano ya amani na kuunda serikali ya umoja wa kitaifa chini ya upatanishi wa umoja wa mataifa
kwa sasa maafisa wa ngazi za juu wa nchi za magharibi wanaonekana kuitembelea libya siku chache zilizopita mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za ufaransa na ujerumani walitembelea nchi hiyo kwa mazungumzo rasmi wataalamu wa mambo wanasema mbali na kujadili masuala ya harakati za makundi ya kigaidi nchini libya viongozi hao wa nchi za kigeni hususan ulaya wako mbioni kugawana keki ya libya na kudumisha malengo yao ya kikoloni chini ya mwavuli wa masuala ya kibinadamu
maafisa hao wa kigeni wametoa mapendekezo ya kufanya mashambulizi ya kijeshi kwa ajili eti ya kuliangamiza kundi la kigaidi la daesh suala ambalo limepingwa na waziri mkuu wa nchi hiyo fayez al siraj ambaye amesema mashambulizi yoyote ya kijeshi nchini humo yatahesabiwa kuwa ni uvamizi dhidi ya libya
pamoja na hayo yote hali ya ndani ya libya bado si shwari jumamosi iliyopita baada tu ya safari ya mawaziri wa mambo ya nje wa ufaransa na ujerumani mjini tripoli kulishuhudiwa mapigano makali katika mji huo mapigano hayo yalishadidi zaidi katika eneo la andalusia lenye idadi kubwa ya balozi za nchi za kigeni na makazi ya wanasiasa na viongozi wa serikali ya umoja wa kitaifa
kwa vyovyote vile inatarajiwa kuwa umoja wa mataifa na jumuiya nyingine za kimataifa zitachukua hatua madhubuti zaidi za kuisaidia serikali ya umoja wa kitaifa ya libya kudhibiti kikamilifu hali ya mambo na kukomesha kabisa mgogoro wa ndani wa nchi hiyo
zaidi katika kategoria hii « machi 8 siku ya kimataifa ya wanawake tathmini juu ya hali ya wanawake barani afrika kugonga mwamba kikao cha opec mjini doha » | 2017-11-21T02:46:27 | http://kiswahili.irib.ir/uchambuzi/item/56461-hali-tete-ya-libya |
ubushinjacyaha bwagaragaje uko bazeye yakwizaga amakuru agamije kwangisha u rwanda amahanga igihecom
kuya 24 kamena 2020 saa 0303
ubushinjacyaha bwagaragarije urukiko ko laforge fils bazeye wari umuvugizi wa fdlr yakoresheje imvugo nyinshi ashinjwa ingabo zu rwanda kwica abaturage muri congo ibintu buvuga ko yakwizaga amakuru atari yo agamije kurwangisha amahanga
kuri uyu wa kabiri nibwo urukiko rukuru urugereko ruburanisha ibyaha mpuzamahanga rwakomeje kuburanisha urubanza ruregwamo bazeye na nsekanabo jean pierre alias abega wari ushinzwe iperereza muri uwo mutwe
ubushinjacyaha bwakomeje kugaragaza ibimenyetso ku byaha bubarega birimo kurema umutwe wingabo utemewe ubwicanyi no kuba mu ishyirahamwe ryiterabwoba
ni urubanza rwabaye abaregwa batari mu cyumba cyuruko ruba mu buryo bwikoranabuhanga mu kwirinda icyorezo cya coronavirus ubushinjacyaha buri ku cyicaro cyabwo abaregwa bari kuri gereza ya nyarugenge naho urukiko ruri i nyanza
ubushinjacyaha bwagaragaje ko bazeye yihariye icyaha cyo gukwirakwiza amakuru atariyo bigamije kwangisha leta y u rwanda mu bihugu byamahanga aho nkumuvugizi wa fdlr yavugaga ko ingabo zu rwanda zinjiye muri congo zikica abasivili
ubushinjacyaha bwumvishije urukiko amwe mu majwi ya bazeye ubwe agaragaza imvugo ze zirema icyaha aregwa cyo kwangisha leta yu rwanda mu mahanga
ubushinjacyaha bugaruka ku cyaha cyo kurema umutwe wabagizi ba nabi buvuga ko bazeye na nsekanabo bombi binjiye mu mutwe wa fdlr bazi neza ko ari umutwe urwanya ubutegetsi bwu rwanda ndetse ngo bazeye yawugiyemo umuvandimwe we col nkundiye awumazemo igihe kinini
buvuga ko nkaka ignace wari umuvugizi wa fdlr yari umusivile aza kwinjira mu mitwe yiterabwoba igamije guhungabanya umutekano wu rwanda mu 1997 yinjira mu gicengezi areka kuba umuyobozi wishuri mu karere ka nyabihu aho avuka
uwo mutwe kandi wigambye ibikorwa bitandukanye byagabwe mu rwanda ndetse byishe abaturage batandukanye
nyuma yo kumva impande zombi umucamanza yemeje ko iburanisha risubikwa urubanza rukazakomeza ku wa 03 nzeri 2020 saa mbiri abaregwa bisobanura ku byaha byose baregwa nubushinjacyaha
bazeye na nsekanabo bafashwe mu 2018 bavuye muri uganda mu nama ku gungabanya umutekano wu rwanda hamwe numutwe wa rnc bafatirwa ku mupaka wa bunagana hagati ya uganda na rdc
bazeye na nsekanabo bakomeje kuburanishwa | 2020-07-09T05:22:48 | https://igihe.com/amakuru/u-rwanda/article/ubushinjacyaha-bwagaragaje-uko-bazeye-yakwizaga-amakuru-agamije-kwangisha-u |
mkutano wa g20 kuanza kesho | matukio ya kisiasa | dw | 01042009
mkutano wa g20 kuanza kesho
rais barack obama wa marekani na waziri mkuu gordon brown wa uingereza wameeleza matumaini yao makubwa katika kupatikana makubaliano ya dunia ili kujitoa katika mporomoko wa kiuchumi
rais barack obama na mkewe michelle obama wakipunga mkono wakati walipowasili mjini london tayari kwa mkutano wa kundi la g20
rais barack obama wa marekani na waziri mkuu wa uingereza gordon brown wameeleza matumaini yao makubwa kuhusu kupatikana makubaliano ya dunia ili kujitoa katika mporomoko wa uchumi wakijaribu kupunguza wasi wasi wa kutokea mgawanyiko na rais wa ufaransa nicolas sarkozy kuhusiana na mafanikio ya mkutano wa kundi la mataifa ya g20 unaotarajiwa kuanza kesho
wakati obama anasema kuwa ana hakika kuwa mkutano huo utafikia muafaka sarkozy ameonya kuwa ufaransa na ujerumani hazitakubali ahadi hewa akishauri kuwa makubaliano sio kitu cha kupatikana juu juu tu
marekani inataka mipango ya kichocheo cha uchumi lakini mataifa mengi ya ulaya badala yake yanataka kulenga katika kupatikana kanuni kali za udhibiti wa sekta ya kifedha
mzozo huo ambao obama anadai umekuzwa mno umepunguza matumaini ya kile kinachoweza kufikiwa katika mkutano huo wa london ambao unaanza kwa chakula cha usiku baadaye leo
kansela wa ujerumani angela merkel amesema leo kuwa anaimani kuwa viongozi wa kundi hilo la mataifa ya g20 katika mkutano wao mjini london watachukua hatua na kuongeza kuwa hawaweze kumudu kuficha vichwa vyao mchangani
hata hivyo ameonya kuwa viongozi hao wa dunia hawapaswi kukubali muafaka dhaifu akisema kuwa ana wasi wasi kuwa mataifa muhimu hayajatambua ni kiasi gani hali ya kuporomoka kwa uchumi wa dunia ilivyo
nakwenda mjini london nikiwa na mchanganyiko wa uhakika na wasi wasi merkel amewaambia waandishi habari mjini berlin kabla ya kwenda mjini london
akiulizwa kuhusiana na tishio la rais wa ufaransa nicolas sarkozy la kutoka mkutanoni iwapo matokeo hayatatosheleza matumaini merkel amesema kuwa anaunga mkono nia ya rais sarkozy ya mkutano huo kutokumalizika kwa kupata makubaliano dhaifu
hata hivyo msemaji wake baadaye aliufahamisha mkutano wa kawaida na waandishi habari kuwa kitisho cha kutoka mkutanoni sio wazo zuri
hata hivyo amekataa miito kwa ujerumani kuchukua juhudi zaidi kujiondoa kutoka katika mporomoko wa uchumi akisema kuwa mipango ambayo tayari imekubaliwa inapaswa kupewa muda kuingia katika mfumo wa jamii
lakini ujerumani imejikuta ikishambuliwa na wanachama wengine wa kundi la g20 ambao wanadai kuwa nchi hiyo ambayo ni muuzaji mkuu wa bidhaa nchi za nje haijafanya vya kutosha kuuondoa uchumi wake katika hali ya kuporomoka
mwandishisekione kitojo
mharirim abdulrahman
kiungo https//pdwcom/p/hor7 | 2018-12-18T10:49:22 | https://www.dw.com/sw/mkutano-wa-g20-kuanza-kesho/a-4145513 |
mchezo monster high coloring online kucheza kwa huru
mchezo monster high coloring
unachezwa 3223
kucheza mchezo monster high coloring online
maelezo ya mchezo monster high coloring
je unajua kwamba frankie shtein vipawa sana msanii msichana ina mengi ya vipaji na kuchora mmoja wao katika darasa juu ya kutembea nyumbani na frankie gani kalamu michoro inayoonyesha kurasa za daftari ya wapendwa wao na marafiki hata hivyo msichana hawezi kusimama na rangi picha zao matumizi markers rangi muhtasari frankie kucheza mchezo monster high coloring online
kiufundi na tabia ya mchezo monster high coloring
mchezo monster high coloring aliongeza 07042015
mchezo unachezwa 3223 mara
mchezo rating 343 nje 5 (28 makadirio)
michezo kama mchezo monster high coloring
download mchezo monster high coloring
embed mchezo monster high coloring katika tovuti yako
kuingiza mchezo monster high coloring kwenye tovuti yako nakala ya kanuni na kuweka katika kanuni html ya tovuti yako pia kama wewe kama mchezo monster high coloring nakala na kutuma kiungo kwa rafiki au rafiki yako yote kushiriki mchezo na dunia
pamoja na mchezo monster high coloring pia alicheza katika mchezo | 2018-12-11T21:38:29 | http://sw.itsmygame.org/1000035696/monster-high-coloring_online-game.html |
mama kijacho mbaroni kwa kujipasua tumbo na kisu ili amtoe mtoto tumboni kwake boss ngasa official website
home habarimbalimbali mama kijacho mbaroni kwa kujipasua tumbo na kisu ili amtoe mtoto tumboni kwake
mama kijacho mbaroni kwa kujipasua tumbo na kisu ili amtoe mtoto tumboni kwake
polisi mkoani ruvuma linamshikiria eva kapinga (20) mkazi wa kata ya mateka halmashauri ya manispaa ya songea kwa tuhuma za kumuua mtoto wake catherine kapingamwenye umri wa mwaka mmoja na nusu kisha kujichoma na kisu tumboni kwa lengo la kutaka kujiua na kumsababishia jeraha kubwa na kulazwa
kamanda wa polisi wa mkoa wa ruvuma zuberi mwombeji alisema tukio hilo lilitokea desemba 1 mwaka huu ya saa 130 jioni katika mtaa wa mateka c kata ya mateka tarafa ya songea magharibi
alisema inadaiwa catherine aliuawa na mama yake mzazi eva
alisema sababu za mauaji hayo hazijafahamika licha ya taarifa za awali kudai kuwa eva alikuwa na malumbano kati yake na mama yake mzazi sofia mayunga ambaye alikuwa akimuuliza kwanini ameamua kushika mimba wakati anajua kuwa ana mtoto mdogo wa umri wa mwaka mmoja jambo ambalo lilimkasirisha na kuamua kujichoma kisu tumboni kwa lengo la kujiua
kwa mujibu wa mwombeji eva baada ya kujichoma kisu tumboni inadaiwa watu waliokuwa jirani walimkimbiza kwenye hospitali ya mkoa na taarifa za tukio hilo zilikuwa zimeshafikishwa polisi na kwamba askari walipofika kwenye eneo la tukio wakiwa wameongozana na mganga walikuta catherine ameshafariki dunia na baadaye walikwenda hospitali ya mkoa na kumkuta eva amelezwa akiwa na hali mbaya akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi
hata hivyo kamanda mwombeji alisema wanaendelea na uchunguzi wa kina kuhusiana na tukio hilo na kwamba utakapokamilika mtuhumiwa eva atafikishwa mahakamani
mama kijacho mbaroni kwa kujipasua tumbo na kisu ili amtoe mtoto tumboni kwake reviewed by boss ngasa on tuesday december 06 2016 rating 5 | 2018-10-21T22:01:24 | http://www.bossngasatz.com/2016/12/mama-kijacho-mbaroni-kwa-kujipasua.html |
raha za pwani blog cuf mtwara yamomonyoka
cuf mtwara yamomonyoka
uledi hassan abdallah
aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la mtwara mjini kwa tiketi ya chama cha wananchi (cuf) kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 uledi hassan abdallah amejivua uanachama wa chama hicho | 2017-08-21T10:29:31 | http://saidpowa.blogspot.com/2012/02/cuf-mtwara-yamomonyoka.html |
thenkoromo blog rais mstaafu mkapa aongoza harambee ya kuchangia mfuko wa udhamini wa kudhibiti ukimwi
posted by bashir nkoromo at 2/14/2018
waziri mpina aahidi serikali kutatua kistaarab mgo
japan yaipatia tanzania msaada wa sh bilioni 773
video mnec salim asas atoa msaada wa milioni tan
naibu waziri mavunde aagiza wakurugenzi kupandishw
maeneo ya kitalii yanayopatikana kusini mwa tanzan
magazeti yote leo jumatatu februari 26 2018
rais dk magufuli aungana na waumini wa parokia teu
polisikilimanjaro yanasa raia wa ethiopia 25 waliongia nchini bila kufuata sheria
gharama ukarabati wa barabara ndani ya jimbo kuongezeka zaiditaasisi ya maendeleo jimbo la vunjo (vdf)
mwanafunzi ashambuliwa na kujeruhiwa vibaya na fisi
wanafunzi 4 wa uganda wavumbua mbinu ya aina yake ya kutambua malaria
ziara katibu mkuu wa ccm kisiwani pemba ashiriki matembezi ya vijana
wizara mpya 22 za serikali ya magufuli
mke wa mtu ni sumu afumaniwa na mke wa rafiki yake
dk magufuli rasmi urais aapishwa leo jijini dar es asalaam
jb mzee majuto na richie wamtembelea mama wa mtoto albinism (albino) aliyeuawa wasanii hao wamwaga machozi
msaada wa mbunge uliokataliwa katibu mkuu wizara ya afya azungumzia | 2018-08-21T09:54:32 | http://bashir-nkoromo.blogspot.com/2018/02/rais-mstaafu-mkapa-aongoza-harambee-ya.html |
hali ya mashariki ya kati | matukio ya kisiasa | dw | 15102010
miito ya ujenzi wa makaazi mepya ya walowezi wa kiyahudi katika jerusalem ya mashariki inatishia kuvunja mazungumzo ya amani kati ya israel na palastina
har homamakaazi ya wahamiaji wa kiyahudi katika eneo la mashariki la jerusalem
israel imeanzisha upya ujenzi wa makaazi ya walowezi katika eneo la mashariki la jerusalem bila ya kujali kitisho cha kuvunjika mazungumzo ya amani pamoja na wapalastinajumuia ya nchi za kiarabu imeonya itautaka umoja wa mataifa iitambue dola ya palastina
waziri wa makaazi wa israel ametangaza mipango ya kujengwa nyumba 238 kwaajili ya wayahudi katika mitaa miwili ya jerusalem ya masharikiramot na pisgat zeev
mkuu wa tume ya palastina katika mazungumzo ya amani saeb erakat ameituhumu serikali ya waziri mkuu wa israel benjamin netanyahu kufanya kila liwezekanalo ili kama alivyosema kuuwa fursa yoyote ya kuanza upya mazungumzo na kuitolea mwito marekani iingilie kati kuupatia ufumbuzi mzozo wa ujenzi wa makaazi ya wayahudi katika ukingo wa magharibi
hii ni miito ya mwanzo ya ujenzi tangu september 26 iliyopiotayalipomalizika marufuku ya miezi 10 ya ujenzi wa makaazi ya wahamiaji wa kiyahudi katika ardhi za wapalastina katika ukingo wa magharibi
ingawa marufuku hayo hayakulihusu eneo la mashariki la jerusalem lililotekwa na kukaliwa na israel tangu june mwaka 1967hata hivyo serikali ya israel ilijiepusha miezi iliyopita kutoa miito ya ujenzi katika mitaa ya wahamiaji wa kiyahudi katika mji huo
tunalaani moja kwa moja uamuzi huu na tunautaka utawala wa marekani uitwike serikali ya israel jukumu la kuvunjika mazungumzo na utaratibu wa amani kutokana na ushupavu wake kutaka kuuwa kila nafasi ya kuanza upya mazungumzo amesema saeb erakat
tangazo hilo ni la kisiasa na limetolewa makusudi kwa lengo la kuvuruga mazungumzo ya amani pamoja na wapalastina amesema hayo hagit ofranmwanaharakati wa vuguvugu linalopinga ujenzi wa makaazi mepyalijiitalo amani sasa
kwa mujibu wa gazeti la israel yediot aharonotserikali ya israel imetoa tangazo hilo la ujenzi wa makaazi mepya baada ya kuiarifu serikali ya marekani
pindi suala la ujenzi wa makaazi ya wayahudi likiseleleajumuia ya nchi za kiarabu inaweza kufikiria uwezekano wa kuutaka umoja wa mataifa uitambue dola ya palastina na kuikubalia uanachama kamiliamesema hayo waziri wa mambo ya nchi za nje wa misri ahmed abu gheith mjini brusselsanasema amelizusha suala hilo jana usiku wakati wa mazungumzo pamoja na mawaziri wenzake wa ujerumaniufaransauengerezahispania na italy
hali ya kukwama mazungumzo ya ana kwa ana ya amani kati ya israel na palastina inatishia pia kukorofisha mkutano unaotaka kuitishwa na rais nicolas sarkozy wa ufaransa wiki ijayo kati ya waziri mkuu wa israel benjamin netanyahukiongozi wa utawala wa ndani wa palastina mahmoud abbas na rais wa misri hosni mubarak mjini paris
mpitiajimabdulrahman
kiungo https//pdwcom/p/pfdl | 2018-07-21T08:24:50 | https://www.dw.com/sw/hali-ya-mashariki-ya-kati/a-6116631 |
music shukurani zangu neema lyimo wa mng'ong'o tim heaven
browse | home | music
| music shukurani zangu neema lyimo wa mng'ong'o
music shukurani zangu neema lyimo wa mng'ong'o
chief hope | 102900 am | music
naitwa neema lyimo wa mng'ong'o hapo mwanzo nilijulikana kama neema lyimo lakini sasa nimeolewa na mr p mng'ong'o ndiyo maana jina limebadilika kidogo na kuitwa neema lyimo wa mng'ong'o
mara ya mwisho nilifahamika kwa wimbo wa tuvuke ng'ambo na baada ya apo nikawa kimya kwa muda mrefu sana kwa sababu niliingia kwenye ndoa nikalazimika kuacha majukumu ya uimbaji na kuwa na familia yangu kwanza katika kipindi hicho nikalea ujauzito kwa miezi tisa na kisha tukajaaliwa mtoto mzuri sana wa kiume anaitwa ethan paul mng'ong'o kwa kipindi kirefu kisichopungua miezi sita nilikaa na mtoto tu na baada ha hapo ndipo nilipopata kibali na kurejea kwenye huduma
ninamshukuru mungu kwa kunipa mume ambaye anaipenda sana huduma yangu na kwa kweli ananisupport katika kila hatua yeye ameniwezesha kufanya album nyingine ambayo itatoka hivi karibuni na sasa nimeanza mipango ya kurecord video baada ya kukamilisha hayo yote ndo nitarelease hiyo album yangu mpya sasa hivi media zimeanza kupiga nyimbo zangu hasahasa unaopigwa sana ni wimbo unaoitwa shukurani zangu
mungu akubariki sana ninachokuomba mtu wa mungu ni kitu kimoja uniombee ili mungu aendele kunisaidia niwe na uadilifu na tabia njema (integrity and good character) ili kabla sijahudumu nimpendeze mungu familia yangu na wanadamu n mungu anitumie katika kuujenga ufalme wake
mwisho kama unahuduma ya mungu popote pale mkutano wa injili semina ibada nk tushirikiane wala usiogope kunialika ili tujenge pamoja ufalme wa kristo mambo ya fedha na gharama usiyafikilie kwanza mungu alinipa kazi na huduma hii bure kabisa jambo la kwanza tumtumikie mungu kwa urahisi ili kuujenga ufalme wa mungu mengine mungu atatupatia kwa wingi na kwa jinsi anayoijua yeye
click hapa kutembelea na kulike ukurasa wa facebook wa neema lyimo wa mng'ong'o
mawasiliano zaidi
namba +255 753 777 057
email neemamngongo01@gmailcom
facebook naitwa neema lyimo wa mng'ong'o | 2016-12-09T05:42:24 | http://www.timheaven.com/2015/02/shukuranizangu.html |
maono ya kazi ya mungu (1) | kanisa la mwenyezi mungu
yohana alimfanyia yesu kazi kwa miaka saba na tayari alikuwa ameandaa njia yesu alipofika kabla ya haya injili ya ufalme wa mbinguni iliyohubiriwa na yohana ilisikika kotekote katika nchi hivyo ilienea kutoka upande mmoja hadi upande mwingine wa uyahudi na kila mtu alimwita nabii wakati huo mfalme herode alitamani kumuua yohana lakini hakuthubutu kwani watu walimheshimu sana yohana na herode aliogopa kwamba kama angemuua yohana wangemuasi kazi iliyofanywa na yohana ilikita mizizi miongoni mwa watu wa kawaida na aliwafanya wayahudi kuwa waumini kwa miaka saba alimwandalia yesu njia mpaka wakati ambapo yesu alianza kutekeleza huduma yake na kwa hiyo yohana alikuwa mkuu zaidi kwa manabii wote yesu alianza tu kazi yake rasmi baada ya yohana kufungwa jela kabla ya yohana hakukuwahi kuwa na nabii aliyemwandalia mungu njia kwa sababu kabla ya yesu mungu hakuwa amewahi kupata mwili na kwa hiyo kwa manabii wote mpaka yohana yeye pekee ndiye angemwandalia mungu mwenye mwili njia na kwa jinsi hii yohana akawa nabii mkuu zaidi wa agano la kale na jipya yohana alianza kueneza injili ya ufalme wa mbinguni miaka saba kabla ya ubatizo wa yesu kwa watu kazi aliyoifanya ilionekana kuwa juu zaidi ya kazi ya baadaye ya yesu ilhali yeye alikuwa hata hivyo nabii tu hakufanya kazi au kuzungumza ndani ya hekalu lakini katika miji na vijiji nje yake hii alifanya bila shaka miongoni mwa taifa la wayahudi hasa wale waliokuwa maskini ni mara chache ambapo yohana alitangamana na watu kutoka ngazi za juu za jamii na alieneza injili miongoni mwa watu wa kawaida wa yudea tu ili kuandaa watu wema kwa bwana yesu na kuandaa maeneo yafaayo kwake kufanya kazi kwa sababu ya kuwa na nabii kama yohana wa kuandaa njia bwana yesu alikuwa na uwezo wa kuanzisha njia yake ya msalaba mara moja punde tu alipowasili wakati mungu alipogeuka kuwa mwili ili kufanya kazi yake hakuwa na jukumu la kufanya kazi ya kuwachagua watu na hakuwa na haja ya kuwatafuta watu binafsi au mahali ambapo angefanyia kazi hakufanya kazi kama hii alipokuja mtu afaaye alikuwa tayari amemwandalia kabla yeye hajawasili yohana alikuwa tayari amemaliza kazi yake kabla yesu kuanza kazi yake kwani wakati ambapo mungu mwenye mwili aliwasili kufanya kazi yake alianza kufanya kazi moja kwa moja kwa wale ambao walikuwa wakimngoja kwa muda mrefu yesu hakuwa amekuja kufanya kazi ya mwanadamu au kazi ya urekebishaji iliyomwangukia mwanadamu alikuwa amekuja tu kutekeleza huduma ambayo ilikuwa yake kutekeleza na mengine yote hayakuwa na uhusiano naye yohana alipokuja hakufanya lolote ila kutoa hekaluni na miongoni mwa wayahudi kundi la wale waliokubali injili ya ufalme wa mbinguni ili waweze kuwa vyombo vya kazi ya bwana yesu yohana alifanya kazi kwa miaka saba ambapo ni kusema kwamba alieneza injili kwa miaka saba wakati wa kazi yake yohana hakufanya miujiza mingi kwa sababu kazi yake ilikua kuandaa njia ilikuwa kazi ya maandalizi kazi zote zingine kazi ambazo yesu alikuwa afanye hazikuwa na uhusiano naye alimwomba mwanadamu tu aungame dhambi zake na atubu na aliwabatiza watu ili waweze kuokolewa ingawa alifanya kazi mpya na kufungua njia ambayo kamwe mwanadamu alikuwa bado hajaitembea bado alimwandalia yesu njia alikuwa nabii tu ambaye alifanya kazi ya maandalizi na hakuwa na uwezo wa kufanya kazi ya yesu ingawa yesu hakuwa wa kwanza kuhubiri kuhusu ufalme wa mbinguni na japokuwa aliendelea na njia ambayo yohana alianzisha bado hakukuwa na mwingine ambaye angeweza kufanya kazi yake na ilikuwa juu zaidi ya kazi ya yohana yesu hangeandaa njia yake mwenyewe kazi yake ilitekelezwa moja kwa moja kwa niaba ya mungu na hivyo bila kujali ni miaka mingapi yohana alifanya kazi bado alikuwa nabii na bado yule aliyeandaa njia miaka mitatu ya kazi iliyofanywa na yesu ilizidi miaka saba ya kazi aliyofanya yohana kwa kuwa kiini cha kazi yake hakikuwa cha kiwango sawa yesu alipoanza kutekeleza huduma yake ambao pia ni wakati kazi ya yohana ilifika mwisho yohana alikuwa amewatayarisha watu wa kutosha na mahali pa kutumiwa na bwana yesu na walitosha kwa ajili ya bwana yesu kuanza miaka mitatu ya kazi na kwa hiyo punde tu kazi ya yohana ilipomalizika bwana yesu alianza rasmi kazi yake mwenyewe na maneno yaliyonenwa na yohana yakarushwa kando hiyo ni kwa sababu kazi iliyofanywa na yohana ilikuwa tu kwa ajili ya mabadiliko na maneno yake hayakuwa maneno ya uzima ambayo yangemwelekeza mwanadamu kwa ukuaji mpya mwishowe maneno yake yalikuwa tu ya matumizi ya muda
kazi ambayo yesu alifanya haikuwa ya mwujiza kulikuwa na mchakato kwayo na yote iliendelea mbele kufuatana na sheria za kawaida za vitu kufikia miezi sita ya mwisho ya maisha yake yesu alijua kwa uhakika kwamba alikuwa amekuja kuifanya kazi hii na alijua kwamba alikuwa amekuja kupigiliwa misumari msalabani kabla ya yeye kusulubiwa yesu alimwomba mungu baba siku zote kama tu alivyoomba mara tatu katika bustani la gethsemane baada ya kubatizwa yesu alitekeleza huduma yake kwa miaka mitatu na nusu na kazi yake rasmi ilidumu kwa miaka miwili na nusu katika mwaka wa kwanza alishtakiwa na shetani na akasumbuliwa na mwanadamu na akapitia majaribu ya mwanadamu alishinda majaribu mengi wakati huo huo alipotekeleza kazi yake katika miezi sita ya mwisho wakati ambapo yesu alikaribia kusulubiwa kutoka kinywani mwa petro yalitoka maneno haya kwamba alikuwa mwana wa mungu aishiye kwamba alikuwa kristo ni wakati huo tu ndipo kazi yake ilijulikana kwa wote na ni wakati huo tu ndipo utambulisho wake ulifichuliwa kwa watu wote baada ya hilo yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba angepaswa kusulubiwa kwa ajili ya mwanadamu na kwamba siku tatu baadaye angefufuka tena kwamba alikuwa amekuja kutekeleza kazi ya ukombozi na yeye alikuwa mwokozi ni katika miezi sita ya mwisho tu ndiyo alifichua utambulisho wake na kazi aliyokusudia kufanya huu pia ulikuwa wakati wa mungu na kazi ilipaswa kutekelezwa hivyo wakati huo sehemu ya kazi ya yesu ilikuwa kwa mujibu wa agano la kale pia na sheria za musa na maneno ya bwana wakati wa kipindi cha enzi ya sheria yote hayo yesu alitumia kufanya sehemu ya kazi yake alihubiri kwa watu na kuwafundisha kwenye masinagogi na yeye alitumia utabiri wa manabii katika agano la kale kuwakemea mafarisayo waliokuwa na uhasama naye na alitumia maneno katika maandiko kufichua uasi wao na hivyo kuwahukumu kwa maana wao walidharau mambo ambayo yesu aliyafanya hasa nyingi ya kazi ya yesu haikufuatana na sheria katika maandiko na zaidi ya hayo kile alichofundisha kilikuwa kikuu kuliko maneno yao wenyewe na hata kikubwa kuliko kile ambacho kilikuwa kimetabiriwa na manabii katika maandiko kazi ya yesu ilikuwa kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu na kusulubiwa tu kwa hivyo hakukuwa na haja kwake kusema maneno zaidi ili kumshinda mtu yeyote mengi ya yale aliyomfundisha mwanadamu yalitolewa kutoka kwa maandiko na hata kama kazi yake haikuzidi maandiko bado aliweza kutimiza kazi ya kusulubiwa yake haikuwa kazi ya neno wala kwa ajili ya kumshinda mwanadamu lakini kwa minajili ya kumkomboa mwanadamu yeye alihusika kama dhabihu ya dhambi tu kwa mwanadamu na hakuhusika kama chanzo cha neno kwa mwanadamu hakufanya kazi ya watu wa mataifa mengine ambayo ilikuwa kazi ya kumshinda mwanadamu bali alifanya kazi ya kusulubiwa kazi ambayo ilifanywa miongoni mwa wale ambao waliamini kulikuwa na mungu japokuwa kazi yake ilifanywa juu ya msingi wa maandiko na alitumia yale yaliyotabiriwa na manabii wa kale kuwahukumu mafarisayo hii ilikuwa ya kutosha kukamilisha kazi ya kusulubiwa kama kazi ya leo ingekuwa bado inafanyika juu ya misingi ya utabiri wa manabii wa kale katika maandiko basi haingewezekana nyinyi kushindwa kwa kuwa agano la kale halina kumbukumbu ya uasi na dhambi zenu nyinyi watu wa china hakuna historia ya dhambi zenu kwa hivyo kama kazi hii bado ingedumu katika biblia hamngeweza kutoa matunda biblia inaandika lakini kwa uchache historia ya wana wa israeli ambayo haina uwezo wa kusadikisha iwapo nyinyi ni waovu ama wema ama ya kukuhukumu hebu fikiria kama ningekuwa wa kuwahukumu nyinyi kadri ya historia ya wana wa israelibado mngenifuata mimi kama mnavyonifuata hivi leo je mnajua jinsi ambavyo nyinyi m wagumu kama hakuna maneno ambayo yalisemwa wakati wa awamu hii basi itakuwa vigumu kukamilisha kazi ya ushindi kwa sababu mimi sijakuja kugongomewa msumari msalabani sharti mimi niseme maneno ambayo ni tofauti na yatokayo kwa biblia ilimradi muweze kushindwa kazi iliyofanywa na yesu ilikuwa tu hatua moja juu zaidi ya agano la kale ilitumiwa kuianza enzi na kuiongoza enzi hiyo kwa nini alisema sikuja kuharibu sheria bali kuitimiza lakini katika kazi yake kulikuwa na mengi ambayo yalitofautiana na sheria zilizotumika na amri zilizofuatwa na waisraeli wa agano la kale kwani hakuja kuitii sheria bali kuitimiza mchakato wa kuitimiza ulikuwa pamoja na mambo mengi halisi kazi yake ilikuwa ya vitendo zaidi na halisi na zaidi ya hayo ilikuwa hai na sio tu kufuata mafundisho ya dini bila ufahamu je waisraeli hawakuitii sabato yesu alipokuja hakuitii sabato kwani alisema kwamba mwana wa adamu alikuwa bwana wa sabato na wakati ambapo bwana wa sabato alikuja angefanya alivyopenda alikuwa amekuja kutimiza sheria za agano la kale na kuzibadilisha sheria yote ambayo hufanywa leo ni kwa msingi wa siku hizi lakini bado yako juu ya msingi wa kazi ya bwana katika enzi ya sheria na hayavuki mipaka ya eneo hili kuulinda ndimi zenu na kutozini kwa mfanoje hizi si sheria za agano la kale leo kile kinachotakikana kwenu sio chenye upeo wa amri kumi tu lakini ni kuwa na amri na sheria ambazo zina ukuu kuliko hizo zilizokuja hapo awali ila hii haina maana kuwa kile kilichokuja hapo awali kimeondolewa kwa kuwa kila awamu ya kazi ya mungu hufanywa juu ya msingi wa awamu ambayo ilikuja hapo awali na kuhusu kile ambacho yehova aliwasilisha kwa israeli kama vile kuwahitaji watu kutoa sadaka kuwaheshimu wazazi wao kutoabudu sanamu kutowadhulumu au kutukana wengine kutozini kutovuta sigara au kutokunywa pombe na kutokula nyamafu au kunywa damu je huo si muundo msingi wa utendaji wenu hata leo kazi iliyotekelezwa hadi leo iko juu ya msingi wa mambo ya zamani ingawa sheria za zamani hazitajwi tena nawe umewekewa madai mapya sheria hizi mbali na kufutwa badala yake zimeinuliwa katika hadhi ya juu zaidi kusema kwamba zimefutwa kuna maana kwamba enzi ya awali imepitwa na wakati wakati kuna amri zingine ambazo lazima uzitii milele yote amri za zamani tayari zimetiwa katika vitendo tayari zimekuwa nafsi ya mwanadamu na hakuna haja ya kurudia kusema amri za kutovuta sigara kutokunywa pombe na kadhalika juu ya msingi huu amri mpya zimeagizwa kufuatana na mahitaji yenu leo kufuatana na kimo chenu na kufuatana na kazi ya leo kutangaza amri kwa ajili ya enzi mpya hakumaanishi kufuta amri za enzi ya kale bali kuziinua juu zaidi ya msingi huu kuyafanya matendo ya mwanadamu kuwa kamili zaidi na kufuatana na uhalisi zaidi kama leo mngetakiwa tu kufuata amri na kutii sheria za agano la kale kwa namna sawa na wana wa israeli na kama hata nyinyi mlitakiwa mkariri sheria ambazo ziliwekwa na bwana hakungekuwa na uwezekano kwamba mngeweza kubadilika kama mngekuwa tu mnatakiwa kutii zile amri chache zilizo na mipaka ama kukariri sheria zisizohesabika asili zenu za zamani zingebaki zimekita mizizi na hakungekuwa na mbinu ya kuzingoa hivyo mngeendelea kuzidi kupotoshwa na hakuna hata mmoja wenu angeweza kuwa mtiifu ambayo ni kusema kwamba amri chache rahisi au sheria zisizohesabika hazina uwezo wa kuwasaidia kujua matendo ya yehova nyinyi si sawa na wana wa israeli kwa kufuata sheria na kukariri amri waliweza kushuhudia matendo ya yehova na kumpa yeye pekee ibada yao lakini hamwezi kufanikisha hili na amri chache za agano la kale haziwezi tu kuwafanya nyinyi kupeana mioyo yenu au kuwalinda lakini badala yake itawafanya muwe wazembe na kuwateremsha mpaka kuzimu kwa sababu kazi yangu ni kazi ya ushindi na inalenga uasi wenu na asili yenu ya zamani maneno yenye huruma ya yehova na yesu yanapungukiwa mno na maneno makali ya hukumu leo bila maneno makali kama haya ingekuwa vigumu kuwashinda ninyi wataalam ambao mmekua wasiotii kwa miaka elfu nyingi sheria za agano la kale zilipoteza nguvu zake kwenu kwa muda mrefu uliopita na hukumu ya leo ni ya kuogofya mno kuliko sheria za zamani ya kuwafaa nyinyi zaidi ni hukumu na wala si vikwazo duni vya sheria kwa kuwa ninyi si wanadamu wa mwanzo kabisa lakini wanadamu ambao wamekuwa fisadi kwa miaka elfu nyingi kile ambacho mwanadamu lazima atimize sasa ni kulingana na hali halisi ya mwanadamu leo kulingana na tabia bora na kimo halisi cha mwanadamu wa siku hizi na hakihitaji kwamba wewe ufuate mafundisho ya dini hii ni kwa minajili ya mabadiliko yaweze kupatikana katika asili zako za zamani na ili uweze kutupa kando dhana zako je unadhani sheria hizi ni mafundisho ya dini hizo ni inaweza kusemwa masharti ya kawaida kwa mwanadamu hayo si mafundisho ya dini unayotakiwa kufuata chukua mfano wa kukataza kuvuta sigaraje hayo ni mafundisho ya dini hayo si mafundisho ya dini yanahitajika na ubinadamu wa kawaida si mafundisho ya dini bali ni sheria kwa wanadamu wote leo idadi kubwa au zaidi ya amri ambazo zimetangazwa si mafundisho ya dini bali kinachohitajika ili kutimiza ubinadamu wa kawaida watu hawakuwa na au kujua vitu kama hivyo zamani na kwa hiyo wanatakiwa kuvitimiza leo ambavyo havihesabiki kama mafundisho ya dini sheria si sawa na mafundisho ya dini mafundisho ya dini ninayozungumzia yanahusu sherehe urasmi au desturi za mwanadamu za kuacha maadili na zenye kosa ni masharti na kanuni ambazo hazimsaidii mwanadamu hazina manufaa kwake na ni kusudi la kitendo lisilo na umuhimu hiki ni kifano cha mafundisho ya dini na mafundisho ya dini kama hayo lazima yaachwe kwani hayampi mwanadamu manufaa yoyote ni yale yaliyo ya manufaa kwa mwanadamu ndiyo yanatakiwa kutiwa katika vitendo
iliyotangulia:kazi na kuingia (10)
inayofuata:maono ya kazi ya mungu (2) | 2019-06-17T12:58:00 | https://sw.godfootsteps.org/the-vision-of-gods-work-1.html |
mahusiano ah jamiiforums
mahusiano ah
thread starter mwanajamiione
10476 87 145
natumaini wote wazima
jamani huu umbeya wa kina geah una mambo eti kuna mwanamke analalamika kuchukuliwa mumewe na mwanamke mwingine ambaye amemteka kupitiliza hadi anasahau familia yake huku akimpa kashfa kibao mkewe nashangaa hivi hata kama ndo mnatuibia hamweziiba kisiri jamani bila kutushika mikono
si bure ndo mana kina mama nao siku hizi wanaapply mama big's principle kuwa yeye anadumishia hapa wapo wanaodumishia kuleee
hivi kina mama nasi huwa tunatekwaga kihivi au wenzetu mko more delicate inside kuliko sie
si unajua ule msemo wa juzi mwenzako akila huku wewe kula kule
aaaaaaaah hiyo ni gia ya wanaume kumega kwa raha zake kama anamponda mke wake kwa nini akimaliza shuhuri iliyo mleta anakumbuka kuna kurudi tena nyumbani kwa nyumba kubwa kwa nn asikae hapo hapo
ehh eti nyie wanaume kwann msihamie huko huko kikaeleweka umemchoka mkeo
hapo chacha maana huyu kamwambia mkewe baada ya kumfuma kwa bi mdogo anamwuliza kimekuleta nini huku kwani nyumbani huna chakula
ammah we umenioa mie nije kula chakula kwani kwetu nlikuwa sili hadi nkakubali unioe ah mnatutenza jamani ila nasikia kuna wanawake pia ambao wananogewaga na nyumba ndogo zao kiasi cha kuwasahau na kuwadharau waume zao
6969 29 0
mie mwanamke mwenzangu acjeshawishika kunifanyia hiko kitendo dharau kubwa sana nitaanza nae then nitamalizana na mhucka kama anakula ale kwa abadu zake za kumtosha
ati usije kuta naye kanusishwa
tatizo wengine (kama huyu alozungumziwa hapa) ana miaka sita na bi mdogo kamnunulia hadi gari na kuitelekeza familia yake kimatumizi anaondoka asubuhi anarudi alfajiri sasa sijui imetokana na uvivu wa mwanajamiione hapa maana naona ka vile mama big kiboko yao ndo kamkamata lolkaambiwa vuvuzela laumiza ngoma za masikio so mama big anaziba taratibndo kanogewa
ndoa hizi zimekuwa ndoa ki kwelihivi jamani nashindwa hata la kusema huyu mwaname ana utu kwelimbona tunatafutiana dhambi za milele
mbona ulipotea au na wewe ulikuwa katika harakati za kulinda kura kama mimi
soma signature yangu mla huliwa mji hayo yote maneno ya kupata vitamu binadamu tuna mambo we acha ukitaka kupata kitu utasema chochote ilimradi ufaidi anamponda ili aonekane ana mapenzi makubwa huko kwa bi mdogo hamna lolote wakati akifika kwa bi mkubwa na magoti anapiga haya mambo huwa yana muda wakishazoeana anaaanza kumuona kama bi mkubwa si unajua mambo ya kipya kinyemi kwenye maisha haya mtu akishajua mpaka ushuzi wako unanukaje anaanza kukudharau na kusahau mazuri yako
mambo mengine sio ya kucheka lakini inabidi tu mie cku hizi namhurumia kweli mtu naeshadadia kuingia kwenye ndoa lakini wacha waingie wajionee wenyewe
hapo sasa yaani ni ngumu kuelewa sijui ndo mambo ya matters of the hearts yaani nyamayao shemeji anakula na da sophy afu ukimwuliza prezidaa mbona siku hizi mambo sivyo aanze tu kukujibu mbofu mbofu na kukuuliza kwani una shida gani huli chakula watoto hawendi ****** aah
finest wacha tu nilikuwa nikiingia humu nakutana na vurumai za uchaguzi zinaniongezea tu stress wakati mie nina zangu za kunitosha
hahahaha hakuna lolote si kunukishwa wala kulambishwakajichetua mwenyewe tu
6776 256 180
hapa nyamayao na mj1mi nasoma kati ya mistari na chini ya mistari
btw hapo pekundu nimetoka hola
kuna sehemu lazima something is wrong
mhh kwa kweli hapana tunauwana taratibu aise mara unashangaa unapata pressure mara cjui kisukari mara cjui kitu gani kwa kumfikiria mwanaume wa hivi mj1 wacha tu maisha haya bac tu mtu kama ameamua kufanya bac na afanye lakini akupe heshima yako jamani kwanini maisha yapo hivi sasa huyo mwanamama kaamua vipi kwamba atakomaa na ndoa au kaamuajemambo mengine ni kuharibu kabisa kila mtu ashike ustaarabu wake
nyamayao bana
utaanza nae kivipi
unajua wanaume wengi wanapokuwa na small house(s) huwa wanajaribu kila ufundi unaowezekana hata kuwakandya wakazao etc ili mradi tu small house naye in return aonyeshe maufundi yake yote
small house zilizostaharabika haiwezi kamwe kutaka kuharibu ndoa ya mwenye nayo kwa sababu as soon as mambo yanaharibika nyumbani then kwa staili ile ile small house inapigwa chini
55148 33484 280
sijui nichangie sijui umri wangu hauniruhusu | 2018-09-24T15:58:45 | https://www.jamiiforums.com/threads/mahusiano-ah.85997/ |
dc kasesela majangiri hawana nafasi kufanya uharifu kwenye mbuga za wilaya ya iringa msumba news blog
dc kasesela majangiri hawana nafasi kufanya uharifu kwenye mbuga za wilaya ya iringa
mkuu wa wilaya ya iringa ambaye ni mwenyekiti wa baraza la maliaasili na misitu richard kasesela wamejipanga kuwadhibiti majangili wote na akiwa ameshika silaha bora ambazo wanazitumia walinzi wa hifadhi village game scouts ambao wanafadhiliwa na shirika la steps
mkuu wa wilaya ya iringa ambaye ni mwenyekiti wa baraza la maliaasili na misitu richard kasesela akiwa pamoja na katibu tawala wa wilaya ya iringa hashimu komba wakiwa kwenye picha moja na viongozi na walinzi wa hifadhi village game scouts
akizungumza wakati alipofanya ziara ya ghafla ya kuwatembelea na kuwapa moyo walinzi wa hifadhi village game scouts ambao wanafadhiliwa na shirika la steps kwa kazi kubwa wanayofanya ya kulinda maliasili zilizopo katika wilaya hiyo
mimi niwapongeze sana maana mnafanyakazi kubwa sana kupambana na majangili huko porini jambo ambalo mnapaswa kupongezwa kwa namna yoyote ile alisema kasesela
kasesela alisema kuwa hifadhi hizo zimekuwa zikivamiwa na majangili hasa pembezoni mwa hifadhi hizo kutokana na kuwa jirani na wakazi ambao wamekuwa wakifanya uharifu huo kutokana na tamaa zao
kasesela aliwaonya majangili kwamba sasa wasirogwe kuingia kwenye mbuga za wanyama kutaka kufanya ujangili wa aina yoyote kwakuwa wanamifumo ya kisasa zikiwemo kamera zimefungwa kwenye maeneo ya mbuga hizo
yoyote atakaye kamatwa kwa ujangili atafikishwa kwenye vyombo husika na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa atakuwa amefanya uharifu ambao haukubariki kisheria alisema kasesela
aidha kasesela alilipongeza shirika la steps kwa kuwafadhili walinzi wa hifadhi village game scouts kwa kuwapa vifaa vya kisasa kwa ajili ya kazi hiyo ya ulinzi kwenye mbuga zilizopo katika wilaya ya iringa | 2019-09-19T02:37:57 | http://www.msumbanews.co.tz/2019/07/dc-kasesela-majangiri-hawana-nafasi.html |
hazina ya maswali >عصمت >شرایط و صفات امام >the recognition of imams >elimu ya akida hazina ya maswali islamquest
nyumbani hazina ya maswali elimu ya akida the recognition of imams شرایط و صفات امام عصمت
maneno yote kama ibara ilivyo kila neno(maneno yaliyo ainishwa tu) kila neno(pamoja na minyambuko yake) hali kwa sasa timuعصمت ► maudhui zote qurani پیامبران hadithi elimu ya akida falsafa tabia irfani fiqhi tarehe nyendendo judgments مبانی شیعه اندیشه های امام خمینی (ره) مفاهیم قرآنی ولایت فقیه و حکومت اسلامی عرفان و اخلاق logic and philosophy know more arabic grammar kipindi chote msaa 24 yaliopiti wiki moja iliyopita wiki mbili zilizopita wiki tatu zilizopita mwezi mmoja uliopita miezi miwili iliyopita miezi sita iliyopita
2736 اشتراک در دین 2015/06/02
8954 روزه های مستحب، مکروه و حرام 2012/05/23
15872 نگهداری و شکار حیوانات 2012/06/17
2849 پوشش 2015/04/18
5866 گوناگون 2012/05/23
7505 هدایت الاهی 2012/05/23
4061 حوادث روز عاشورا 2012/05/23
6992 قضای روزه و کفارات 2012/05/23
5539 گوناگون 2012/05/23 | 2020-01-18T10:26:41 | http://www.islamquest.ir/sw/archive/category/1496 |
mwigulu nchemba alivyozindua kwa kishindo kampeni za ccm kalenga ~ uvccm blog thumbnails===nvarscontrolnav&&0===nvarsthumbcaptions){var c=sattr(datathumbcaption)==c&&void 0==c&&(a+=''+c+)}ncontrolnavscaffoldappend(
home » » mwigulu nchemba alivyozindua kwa kishindo kampeni za ccm kalenga
katibu wa ccm wilaya ya mufindi miraji mtaturu alionyesha mbao zenye misumari inayodaiwa kutegwa njiani na chadema kwa nia ya kudhuru msafara wa mgombea wa ccm katika jimbo la kalenga | 2017-08-20T07:55:11 | https://uvccmtz.blogspot.com/2014/02/mwigulu-nchemba-alivyozindua-kwa.html |
Subsets and Splits