text
stringlengths 43
182k
| timestamp
timestamp[s] | url
stringlengths 16
3.37k
|
---|---|---|
matondo hii imekaa vizuri polisi akataa rushwa ya dola 3000 atuzwa tsh 4000000
hii imekaa vizuri polisi akataa rushwa ya dola 3000 atuzwa tsh 4000000
hongera pc john anthony mwesongo wewe ni mfano wa kuigwa picha na maelezo ni kutoka kwa mzee wa mshitu
labels matukio mikasa
mzee wa changamoto march 17 2010 at 1216 am
ninalowaomba hawa wahusika wa jeshi wamuhamishe kisha wasiseme anahamia wapi maana kama ulivyoandika kuwa waliotaka kumpa pesa ni wauza madawa ambao wana mtandao (network)
namtakia maisha ya salama na yenye utii | 2017-11-24T13:16:46 | http://matondo.blogspot.com/2010/03/hii-imekaa-vizuri-polisi-akataa-rushwa_17.html |
yanga wamebalance mzani | shaffihdauda
home kitaifa yanga wamebalance mzani
ushindi wa yanga 31 dhidi ya stand united umeipa yanga pointi tatu ambazo zinaifanya ifikishe pointi 46 na kuifikia simba licha kwamba wekundu wa msimbazi wanaendelea kuongoza ligi kwa tofauti ya magoli
yanga imecheza mechi 21 mchezo mmoja zaidi ya simba ambayo imecheza mechi 20 hadi sasa
kwa muda mrefu simba iliongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba lakini yanga wametoka nyuma na kuziba gap hilo la pointi zote baada ya mechi 13 simba ilikuwa inaongoza ligi kwa pointi 29 huku yanga ikiwa nafasi ya tano ikiwa na pointi 22
februari 4 2018 yanga ilikuwa nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31 wakati huo sumba ilikuwa inaongoza ligi kwa pointi zake 38 huku kila timu ikiwa imecheza mechi 16
magoli ya yanga yamefungwa na ally ally (alijifunga) dakika ya saba ibrahim ajibu akafunga goli la pili dakika tano baadaye obrey chirwa ameifungia yanga bao lililokamilisha ushindi wa yanga goli pekee la stand united limefungwa na mayanga dakika ya 83
ushindi wa yanga leo ni wa nane mfululizo katika michezo nane iliyopita kwenye ligi baada ya kutoka suluhu (00) dhidi ya mwadui kwenye uwanja wa uhuru ilianza kushinda mchezo dhidi ya ruvu shooting januari 21 2018 hadi leo
previous articlepointi 23 kati ya 30 ugenini pointi 21 mfululizo lwandamina ni tishio
next articlevideo magoli yote yanga vs stand united machi 12 2018
kitaifa7695 | 2018-04-24T06:28:29 | http://shaffihdauda.co.tz/2018/03/12/yanga-wame-balance-mzani/ |
dubai metro ya ardhi baada ya 2017 | rayhaber | raillynews
nyumbaniworldasia971 falme za kiarabudubai metro itapita baada ya 2017
30 / 03 / 2012 971 falme za kiarabu railway general headline metro
inaripotiwa kwamba dubai metro inayojulikana kama dereva wa dunia mrefu zaidi bila dereva itafunika 2017 wakati mfumo wa basi wa mji utafikia gharama ya 2016 kwa kuongeza idadi ya abiria kutumia mfumo wa usafiri wa umma imeonekana ongezeko kubwa sana na mfumo huu wa usafiri umesababisha akiba ya dola milioni 411
mkuu wa road na usafiri authority mattar al tayi metro unatarajiwa kupita nchi uokoaji wa gharama ndani ya miaka mitano na kuongezeka kwa idadi ya abiria pamoja na mapato kutokana na utaratibu wa majina ya kituo na matangazo mengine kwa kukodisha maduka ya rejareja alisema ilikuwa ni iwezekanavyo
akizungumza katika mkutano wa reli rasmi katika london mfumo subway ni upya baadhi ya maeneo ya mkataba na kusema kuwa njia bora ya akiba kubwa alifanya kutokana na matumizi
vile vile alisisitiza kuwa baadhi ya njia za mabasi ya jiji zimebadilishwa na kwamba baadhi yao yameunganishwa na hivyo kupunguza gharama za mafuta
el tayir alisema kuwa shida kubwa waliyo nayo wakati walianza kazi ilikuwa msongamano wa trafiki katika mji na walichukua hatua muhimu za kutatua kulingana na utafiti gharama ya kila mwaka ya migogoro ya trafiki huko dubai kabla ya mgogoro wa kimataifa ilikuwa zaidi ya $ 1 milioni katika 350
idadi ya watu wanaotumia usafiri wa umma huko dubai kituo cha kibiashara cha falme za kiarabu (uae) ni 2005 milioni katika 91 ambayo ni 2011 katika 190 hivyo sehemu ya usafiri wa umma kwa usafiri wa jumla imekuwa 2006 katika 6 wakati katika 2011 imefikia 10
katika uae na majimbo mengine ya ghuba ambapo petroli ni kuhusu senti 50 watu kwa ujumla hutumia zana maalum za usafiri
reli 5 itavuka ardhi kwa miaka
kutoka bursa teleferik inc hadi dubai
dubai metro ramani
kikundi cha serco cha uingereza cha kazi ya dubai metro hadi 2021
ankaraizmir line ya treni ya juukasi hupita kupitia salihli
yht itapita kupitia ereğli
treni itapita kupitia gümüşhane
usküdarçekmeköy metro ambayo itapita
furahia ladha ya theluji katika uludağ
uwekezaji wa miundombinu gmkurtalan mradi wa reli ya cizre mpakani 2013 inatarajiwa | 2020-01-28T14:09:28 | https://sw.rayhaber.com/2012/03/Subbai-chini-ya-ardhi-itakuwa-nyeusi-baada-ya-2017/ |
lowassa mbowe watakiwa kuripoti polisi leo | magazeti ya leo| tanzania news |tanzania today
wanafunzi 24 waliopata mimba watakiwa kuripoti polisi
mkuu wa wilaya ya rufiji mkoani pwani nurdin babu ameagiza wanafunzi 24 wa shule mbalimbali za sekondari wilayani humo waliopata ujauzito kuripoti kituo cha polisi cha wilaya novemba 25 mwaka huu ili watoe ushirikiano kukamatwa watu waliowatia mimba
agizo hilo la naibu spika limetolewa leo bungeni mjini dodoma wakati akitolea ufafanuzi mwongozo wa mbunge wa ukonga mwita waitara (chadema) aliyeiomba serikali
mamlaka nchini tanzania imewataka watu watatu inaowashutumu kwa kuwa wapenzi wa jinsia moja kuripoti kwa maafisa wa polisi ili kuhojiwa la sivyo wakamatwe
mbunge wa kawe na mwenyekiti wa baraza la wanawake la chadema (bawacha)halima mdee
kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi kinondoni camillius wambura alisema kuwa mbunge huyo ataripoti kituoni | 2019-05-24T15:26:21 | http://www.tanzaniatoday.co.tz/news/lowassa-mbowe-watakiwa-kuripoti-polisi-leo |
kushangaza zaidi binafsi au biashara aviation charter ya boeing 757 ndani jet binafsi mapambo tazama mwisho na wysluxurycom | 2018-06-23T00:45:15 | https://www.wysluxury.com/boeing-757-inside-private-jet-decoration/?lang=sw |
pichachampion francis cheka akiwa india tayari kumkabili vijender singh 17 dec lewis mbonde blog
pichachampion francis cheka akiwa india tayari kumkabili vijender singh 17 dec
lewis mbonde wednesday december 14 2016 0 masumbwi
mkutano na waandishi wa habari new delhi india
champion francis cheka akiwa na promota wake jay msangi new delhi india
ameuambia mtandao huu kuwa tumefika salama na naendelea vzuri na mazoezi sitawaangusha ntarudi nyumbani na ushindi
promota jay msangichampion francis cheka na kocha wake mzee abdalah salehe komando
championi francis cheka
posted by lewis mbonde at wednesday december 14 2016 | 2017-09-20T20:05:10 | http://habarikablog.blogspot.com/2016/12/pichachampion-francis-cheka-akiwa-india.html |
scooper kenya for you news wanamgambo12waalshabaabwauliwakatikamsituwabonihukolamu
wanamgambo 12 wa al shabaab wauliwa katika msitu wa boni huko lamu
wanajeshi wa kikosi cha ulinzi cha kenya (kdf) alhamisi waliwauwa wanamgambo 12 wa alshabaab katika shambulio katika kambi yao ndani ya msitu mkubwa wa boni katika kaunti ya lamu timu maalum ya operesheni ya kdf iliwashawishi magaidi hao kwenye kambi yao ya korisa kotile ambayo imekuwa maficho yao kwa muda mrefu kambi hiyo iko nginda kati ya korisa na bargoni
habari nyinginemtu mmoja awekwa karantini kaunti ya lamu baada ya kuonyesha dalili za corona
kati ya waliouawa alikuwa kamanda kutoka mkoa wa pwani ambaye alikuwa akitoa msaada wa akili na vifaa kwa magaidi waliojificha msituni
wanajeshi wa kdf walipata silaha pamoja na bunduki tatu za ak47 majarida saba risasi zaidi ya 1000 vifuko na kibeti cha maji shambulio hilo linakuja wiki moja baada ya vikosi maalum kuua wanamgambo sita na kuteka mmoja katika kaunti ya garissa hili ni pigo kubwa kwa kundi la watu wenye msimamo mkali kwani wanamgambo waliowekwa kwenye msitu wanaweza kufa kwa njaa kwa kukosa vifaa vya chakula na risasi kambi hiyo ilikuwa moja tu iliyobaki nchini kenya ambayo ilitumia kuratibu shughuli zao
breaking un implicates saudi prince in amazon ceo jeff bezos' hacked phonebruno fernandes crowned premier league player of the month for februaryworld war 3 $80 million bounty on donald trump's head by iranshocking huge sinkhole swallows bus and pedestrians in china (photos) heartless mother tortures baby to death because he pulled down the television | 2020-04-07T08:00:38 | https://scoopernews.com/kenya/000/2020/03/20/wanamgambo-12-wa-al-shabaab-wauliwa-katika-msitu-wa-boni-huko-lamu/9061458 |
wakala wa usajili wa biashara na leseni (brela)yashiriki mafunzo ya hataza nchini misri | full shangwe blog
home mchanganyiko wakala wa usajili wa biashara na leseni (brela)yashiriki mafunzo ya hataza nchini
wakala wa usajili wa biashara na leseni (brela)yashiriki mafunzo ya hataza nchini misri
tanzania ikiwa kama mwanachama wa shirika la miliki bunifu duniani (world intellectual propertywipo) kupitia wakala wa usajili wa biashara na leseni (brela) iliyopo chini ya wizara ya viwanda na biashara inashiriki mafunzo ya hataza kwa nchi za africa (training course on patent search and examination for african countries) nchini misri kuanzia tarehe 17/11/2019 hadi 21/11/2019
mafunzo hayo yamedhaminiwa na shirika la miliki bunifu duniani (wipo) nchi ya misri na ofisi ya hataza ya misri na kuhudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi 15 za africa tanzania imewakilishwa na bi suzana sensoafisa mwandamizi kutoka kitengo cha miliki bunifubrela
mafunzo haya yanamanufaa kwa taifa letu kwenye maswala ya uvumbuzi ili kuweza kuendana na kauli mbiu ya serikali ya viwanda
vumbuzi zinahitajika ili kuwa na bidhaa na huduma zenye ubora na zenye kukidhi mahitaji ya wananchiili kuendana na ulimwengu wa sasa wa technolojia
previous articlewanafunzi watakiwa kupewa stadi za maisha wakiwa bado shuleni
next articlemkoa wa lindi wajivunia mafanikio miaka 4 ya jpm | 2019-12-07T16:35:32 | https://fullshangweblog.co.tz/2019/11/18/wakala-wa-usajili-wa-biashara-na-leseni-brelayashiriki-mafunzo-ya-hataza-nchini-misri/ |
kurasa zinazohusiana arusha urban water supply and sanitation authority auwsa
kiingerezakiswahili
mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira arusha
kuhusu mamlaka
muundo wa mamlaka
auwsa departments
auwsa units
utawala na wafanyakazi
watendaji wakuu
huduma ya maji
huduma ya majitaka
shughuli za mazingira
vyanzo vya maji
mkataba wa huduma
ankara za maji
maombi mapya
jinsi ya kulipa ankara
utaratibu wa ulipaji
kukata na kuunganisha
machapisho na ripoti
kurasa zinazohusiana
http//wwwtanzaniagotz
the portals main objective is to enable a one stop center interface for public services delivery in a transparent easy and cost effective manner from various public institutions for the benefit of citizens
https//wwwmajigotz
wizara ya maji ilianzishwa rasmi kwa tangazo la serikali namba 494 la tarehe 17 desemba 2010 na kukabidhiwa majukumu ya kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji
arusha city council
http//wwwarushaccgotz/
arusha was declared township authority in 1948 with population of 5320 inhabitants in 1980 was upgraded to municipality and acquire a city status in 2012 as the hub of the countrys tourist industry arusha
energy and water utilities regulatory authority (ewura)
http//wwwewuragotz/
the energy and water utilities regulatory authority (ewura) is an autonomous multisectoral regulatory authority established by the ewura act cap 414 of the laws of tanzania it is responsible for technical and
association of tanzanian water suppliers (atawas)
http//atawasortz/
the association of tanzanian water suppliers (atawas) is a membership based association operating in tanzania mainland registered under the societies ordinance of 1954 and its amendments atawas was established
giz tanzania water
http//wwwswsdortz/home/
the support to the water sector development in tanzania (swsd) is a bilateral development cooperation programme between the united republic of tanzania and the federal republic of germany the programme is
malipo ya ankara
angalia akara yako hapa
anwani zetu
arusha urban water supply and sanitation authority auwsa
tel +255 272547186/ 2547163
fax +255 272547163/ 2548981
call centre 0800110069
email md@auwsagotz
sehemu za tovuti
mhe rais akikagua mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa katika jiji la arusha
tenki la shamba la mbegu (seed farm) lenye uwezo wa kubeba maji lita milioni kumi
© copyright 2019 mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira arusha
maswali ya kujiuliza
maoni na maulizo | 2019-11-15T03:05:21 | http://www.auwsa.go.tz/sw/resources/links |
maganga media mkutano wa haki za binadamu london ' '' var month = [123456789101112] var month2 = [janfebmaraprmayjunjulaugsepoctnovdec] var day = postdatesplit()[2]substring(02) var m = postdatesplit()[1] var y = postdatesplit()[0] for(var u2=0u2
home » habari muhimu maganga media news » mkutano wa haki za binadamu london
mkutano wa haki za binadamu london
by emmanuel maganga jun 18 2012
mshiriki kutoka tanzania alistidia rugaitika akiwa katika mkutano wa european leadership and human rightsprotection of the unempowered and the dispossessed uliomalizika jioni hii jijini london katika jumba la bunge la uingereza
baadhi ya washiriki wengine walioshiriki kwenye mkutano huokutoka kushoto mshiriki kutoka cameroon ambaye pia ni mwandishi wa habaritosamawe kutoka tanzaniamr amone toka uganda na mshiriki kutoka rwanda
mshiriki kutoka tanzania katikati akiwa na mshiriki kutoka uganda kulia mr amone
na msemaji kwenye huo mkutano mr keith best ambaye ni chief executivefreedom from torture uk | 2018-12-19T02:23:27 | http://maganga-resources.blogspot.com/2012/06/mkutano-wa-haki-za-binadamu-london.html |
ghasia za mtwara tz mbunge atiwa mbaroni | radio qiblaten 1036 fm
ghasia za mtwara tz mbunge atiwa mbaroni 30 rajab1434
polisi nchini tanzania wamemkamata mbunge wa mtwara mjini hasnain
murji kwa tuhuma za kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bomba la gesi kutoka mkoani humo kwenda mji mkuu wa nchi hiyo dar es salaam
msemaji wa jeshi la polisi nchini tanzania advera senso amenukuliwa na vyombo vya habari nchini tanzania akisema kuwa murji ambaye ni mbunge
wa chama tawala ccm alikamatwa nyumbani kwake maeneo ya shangani mjini mtwara hivi karibuni pia viongozi wanne wa vyama vya upinzani mkoani mtwara walikamatwa na kufikishwa katika mahakama ya mtwara juni 4 wakikabiliwa na mashtaka matatu ya kula njama kufanya uchochezi na kuamsha hisia mbaya miongoni mwa watanzania
murji amekamatwa ikiwa zimepita zaidi ya wiki mbili tangu kutokea vurugu kubwa mkoani mtwara ghasia hizo katika mkoa huo wa kusini magharibi mwa tanzania zilidumu kwa siku mbili ambapo polisi walipambana na makundi ya vijana wanaopinga mradi wa bomba la gesi kujengwa watu kadhaa walipoteza maisha katika vurugu hizo na mali nyingi kuharibiwa wakaazi wa mtwara wanapinga wazo la kusafirishwa gesi
nje ya eneo hilo kwa njia ya bomba wanasema gesi inapaswa kusafishwa katika eneo hilo kabla ya kusafirishwa ili wenyeji wapate ajira | 2017-06-29T09:12:11 | http://radioqiblaten-fm.blogspot.com/2013/06/ghasia-za-mtwara-tz-mbunge-atiwa-mbaroni.html |
tungependa kuwajulisha kuwa kampuni yetu itakuwa imefungwa kwa ajili ya likizo majira ya joto kutoka agosti 6 hadi 18 agosti katika kipindi kwamba sisi si kuwa na uwezo wa kutoa msaada lakini sisi kuchukua huduma ya maombi yote yako kwa haraka kama sisi kupata nyuma kazi
tunawashukuru sana kwa ushirikiano wenu na uelewa
sisi pia napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru kwa pongezi yako yote msaada na mapendekezo kwamba msaada plugin hii muhimu kukua
booking kalenda husaidia kwa urahisi kuongeza kwa wordpress yako mwenyewe tovuti nguvu na rahisi mfumo booking katika dakika chache
msimamizi anaweza kuunda kalenda kwa ajili ya huduma moja au zaidi ambayo inapatikana kwa booking na chaguo kuweka tidsramar mbalimbali kwa ajili ya kila siku (jumatatu kwa njia ya jumapili) na sifa nyingine wote unaweza kupata chini wateja itakuwa kuangalia kalenda na urahisi mahali kutoridhishwa wote wateja na msimamizi kupokea taarifa ya barua pepe zao
je una kituo cha michezo unaweza kuunda booking kalenda kwa kila mahakama mchezo
je ofisi yako kupokea wateja kwa kuteuliwa unaweza kuunda booking kalenda ya kila mtaalamu
je wewe ni mpishi juu ya mahitaji hebu wateja wako urahisi kitabu huduma wako wa kupikia
je wewe mwenyewe biashara kukodisha baiskeli unaweza kuweka kalenda kwa kila baiskeli
kama hawataki kugusa code yoyote hii ni lazima kuwa chombo kwa ajili yenu jopo utawala hauhitaji ujuzi wowote coding kufunga na kufanya kazi yake wewe tu na kuweka yako vigezo configuration msingi kama vile tovuti yako url barua pepe yako db
inafaa wakati upatikanaji mara moja inayoonekana
preview instantaneous inapatikana wakati inafaa rollover
alifanya rahisi netsurfing katika kuchagua miezi na siku
kutoridhishwa nyingi uwezekano
rahisi kutumia interface
idadi ya ukomo wa kalenda ya kuweka (kila kalenda inaweza kutaja huduma mbalimbali inapatikana kwa reservation)
idadi ya ukomo wa inafaa wakati kuweka muda wa kila mmoja
customizable idadi ya kutoridhishwa inapatikana kwa yanayopangwa
kila kalenda ana uhuru wake mwenyewe seti ya mazingira
mara moja kuundwa kalenda uwezekano wa kurekebisha kila yanayopangwa wakati moja kwa moja au katika kikundi wakati wowote
uwezekano wa kuongeza inafaa tofauti kwa siku kwa urahisi
uwezekano wa kuweka wewe siku ya kufunga
uwezekano wa kuchagua jinsi siku nyingi kabla ya mtumiaji ina kitabu inafaa
chaguo kuweka mashamba ya lazima ya aina booking
fomu booking kinasa kuwawezesha au afya
nafasi ya uchaguzi jinsi ya kuthibitisha kutoridhishwa (moja kwa moja kuthibitishwa kwa barua pepe au manually katika admin jopo)
paypal ushirikiano
reservation csv usafirishaji
tarehe format configuration (uchaguzi kati ya marekani na uingereza tarehe format)
mfumo wa muda configuration (uchaguzi kati ya saa 12 asubuhi / mchana na saa 24 wakati format)
kuarifiwa kwa admin na wateja alimtuma katika mfumo
uwezekano wa kuweka maandiko email notification kwa mfano booking barua pepe ya uthibitisho
hakuna ujuzi coding required
toleo la sasa 300
update kutoka toleo any kwa 300 ifuatavyo hatua hizi
1 kufanya backup ya plugin folder yako zilizopo na database
2 deactivate plugin kutoka admin yako jopo kama wewe ni mbio multisite deactivate katika maeneo yote
3 nakala wpbooking kalenda folder (toleo 300) na overwrite wpbooking kalenda folder ya toleo la awali
4 reactivate plugin
5 kwenda plugin kuu ya ukurasa kubonyeza kwenye orodha kushoto juu booking kalenda saa ya juu ya ukurasa utaona sanduku njano kusema kwamba unaweza kuokoa marekebisho kufanywa na langphp files katika toleo la awali bonyeza kiungo zinazotolewa na pakia mafaili zamani kutoka backup yako
nb kama si mabadiliko yoyote ya langphp files do not kufanya utaratibu namba 5
nb kumbuka kwamba si maandiko yote itakuwa usahihi updated kuangalia yao katika mpya usimamizi nakala sehemu
ecommerce all items uteuzi booking booking mfumo kalenda cms usimamizi organizer kodi reservation ratiba tiketi | 2018-05-21T01:15:55 | https://sw.worldwidescripts.net/wp-booking-calendar-43152 |
haki za kiuchumi zilivyojadiliwa katika mkutano wa haki za binadamu barani afrika rfi
imetangazwa tarehe 19112018 imehaririwa 19112018 saa 0915
onesmo ole ngurumwa ni mwanaharakati kutoka tanzania aliyeshiriki mkutano wa 63 wa haki za binadamu barani afrika uliomalizika hivi karibuni nchini gambia mwananchi
hivi karibuni kulifanyika mkutano wa 63 wa haki za binadamu barani afrika ambao uliangazia mwenendo wa haki za binadamu kwa mataifa mbalimbali ya afrika miongoni mwa agenda zilizojadiliwa ni haki za kiuchumi fredrick nwaka amekuandalia makala haya
saudi arabiahaki za binadamumauaji | 2019-07-23T22:06:59 | http://sw.rfi.fr/siasa-uchumi/20181119-haki-za-kiuchumi-zilivyojadiliwa-katika-mkutano-wa-haki-za-binadamu-barani-afr |
ni marufuku walimu kukusanya michango ya wanafunzi nchimbi
ni marufuku walimu kukusanya michango ya wanafunzi nchimbi
mkuu wa mkoa wa singida (kushoto) akitoa maelekezo kwa viongozi wa mamlaka ya bonde na viongozi wa wilaya ya mkalama juu ya namna bora ya utunzaji wa mazingira
mkuu wa wilaya ya mkalama mhe mhandisi jackson masaka akimuelezea jambo mkuu wa mkoa wa singida mhe daktari rehema nchimbi katika kituo cha upimaji wa wingi wa maji kijiji cha iambi
mkuu wa mkoa wa singida na viongozi waandamizi wa wilaya ya mkalama wakishiriki ufunguzi wa darasa la kisasa lililojengwa na shirika la 'norwegian church aid' katika kijiji cha munguli jana
afisa miradi wa mashirika ya 'norwegian church aid' (nca) na 4 corners cultural program (4ccp) nelson faustine akielezea mchakato mzima wa ujenzi wa darasa la kisasa uliofanywa na mashirika hayo katika kijiji cha munguli mbele ya mkuu wa mkoa wa singida mhe daktari rehema nchimbi jana
mkuu wa mkoa wa singida mhe daktari rehema nchimbi akiwa kwenye picha ya pamoja na mshauri mkuu wa masuala ya maji kutoka shirika la 'norwegian church aid' nca manford hart wakati wa ziara yake jana katika kijiji cha munguli
mkuu wa mkoa wa singida mhe daktari rehema nchimbi akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa wilaya ya mkalama mhe lameck itungi wakati wa ziara yake jana katika kijiji cha munguli
mkuu wa mkoa wa singida mhe daktari rehema nchimbi (kushoto mbele) akiwa ndani ya darasa lililojengwa na shirika la 'norwegian church aid' mara baada ya kulifungua jana katika kijiji cha munguli
mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya mkalama mhandisi godfrey sanga akiwaasa wananchi wa kijiji cha munguli juu ya umuhimu wa kutumia vyema fursa wanazozipata
mkuu wa wilaya ya mkalama mhe mhandisi jackson masaka akizungumza machache muda mfupi kabla ya kumkaribisha mkuu wa mkoa wa singida katika kijiji cha munguli jana
viongozi waandamizi wa kanisa la hydorm na wawakilishi wa shirika la 'norwegian church aid' wakipokea cheti kutoka kwa mkuu wa mkoa wa singida cheti hicho kimetolewa na uongozi wa wilaya ya mkalama kama ishara ya kushukuru kwa mchango uliotolewa na shirika hilo wilayani hapa
mkuu wa mkoa wa singida mhe daktari rehema nchimbi akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa wilaya ya mkalama pamoja wawakilishi wa shirika la 'norwegian church aid' kutoka nchini norway jana katika kijiji cha munguli nyuma yao ni paneli za sola zinazohakikisha upatikanaji wa maji kijijini hapo muda wote
posted by mkalama yetu at 0339 | 2019-01-18T02:25:24 | http://mkalamayetu.blogspot.com/2018/01/ni-marufuku-walimu-kukusanya-michango.html |
matukio mbalimbali ya ofisi ya waziri mkuu bungeni leo jijini dodoma habari na matukio
home habari habari na matukio kitaifa matukio mbalimbali ya ofisi ya waziri mkuu bungeni leo jijini dodoma
kajunason at april 09 2019 habari habari na matukio kitaifa
waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu (sera bunge kazi vijana ajira na wenye ulemavu) jenista mhagama (mwenye blauzi nyeusi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya mawaziri na wabunge nje ya ukumbi wa bunge dodoma wa kwanza kushoto ni waziri wa elimu sayansi na teknolojia profesa joyce ndalichako (picha zote na ofisi ya waziri mkuu) | 2019-04-26T12:27:15 | http://www.kajunason.com/2019/04/matukio-mbalimbali-ya-ofisi-ya-waziri.html |
irene mwamfupe jamii rose muhando kwa utapeli too much
rose muhando kwa utapeli too much
lile jinamizi la kupokea fedha kwa ajili ya kushiriki tamasha la kuimba nyimbo za injili kisha kutotokea siku ya tukio linazidi kumwandama nyota wa muziki huo nchini rose athuman muhando safari hii akidaiwa kumliza tena mtu ijumaa wikienda lina kesi hiyo mkononi
nyota wa muziki huo nchini rose athuman muhando
kwa mujibu wa chanzo makini cha ndani safari hii ameendelea kupokea fedha kutoka kwa mshirika wake kwenye mambo ya injili alex msama kwa makubaliano ya kushiriki tamasha la krismasi kwenye uwanja wa samora mjini iringa lakini siku ya tukio ijumaa iliyopita mwanadada huyo hakutokea
chanzo kilisema hivi jamani mnajua kuwa rose mhando amemliza tena alex msama amepokea fedha kwa ajili ya kushiriki tamasha la krismasi iringa lakini pamoja na kupokea fedha hizo ameingia mitini
hii ni mara ya pili kwenye uzinduzi wa albamu ya msanii john lisu pale diamond jubilee (dar) rose alipokea shilingi milioni moja kutoka kwa msama lakini siku ya uzinduzi hakutokea
kusema ukweli huu utapeli wa rose wa kuchukua fedha za watu halafu hatokei sasa imekuwa too much nimesikia habari kwamba ameogopa kutokea uwanjani hapa ambako tamasha lilifanyika kwa kuhofia mimba yake kuonekana maana kwa sasa ni kubwa
bw alex msama
baada ya madai hayo wikienda lilimvutia waya muandaaji wa tamasha hilo msama ambapo alisikiliza kwa muda madai ya mwandishi na mwishowe alikata simu bila kusema chochote
rose naye aliposakwa kwa njia ya simu iliita bila kupokelewa ikiwa ni mtindo aliouanzisha siku za karibuni anapotafutwa na waandishi kwa ajili ya ufafanuzi wa habari yake yoyote ile
mbali na msama kudaiwa kulizwa kiasi hicho cha pesa ambacho hakikujulikana ni shilingi ngapi ikiwa ni mara ya pili ndani ya mwaka mmoja rose pia ana madai mengi kutoka kwa watu mbalimbali kwamba amekuwa akipokea pesa kwa makubaliano ya kufanya shoo lakini anaingia mitini kwa kuzima simu au kutopokea akipigiwa
labels rose muhando staa wetu | 2018-07-17T23:28:15 | http://irenemwamfupejamii.blogspot.com/2014/12/rose-muhando-kwa-utapeli-too-much.html |
june 11 2019 mwanahalisi online
regina mkonde 5 days ago 1610 views
mwandishi wetu 5 days ago 1997 views
faki sosi 5 days ago 1827 views
serikali imeitaka mahakama ya rufani kuirudisha kesi ya jinai no 245 ya mwaka 2012 inayomkabili sheikh ponda issa ponda katika mahakama ya kisutu ili atiwe hatiani anaripoti faki sosi (endelea) ombi
mwandishi wetu 5 days ago 2505 views
danson kaijage 5 days ago 1198 views
regina mkonde 5 days ago 1434 views
faki sosi 6 days ago 1718 views
sheikh ponda issa ponda katibu wa jumuiya na taasisi za kiislamu tanzania leo tarehe 11 juni 2019 anapandishwa kizimbani kwenye mahakama ya rufani jijini dar es salaam baada ya serikali | 2019-06-16T18:38:03 | http://mwanahalisionline.com/2019/06/11/ |
angela merkel ateuliwa na rais wa shirikisho kuwa kansela | matukio ya kisiasa | dw | 05032018
angela merkel ateuliwa na rais wa shirikisho kuwa kansela
kifungu hicho cha sheria ndicho kinachofungua njia ya kuchaguliwa kiongozi wa serikali anaechaguliwa ni yule mwenye kudhibiti idadi kubwa ya wabunge na sio tu wabunge waliohudhuria zoezi la kupiga kura ndio maana vyama vinavyounda serikali ya muungano hujitahidi kufanya kila liwezekano ili kuhakikisha wabunge wao wote wanahudhuria kikao cha kumchagua kansela
katika mhula wake huu wa nne kansela merkel hatoweza kutegemea sauti nyingi kama ilivyokuwa alipopigiwa kura mwaka 2013 serikali ya wakati ule ya muungano wa vyama vikuu au groko kama inavyoitwa ilikuwa na jumla ya wabunge 504 kutoka jumla ya wabunge 631 kaatika bunge la shirikisho bundestag serikali hii mpya lakini ina wabunge 399 tu kutoka jumla ya wabunge 709 kwa hivyo marchi 14 wabunge wasiopungua 355 watabidi wampigie kura angela merkel aweze kuchaguliwa kuwa kansela
baada ya rais wa shirikisho kumpendekeza kansela mteule merkel ametilia mkazo umuhimu wa kuharakishwa mambo ili serikali mpya ipate kuwajibika ipasavyoitakuwa muhimu kuharakisha kwasababu serikali itakapoundwa tu kazi inabidi ianze na mie kama kansela mteule natumai nitachaguliwa nitafanya kila niwezalo na kwa nguvu zangu zote ili serikali hii iwajibike ipasavyo mbele ya wananchi nchini ujerumani
kansela merkel pamoja na rais wa marekani donald trump na rais wa urusi vladimir putin
ujerumani kushirikiana zaidi na ufaransa barani ulaya
kansela merkel ameahidi kuipatia ujerumani sauti ya nguvu barani ulaya kuweza kukabiliana na changamoto zinazousumbua umoja huotunashuhudia kila siku jinsi umoja wa ulaya unavyotakiwa uwajibike na sauti ya nguvu ya ujerumani kwa ushirikiano na ufaransa na mataifa mengine wanachama ni muhimu amesema kansela merkel kabla ya mkutano wa kamati kuu ya chama chake cha christian democratic unioncdu
miongoni mwa changamoto zinazoukabili umoja wa ulaya kansela merkel ametaja vurugu katika biashara ya kimataifa zinazochochewa na rais donald trump wa marekani na mzozo wa syria ambako licha ya kwamba umoja wa ulaya hauhusiki lakini unasababisha mikururo ya wakimbizi kuingia ulaya kwa wingi ambao haujawahi kushuhudiwa tangu mwaka 1945
wakati huo huo utafiti wa maoni ya wananchi unaonyesha kura ya ndio ya spd kwa serikali ya muungano wa vyama vikuu imewapatia faraja idadi ya wanaokiunga mkono chama hicho imeongezeka na kufikia asili mia 19 huku cdu/csu wakipoteza nukta moja na kubakiwa na asili mia 34
mada zinazohusiana angela merkel jeshi la ujerumani bundeswehr ujerumani bonn frankwalter steinmeier bunge uchaguzi ujerumani 2017 mkutano wa usalama munich helmut kohl bundeswehr
maneno muhimu ujerumani angela merkel bunge mazungumzo ya kuunda serikali
kiungo https//pdwcom/p/2tj0r
spd yawachagua norbert walterborjans na saskia esken 01122019
wakosoaji wakubwa wa muungano unaounda serikali ya kihafidhina inayoongozwa na kansela angela merkel wameshinda uchaguzi katika uongozi wa chama cha social democrats spd nchini ujerumani siku ya jumamosi (30112019) | 2019-12-10T02:19:33 | https://www.dw.com/sw/angela-merkel-ateuliwa-na-rais-wa-shirikisho-kuwa-kansela/a-42833745 |
usiku wa kisasi liverpool kukumbusha ya barcelona psg kazi anayo kwa dortmund leo gazeti la dimba
home makala usiku wa kisasi liverpool kukumbusha ya barcelona psg kazi anayo kwa dortmund
atletico madrid watakuwa wageni wa vinara wa ligi kuu england liverpool katika uwanja wa anfield kwenye mchezo wa pili wa hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa ulaya baada ya ule wa kwanza diego simeone kuondoka kifua mbele kwa ushindi wa bao 10 dhidi ya jurgen klopp
simeone atakutana na moja ya timu bora duniani kwa sasa huku atletico madrid wakiwa nafasi ya tano katika msimamo wa ligi kuu hispania la liga nyuma ya barcelona real madrid sevilla fc na getafe
liverpool ni timu imara msimu huu lakini vipigo vitatu walivyopata msimu huu vimetoka katika michuano hii ilitokea katikati ya septemba mwaka jana walipofungwa na napoli wakati ambao timu hiyo ya jurgen klopp akiwa kileleni kwa tofauti ya pointi tano tu
pia wakali hao wa england walifungwa mabao 30 na watford katika mchezo wa ligi kuu england ikiwa ni kichapo cha kwanza kwao kisha kukubali kichapo cha mabao 20 kutoka kwa chelsea kwenye mechi ya kombe la fa
licha ya ubora walionao na kufanya vizuri katika ligi kuu england mchezo wa leo dhidi ya atletico madrid ya diego simeone unatarajiwa kuwa mgumu kutokana na timu hizo mbili kucheza mpira wa nguvu na kasi ukizingatia mechi ya kwanza iliyochezwa hispania mwenyeji alipata ushindi
habari za timu zikoje
atletico walicheza michezo yao ya karibuni bila wachezaji wao nyota kutokana na kukumbwa na majeraha watacheza dhidi ya liverpool iliyokuwa na mastaa wao kwa asilimia kubwa
beki wa kulia wa atletico kieran trippier ataukosa mchezo wa leo sababu ya majeraha ya nyama za paja tayari mchezaji huyo raia wa england amekosa mechi sita zilizopita
mshambuliaji joao felix ambaye alisajiliwa kwa pauni milioni 113 msimu huu anatarajia kuwa sehemu ya kikosi cha simeone huku hivi karibuni aliwakaribisha mastraika wake tegemeo alvaro morata na diego costa waliokuwa nje kwa majeraha
akiwa mshambuliaji alyefunga robo ya mabao ya atletico msimu huu uwepo wa morata katika kuiongoza safu hiyo ya ushambuliaji litakuwa jambo muhimu kwa timu hiyo ya hispania dhidi ya vijana wa klopp
liverpool wana wachezaji wawili ambao wapo nje kwa muda mrefu nathaniel clyne na xherdan shaqiri huku klopp akitarajia kumkaribisha kikosini nahodha wake jordan henderson
pia kwa upande mwingine watakosa huduma ya kipa wa tegemeo raia wa brazil alisson becker ambaye alipata majeraha ya nyama za paja mazoezini
rekodi zao zikoje
timu hizo zimekutana mara tano katika michuano ya ulaya mara ya mwisho ilikuwa msimu wa 2009/10 kwenye nusu fainali ya ligi ya europa na atletico walishinda kwa mabao ya ugenini baada ya sare ya mabao 22
kwa mara ya kwanza zilikutana katika hatua ya makundi msimu wa 2008/09 na mchezo kumalizika kwa sare ya bao 11 ndani ya mechi hizo tano walizokutana liverpool ameshinda mara moja huku wakienda sare mbili na atletico madrid wakishinda mara mbili
hata hivyo uwanja wa anfield utakuwa na kumbukumbu nzuri kwa liverpool ambao walipindua meza kwa kuifunga mabao 40 barcelona msimu uliopita baada ya kuchapwa mabao 30 mchezo wa kwanza uliochezwa nou camp msimu uliopita
simeone hana rekodi nzuri kipindi cha karibuni atletico wameshinda michezo mitatu tu kati ya tisa waliyocheza katika mechi za la liga na spanish cup ambako waliondoshwa na timu ya daraja la tatu cultural leonesa
licha ya matokeo hayo mabaya kwenye ligi wapo nafasi ya tano wameachwa mbali na timu mbili za juu real madrid na barcelona ambao wanakimbizana kwenye mbio za ubingwa huku atletico wakifanikiwa kupata pointi moja tu kwa vigogo hao katika michezo miwili waliyocheza
katika idara ya ulinzi wanaendelea kufanya vizuri mabeki na kipa wao jan oblak wanafanya kazi na jitihada kubwa isipokuwa kwenye safu ya ushambuliaji ambayo imelegalega na kuiangusha timu hiyo
kutoka michezo 27 waliyocheza msimu huu ya la liga wamefunga mabao 31 tu huku wakifungwa 21 na kuwa kati ya timu zilizoruhusu mabao machache msimu ndani ya ligi kuu lakini idara ya ushambuliaji inayoongozwa na morata wameshindwa kufanya kazi yao vizuri
leo kama wakicheza na kufanikiwa kuwazuia liverpool kufunga bao itakuwa faida kwao kwani watakuwa salama na watafanikiwa kusonga mbele kwenye michuano hiyo
vinara hao wa ligi kuu england wapo imara katika idara ya ulinzi kwa wiki za karibuni wamekuwa wakifanya vibaya katika michezo minne iliyopita wameruhusu kufungwa mabao zaidi manne
vikosi vitakuaje
liverpool xi adrian alexanderarnold gomez van dijk robertson henderson fabinho wijnaldum salah firmino mané
atletico xi oblak trippier savic felipe renan lodi saul partey llorente koke felix morata
tutarajie nini ufaransa
borussia dortmund watakuwa wageni wa wakali wa ufaransa psg katika mchezo wa pili wa hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa ulaya mara baada ya kushinda mabao 21 ule wa kwanza katika uwanja wa signal iduna park
psg walisonga mbele baada ya kuwa vinara katika kundi a lililokuwa na real madrid huku borussia dortmund wakikatama nafasi ya pili kwenye kundi f lililokuwa na barcelona na inter milan
timu zote mbili zikiwa katika viwango vya juu kwenye michezo yao ya ligi huku psg akiwa na kazi kubwa ya kufanya ya kushinda ushindi wa mabao 20 ili kusonga mbele katika michuano ya ulaya
kabla ya mchezo wa kwanza uliochezwa ujerumani timu hizo mara ya mwisho kukutana ilikuwa mwaka 2011 pia mchezo wa leo utawakutanisha vijana wanaotabiriwa kufanya makubwa katika ulimwengu wa soka akina jadon sancho kylian mbappe na erling haaland
habari zao zikoje
katika mchezo huo inatarajiwa kwa psg kumkaribisha neymar ambaye alikosekana katika michezo ya hivi karibuni ya kikosi hicho kilichopo kileleni katika msimamo wa ligi kuu ufaransa
itakumbukwa neymar alikosa michezo mitatu ya hatua ya makundi msimu huu kutokana na kupewa adhabu kwa kuwatolea maneno machafu waamuzi msimu uliopita
supastaa huyo raia wa brazil bado hajaonesha kiwango kizuri katika michuano hiyo ya ulaya msimu huu amefunga mabao mawili kwenye michezo mitatu aliyocheza mpaka sasa
hata hivyo kocha wa psg thomas tuchel bado hajathibitisha kama mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 atakuwa sehemu ya kikosi kwani wamefanikiwa kufanya vizuri michezo minne ambayo mbrazil huyo alikosekana kwa kufunga mabao 17
dortmund wataendelea kukosa huduma ya nahodha wao marco reus ambaye yupo nje kwa majeraha ya misuli huku akitarajiwa kurejea machi mwaka huu
emre can ambaye alisajiliwa mwezi uliopita kutoka juventus amefanikiwa kuonesha kiwango kizuri katika michezo aliyocheza na kufanikiwa kufunga bao nzuri kwa shuti kali la mita 30 dhidi ya timu yake ya zamani bayer leverkusen
mchezo huohuo dortmund walishuhudia kiungo wao julian brandt akipata majeraha ya enka ingawa bado haijathibitishwa kama utaikosa mechi ya leo dhidi ya psg
ziliwahi kukutana
kabla ya mechi ya kwanza iliyochezwa uwanja wa signal iduna park klabu hizo hazijakutana kwa miaka 10 sasa mwaka 2010 walicheza michezo miwili na yote kuisha kwa sare katika kundi j la michuano ya ligi ya europa lakini psg walifanikiwa kusonga mbele
straika robert lewandowski ambaye sasa ni kinara katika orodha ya wafungaji wa ligi kuu ujerumani bundesliga akiwa na bayern munich aliingia kutokea benchi kwenye mchezo wa mwisho uliochezwa uwanja wa parc des princes hata hivyo alishindwa kuonesha cheche zake na mechi kuisha bila kufungana
vikosi vitakuwaje
psg xi navas kehrer silva kimpembe bernat gueye marquinhos paredes di maria mbappe neymar
dortmund xi burki piszcek hummels zagadou hakimi can witsel guerreiro sancho haaland hazard
previous articlebarca napoli bila mashabiki kisa corona
next articlecorona ilivyotibua mipango ya mastaa hawa
simba ya mo dewji haipoi
kirumba yaongoza kufungwa mabao mengi vpl 2016/17
mambo matano yaliyosisimua siku 100 za mourinho old trafford | 2020-05-29T17:52:35 | http://www.dimba.co.tz/usiku-wa-kisasi-liverpool-kukumbusha-ya-barcelona-psg-kazi-anayo-kwa-dortmund-leo/ |
burundi wamiminika uchaguzi wa rais bbc swahili
burundi wamiminika uchaguzi wa rais
http//wwwbbccom/swahili/habari/2015/07/150720_burundi_elexviolence
image caption bujumbura burundi
kumetokea ufyatulianaji wa risasi na milipuko usiku kucha nchini burundi usiku wa kuamkia uchaguzi wa rais uliozua utata kiongozi wa sasa wa nchi hiyo anawania muhula wa 3 kama rais licha ya madai kuwa anakwenda kinyume na katiba ya nchi
viongozi wengi wa upande wa upinzani wameapa kususia uchaguzi huo
saa chache tu kabla ya kufunguliwa shughuli ya upigaji kura milipuko ya gruneti iliripotiwa jijini bujumbura na kufuatiwa na milio ya risasi maeneo mengine risasi hizo zilisikika kwa wingi zaidi mjini humo japo haikuwa wazi ni nani hasa anayefyatua risasi hizo
kwa mujibu wa mshauri wa kisasa wa rais haya ni mashambulio yanayofanywa na 'magaidi' wanaonuia kuvuruga shughuli ya uchaguzi
mnamo mwezi mei kundi la wanajeshi wa ngazi ya juu nchini burundi walijaribu kufanya mapinduzi yaliyotibuka hata hivyo sasa baadhi yao wametishia kufanya shambulio lingine
hofu ya kuwa uchaguzi huu huenda ukalitumbukiza taifa hilo katika mzozo mbaya zaidi wa kisiasa imeifanya jamii ya kimataifa kuitisha kuahirishwa kwa uchaguzi na kupendekeza mashauriano ya amani
wito kama huu uliambulia patupu mwishoni mwa wiki mashauriano ya amani yalivunjika na uchaguzi ndio huu unafanyika huku wito wa kuahirishwa kwake ukipuuziliwa mbali
takriban watu 70 wamefariki katika maandamano ya awali kupinga uchaguzi huuhuku wengine zaidi ya elfu 160 wakiikimbia nchi kwa hofu ya kuzuka mapigano | 2017-12-15T10:42:59 | http://www.bbc.com/swahili/habari/2015/07/150720_burundi_elexviolence |
athari za kuwatunukia na kuwarudi watoto
kwa kawaida binadamu yeyote hupenda kutiwa moyo na hujisikia vibaya anaposhutumiwa japo anaweza kukosolewa kistaarabu asijisikie vibaya kwa watoto wadogo umakini zaidi unahitajika kuliko ilivyo kwa watu wazima kwa vile wanahitaji kutiwa moyo kwa kila wanalojifunza ili wajenge tabia ya kujiamini kuwashutumu kila mara kuna madhara makubwa kuliko faida endelea na mfululizo wa makala zetu kutoka kitabu cha shirika la uchapishaji wa lugha za kigeni la beijing china juu ya afya
hamu ni mwalimu mwema jambo la namna ya kuchochea hamu ya mtoto ya kupenda masomo linazidi kuangaliwa wazazi wengi hutumia njia ya kutunukia na kuwarudi watoto wao ili kuchochea hamu yao lakini hawajui kwamba kuwatunukiwa na kuwarudi huweza kushusha hamu kwani hami inayochochewa kwa njia hiyo huwa ya muda tu
kwa nini basi inatokea hali ya namna hiyo kwanza kusoma sawasawa na kucheza ni jambo la kufurahisha na linategemea hiyari ya watoto kama watoto wanajifunza masomo yaliyolingana na kiwango chao cha akili na wanapata furaha katika wakati wa kusoma wataweza kujifunza kwa hiyari yao katika hali hiyo kuwatunukia kutaweza kushusha hamu iliyowajia kwa hiyari uchunguzi ufuatao unaweza kuthibitisha ukweli huo tuwagawanye watoto wanaopenda kuchora kuwa vikundi viwili watoto waitwe kuingia katika chumba kidogo mmoja baada ya mwingine watoto wa kikundi cha kwanza waambiwe mtoto anayechora picha nzuri atatunukiwa zawadi ni kitabu chenye picha nzuri ambacho huwavutia sana watoto halafu watoto wakachora kwa furaha na kupewa zawadi kwa watoto wa kikundi cha pili wasitajiwe zawadi ila waambiwe napenda sana kuona picha iliyochorwa na mtoto je utapenda kunichorea picha moja baada ya kusikia maombi ya watu wazima wataanza kuchora picha mwishowe tukihesabu picha picha tutagundua kwamba picha zilizochorwa na watoto wa kikundi cha kwanza ni nyingi sana hii inaonyesha kwamba kutunukia kunaleta matokeo mazuri zaidi lakini jambo linalostahili kuangalia ni kwamba wiki mbili baadaye tangu kufanya uchunguzi huo hatuna budi kuchunguza jinsi watoto wanavyocheza nje ya wakati wa masomo wanaweza kuchezea vipuzi vyao au kuchora picha wawekee kalamu na karatasi mezani na kila atakayependa kuchora basi atachora tu mwishowe tutagundua kwamba picha zilizochorwa tu mwishow tutagundua kwamba picha zilizochorwa na watoto wa kikundi cha kwanza yaani wanaotunukiwa zawadi ni chache sana
hii ni kwa sababu hamu yao ya kuchora picha imeshuka lakini watoto wa kikundi cha pili wanaendelea kupenda kuchora picha kama zamani kwani shauku yao haikutawaliwa na zawadi kwani shauku yao haikutawaliwa na zawadi bali na uchoraji tu
kwa hivyo kutunukia kunaweza kuchochea hamu ya watoto katika muda maalum tu na tunaposita kufanya hivyo hamu itashuka sana hata ikawa kidogo kuliko zamani
pili matokeo ya kusoma hayaonekani mtu fulani anaposema anafanya juhudi kwa ajili ya kutanzua matatizo lakini pengine anafikiri mambo yasiyohusiana na masomo yake
hali hii haiwezi kutambuliwa kutoka kijuujuu kutunukia na kurudi kunategemea matokeo ya matendo siyo kuzingatia kiwango cha juhudi yake hivyo ikatokea hali ya mtu anayetanzua tatizo atatunukiwa na asiyetanzua tatizo ataadhibiwa matokeo yake ni kwamba baadhi ya watoto wanafikiri ninajifunza kwa bidii sana kwa nini siwezi kupata zawadi badala ya kualaumiwa watajihisi kuwa ni watu wasiokuwa na uwezo na hivyo kufifisha hamu yao ya kusoma alikuweko mtu mmoja aliyewahi kufanya uchunguzi fulani kuhusu watoto watoto walifanya jihudi kubwa kutafuta lakini hawakufanikiwa baada ya kumaliza swali hilo watoto walipewa swali jingine yaani walitakiwa kutunga maneno yenye maana kwa kutumia herufi zilizotawanyika swali hili ni rahisi sana walakini matokeo yalionyesha kwamba watoto walioshindwa mara nyingi katika swali la kwanza walishindwa tena kwa mujibu wa uwezo wao ilikuwa rahisi kwao kujibu swali hilo lakini baada ya kushindwa mara nyingi walijihisi kwamba hawana uwezo tena wakaona kwamba hata kama watafanya kwa juhudi kiasi gani bado hawataweza kufaulu matokeo yatakuwa tofauti kabisa kama wakipewa swali rahisi kwanza na wanatanzua vizuri kwa juhudi zao
bila kuzingatia kiwango cha juhudi cha watoto tunawarudi eti kwa sababu hawawezi kutanzua swali kwa kufanya hivyo hata baadaye wakikuta swali lililoweza kutanzuliwa hawatokuwa na hamu ya kufanya hivyo jambo ambalo la kusikitisha ni kwamba katika wakati fulani mtu akikosewa kuadhibiwa atajiona yeye ni mtu asiyekuwa na uwezo hivyo hujenga mazoea ambayo humuathiri kwa upande mwingine
kwa ajili ya kukuza akili ya watoto tusitumie akili nyingi katika kuwatunukia na kuwarudi watoto bali tungefanya chini juu katika kuwafundisha watoto jinsi ya kujifanyia mambo yao kwa furaha
watakatifu paulo na petro mitume waliouawa kinyama mithili ya kuku asiyekuwa na mwangalizi
maneno ya mitume hao wawili ambayo ni ya maana zaidi kuyakumbuka ni mengi wafilipi waliandikiwa barua na mtume paulo akisema ninavyoona kila kitu ni hasara kwangu hasara tupu kwa ajili ya jambo bora zaidi yaani kumjua bwana wangu yesu kristo
maneno hayo yapo kwenye kitabu cha wafilipi 38
na tena mtakatifu mtume paulo akaongeza tena maneno mengine makubwa yaliyopatikana katika (2 tim 12) akisema namjua yule niliyemwamini na nina hakika kwamba yeye anaweza kukilinda salama mpaka siku ile
naye mtakatifu petro baadhi ya maneno yake makuu ni bwana wewe wajua yote wewe unajua kwamba ninakupenda na alipomuuliza yesu sisi tumeacha yote na tutakufuata tutapata nini basi
akajibiwa kwamba ninyi mlioacha yote na kunifuata mimi mtapokea mara mia na kurithi uzima wa milele
labda kwa kumtazama petro tunambiwa alikuwa miongoni mwa mitume waliokuwa pamoja na simoni bin yohane aliyekuwa mtu mwenyeji wa betsaida mkoani galilaya huko israel
yeye simoni bin yohane alikuwa mvuvi alipoitwa na bwana yesu ili amfuate mara simioni bin yohane alikubali akaziacha nyuma zile nyavu zake mashua yake na hata ndugu zake
basi petro tuliyemuona kuwa miongoni mwa mitume aliyekuwa wa kwanza kuungama kwamba yesu ni mungu akisema ndiwe kristo mwana wa mungu mzima ndipo bwana alipomweka kuwa mchungaji wake mkuu wa kundi lake lote yaani kanisa akasema
wewe ndiwe petro (maana yake ni mwamba) na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu na nguvu za jehanamu hazitaweza kulishinda
petro alikuwa mtu hodari sana na alimpenda mno mwalimu wake hata akataka kumfia hata katika bustani ile ya kule gestemane alijaribu kumtetea kwa upanga ingawa baadaye alikuja jionesha kuwa mwoga alipomkana yesu mara tatundiyo maana hata baada ya kufufuka kwake bwana yesu alimuuliza mara tatu kama kweli alimpenda kikwelikweli
petro ndiye aliyekuwa wa kwanza kutoa hotuba na kuanza kuwabatiza watu na ndiye yeye huyo aliyembatiza korneli yule mtu wa kwanza ambaye hakuwa myahudi aliyetaka kumwamini yesu kristo
petro alifanya hivyo akiitikia sauti aliyosikia katika njozi na baadaye akahudhuria katika mikutano mjini yerusalemu ambapo mitume waliamua kuwa siyo lazima kwa wakristo wa mataifa kushika sheria ya musa
kisha petro alipohama hapo yerusalemu akaenda huko antokia uturuki na kulisimamia kanisa la mji huo kisha baada ya miaka kadhaa petro alihamia roma akawa askofu wa kwanza wa mji huo
tunaambiwa kuwa wakati ule wa utawala wa kaisari nero wakristo waliodhulumiwa mno na ndivyo hali hiyo ilivyompata pia petro alikamatwa na kufungwa gerezani kwa ajili ya dini yake ya kikristo
pia tunaelezwa kuwa kati ya mwaka 64 au 65 petro anayekumbukwa na kanisa kila tarehe ya 29 ya mwezi juni kila mwaka pamoja na mtume paulo alihukumiwa kifo kwa ajili hiyo ya dini yake
kwa kadri ya mapokeo petro alihukumiwa akasulubiwa kichwa chini na miguu juu kwa sababu alivyoona yeye mwenyewe hakustahili kusulubiwa sawa na na bwana wake yesu kristo mtakatifu paulo yeye alikuwa ni mwenyeji wa mji wa tarso huko uturuki na inaelezwa kuwa alizaliwa katika familia ya wafarisayo
yeye mwenyewe anaelezwa kuwa hapo awali alikuwa mtesi mkali sana wa wakristo kwa kuwa aliona namna yao ya kuishi ilikuwa kinyume kabisa na sheria za musa
alipoelekea damasko nchini siria aliguswa na neema za bwana akaona ukweli ulivyokuwa paulo sasa akawa hapo paulo alikwenda arabia na kwa kadri ya masimulizi ya mapokeo alikaa mwenyewe jangwani akifundishwa na bwana wetu mwenyewe mambo mengi ya dini ya kikristo kwa namba ya kiroho
baadaye paulo akawa muumini mzuri wa bwana yesu akabatizwa na anania kisha mmisionari mkuu kwa vile mara nyingi alisafiri sana katika nchi za ng'ambo na kuunda makanisa mengi wakati wa safari tatu korinto filipi tesalonike efaso galatia kolosai na kadhalika
kazi ya mtakatifu mtume paulo ilikuwa ngumu kwa kuwa mara nyingi alipokuwa safarini alipata mateso mengi kwa ajili ya bwana
mara kadhaa alitupiwa mawe akafungwa gerezani akavumilia baridi kali njaa kiu na hata mara nyingi alikokotwa na mawimbi ya baharini
alipata faraja ya kiroho alipochukuliwa juu hadi uwingu wa tatu mwishowe alikamatwa na kufungwa gerezani kwa kuwa kwa amri ya kaisari nero aliuawa na kukatwa kichwa
hali ya utumishi katika kazi ya mungu iliyofanywa na mitume hawa petro na paulo haina budi kuwa kioo na mfano bora wa maisha yetu tuishi kwa kadri ya mapenzi yake tukijua bila msaada wa yesu kwetu hakuna ahueni
kwa nini tunahitaji msingi wa maadili (4)
tofauti za maoni juu ya mambo fulani fulani zisiwe sababu ya uhasama bali ziwafanye watu kutafakari pamoja ni katika kutafakari hivi pamoja ndio uchambuzi wa masuala kunaweza kufanyika pia mikakati na makubaliano bora kukabili masuala magumu
ndio kusema lazima kuwe na utaratibu wa uongozi mbalimbali kukutana mara kwa mara njia nyingine ni kwa kutoa maoni yao katika vyombo vya habari jambo linaloanza kujitokeza nchini tanzania sasa hivi
badala ya kukilaumu tu kitu kiitwacho 'serikali' ni bora zaidi kupendekeza utatuzi bora zaidi wa masuala
kunaweza kuwa na kongamano ili kuwapa fursa viongozi mbalimbali kutoa maoni yao juu ya mambo mengi muhimu sio tu juu ya siasa mikutano ya aina hii inakosekana ingawa hapo na pale imefanyika inatakiwa iratibiwe barabara
mathalani kungeweza kuundwa baraza la viongozi kwa minajili hivyo hilo lingekuwa juu ya vyama vya siasa mabaraza ya viongozi yangeweza kuundwa katika ngazi ya wilaya mkoa na taifa au pia katika viwango vya wanataaluma na wanataaluma mbalimbali kama madaktari waandishi wa habari wanasheria na kadhalika hao wangeunda vyama vyao huria (vyama huria vitazungumziwa zaidi katika kifungu kinachofuata)
mabaraza ya aina hiyo na vyama hivyo vingepewa uhuru na madaraka kuhakikisha kuwa mapendekezo yao haya na malengo ya kisiasa
vyama huria
kuna vyama huria vingi katika tanzania kama spotiutamaduni biashara haki za binadamu kina mama nk vingi zaidi vingeweza kuanzishwa katika mazingira yetu mapya kisiasa kwahitajika sana vyama kama vya biashara vya ushirika na wakulima vya wafanyakazi vya wazazi nk
kati ya dalili nzuri ni kuanzishwa vyama katika mwelekeo tunaozungumzia hapa itachukua muda kushamiri lakini matunda yake mema ni ya uhakika lazima tuhimize sana mwelekeo huo tena toka ngazi ya chini tunataka tuone kazi ya serikali ikiwa yakutegemeza juhudi za watu badala ya kutupangia vitu toka juu
kumbe vyama hivi havipingani na mwenye mamlaka hivi ni vikundi vya watu wenye mielekeo sawia na wenye mambo yale yale yanayowakera ni kwa kuvikubali vikundi kama hivyo na mambo inavyosimamia ndio siasa zinazoundwa nchini zitaihusisha jamii nzima hapa ndipo inapowezekana kupanga mambo kwa manufaa ya wote
mara nyingi watu hawaambiwi sheria gani zinatungwa au siasa gani zinabuniwa hivyo ni kuwanyima haki yao lazima watu wahusishwe na maamuzi yanayogusa maisha yao na watoe maoni yao
usipotafuta kujua maoni ya watu kabla ya kufanya maamuzi yanayowagusa utapata matatizo baadaye kama mgomo suala la ardhi huko monduli ni mfano mmoja kufanya mambo kirisiri katika mambo yahusuyo jumuia nzima ni dalili za udhaifu
tuchukue kwa mfano matatizo yaliyojitokeza mashuleni kama kungekuwepo na vyama vya waalimu na wazazi utatuzi wa mambo ungewezekana kabisa badala ya mikasa iliyotokea hapo hoja za wahusika zingeangaliwa kwa makini zaidi
kutilia maanani mapendeleo na mapendekezo ya watu ni njia bora ya kuimarisha jamii na kielelezo cha utungaji sheria na kanuni hivi tofuati zilizopo nchini lazima zisiwe tushio bali huchangia uboreshaji wa maisha ya jamii
wengi huchukulia tofauti kuwa tishio kwa vyovyote ni lazima kuhakikisha kwamba hakuna kikundi kimoja kugandamiza vingine
kadiri mambo yalivyo sasa ni vikundi vya biashara ndiyo vyenye uwezo zaidi na kujitetea vyenyewe kuliko walimu au walaji
hui sio mwelekeo bora
tofauti za dini hazipewi makini unaotakiwa ili zisisababishe uhasama katika ya waumini hata kuhatarisha amani
tusijaribu kulikwepa suala hili kama wanataaluma wakristo lazima tutoe mchango wetu wa mawazo au tuwaalike wanataaluma wa dini tofauti nao wafanye vilevile pamija tuweke msingi unaotakikana katika jamii yetu ya kitanzania
hapa chini tunazichambua tofauti zetu za kidini na jinsi tunavyoweza kuziishi bila matata
3 uwingi wa dini na athari zake kijamii na kisiasa
tunaishi katika jamii yenye dini mbalimbali na tofauti hivyo ni wazi athari zake zitaonekana katika nyanja za kisiasa
pengine masuala nyeti ya kidini hujitokeza na mungu bariki yakapita bila kuharibu amani ila haitoshi kuridhika na kutoharibika amani lazima tuchambuue tofauti zetu kidini makundi makumbwa ndio wakristu waislam wafuasi wa dini za jadi na yapo makundi madogo madogo kama wahindu
makundi hayo makubwa ya dini nayo yamegawanyika yenyewe wapo wakristu wa madhehebu mbalimbali yenye mitazamo tofauti kadhalika waislamu nao wamegawanyika hivi vitendo vya kundi fulani la wakristu au waislamu haviwezi moja kwa moja kueleweka kuwa vitendo vya wakristo au waislamu wote
hivi tuanze kuelewana kwanza na wale walio karibu zaidi nasi
hata hivi tukubali kwamba sio kila mtu atajiunga na mazungumzo ya maelewano kati ya dini tofauti tusiwakubali wale wenye lengo la kuendeleza maslahi yao huku wakiharibu maelewano wakijidai kuwakilisha dini fulani vikundi vya kikristu au vya kiislamu vinavyoelekea kuvigandamiza vingine haviwakilishi ukristu uislamu au dini za jadi kupuuza tofauti zetu ni kujipambaza wenyewe tusidhani kwamba athari za dhambi hazigusi tabia na maoni ya dini yetu
mathalani tunaelewa nini na dhana kama haki uhuru demokrasia dhamiri tuna maoni tofauti hapa na ni vema tusipuuze neno hilo
tena sio tofauti kati ya wakristo na waislamu hata kati ya wakristo mathalani wakatoliki na walokole wana maoni tofauti juu ya dhana hizo za msingi
hivi zipo tofauti kati ya wakristo na wafuasi wa dini za kijadi kama wasuni na washiha kati ya waislamu
wapo wale wanaodadisi kwamba hapa tanzania siasa haina dini au katika ngazi ya mitaa na vijiji hakuna shida kusema hivi ni kukosa kina katika kuyaelewa maisha ya jamii
jamii yahitaji kukubaliana katika yale tunayoyapa thamani ili kubuni siasa za kujenga tusipokuwa na msingi wa pamoja wa maadili tutawezaje kubuni siasa bora ya elimu ya familia au kutoa miongozi ya maadili ya waandishi wa habari wanataaluma au wanajeshi ikiwa dini zetu tofauti zina namna tofauti ya kuelewa dhana za msingi kama demokrasia na uhuru wa dini tutawezaje kukubaliana kuheshimiana kweli pasipo kukaa pamoja na kujadiliana
uzoefu watufundisha wazi kwamba amani katika taifa letu itakuwa ndoto pasipokuwepo na amani kati ya dini mbalimbali pasipo majadiliano hapawezi kuwa na amani kati ya dini zetu mbalimbali
majadiliano hayatawezekana tusipokubali kuwapokea na kuwaheshimu wenzetu wa dini tofauti wawe wakristu waislamu au wafuasi wa dini za jadi tusipotambua kuwa mungu yuko kati ya wengine na kwamba nao hushika dini yao kwa moyo hatuwezi kuheshimiana
bila kutakiana mema na kuvumiliana hakuna uwezekano wa kuwepo na mawasiliano ya kina tunalazimika kuishi kwa kujihami hapo jamii inakosa maelewano ya kweli na kuishi maadili ya nipe nikupe badala ya kuaminiana na kutenda pamoja kwa manufaa ya wote
hii ina maana kwamba lazima tujifunze kuwaeleza watu wengine tofauti zilizopo kati yetu nao katika lugha wanayoielewa lazima tuepuke lugha ya majigambo au mantiki ya 'jahad' kuwashinda wengine kwa mabavu mapesa au kwa kutumia jeuri
wapo watakaodai kwamba wakristu waislamu na wafuasi wa dini ya jadi ni awali ya yote watanzania ni kweli tunao umoja hapa tunaweza kujenga jamii juu yake
ila lazima tukiri pia kwamba tunazo tofauti kati yetu zinazotungwa imani za dini hukua na kuharibu tabia na mitazamo yetu kijamii na kisiasa kupuuza tofauti hizi ni kufanya mambo juu juu
tuendeleze udadisi huu kwa kuangalia mifano miwili uhuru wa dini na mtazamo wa imani za kidini mintarafu haki za binadamu athari zake kwa siasa ni wazi
uhuru wa dini na uhuru wa dhamira
ukristo na uislamu kila imani moja hufundisha kwamba zinashika ukweli wote hivi wale wanaofuata imani tofauti ni kuishi katika makosa ya imani au kwa vyovyote kupungukiwa na ufunuo
kumekuwa na mang'amuzi mapya kati ya wakatoliki katika kuelewa mafundisho ya uhuru wa dini na uhuru wa dhamiri
kabla ya mtaguso wa pili wa vatikano (19621965)kanisa katoliki kimsingi lilifundisha kwamba ukweli tu ndio ulikuwa na haki ya kuzingatiwa kosa lingeweza kuvumilika tu katika mazingira fulani fulani kama pale tokeo jema zaidi lilipotarajiwa kama kutarajia lingetunza amani katika taifa
baada ya mtaguso wa vatikano ii kanisa katoliki limekubali kwamba uhuru wa dhamiri na uhuru wa dini ni haki ya mwanadamu watu wanao uhuru wa kufuata dini yoyote ikiwa wanatafuta ukweli kwa dhati na wapo wazi kupokea maongozi ya mungu
waislamu hawakubali msimamo huo mpya wa kanisa katoliki
hao wapo tayari kuwapa uhuru na haki watu wa dini za kitabu (wayahudi wakristu wazoroa striani) katika nchi za kiislamu hao hulindwa lakini wanawezekana mipaka na pengine hata wanatanguliwa mathalani muislamu anaweza kumwona mkristu lakini sio mkristo kumwoa muislamu kumwingiza muislamu dini nyingine ni marufuku
ziwa orra sehemu ya 'utakaso' kwa waethiopia
na masha otieno jr
mwendo wa masafa mafupi kutoka jiji la addis ababa mji mkuu wa ethiopia unalifikia ziwa mashuhuri kabisa la orra arsedi
ukilitazama kama mandhari ya kawaida ni kweli laonekana kuwa ziwa zuri la kuvutia hasa kwa maumbile yake ya asili na maji yake matulivu kwako kama mtalii ziwa hili lina maana ya maumbile ya asili tu aliyoyaumba mwenyezi mungu na wala si zaidi ya hapo
lakini hivyo sivyo ziwa orra arsedi lilivyo kwa dini ya oromo inayokusanya kabila la wa oromo ambalo ni mojawapo kati ya makabila makubwa kabisa nchini ethiopia
wa oromo ambao kwa asili ni wafugaji na wafanyabiashara wanaamini kuwa ziwa orra ni la utakaso na pia ndilo chimbuko la jinsia mbili za binadamu zilizopo leo juu ya uso wa dunia wakimaanisha mume na mke
dini ya oromo kulingana na kumbukumbu za wanahistoria imekuwepo yapata miaka 1000 kabla ya kuzaliwa kristo
profesa thomas vilatman ni mtaalamu wa elimu ya sayansi ya jamii katika khuo kikuu cha addis ababa yeye anayo yafuatayo ya kusema kuihusu dini ya waoromo
waoromo wanaamini dini yao ni dini ya mungu mmoja isipokuwa ina mambo yafananayo na uislamu na uyahudi
waoromo huja kwenye ziwa orra ili kujitakasa katika kipindi cha mwisho wa mwaka na kile cha mwanzo wa mwaka waoromo hujitakasa kwa kuoga ziwani kitendo wanachoamini kuwa kinasafisha dhambi zao na kuwawezesha kupata nguvu za uzazi
lakini si waoromo peke yao waliotambika kwenye ziwa hili jarida la africa now toleo la agosti mwaka 1982 lilichapisha makala kuhusu viongozi wa mataifa ya kiafrika na imani za uchawi ambapo ndani ya makala hiyo ilielezwa kuwa aliyekuwa mfalme wa ethiopia na mwanzilishi wa umoja wa nchi huru za kiafrika hayati haille sellasie zama za utawala wake alipata kufukia kichwa cha binadamu kwenye ufukwe wa ziwa hilo la utakaso ili kujikinga kwa imani ya ushirikiana kulinda dola yake
haille sellasie pamoja na jitihada hizo zote baadaye alipinduliwa na kuondolewa madarakani alitawala kwa mkono wa chuma akiacha uchumi wa ethiopia ukiwa taabani wananchi wakidhoofu kwa njaa na kukata tamaa ya maisha
miaka mingi baada ya kufa haille sellasie dini ya waoromo ingali ikiendelea kwa kasi huku wakiendelea kujitakasa kama kawaida yao kwa kuoga maji ya ziwa orra
waoromo wanaamini kuwa mungu aliumba kwa siku 2 baadaye aliibuka kiumbe mtakatifu aitwaye ora kutoka ndani ya ziwa la utakaso kiumbe huyo baada ya kuibuka ndani ya maji akagawanyika sehemu mbili sehemu moja ikawa mwanamke na sehemu nyingine ikawa mwanaume waoromo wanaamini kiumbe huyo aliyeasisi jinsia mbili za binadamu aliibuka kutoka ziwani siku ya 21
waoromo pia wanaamini juu ya unajimu na nyota siku zote huabudu chini ya mkuyu wakiamini ndiyo sehemu ya ibada dini yao imewapelekea kujenga imani kuwa mungu husikia kilio zaidi akiitwa chini ya mti wa mkuyu
pamoja na kuamini yote hayo ipo imani iliyojengeka miongoni mwa jamii zingine za waethiopia kuwa waoromo ni wapagani wanaoamini juu ya dini za jadi na siyo mungu kama wanavyodai
waoromo binafsi wanazikanusha tshutuma hizo na wanadai kuwa hawako kama watu wanavyofikiri wala hawaamini dini ya jadi bali imani hiyo imekuja kwenye hisia za watu kwa sababu waoromo wanathamini sana uhai na mali za a sili kama mimea na wanyama hivyo wao wanajitetea kwa kudai wanaamini juu ya uwepo wa mungu mmoja muumba mbingu na nchi | 2017-07-26T06:30:33 | http://kiongozi.tripod.com/K2000/makalamachi5.htm |
(showing articles 33401 to 33420 of 37949)
09/11/180508 _makamu mkuu wa chuo
09/11/180510 _jafo aishukia manis
09/11/180514 _wananchi mkuranga
09/11/180520 _taasisi ya manjano
09/11/180536 _mahafali ya sekonda
09/11/181031 _ mwanafunzi chuo k
09/11/181034 _makamu wa rais amal
09/11/181745 _kamati ya maadili y
09/11/181751 _taarifa kwa umma k
09/11/181752 _waziri dkt kigwanga
09/11/181756 _waziri mkuu majaliw
09/11/181942 _faru wa serengeti k
09/11/181943 _wambura awaonya waa
09/11/182051 _queen mlozi awaomba
09/11/182053 _soma vichwa vya hab
09/12/180043 _emirates wajipanga
09/12/180251 _tawa yawakamatapok
09/12/180409 _dc kawawa apiga mar
09/12/180447 _serikali kukuza uch
09/12/180833 _rais dkt magufuli
older | 1 | | 1669 | 1670 | (page 1671) | 1672 | 1673 | | 1898 | newer
09/11/180508 makamu mkuu wa chuo kikuu ardhi azindua mafunzo ya vyuo vikuu 12 vya afrika kuhusu mbinu na namna ya kutathmini athari zitokanazo na maafa
09/11/180510 jafo aishukia manispaa ya ilala katika utekelezaji wa miradi
1 waziri wa nchi ofisi ya raistawala za mikoa na serikali za mitaa(tamisemi) selemani jafo akiwa na mkuu wa wilaya ya ilala sophia mjema katika eneo la machinjio ya vingunguti
waziri wa nchi ofisi ya raistawala za mikoa na serikali za mitaa(tamisemi) selemani jafo akifanya ukaguzi wa ujenzi wa miundombinu katika kituo cha afya mnyamani
1 waziri wa nchi ofisi ya raistawala za mikoa na serikali za mitaa(tamisemi) selemani jafo akipata maelezo ya ujenzi wa hospitali ya kivule inayo jengwa katika manispaa ya ilala
waziri wa nchi ofisi ya raistawala za mikoa na serikali za mitaa(tamisemi) selemani jafo akipata maelezo ya ujenzi wa hospitali ya kivule inayo jengwa katika manispaa ya ilala
wadau wa machinjio ya vingunguti wakitoa maoni yao wakati wa ujio wa waziri wa nchi ofisi ya raistawala za mikoa na serikali za mitaa(tamisemi) selemani jafo
waziri wa nchi ofisi ya raistawala za mikoa na serikali za mitaa(tamisemi) selemani jafo amechukizwa na kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya manispaa ya ilala
jafo ameonyeshwa kukerwa wakati alipokuwa katika ziara ya kikazi mkoani dar es salaam katika manispaa ya ilala katika ziara hiyo
waziri jafo ametembelea machinjio ya vingunguti ambayo hivi kalibuni ilitengewa fedha shilingi bilioni 8 kwa ajili ya kujenga machinjio ya kisiasa pia ametembelea kituo cha afya cha mnyamani ambacho kimepewa fedha shilingi milion 500 pamoja na ujenzi wa hospitali ya kivule
jafo ameonyeshwa kutofurahishwa na kusuasua kwa miradi hiyo kwani ujenzi wa machinjio ya vingunguti haujaanza hadi sasa licha ya kupokea fedha za awali zaidi ya shilingi bilion tatu zaidi ya miezi mitatu iliyopita
pia amebaini kasi ndogo ya ujenzi wa miundombinu katika kituo cha afya mnyamani licha ya kupokea fedha tangu mwanzoni mwa mwezi juni 2018 kutokana na hali hiyo
waziri jafo amemtaka mkurugenzi mpya wa manispaa hiyo jumanne shauri kubadilisha kasi ya utendaji katika manispaa hiyo ili fedha za serikali ziweze kuleta mabadiliko yanayokusudiwa katika manispaa hiyo
aidha waziri jafo amewashangaa viongozi na watendaji wa manispaa hiyo kwa kutotoa fedha zozote kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya kuvule kitendo kilichosababisha ujenzi huo kusimama kwa zaidi ya miaka miwili wakati manispaa hiyo imekusanya zaidi ya shilingi bilion 44 katika mwaka wa fedha 2017/2018 kutoka vyanzo vyake vya ndani
jafo ameelezea kwamba serikali kuu imetenga fedha shilingi bilioni 15 katika bajeti ya mwaka huu 2018/2019 kwa ajili ya hospitali hiyo ya kivule lakini ameitaka manispaa hiyo kuacha kubweteka kwa kutegemea fedha za serikali kuu pekee wakati manispaa hiyo ina uwezo mkubwa wa mapato
09/11/180514 wananchi mkuranga wanufaika na kilimo
na emmanuel massakaglobal ya jamii
wilaya ya mkuranga ni moja ya wilaya saba zilizopo mkoani pwaniambapo wakazi wake hujishughulisha sana na shughuli za kilimo ili kujipatia kipato
wilaya ya mkuranga inalima mazao mbalimbali ya biashara na ya chakula ikiwemo mihogombaazi korosho machungwa ufuta mananasi pamoja na nazi
akizungumza wilayani mkuranga mkoani pwani umri manage mkulima wa mihogo na bamia alisema kuwa kilimo kimemsaidia kwani ndio kinachoendesha maisha yakemimi nalima bamia linaniongezea kipato changu cha kila siku pia namsaidia mume wangu baadhi ya majukumualisema
manage alitoa wito kwa wanawake wote nchini kuacha kujibweteka na kuacha utegemezi masala yake wajishughulishe katika shughuli mbalimbali za maendeleo
mfanyabiashara na mkulima wa bamiaumri manage akizungumza na michuzi blog kuhusiana kilimowananchi wakivuna mihogo kama walivyokutwa na kamera yetu
wananchi wa wilaya ya mkuranga mkoa wa pwani wakivuna mihogo kama walivyokutwa na kamera yetupicha na emmaniel massaka wa global ya jamii)
09/11/180520 taasisi ya manjano foundation yatoa mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake wa kigoma
mafunzo hayo yalikuwa na lengo la kumsaidia mjasiriamali mwanamke kujikwamua na kujiongezea kipato awamu ya kwanza ni kumfundisha maswala ya biashara namna ya kuibua na kubuni miradi mbalimbali namna ya kuandika mpangilio wa biashara ikiwemo matumizi sahihi ya rasilimali muda kutokufuja fedha na pia namna ya kujitunzia akiba itokanayo na biashara yake awamu ya pili walipata ujuzi jinsi ya kupamba ma harusi na matumizi sahihi ya vipodozi salama vya luvtouch manjano
baada ya wanawake hawa kuhitimu mafunzo haya taasisi ya manjano foundation itawaunganisha na taasisi za fedha zinazotoa mikopo bila riba ili waweze kupata mtaji wa kununua bidhaa za vipodozi kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha biashara zao wakiwa chini ya uangalizi maalum wa taasisi hiyo kwa lengo la kuhakikisha kila mhitimu wa mafunzo haya anapiga hatua na kuweza kujitegemea taasisi ya manjano imefanikiwa kuwawezesha zaidi ya wanawake 500 kutoka mikoa ya dar es salaam mwanza arusha dodoma mbeya mtwara kigoma na unguja zanzibar
wengi wa wahitimu wa mradi wa manjano dreammakers wamefanikiwa kuanzisha biashara zao na kuwa mawakala wa bidhaa za luvtouch manjano kwa mwaka huu taasisi ya manjano wanajipanga pia kumalizia kwa kuwawezesha kiuchumi na kutengeneza ajira kwa vijana wa kike na wanawake wa mkoa wa tabora
09/11/180536 mahafali ya sekondari ya john baptist yafana
09/11/181031 mwanafunzi chuo kikuu iringa ashinda milioni 2394 za mbet
09/11/181034 makamu wa rais amalizia ziara yake wilaya ya buhigwe mkoani kigoma
09/11/181745 kamati ya maadili ya taifa yaitaka chadema kutekeleza maamuzi yaliyotolewa na kamati ya maadili jimbo la ukonga
09/11/181751 taarifa kwa umma kuhusu takwimu za deni la serikali kwa benki kuu ya tanzania
09/11/181752 waziri dkt kigwangalla aruhusiwa kutoka hospitali
09/11/181756 waziri mkuu majaliwa afungua mkutano wa tano wa wadau wa lishe atahadharisha ulaji usiofaa
09/11/181942 faru wa serengeti kulindwa kwa vifaa maalumu
09/11/181943 wambura awaonya waamuzi ligi kuendelea wikiendi hii
09/11/182051 queen mlozi awaomba wapiga kura kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo
pichani kulia katibu mkuu uwt queen mlozi akimuombea kura mgombea wa udiwani kwa tiketi ya ccm katika kata ya kizota mkoani dodoma ndugu jamal paul katika kampeni hizo ndugu mlozi amewaomba wakazi wa kata hiyo kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi wakati wa kupiga kura na kumchagua kiongozi atakae wafaa na kuwaletea maendeleo ya kweli na si maneno matupu
katibu mkuu uwt queen mlozi akiagana na mbunge wa dodoma mjini mh antony mavunde mara baada ya mkutano wa kumnadi mgombea wa udiwani kwa tiketi ya chama cha mapinduzi (ccm) katika kata ya kizotauliofanyika jana
09/11/182053 soma vichwa vya habari magazeti ya leo jumatano septemba 122018
09/12/180043 emirates wajipanga kutoa huduma bora kwa wateja
09/12/180251 tawa yawakamatapokonya baiskeli 60 nyaya 100 za majangiri
09/12/180409 dc kawawa apiga marufuku wanaoshiri kukaribisha mifugo kiholela
09/12/180447 serikali kukuza uchumi kwa kudhibiti fedha za ziada katika mzunguko
09/12/180833 rais dkt magufuli amuapisha mkurugenzi mkuu wa takukuru katibu mkuu wa wizara ya afya pamoja na balozi mmoja ikulu ya chamwino jijini dodoma | 2019-12-13T17:18:25 | http://jiachie1.rssing.com/chan-7007640/all_p1671.html |
lenzi ya michezo msimamo wa ligi daraja la kwanza kwa makundi yote jinsi ulivyo sasa
msimamo wa ligi daraja la kwanza kwa makundi yote jinsi ulivyo sasa
1 ashanti united 9 5 3 1 13 5 8 18
2 kiluvya united 9 4 4 1 9 4 5 16
3 friends rangers 9 3 5 1 9 4 5 14
4 africa lyon 9 4 2 3 10 6 4 14
5 kmc fc 9 3 3 3 6 8 2 12
6 polisi dar 9 2 5 2 5 6 1 11
7 mji mkuu 9 2 2 5 7 12 5 8
8 polisi dodoma 9 1 0 8 4 18 14 3
1 ruvu shooting 9 7 1 1 21 5 16 22
2 njombe mji 9 5 1 3 10 8 2 16
3 kurugenzi fc 9 4 2 3 10 9 1 14
4 jkt mlale 9 3 4 2 10 7 3 13
5 polisi morogoro 9 3 2 4 8 11 3 11
6 lipuli fc 9 2 4 3 6 11 5 10
7 kimondo fc 9 3 1 5 5 12 7 10
8 burkinafaso fc 9 0 3 6 6 13 7 3
1 geita gold fc 9 5 3 1 14 4 10 18
2 jkt oljoro 9 5 3 1 9 7 2 18
3 polisi tabora 9 5 2 2 12 4 8 17
4 panone fc 9 3 2 4 10 8 2 11
5 mbao fc 9 3 2 4 9 16 7 11
6 rhino rangers 9 1 6 2 4 7 3 9
7 polisi mara 9 1 5 3 6 9 3 8
8 jkt kanembwa 9 0 3 6 4 13 9 3 | 2017-10-20T17:54:22 | http://pallangyor.blogspot.com/2016/01/msimamo-wa-ligi-daraja-la-kwanza-kwa.html |
soma katika chinese cantonese (simplified) kiajemi kibikoli kichewa kichina (kikantoni) kichina (kilicho rahisi) kichina (cha kitamaduni) kidachi kidenishi kiewe kiga kihiligaynoni kihungaria kiigbo kiingereza kiitaliano kijerumani kikorea kikreoli cha haiti kikwechua (cha bolivia) kilithuania kimalagasi kimyanmar kiosetia kipolishi kireno kirumania kisamoa kishona kisilozi kislovaki kislovenia kisranantongo kiswahili kitsonga kitswana kituruki kiukrania kiurdu
yehova anataka uwe na shangwe (zab 1002) ukiwa mmoja wa watumishi wake inaelekea wewe pia una shughuli nyingi sana labda hukuwa na shughuli nyingi hivyo kabla hujaweka maisha yako wakfu kwa mungu lakini sasa huenda madaraka ya kimwili na ya kiroho yakakufanya uhisi umelemewa huenda hata ukahisi kwamba una hatia unapokosa kutimiza mambo yote uliyopanga kutimiza unaweza kupata jinsi gani usawaziko unaofaa na kuendelea kuwa na shangwe ya yehovaneh 810
unaishi katika nyakati za hatari na hivyo unakabili mikazo mingi basi unahitaji kuwa na ratiba nzuri kuhusiana na hilo shauri hili la mtume paulo lililoongozwa na roho ya mungu linafaa sana endeleeni kuangalia sana kwamba jinsi mnavyotembea si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima mkijinunulia wakati unaofaa kwa sababu siku hizi ni zenye uovuefe 515 16
kupatana na shauri hilo lenye hekima unaweza kupanga jinsi gani miradi unayoweza kutimiza na kusawazisha funzo la kibinafsi daraka la kuitunza familia utumishi wa shambani kazi ya kimwili na shughuli nyingine za lazima
je unakumbuka shangwe uliyokuwa nayo ulipojiweka wakfu kwa mungu na kubatizwa ulikuwa na shangwe kwa sababu ulipata ujuzi kumhusu yehova na makusudi yake huenda ulijifunza kwa bidii kwa miezi mingi na hivyo ukapata shangwe na uelewaji huo bila shaka jitihada hizo zote hazikuwa za bure funzo hilo lilibadili maisha yako na kuyaboresha
ili uendelee kuwa na shangwe unahitaji kuendelea kujilisha kiroho ikiwa unajikaza sana ili upate wakati wa kusoma na kujifunza biblia chunguza ratiba yako kujifunza na kutafakari hata kwa dakika chache tu kila siku kutakusaidia kuwa na uhusiano wa karibu zaidi pamoja na yehova na bila shaka utapata shangwe nyingi
watumishi wengi wa mungu wanaweza kununua wakati fulani wanaotumia kwa ajili ya mambo yasiyo ya maana sana na kuutumia kufanya mambo ya maana jiulize ninatumia wakati mwingi kadiri gani kusoma magazeti ya kilimwengu kutazama televisheni kusikiliza muziki au kufuatia burudani fulani ninayopenda mambo hayo yanaweza kufurahisha ikiwa tu yanafanywa kwa usawaziko (1 tim 48) ukitambua kwamba una tatizo la kupanga wakati wako vizuri rekebisha ratiba yako
adam ambaye ni mume baba mwenye watoto watatu na mzee wa kutaniko anaeleza kinachomsaidia ninajitahidi kuishi maisha rahisi ninaepuka burudani na vitu vya kimwili vinavyohitaji wakati mwingi si kwamba ninaishi maisha ya kujinyima lakini ninafurahia tu burudani ya kawaida
kutafakari kuhusu matokeo mazuri ya maamuzi yako kunaweza kukusaidia kupata tena shangwe yako na kuendelea kuwa na mtazamo mzuri kwa mfano mariusz mzee wa kutaniko mwenye watoto watatu anasema hivi nilipoanza kujifunza biblia nilianza kuwa na mtazamo mzuri kuhusu wakati ujao bado ninakabili matatizo mara kwa mara na ni yehova tu anayejua mengi ya matatizo hayo lakini kwa sababu ya utegemezo wake ninatazamia wakati ujao nikiwa na shangwe
kama kisa cha mariusz kinavyoonyesha kuwa na mtazamo mzuri hakutaondoa mahangaiko yote lakini mtazamo mzuri unaweza kukusaidia ujihisi vizuri na upambane vizuri zaidi na matatizo ya maisha tunasoma hivi siku zote za mwenye kuteseka ni mbaya lakini mtu aliye mchangamfu moyoni huwa na karamu sikuzote (met 1515) tafakari pia kuhusu upendo ambao tayari mungu amekuonyesha kutafakari kuhusu upendo huo kunaweza kujenga upendo wako kwa mungu na kuongeza shangwe yako ya kimungumt 2237
kumtanguliza yehova na mambo ya kiroho maishani kunaongeza shangwe katika familia kuonyesha sifa za kikristo kunapunguza matatizo ya kutoelewana na kunaisaidia familia kuwa na uhusiano wa karibu zaidi na wenye kupendeza zaidi hivyo familia yote itafurahia hali ya umoja na nyumba yenu itakuwa na amani ya kwelizab 1331
kushiriki katika utendaji wa kiroho mkiwa familia kunaleta shangwe nyingi ya kweli mariusz anaeleza hivi ninathamini sana wakati tunaotumia pamoja tukiwa familia mke wangu ananiunga mkono kabisa inapowezekana anaambatana nami katika huduma ya shambani au ninaposafisha uwanja kabla ya makusanyiko na pia anaambatana nami ninapoenda kutoa hotuba za watu wote katika makutaniko mengine jambo hilo linanitia moyo
maandiko yanawaamuru wakristo waandalie familia zao mahitaji ya kimwili (1 tim 58) lakini ikiwa kazi ya kimwili inachukua nguvu na wakati mwingi sana inaweza kukufanya upoteze shangwe katika utumishi wa mungu sali kwa yehova kuhusu jambo hilo (zab 5522) wakristo fulani wameamua kwamba ili watangulize ufalme wa mungu wanahitaji kutafuta kazi nyingine hakuna mkristo anayepaswa kuruhusu faida za kifedha anazopata kwa kufanya kazi inayohitaji nguvu na wakati mwingi sana zimzuie kufuatilia mambo ya kiroho ambayo ni ya maana zaidimet 223
unaweza kunufaika ukiandika faida na hasara zote za kazi yako ya sasa au kazi unayofikiria kuanza bila shaka ungependa kupata mshahara mzuri na kazi yenye kuridhisha hata hivyo je kazi yako ya sasa inakusaidia kujenga hali ya kiroho ya familia yako chunguza kwa uzito mambo yote na ufanye maamuzi ambayo yanaonyesha kwamba unatanguliza uhusiano wako pamoja na yehova
ikiwa kazi yako ya sasa inakuzuia kukua kiroho unahitaji kurekebisha hali zako wakristo wengi wamefanya mabadiliko makubwa ili wapate wakati wa mambo ya kiroho ndugu mmoja huko poland anasema hivi pindi moja sikuwa na jambo lingine la kufanya ila kuacha kazi katika kampuni moja kwa kuwa mara nyingi nilisafiri kwa sababu za kibiashara sikuwa na wakati wa kutosha kushughulikia ipasavyo mambo ya kiroho au kuitunza familia yangu sasa anapata riziki kwa kufanya kazi ambayo haihitaji nguvu na wakati wake mwingi sana
pata shangwe kwa kuwasaidia wengine
yesu alisema kwamba kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea (mdo 2035) wakristo wana nafasi nyingi za kutoa kwa njia hiyo nyakati nyingine ili upate shangwe na kumletea mtu mwingine shangwe unahitaji tu kutabasamu kwa uchangamfu kumsalimu kwa mkono au kumshukuru kutoka moyoni kwa sababu ya jitihada anazofanya katika mgawo wake wa kiroho
mtume paulo aliwatia moyo hivi wakristo wenzake semeni kwa kuzifariji nafsi zilizohuzunika tegemezeni walio dhaifu (1 the 514) watu waliohuzunika wanaweza kuhisi kwamba hawawezi kukabiliana na matatizo kwa nguvu zao wenyewe je unaweza kuwasaidia watu kama hao ukiona kwamba mmoja wa ndugu zako anapoteza shangwe yake katika utumishi wa yehova jitahidi kumtia moyo kufanya hivyo kutakutia moyo pia matatizo fulani hayawezi kutatuliwa na mwanadamu yeyote hata hivyo unaweza kumhurumia kutoka moyoni ndugu yako na kumhimiza ategemee msaada wa yehova ambao haushindwi kamwe wale wanaomtegemea hawatakata tamaa kamwezab 2710 isa 591
hatua nyingine inayofaa ni kumwalika yule ambaye anaonekana hana shangwe ahubiri pamoja nawe yesu alipowatuma wale wanafunzi 70 aliwatuma wawiliwawili (luka 101) je huamini kwamba kwa kufanya hivyo alituandalia njia ya kutiana moyo je unaweza kuiga kielelezo hicho leo kwa kuwasaidia wakristo wengine wapate tena shangwe
leo kuna mambo mengi ambayo yanaweza kutufanya tuhangaike hata hivyo paulo anatuhimiza hivi shangilieni sikuzote katika bwana mara nyingine tena nitasema shangilieni (flp 44) kwa sababu unampenda mungu unamtii na unavumilia unapoendelea kufanya kwa bidii kazi ambayo amekupa maisha yako yana kusudi hilo linakuletea shangwe na zaidi ya hayo yehova anakusaidia kushughulika na mikazo na matatizo ambayo unakabilirom 26 7
kwa macho ya imani tunatambua jinsi tulivyo karibu sana kuingia katika ulimwengu mpya ambao yehova anaahidi ulimwengu huo mpya utatuletea baraka na sababu nyingi kama nini za kushangilia (zab 3734) kwa hiyo tunaweza kushangilia na kuendelea kukazia fikira jinsi yehova anavyotubariki sana hata sasa hivyo tunaweza kumtumikia yehova kwa kushangiliazab 1002
[mchoro katika ukurasa wa 8]
huenda ukahitaji kurekebisha ratiba yako ili uendelee kuwa na shangwe
burudani na tafrija
kuitunza nyumba na familia
mikutano ya kikristo
je unaweza kuwasaidia wengine kupata tena shangwe | 2020-02-28T20:49:03 | https://www.jw.org/sw/maktaba/magazeti/w20091215/Kumtumikia-Mungu-kwa-Bidii-na-Shangwe/ |
official black n white @bla_official instagram profile mulpix
volkswagen vw volkswagenim tã¼rkiye هاوڕێ köy kalıcıdudak kıltekniği permanentmakeup 펄러비즈 펄비즈 비즈 folding bike bicycle 백현 exo baekhyun baekhyunee long arm 4 link drawing skull art artist cage cf kyokushin kuwait hago cafe love vc eu sempre amo volare ordinarilyunique lifestyle meninos lindos e repost برياني الدياي siku ya chunusi hips p tomo smk 974 sexy fashionhijab hijabootdindo hijab hijabers dunia al عماني bait グッジョバ uniqlo ユニジョ uniqloginza
bla_official instagram photos and videos
bla_official official black n white @bla_official mentions
tuacheee ujinga na kudanganyanaaa tuacheee ujinga na kudanganyanaaa
bla_official
black n white black n white
hdlloh hdlloh
hatasielewiii ilikuwajeee uyu jamaaa naona black n white yuu hatasielewiii ilikuwajeee uyu jamaaa
naona black n white yuu
mwisho wa mchezo ndio hapa haraka zote zinakwishaaaa mwisho wa mchezo ndio hapa haraka zote zinakwishaaaa
kama unaweza unaweza tu kama unaweza unaweza tu
somo kwa wanawake mume darling nina kikao mkoani kesho naomba niandalie vitu please mke dada zile nguo za baba pamoja na soksi ulifua dadandio nimepanga kabatini mama anarudi chumbani na kumuomba hubby wakacheki tv sebulen lakini baada ya muda mama anamuita dada akapange suruali somo kwa wanawake
mume darling nina kikao mkoani kesho naomba niandalie vitu please
mke dada zile nguo za baba pamoja na soksi ulifua
dadandio nimepanga kabatini mama anarudi chumbani na kumuomba hubby wakacheki tv sebulen lakini baada ya muda mama anamuita dada akapange suruali kadhaa na mashati kwa ajili ya safari ya kesho dada anapanga kila kitu anatoka
mke kama tayari hakikisha unarekebisha yale mashuka pale kitandani weka na maji bafuni dada anafanya na kwenda zake kulala asubuhi dada anaamka mapema na kuandaa kila kitu ikiwemo na chai baba anakunywa chai na kutaka kuondoka
mke dada msindikize baba ili ufunge geti sababu bado ni giza😂
dada sawa mama dada anatoka na begi la baba hadi nje kwavile mkewe yupo ndani baba anamtaka dada abaki vizuri na watoto dada anaitika na kusema nawao wanamuombea safari njema baada ya muda baba anarudi toka safari
mke huku akitabasamu dada si umemuona baba amerudi vipi chakula tayari
dada ndio
mke haya kapange meza vizuri mimi naandaa juice baada ya muda wanakula na baba anagundua juice sio nzuri anaamua kuiacha na kusema leo wamesahau kuweka baadhi ya vitu hivyo hataweza kuinywa
baadae baba anakumbuka kuwa aliacha boxer zake kwenye ndoo ya maji chumban na kufunika mfuniko anamuuliza mama vipi zile nguo zangu kwenye ndoo zilifuliwa maana nilisahau kusema kama zina maji
mke dada njoo hapa hivi zile nguo za baba chumbani ulifua
dada ndio mama lakini hasemi kama alianua na kuweka chumbani kwake akidhani atakunja baada ya kazi kupungua
mke darling zilifuliwa
mume na watoto vipi wameshalala
mke anajibu wamelala darling
mume vipi dereva wao alifika kuchukua pesa yake
mkedada eti uncle hassan amechukua pesa yake
dadahapana wamembadilishia gari uncle hassan amesafiri kwa muda
mketutampatia darling siku akirudi acha dada aendelee kuitunza
mume basi vizuri ehee vipi na tution walienda leo
mke ndio walienda anamgeukia dada si eti ee walienda si eti
dadahapana kelvin anaumwa leo siku ya pili nilinunua dawa dukan nimempa lkn hajambo
mkeanashangaa hee mtoto mgumu huyu kumbe jana alikua mgonjwa halafu wala alikua anacheza tu jamani watotoasante dada umefanya vizuri
mume haya
hawa jamaaa wanaweza wakakungawa vipande viwili hawa jamaaa wanaweza wakakungawa vipande viwili
usiombe ukawa na gunduuu usiombe ukawa na gunduuu | 2020-01-29T06:17:23 | https://mulpix.com/bla_official |
je ni desturi ngapi za kidini unazozizingatia ni mara ngapi wewe umeasi dhidi ya neno la mungu na kwenda kwa njia yako mwenyewe ni mara ngapi wewe umetia katika vitendo neno la mungu kwa sababu wewe kwa kweli unajali mizigo aliyobeba na unatafuta kutimiza mapenzi yake lielewe neno la mungu na uliweke katika vitendo kuwa mwenye maadili katika vitendo na matendo yako huku si kutii sheria au kufanya hivyo shingo upande kwa ajili ya kujionyesha badala yake haya ni kutenda ukweli na kuishi kulingana na neno la mungu kutenda kama huku pekee ndiko hutosheleza mungu desturi yoyote inayompendeza mungu si kanuni bali ni kutenda ukweli baadhi ya watu wana upendeleo wa kujivutia nadhari mbele ya kaka na dada zake katika kristo anasema yeye ni mdeni wa mungu lakini akiwapa kisogo yeye hatii katika vitendo ukweli ila anafanya tofauti kabisa je hii si ni kama wale mafarisayo wa dini mtu ambaye anampenda mungu kwa kweli na ana ukweli ni yule ambaye ni mwaminifu kwa mungu lakini bila ya kufichua kwa nje yeye yuko tayari kutia katika vitendo ukweli wakati mambo yanapotokea wala hasemi au kutenda kinyume cha dhamiri yake anaonyesha hekima wakati mambo yanapotokea na ni mwenye maadili katika matendo yake bila kujali mazingira mtu kama huyu ni mtu ambaye anahudumu kwa kweli kuna baadhi ya watu ambao mara nyingi shukrani zao kwa kuwa wadeni wa mungu ni kwa mdomo tu siku zao huisha wakiwa na nyuso za wasiwasi kukaa katika hali isiyo halisi na kuvalia uso bandia wa mnyonge aibu gani hii na kama ungemuuliza ni kwa njia zipi wewe ni mdeni wa mungu tafadhali niambie hangeweza kutamka lolote kama wewe ni mwaminifu kwa mungu basi usizungumze kuhusu uaminifu wako kwa umma bali tumia matendo yako halisi ili kuonyesha upendo wako kwa mungu na kumwomba kwa moyo wa kweli wale wanaotumia maneno pekee kushughulika na mungu ni wanafiki wote baadhi yao husema kuwa wao ni wadeni kwa mungu katika kila sala na kuanza kulia wakati wanasali hata bila uwepo wa roho mtakatifu watu kama hawa wamepagawa na mila na desturi za kidini na fikra wanaishi na mila hizo na fikra kama hizo daima wakiamini kwamba hatua kama hiyo humpendeza mungu na kwamba kumfuata mungu kijuujuu au machozi ya huzuni ndivyo humpendeza mungu ni kitu kipi kizuri kinachoweza kutoka kwa watu kama hao wa kushangaza ili kuonyesha unyenyekevu wao baadhi yao huonyesha neema bandia wakati wanazungumza mbele ya watu wengine baadhi yao kwa maksudi hujitoa wakati wowote kwa utumishi mbele ya watu wengine kama mwanakondoo asiye na nguvu yoyote je hii ni namna ya watu wa ufalme mtu wa ufalme sharti awe wa kusisimua na aliye huru asiye na hatia na aliye na uwazi mwaminifu na wa kupendeza mtu aishiye katika hali ya uhuru ana tabia za kiajabu na heshima na anaweza kuwa shahidi kokote aendako yeye ni mmoja wa wapenzi wa mungu na wanadamu wale ambao ni wanafunzi katika imani huwa na matendo mengi ya nje lazima kwanza wapitie kipindi cha ushughulikiaji na kuvunja wale ambao wana imani kwa mungu katika nyoyo zao hawawezi kutofautishwa na wengine kwa nje lakini vitendo na matendo yao ni ya kupongezwa kwa wengine watu wa aina hii pekee ndio wanaweza chukuliwa kuwa wanaishi kwa kudhihirisha neno la mungu ukihubiri injili kila siku kwa mtu huyu na yule ukiwaleta kwa wokovu ilhali mwishowe wewe bado unaishi katika sheria na mafundisho basi wewe huwezi kuleta utukufu kwa mungu namna hii ya watu ni watu wa dini na ni wanafiki mno kila mara watu wa kidini kama hao wanapokusanyika wanaulizana dada uko vipi siku hizi anajibu nahisi kuwa mimi ni mdeni wa mungu na siwezi kutosheleza matakwa ya moyo wake mwengine anasema mimi pia ni mdeni wa mungu na nimeshindwa kukidhi matakwa yake sentensi na maneno haya machache pekee yanaonyesha maovu yaliyo ndani ya nyoyo zao maneno kama hayo ni ya kuchukiza zaidi na yenye makosa sana asili ya watu kama hao inaleta upinzani kwa mungu wale ambao huzingatia ukweli halisi huwasilisha vilivyomo katika nyoyo zao na kufungua mioyo yao katika mawasiliano hakuna shughuli hata moja ya uongo hakuna heshima ama salamu na mazungumzo matupu wao huwa na uwazi na hawafuati sheria za duniani kuna wale ambao wako na upendeleo wa kujionyesha kwa nje hata bila maana yoyote wakati mwenziwe anaimba yeye anaanza kucheza bila hata kujua kuwa wali kwenye sufuria yake umeshaungua watu wa namna hii si wacha mungu au waheshimiwa bali ni watu wa kijinga kupindukia hizi zote ni dalili za ukosefu wa ukweli baadhi yao hukusanyika kuzungumza kuhusu mambo ya maisha katika roho na ingawa hawasemi kuhusu kuwa kwao wadeni wa mungu wao hubaki na upendo wa kweli kwa mungu ndani ya mioyo yao kuwa kwako mdeni kwa mungu hakuhusiani na watu wengine wewe ni mdeni kwa mungu si kwa mwanadamu kwa hiyo ina maana gani ya wewe daima kuzungumzia haya kwa watu wengine lazima uweke umuhimu kwa kuingia katika hali halisi si kwa bidii ya nje au maonyesho je matendo ya kijuujuu ya mwanadamu yanawakilisha nini hayo huwakilisha mwili na hata matendo yaliyo bora zaidi ya nje hayawakilishi maisha ila tabia yako tu mwenyewe matendo ya nje ya mwanadamu hayawezi kutimiza tamaa za mungu wewe daima huzungumza kuhusu udeni wako kwa mungu lakini huwezi kuyakidhi maisha ya wengine au kuwafanya wengine kumpenda mungu je unaamini kwamba matendo hayo yatamridhisha mungu unaamini kwamba hii ndiyo hamu ya moyo wa mungu kwamba haya ni ya roho lakini kwa kweli huu ni ujinga unaamini kwamba yale yanayokupendeza wewe na unayotaka ni yale yanayomfurahisha mungu je inawezekana kuwa unayoyataka wewe yanaweza kuwakilisha anayotaka mungu je tabia ya mwanadamu inaweza kumwakilisha mungu yale yanayokupendeza wewe ndiyo hasa yale humchukiza mungu na mienendo yako ni ile ambayo mungu huchukia na kukataa kama wewe unahisi kuwa u mdeni basi nenda na usali mbele za mungu hakuna haja ya kuyazungumzia mambo haya kwa watu wengine usipoomba mbele za mungu na badala yake mara kwa mara unavuta nadhari kwako wewe mwenyewe mbele ya wengine jambo hili linaweza kutimiza hamu ya moyo wa mungu kama matendo yako daima ni katika kuonekana tu hii ina maana kuwa wewe ni mtu bure zaidi ya wote ni mtu wa aina gani yule aliye na matendo mema ya kijuujuu tu lakini hana uhalisi watu kama hao ni wafarisayo wanafiki na watu wa dini msipoacha matendo yenu ya nje na hamuwezi kufanya mabadiliko basi mambo ya unafiki ndani yenu yatazidi kuimarika namna mambo ya unafiki yanavyozidi kuwa ndivyo upinzani kwa mungu unavyozidi na mwishowe aina hii ya watu hakika watatupiliwa mbali
je matendo ya kijuujuu ya mwanadamu yanawakilisha nini hayo huwakilisha mwili na hata matendo yaliyo bora zaidi ya nje hayawakilishi maisha ila tabia yako tu mwenyewe matendo ya nje ya mwanadamu hayawezi kutimiza tamaa za mungu wewe daima huzungumza kuhusu udeni wako kwa mungu lakini huwezi kuyakidhi maisha ya wengine au kuwafanya wengine kumpenda mungu je unaamini kwamba matendo hayo yatamridhisha mungu unaamini kwamba hii ndiyo hamu ya moyo wa mungu kwamba haya ni ya roho lakini kwa kweli huu ni ujinga unaamini kwamba yale yanayokupendeza wewe na unayotaka ni yale yanayomfurahisha mungu je inawezekana kuwa unayoyataka wewe yanaweza kuwakilisha anayotaka mungu je tabia ya mwanadamu inaweza kumwakilisha mungu yale yanayokupendeza wewe ndiyo hasa yale humchukiza mungu na mienendo yako ni ile ambayo mungu huchukia na kukataa kama wewe unahisi kuwa u mdeni basi nenda na usali mbele za mungu hakuna haja ya kuyazungumzia mambo haya kwa watu wengine usipoomba mbele za mungu na badala yake mara kwa mara unavuta nadhari kwako wewe mwenyewe mbele ya wengine jambo hili linaweza kutimiza hamu ya moyo wa mungu kama matendo yako daima ni katika kuonekana tu hii ina maana kuwa wewe ni mtu bure zaidi ya wote ni mtu wa aina gani yule aliye na matendo mema ya kijuujuu tu lakini hana uhalisi watu kama hao ni wafarisayo wanafiki na watu wa dini msipoacha matendo yenu ya nje na hamuwezi kufanya mabadiliko basi mambo ya unafiki ndani yenu yatazidi kuimarika namna mambo ya unafiki yanavyozidi kuwa ndivyo upinzani kwa mungu unavyozidi na mwishowe aina hii ya watu hakika watatupiliwa mbali | 2020-05-31T08:55:42 | https://sw.godfootsteps.org/recital-focus-on-reality-not-religius-rituals.html |
hahaha hapa ndio utajua utamu wa siasa sasa vijana inabidi wajifunze kitu katika katukio haya ya picha ili kupunguza mikumbo siasa ni upendo bwana tazama humu uone walichokuwa wakizungumza
home » unlabelled » hahaha hapa ndio utajua utamu wa siasa sasa vijana inabidi wajifunze kitu katika katukio haya ya picha ili kupunguza mikumbo siasa ni upendo bwana tazama humu uone walichokuwa wakizungumza
20150915t0221000700
artikel terkait hahaha hapa ndio utajua utamu wa siasa sasa vijana inabidi wajifunze kitu katika katukio haya ya picha ili kupunguza mikumbo siasa ni upendo bwana tazama humu uone walichokuwa wakizungumza | 2017-01-21T04:18:40 | http://utamuutamu.blogspot.com/2015/09/hahaha-hapa-ndio-utajua-utamu-wa-siasa.html |
yaaap nikiwa na maswahiba zangu wa tbc1 kushoto ni nick marwa na katikati ni maimartha jessenikiwa na rafiki yangu mambaye ni kocha wa timu ya taifa ya soka chini ya miaka 23 jamhuri kihwelu aka 'julio'nikiwa na mshambuliaji machachari wa timu ya simba ya jijini dar musa hassan aka 'mgosi'sambamba na swahiba 'jb' ambaye ni mcheza filamu nguli nchini | 2017-07-23T22:40:46 | http://kinyaiyas.blogspot.com/2011/04/jiachie-na-ben-kinyaiya_14.html |
kumbu kumbu ya waamini marehemu wote | vatican news
tarehe 2 novemba mama kanisa anaadhimisha kumbu kumbu ya waamini marehemu wote (ansa)
kumbu kumbu ya waamini marehemu wote
baba mtakatifu amekumbusha kwamba tarehe 2 novemba kila mwaka mama kanisa anawakumbuka waamini marehemu wote papa francisko anatarajiwa kuadhimisha ibada ya misa takatifu kwenye makaburi ya laurentino yaliyoko mjini roma
baba mtakatifu francisko mara baada ya sala ya malaika wa bwana siku kuu ya watakatifu wote tarehe mosi novemba 2018 kwenye uwanja wa kanisa kuu la mtakatifu petro mjini vatican amechukua fursa hii kuwasalimia na kuwatakia heri na baraka mahujaji na wageni kutoka ndani na nje ya italia waliohudhuria sala ya malaika wa bwana kwa namna ya pekee kabisa amewashukuru wale wote walioshiriki katika shindano la mbio za watakatifu yaliyoandaliwa na mfuko wa utume wa don bosco kwa kushiriki kwa furaha katika maadhimisho haya baba mtakatifu anawashukuru kwa mkakati na uwepo wao
baba mtakatifu amekumbusha kwamba tarehe 2 novemba kila mwaka mama kanisa anawakumbuka waamini marehemu wote papa francisko anatarajiwa kuadhimisha ibada ya misa takatifu kwenye makaburi ya laurentino yaliyoko mjini roma anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kumsindikiza kwa njia ya sala katika maadhimisho ya siku hii maalum iliyotolewa na mama kanisa kwa ajili ya kuwakumbuka na kuwaombea wale wote waliotangulia mbele ya haki wakiwa na alama ya imani na sasa wanapumzika kwenye usingizi wa amani mwishoni amewatakia waamini na mahujaji wote siku kuu njema ya watakatifu wote
marehemu wote
01 november 2018 1601 | 2019-05-22T08:36:08 | https://www.vaticannews.va/sw/pope/news/2018-11/papa-francisko-marehemu-wote-novemba-makaburi-laurentina-roma.html |
ningekuwa nafasi ya wenger | jamiiforums | the home of great thinkers
discussion in 'sports' started by kashengo may 27 2012
chamackhsquillaqibendtnerfabianskidiaby wote ningewatoa
chamackhsquillaqibendtnerfabianskidiaby wote ningewatoaclick to expand
huna tofauti na wenger huo ndio upuuzi ambao amekuwa anaufanya miaka nenda rudi kupenda vya chee nomaclick to expand
ali mradi iwepo culture ya kuretain wachezaji na kuongeza reinforcement whenever possibleila ukununua kiboya unaishia kama liverpool ebu fukiria downing ametua kwa paund mil 20 na hana goli wala assist msimu mzimathe same to carrolhanderssontimu inayoweza kuwatunza wachezaji wakakaa pamoja mda mrefu baadae huzoena na kujiaminikuna mambo hayawezekani pale arsenal hata tufanyeje kwani kuwepo peter hillwoodgazidisstan kraonke na wenger iyo ni (tight budget each year) na man u naona nao wameia dopt hii kanuniclick to expand
hapo kwenye nyekundu tu ndio kuna pointi zingine zote ni pumba na hiyo pointi wenger kaishindwa wenzake wote (ferguson maurinho et al) wameweza kubalance young and old hata milan ya wazee imeweza kufanya retention ya oldies na kusustain youngsters ila wenger ndio kwanza anaanza tena upuuzi ule wa mwaka jana kwenye sakata la rvpclick to expand
naelewa yote hayo pamoja na mtizamo wangu kuuona ni pumba ila nakwambia timu kufanikiwa si kama lazima mtumie mapesa meengi maana timu hata kama ina academy nzuri ya soka itafanya vizuri kwa budget ndogo na kununua wachezaji wachache na suala la rvp ilo ni kosa la board nzima kulewa pesa wanazoingiza bila kujua bila ya wachezaji hwawezi kupata hayo mapesa na upande mwingine huyu huyu rvp ata akiondoka hatopata watu wakamvumilia na miguu yake flagile kama ileseven season consecutively yuko majeruhi ila leo anataka aende city kama atakomaa akwende alafu siku akiumia wananunua stiker mpya warabu wanataka machekoclick to expand
arsenal ndiyo club pekee inayotengeneza super profit pale uk na inawezekana kuliko clubs nyingi eu vikombe ni moja ya malengo ya clubs lakini hela kwanza it's all about strategies umkhontowesizwe said
mkuu hii si ungeweka tu kwenye post ya watu wa assnol kuna ulazima gani wa kuanzisha thread mpya nadhani huu nao ni ubadhirifu au matumizi mabaya ya jfclick to expand
hakika ukichaa ni kukirudia kitu kile kile tena na tena ukitarajia matokeo tofauticlick to expand
kichaa mwenyewe na mdomo wako mchafu huwezi comments mpaka utukane pambavclick to expand
si kweli nafanana na wenger katika philosophy yake anawafukuza watu waliofikia 30 kitu ambacho ni kosa kubwa timu inakosa winning mentalit na experience imagine mtu kama gallaspiresgilbertoeduvieiraparlourraulen wote hao aliwakatalia 2 years contarct kisa wako miaka 30 huu ni upuuzi wa arsenal mwingine nisio kubaliana nao siku zote
umemsahau frimpong back up ya songclick to expand
si kweli nafanana na wenger katika philosophy yake anawafukuza watu waliofikia 30 kitu ambacho ni kosa kubwa timu inakosa winning mentalit na experience imagine mtu kama gallaspiresgilbertoeduvieiraparlourraulen wote hao aliwakatalia 2 years contarct kisa wako miaka 30 huu ni upuuzi wa arsenal mwingine nisio kubaliana nao siku zoteclick to expand
mzee wenger sijui anafikiria nini sasa hviclick to expand
now you are talking huu ushauri ni tofauti kabisa na uliotoa mwanzo hapo pekundu ndio pointiclick to expand
tatizo kaka umeniparamia ukadhani mi siiijui arsenal kisa cha kufanya vibaya kila msimu tatizo kwanza ni kushindwa kuwabakiza nyota wakeclick to expand | 2017-04-27T15:30:58 | https://www.jamiiforums.com/threads/ningekuwa-nafasi-ya-wenger.269485/ |
hapana chezea mange kimambi awapa bakora maadui zake | habari za walimwengu
home » » hapana chezea mange kimambi awapa bakora maadui zake
hapana chezea mange kimambi awapa bakora maadui zake
written by bewith jeddy on wednesday july 16 2014 | 1022 am
usipojipanga ntakupangalol
mange 44 comments jul 162014 uncategorized
first of all mungu atawalaani sana kwa kunishuhudia uongo mwezi huu mtukufu cha pili atawalaani pia sababu instead of mimi kukaa nikiweka products kwenye website yangu nimekaa na deal na wapuuzi ila this time imebidi nijibu sababu my reputation is on the line my whole business structure
depends on my reputation as an honest and fair business woman kwa hiyo lazima nijibu hili
kama mnavyonijua huwa siongei bila evidence haya twende kazi
the whole idea ya high end wigs ilianzia na rafiki yangu mmoja anakaa nigeria
aliniuliza about a wig i once used nikamwambia bei akashangaa sana akasema in nigeria zinauzwa $1500
kwa hiyo nikimuuzia whole sale kwa 800 au 900 atatengeneza hela na atawa undercut wauzaji wa huko atayauza kwa 1200
mpare na mie hapo hapo nikapata business idea nikasema let me find the very best ones basi nikampata huyu dada on insta kwa kweli nikadata
hiyo hapo ni link ya website naomba muangalie bei hiyo ni bei ya yeye kukutengenezea wigi tu ila unamtumia nywele zako mwenyewe anakutengenezea wigi
tumeelewana eeeh hiyo ni bei ya utendani kazi bila nywele wapuuzi wengi hapa ndo walipojichanganya sasa ngoja niwape shule
huyu dada aliweka mpaka na link ya kampuni aliponunulia nywele ya wigi nililokuwa nimelipenda na ukweli ni kwamba mimi siwezi kuuza kitu without me trying it out first nikasema ngoja ninunue nywele nimtumie anitengezee nione quality yake kabla sijawatumia wateja
naomba uweke akiba akilini kwamba cheapest price yake hapo kasema ni $175 sasa tuchukue hiyo 175 tuache na bei ya express ambayo ndo ningekuwa natumia
basi mpare nikatoka mdogo mdogo mpaka kwenye hiyo website maana nilitaka niwe natumia the very best hair possible
jamani kumbukeni issue imetokea jana usiku naomba muangalie bei za nywele alafu na wewe mwenyewe nenda ukaangalie
basi nikanunua nywele bundle 3 hapo hapo jinsi nilivyokuwa na mcheche yani nilikuwa nafatisha maelezo ya mtengeneza mawigi to the t maana nilitaka nywele zitoke vile vile
hii ndo payment niliyofanya kupitia pay pal bundle 3 hizo jamani chekini bei $400 hizo chenji ntazisamehentampa leila apandie mabasi brooklyn
haya sasa naomba tujumlishe dola 400 + 177 ya yule dada how much is that $575 sawa eeh
haya twende kazi kama mlivyoona kwenye post zangu jana kuhusu nywele nilisema wigi zote zitakuwa na lace closure
haya hii ndo bei ya lace closure naomba kuweka msisitizo kuwa hii website ni website niliyonunulia nywele pia
ni website ambayo nimetoa kwa huyo huyo mtengeneza mawigi maana nilitaka nywele zitoke vile vile jinsi navyowapenda wateja wangu
yani nilifata maelezo yake kama nasoma swali la mtihani
kwenye ile 575 yetu naomba uongeze 124
how much imefika hapo $699 sawa eeeh bado tupo pamoja
sasa naomba uweke na usafiri wa kutoka marekani mpaka africa kila mtu anajua dhl fedex etc cost ya kutuma hili wigi kwako
will cost between 3060 mpaka hapo wigi lako limenicost more than $700 dollars tuseme limenicost between 730760
mimi niliwapa cost ya 800 sasa wapenzi wangu niambie faida ya dola 4050 kwa kila wigi la dola 800 ni mbaya naomba niambieni ni mfanyabiashara gani angefanya hii na kujipa faida ya around 50 dollars only mtu mwingine si angetafuta hata profit ya 50 watu hawajui mimi nimesomea biashara naamini ntapata faida kubwa kwa kuuza vitu vingiiiiiiiii kwa profit ndogo kuliko kuuza vitu vitatu kwa profit kubwa
basi sister wenu jinsi nilivyo na haraka nikamtumia email huyo mnugu anaetengeneza hayo mawigi nikamweleza kuwa nimeshanunua nywele kwenye
kampuni aliyoitaja yeye na nimezituma nywele ziende kwake moja kwa moja nyewele zinatoka canada sasa nikaona zitoke canada zije kwangu then nimtumie
huyu dada ntachelewa so nilivyonunua nikaweka shipping address ya huyu mafrican american ili tufanye fasta zaidi
na hapo hapo nikamweleze kuwa naomba tufanye biashara nna market kubwa sana africa jamani hivi mtu anaetaka kuiba kazi ya mtu akaifanya yake hivi kweli anaongea na mwenye mali kumwambia wafanye biashara ingekuwa nimeweka picha za wigi zake alafu nikajifanya nimetengeneza mie nikauza its another story but i informed her ila ukweli lazima usemwe na kwenye makosa lazima nikubali kosa langu mimi hapa ilikuwa ni kiherehere cha kurusha picha
kabla huyu mnugu hajanibu kuwa anaweza au hawezi mie nilijua hii ni kampuni na kwamba wanatengeneza tu mawigi only baada ya kumtumia nywele ndo nimekuja kujua kuwa anachukua order kwa appoitnment na yupo peke yake mie nilijua yeye ni ndo mwenye kampuni ya nywele wana produce nyingi kumbe sio
naombeni msome email yangu na msome jibu lake hakunijibu chochote kuhusu biashara mie nikadhani labda anafikiria then ataniambia baadae ila mie nikaanza tangaza mawigi maana nilidataje nae na nilijua wengi sana africa wanatafuta mawigi high quality hawapati niliiona fursa jamani
nikachukua picha za nywele zake nikatoa logo nkaziweka sasa jamani hapo nimekosea nini hivi mlitaka niache logo ili mjue nimetoa wapi sasa hapo nafanya biashara au nacheza makida si bora nikae ninyonyeshe mwanangu na pia sikuona ni big deal kutumia picha za mtu ambae naenda kununua products kwake ni kama niweke products za gucci kwenye website yangu si ntatumia picha za gucci unadhani gucci watanimind no ways as long as
nauza the original gucci na sio fake gucci alafu natumia picha zao na jina lao sisi watu weusi tuna laana za drama jamani
haya tuendelee na story
kwa vile jana niliingia kulaa saa moja asubuhi sababu ya website leo nimeamka around saa 6 mchananaamka nakuta missed calls zaidi ya mia whatsapp message ndo hazisomeki wanaonipenda wakiniambia niamke ningie instagram
ndo nkakutana na hii kwanza huyu ndo mtengeneza nywele mwenyewe akarusha hiyo basi nikajikaza nikawa calm nikaanza kusoma maelezo ya huyu mnugu
kidogo nilimwelewa na pia sikumwelewa kwanza kabisa yeye mwenyewe kwenye comments zake amekubali kuwa nilim contact kuwa tufanye biashara africa
ila akasema hakunijubu kituwhich is true akadai nataka kuiba kazi yake hivi watu weusi tukoje jamani i think ndo maana all great inventions in the world zimefanywa na mtu mweupe weusi akili zetu ni drama drama and drama and not money jamani nauliza tena mtu anaetaka kuiba kazi yako huwa anakuomba mfanye biashara pia kwenye post zangu nilisema kabisa ni mtu mwingine anaetengeza hizi wigi sio mimi na nikamsifia sasa hapo inakuwaje ila katika kusoma comments pia nikaelewa kuwa huyu dada amekuwa pumped sana na watanzania wenzangu ambao ndo wamempa kichwa na kumwambi its true im a scammer one big point niliyotoka nayo kwenye comments za huyu dada na ambacho ndo kilichomuuzi sana huyu dada ni kwamba alidhani mie nitamlalia kibiashara kwamba nanunua kwake wigi $150 then mie naenda kuuza $800 akapanick akasema naweka profit ya 400 mneona point ya mnugu hapo kati ya vyote alichochukia ni hicho cha mimi kupata profit ya 400 hivi jamani mie ntakuwa mwizi wa kiasia gani jamani kujiwekea profit kubwa hivyo
huyu dada alidhani na mie ntafanya biashara na nyie kama yeye anavyofanya biashara na wateja wake alidhani kwamba nimewapeni hiyo bei ya $800 alafu
mnanunua nywele zenu wenyewe mnanitumia kama vile wateja wake yeye wanavyofnya hivyo dola $150 yeye ana charge bila nywele nywele anataka ukatafute mwenyewe umtumie ila mimi biashara yangu ilikuwa tofauti kwanza najua tanznaia africa hakuna nywele za viwango vya juu na zikiwepo hazishikiki
so mie kama nilivyoeleza jana naweka nywele mwenyewe hakuna kunitumia nywele mnaona hapo mnugu alipojichanganya hakukaa chini akafikiria maybe she is buying the hair too akadhani nawapiga juu kwa juulol ila narudia tena watu weusi ndo tatizo letu uwezo wa kufikiri huwa ni mdogo sana tunapenda ziaidi drama kuliko kukaa chini na kufikiria
another thing pia ndo maana weusi hatuendelei maana mtu anaumia wewe uta make money kuliko yeye sasa yeye huyu mwenywe mawigilets say kweli n
ningekuwa mtu wa tamaa nikawa napata 400 yeye inamuhusu nini yeye si anauza kwangu na mimi nikauze navyoweza inahusu nini napata profit gani hata kama ingekuwa kweli napata that much black tumeumbwa na roho za vikorosho kuliko yeye awaze kuwa biashra yake itakuwa ntamuuzia yeye anawaza mimi ntapata nini lol
sasa ndugu zangu wa bongo kwa vile mmemjua huyu please naomba mmoja tu aende front akanunua kwake aone kama hajaspend what i spent or more than that hapo ndo mtakapojua thamani yangu kwenu kwenye kuwaletea products bora kwa bei poa sana unless kama utamtumia nywele za mchinalol
haya tuendelee na habari
haya sasa ngoja niwapange hawa magume gume yalomshinda mtume
basi bwana ngoma ikapata mchezaji mnakumbuka some comments humu navyowaambiga anaandika linda privati jeti wengine
mkasema linda yupo busy anashona hana time haya mmeona sasa yani istagram page yake imejaaa hii issue yani kaivalia njuga
naomba msome hiyo comment yake hapo na yeye analia na mimi kumake 400 hivi kumbe mnaijua hollywoodshopaholics nilidhani hamuuijualol
anyways linda namsamehe maana dozi aliyopata last yr bado inampelekesha she never got over it ila mwanamke wa kiislam kutafuta shari mwezi wa ramadhan inahusu jamani alafu akitoka hapo anaenda kuswali anapiga picha sugu za miguu anasema anasali sana lol lakini namsaheme as you all know
mtu yoyote ambae alishatumia unga au kuuza unga akili zao huwa hazirudi kuwa fresh maana huyu jimama nae badala akae ahta afikirie hivi kweli mange anaweza kununua kitu dola 175 alafu akauza dola 800 yani badala afikirie linakulupuka tu huyu laana za watoto wa watu alowafanya mandondocha na midawa yake itamsumbua mpaka anakufa hivi mama gani unamjua wewe wa age yake anaefanya ujinga huu instagram
kilichonisikitisha zaidi ni kwamba na yule mwanae leyla anae eti kavalia njuga issue omg huyu mtoto yani kweli amekuwa shangingi kama mama yake
i swear to god mie bhoke akikutana na watu ambao siongei nao ataenda na kuwaamkia wabaki wanashangaa maana she doesnt know that side of my life na wala simuhusishi mtoto imagine huyu leila badala akarudie amalize high school eti nae ana deal na drama za mamake instagram i feel bad for this kid duh mwenyewe mungu amuepushe huyu mtoto maana anapoelekea ni atakuwa shangingi ka mamake
hivi we shangingi mzee unapata wapi muda na mimi si unajifanya uko busy una madeal why are you still on my caseunajifanya unajua biashara ungekuwa unajua biashara maduka yako yale ya mwaka 47 yasingekufa ungekuwa nayo hadi leo ila sababu ni mshari na mwenye roho mbaya ndo maana leo hii at that age bado unashindani with people 10 yrs your junior by now ulitakiwa uwe on a whole different league ila bado unasugua gaga at that age
hivi ukiulizwa for the more than 15 yrs that you have been in america umepata nini utasemaje naomba kuuliza tu
zaidi ya kuzaa watoto wanne na wanaume wanne watoto wasiotakiwa na baba zao mpaka unawapa jina la babako kwani ulizaa na babako
first born wako ulishindwa hata kum guide angalau amalize high school really free education na bado mtoto hamalizi high shcool sasa umeone matokeo yake anaingilia ugomvi wa watu wazima yani keshakuwa kama mamake huko aliko asipoanza kudeal drugs sijui maana ndo ilikuwa kazi ya mamake
haya huyu changu wa wa west nae akapokea issuelol
hivi mmeona waliojifanya kuvalia njuga ni wale wale mataahira wetu wa kila siku hakuna mwenye akili zake alieongelea hili coz
wanajua lazma kuna kitu ndani yake especially cos mimi nilikuwa sijaongea
we stella uwiiiii unikome na uniache naomba uendelee kudeal na washenzi wenzio uwiii niache sawa umekaa marekani more than 10yrs
hivi ukiulizwa ume achieve nini marekani utasema nini nahisi utasema makalio yako yamekuwa makubwa jinsi ulivyo punguwani baba yako (ex boyfriend wako) alihonga
kanisani wakaachwa mayatima wa ukweli ukajifanya wewe yatima ukachukua nafasi ya mayatima wa ukweli badala sasa uje huku ufanye ya maana
umekalia kufanywa mpira wa dana dana na wanaume you came here on a full scholarship sababu ya uyatima feki wako na bado shule imekushinda mpaka student visa ikawa revoked darasani huendi kazi kwenda mabaa kuvizia wanaume
kwanza siongei na illegal immigrants mimi badala ukae utafute makaratasi unakaa kunitafuta mimi unajibenua benua insta maskini vitoto vya watu watu huko bongo vinadhani maisha marekani mazuri kumbe hamna kitu maisha ya kubangaiza ulalwe na wawest ndo ukanunue kiatu au nywele eti mzuri wazuri wanaachwaungekuwa mzuri usingekuwa unapigwa kibuti kila baada ya siku mbili kha mwanamke gani usieweza kukaa na bwana hata mienzi 6
mimi sio mwenzio mimi ni mtafutaji kima wewe nna uwezo wa kulala nikala nikavaa bureeee nna mume mwenye upendo na mapenzi na mimi na uwezo wa kuniacha niwe stay at home mom lakini its not im my nature mimi ni mtafutaji nataka kuwa na changu nahangaika mpaka mume wangu hanielewi why nahangaika hivi anatamani nikae nyumbani nimlele wanae full time ila najua kuna leo na kesho mungu anaweza kumchukua mume wangu je ntaanzia wapi ntaleaje wanangu
ndo maana najituma na sijaanza leo nilikuwa nna baba mwenye kunipa more than what i needed na still i was hustling uliza waliosoma na mimi uni
nimeanza kuandaa miss dar indian ocean mwaka 2003 na hapo nakaa home nalelewa na baba yangu nna kila kitu ila bado nilikuwa nahangaika kwenye jua dar natafuta sponsorship ya miss dar indian oceanmpaka babangu siku moja alilia machozi kuwa namwaibisha jinsi navyoomba watu hela ya sponsorship nikamwelesha maana ya sponsorship akaelewa ila akaniuliza how much will i make kwenye show nkamwambia 15m akasema niache atanipa hizo pesa kesho yangu akanipa cheque 15m nikarudi zangu hostel mabibo na bado nikaandaa kisirisiri kaja kujua nishafanya show nikamrudishia pesa zake thats just me napenda kuwa na kitu changu hata kama kinanipa dola 10 ila ni changu sasa wewe mwenzangu ni tofauti ukishalalwa ukapewa dola 100 ukaenda kununua nguo ukapiga picha ukaweka insta basi umeridhika na maisha
sasa mwenzio nna hustle wewe unataka kuniharibia biasharatatizo nimesoma hata siku moja mburula alieishia form 4 will not be my down fall hivi kweli u thought wewe na huyo ex muuza unga ndo mngeniaibisha leo wewe hapa kisiki hamniwezi
we endelea kujibenuabenua huko instagram hayo ndo unayoyaweza ila chonde chonde wadogo zangu mlioko bongo msije pagawa na mapicha marekani hamna kitu huyo nyau hata akifiwa na babake (ex boyfriend) hawezi kwenda kuzika hana papers na mtu akimshikia bango anarudishwa bongo juu juu
hana elimu hana future sasa anataka kuingia kwenye hollywshopaholics nikome mchaga wewe alafu sijui mchaga gani huyu jamani uwiii wachaga naowajua mimi very hard working ni watafutaji wa hela kwa kweli sijui wachaga wauza sura
haki ya nani ukiniwekea huyu na flora lyimo mbuta nanga mara 100 mbuta nanga bora mbuta nanga anapiga picha na chupi anazouza angalau anapata vijihela vya kubadilisha mboga sasa huyu anapiga picha na chupi huku halipwi uchangu usiolipa ni shiderrr
ungekuwa na akili ungetafuta bwana wa kukuhonga elimu usome angalau siku ukirudishwa kwenu uwe na elimu sasa wewe unataka kuhongwa kuongezewa makalio shule inasaidia sana hivi wanaume gani siku hizi wanaoa wanawake sababu ya matako makubwawenzio tulivyokutana na waume zetu hatukuomba hela ya kiatu tuliomba kusomeshwa masters sasa wewe punguani ukilipiwa nywele saloon basi miguu yote unaachia angle 90 degrees
wewe na huyo mvuta bangi mwenzio mnikoooooo i have been in this country for 2 yrs only and made significant progress bado sijafika napopataka au kupata mafanikio makubwa ila atleast nimesonga mbele and thats 2 yrs baby come check me after 5 yrs na huyo jinga anaetangza kona zote mange hana nyumba us au bongo mwambie aendelee kuchungulia humu kuna simu atapata ugonjwa wa moyomfyuuuuuu
haya stella (changu wa wawest) na linda private jeti aka muke ya mume mwenye bankruptcy nawapeni kazi
naomba muongee na huyo african american wa mawigi kwa vile mmeshakuwa shoga zake
please mwambie nywele zangu nimezituma kwake as she can see kwenye hii risiti ya pay pal please mwambie akizipata tu anitumie fastaaaaaa
uwii angejua vilaza anaoongea nao hakuna hata mmoja mwenye uwezo wa kununua hata wigi la
$50 let alone la dola mia 800
haya nimemaliza mnanijua nikichukia huwa naandika kitabu poleni someni taratibuchukua hata siku tatu sio lazma umalize leo leo
wateja wangu wa mawigi hii biashara ipo pale pale tena sana sana sasa hivi mmjua jinsi gani im fair kwenye biashara nahisi ndo mtanunua zaidi
niliwaambie instagram subirini nikijieleza mtanipenda mara 100 ya zamanilol
kwa wateja wangu mliopenda zile wigs jana hakijaharibiaka kitu nimempata mtu mwingine tena huyu kasema ni family business
wako kama wanne sisters wanatengeneza wakinitumia picha tu nawarushia insta
what a waste of my time yani leo ningemaliza website yangu naona ila ndo hivyo mashetani waliona watucheleweshe kidogo kwa mlioenda kunitetea pande zile ahsanteni sana si mnajua wale mablack hawanijui basi wakiona kina mama bankruptcy wanacomment ushuzi wanaamini
ps kuna mtu nimeshangaa hakuingia kwenye hii ngoma yani sijaamini maana huyo ndo zamani ndo angelianzisha big up rachel temu umekuwa siku hizinimekupenda burelolhawa nyau wengine wamegoma kuelewa somo ila wataelewa tu
source uturncotz | 2017-12-15T13:44:36 | http://www.bewithjeddy.com/2014/07/hapana-chezea-mange-kimambi-awapa.html |
wanakijiji wamwagia sifa rais magufuli kwa kutoa agizo hili kuhusu wao ~ g sengo
wanakijiji wamwagia sifa rais magufuli kwa kutoa agizo hili kuhusu wao
monday october 21 2019 habari no comments
na timothy itembe mara
wananchi wa kijiji cha nyamwaga wilayani tarime mkoani mara wamempongeza rais john pombe magufuli kwa kuagiza halmashauri ya tarime vijijini kuhama nyamwaga ili kusogeza huduma karibu na wananchi
akiongea kwa niaba ya wenzake mwenyekiti mstaafu kirigiti sasi alisema kuwa ndoto zake alizokuwa nazo hapo nyuma ni kuona mji wa nyanwaga unakuwa mji mkubwa na ndoto hizo zimetimizwa
mstaafu huyo aliongeza kuwa yeye binafsi aliwiwa na maendeleo ambapo katika uongozi wake alishawishi mgodi wa kuchimba madini ya dhahabu uliopo nyamongo acacia na kusaini mikataba ya kutekeleza shuguli za miradi ya maendeleo ndani ya kijiji hicho ikiwemo kulima barabara zinazozunguka mji wa nyamwaga pamoja na kujenga shule ya nyamwaga sekondari hayo wameyatekeleza kumebaki kujenga walitekeleza lakini bado kuna moja hawajatekeleza kama vile ujenzi wa chuo cha veta na ukamilishaji wa madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya jk nyerere
kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri hiyo apoll tindwa alitumia nafasi hiyo kuwataka watumishi wake kuhamia nyamwaga ili kuwakaribu na wananchi wa nyamwaga katika kutoa huduma
namshukuru rais john pombe magufuli kwa utendaji kazi wake nasi kama halmashauri tunatekeleza agizo alilotoa tarehe saba mwezi huu la halmashauri kuhamia nyamwaga ili kusogeza huduma karibu na wananchi nami nasema watumishi wangu ifikapo mwisho wa mwezi huu wote wawe wamehamia nyamwaga kwa sababu mimi tayari nilishahamia na mizigo yangu lengo ni kusogeza huduma kwa jamiialisema tindwa | 2020-05-28T04:57:14 | https://gsengo.blogspot.com/2019/10/wanakijiji-wamwagia-sifa-rais-magufuli.html |
bustani ya manispaa ya iringa kuwa kivutio kizuri cha utalii mkoani iringa bongo leaks
bustani ya manispaa ya iringa kuwa kivutio kizuri cha utalii mkoani iringa
bustani ya manispaa ya iringa inavyoonekana kwa sasa
vyakula na vinywaji vya aina mbalimbali vimeanza kutolewa kwenye bustani hiyo na kampuni ya imara foods iliyopewa tenda ya kuendeleza bustani hiyo
bustani ya halmashauri ya manispaa ya iringa itafanywa kuwa kivutio cha kwanza cha utalii katikati ya mji wa iringa hiyo ni kwa mujibu wa mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya iringa theresia mahongo
mpango huo ni jitihada za halmashauri hiyo kuunga mkono harakati za kitaifa za kuboresha shughuli za utalii nchini na hasa baada ya mkoa wa iringa kutangazwa kuwa kitovu cha utalii kusini mwa tanzania
ili kufikia lengo hilo mahongo alisema mwaka jana halmashauri hiyo ilitangaza tenda kwa ajili ya kumpata mwekezaji atakayesaidia kuboresha mazingira ya bustani hiyo ili yavute watalii wa ndani na nje
tunataka bustani ile iwe na hadhi kubwa iwe na hadhi ya kimataifa itakayoleta sifa kwa manispaa yetu na taifa kwa ujumla kwa kukuza shughuli za utalii mkoani iringa alisema
mahongo alisema mchujo ulifanywa kwa umakini mkubwa uliiwezesha kampuni ya imara foods kuibuka kidedea dhidi ya kampuni nyingine
aliipongeza kampuni hiyo kwa kuanza maboresho ya bustani hiyo kwa kupanda miti ya kivuli maua na nyasi za kuteleza ili kuwavutia watalii wengi zaidi
afisa utalii wa shirika la hifadhi ya taifa (tanapa) wa ofisi ya kanda ya nyanda za juu kusini iliyopo mjini iringa risala kabongo alisema manispaa ya iringa ni lango la watalii wanaokuja mkoani iringa kutembelea vivutio mbalimbali ikiwa ni pamoja na hifadhi kubwa kuliko zote nchini ya ruaha
alisema mbali na kuboresha mazingira yake shughuli za kuboresha vivutio vya utalii zinatakiwa kwenda sambamba na ujenzi wa miundombinu mbalimbali kama ujenzi wa hoteli za kitalii na maeneo ya kupumzikia
mmoja wa wakurugenzi wa imara foods peter christopher alisema kazi ya kuboresha bustani hiyo imeanza kwa kasi kubwa na watalii wa ndani na nje watagemee makubwa katika kipindi kifupi kijacho
tutazingatia vipengele vyote vilivyopo katika mkataba wetu tumedhamiria kuifanya manispaa ya iringa iwe mfano wa shughuli za utalii kusini mwa tanzania alisema
alisema mbali na kupanda maua ya kuvutia nyasi na miti ya vivuli katika bustani hiyo wataweka vivutio vingine mbalimbali vikiwemo vinywaji na vyakula vilivyozoelekea na vile vya kitamaduni
tunajipanga kuanza kutengeneza vyakula vya kitamaduni kwasababu ni sehemu muhimu katika kukuza utalii mfano wa vyakula hivyo ni kama ugali wa muhogo na nyama ya wanyama wadogo kama sungura na simbilisi alisema
alisema utalii wa vyakula vya asili umekuwa ukivutia watalii wengi katika miji mingine ya kitalii ukiwemo arusha
alisema maboresho mengine katika bustani hiyo yatakuwa yakifanywa kwa kuzingatia mahitaji ya wadau na maelekezo ya manispaa hiyo
kuboreshwa kwa bustani hiyo kumeelezwa na wadau wa maendeleo ya manispaa ya iringa kwamba kutaongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi ya taifa ya ruaha
hifadhi ya ruaha kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na hifadhi za taifa (tanapa) ndiyo inayoongoza kusini mwa tanzania kwa safari za utalii hifadhi ya kwanza ni serengeti | 2018-10-17T07:23:10 | http://www.frankleonard.info/2014/04/bustani-ya-maniaspaa-ya-iringa-kuwa.html |
jafo awaonya wakandarasi washauri wa miradi ya maji habari za jamii
home / unlabelled / jafo awaonya wakandarasi washauri wa miradi ya maji
dotto mwaibale 359 am
naibu waziri ofisi ya rasi tamisemi selemani jafo akisikiliza taarifa ya mradi wa maji mkoyo
aidha amebaini kampuni hiyo mshauri huyo ndiye yule yule aliyesimamia mradi kijiji cha itiso ambao
aliutembelea mradi huo mwezi agosti mwaka huu na kukumbana na changamoto nyingi | 2018-02-22T01:01:54 | http://www.habarizajamii.com/2017/09/jafo-awaonya-wakandarasi-washauri-wa.html |
magufuli na mivutano ya madaraka ccm serikalini raia mwema
magufuli na mivutano ya madaraka ccm serikalini mar 09 2017 by evarist chahali in makala katika hitimisho la makala yangu katika safu hii wiki iliyopita niliahidi kuwaletea uchambuzi kuhusu mivutano ya kugombea madaraka (power struggles) ndani ya chama tawala ccmkwa bahati nzuri kati ya makala hiyo na hii kumejitokeza tukio ambalo linaweza kuhusishwa na mada hiyo ninayoiongelea katika makala hii
baruapepe evarist@chahaliorg blogu wwwchahalicom twitter @chahali one thought on magufuli na mivutano ya madaraka ccm serikalini pingback tanzania is parliament waking up | democracy in africa trackback tanzania is parliament waking up | democracy in africa leave a reply cancel reply your email address will not be published required fields are marked *comment name * email * website mitandao ya kijamii twitter facebook google plus rss youtube instagram machapisho mapya kimataifa nini kitatokea marekani korea kaskazini zikipigana vita 0 comments | 2017-04-29T07:33:47 | http://www.raiamwema.co.tz/magufuli-na-mivutano-ya-madaraka-ccm-serikalini/ |
muwsa yaanzisha mfumo mpya kuhifadhi taarifa kilimanjaro yetu
home » » muwsa yaanzisha mfumo mpya kuhifadhi taarifa
muwsa yaanzisha mfumo mpya kuhifadhi taarifa
mamlaka ya majisafi na majitaka moshi (muwsa)
alisema mfumo wa kielektroniki wa utunzaji taarifa utakapokuwa umeandaliwa vema mamlaka itakuwa kwenye kiwango ambacho mteja hatakuwa na haja ya kupanga foleni kulipia ankara | 2018-03-19T18:05:48 | http://kilimanjaro-yetu.blogspot.com/2014/01/muwsa-yaanzisha-mfumo-mpya-kuhifadhi.html |
mashindano ya kumuenzi marehemu hassan gharib yazinduliwa zanzinews
home michezo mashindano ya kumuenzi marehemu hassan gharib yazinduliwa
mwakilishi wa jimbo la dimani dkt mwinyihaji makame mwadini akikaguwa timu katika ufunguzi wa mashindano ya hassan gharib cup bweleo mkoa wa mjini magharibi unguja alliempa mkono ni mchezaji wa timu ya mitondooni khamis ali picha na mwajuma juma
mwakilishi wa jimbo la dimani dkt mwinyihaji makame mwadini amezinduwa rasmi mashindano ya pili ya kumuenzi marehemu hassan gharib
mashindano hayo yatafanyika katika uwanja wa bweleo ambapo mwakilishi huyo aliwataka wachezaji wa timu shiriki kucheza kwa amani na utulivu ili kuendeleza kwa vitendo matendo ya marehemu
alisema kuwa wanafanya mashindano hayo kwa lengo la kumuenzi marehemu hassan gharib ambae alikuwa mdau mkubwa wa mpira pamojana kupenda amani na utulivu
hivyo wanachokitaka wao ni kuona mashindano hayo yanatumika kwa kuonesha vipaji na soka la upinzani litakalovutia watazamaji
mapema akisoma risala mwenyekiti wa kamati ya mashindano hayo said majid alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni vilabu kuomba kuongezewa kwa zawadi ili ziweze kulingana na zawadi za mashindano mengine ya ndondo ambayo hapa zanzibar ili kuzidi hamasa na timu nyengine zaidi zizidi kushiriki
michuano hiyo inashirikisha timu 16 yana lengo la kulienzi jina la kaka yao marehemu hassan gharib ambae alikuwa ni miongoni mwa wanabweleo amabao ni muhimili mkubwa wa timu hiyo | 2019-10-21T02:52:14 | http://www.zanzinews.com/2019/06/mashindano-ya-kumuenzi-marehemu-hassan.html |
matukiomichuzi je umezaa mtoto nje ya ndoa fanya haya ili kumwezesha kurithi baada ya kifo chako
unao watoto wa namna mbalimbali unao uliowazaa ndani ya ndoa na wale uliowazaa nje ya ndoa unawapenda sana wote kwa usawa kwasababu wote ni watoto wako kuna suala la kifo na ungependa baada ya kifo chako watoto wako wote wafaidi kidogo ulichochuma lakini je hilo umelijengea mazingira ni muhimu sana ujue kuwa suala la watoto wako kufaidi ulichonacho halitokani na matakwa yako laa hasha bali linatokana na matakwa ya sheria wewe waweza kuamua watoto wako wote wa nje ya ndoa na wale wa ndani ya ndoa wapate mali lakini baadhi wakakosa kutokana na msimamo wa sheria ni hapo unapotakiwa kuandaa mazingira yanayoendana na matakwa ya sheria ili watoto wako wote waweze kufaidi machumo yako 1fanya haya ili kuwawezesha watoto wa nje ya ndoa kurithi
uhuru wako wa kugawa mali kwa wosia upo katika 1/3 basi na si vinginevyo na ni kusema kuwa mtoto/watoto wa nje ya ndoa haki yao ipo katika 1/3 tu ikiwa utampatia mali zaidi ya 1/3 basi anaweza kunyanganywa kwahiyo uelewe kuwa wosia utakaoandika unahusu 1/3 ya mali tu zingatia kuwa usipoandika wosia kugawa 1/3 yote au sehemu yake kwa mtoto/watoto uliowazaa nje ya ndoa basi hawatapata mali kabisa baada ya kifo chako na hii ni kwasababu watoto hao hawaruhusiwi kurithi kisheria kwahiyo utaona kuwa unachotakiwa kufanya ili hao watoto wasikose ni kupiga hesabu ili kupata 1/3 ya mali yako na kuwapa yote au sehemu yake | 2016-10-25T01:31:36 | http://michuzi-matukio.blogspot.com/2016/08/je-umezaa-mtoto-nje-ya-ndoa-fanya-haya.html |
kalaba nje mazembe dhidi ya yanga ulimwengu anaanza bin zubeiry sports online kalaba nje mazembe dhidi ya yanga ulimwengu anaanza bin zubeiry sports online
mwanzo > yanga > kalaba nje mazembe dhidi ya yanga ulimwengu anaanza
mshambuliaji tegemeo wa tp mazembe ya drc ranford kalaba hatacheza dhidi ya yanga jioni ya leo uwanja wa taifa dar es salaam katika mchezo wa kundi a kombe la shirikisho afrika kutokana na kuwa majeruhi
kalaba hayumo kabisa katika orodha ya wanaoshiriki mchezo wa leo jambo ambalo hakika ni pigo kwa mazembe katika mchezo huu wa ugenini
mshambuliaji mtanzania thomas emanuel ulimwengu ameanzishwa pamoja na koffi christian na christian luyindama katika safu ya ushambuliaji
ranford kalaba (kushoto) akiwa na kocha mfaransa hubert velud wa mazembe muda huu uwanja wa taifa kabla ya mchezo na yanga
thomas ulimwengu (katikati) akipasha muda huu na wachezaji wenzake wa mazembe
wachezaji wa yanga wakipasha muda huu kabla ya mechi
vikosi kamili vya leo ni yanga deo munishi dida juma abdul mbuyu twite vincent bossou kevin yondan thabani kamusoko haruna niyonzima deus kaseke juma mahadhi obrey chirwa na donald ngoma
tp mazembe sylvain gbohoud guelassiognon jean kasusula issama mpeko salif coulibaly rodger asale adama traore merveille bope nathan sinkala koffi christian christian luyindama na thomas ulimwengu
benchi robert kidiaba muteba joel kimwaki deo kanda jonathan bolingi daniel nii adjei jose bodibake mpongo richard kissi boateng na jonas sakuwaha
item reviewed kalaba nje mazembe dhidi ya yanga ulimwengu anaanza rating 5 reviewed by bin zubeiry sports online | 2018-06-20T11:10:07 | http://www.binzubeiry.co.tz/2016/06/kalaba-nje-mazembe-dhidi-ya-yanga.html |
pinda apata wakati mgumu bunda mwakyembe akana kumshambulia lowassa na sitta aja na mambo matanomagazetini june 04 millardayocom
pinda apata wakati mgumu bunda mwakyembe akana kumshambulia lowassa na sitta aja na mambo matanomagazetini june 04
waziri mkuu mizengo pinda atakipa wakati mgumu chama cha mapinduzi (ccm) wilayani bunda baada ya baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo kutishia kuwa hawatakipigia kura kutokana na kiongozi huyo kutoa ahadi hewa ya upatikanaji wa maji safi na salama
wakazi hao wameapa kuwa labda ahadi hiyo iliyotolewa na waziri pinda machi mwaka jana itekelezwe kabla ya uchaguzi mkuu kinyume cha hivyo hawataipigia kura ccm ili kuonyesha kuwa hawaridhiki na namna wanavyodanganywa
wakazi hao walitoa tishio hilo juzi katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ccm akiwamo katibu wa ccm mkoa wa mara adam ngalawa na naibu katibu wa umoja wa vijana wa ccm (uvccm) mfaume kizigo
wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye mkutano huo walisema wameazimia kutoipigia kura ccm katika uchaguzi mkuu wa oktoba kwa kuwa viongozi wa ccm na serikali yake wanatoa ahadi za uongo na zisizotekelezeka
michael kweka alitaja ahadi iliyotolewa na waziri mkuu mizengo pinda machi mwaka jana kwamba tatizo la maji lingekoma juni kuwa ni moja ya ahadi hewa za viongozi wa serikali ya ccm zinazowachefua wananchi
hatutawapigia kura za urais ubunge wala udiwani wagombea wote watakaoletwa na ccm mwaka huu kwa kuwa wanakuwa wakitudanganya kwa ahadi hewakweka
kweka alisema akiwa ziarani wilayani bunda machi mwaka huu waziri mkuu mizengo pinda alitoa ahadi kwamba tatizo la maji lingekwisha ifikapo juni mwaka huu lakini hadi sasa hakuna dalili zozote za kumaliza kero hiyo
alisema hali hiyo inawafanya wakazi wa mji huo ambao wamekuwa wakidamka nyakati za usiku kutafuta huduma ya maji safi na salama kuichukia serikali ya ccm wakiamini kuwa haiwajali mimi kero yangu ni maji hiki kimekuwa kilio chetu kwa muda mrefu
lakini kinachotuumiza ni ahadi hewa za viongozi wa serikali ya chama chetu cha mapinduzi kuhusu mradi unaotekelezwa hapa mnaonaje tukiwanyima kura sababu mmezidi ubabaishaji alisema mkazi mwingine wa eneo hilo akiwahoji viongozi wa ccm waliokuwapo meza kuu
nyerere lucas aliilalamikia serikali ya ccm kwa kile alichoeleza kuwa imeshindwa kutimiza ahadi zake za kuboresha miundombinu ya barabara wilayani humo kama ilivyoahidi katika uchaguzi mkuu uliopita na kuwafanya wakazi wa maeneo hayo kusafiri kwa tabu kutafuta maji mbali na maeneo yao kero nyingine walizolalamikia wakazi wa wilaya hiyo ni mikopo kwa vijana na akinamama
walisema mikopo kwa makundi hayo imekuwa ikitolewa kwa watu maaalum hasa vikundi vinavyomilikiwa na watumishi wa serikali jambo ambalo limeonekana kwamba kuna nia ya dhati ya kuwasahau wananchi
hata hivyo katibu wa ccm mkoa wa mara adam ngalawa katika majibu yake ameshindwa kueleza lini mradi huo wa maji utakamilika badala yake akasema umepangwa kutekelezwa katika bajeti ya mwaka
wanasiasa wanaojiandaa kuingia katika uchaguzi mkuu wametakiwa kumuomba mungu ili awape nafasi hizo kwa njia sahihi kuliko kutumia sangoma
wito huo ulitolewa jana na mchungaji samuel mshana kwa niaba ya askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheri tanzania (kkkt) dayosisi ya dodoma katika ibada ya kuuaga mwili wa marehemu eugen mwaiposa aliyekuwa mbunge wa jimbo la ukonga (ccm)
mwaiposa alifariki dunia juzi akiwa usingizini kwa kile kilichoelezwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu mwili wake ulisafirishwa jana kwa ndege ya kukodi kupelekwa dar es salaam ambako utazikwa keshokutwa nyumbani kwake kipunguni dar es salaam
ilikuwa ni siku ya huzuni jana wakati wa ibada iliyofanyika kwenye viwanja vya bunge mjini dodoma iliyohudhuriwa na umati wa waobelezaji wakiwamo wabunge wafanyakazi viongozi wa mkoa na taifa akiwamo katibu mkuu kiongozi balozi ombeni sefue
katika bunge la kumi huyu ni mbunge wa saba kufariki dunia
akihutubia kwenye ibada hiyo mchungaji mshana alisema ni wakati wa kuangalia namna watu wanavyopaswa kutafuta madaraka kupitia njia zisizofaa
serikali katika ibada hiyo iliwakilishwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na bunge jenister mhagama ambaye alisema hadi mwaiposa kabla ya kukutwa na umauti alionekana mwenye afya njema na aliomba kuchangia katika hotuba ya wizara ya afya mhagama alisema serikali na chama cha mapinduzi vimepoteza mtu mahiri ambaye pengo lake halitazibika na kutoa rambirambi ya sh5 milioni
waziri wa uchukuzi samuel sitta ametangaza nia ya kugombea urais kwa tiketi ya ccm akieleza kuwa anataka kulifanyia taifa mambo matano ikiwa ni pamoja na kutenganisha biashara na siasa na kusimamia maadili ya viongozi wa umma
alitaja mambo mengine kuwa ni kusimamia muungano kukamilisha mchakato wa kuandika katiba mpya kuweka mfumo wenye motisha kwa wote ili kuchochea uchumi endelevu na wa viwanda vita dhidi ya rushwa na kukiimarisha chama cha mapinduzi (ccm) kiuchumi
sitta alitangaza nia hiyo jana kwenye ikulu ya wanyanyembe iliyopo itetemia takriban kilomita saba kutoka mjini tabora
ili kukomesha tatizo hilo (la rushwa) hatuna budi kutunga sheria itakayotenganisha biashara na uongozi sitta alisema akiungana na rais jakaya kikwete ambaye pia aliwahi kuahidi kutenganisha siasa na biashara lakini hadi sasa bado hajatunga sheria hiyo
mtu achague moja biashara au uongozi wa siasa ikiwa mfanyabiashara atataka kuingia katika uongozi wa siasa itabidi akabidhi mali na biashara zake kwa mdhamini atakayeziendesha wakati mhusika anatumikia umma alisema spika huyo wa bunge la tisa
alisema mikataba mibovu ya huduma na mauzo ununuzi hewa ununuzi uliojaa unyonyaji uteuzi wa wazabuni kwa rushwa na hasa rushwa katika ajira imelisababisha taifa hasara kubwa
alisema hatua ya pili ya kupambana na rushwa ni kutunga sheria mpya zilizo kali na ambazo zitakuwa na matokeo ya kumzuia mtu asitamani kusaka rushwa
katika hilo tutahakikisha mali za viongozi zinatajwa kwa uwazi mali isiyolingana na kipato na kukosa maelezo ya kutosheleza itaifishwe kesi za rushwa ziwe na utaratibu wenye uwazi alisema mbunge huyo wa urambo mashariki
tume inayoshughulikia maadili ya viongozi ipewe nguvu kubwa za uchunguzi na ufuatiliaji wa mali za viongozi bila kuzuiliwa na mamlaka yoyote pia tume ifanye kazi zake kwa kuyaweka mambo wazi kuhusu watuhumiwa tuhuma zao majibu yao na hatua zinazofuatia vikao vya tume vya kusikiliza mashauri ya maadili viwe vya wazi kwa wananchi
alisema adhabu ya utoaji na wapokeaji rushwa itakuwa kali na iambatane na mali zitakazothibitika kupatikana kwa rushwa zitataifishwa
mji wa dodoma na viunga vyake leo unatarajiwa kuwaka moto baada ya vigogo sita wa chama cha mapinduzi (ccm) watakapokuwa wanachukua fomu ya kuwania urais wa jamhuri ya muungano wa tanzania
vigogo wanaochukua fomu leo ni pamoja na makamu wa rais dk mohamed gharib bilal mawaziri wakuu wastaafu edward lowassa na frederick sumaye waziri wa ujenzi dk john magufuli waziri wa uchukuzi samuel sitta na balozi ali abeid karume
idadi hiyo ya wanaochukua fomu za kuomba kuwania urais itafikisha jumla ya makada 11 wa ccm ambao tayari wamekwisha kuchukua fomu za kuomba ridhaa kwa chama chao kuwania nafasi ya juu ya uongozi nchini
wengine waliochukua fomu jana ni waziri wa kilimo chakula na ushirika steven wasira waziri wa nchi ofisi ya rais (kazi maalum) prof mark mwandosya mbunge wa afrika mashariki makongoro nyerere na balozi amina salum ali
lowassa alitakiwa kuchukua fomu jana lakini aliahirisha kutokana na msiba wa mbunge wa ukonga marehemu eugen mwaiposa aliyefariki dunia usiku wa kuamkia juzi mjini dodoma
kwa mujibu wa ratiba hiyo wa kwanza kuchukua fomu atakuwa siyatemi akifuatiwa na sumaye dk bilal balozi karume lowassa na atakayefunga dimba ni dk magufuli
zaidi ya tembo 10000 katika hifadhi ya ruaharungwa wamepotea ama hawajulikani walipo
akitangaza matokeo ya sensa ya tembo ya mwaka 2014 mjini hapa jana waziri wa maliasili na utalii lazaro nyalandu alisema wataalam wa hifadhi wameshindwa kubaini waliko au nini kimewatokea tembo hao na kulinganisha kupotea huko sawa na ilivyotokea kwa ndege ya malasia machi mwaka huu ambayo haijaonekana hadi leo
sensa hiyo ilifanywa na shirika la taifa la utafiti wanyamapori (tawiri) frankfurt zoological society na vulcan inc katika eneo la kilomita za mraba 268692 ambazo ni sawa na asilimia 283 ya eneo lote la nchi kuanzia mei hadi novemba 2014
maeneo ilikofanyika sensa hiyo ni serengeti tarangiremanyara katavirukwa burigibiharamulo malagarasimuyovosi soulusmikumi na ruaharuangwa mkomazi na saadani
wizara yangu inajipanga kikamilifu kujua sababu za kupotea kwa tembo haoje waliuawa au waliondoka katika eneo la hifadhi kwa kawaida kama kuna idadi kubwa ya vifo vya wanyama kama hiyo kunakuwa na mabaki ya mizoga au mifupa kitu ambacho hakijaonekana tangu kupotea tembo hao alisema
idadi ya tembo katika hifadhi ya ruaharungwa imepungua kutoka 20000 mwaka 2013 hadi kufikia 8272 mwaka 2014
tembo 10000 katika hifadhi ya ruaharungwa hawajulikani walipo na wala mizoga yao haijaonekana wamepotea kama ile ndege ya malasia hali hii inatufanya kuendesha sensa nyingine majira ya kiangazi kuanzia agosti hadi novemba wataalam wanajiuliza kila siku tembo hao wamepotelea wapi hizi ni habari zinazosumbua alisema
aidha alisema matokeo ya sensa hiyo pia yamebaini kuwapo kwa upungufu mkubwa katika mfumo wa ekolojia ya ruaharungwa
akitangaza matokeo ya ujumla ya sensa hiyo nyalandu alisema imeonyesha kupungua kwa tembo kutoka 110000 mwaka 2009 hadi 43330 mwaka 2014
hata hivyo waziri huyo alisema idadi ya tembo imeongezeka kutoka 13000 mwaka 2013 hadi 15217 mwaka jana ongezeko ambalo ni zaidi ya tembo 2000
waziri wa ushirikiano wa afrika mashariki dk harrison mwakyembe ameibuka na kusema hajawahi kumshambulia kwenye mitandao waziri mkuu wa zamani edward lowassa kuhusu sakata la richmond
kauli hiyo ya dk mwakyembe imekuja siku chache baada ya kusambazwa kwa waraka unaodaiwa kuandikwa naye ukimuhusisha na tuhuma za kumshambulia lowassa jambo ambalo amelifananisha kuwa ni sawa na siasa za kitoto
alisema kutokana na kusambazwa kwa waraka ambao umeandikwa nyadhifa zake za ubunge na uwaziri hivi sasa ameshaanza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya watu waliokuwa wakiusambaza
waziri mwakyembe ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mwanahabari alisema anapata shaka hata na baadhi ya vyombo vya habari pamoja na mitandao hiyo na kudai kuwa anamshambulia lowassa
ninashangazwa sana na hii mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari (magazeti) vimekuwa vikiandika vitu vibaya ikiwa ni pamoja na kumshambulia lowassa wakati hata siku moja sijazungumza nao
kitendo cha baadhi ya watu wa aina hii kuwaandika vibaya wanasiasa katika mitandao ya kijamii kwa kutumia majina ya watu wengine ni ishara ya woga wa kisiasa na kushindwa kujiamini katika misimamo yao
kinachonikera kupindukia ni kuwa taarifa hizo sijawai kuziandika ila kuna mtu ama kundi maalumu la watu limeziandika na kuweka jina langu na nafasi zangu za uongozi kama mbunge na waziri huu si uungwana na wala si siasa kwa kuchezea majina ya watu kama siasa zimefika huku basi ni za hatari alisema
dk mwakyembe ambaye pia ni mbunge wa kyela mkoani mbeya alisema katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu watu wanapaswa kuacha woga na kutojiamini
kitendo cha kutumia majina ya watu na kuelezea hisia zao ni kukosa ujasiri na hata yanayosambazwa kwenye mitandao hayaendani na hadhi yangu kiongozi sina tabia ya woga na uongo alisema
alisema baada ya kupata taarifa zilizopo mitandaoni alilazimika kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kitengo cha makosa ya mtandaoni pamoja na mamlaka ya mawasiliano tanzania (tcra) ili kulalalimikia mchezo huo mchafu
dk mwakyembe alisema vyombo hivyo vimeshaanza uchunguzi mkali ili kuwabaini watu walioandika na kutuma taarifa hizo
alisema kutokana na hali hiyo amedhamiria na kuhakikisha kesi ya kwanza ya matumizi mabaya ya mitandao inaanzia kwake kwa kuwa hana utamaduni wa woga na watu wanapaswa kuwa wazi endapo wanakuwa na vitu na si kutumia majina ya watu
dk mwakyembe alisema anashangazwa na watu kutumia jina lake kumchafua kwa kuwa hana tatizo na mtu yeyote na kama chanzo ni suala la richmond ilikuwa ni kazi aliyopewa na bunge
baadhi ya wagonjwa wa hospitali ya taifa muhimbili (mnh) wamelalamikia hatua ya uongozi wa hospitali hiyo kushindwa kuchukua hatua za dharura za kutoa huduma za ctscan ambayo imeharibika kwa kipindi cha miezi miwili sasa
wagonjwa hao walisema wamekuwa wakiteseka kwa kipindi cha miezi miwili sasa bila kupata huduma hiyo
mmoja wa wagonjwa hao aliyejitambulisha kwa jina la rashid omari alisema ni mwezi wa pili sasa amekuwa akienda na kurudi hospitalini hapo bila ya kupata huduma
kila nikifika bado nakutana na bango la ujumbe unaosomeka mashine ni mbovu mafundi wanafanya matengenezo nimekuwa nikienda na kurudi huku tatizo likizidi kukuwa mpaka sasa sijui hatima yangu itakuwaje omari
ofisa uhusiano wa hospitali hiyo aminiel eligaesha alikiri kuharibika kwa mashine hiyo na kusisitiza kuwa tayari uongozi umeshaagiza kifaa cha mashine hiyo kutoka nchini afrika kusini
tunatarajia kifaa hicho kitafika haraka iwezekanavyo ili kuweza kuwapatia huduma ya kipimo cha ctscan wagonjwa wetu wanaokuja kwa ajili ya kufanyiwa kipimo hicho ligaesha
baraza kuu la uongozi la chama cha wananchi (cuf) limemvua uanachama mjumbe wake kutoka mkoa wa shinyanga chifu lutayosa yemba
chifu yemba ambaye pia alikuwa ni mpinzani wa prof ibrahim lipumba katika kuwania uenyekiti wa cuf kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka jana alivuliwa uanachama kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za chama pamoja na kutumia vibaya jina la mwenyekiti wa chama hicho
chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho cha baraza kuu kilichoanza vikao vyake jana jijini dar es salaam kilisema kuwa tuhuma za mjumbe huyo zilifikishwa mbele ya kikao hicho na kufikiwa uamuzi huo
kikao cha baraza kuu bado kinaendelea hapa na ajenda kubwa ilikuwa ni tuhuma dhidi ya chifu yemba ambaye anadaiwa kutumia jina la mwenyekiti wa chama kuanzisha saccos na hata kusababisha chama kudaiwa shilingi milioni 12
lakini pia amekuwa akitumia jina la mwenyekiti wa chama profesa lipumba katika mradi wake huo binafsi ambao anauendesha na hata kusababisha chama kuingia katika mgogoro hasa katika mkoa wa shinyanga kilisema chanzo hicho
chifu yemba alipambana na profesa lipumba katika uchaguzi wa kuwania nafasi ya uenyekiti ambapo alipata kura 30 huku lipumba akishinda kwa kura 659 na kufanikiwa kukiongoza tena chama hicho
chanzo hicho kilisema baada ya kufikiwa kwa uamuzi wa kuvuliwa uanachama kwa mjumbe huyo wa baraza kuu alitolewa nje ya ukumbi kwa ulinzi maalumu hadi nje ya geti na kuondoka
yemba kwa muda amekuwa haelewani na hata kushambuliana katika mitandao ya kijamii na naibu mkurugenzi wa habari na uenezi abdul kambaya ambaye hivi karibuni alishindwa kura za maoni za kuwania ubunge wa jimbo la kinondoni
kutokana na kushindwa huko kwa kambaya kuliibua hisia mbalimbali miongoni mwa wana cuf hali iliyosababisha baadhi ya kikundi cha watu kuandamana na kwenda makao makuu ya cuf kufikisha malalamiko yao kuhusu mwenendo wa uchaguzi kinondoni
alipotafutwa naibu mkurugenzi wa habari wa uenezi wa cuf abdul kambaya alithibitisha kuvuliwa uanachama kwa chifu yemba na kikao cha baraza kuu la uongozi la cuf
related itemsw
← previous story ninazo tayari stori kutoka kwenye kurasa za magazeti ya tz leo june 04 2015 kuanzia udaku hardnews na michezo
next story → michelle na obama mugabe lowassa na rais jk mandela mkapa kwenye pichaz zao za zamani | 2020-06-06T04:54:56 | https://millardayo.com/news0415/ |
makamu wa rais afungua mkutano wa mobile 360 africa jijini dar es salaam ~ blogu ya wananchi ' if(imglength>=1) { imgtag = ' | 2017-08-18T20:19:43 | http://www.lemutuz.com/2017/07/makamu-wa-rais-afungua-mkutano-wa.html |
james sinclair a friend or foe | page 3 | jamiiforums
huko huko kama ndiko nyumbani basi kaa mkao wa kuhama maana rais kishasema afadhali wachimbe dhahabu kuliko kulima
wazee ambao mko interested send me your email nitakuwa nawapatia vitu exclusive na tunaweza kuandika mengine ambayo hatuwezi kuyaanika hapa maana wanasema kwenye kuku wengi i'll keep your contacts in strict confidence mwanakijiji@journalistcom
haki ya nani nitaua mtu atakayegusa kashamba kangu pale kagunga
bila kuwa na nia ya kuundermine hii move hebu wajameni tueleweshane hapa kaswali alikouliza mwanasiasa' ni hisa kiasi gani zinahitajika kuwa kwenye board ya maamuzi
na vipi kama wazalendo wakifanikiwa kuitwaa kampuni hiyo halafu makuwadi wa soko huria wakainyang'anya hizo hati miliki maana kupewa huko siyo kwa sababu ya nia njema bali ni kutokana na wao kutupiwa makombo na huyo mwivi kisha tukasikia tuna tender upya hii kazi iliyokuwa inafanywa na sinclair kisha hapo hapo anarudi sinclair na kampuni nyingine may be this time dowans holding
hivi maneno haya yana ukweli gani
hisa zao zinauzwa toronto new york na london mtanzania yeyote atakayekuwa na hisa huko ujue ana mkono mrefuyaani kishaiba nyumbani kuwekeza kwenye kampuni hiyo huyu jamaa kamwajiri kijana wa george kahama pale dsm na kila mara rais kikwete anapokuja marekani wanakutana sijui wana dili gani lakini kama alivyosema dua huyu ni kibaka wa kutupa mbali
serikali ya awamu ya tatu ilifanya watanzania wote tuwe wajinga kwa hiyo hivi sasa tunaliwa kiulaini na huyu jamaa
this thug cannot be our friend even a single minute ni friend wa mkapa sumaye kikwete na lowassa wakati kikwete alipokohoa kuwa anataka kupitia upya mikataba yote ya madini akanyamazishwa
tanzania pale hatuna sheria kamili ya ardhi bado ardhi nyingi ni mali ya taifa yeye alivyopata haki ya kumilki ardhi yenye madini bado ni kitendawili kweli kweli huu ndio ule ukoloni uliojulikana miaka hiyo ya sabini kuwa ukoloni mamboleo zamani walikuja kwa na kutunyanganya ardhi kwa nguvu na ikilazimika kwa mtutu wa bunduki leo hii wanakuja na kuwalaghai viongozi wetu wapumbavu na kisha kutunyananya ardhi tatizo la afrika limekuwa ni kwenye ardhi miaka nenda rudi ni kama vile sisi wenyewe hatujui matumizi ya ardhi nzuri
wazo la kununua share ni zuri lakini linataka watu ambao wako committed ili kulifanikisha tunaweza kupata angalau watanzania 10 000 ambao wanaweza kuwekeza lets say kila mmoja share 1000 kwa hiyo kila mtu atakuwa na at least canadian $ 6000 kwa bei ya leo ili kuifikia hiyo 2 mwanakijiji mimi naona tuanze kukusanya list tujipange kila mwezi kuanza kununua shares tukijipa muda ie kila mwezi kununua share at least canadian $ 200 kwa wanaojiweza zaidi wanunue zaidi nafikiri tutafanikiwa inabidi tuwe na broker mmoja pale toronto ili asituchaji bei mbaya kwa kila transaction target ikiwa minimum of 1000 shares kwa kuanzia
floated shares zipo 527 376 629 share ambazo ni outstanding ni 86 455 185 ukitaka kuona zaidi symbol ya kampuni hii ni tnx bei ya leo canadian $ 604 kwa share
inabidi tuangalie hizo outstanding shares pengine ndio kwa ajili ya wabongo inabidi kufuatilia hili
tnx ni cboe 10year treasury yield index mimi huwa natafuta stocks kwa kupitia website hii http//wwwmarketwatchcom/ nimejaribu kutafuta hiyo ya tnx sikuiona kama inahusiana chochote na tanzania hebu mwenye kujua symbol kamili ya hii kampuni atuambie
nenda kwenye toronto stock exchange au ftse ya hapa london halafu kuna sehemu wanauliza unataka share zipi utaona mahali wameandika jina la kampuni ausymbol ya kampuni hapo weka tnx halafu utaona hizo bei za leo
au gonga hapahttp//ukmoneycentralmsncom/investor/quotes/quotesaspsymbol=catnx
huwezi kujua nini kinaendelea kwenye kampuni hii kwani wamekuwa wasiri sana ie hata report yao ya mwaka huwezi kuiona mpaka uwe na share kwa hiyo huwezi kujua nani anavuta kamba ngoja mie nitanunua some shares nianze kujua kulikoni na nani ana nini itabidi tuvute subira kwa hili lakini mimi nitanunua tu maana nataka kujua nini kinaendelea hapo
nikisha nunua nitafahamu nani ana nini na kiasi gani
ninavyojua mimi makampuni yanatofautiana lakini kama kampuni iko listed in uk then ni rahisi ukiwa na shares za paundi kumi basi uko entitled kupata taarifa zote za kampuni
sasa mlioko uk mna siku mbili tuu kwani ni muhimu kumuuliza rais akija huko kuhusu hili
kwa taarfa zaidi basi mnaweza kuingia hapa
http//wwwlondonstockexchangecom/engb/pricesnews/prices/priceshelp/
na kama kampuni iko lregisterd in uk basi ni rahisi nadhani unatakiwa kulipia kiasi kidogo tu kupata info zote kuhusus kampuni
http//wwwcompanieshousecom/
na kama hiyo kampuni inatuhuma za unyanyasaji basi mseme kwani ni rahisi kuwaasemea kwa wabunge wao na kuna website maalum ambayo unaweza kumwaga upupu wote kuhusu hiyo kampuni pamoja na watendaji wake
sasa mbaona hamjasema zaidi jinsi mtoto wa george kahama anavyohusiana na hawa jamaa
kwani si alikuwa anafanya kazi pale ubalozi wa ukdar
asante nimeipata ninaweza kuiweka kwenye portfolio yangu wall street kwa kutumia symbol ya catnx au tre tatizo ni kuwa siwezi kupata taarifa kamili za kampuni kama vile analyst information insider actions financial reports na vitu kama hivyo hata hivyo nitajaribu kununua shares kadhaa hasa kwa vile bei yao ni nafuu kweli kwa share naona walianza kuuza share kwe bei ndogo sana chini ya dola moja na bei yao imepanda haraka sana mwaka wa 2005 tu hebu ona chart yao hapa chini
website yao iko hapa kuna mahali jamaa huyu anasema
tanzanian mining laws model for other african countries what a joke
intbasicchartgif
nimeshindwa kusoma ripoti hii nadhani lazime ni signin kwenye website yako
mwlkichuguu
inafunguka hapo panapoonekana unahitajika kusaini usipatilie mananiscrol down utaona kuna sehemu mbili ya kudown load na ya open sasa click kwenye hiyo link ya kufungua utaweza kuisoma inafunguka hata hivyo ni mpaka idownload lakini inafanya haraka
kichuguu kuna kitu hujafanya sawa maana nimejaribu kusign out kila mahala na kuingia humu na kufungua hiyo link na nimeweza kuona so jaribu tena na kama watu wengine mna tatizo hilo hilo basi nitabadilishe baadaye na kuweka kwenye site nyingine kuna habari nyeti kweli na za kushangaza
the attachment is here below zaidi
hapo wa jf mmenena i am in
yaleyale ya carl peters na chief mangungo wa msovero
again we need to focus so far nimepata watu watatu tu kwenye email ambao wako interested hatutafika wa ndugu kama tutaamua kufanya hivi it'll take angalau dola 5001000 kuweza kununua shareskwa kila mtu hatuna harakatukitaka kufanya hivi by june basi tujiandae how we gonna do that tutaamua but the first thing is committment and if you think you can put aside that amount of money until juneukisave angalau $5000 a week from march to the end of may you'll hava at least $650 na tukipata angalau watu 50 tu we'll be able to invest about $32500 sawa na karibu shilingi milioni 42 is that idealistic of course is that overtly ambitious absolutely is it doable you betcha are there about 50 tanzanians out there willing to do this in two days i got three watanzania wangapi wako members hapa jf 808 ambao wako active 270 kati ya hao waliotembelea leo peke yake hadi saa 300asubuhi ni 52 now you guys tell me am i too optimistic probably
i am in too tutawasiliana
ili tuweze kufanikiwa tusiwe na wasiwasi wa fedha kwanza moyo na kujiandaa ndilo la msingi
a tujue idadi ya watanzania ambao wako tayari kuingia na kununua hisa (wapo tayari watanzania wenye hisa kwenye kampuni hiyo) tunataka kuhakikisha kuwa wengi wenye hisa kwenye kampuni hiyo kama mtu mmoja mmoja ni watanzania
b tukishajua tuko wangapi ambao tuko tayari kuanza kuweka akiba ya kati ya dola 500 na 1000 basi tunakubaliana wakati muafaka wa kuamua hatua inayofuata
kama hatuwezi kupata angalau watu 50 it is not worthy it
c tutajaribu kuwapata watu wa nico au tuf tuone kama na wenyewe wanaweza kuwa wana hisa
pesa zinazochumwa nchini mwetu zirudishwe kwetu
debate james baldwin debating william f buckley at cambridge union 1965 jamii intelligence 3 oct 23 2019
james 'whitey' bulger jambazi sugu aliyehusishwa na mafia marekani afariki kwa njia ya kushangaza gerezani jamii intelligence 2 nov 8 2018
kutana na james hobson injinia anayetengeza characters wa marvels & dc comics video games kuwa halisia jamii intelligence 130 aug 6 2018
kwanini kazi nyingi za kijasusi ni za kifamilia (familyfriendly) jamii intelligence 47 jul 13 2018
debate james baldwin debating william f buckley at cambridge union 1965
kwanini kazi nyingi za kijasusi ni za kifamilia (familyfriendly)
threads 1379065
members 525302
posts 33733605 | 2020-01-19T04:00:07 | https://www.jamiiforums.com/threads/james-sinclair-a-friend-or-foe.1747/page-3 |
as vita wa tatu kagame yanga na azam nyasi zinaipata fresh hivi sasa bin zubeiry sports online as vita wa tatu kagame yanga na azam nyasi zinaipata fresh hivi sasa bin zubeiry sports online
mwanzo > untagged as vita wa tatu kagame yanga na azam nyasi zinaipata fresh hivi sasa
as vita wa tatu kagame yanga na azam nyasi zinaipata fresh hivi sasa
fainali ya klabu bingwa ya soka afrika mashariki na kati kombe la kagame kati ya yanga sc na azam fc inaendelea hivi sasa uwanja wa taifa dar es salaam baada ya kumalizika kwa mechi ya kusaka mshindi wa tatu as vita ya jamhuri ya kidemokrasia ya kongo (drc) ikiifunga 21 apr ya rwanda
mechi kati ya yanga na azam inachezeshwa na refa thierry nkurunzinza kutoka burundi akisaidiwa na simba honore wa rwanda na peter sabatia wa kenya wakati mezani atakaa issa kagabo wa rwanda kamisaa hassan amir wa somalia na mtathmini wa marefa ni anangwe robert wa kenya
yanga sc ally mustafa barthez stefano mwasyika oscar joshua nadir haroub cannavaro kevin yondan athumani iddi chuji rashid gumbo haruna niyonzoma said bahanuzi hamisi kiiza na david luhende benchi shamte ally juma seif ladislaus mbogo idrisa assenga na jerry tegete
azam fc deo munishi dida ibrahim shikanda erasto nyoni said mourad aggrey morris jabir aziz kipre tcheche salum abubakar john bocco adebayor ibrahim mwaipopo na ramadhan chombo redondo benchi mwadini ally samir haji nuhu joseph owino george odhiambo mrisho ngassa khamis mcha vialli na gaudence mwaikimba
item reviewed as vita wa tatu kagame yanga na azam nyasi zinaipata fresh hivi sasa rating 5 reviewed by mahmoud bin zubeiry | 2020-05-25T04:29:08 | http://www.binzubeiry.co.tz/2012/07/as-wa-tatu-kagame-yanga-na-azam-nyasi.html |
mhbalozi mpya wa tanzania washington dc apokelewa na watanzania wa dc | sunday shomari
home karibu mhbalozi mpya wa tanzania washington dc apokelewa na watanzania wa dc
by sundayshomari september 18 2010 0 259 share on facebook
tweet mheshimiwa balozi wa tanzania mwanaidi maajar akiwasili nyumbani kwake bethesda maryland baada ya kukabidhi hati zake white house huku pembeni yake akitazama ni bwsuleiman saleh(suti nyeusi) share thisclick to share on twitter (opens in new window)click to share on facebook (opens in new window)click to share on google+ (opens in new window)
tweet previous articlenext articlekibaki ailaumu jumuiya kimataifa kuhusu somalia sundayshomari related articlesmore from author
rais magufuli alipozungumza na wawakilishi wa umoja wa sekta binafsi tanzania december 3 2015 kesi ya talaka ya mmiliki wa stmathew yaahirishwa tena august 30 2015 mke wa rais nigeria amuumbua mume wake hadharani october 15 2016 kenya tanzania bussiness forum in nairobi october 10 2015 load more uchaguzi 2015 | 2017-07-26T22:26:53 | http://sundayshomari.com/mh-balozi-mpya-wa-tanzania-washington-dc-atoa-wito-kwa-jumuiya/ |
mbeya city sasa yaamua kurudisha 'majembe' yake yalioondoka | boiplus blogspot
» mbeya city sasa yaamua kurudisha 'majembe' yake yalioondoka mbeya city sasa yaamua kurudisha 'majembe' yake yalioondoka a+
mbeya city ipo kwenye mchakato wa mwisho wa kumrudisha mchezaji wao deo julius ambaye anakipiga katika timu ya kagera sugar inayoshiriki ligi kuu bara
kagera sugar ilimsajili mchezaji huyo kutokea city baada ya kushindwa kumpa mkataba mpya baada ya ule wa awali kumalizika na hivyo kuuamua kujiunga kagera kwa mkataba wa mwaka mmoja
deo julius
mchezaji huyo ambaye kwasasa yupo jijini mbeya ameiambia boiplus kuwa tayari mazungumzo ya pande mbili mbeya city na kagera sugar ya kuvunja mkataba wake yanaendelea vizuri na huenda akasaini mkataba muda wowote kuanzia sasa
deo amesema kuwa kikubwa anachokiangalia ni fedha na wala hachagui wapi afanye kazi kwani mpira ndio ajira yake hivyo haoni tatizo kurejea kwenye timu yake ya zamani
''ni kweli nitarudi mbeya hapa nasubiri viongozi wa mbeya city wamalizane na viongozi wangu wa kagera maana kule nina mkataba sina tatizo kurudi city kwani ninachokiangalia sasa ni masilahi na kucheza soka ndiyo ajira yangu'' alisema deo | 2016-12-03T09:36:37 | http://boiplus.blogspot.com/2015/11/mbeya-city-sasa-yaamua-kurudisha.html |
madereva makodakta wa daladala wenye lugha chafu kukamatwa
20 september 2019 friday 1004
mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa ardhini kanda ya nyanda za juu kusini (latra) imesema inawachunguza na itawachukuli hatua za kisheria madereva na makondakta watakaobainika kutumia lugha chafu kwa abiria
meneja wa latra kanda hiyo denis daudi amesema hatua hiyo inafuatia baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa abiria wanaodai tiketi wanaposafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine ndani na nje ya jiji la mbeya
kodakta au dereva hapaswi kukiuka sheria na taratibu zilizoweka ikiwamo kutoa lugha chafu kwa abiria naomba abiria wanapopata shida hii walete malalamiko yao katika ofisi yetu na hata kwa askari wa barabarani (trafiki) amesema na kuongeza
sheria ipo na kwa mujibu wa sheria adhabu atakazokutana nazo dereva au kodakta ni kutozwa faini ya sh 50000 au kufikishwa mahakamani
abiria wanaosafiri kutoka stend kuu ya mabasi ya mikoani kuelekea katika mamlaka ya mji mdogo wa mbalizi na kutoka sokomatola kwenda uyole wamelalamikia kuwepo kwa baadhi ya makondakta kutokuwa wastaarabu na kutumia lugha za kejeli pindi wanapodaiwa tiketi
tumpale saimon amesema ipo haja ya vyombo husika kufanya uchunguzi na kuwawajibisha ili waweze kutambua majukumu yao na kutii sheria bila shuluti
gwamaka fredy mkazi wa iyunga ameishauri serikali kufanya usajili wa makondakta na madereva pamoja na wamiliki wa makampuni waliyowaajiri ili yanapojitokeza majanga hususan ya ajali ukikwaji wa sheria iwe rahisi kuwabaini na kuwafikisha katika vyombo vya sheria | 2019-10-18T16:20:17 | http://www.azaniapost.com/habari-maalum/madereva-makodakta-wa-daladala-wenye-lugha-chafu-kukamatwa-h24462.html |
love created by naisha listen
playlist creator naisha
1 missing me (remix) 615 exclusive305
naisha has no other uploads | 2018-10-17T07:32:18 | https://audiomack.com/playlist/naisha-21/love |
discussion in 'jukwaa la elimu (education forum)' started by persie aug 22 2012
kachaguliwa st john's ya dar (st mark's) baf lakini yupo saut anapiga pre entry programme bba in procurement anaomba ushauri aende wapi na wapi kuna soko kubwa la ajira
nenda baf kijana
aiseee baba yangu mi nadhani ungekwenda tcu ukaombe wakupe ushauri coz pale ndipo kwenye wataalamu
unamuombea dogo ushauri akili kumkichwa yeye hajui cha kufanya
alie soma/anaesoma st john hiyo baf funguka kuhusiana na quality yake ukilinganisha na baf ya vyuo vingine kama mzumbe na muccobs
koromeo said
unamuombea dogo ushauri akili kumkichwa yeye hajui cha kufanya[/q
ndo jibu anko zote anapenda bt hajui yenye opportunity costs kubwa na ndogoclick to expand
aiseee baba yangu mi nadhani ungekwenda tcu ukaombe wakupe ushauri coz pale ndipo kwenye wataalamuclick to expand
nenda baf kijanaclick to expand
quality vp ukilinganisha na ya vyuo vingine
dogo bongo hapa kwa sasa procurement hiko juu asikwambie mtu nakushauri ukasome hiyo manunuzi prokyuament mana sio vyuo vingi vinafundisha hiyo pia ukiangalia hata serikialini wametilia mkazo swala la procurement
nikwambie dogo baf bcom bachelor of accounting ni kitu kimoja kuna maelfu na maelfu ya watu katika field hizo pia kutoka katika field hiyo ni kujuana au kama wewe ni kichwa kweli kichwa cha kupata first class au upper second kali ambazo hizo ni za ma tooo kasome manunuzi mdogo wangu usije ukatusumbua mtaani hela ya kula
nikwambie dogo baf bcom bachelor of accounting ni kitu kimoja kuna maelfu na maelfu ya watu katika field hizo pia kutoka katika field hiyo ni kujuana au kama wewe ni kichwa kweli kichwa cha kupata first class au upper second kali ambazo hizo ni za ma tooo kasome manunuzi mdogo wangu usije ukatusumbua mtaani hela ya kulaclick to expand
tatizo lenu vijana ni kwamba nyote by instinct ni mafisadi hata kama post zenu nyingi hapa ni za kulaani mafisadi mnalaani kwa vile hamjapata nafasi ya kuingia lakini malengo yenu ni kujiunga katika kundi la mafisadi financial sector hapa tz ni kubwa na inaendelea kukuwa na kuwa diversified kwa hiyo kama unayo baf 'worth the salt' prospect ni nyingi lakini ni sector inayoangalia vichwa siyo makaratsi | 2016-10-24T07:19:15 | http://www.jamiiforums.com/threads/naomba-ushauri-wako.311935/ |
wakulima wafanyakazi wa mkonge walia kwa dc korogwe msumba news blog
wakulima wafanyakazi wa mkonge walia kwa dc korogwe
baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha mkonge hale kilichopo chimi ya kampuni ya katani ltd wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya korogwe kissa kasongwa (hayupo pichani) alipofika kiwandani hapo kuzungumza nao (picha na yusuph mussa)
mkonge huu wa mmoja wa wakulima wa shamba la mkonge hale wilayani korogwe ambao umeharibika unadaiwa kuvunwa mei 3 2019 kisha kutelekezwa ukiwa shambani
baadhi ya wafanyakazi na wakulima wa shamba la mkonge hale lililopo wilaya ya korogwe mkoani tanga wamelalamika kuwa hawaridhiki na mwenendo wa chama cha ushirika wa wakulima wa mkonge hale (amcos)
walitoa dukuduku lao juzi mbele ya mkuu wa wilaya ya korogwe kissa kasongwa alipotembelea kiwanda cha mkonge hale kilichopo chini ya kampuni ya katani ltd ili kusikiliza changamoto za wafanyakazi ikiwa ni muendelezo wa kutembelea viwanda vya mkonge vya magoma mwelya ngombezi magunga na hale
mkuu wa wilaya mimi nilipewa kazi ya usimamizi na amcos ya hale ya kusimamia wakataji na kuwalipa na kazi hiyo ya malipo nilikuwa naifanya kila jumamosi lakini nilisimamishwa kazi baada ya kuambiwa nimepoteza mkonge wa wakulima nataka kusema mbele yako mkonge ulikuwepo na meta zilizokatwa zilikuwa sawa lakini kuna watu ili kunihujumu walichukua baadhi ya mkonge huo na kwenda kuutupa ili meta zangu ziwe pungufu
bado kuna mkonge mwingine umebaki eneo hilo kwani una muda mrefu ulikuwa umekatwa (tangu mei 3 2019) lakini ulishindwa kusombwa kwa wakati ili uweze kufikishwa kiwandani hofu yao ni kuwa mkonge huo ungeletwa kiwandani wakati muda umepita mkonge wake ungekuwa wa daraja la chini sana mkuu wa wilaya nipo tayari kuweka mafuta kwenye gari lako ili ukaone mkonge huo uliotelekezwa shamba alisema omar chuma
mkulima emmanuel cossam alisema mkonge wake haujakatwa kwa muda mrefu huku yeye akiwa na matatizo mbalimbali ikiwemo kumuuguza baba yake hivyo kumuomba mkuu wa wilays aweze kumsaidia ili mkonge wake ukatwe
mimi nimekuwa nalia na uongozi wa amcos wanisaidie namna ya kukata mkonge ili nimuuguze baba yangu mzazi ambaye anaumwa ugonjwa wa tezidume lakini sasa ni muda mrefu na kilio changu hakijasikilizwa hivyo mkuu wa wilaya naomba unisaidie kwa hilo alisema cossam
kasongwa alitaka kujua uongozi kama unayajua malalamiko hayo huku akiagiza uongozi wa amcos pamoja na kuwa wanakata mkonge kwa zamu lakini mkulima anaeuguliwa na baba yake apewe kipaumbele ili aweze kumuuguza mzazi wake
korogwe ndiyo wilaya inayoongoza kwa kilimo cha mkonge tanzania nzima naomba sifa hizo ziendane na hali halisi sio watu tunasifiwa nchi nzima halafu wakulima na wafanyakazi wake wa mkonge choka mbaya nataka kampuni ya katani ltd na amcos muhakikishe mnawalipa kwa wakati wakulima na wafanyakazi wa mkonge alisema kasongwa
hata hivyo kasongwa aliipongeza kampuni ya katani ltd kwani katika viwanda vitano vya kusindika mkonge vya hale mwelya ngombezi magunga na magoma kiwanda cha hale wafanyakazi wanadai mshahara wa nusu mwezi wa agosti mwaka huu tena ni kwa sababu katani ltd hawajalipwa sh milioni 18 na amcos
wafanyakazi wa katani ltd niseme ninyi hapa mna maisha mazuri tofauti na wenzenu huko kote nilikopita ninyi peke yenu ndiyo mnadai fedha kidogo tangu utaratibu mpya umeanza wa kuwa chini ya amcos tena mnadai nusu mwezi nina hakika baada ya katani ltd kulipwa hizo fedha nao watawalipa mshahara wenu alisema kasongwa
meneja wa kiwanda cha mkonge hale nassoro mpate alisema wanaidai amcos sh milioni 18 huku mwenyekiti wa amcos hale abdallah kamili akikiri deni hilo na kudai wangelipa fedha hizo kwa katani ltd wiki hii ili nao wawalipe wafanyakazi
kamili aliahidi kushughulikia malalamiko hayo ya wakulima na wafanyakazi huku akiahidi kumpa kipaumbele cossam ili avuniwe mapema mkonge wake ili aweze kumuuguza mzazi wake na huku akiahidi kufuatilia suala la mkonge kutupwa na mwingine kuachwa shamba wakati ulishakatwa
akizungumza na mwandishi wa habari hizi sept 5 kamili alisema hana uhakika na tuhuma zilizotolewa kuhusu mkonge kutupwa porini na mwingine kuachwa shambani lakini kesho jumamosi (sept 7) kamati ya nidhamu ya amcos hale itakaa na wahusika ili kuweza kujua ukweli wa jambo hilo
mwandishi unaposema una ushahidi wa picha ya mkonge uliotupwa ama kuachwa shamba mimi hilo siwezi kuthibitisha unajuaje kama huo mkonge ni wa sehemu hiyo ili kupata ukweli wa hilo kamati ya nidhamu ilikuwa ikae leo (jana) lakini kutokana na vikao vingi hapo korogwe kikao hicho kitafanyika jumamosi alisema kamili | 2019-11-15T08:18:10 | http://www.msumbanews.co.tz/2019/09/wakulima-wafanyakazi-wa-mkonge-walia.html |
religious jamii islam
moja ya siku muhimu sana katika kalenda ya kiislamu ni eid alfitr husherekewa siku mbili kuhitimisha mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani ambao hudumu kwa mwezi mmoja tuangalie kwa umakini tamaduni za sikukuu hii ambazo kwa asili yake husherekewa na familia na jamii 1 eid alfitr inaashiria mwisho wa ramadhan eid alfitr hufanyika siku ya []
waumini wa dini ya kiislamu popote walipo katika kipindi hichi cha kusherehekea uzawa wa kiongozi wa dini hiyo ulimwenguni mtume muhammad { saw } wana wajibu wa kupitisha maazimio ndani ya nafsi zao ya kuachana na maovu na kukumbatia mema yote kama alivyokuwa akiyahubiri kiongozi huyo wakati wa uhalifa wake makamu wa pili wa rais []
mwenyekiti wa mwinyi baraka islamic founation sheikh issa othoman issa imamu wa msikiti wa maamuru upanga ( wa kwanza kutoka kushoto) akimkabidhi mshindi wa kwanza wa shindano la quran kwa njia ya tajweed rajei ayob funguo ya pikipiki | 2020-08-13T08:54:56 | https://www.jamiiislam.co.tz/category/religious/ |
uandikishaji daftari la wapiga kura bado bbc news swahili
uandikishaji daftari la wapiga kura bado
http//wwwbbccom/swahili/habari/2015/02/150212_tanzania_bvr
image caption nembo ya tume ya uchaguzi tanzania chini yake ni mwanamke mmoja akimsaidia mwenzake kumwonyesha sehemu ya kupiga kura
tume ya uchaguzi nchini tanzania imesogeza mbele kwa wiki moja zaidi tarehe ya kuzinduliwa kwa zoezi la daftari la wapiga kura litakalotumia mfumo mpya wa kieletroniki yaani biometric voters registration bvr zoezi hilo ambalo litaanza rasmi katika mkoa wa njombe na baadae kufuatia katika mikoa mengine ya tanzania hivi sasa linatarajiwa kuanza tarehe 23 ya mwezi huu badala ya tarehe 16 kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali
mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo amesema lengo la mabadiliko hayo ni kuvipa fursa vyama vya kisiasa kujiandaa na kuandaa watu wake hata hivyo baadhi ya viongozi wa vyama vikuu vya kisiasa wamesema kauli hiyo haina ukweli wowote na kwamba tume inajikosha kwa sababu haina vifaa vya kutosha vya kuendesha uandikishaji huo mwandishi wa bbc aboubakar famau kutoka dar es salaam ametuandalia taarifa ifuatayo
wakati ikiwa imesalia miezi miwili tu na wiki kadhaa kabla ya tarehe iliyopangwa ya kupiga kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa wasi wasi unazidi kutanda miongoni mwa viongozi mbali mbali wa vyama vya kisiasa hapa nchini tanzania iwapo tume ya uchaguzi nchini humu itaweza kuboresha daftari la wapiga kura katika kipindi cha muda mfupi uliobakia baadhi ya viongozi hao wamesema kwamba licha ya tume hiyo kutovishirikisha vyama vya kisiasa katika baadhi ya maamuzi yake lakini pia wamebaini kwamba mpaka sasa tume hiyo inakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya uandikishaji kwa sababu havijaingia nchini kama ambavyo anabaini freeman mbowe mwenyekiti wa chadema
image caption ibrahim lipumba mwenyekiti wa cuf
mfumo huyo mpya kwa tanzania wa bvr utaigharimu tume kiasi cha fedha za kitanzania shilingi bilioni mia mbili na tisini na tatu ambazo mpaka sasa haijafahamika iwapo fedha hizo zimepatikana au la kwa upande wake prof ibrahim lipumba ambae ni mwenyekiti wa chama cha wananchi cuf anaelezea kuwa kukosekana kwa utaalam miongoni mwa wafanyakazi wa tume kunaweza kuwa kikwazo cha kufanikisha zoezi hilo
hata hivyo jaji damian lubuva ambaye ndiye mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini tanzania anasema madai hayo ni uoga wa wanasiasa ambao hawataki mabadiliko katika mifumo ya uchaguzi
uandikishaji wapigakura umepangwa kufanyika nchi nzima kwa muda wa siku sitini kuanzia mkoani njombe tarehe 23 mwezi huu ambapo watanzania zaidi ya milioni 23 wanatarajiwa kujitokeza katika uandikishaji huo hata hivyo kwa mujibu wa wachambuzi wa mambo haijafahamika iwapo raia wengi watajitokeza kwa sababu kazi ya kuwahamasisha raia bado haijafanyika na vile vile baadhi ya watanzania wanaweza kuikosa fursa hiyo ikizingatiwa ni msimu wa wakulima kuingia mashambani kabla ya mvua za masika aboubakar famau dira ya dunia bbc dar es salaam | 2018-05-24T11:08:07 | http://www.bbc.com/swahili/habari/2015/02/150212_tanzania_bvr |
triton apdata msimamizi wa mafunzo ya kozi katika gurgaon
triton apmsimamizi wa data mafunzo ya kozi katika gurgaon
triton apdata msimamizi mthibitishaji wa kozi ya gharama katika gurgaon
taasisi ya triton apdata administrator kozi katika gurgaon
triton apdata msimamizi wa mafunzo katika gurgaon
triton apdata msimamizi mtihani wa kozi katika gurgaon
triton apdata msimamizi mtaalam wa kozi katika gurgaon
bora triton apdata msimamizi wa mafunzo ya kozi online
triton apmtawala wa data mafunzo ya kozi
katika kozi hii utajifunza jinsi ya kupima kupelekwa kwa sasa jinsi ya kusimamia sera na ripoti kushughulikia matukio na mwisho kuboresha na kusimamia mfumo wa apdata utakuwa na ujuzi wa kuunda sera za data kujenga vigezo vya desturi na kutumia sera zilizopangwa usimamizi wa tukio taarifa na usanifu wa mfumo na matengenezo
maarifa makali ya suite ya tcp / ip
maarifa ya firewall
inakubaliana na apweb na apemail
kuepuka trafiki na mlinzi
uvumbuzi na serikali za apdata
shughuli ya maisha ya maisha
mbinu ya uumbaji wa sera za dlp
vipengee rahisi
maandiko na vigezo vilivyotanguliwa
watumiaji & mwisho
mwisho wa takwimu
matukio na taarifa
ufuatiliaji wa kazi ya matukio ya juu
admins zilizowekwa
hitilafu ya hatua
upatikanaji wa juu wa meneja wa apdata
tahadhari matukio ya mfumo | 2018-09-23T12:11:48 | https://itstechschool.com/sw/course/triton-ap-data-administrator-course/ |
dira yangu museveni aanza kuonesha dalili za udikteta
ukisikia hakuna demokrasia basi ndio hapa uganda kweli museveni amemtia kizuizini mpinzani wake mkuu ambaye amekuwa akidai museveni ni dikteta
huku akiwa jela jana washtakiwa wengine wanaoshtakiwa naye walipewa dhamana ya bei mbaya dola elfu sita kwa kila mmojapamoja na kwamba hela hiyo ililipwa lakini hawakuweza kutoka kwani wanajeshi walifika na kuiteka mahakama wakidai wanataka kuwakamata hao jamaa somahapa jamaa wakiongozwa na wanasheria wao walikataa kutoka na kuwa huru na wakabaki gerezani kwani haijulikani wanajeshi walitaka kuwapeleka wapi
nakwambia dalili za udikteta zimeanza kujionesha hapalakini yote hii imemuongezea umaarufu dr besyige mpinzani mkuu wa museveni
museveni jana alikutana na mabalozi wa nchi za majuu na akawatisha kwelikweli kuna kila dalili ya museveni kuchokwa na waganda wengi lakini yeye sasa ameamua ni ubabe tu somahapa
ila ningependa pia msome makala moja nzuri sana ambayo inaeleza ni kwa vipi kumtia kizuizini besyige kuna athari kadhaa na ni kwa vipi kunachangia demokrasia ya nchi hii iliyotawaliwa na wanajeshi somahapa
posted by innocent kasyate at 439 am | 2018-03-22T19:44:20 | http://funguajicho.blogspot.com/2005/11/museveni-aanza-kuonesha-dalili-za.html |
nyumba inauzwa ipo kigamboni kibada dar es salaam dar es salaam
nyumba inauzwa ipo kigamboni kibada dar es salaam private
price 60000000tsh00
nyumba inauzwa ipo kigamboni kibada nyumba ya vyumba 3 vya kulala stininroom dining room kitchen stoo toilet parkin umeme upo maji yapo nyumba full tairizi nyumba aipo mbali na barbara ya rami km dk 5 kwa miguu kufika k nyumba nyumba hati ya ke ya serekali ya mtaa nyumba ukubwa wa kiwnja sqm 400 nyumba ipo vinzuri nyumba mpya kwenda saiti chaji ya dalali elufu 20
nyumba inauzwa ipo kigamboni kibada listings360 nyumba inauzwa ipo kigamboni kibada listings360 kawambwa property sales rentals listings360 property sales rentals dar es salaam le bon coin property sales rentals dar es salaam listing property sales rentals dar es salaam let go property sales rentals dar es salaam property sales rentals dar es salaam houses for sale listings360 houses for sale dar es salaam le bon coin houses for sale dar es salaam listing houses for sale dar es salaam let go houses for sale dar es salaam houses for sale dar es salaam listings360 dar es salaam
p 6 months ago real estate & property ✅ property for sale dodoma
nyumba inauzwa ipo mbande dar es salaam
nyumba inauzwa ipo mbondore dar es salaam
nyumba inauzwa ipo magole dar es salaam
nyumba inauzwa ipo kigamboni dar es salaam
nyumba inauzwa ipo tabata ruiti dar es salaam
nyumba inauzwa ipo chanika mwisho dar es salaam
nyumba inauzwa ipo kigamboni geza dar es salaam
nyumba inauzwa ipo mbagala kwa dar es salaam
nyumba inauzwa ipo kitunda kivure dar es salaam | 2020-04-06T14:14:11 | https://listings360.co.tz/nyumba-inauzwa-ipo-kigamboni-kibada-dar-es-salaam/9432874.html |
jack ma | jamiiforums
hii ni aibu kubwa ndege tumenunua kwa keshi vifaa vya kupambana na corona tumesubiri msaada wa jack ma
ni aibu kubwa eti nchi kubwa kama hii ambayo tumejitapa kujenga nchi kwa pesa zetu na kuwa hatuhitaji misaada leo hii tumeshindwa kununua vifaa vya kupima na kujilinda na corona mpaka tumesubiri msaada wa jack ma tatizo hapa sio kupokea msaada tatizo ni kubweteka na kusubir msaada wiki
first deals under continental freetrade pact planned for july ma wants africa entrepreneurs to be celebrated as heroes jack ma the cofounder of alibaba group holding ltd said african entrepreneurs will find countless opportunities in ecommerce logistics and epayments as the continent
jack ma anasema kwamba
kuwa na degree au kuwa na phd haimaanishi kuwa unaweza au unafahamu kila kitu kila siku kuwa mtu wa kujifunza kutoka kwa watu wanaokuzunguka kila siku katika maisha yako ya kila siku hasa kwa jamii inayokuzunguka kuna elimu zaidi ya iyo degree yako au phd yako usipende kujiona kama muweza wa | 2020-04-05T19:47:34 | https://www.jamiiforums.com/tags/jack-ma/ |
wabunge filikunjombe na mngongo wasimikwa kuwa walezi wa uwt ~ uvccm blog thumbnails===nvarscontrolnav&&0===nvarsthumbcaptions){var c=sattr(datathumbcaption)==c&&void 0==c&&(a+=''+c+)}ncontrolnavscaffoldappend(
home » » wabunge filikunjombe na mngongo wasimikwa kuwa walezi wa uwt
wabunge filikunjombe na mngongo wasimikwa kuwa walezi wa uwt
mbunge filikunjembe na mafulu wakipongezwa kwa kuteuliwa walezi wa uwt njombe
dr suzana kolimba wa tatu kushoto akipongezwa kwa mchango wake uwt
walezi wa uwt mkoa wa njombe mbunge wa ludewa deo filikunjombe ( kulia ) na mbunge wa viti maalum mkoa wa iringa lediana mafulu wakipongezana kwa kuteuliwa kuwa walezi wa uwt mkoa wa njombe
wabunge filikunjombe na lediana wakiwa katika pozi
chanzomjengwablog | 2018-07-22T09:00:11 | https://uvccmtz.blogspot.com/2014/08/wabunge-filikunjombe-na-mngongo.html |
wee tafuta mkwanja kwa juhudi zote prezzos girlfriend amber lulu offers hamisa mobetto support priority10news | exclusive east africa newsentertainment and technology
home / celebrities & gossip / entertainment / wee tafuta mkwanja kwa juhudi zote prezzos girlfriend amber lulu offers hamisa mobetto support
wee tafuta mkwanja kwa juhudi zote prezzos girlfriend amber lulu offers hamisa mobetto support
unknown 6/13/2018 0
hamisa mobetto come under heavy fire from diamond platnumzs family when a new song iyena was released the music video showed diamond and zaris wedding
hamisa was forced to call out diamond on social media for failing to defend her against attacks from members of his family including his mother and sister
lakin ndugu zako hawabebeki its too much talk to your familia maana wewe ni mwanaume na uwezo wa kunyamalizana pia waambie unahitaji mke sio house girl wa nyumbamwanamke kazi yake kukupikia ule nk au nlikua sikupikii tena sio wewe tu na ndugu zako mkala na kusanza leo imekua hamisa hajui kupika kusafisha nyumba kwahiyo chumba chako tukimaliza lalana huwa anasafisha nani au walitala niende kwafulia vyupi vyao nikimaliza niwapigie deki mpaka chumbani kwao wakishindwa kuniheshimu basi waambie waheshimu damu yako wrote hamisa mobetto on instagram
prezzos girlfriend amber lulu has come out to offer her support to hamisa mobetto the popular video vixen encouraged mobetto to ignore the distractions from haters and focus on making money
mimi namuamini sana mobetto na ninajua kwamba ni mwanamke anayejiamini kwa kila kitu kwa hivyo hili lililomtokea ni changamoto tu katika maisha niseme tu kwamba yeye aendelee na biashara zake kwa nguvu zote na kufanya kazi ili aweze kulea familia yake achukulie hii ndio changamoto ya yeye kukaza buti na kutafuta mkwanja kwa juhudi zote mwanaume kama anampenda atarudi tu said amber lulu during an interview with star showbiz | 2019-06-19T03:31:53 | http://www.priority10.ml/2018/06/wee-tafuta-mkwanja-kwa-juhudi-zote.html |
seoul korea kusini yaanza juhudi za kuwakoa mateka wake | habari za ulimwengu | dw | 26072007
seoul korea kusini yaanza juhudi za kuwakoa mateka wake
korea kusini imeanza juhudi za kidiplomasia kuwaoka mateka wake 22 wanaozuiliwa na watekaji nyara nchini afghanistan mjumbe wa korea kusini baek jong chun ameondoka leo mjini seoul kwenda afghanistan
baek jong chun ni katibu mkuu anayehusika na sera za kigeni na usalama katika ofisi ya rais na amekwenda afghanistan kama mjumbe maalumu wa rais wa korea kusini roh moo hyun
ziara yake inafanyika kufuatia kuuwawa kwa mateka mmoja miongoni mwa mateka 23 waliotekwa nyara na wanamgambo wa taliban
korea kusini imelaani vikali kuuwawa kwa mchungaji wa kanisa la kiprotestanti la presbiteri mjini seoul bae hyungkyu aliyekuwa akiwaongoza wenzake kufanya mradi uliodhaminiwa na kanisa hilo nchini afghanistan
taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais wa korea kusini roh moo hyun imesema mauaji ya raia asiye na hatia ni kitendo kiovu ambacho hakiwezi kuhalalishwa kwa sababu yoyote ile na wala hakiwezi kuvumilika
msemaji wa taliban qari mohammed yousuf amesema leo mateka wote 22 wako salama kufuatia ahadi waliyopewa na serikali kwamba suluhisho la amani litapatikana kuhusiana na swala hilo
kiungo https//pdwcom/p/cbey | 2018-08-19T14:38:56 | https://www.dw.com/sw/seoul-korea-kusini-yaanza-juhudi-za-kuwakoa-mateka-wake/a-2904760 |
john mnyika uzinduzi wa mradi wa kinamama mji mpya
posted by john mnyika at 1141 pm
nasimama na wabunge na makamanda wetu waliokamatwa | 2019-08-23T00:02:30 | http://mnyika.blogspot.com/2017/12/uzinduzi-wa-mradi-wa-kinamama-mji-mpya.html |
pinda wa zamani wa kituo cha disney anasema amedhulumiwa na wapiga picha wa hollywood martin vrijland
chanzo wanafunzi wa wanafunzi com
nyota wa zamani wa kituo cha disney ricky garcia amekuwa nyota mpya ya watoto kulipua filimbi ya mlipuko wa ugonjwa wa hollywood anamtuhumu meneja wake wa zamani kuwa amemnyanyasa kingono kwa miaka na kuruhusu vibuni vingine vya hollywood kumtumia kama toy ya ngono garcia alidai kwamba dhuluma ya joby harte ya hot rock media ilianza wakati alikuwa na umri wa miaka 12 tu kulingana na ripoti iliyochapishwa na ukurasa wa sita alhamisi dhuluma hiyo iliendelea kwa miaka kadhaa baadaye kesi ya korti katika korti kuu ya kaunti ya la ilidai (ona hapa) kwa bahati nzuri aina hiyo ya kitu hufanyika tu huko amerika kwa sababu tumesahau kituo chetu cha huduma cha mchana cha amsterdam robert m ni nani walikuwa wanunuzi wa wale watoto waliodhulumiwa tena
tunaanza kuzoea kwanza jimmy savile nchini uingereza kisha jeffrey epstein huko merika na sasa kesi hii tena kwa kweli sisi wenyewe tulikuwa na katibu mkuu wa haki ambaye alishutumiwa kwa pedophilia (joris demmink) lakini hiyo haijawahi kuthibitika kuwa ngumu kwa hivyo huko uholanzi sio mbaya sana mbali na ukweli kwamba mitandao kubwa ya ponografia ya watoto imewahi kuzinduliwa nchini uholanzi na kwamba hapo zamani tulikuwa na seneta wa pvda ambaye nyumba yake ilijaa na ponografia ya watoto lakini hebu tunabaki kuwa nchi tamu nzuri jina la seneta huyo alikuwa edward brongerma na faili za ponografia za watoto sasa ni nyenzo za kisayansi za msingi ambaye yuko nyuma ya elimu ya ngono katika shule zetu za msingi lakini pia tutafanya hivyo tena halafu tunayo filamu za unyanyasaji wa kijinsia ambazo watoto wachanga na watoto wachanga wananyanyaswa kijinsia sio zabuni
kesi za pedophilia za nyakati za hivi karibuni zinaonekana kuwa na athari ya kuzoea ikiwa tunaona ujumbe wa kutosha kutoka kwake itakuwa na athari ya kuamini kwamba hii ni hitaji la kingono la wanaume fulani kwa kuongezea daima ni juu ya watoto wadogo wa (wacha tuseme) kikundi cha umri 12 + watu wengi wanaweza hata kuchagiza mabega yao kwa siri kwa hiyo (ikiwa unaona kitu kibaya lakini mara nyingi vya kutosha katika habari hali hujitokeza hata iwe mbaya) mchunguzi wa marc dutroux kesi ya robert m kesi ya ponografia ya watoto wa zandvoort na jam za trafiki za edward brongersma hata hivyo zimeonyesha kuwa kuna uwezekano kuwa kuna soko kubwa la unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto wadogo sana (watoto wachanga na watoto wachanga)
ingawa nina wasiwasi kuhusu uwezekano wa kwamba david icke (tazama hapa chini) ni fungu lililodhibitiwa (labda hana fahamu) hiyo haimaanishi kwamba haonyeshi ukweli mwingi hiyo ni kazi yake upinzani uliodhibitiwa lazima ufunue ukweli mara tu msaada ukiwa mkubwa bomu limepigwa chini chini na umeshughulika na kikundi hicho katika 1x kwa hivyo mimi huchukua msimamo kwamba anatoka na sehemu kubwa za ukweli sio kwamba yeye haoni kila wakati kwamba tunachezwa pia na mbwembwe na psyops (lakini wakati anakaguliwa hawezi kudhihirisha kuwa) icke pia inakuja na ufunuo ambao tayari umetengenezwa kwenye njia zingine lakini kazi yake ni kuvutia ubinadamu wa kuamsha hadithi ya ibada ya sabasaba hapa chini (tazama video) labda ni msingi wa ukweli pedophilia ni sehemu muhimu ya kanuni za kabbalistic za ibada hii kwa maoni yangu hata hivyo kikundi hiki kinasimamiwa (tazama maelezo hapa chini)
kilicho muhimu kuelewa ni kwamba sisi (kama david icke anavyodai kwa usahihi) tunashuhudia hati ambayo mambo mawili yanainuliwa kwa makusudi hadi urefu mkubwa katika hili uovu pia huchukuliwa kwa urefu mkubwa hiyo ndiyo kazi ya hawa kabbalists na ibada ya sabbatan ikiwa unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto wachanga umekuwa ukiendelea kwa vizazi (ndani ya hizi damu) ni kama ilivyochomwa ndani ya dawa ya binadamu kama kumbukumbu ya msingi hii ndio jinsi avatar ya mwanadamu inavyofanya kazi (kama ilivyoelezwa katika makala hii soma) jalada kubwa la pedophilia katika media na media mbadala pia ina athari hiyo aina ya hali ya kukosa fahamu kwa jambo hilo hufanyika na duka zetu za dna hujali kama ukweli wa msingi
waliowajibika
ikiwa tunataka kuona kwa nini tunaona uzushi huu na kwa nini kikundi cha wasabati kinatimiza jukumu lake katika maandishi ya bwana basi tunahitaji kuona kupitia kiini cha ukweli wetu kiini hicho ni kwamba watu fulani katika mikoa ya juu wanaendeshwa na mjenzi wa ukweli huu wa simulative halo subiri kidogo je tunapata nini tena ukweli simulativendio wewe na wewe tunaona ulimwengu huu na ulimwengu huu lakini kwa kweli uko nje yake tunaangalia na kucheza katika simulation hii kupitia avatar yetu mwili wetu
kikundi kinachojaribu kudhibiti ulimwengu huu kulingana na hati ya bwana huunda maandamano ambayo yanadhibitiwa na wajenzi wa ukweli huu halisi je unatukumbusha sinema matrix hiyo inakuja karibu sana katika makala hii ninaelezea kwa undani kile unapaswa kufikiria katika simulation jinsi inavyofanya kazi sawasawa na kwa nini mwili wako ni avatar yako ninapendekeza kusoma nakala hiyo vile vile kwa sababu vinginevyo unaweza kufikiria kuwa unasikiliza hadithi ya kutamani kulingana na filamu hiyo kutoka miaka ya tisini
kikundi kinachodhibitiwa (avatar) kina ushawishi mkubwa wanajaribu kushinikiza wachezaji kwenye mwelekeo fulani baada ya yote ni sheria ambayo simulation lazima msingi wa uhuru wa kuchagua vinginevyo isingekuwa simulizi lakini uamuzi (ambapo kitu tayari kiko tayari) filamu njia yako ya asili ya fahamu inacheza hii simulizi ya wachezaji wengi na chaguzi zako zinabaki bure kwa hivyo unaweza pia kuamua kuto kushirikiana na hati timu ya avatar (midundo ya damu) ambayo inadhibitiwa na mjenzi / timu ya wajenzi wa simulizi hii lazima ichukue rangi hii kwa njia ambayo ni ngumu sana (au karibu kabisa) kuchagua tofauti kuliko hati ya bwana kwa mfano umetengenezwa kwa kutegemea pesa na ni vigumu kujiondoa kwenye mfumo wao kundi hilo la waadharia ni kwa maoni yangu maelewano ya kidemokrasia (kama ilivyoelezewa) na ibada iliyotajwa na icke inatimiza kazi katika hati ya bwana ambayo wanajaribu kutekeleza
uelewa wa kimsingi na suluhisho
ni muhimu kuelewa uendeshaji wa simulizi hii (ambayo tunafikiri ni ulimwengu wetu wa kweli) tambua maandishi ya bwana na uelewe jukumu la wachezaji tofauti walakini ni muhimu zaidi kuendelea kukuonyesha kwamba hali yako ya asili ya fahamu inaona ukweli huu halisi na kwamba kwa hivyo haujashikwa hapa umetambuliwa sana na udanganyifu huu karibu kila siku ninapambana na shida zinazofanana ninajali ubaya wote ulimwenguni na ni njia gani inaenda kikundi cha kudhibiti mfumo wa kudhibiti na maandishi ya bwana yanaonekana kukumbatia yote na nguvu kwamba inaonekana hakuna njia ya kutoka kila siku lazima nitajiambia mwenyewe kuwa mimi ni aina ya asili ya fahamu ambayo ni nguvu sana kuliko kila kitu kinachotokea katika ukweli huu wa simulative
in makala hii (na vifungu vya msingi kupitia viungo vya bluu) ninaelezea kuwa sisi ni wachezaji katika simulizi ya virusi vya luciferian ni muhimu kuelewa kanuni hiyo ili tuelewe ni hatua gani tunaweza kuchukua (kwa kiwango cha ufahamu) kwa sababu sisi ni wakubwa zaidi kuliko wale wasabato wote kabbalists damu za aristocracy na lusifa pamoja lengo linapaswa kuwa juu ya hiyo
kumbuka chukua wakati na juhudi kupitia vifungu vilivyounganishwa ni jambo ngumu ambalo kwa kweli halina ugumu hata mara robo inapoanguka tafadhali pia jitahidi kuwa mshiriki au toa toleo moja kwa nl27 abna 0558 4469 22 kwa jina la martin vrijland foundation kwa sababu msaada wako unahitajika sana asante mapema
orodha ya kiungo cha chanzo thetruthrevolutionnet
makosa ya pedophile ya uingereza na tafsiri ya nieuwsuur kwa uholanzi
zika maambukizi ya virusi sasa pia kwa njia ya kuwasiliana na ngono
tags channel disney featured unyanyasaji pedophilia ricky garcia ngono str ngozi
« simu ya haraka lazima tuweke media nje ya hatua sasa
je kutakuwa na vita kati ya amerika na irani haraka sana sasa »
ziara ya jumla 13139232 | 2019-10-22T09:05:58 | https://www.martinvrijland.nl/sw/uchambuzi-wa-habari/Asterisk-ya-zamani-ya-Disney-Channel-inasema-kuwa-imedhulumiwa-na-pedophiles-za-Hollywood/ |
wanafunzi wa nelson mandela watakiwa kuwa mstari wa mbele kusaidia utatuzi wa matatizo ya mazingira | lukwangule entertainment
wanafunzi wa nelson mandela watakiwa kuwa mstari wa mbele kusaidia utatuzi wa matatizo ya mazingira | 2018-05-25T18:51:37 | http://lukwangule.blogspot.com/2016/11/wanafunzi-wa-nelson-mandela-watakiwa.html |
kwa taarifa yako safari ya gospel kitaa hadi hivi sasa gospel kitaa™
home / ambwene mwamwaja / boniface kazi / gospel kitaa / kwa taarifa yako / silas mbise
/ kwa taarifa yako safari ya gospel kitaa hadi hivi sasa
kwa taarifa yako safari ya gospel kitaa hadi hivi sasa
januari 2012 wafuasi wakiwa 600
gospel kitaa ambayo imeanza mwaka 2011 imekuwa na lengo hasa la kuwavuta vijana na kuwafanya wawe watumishi wa mungu kwa namna ambavyo anapenda wamtumikie kwa taarifa yako jina la gospel kitaa lililenga hasa jamii ya watu mbalimbali kwanza gospel ikilenga kuwavuta wale wote wanaopenda na wasio na mashaka na injili na pia neno kitaa likiwalenga vijana moja kwa moja ambao hufika kutazama kinachojiri kitaani
kwa mwendo wa kusuasua na kama mzaa ndivyo ambavyo blogu hii ilianza ikiendeshwa na ambwene m mwamwaja kabla ya kuungana naye elie j chansa na kisha silas e mbise na hivi karibuni boniface kazi kwa taarifa yako team gk wanaoonekana ni hao 4 ila pia kuna wale ambao hawaonekani mmojawapo ni wewe unayetembelea tovuti kila siku )
mwaka 2011 mwezi aprili ndio ambapo habari ya kwanza iliandikwa kwenye blog hii ambayo ilikuwa inamhusu mwimbaji joyce mlabwa ambaye alikuwa ametoa toleo lake la pili la album ya picha za sauti (bofya hapa kusoma) kipindi hicho blog ikifahamika kama gospelkitaablogspotcom
mwezi aprili ulishuhudia habari moja tu ikiandikwa kisha ikifuatiwa na habari mbili kuandikwa mwezi mei kisha kufuatiwa na miezi 4 ya ukimya kutokana na majukumu mengine ya kujenga taifa hata hivyo nguvu iliongezwa mara baada ya timu kuongezeka baada elie kujunga na gk ambapo mwaka 2012 ukashuhudia jumla ya habari 750 zikiandikwa kulinganisha na habari 18 kwa mwaka 2011
kwa taarifa yako gk ambayo ilizaliwa jijini manchester uingereza ambako wazo la ambwene kuwa na blog ya kuandika habari za kristo lilikamilika kwa vitendo akisaidiwa na rafiki yake dkt mbonea mrango ila kwa taarifa yako makao makuu ya gospel kitaa yalikuwa kurasini kwenye majengo ya wapo radio fm ambako timu nzima ilikutana hapo iliendelea kufanya vema na kuanza kupata wadau mbalimbali ambao pia walikuwa wakiisikiliza wapo radio fm kwa njia ya mtandao mara tu ilipoanza na hicho ndio chanzo cha mitandao mingine mingi kunakili ratiba ya vipindi kama ilivyoandikwa ikiwemo mitandao ambayo haiandiki kuhusu habari za injili
julai 2014 wafuasi 9000
uanzishwaji wa ukurasa wa facebook ulifanikisha kueneza injili kwa watu wengi zaidi ambapo wafuasi walianza kufuatilia mtandao huu kutoka kila kona ya dunia ufuatiliaji wa habari za makanisa mbalimbali bila ya kubagua imekuwa sababu nyingine ya gk kupata mashiko ambapo pamoja na kukua kwake changamoto nazo zilizidi kukua ikiwemo ile ya kufuatilia habari kwa muda mrefu na kisha mara baada ya kuandika watu wengine kuinakili kama ilivyo na kuifanya yao (bila kueleza chanzo chao) kwa taarifa yako hilo ndilo lililopelekea kuanza mfumo wa kuweka alama kwenye picha na video ambazo gk imezipiga tazama baadhi ya video hizo kwa kubofya hapa
kwa kadri siku zilivyokuwa zinaenda na changamoto kuzidi ndivyo ambavyo kumekuwa na mabadiliko kadha wa kadha ili kuendana na teknolojia kuwezesha kufikisha injili katika viwango vya juu mwaka 2013 ulishuhudia mabadiliko ambayo kwa kwa taarifa yako hata mitandao mingine ililazimika kuiga mfano ambapo gospel kitaa ilihama kutoka wwwgospelkitaablogspotcom kwenda wwwgospelkitaacotz/ ukiuliza waendeshaji safari kwao bado kufika mwisho
ni mengi yangewezwa kuzungumzwa kuhusu safari ya gk hadi kufikia hivi sasa ila kiufupi tunaamini kwamba kuna mahala mtu huguswa na kile ambacho huwa tunakichapisha hapa aidha kwa utafiti wetu ama kupitia walimu mbalimbali na wahubiri ambao hutuma mafundisho yao kwa ajili ya kukufikia kama ambavyo hatutozi kwa ajili ya kuweka mafundisho kutoka kwa mtu yeyote ndivyo tunaamini kwamba mafundisho yanafanyika baraka kwako maoni yako ni muhimu kama kuna mafundisho uliyoguswa nayo jambo ambalo pia linamtia moyo mwalimu kuendelea kufundisha kama ungependa kuwa sehemu ya team gk kwenye mkoa wowote uliopo milango yetu iko wazi kwa ajili ya kumtwalia bwana yesu utukufu
ila kama ulikuwa hujui kwa taarifa yako team gk na majukumu yao ni kama ifuatavyo ambwene mwamwaja mkurugenzi/mwandishi mwandamizi elie chansa mhariri/mpiga picha mkuu silas mbise mratibu/mwandishi mpiga picha boniface kazi mpiga picha/graphics
katika yote tunayofanya na kupitia tunamshukuru mungu kwa kutuwezesha kueneza injili kwa mfumo wa dijitali pamoja na yote kwa taarifa yako mtandao huu usingefaa kitu kama haukupata watembeleaji wa kila siku kama wewe ahsante sana endelea kueneza ujumbe kwa wengine injili na izidi kusonga mbele
hiyo ndio kwa taarifa yako vinginevyo tukutane wiki ijayo | 2016-12-11T11:48:16 | http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/04/kwa-taarifa-yako-safari-ya-gospel-kitaa.html |
wimbi wikipedia kamusi elezo huru
mfano wa wimbi katika maji[hariri | hariri chanzo]
mawimbi ya aina nyingi[hariri | hariri chanzo]
tabia za wimbi[hariri | hariri chanzo]
what is a wave (physicsclassrom)
what is a wave (pbslearningmedia)
waves / physics for kids
rudishwa kutoka https//swwikipediaorg/w/indexphptitle=wimbi&oldid=996089
ukurasa huu umebadilishwa kwa mara ya mwisho tarehe 29 aprili 2017 saa 1548 | 2017-10-19T01:56:21 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Wimbi |
watu na simba yao kwa raha zao na wanapendeza 'mashaallah' bin zubeiry sports online watu na simba yao kwa raha zao na wanapendeza 'mashaallah' bin zubeiry sports online
mwanzo > simba > watu na simba yao kwa raha zao na wanapendeza 'mashaallah'
watu na simba yao kwa raha zao na wanapendeza 'mashaallah'
mashabiki wa simba wakiwa uwanja wa taifa mjini dar es salaam wakati wa mchezo wa ligi kuu ya vodacom tanzania bara dhidi ya tanzania prisons aprili 16 uwanja wa taifa mjini dar es salaam simba ilishinda 20
item reviewed watu na simba yao kwa raha zao na wanapendeza 'mashaallah' rating 5 reviewed by mahmoud bin zubeiry | 2019-09-18T22:22:35 | http://www.binzubeiry.co.tz/2018/04/watu-na-simba-yao-kwa-raha-zao-na.html |
hapa kwetu kwenye baa hakuna udini
umeniwazisha sana tu profna siku hizi kirahisi wapayukao sana neno amani unaweza kukuta ndio waanzisha vita yani(
ila kwa ujumla mie naamini tanzania hatuna serekali yenye nguvu sasa hivi ndio maana kuanzia udini tatizo la malawi tukiachilia mbali mapungufu kidhaifu ambayo hayahitaji hata misaada kama tuaminishwavyo yafanyavyo tanzania imelala(
prof unapaswa ujue kuwa kuna waislamu jina(wengi wao wamezaliwa tu na wazee wa kiislamu) na waislamu waliosoma dini yao uislamu si dini ya kuzaliwa kama ulivyo ukristo na baadae kwenda kubatizwa uislamu ni matendo ni sawa na kusema waislamu ndio magaidi matendo ya watu ndio yanayowapelekea kujulikana imani zao hao unaowaona kwenye vilabu vya pombe wanakunywa wanaitwa wanafiki katika uislamu hao ni wabaya kuliko makafiri katika quran tunaambiwa kuwa wanafiki watakuwa wa mwanzo kuingia motoni na watakuwa chini kabisa angalia aya hii4145 the hypocrites will be in the lowest depths of the fire no helper wilt thou find for themkwahiyo hilo naomba ulijuekuhusu ubaguzi wa kidini upo sehemu nyingi ikiwemo chuo kikuu dar walimu wengi walioonekana kuwa ni waislamu wa kweli pale chuoni walikuwa wakipata vitisho na kuitwa wakiulizwa masuali kuhusiana na misimamo yaopia bahati mbaya katika shule za wakristo iko ubaguzi wa dininakumbuka niliwahi kuwatembelea vijana wa kiislamu katika shule za bara na walikuwa wakilalamikia kuwa walikuwa wanalazimishwa kwenda kusafisha mabanda ya nguruwe na wakizuiliwa kusali
ndugu anonymous shukrani kwa changamoto yako hapa kijiweni pangu ni sehemu ya fikra huru kwa hivi jisikie nyumbaninina dukuduku na masuali kadhaa kutokana na kauli zako kwanza umesema kuwa uislam ni matendo kama ni hivyo basi wale waislam ninaojumuika baa angalau wana hii dalili moja kuwa ni waislam kwani matendo yao ni pamoja na kuwa sambamba na binadamu wenzao bila ubaguzi bila udini nimeeleza hayo katika makala yangu umewaita hao wanafiki hapo nashindwa kukubali kwa sababu anayemjua mnafiki ni muumba peke yake binadamu hana upeo wa kumjua binadamu mwenzake kiasi hicho na akijipa wadhifa wa kumhukumu mwenzake namna hii naona anajifanya yeye ana uwezo wa muumba katika dini zetu hiii huitwa kufurunapendekeza kuwa sote tuwe makini na suala hilo la kuwahukumu wenzetu kwani tunajiweka katika hatari ya kutotambua uwezo na wadhifa wa mungu (allah)umesema pia kuwa katika uislam hao {wanafiki} ni wabaya kuliko makafiri mimi nakunywa nao baa na sijaona ubaya wao ni watu wazuri ambao tunakaa nao pamoja kwa amani siwaogopi bali nawaogopa wale ambao wamejiaminisha kuwa wao ni waislam safi kabisa (yaani akina boko haram al shabab na wengine) na wanatuvizia ili watulipue huko baa hao ndio nawaogopaunafanya vema kunukuu quran waumini tunapaswa kurejea kwenye misahafu ili tusipotee njia lakini quran ni kitabu cha allah anayeongea ni allah na mwenye ufahamu kamili ni allahtukisoma aya kama hiyo uliyonukuu haimaanishi kuwa sisi binadamu tunaweza kumtambua nani mnafiki ingawa ametajwa katika quran mwenye uwezo wa kumtambua mnafiki na kumwadhibu ni allah kama nilivyosema hapo juu wanadamu tujihadhari na hiki kishawishi cha kujitwalia mamlaka ambayo hatuna kwani sisi ni viumbe dhalili mnomakala yangu iliongelea suala la kutokuwepo udini katika baa sikujiingiza katika kuongelea uwepo au kutokuwepo kwa udini sehemu zininge katika jamii ya tanzania tukitaka kuongelea suala hilo kwa upana basi tutataja sehemu nyingi taasisi nyingi za wakristo na za waislam kwa mfano hatuwezi kufumbia macho udini uliopo visiwani ambako makanisa zaidi ya ishirini yamechomwa moto hilo nalo itabidi tulijumlishe katika uchambuzi tusimpendelee mdini mkristu wala mdini muislamumetoa mfano wa waislam kushurutishwa kwenda kusafisha mabanda ya nguruwe kama hilo limetokea na jambo la kulaaniwa na yeyote anayeheshimu imani za wanadamu wote papo hapo nami nimesikia kuwa kuna sehemu fulani tanzania ambako mkristu akionekana anakula wakati wa mwezi mtukufu ananyanyaswa hiyo nayo ni hujuma kwani mwezi mtukufu ni wa waislam sio wakristu mimi mkristu nikienda sehemu ya aina ile nahitaji kuona hoteli ambapo naweza kupata chakula naziheshimu dini zote na nategemea nami kuheshimiwa kutokana na imani yangututafakari mambo hayo kwa uwazi napenda kugusia pia hoja yako ya mwanzo kabisa kwamba kuna waislam jina yaani ni kwamba tu wamezaliwa na wazee wa kiislam naona hii ni hoja muhimusasa basi wale waislam waliosema wataendesha kampeni nchi nzima ili kushinikiza sensa iwe na kipengele cha dini walikuwa na huu upeo wa kupambanua waislam na waislam jina au maana yao ilikuwa kwamba kila hassan maryam mustafa na zubeda ni muislamna je wakati ule wa mgogoro wa shule ya ndanda tulipoambiwa waislam wananyanyaswa pale palikuwa pamefanyika uchambuzi na kubaini kuwa wale wote walikuwa ni waislam au walikuwepo pia waislam jina tufanye uchambuzi huo nchi nzima
profhao jamaa wanaojiita waislamu na kisha ukawakuta baa hawana matendo mema kwa mujibu wa uislamu uislamu uko very clear unaposema katika aya tofauti kuwa wale walioamini na kisha wakafanya matendo mema matendo mema katika uislamu uislamu yako very clear na baadhi yake yanafanana na matendo mema ya dini nyengine matendo mauvo pia yako wazi sasa kunywa pombe ni katika mambo yaliyokatazwa katika uislamu sasa mtu anaekunywa pombe anakuwa ni mnafiki wanafiki wanajulikana wazi katika uislamu quran imetufahamisha wanafiki ni nani na katika hadithi za mtume(saw) zimeweka alama zote za wanafiki(ukipenda na nikipata nafasi naweza kukuelezea alama hizo)kwako wewe hao jamaa unaokunywa nao hawana makosa lakini katika uislamu hao wana makosakauli yako hii nahisi ni sawa na wale wanaowahifadhi al qaeda kule pakistan wanawahifadhi kwasababu wanawaona hawana makosa wanaona wanaenda nao msikitini wanafunga nao na wanawapatia misaada wao wanahisi al qaeda kushambulia wamarekani au kushambulia watu wanaotofautiana nao wakiwemo mashia kwao wao sio makosa hayo lakini haya ni makosa katika uislamu kwahiyo it does not matter kwamba wewe unamuona mtu ni mwema machoni mwako kama mtu anafanya matendo yalitokatazwa katika uislamu na akajiita muislamu uislamu hauna jina la kumuita mtu huyo isipokuwa ni mnafiki huyo ni muovu mbele ya uislamu huyo ni muovu kuliko kafiri kwasababu huyo ni adui miongoni mwenu(chui alievaa ngozi ya paka au mbuzi) kwa kuwa uko nje muda mwingi inaonekana hujui kinachoendelea zanzibar unachokijua ni kile ulichosoma kwenye magazetisijui kama katika taaluma hili ni sawa kuongelea kitu ambacho hujakifanyia utafiti mtu kama wewe uliesoma usifanye analysis kwa kauli za kusikiaukitaka kujua kilichotokea zanzibar ama njoo ufanye utafiti au uliza watu walioshuhudia usiwe simplistic kiasi hicho mimi nakuheshimu sana kwa elimu yako na napata tabu sana kuona wakati mwengine unavyochambua mambo kama watu wanaotaka kuuza magazeti yaoalshabab boko haram na wengineo kama hao ni makundi ya wanafiki matendo yao ni maovu inaonekana hii mada unaipanua zaidi na zaidi kwa bahati mbaya nasikitika sina muda mwingi wa kuandika lakini kwa ufupi sisi waislamu tunatakiwa tuwaogope watu wote ambao matendo yao hayaendani na mafundisho ya dini ya kiislamu
profesa mbele asante sanahilo mimi nilikuwa silijui kwamba kumbe kwenye baa watu wa dini tofauti tunapendana asante kumbe kusoma ni kuelimika hilo nalo nimelipata ni kweli pamoja na huyo anon kupinga lakini baa ndio kuna upendo zaidi kuliko kwenye nyumba za ibada maana kwenye nyumba za ibada kumejaa vitisho mara kwenda motonimara sijui niniasante sana yaani leo umenipa kitu ambacho sikukitegemeani mimi mwislamu ni siyekuwa wa kuzaliwavipi bado upo songea dar utapita lini
ndugu anonymous wa kwanza ungefanya vema kutusaidia sisi wengine kufahamu yaliyotokea zanzibarkama muumba amekupa fursa ya kuishi na kufahamu jambo unawajibika kuwamegea wengine kwani chochote tulicho nacho kinatoka kwa muumba na ni dhamanakama tunakubaliana hebu tupe angalau dondoo kuhusu ukweli wa yaliyojiri zanzibar
polisi ruvuma wakamata tena pembe za ndovu
dar majambazi yajeruhi yapora begi
shaibu nnunduma ateuliwa kuwa mkurugenzi wa wilaya ya nyasa
kunradhi malawi na tanzania
tanzania yanguinayotunza ubongo wa digitali ndani ya fuvu la analogia
au maturing
uvutaji sigara unavyoteketeza mamilioni ya watu | 2013-05-23T22:35:53 | http://hapakwetu.blogspot.com/2012/08/kwenye-baa-hakuna-udini.html |
hii ndio yanga banayatenga bilioni 2 za kufanya usajili wa kishindochuji aomba kurudi yanga kukipiga msimu ujao habari online na elimtaa
habari online na elimtaa 2017 at 0605pm blogger ifttt june 05 uncategorized hii ndio yanga banayatenga bilioni 2 za kufanya usajili wa kishindochuji aomba kurudi yanga kukipiga msimu ujao
hii ndio yanga banayatenga bilioni 2 za kufanya usajili wa kishindochuji aomba kurudi yanga kukipiga msimu ujao
unknown 60600 pm 2017 at 0605pm blogger ifttt june 05 uncategorized
sasa yanga kumekucha baada ya kumaliza pilikapilika za kushangilia ubingwa wa ligi kuu tanzania bara sasa klabu hiyo inataka kuanza kazi ya kuunda kikosi kipya kwa ajili ya msimu ujao
kamati ya utendaji wa yanga imeunda kabineti ya watu watano na kuwakabidhi sh bilioni 2 kwa ajili ya kufanya mazungumzo na nyota wao wanaomaliza mikataba mipya na kufanya usajili ili kuongeza nguvu kwenye kikosi chao
mwenyekiti wa kabineti hiyo ni hussein nyika makamu wake ni mustapha ulungo huku wajumbe wakiwa ni katibu mkuu wa yanga charles mkwasa na kocha wa klabu hiyo george lwandamina
moja ya majukumu yatakayowakabili ni kuhakikisha wananasa saini za wachezaji wanaotajwa kuwaniwa na klabu hiyo ambao ni salmin hoza yusuph ndikumana mbaraka yusuph jamal mwambeleko michael gradiel raphael daudi mrisho ngassa youth rostard said ndemla ibrahim ajib na jonas mkude
ili kupata nafasi ya kuwasajili wachezaji hao klabu hiyo imepanga kuacha nyota wao 15 ambao hawakuwa na nafasi katika kikosi hicho na kusuka upya timu kwa ajili ya msimu ujao
kamati imeazimia kusajili wachezaji wengi vijana ambao wana uwezo na wenye ubora wa kucheza yanga na kuwaacha wachezaji 15 ambao walikuwa hawana nafasi ya kucheza wamedhamiria kujenga timu imara yenye hadhi na mashindano ya kimataifa ndiyo maana wametenga fungu hilo la fedha alisema mjumbe huyo
aliongeza kuwa mbali na kufanya usajili huo wa nguvu lakini kamati hiyo leo inatarajia kuanza mazungumzo na wachezaji deus kaseke donald ngoma amis tambwe haji mwinyi thaban kamusoko vincent bossou na wengine ambao mikataba yao ya kuichezea timu hiyo imemalizika hivi karibuni na kupendekezwa na kocha lwandamina kuendelea kuwa nao
mmoja wa wajumbe wa kabineti hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema kesho (leo) jumatatu tutaanza kazi ya kuzungumza na wachezaji wote ambao walimalizia mikataba yao ambao wamependekezwa kubaki na kocha lwandamina baada ya hapo itakuja zamu ya wachezaji wapya ambao watakuwa wameorodheshwa kwenye ripoti ya kocha wetu
kwa upande wake mkwasa alisema yanga ni timu kubwa na wamejipanga kufanya usajili wa nguvu wenye tija utakaowezesha kutetea ubingwa wao msimu ujao
tumejipanga kila eneo ili kufanya usajili wa nguvu wenye tija ambao utazingatia vigezo vyote na mimi ndio nitaongoza jahazi hilo alisema mkwasa
katika mipango yao ya usajili yanga wanadai kuwa na mpango na kuanza na beki wa kushoto wa azam gadiel michael ili kucheza pamoja na haji mwinyi kwenye klabu hiyo
naye kiungo wa zamani wa timu hiyo athumani idd chuji ameomba kurejea tena kundini kuvaa viatu vya justine zullu mkata umeme na kusema uwezo wa kuitumikia timu hiyo ya jangwani bado anao kama akipewa nafasi katika eneo la kiungo mkabaji
nimeiangalia yanga msimu uliomalizika nimegundua bado ninao uwezo mkubwa wa kuichezea timu hiyo pamoja na umri wangu wa miaka 29 bila shaka ninaweza kulitibu tatizo la kiungo mkabaji ambalo limekuwa likiwasumbua yanga kwa muda mrefu alisema pass master huyo chuji
akizungumza kuhusiana na ombi hilo la chuji kutaka kurejea tena yanga mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya yanga paulo malume alisema amelisikia suala hilo na atalipeleka mahali husika kwa ajili ya kulitolea maamuzi lakini yeye hawezi kusema lolote
nimelisikia suala la mchezaji huyo kwa kifupi nitalipeleka mahala husika tuone nini watasema kila mtu anamfahamu chuji alikuwa ni mchezaji wetu lakini muda mrefu umepita tangu aondoke hivyo ngoja tuone watasemaje alisema malume
from blogger http//ifttt/2rll5dt | 2019-08-24T13:16:24 | http://eliabu.blogspot.com/2017/06/hii-ndio-yanga-banayatenga-bilioni-2-za.html |
22 kwa waorthodoksi na waorthodoksi wa mashariki
katika uyahudi [hariri]
jina linalotumika zaidi ni tzadik (mtu wa haki mwadilifu) aliyejitahidi kufuata torati
katika ukristo [hariri]
katika kanisa katoliki [hariri]
klara wa asizi alivyochorwa na simone martini katika basilika la mt fransisko wa asizi huko asizi
kwa wakatoliki mtakatifu ni yule aliyemfuata yesu kristo akiishi kwa upendo na maadili mengine yanayoutegemea hasa aliyeyatekeleza kwa kiwango cha ushujaa katika kufia dini au katika maisha ya kila siku
utakatifu si wa aina moja bali kila binadamu anatakiwa kuitikia siku kwa siku wito maalumu aliopewa na mungu hivyo yeyote anaweza na kupaswa kulenga utakatifu bila ya kujali sifa zake za kibinadamu tu
ili kuzuia udanganyifu kanisa katoliki linamuachia papa kusimamia kesi ndefu za kumtangaza mtakatifu mpya miaka baada ya kifo chake
wakatoliki wanawapatia bikira maria na watakatifu wengine heshima ya pekee kama marafiki wa mungu lakini si ibada halisi heshima hiyo inadai wajitahidi pia kufuata mifano yao kama wao walivyofuata ile ya yesu
kwa waorthodoksi na waorthodoksi wa mashariki [hariri]
masalia ya demetrio wa thesalonike katika kanisa lake huko thesalonike
makanisa ya kiorthodoksi yanamuita mtakatifu hasa anayesadikiwa yuko katika paradiso kuanzia adamu na eva mose na manabii wengine lakini pia malaika ni mungu anayefunua watakatifu wake kwa kuitikia sala anazotolewa kwa kuwapitia na kwa kutenda miujiza wakristo wanaanza kuwatambua lakini uamuzi wa mwisho unachukuliwa na sinodi ya maaskofu
waorthodoksi wanawatendea watakatifu kama watu hai kwa sababu wanaishi mbinguni pamoja na kristo mfufuka ingawa miili yao haijaungana tena na roho zao kila mtu anapobatizwa anapewa jina la mtakatifu fulani kama msimamizi kwa maisha yake yote
katika uprotestanti [hariri]
madhehebu mengi hayakubali mawazo hayo yakipenda kusisitiza kwamba wokovu unamtegemea mungu tu hata hivyo mara nyingi waamini bora wanakumbukwa kwa heshima na kuchukuliwa kama mfano (taz confessio augustana art 21) hasa waanglikana wanakaribia msimamo wa wakatoliki na kuadhimisha sikukuu za watakatifu kadiri ya kalenda maalumu
katika uislamu [hariri]
rudishwa kutoka http//swwikipediaorg/w/indexphptitle=mtakatifu&oldid=883974 jamii diniwatakatifu wakristo urambazaji
ukurasa huu umebadilishwa kwa mara ya mwisho tarehe 9 machi 2013 saa 2148 | 2013-05-20T03:14:49 | http://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu |
mkuu wa wilaya ya iramba mkoani singida mhe emmanuel luhahula amefanya ziara katika kijiji cha kisonga lunsanga kata ya mtekente pamoja na kijiji cha luzirukuru tarafa ya ndago wilayani iramba ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kufanya mikutano na wananchi ili kuhamasisha shughuli za maendeleo na kusikiliza kero zao leo tarehe 25032019
katika ziara hiyo mkuu wa wilaya ya iramba amekabidhiwa madawati 20 kutoka kwa wananchi wa kijiji cha kisonga kata ya mtekente tarafa ya ndago kwa ajili ya shule ya msingi kisonga ili kuunga mkono jitihada za serikali
akizungumza na wananchi wa kijiji cha kisonga mkuu wa wilaya ya iramba amewashukuru sana kwa ushirikiano wao na kwa kujitoa kuchangia madawati
kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya iramba kennedy thobias mpanduji amekabidhi madawati hayo kwa mkuu wa shule ya kisonga na uongozi wa shule na kuwataka wayasimamie aidha amewataka wanafunzi wayatumie vizuri ili baada ya miaka ijayo wadogo zao watakapo kuja wasipate tabu ya madawati na uongozi usichangie tena madawati isipokua wachangie vitu vingine vya maendeleo
mhe luhahula amewapongeza walimu na wananchi wa kata ya mtekente kwa kuongeza ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba wilayani iramba mwaka huu nawapongeza sana walimu wa wilaya ya iramba na wazazi kwa kupeleka chakula mashuleni kwa ajili ya watoto wetu na hatimaye kupanda kwa ufaulu wa mitihani ya darasa la saba mwaka huu hongereni sana kwa ushindi wa darasa la saba watoto wote walifauru kujiunga na kidato cha kwanza katika shule ya msingi kisonga wananchi lazima mshirikiane na watalaamu ili kudumisha ufaulu wa wanafunzi wetu viongozi wote kuanzia ngazi ya tarafa lazima kuwashirikisha wazazi na kuwaelemisha maana halisi ya elimu bila malipo na kuhakikisha watoto wote wanakwenda shule na wanakula chakula simamieni suala la utoro na hakikisheni watoto wote wanakwenda shule hakikisheni watoto wote wanakula chakula shuleni watoto lazima wale sio ombi kwenye vijiji vyote ninatumia mamlaka kuagiza hili na sio ombi watoto lazima wale alisema mhe luhahula
ameongeza kusema wazazi wanawajibika kikamilifu katika kuhakiksiha watoto wao wanapata elimu kuwalinda na ukatili wa kijinsia pamoja na kupinga ndoa za utotoni ambazo zinawakatisha watoto masomo wazazi lazima kuwalinda watoto wenu na wakina mama waache tabia ya kufika wanaume wanaowapa wanafunzi mimba ikibainika mtoto wako amepewa mimba wazazi mtawajibishwa kwa mjibu wa sheria alisema mhe luhahula
aidha mkuu wa wilaya iramba amewataka wananchi kuhakikisha wanasajili watoto wao wenye umri chini ya miaka mitano ili wapate vyeti vya kuzaliwa ambavyo vimetolewa bure na mhe rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john joseph pombe magufuli mpaka sasa tumekwisha sajili zaidi ya watoto 11000 simamieni upatikanaji wa cheti cha kuzaliwa na hakikisheni mnakitunza maana ukipoteza utalazimika kutoa gharama kukipata ofisi ya mkuu wa wilaya
mhe luhahula aliongeza kusema sote tunaona hali ya hewa yote tunamwachia mungu lakini hakikisheni wananchi mnatunza chakula mwenye mfugo avune na kununua chakula maana ni fedhea sana familia kukosa chakula
mkuu wa wilaya ya iramba ameagiza viongozi kuanzia ngazi ya tarafa simamieni ugawaji wa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo wadogo ili viishe kufanya hivyo tutakua tunaunga mkono juhudi za mhe rais dkt john joseph pombe magufuli wajasiliamali wasisumbuliwe wasitozwe ushuru wowote wachangie elfu 20000/= amabyo ni gharama ya kutengeneza kitambulisho hicho watendaji wa kata watendaji wa vijiji na wenyeviti wa vijiji simamieni suala hili la vitambulisho vya wajasiliamali wadogo tusimamieni nidhamu kuheshimiana viongozi wote wa serikali na hakikisheni mnatekeleza wajibu wenu kwa kufanya kazi alisisitiza mhe luhahula
mkuu wa wilaya ya iramba amewataka wananchi kujenga utamaduni wa kuchangia mapato ili kuleta maendeleo kwenye maeneo yao wananchi tujengee utamaduni wa kutoa mapato hakuna nchi iliyoendelea kwa kutegemee misaada tunahitaji kukamilisha ujenzi wa zahanati ili huduma za afya zipatikane kwa wananchi jipangeni kuhakikisha majengo haya yanakamalika alisema mhe luhahula
akiwa katika ziara ya kusikiliza kero za wananchi na kuhamasisha maendeleo mkuu wa wilaya ya iramba ametembelea ujenzi wa jengo la zahanati ya mtekente ili kutazama maendeleo ya jengo hilo ambalo limefikia hatua ya lenta
vile vile mhe luhahula amewataka viongozi ngazi ya tarafa kata na kijiji kutatua migogoro ya wananchi kupitia vyombo vya kisheria ameongeza kwa kusema kumetokea wimbi kubwa la mauaji na vifo katika maeneo yenu mauaji na vifo hivi vinatokea kwa watu kuuana kujinyonga watu kupotea kusipojulikana na watoto kutumbukia kwenye madimbwi/visima vya maji mnafanya unyama wananchi mnawajua wanaofanya unyama huu haiwezekani wazee wangu mnawajua wanaofanya haya sio watu wazima kama nyinyi lakini ni watoto wenu haiwezekani tukageuza kisonga kuwa jehanamu mwenyekiti wa kijiji mtendaji wa kijiji na mwenyekiti wa kitongoji ambapo matukio haya yametokea paundwe jeshi la ulinzi mara moja sitaki kusikia mauaji yanatokea tena viongozi kuanzia ngazi ya kata itisha mkutano na kubaini wote wanaofanya mauaji haya alisisitiza mhe luhahula
wananchi wanatakiwa kutatua migogoro yao kupitia ofisi za kiserikali au kwa kuwatumia viongozi wa kijamii walio katika maeneo yao na kwamba kujinyonga au kumuua mtu ambaye una mgogoro/ugomvi naye haisaidiii kutatua mgogoro huo wala kumaliza ugomvi huo serikali haitasita kumchukulia hatua kali za kisheria yeyote atayebainika kujiusisha na mauaji
ameagiza viongozi na wananchi kuchukua hatua za taadhari katika visima na mabwawa yaliyo katika maeneo yao ili kuepusha vifo vinavyotokana na watoto kutumbukia kwenye mabwawa/visima hivyo na kuwalinda na kuwachunga watoto wao wasicheze katika maeneo hatarishi mtoto akitumbukia kwenye bwawa/kisima lazima wazazi wachukuliwe hatua kari za kisheria kwa sababu ya uzembe wa kulinda watoto wao aliongeza kusema mhe luhahula
mhe mkuu wa wilaya ya iramba emmanuel luhahula amewataka wananchi kudumisha usafi wa mazingira na kuwataka wazazi kuacha tabia ya kuwalea wanafunzi watoro niliagiza kila kaya na taasisi zote kujenga choo bora na watendaji wote kukomesha suala la utoro shuleni endapo atakapopatikana mwanafunzi mtoro kamata mzazi wake ili tuzalishe watoto wasomi na hatutaki kuzalisha wajinga amesema
mkuu wa wilaya ya iramba amewataka viongozi wa kata kuhakikisha wanasoma mapato na matumizi kwa wananchi kuhusu fedha mbalimbali wanazozikusanya ili kuwajengea imani ya kufaham fedha iliyochangwa na namna ilivyotumika
mkuu wa wilaya ya iramba mhe emmanuel luhahula amewaomba viongozi wa mazehebu mbalimbali kusaidia serikali kwa kuwafichua wale wote wanaotumia makanisa au misikiti kufanya maovu na kuiombea wilaya ya iramba iwe salama niwaomba viongozi wa dini mtusaidie kuwafichua watu wanaotumia vyombo vya dini kufanya maovu nilazima viongozi wa dini tulinde amani yetu na kudumisha kulinda amani ya wilaya yetu
mkuu wa wilaya ya iramba amewataka wananchi kutoa taarifa kwa wale ambao wanawaomba rushwa suala la rushwa halina mjadala rushwa ni adui wa haki usikubali kununua haki yako wananchi mnaombwa rushwa lakini hamtoi taarifa wananchi toa taarifa ili tuwakamate hao waarifu alisema mhe luhahula
afisa takukuru wilaya ya iramba ndg benjamin masyaga alisema rushwa ni tatizo ambalo athari zake zinamgusa kila mwananchi tatizo hili linasababisha jamii kukosa imani na serikali yao amani baina ya wanajamii kujenga matabaka ya walionacho na wasiokuwa nacho vilevile rushwa imekuwa chanzo cha kudhoofisha huduma zinazotolewa katika jamii kila mwananchi sehemu alipo aweze kushiriki kutoa taarifa za vitendo vya rushwa bila kuchukua muda mrefu kila mwananchi anawajibika kuzuia vitendo vya rushwa na kutoa taarifa hizo ili kuchukuliwa hatua stahili za kisheria dhidi ya wala rushwa na kutokomeza rushwa nchini
ametoa wito wa kukataa kujihusisha na vitendo vya rushwa ikiwemo kutoa au kupokea rushwa na kuhakikisha wanatoa taarifa za vitendo vya rushwa katika ofisi za takukuru zilizo wilayani iramba au kwa kupiga simu ya bure namba 113 au kwa vyombo vingine vya dola na viongozi wanaohusika
ameongeza kusema wananchi watoe ushirikiano kwa takukuru na vyombo vingine vya dola na kuwa tayari kutoa ushahidi wa vitendo vya rushwa kwakuwa mara nyingi takukuru imekuwa ikishindwa kufikia malengo kutokana na wananchi kutotaka kutoa ushirikiano
afisa uhamiaji wilayani iramba ndg collins soka amewataka wananchi wa wilaya ya iramba kutoa taarifa wanapobaini uwepo wa wahamiaji haramu ili kuthibiti raia wa kigeni na yeyote atayebainika kuficha wahamiaji haramu kwenye eneo lake atachukuliwa hatua kali za kisheria alitoa wito huo kwa wananchi kutowahifadhi wahamiaji haramu kwenye makazi yao sambamba na kuwataka watoe taarifa kwenye vyombo vya dola pale wanapogudua kuna mgeni asiyeeleweka na wanamtilia mashaka kwenye makazi yao mhamiaji haramu ni raia wa kigeni anayeingia nchini na kuendelea kuishi nchini bila kufuata taratibu na sheria za uhamiaji au anayeingia nchini kwa mujibu wa sheria za uhamiaji lakini akaendelea kuishi nchini kinyume na sheria kanuni na taratibu wananchi kutoa taarifa kwenye ofisi za uhamiaji kituo cha polisi au serikali za mitaa pindi unapohisi kuwepo wahamiaji haramu mahali popote ushiriki wako katika kuwafichua wahamiaji haramu ni muhimu sana katika kuimarisha ulinzi usalama na maendeleo ya nchi
mhe mkuu wa wilaya amewaomba wenyeviti wa vitongoji wote na mabalozi kusimamia na kuimarisha madaftari ya wageni ili kuahakikisha tunatokomeza uhamiaji haram
akiongea na wananchi wa luzirukuru amewapongeza kwa juhudi zao za kutunza miti nimefurahishwa sana na hali ya hewa ya hapa nimefanya operesheni ya kuzuia ukataji miti leo tukisema tufyeke miti miti yetu itapotea na maeneo haya tutayakimbia sehemu zingine mazao yamenyauka kwa sababu ya kukata miti na hawapati mvua ya kutosha lazima tuifadhi miti ili tuwe na uoto wa asili enedeleni kuifadhi misitu ili tuweze kupata mvua mvua tunayoipata hapa iramba inatokana na misitu iliyopo hapa lunzirukuru winduwindu na maeneo mengine hiyo ndo inatuletea mvua pamoja na ziwa kitangiri alisema mhe luhahula | 2019-10-20T08:21:39 | http://irambadc.go.tz/new/mkuu-wa-wilaya-ya-iramba-mkoani-singida-mhe-emmanuel-luhahula-amefanya-ziara-katika-kijiji-cha-kisonga-na-lunsanga-kata-ya-mtekente-tarafa-ya-ndago-wilayani-iramba |
wabunge msiwaangushe watanzania | gazeti la jamhuri
jamhuri november 28 2014 wabunge msiwaangushe watanzania20141128t091329+0000 siasa
kuanzia kesho watakuwa na fursa ya kujadili ripoti ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali inayohusu ufisadi wa fedha katika akaunti ya escrow
umoja wa wabunge katika kuijadili kashfa hii umeshaonekana na ni wazi kuwa watanzania wanasubiri kusikia kile wanachotarajia nacho si kingine bali mjadala wenye tija kwao na kwa taifa lao kwa jumla
mara kadhaa mijadala ya aina hii imekuwa ikitawaliwa na jazba wananchi hawatarajii kuyaona hayo shida yao si kuona au kusikia ufundi katika uzungumzaji bali ni kuona au kusikia hoja zenye mantiki na vionjo vyenye mwelekeo wa kutetea maslahi ya wananchi na nchi yao
wananchi hawatarajii kusikia kunakuwapo ujanja ujanja wa kukwepesha hoja kwa visingizio visivyo na maana kama vile madai ya kwamba kuibuliwa kwa escrow eti ni matokeo ya harakati za urais mwakani
wabunge ni watumishi wa wananchi wametumwa na wananchi ili wawawakilishe kama nchi hii ingekuwa na uwezo wa kuwa na ukumbi wenye kuhimili watu milioni 45 wa tanzania bila shaka kazi hii ingefanywa na wananchi wenyewe lakini kwa kuwa hakuna ukumbi wala mantiki ya watu wote hao kukusanyika pamoja ndio maana wabunge 352 wamechukua dhamana ya kuwawakilisha wananchi wote wa tanzania
mijadala ya monofu ya samaki epa na hata richmond ilithibitisha kuwa nchi ikiwa na wabunge makini haiwezi kuishiwa hoja za kujadiliwa bungeni huu wa escrow ni kielelezo kingine kinachothibitisha kuwa wabunge wakiamua kuna madudu mengi sana ambayo yanaweza kuibuliwa na hata kufikia hatua ya kuwawajibisha wahusika
matarajio yetu ni kuona baada ya escrow wabunge wanahoji ufisadi katika maeneo mengine kama kule wizara ya maliasili na utalii ambako kumegeuzwa kuwa mgodi wa mafisadi wachache ambao wanaungwa mkono na kulindwa na viongozi wa wizara
moto huu wa escrow ukielekezwa katika tawala za mikoa na serikali za mitaa (tamisemi) tuna hakika asilimia 90 ya wakurugenzi na watendaji wengine watafikishwa katika vyombo vya sheria na hata kufungwa
watanzania wamechoka kuibiwa haiingii akilini kuona maskini wakiyakimbia makazi kwa kukwepa kukamatwa kutokana na michango ya maabara lakini kukawapo kundi la wachache walioamua kufaidi bila huruma mabilioni ya fedha za umma
huu ni wakati wa wabunge kusimama kidete kufanya kazi ya kweli ya uwakilishi wa wananchi ni wakati wa kuthibitisha kuwa mhimili wa bunge ukiamua kufanya kazi hakuna kinachoshindikana katika nchi hii
mwisho tunawasihi wabunge watende haki wawe tayari kuwawajibisha wote waliohusika kwenye sakata hili lakini wasitumie mwanya huu kuwakomoa wabaya wao kisiasa kama tulivyoona katika ripoti ya operesheni tokomeza macho na masikio ya watanzania sasa yanasubiri kuona na kuasikia kazi iliyotukuka kutoka kwa wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania kwa pamoja tukiamua tanzania bila ufisadi inawezekana kabisa
« nyaraka za ufisadi zachomwa ngorongoro
escrow ni jaribu kubwa kwa katiba » | 2017-08-22T03:26:02 | http://www.jamhurimedia.co.tz/wabunge-msiwaangushe-watanzania/ |
diwani chadema ahamia ccm kisa biashara zake haziendi vizuri mtembezi
home habari diwani chadema ahamia ccm kisa biashara zake haziendi vizuri
diwani chadema ahamia ccm kisa biashara zake haziendi vizuri
matukio ya madiwani kuhama chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) na kujiunga na chama cha mapinduzi (ccm) yamezidi kushika kasi baada ya diwani wa tano wa kata ya olsunyai elirehema nnko kuhama chama hicho jana
aidha tangu kuanza kwa matukio ya kujiuzulu madiwani wa chama hicho mwaka jana hadi sasa wamefika watano walioachia ngazi
madiwani wa chadema waliojiuzulu na na kjiunga ccm ni credo kifukwe (muriet) geyson ngowi (komandolu) ambao tayari kaza zao uchaguzi umesharudiwa na ccm kuzinyakua
wengine ambao wamejiuzulu karibuni na uchaguzi bado kufanyika ni elirehema nnko (olsunyai) prosper msofe (daraja mbili) na obeid mengoriki wa kata ya terati
akizungumza jana wakati akitangaza kuachia ngazi chadema na kujiunga ccm elirehema alisema sababu kubwa ya kuhama ni za kibiashara
biashara zangu haziendi vizuri nadhani nikiwa ccm zitabadilika natakuwa nzurialisema
sababu hiyo aliyotoa diwani huyo inakuwa tofauti na walizotoa wenzake waliomtangulia kutoka chama hicho ambao wanadai sababu kubwa ni kuguswa na jitihada za rais john magufuli na kuamua kumuunga mkono kwa kujiunga na chama tawala
previous articlevigingi 7 bajeti kuu ya serikali vyatajwa
next articlemagufuli kuzindua ujenzi wa reli dodoma
nape afunguka dosari za uchaguzi wa madiwani
mwandishi wetu november 27 2017 | 2018-09-24T14:16:25 | http://mtembezi.co.tz/2018/03/14/diwani-chadema-ahamia-ccm-kisa-biashara-zake-haziendi-vizuri/ |
mbunge viti maalum ccm anusurika kifo ajalini leo ~ daily newshabarileo ' if(imglength>=1) { imgtag = '
mbunge viti maalum ccm anusurika kifo ajalini leo
toyota vx lenye namba za usajili t329 dgk alilokuwa akisafiria mbunge wa viti maalum mkoa wa ruvuma sikudhani chikambo (picha ndogo) iliyopata ajali na kusababisha kifo cha mtu mmoja leo mchana eneo la dumila wilaya ya mvomero mkoani morogoro
mbunge huyo pamoja na watu wengine watano walikuwa wakisafiri kutoka dodomna kwenda jijini dar es salaam ndipo gari walilokuwa wakisafiria toyota vx lenye namba za usajili t329 dgk kupasuka gurudumu na kuacha njia na kupinduka na kusababisha kifo cha ndugu wa mbunge huyo
dereva alikuwa anakwepa shimo lakini kutokana na ukubwa wa shimo tairi lika tumbukia na kupasuka gari iliyumba na kupoteza mwelekeo na kupinduka mara tano kabla ya kusimamaalisema sikudhani
alisema aliyepoteza maisha ni ndugu wa karibu wa kiume aliyekuwa akiishi dodoma na kufanyia kazi za ujenzi wa nyumba
alisema baada ya ajali walikimbizwa hospitali ya kanisa katoliki dumila na baadae kuhamishiwa hospitali ya rufaa mkoa wa morogoro
wabunge mbalimbali wa mkoa wa morogoro wakiongozwa na mbunge wa morogoro mjini abdulaziz abood mbunge wa morogoro kusini mashariki omary mgumba mbunge wa mtera livingstone lusinde na mbunge wa viti maalumu vyuo vikuu dk jasmine tisekwa walimtembelea na kumjulia hali
dk tisekwa ndiye alimsaidia mbunge mwenzake na majeruhi kuletwa hostitali kuu | 2018-05-26T15:58:07 | http://dailynewstzonline.blogspot.com/2017/07/mbunge-viti-maalum-ccm-anusurika-kifo.html |
sekondary ya mataira | jamiiforums | the home of great thinkers
sekondary ya mataira
discussion in 'jokes/utani + udaku/gossips' started by senator p nov 6 2011
kuna sekondar moja iko mjini kahama shinyangajna limehfadhiwayaani ile sekondary ni ya mataira director wa shule elimu yke darara la pilimkurungenz wke hakusomamkuu wa shule ana digrii lakin hana maamuz yoyote hta km mwanafunz hafai ktk taarumasecond master hana sfa wala uwezo na huwa anavuta bng ktk vyoo vya walimuyote tisa + 1=91academic & ndio wenye busaratatzo hawana maamuzwenye maamuz ni mwasibuambaye nae hajasomea uhasibu
md kuna lugha nyingi ambazo unazizuia lakini kama mtu je ametumia lugha ya kumkashifu binadamu mwenzake kama vile kutumia neno 'taahira' kubeba uchafu au uwezo mdogowa kufikiria mtu alionao mie naona concept hiyo ni wrong kutumiwa katika kuelezea mambo machafu au uwezo mdogo wa kufikiria mtu alio nao kwani nielewavyo mtu 'taahira' ni mwenye ulemavu wa akili 'means people with mild or severe interlectual disability and who may need support in learning living skills
tusitumie lugha ngumu za kuwadhalilisha wenzetu ndugu yangu yawezekana ni ndugu yako au jirani yako au ndugu yangu au jirani yangu au mwanangu
critical thinkers in here at jf never use abusive language punguza makali
kama umewahii kupitia walau shule ya msingi na hapa kwetu tv na radio nyingi zinatangaza kwa kiswahili na hata magazeti yanaandika kwa kiswahili na kiswahili ni lugha ya taifa lakini bado umeandika kwa kiswahili cha daraja hilobasi chonde chonde usiende kuomba kazi tanesco maana mgao wa umeme utaongezeka hahahaha
speak openly hebu itaje hatuna muda wa majungu hapa jf hata kama ni utani
mdau uliotoa huu uzi we nani kwenye iyo shule
saikoloj ipo poa sana mdau
likes received 20288
yeye ni msaidizi wa director na ndiye mlinzi mkuu
duh hiyo itakuwa kubwa kulko ila shule yenyew kama nilishaiski siyo ra's kwelokey poa ndo yenyewe nimeikumbukaila mwakani wana mpango wa kwenda kupata milembe kupata tiba isikuumize mno
yeye ni secondmisstress
kwahiyo iwe je
kama academic mrelimu yake ngumbaroo
godfrida member
sio kweli
haya majungu bwana wakuajiri wewe bac c unajiona timamu | 2018-01-16T16:28:57 | https://www.jamiiforums.com/threads/sekondary-ya-mataira.189604/ |
ajira za walimu 2016 soma hapa habari mpya kuhusu post za walimu 2016
author topic ajira za walimu 2016 soma hapa habari mpya kuhusu post za walimu 2016 (read 575 times)
« on february 16 2016 123050 pm »
serikali inatarajia kutoa ajira 40000 kwa walimu wa shule za msingi na sekondari mwaka huu
naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa (tamisemi) suleiman jaffo alilieleza nipashe jana kuwa idadi hiyo inalenga kupunguza upungufu wa walimu shuleni
sambamba na hilo ameahidi kushirikiana na halmashauri ya manispaa ya temeke kuwezesha wanafunzi zaidi ya 5800 wa shule ya msingi majimatitu wanapata elimu bora
alisema idadi hiyo ya wananfunzi ni sawa na idadi ya shule sita za msingi hivyo itagawanywa katika shule za jirani pamoja na kujenga madarasa mapya katika shule hiyo
ongezeko hili la wanafunzi waliojiandikisha darasa la kwanza mwaka huu limetokana na mfumo wa serikali kutoa elimu bure na lengo la serikali ni kutoa elimu bora hivyo kama serikali tutahakikisha tunaboresha mazingira kwa kuweka madawati ya kutosha madarasa na walimu hivyo hakuna mwanafunzi atakayekaa chini kuanzia mwezi wa sita alisema jaffo
pia alisema serikali itahakikisha inaongeza majengo katika shule hiyo pamoja na kujenga shule mpya umbali wa kilomita moja kutoka shule hiyo ilipo katika kiwanja kilichotolewa na katibu mkuu kiongozi mstaafu balozi martin lumbanga kwa ajili ya kujenga shule mpya
alimtaka mkurugenzi wa manispaa hiyo photidas kagimbo kuangalia uwezekano wa kujenga jengo la ghorofa katika kiwanja hicho ili kukidhi mfumuko wa wanafunzi wanaoandikishwa kila mwaka pamoja na kupunguzia wanafunzi wa shule ya mbagala majimatitu katika shule hiyo mpya
pia aliwataka kuwashirikisha wamiliki wa viwanda wa manispaa hiyo mchakato wa ujenzi wa madarasa ili kukamilisha kazi hiyo kwa wakati
jafo pia alimtaka ofisa elimu wa wilaya hiyo angel frank kuhakikisha walimu wa shule hiyo wanaotakiwa kupandishwa daraja wanafanyiwa hivyo pamoja na kulipwa mishahara stahiki kwa wakati kutokana na kazi kubwa wanayoifanya ya kulea watoto hao
naye mkuu wa shule hiyo abdallah ngomi alisema shule ina zaidi ya wanafunzi 5800 walimu 77 wakati mahitaji yakiwa ni walimu 131 na madawati 900 hali inayowalazimu kuweka madawati 52 katika darasa moja badala ya 15 huku mahitaji ya kwa shule nzima yakiwa ni 1959
tuna uhitaji wa vyumba vya madarasa 131 na kwa sasa tunavyo 22 pekee na tunatarajia kujenga 10 hivyo mahitaji ni 109 matundu ya vyoo pia tunahitaji 203 wakati tunayo 36 tu
kutokana na idadi hiyo kubwa wanafunzi wanalazimika kusomea nje na wengine kuingia kwa awamu alisema
mwaka huu shule hiyo imeandikisha wanafunzi 1022 wa darasa la kwanza idadi ambayo ni sawa na wanafunzi wa shule moja
jisajiri hapa chatguest kupitia link yangu hapo chini ili nikupe taarifa kwenye email yako siku wakitangaza post za ualimu 2016
click my link join i will tell you how to get money from this website join now http//wwwchatguestcom/indexphpaction=refferalsrefferedby=15
tembele chatguestbonyeza link hapo chini na ujisajili
re ajira za walimu 2016 soma hapa habari mpya kuhusu post za walimu 2016
« reply #1 on february 16 2016 051135 pm »
wafanye haraka katika kuajiri walimu maana hali si nzuri kwa shule zetu waache kuwaweka pia vijana mda mrefu kitaa
mtandao bora unaokulipa kwa kila kazi utakayofanya kupitia hapa jisajili sasa uongeze kipato chako bonyeza=>
http//wwwchatguestcom/indexphpaction=refferalsrefferedby=1730
refferal name thebeast
karibu chatguest ulipwe sasa ukiwa unasoma
« reply #2 on february 20 2016 100617 pm »
lini serikali itaajili walimu maana shule zetu zimelemewa kwa kuwa na wanafunzi wengi kupita uwezo | 2020-07-06T04:30:52 | http://www.chatguest.com/education-forum(jukwaa-la-elimu)/ajira-za-walimu-2016-soma-hapa-habari-mpya-kuhusu-post-za-walimu-2016/ |
godoni vu'a maiu'ina epasasi 1
☰ epasasi 1 ◀ ▶
epasasi
1 na porura godoni ura ijino jesu keriso oni apasorua rejuta ꞌenaꞌomo godoni ehija epasasi hijura kaꞌene jesu keriso oni vaji uchaha paꞌajihi punaꞌe veju 2 maiji vwihaniꞌina ꞌee matauviꞌina kaꞌene godi núni oma ꞌee natohwa jesu keriso oni rena roajija ja puꞌúmuna
keriso oni vaji ꞌavena huni merajihiꞌina
3 núni natohwa jesu keriso oni godi ꞌee omiji taꞌaroha hura ꞌavena huni merajihiꞌina kaꞌene akúpi ꞌahi navujija keriso oni vaji mahoꞌo merajúha paranana 4 ꞌene hu nú mweꞌa pavejiꞌini huni vaji iji pijúhana ꞌejakame nú huni unaꞌi oja mahiꞌina rene akuaviꞌina rene ꞌee sisea panamuhiꞌinaꞌe reꞌavarono iji pijúhana 5 ꞌene jesu keriso oni vaji huni harihijaꞌe ꞌekuhunijaho nitama huni ura ijino hu ura renajaꞌinaꞌe amairiaramana 6 ꞌene huni maiji vwihaniiꞌini jihuni pinaniji taꞌaroꞌavarono hura oja múhiꞌini jihuni vaji maꞌekuana 7 ꞌene hura ori huni ꞌaa vajijino niꞌajúhe kúꞌo ꞌekuana huni maiji vwihaniiꞌina kaꞌene ituꞌoꞌuna namuna vajijino núni sisea vwihanúe aremana 8 ꞌene hura huni maiji vwihaniiꞌina kaꞌene ituꞌona namuna vajijino vwiha mamaa mahoꞌone ꞌee henaka mahoꞌo ꞌusesamúhana 9 godi huni ura ijihuni hemijaho vejume núnunaꞌa samaumaa renana godi huni ura ijino keriso oni vaji hu ura renajaꞌinaꞌe venana 10 ꞌene vea roe areri rena parajakaviꞌi uneunecha mapoka keriso oni vaji ichutoi navura ꞌee mweꞌi navura ꞌekaroe huni harura hari nahuna 11 hura nitama huni ura ijino iji pijúhana hura amairiarama jaꞌinaꞌe ꞌee huni aachia ꞌuꞌo ꞌekara ꞌene uneunecha mahoꞌo hura ura rene ꞌee ꞌwarama jaꞌinaꞌe rejara 12 ꞌejakame ikehuni urijaho nú ea kaꞌene amuraꞌe keriso nimaa rojujaho huni mamaiji taꞌarohuna 13 ja ꞌuꞌo huni vaji huni ira nimaiji hene ꞌee vuꞌa maa maiuꞌina kaꞌene ja niꞌajihana ka ja nimaa rojume huni ꞌavena kaꞌene nahama ꞌwaramajaho joni vaji huni tatua vene mihana 14 huni ꞌavena kaꞌene nú múhajaho huni aachiji ꞌekahuna tatua vene múhana ꞌene godi omaꞌe rehunaꞌe kúꞌo ꞌuname ꞌimenúa avanana ꞌene huni mamaiji taꞌaroꞌavarono avanana
15 ikehuni hahi na joni vaji natohwa jesu nimaa rojuji hene ꞌee jara godoni ehija mahoꞌo oja mihuji hejujaho paꞌuhuname paturanaꞌikaꞌi 16 na jonijihunaꞌe joni ihi ꞌurihe siporua ꞌone teimani ꞌwavura 17 ꞌejakame núni natohwa jesu keriso oni godi ꞌee oma kaꞌene pinana rukinijara vwiha kaꞌene vwiha mamaa vwihane ꞌee jonunaꞌa veje samaumaa rene ꞌee hu hena kahunijaho samaumaa rehuna 18 ꞌene na siporua ꞌojujaho joni oja jaraa kame hura maa irakijihunaꞌe ja ꞌumenaajaho hena kahuna ꞌene huni uneunecha mapoka mavarasaꞌina kaꞌene huni ehijijipo ꞌekujija hena kihuna 19 ꞌene huni harura niꞌimaꞌura kaꞌene nú nimaa rojiꞌina kihipunaꞌi veꞌamajaho hena kahuna ike harura niꞌimaꞌura kaꞌene núni vaji kaukara venujaho 20 ijí harura kajara kerisora kwamajaho vejume ꞌurinana ꞌene vejume akúpi ꞌahi godoni ija manaꞌinijaꞌi asuma hinana 21 iviamai ikehuni vea ikeru pana kaivo túnaꞌa ꞌuꞌo ꞌajohaiꞌina mamaꞌina harura ꞌee harura mahoꞌo ꞌee iha ichaꞌina kaꞌene ja ꞌurihujaho asitaha parane huri hinana 22 ꞌene godira uneunecha mahoꞌo huni mumora hari irechamana ꞌene uneunecha mahoꞌo ꞌee sosia hura húmata rehunaꞌe mahana 23 ꞌene sosijaho huni haha kaꞌene hu ijihuni vaji mahoꞌo areri rena paranujina ꞌee hu uneunecha mahoꞌo areri rena paranu | 2019-09-15T15:58:07 | https://ebible.org/study/content/texts/mcq/EP1.html |
trump putin kupambana na isis | mtanzania
home kimataifa trump putin kupambana na isis
trump putin kupambana na isis
rais wa marekani donald trump na vladimir putin wa urusi wamekubaliana kuhakikisha wanapambana kwa nguvu zote ili kundi la wapiganaji wanaojiita islamic state (is) linashindwa vita nchini syria
kwa mujibu wa maofisa wa rais wa urusi wamesema viongozi hao wawili wamekutana jana kwa muda mfupi pembezoni mwa mkutano wa viongozi wa nchi za asia na pasific nchini vietnam
viongozi hao wawili walikutana mara tatu katika kipindi cha saa 24 katika mji wa da nang hata hivyo hakuna taarifa rasmi kutoka kwa serikali ya marekani kuhusu tamko lililotolewa na serikali ya urusi
mkutano kati ya rais trump na vladimir putin ulitarajiwa kufanyika wakati wa mkutano huo wa apec lakini ni maelezo machache sana ambayo yametolewa
wawili hao walikutana kwa mara ya kwanza julai katika mkutano wa nchi tajiri zaidi duniani g20 katika mji wa hamburg nchini ujerumani
maswali kuhusu uhusiano wa donald trump na urusi yamekuwa yakiulizwa mara kwa mara wasaidizi wake wakuu wa zamani wanachunguzwa kwa tuhuma za kushirikiana na urusi kuingilia uchaguzi wa urais wa marekani wa mwaka 2016 lakini serikali ya urusi imekanusha tuhuma hizo
ingawa ikulu ya marekani haijasema chochote kuhusu mkutano wa wawili hao taarifa ya kremlin iliyotolewa jana imesema viongozi hao waliafikiana kwamba mzozo wa syria hauwezi kutatuliwa kwa njia ya kijeshi
aidha viongozi hao wamekaririwa wakisema kujitolea kwao kutasaidia kuwashinda magaidi wa isis na kuzitaka pande zote kushiriki mazungumzo ya amani ya geneva
kwa mujibu wa shirika la habari la interfax la urusi wameahidi kuendelea kudumisha njia za mawasiliano za kijeshi kati ya majeshi ya urusi na marekani kuzuia uwezekano wa kushambuliana na is
urusi imekuwa ikiunga mkono serikali ya rais bashar alassad katika vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyodumu miaka sita sasa marekani nayo huwasaidia waasi wa makundi ya waarabu wa syria na wakurdi
tangu 2014 marekani imeongoza muungano ambao umekuwa ukitekeleza mashambulio ya kutoka angani dhidi ya isis nchini syria
previous articleujue ugonjwa wa homa ya ini
next articleputin aunga mkono soko huru asia pasifiki
urusi misri kuimarisha ushirikiano | 2018-10-17T03:41:24 | http://mtanzania.co.tz/trump-putin-kupambana-na-isis/ |
pitio la 0933 16 januari 2020
93 bytes added miezi 5 iliyopita
→jeshi la taifa
pitio la 0826 16 januari 2020 (hariri)
417522121 (majadiliano)
(→jeshi la taifa)
pitio la 0933 16 januari 2020 (hariri) (tengua)
chipalo e (majadiliano | michango)
d (→jeshi la taifa)
== jeshi la taifa ==
jeshi la taifa ni chombo kilichoanzishwa kisheria chenye silaha na askari wenye mafunzo ya kivita amabao kazi yao ni kupambana kivita kulinda ardhi ya nchi husika dhidi ya uvamizi kutoakutoka nje nchi huwa na jeshi moja la kulinda mipaka yakyake dhidi ya uchokozi kutoka nje lakini pia huwa na majeshi 'usu' kadhaaa kwaajili ya kulinda usalaama wa ndani kwa mfano majeshi ya nchi ni kama [[jeshi la uganda updf jeshi la tanzania tpdf nk|jeshi la uganda updf jeshi la tanzania tpdf nk]] majeshi usu ni kama polisimagerezauhamiaji zimamoto na tanapa
shughuli nyingi za majeshi hutofautiana kulingana na kitengo husika cha jeshi kwa mfano jeshi la nchi kavujeshi la anga na jeshi la majini haya ndiyo matawi makuu matatu ya jeshi kwa historia jeshi la anga lilikuwa pamoja na jeshi la ardhiardhini hasa kwa historia ya [[uchina]] ama [[jeshi la ukombozi wa umma wa uchina]] ilichanganya (jeshi la ardhi jeshi la majini jeshi la anga divisheni za makombora na usayari) kwa tawi moja
majeshi ya kisasa yaitwa pia ''huduma'' ama ''[[askari watawala]]'') hii inaweza kuhusu pia matawi ya [[vita]] [[jeshi la nchi kavu]] [[kifaru (vita)|vifaru]] [[makombora]] na [[mhandisi wa jeshi]] na pia [[wasafirishaji]] wa matawi kama [[mawasiliano ya kijeshi|mawasiliano]] [[jeshi la watambuzi|watambuzi]] [[daktari wa kijeshi|daktari]] [[jeshi la vifaa|wapeleka vifaa]] na [[jeshi la ndege]] (tofauti na jeshi la anga)
jeshi laweza kuwa kubwa kama chama [[chama cha jeshi]] ([[shurutisho la jeshi|shurutisho]]) ambayoambalo inalina kundimakundi nyingimengi zaidi zaya [[askari]] jeshi tofauti hujigawa kulingana na utamaduni wao &mdash hasa marekani ([[jeshi la kwanza la marekani]]) kwa [[jeshi la uingereza]] jeshi kwa shurutisho ni jeshi la kwanza na marekani ni divisheni ya kwanza
([[jeshi kikundi]] ama [[kinara|jeshi kinara]]) ni shurutisho kubwa zaidi kulingana na umma utatuzi na ushirikana
chipalo e
rudishwa kutoka https//swwikipediaorg/wiki/maalummobilediff/1097896 | 2020-07-06T00:51:53 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Maalum:MobileDiff/1097896 |
habari na matukio hati za bayport zatolewa kwa mtindo wa aina yake
hati za bayport zatolewa kwa mtindo wa aina yake
meneja biashara wa bayport financial services thabit mndeme kushoto akimpatia hati ya kiwanja cha vikuruti mteja wao ibrahim yusuph ismail nyumbani kwao kariakoo jijini dar es salaam leo mchana kwa wiki hii tu bayport imeamua kuwapelekea hati za viwanja wateja wao katika maeneo yao ya makazi na maofisini kwao na mwandishi wetu dar essalaam
rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania dkt john pombe magufuli akimkabidhi nyenzo za kazi dkt harrison mwakyembe baada ya kumuapisha ku | 2017-03-27T06:38:05 | http://www.kajunason.com/2016/03/hati-za-bayport-zatolewa-kwa-mtindo-wa.html |
kimbuga neymar mbappe chatikisa ligi kuu england mwanaspoti
kimbuga neymar mbappe chatikisa ligi kuu england
kwa hali ilivyo ndani ya miaka mitatu ijayo kwa maana ya kuanzia sasa ligi kuu england itakuwa kwenye hatari ya kuondokewa na mastaa wake wote wa maana
london england nyota eden hazard ameshaondoka zake msimu unaokuja hatakuwapo kwenye ligi kuu england tena paul pogba na romelu lukaku nao wanapiga hesabu za kuipiga kibuti ligi hiyo baada ya kuwapo kwa taarifa kwamba wawili hao wapo kwenye mikakati ya kuachana na manchester united
christian eriksen naye yupo njiani kuachana na tottenham hotspur huku mastaa alexandre lacazette na pierreemerick aubameyang wamekuwa kwenye maneno maneno ya kuachana na arsenal kama si dirisha hili la majira ya kiangazi bas lile la mwakani
supastaa mohamed salah ameshaweka wazi kwamba huenda msimu utakaoanza utakuwa wa mwisho kwake kuitumikia liverpool huku jambo kama hilo likitarajiwa kutokea kwa mkali mwenzake wa huko anfield sadio mane hivyo hivyo mastaa wa maana wanavyotarajia kuachana na ligi kuu england kwenye kipindi hiki cha uhamisho
lakini wasiwasi zaidi unakuja kutokana na ukweli ni kwamba hata mastaa wa ligi nyingine waliotazamiwa kuja kwenye ligi kuu england wanawaza kwenda kwenye timu nyingine za huko italia hispania na ufaransa
mastaa neymar antoine griezmann kylian mbappe na paulo dybala wote hawatajwi kuwa na mpango wa kwenda kukipiga kwenye ligi kuu england
akili ya mastaa hao kwa sasa ni kwenda kwenye klabu za huko hispania kama si barcelona basi ni real madrid huku paris saintgermain na juventus nazo zikiwa na mvuto mkubwa kwa mastaa wenye majina makubwa kuliko timu za ligi kuu england wakiwamo vigogo manchester united manchester city arsenal chelsea tottenham na liverpool
baada ya timu za england kutamba kwenye soka la ulaya kwa msimu uliopita kwa maana ya michuano ya europa league na ligi ya mabingwa ulaya wababe wa hispania real madrid na barcelona zimeamua kumeza mate ya akili ikiwa pamoja na kufanya usajili wa maana ili kuwa na vikosi vya kutisha msimu ujao
juventus nao wamekuwa wakiimarisha wakiwanasa mastaa wa nguvu akiwamo aaron ramsey aliyetoka arsenal moja ya wababe kwenye ligi kuu england
kwa hali ilivyo ndani ya miaka mitatu ijayo kwa maana ya kuanzia sasa ligi kuu england itakuwa kwenye hatari ya kuondokewa na mastaa wake wote wa maana kutokana na ukweli kwamba wakali wake wa sasa wanaoipa hadhi ligi hiyo kama vile pogba mo salah mane lukaku eriksen na hata harry kane wanaweza kushawishika kuachana na ligi hiyo wakati vigogo real madrid au barcelona zitakapohitaji saini zao
ilikuwa rahisi sana kwa barca kunasa huduma ya philippe coutinho januari mwaka jana na ilikuwa rahisi kwa real madrid ilipowang'oa hazard na thibaut courtois kwenye ligi kuu england kama ilivyotaka kumng'oa pia pogba na eriksen
barcelona wanapiga hesabu za kumnasa victor lindelof kutoka man united kitu ambacho kinazidi kuivuruga zaidi ligi kuu england katika miaka ya karibuni
wakati wote wa ligi kuu england wanasakwa na real madrid barcelona psg na juventus na kinachoonekana ni kwamba timu hizo zitakwenda kugawana mastaa hao kutokana na nguvu yao ya kifedha na mikakati ya kujijenga kwa mipango ya kutamba kwenye mchezo huo huko ulaya na duniani
hakuna dalili pia ya kumwona neymar mbappe au griezmann kutua kwenye ligi kuu england na hivyo kutishia usalama wa mastaa zaidi kwenda kucheza ligi hiyo licha ya kwamba imekuwa ikisifika kwa kutoa mishahara mitamu | 2019-09-18T14:08:07 | https://www.mwanaspoti.co.tz/soka/Kimbuga-Neymar--Mbappe-chatikisa-Ligi-Kuu-England/1799484-5172594-u8k9lz/index.html |
athari ya kirusi cha zika ~ nasaha zetu
athari ya kirusi cha zika
unafiki wa nchi za ulaya na amerika
kushoto ni mtoto aliyeathirika na kirusi cha zika
kirusi cha zika kina mahusiano ya karibu na kirusi kinachosababisha homa ya dengue homa ya manjano (yellow fever) iki kirusi kimegunduliwa miaka ya 40
wataalam wa afya wanahisi kirusi hiki kilianzia aidha nchi za kiafrika au asia na inasemekana mwaka 1947 kwenye msitu wa zika nchini uganda karibu na ziwa viktoria walichua aina ya nyani wenye mikia mifupi wakati kwa ajili ya utafiti wa chanjo ya homa ya manjano (yellow fever)
baadae wakaja kugundua kuwa njani waliokuwa wakiwafanyia majaribio wamepata aina ya homa tofauti na homa ya manjano ndipo homa hio wakaita zika na vijidudu vilivyo sababisha hiyo homa ambavyo kwa asili vinatokana na virusi vya homa ya manjano wakavipa jina zika virus hii ilikuwa miaka ya 1950
baadae kwenye miaka ya 60 alipatikana mgonjwa nchini nigeria na ugonjwa ukaenea inakisiwa ni kuanzia miaka ile ya 1950 mpaka 1981
baadae wagonjwa kadhaa wakaanza kupatikana kwenye nchi za kiafrika kama vile afrika ya kati misri sierra leone tanzania na uganda na nchi zilizo asia kama vile india indonesia malaysia philippines thailand na vietnam
kirusi hiki kinasambazwa na aina fulani ya mbu na haswa kipindi cha mchana kirusi hiki kinaambukiza na kama mama ni mja mzito basi kondo lake au mfuko wa kizazi uathirika na mtoto aliyeko tumboni naye uathirika kwenye ubongo wake na mtoto uzaliwa akiwa mwenye matatizo ya kiakili
miaka yote hoyo hakuna nchi yoyote ya ulaya au shirika lolote la kimataifa lililothubutu kusema chochote au kuchukuwa hatua yoyote kudhibiti kuenea kwa kirusi hiki kwa sababu hakikuwepo kwenye nchi za ulaya na amerika
mwaka 2014 kirusi au wagonjwa walianza kupatikana kwenye nchi zilizo kwenye ukanda wa bahari ya pacific haswa nchi zinazojulikana kama french polynesia
nchi ambazo ugonjwa huu umeenea ni new zealand samoa tonga cook islands tuvalu tokelau niue wallis futuna papua new guinea na visiwa vya solomon na fiji
baadae mwaka 2015 nchi za mexico amerika ya kati nchi za karibbeian amerika ya kusini kama vile brazir kirusi cha zika kimetangazwa kuwa ni janga la kitaifa
mwezi december mwaka 2015 nchi za ulaya (european) kupitia kituo cha kuzuia na kudhibiti magonjwa nchi za ulaya (european centre for disease prevention and control) wameweza kutoa ripoti kamili jinsi kirusi iki kinavyo athiri binadamu na hatua za kuchukua haswa kwa wamama wajawazito
na hii imetokana kuwa nchi za ulaya na amerika kuna wagonjwa ambao wameathirika na kirusi iki kama vile tulivyo shuhudia wagonjwa wa ebola walipopatikana nchi za ulaya na amerika ndio nchi hizi zikazibduka na kuona kuwa ili ni tatizo la nchi zote ulimwenguni na si nchi za kiafrika na asia tu peke yake
hapa ndio utaona kuwa hizi nchi kama janga alija wakuta mashirika ya kimataifa kama vile shirika la afya duniani who (world health organisation) uwa awachukulii kuwa haya majanga yanayoikumba afika au nchi zilizo eshia (asia) yanaweza kufika kwenye nchi za ulaya na amerika ni mpaka pale wakipatikana wagonjwa kwenye nchi zao ndio utaona kuwa wakichukua hatua za kudhibiti na hata kufanya uchunguzi wa kina jinsi ya kuzuia au kutibu kwa magonjwa husika | 2017-08-20T08:07:47 | http://nasahazetu.blogspot.com/2016/02/athari-ya-kirusi-cha-zika.html |
bob wine aachiwa kwa masharti magumu kesi yake yaendeshwa kwa njia ya video mwenyewe akiwa gerezaniawasiliana na hakimu kupitia teknolojia hiyo | robengo16
msanii na mwanasiasa wa upinzani nchini uganda robert kyagulanyi ameachiwa kwa dhamana na mahakama mjini kampala japo kwa masharti makali
mchakato wa kulisikiliza ombi lake la dhamana uliendeshwa kwa njia ya video akiwa gerezani luzira aliweza kuwasiliana na hakimu kupitia mawasiliano hayo ya video hatua ilioepusha kutokea kwa vurugu kama ilivyotarajiwa iwapo angasafirishwa hadi mahakamani
ameshtakiwa kwa kushiriki katika maandamano ya haramu mnamo mwaka jana ya kupinga kodi ya kutumia mitandao ya kijamii maarufu uganda kama ott
wafuasi wa mbunge robert kyagulanyi walionekana wakiimba wimbo wao wa ushindi baada ya hakimu wa mahakama ya buganda road kukubali ombi la bobi wine kupewa dhamana
uamuzi huo ulitolewa katika kikao kilichochukua muda wa saa nne upande wa serikali ukipinga apewe dhamanakabla ya hakimu kumpatia dhamana bobi wine alipewa fursu ya kuzungumuza
napenda kusisitiza kwamba sio mimi ninayeshitakiwa mahakamani ni mahakama yenyewe maamuzi ya mahakama itakayotowa sio tatizo kwangu mimi nitaendelea na kusema ukweli
kazi yangu ni kutetea haki kazi yangu ni kupigania haki yako wewe hakimu na mimi na raia wengine wa uganda kama itakuwa haki mimi kubaki hapa korokoroni nitamushukuru mwenyezi mungu kwa sababu nina kazi nyingi za kufanya hata hapa gerezani alisema mwansiasa huyo wa upinzani
masharti magumu aliopewa bobi wine
kyagulanyi amepewa masharti magumu ya dhamana kulingana na umarufu wake anapopita mjini anakuwa na wafasi wakubwa wakimufatilia na katika masahriti hayo amekatazwa kuhusika katika mkusanyiko au maandamano kama anavyosema wakiri wake asumani basalilwa
haya masharti yanashangaza kwasababu ni nani ana uwezo wa kusema maandamano ni mazuri au mabaya
kama hiyo nguvu wanajipatia polisi rafiki yetu bobi wine asiwe huru nchini mwetu kwasababu polisi wanaweza kukamata watu bila mpango wanaweza kukukamata ukiwa unafanya kazi yako unaenda kula wanakukamata kama ni mahakama itasema mkutano huu ni haramu hivyo ni vizuri lakini kama ni polisi kutakuwa na vita vingi amesema asuman
licha ya mashariti aliyopewa mawakili wake hawakufurahishwa na mfumo wa mahakama uliotumiwa wa teknolojia bila ya kuwasiliana na mteja wao akiwa luzira
sio teknolojia mbaya lakini leo sheria yetu uganda inasema ni lazima uje mahakama uwasilishe ombi kama unataka kufanyisha video conference lakini hakuna aliyekuja hapa kuwasilisha ombi hilo kwa hivyo kilichofanyika hapa ni kinyume cha sheria
watu waliokuwa mahakamni hawajafurayishwa na maamuzi ya mahakama jinsi serikali inavyomunyima haki za kufanya kazi robert kyagulanyi
hakuna demokrasia hapa kila anayetaka kuwa rais anawekwa mahabusu ameeleza raia mmoja aliokuwepo nje ya mahakama kampala
kampeni mpya ilianzishwa katika mitandao ya kutaka bobi wine aachiliwe huru huku baadhi wakizungumzia hatua hiyo kama ya kutia wasiwasi
mashirika ya kutetea haki za binaadamu likiwemo la marekani tom lantos human rights commission na shirika linaloshinikiza uongozi wenye maadili na demokrasia kwa wote vanguard africa yameshutumu hatua hiyo ya serikali ya uganda
bobi wine alikamatwa siku ya jumatatu wakati akilipokuwa njiani kupeleka barua makao makuu ya polisi kuwafahamisha anakwenda kufanya mandamano ya kumunyima haki zake za kufanya kazi yake ya muziki ikiwa tangu mwaka jana wamezuia matamasha 124
← previous story vituo 13 vya radio na televisheni na wanahabari wa futwa kwa upotoshaji na kuchochea ghasia nchini uganda
next story → mfahamu nyoka mwenye macho matatu aliyegunduliwa na maafisa wa wanyama pori | 2019-06-16T00:28:49 | https://robengo16.com/2019/05/03/bob-wine-aachiwa-kwa-masharti-magumu-kesi-yake-yaendeshwa-kwa-njia-ya-video-mwenyewe-akiwa-gerezaniawasiliana-na-hakimu-kupitia-teknolojia-hiyo/ |
matokeo ya form two 2019
form two examination results 2019/2020 how to watch matokeo ya kidato cha pili 2019 bonyeza hapa matokeo ya kidato cha nne 2019 bonyeza matokeo ya darasa la nne 2019/20 standard four results 2019 tazama matokeo ya kidato cha pili 2019 form two results 2019 here
matokeo ya kidato cha nne (csee) 2011 link1 matokeo ya kidato cha nne (csee) 2011 link2 matokeo ya kidato nbc bank jobs 2012 specialist branch operations (8 posts) qualifications • bachelor of commerce or related degree • 2 yrs experience in branch operations
jan 09 2020 · check matokeo ya kidato cha pili 2019 matokeo ya kidato cha pili 2019 tanzania form two results 2019/2020 necta form two 2019 results matokeo ya form two 2019 necta matokeo ya form two 2019/2020 ftna 2019 results form two matokeo ya form two 2019 form two secondary education examinations (ftsee) and standard four national assessment (sfna
matokeo 4609 likes · 35 talking about this here are the examination results and past papers for form two form four and form six also exams results for std four & std seven
matokeo ya usaili wa interns import inspection noticesvacancies | shirika la viwango tanzania linapenda kuwataarifu waombaji wa nafasi za mafunzo kwa vitendo kazini (internship) waliofanya usaili tarehe 14092019 kuwa matokeo yapo tayari read more
kwa habari picha na matukio tembelea zanzinews tangaza nasi kwa bei nafuu (advertise with us ) tupigie 0777 424152 au tuandikie (email) [email protected]
jan 24 2019 · zanzibar yaula na chuya shule 10 bora kitaifa matokeo kidato cha nne posted by wahida | jan 24 2019 baraza la mitihani la taifa (necta) limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2018 ambapo shule ya wasichana ya st francis ya mkoani mbeya imeongoza kitaifa
matokeo ya mitihani kwa madarasa yoteexamination result here form two past papers questions and answers matokeo ya kidato cha nne mwaka 20182019 | necta
s1098 maji ya chai s1099 nyehunge s1100 ruiwa s1101 luagala s1102 mahuta t d f s1103 busongo s1104 idodi s1105 suba s1106 kikaro s1107 mwamashimba s1108 myamba s1109 stdorcas seminary s1110 kaloleni s1111 mashingia s1113 chanjagaa s1114 shelui s1115 bukandwe s1116 mtipe s1117 dabalo s1118 mlongwema s1119 zanzibar commercial
nectaform fourtwo&standard four resultmatokeo ya kidato cha nne na pili 2019 january 9 2020 january 16 2020 8 comments nectaform four two&standard four resultmatokeo ya kidato cha pili 2019 form four results 2019 | csee necta results 2019 |
i'm so excited to introduce you to news matokeo ya kidato cha pili 2017 2018 fuatilia hapa matokeo ya necta matokeo ya kidato cha nne 4 2018 2019 news alert necta imetangaza matokeo ya kidato cha nne 2017 necta form two and standard four national assessment examination
form two national assessment 2019/2020 matokeo form two 2019/20 the national examinations council of tanzania administered the form two national assessment (ftna) since 2014 the form two national assessment formats have been prepared taking into account the topics stipulated in the syllabuses currently in use
nectaform four two&standard four resultmatokeo ya kidato cha pili 2019 form two and standard four examination result 2019 summary of
form two ftna results 2019/20 (matokeo ya kidato cha pili) by maujanjamusic form two results click here form two results click here dear reader leave a comment below tags entertainment share this share it tweet share it share it pin it do not forget like our page below to get more songs for response
s1098 maji ya chai s1099 nyehunge s1100 ruiwa s1101 luagala s1102 mahuta tdf s1103 busongo s1104 idodi s1105 suba s1106 kikaro s1107 mwamashimba s1108 myamba s1109 stdorcas seminary s1110 kaloleni s1111 mashingia s1113 chanjagaa s1114 shelui s1115 bukandwe s1116 mtipe s1117 dabalo s1118 mlongwema s1119 zanzibar commercial
tazama matokeo ya kidato cha pili 2019 form two results 2019 here form two examination results 2019/2020 how to watch matokeo ya kidato cha pili 2019 bonyeza hapa matokeo ya kidato cha nne 2019 bonyeza 24 signs that show some wants to start love relationship with you
form four results 2019/2020 | csee necta (matokeo ya kidato cha nne 2019) author ajira faster date january 09 2020 tags matokeo ftna results 2019 matokeo form two 2019 by necta form two national assessment result 201920 matokeo ya upimaji wa kitaifa wa kidato ch
matokeo ya kidato cha plili&darasa la nne form two & standard four national assessment results january 2018/2019 the national link 1 click here for form two national assessment results after council darasa la nne kidato cha pili national plili standard
matokeo ya mtihani wa maarifa (qt) 2019 matokeo ya upimaji wa kitaifa wa kidato cha pili (ftna) 2019 the national examinations council of tanzania (necta) is government institution which was established by the parliamentary act no 21 of 1973 necta is responsible for the administration of all national examinations in tanzania read more
matokeo ya kidato cha pili na darasa la nne form two & standard four national assessment results january 2018/2019 national examinations council of tanzania announced form two and standard four national assessment results
all about deepening the connection with information matokeo halisi matokeo kidato cha pili 2018 2019 tazama matokeo ya kidato cha pili 2017 2018 hapa ð ¥hotâ hotð ¥ matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha pili 2014 wel e necta tanzania national examination results allow students to check the acsee results 2018 2019 by sms through mobile phone if you do not have internet
all about deepening the connection with information matokeo halisi matokeo kidato cha pili 2018 2019 tazama matokeo ya kidato cha pili 2017 2018 hapa ð ¥hotâ hotð ¥ matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha pili 2014 wel e necta tanzania national examination results
matokeo ya kidato cha nne 2019 dodoma looking for form four examination results 2019 necta form four results 2019 form four results 2019/2020 form four results 2019/20 form four results 2019/2020 necta results 2019 matokeo ya form four 2019/20 wwwnectagotz 2019 csee matokeo ya form four 2019/2020 artikel terkait unknown next post
ftna results 2018 form two national assessment result 2019 2020 have been announced today necta allow students to check the ftna results 2019 2019 by sms through their mobile or online by using the following liks
matokeo ya kidato cha nne 2019 after tanzania mainland had pulled out of the east african examinations council in 1971 and before necta was established by law in 1973 the curriculum and examinations section of the ministry of education was responsible for all examinations
necta | form two national examination result 2018/2019 by tubongemedia january 04 2019 form two national results the decision to establish necta was a followup of
nectaform fourtwo&standard four resultmatokeo ya kidato cha nne na pili 2019 after tanzania mainland had pulled out of the east african examinations council in 1971 and before necta was established by law in 1
january 8 2018 katibu mtendaji wa necta dk charles msonde ametangaza matokeo ya mitihani ya upimaji wa darasa nne na kidato cha pili iliyofanyika november 22 na 23 2017 huku idadi kubwa ya wanafunzi wakifanya vyema katika mitihani hiyo
jan 18 2019 · yatazame hapa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2018 january 24 2019 baraza la mitihani tanzania necta limetangaza matokeo ya kidato cha nne csee 2018 na matokeo ya mtihani wa maarifa (qt) 2018
jan 14 2019 · jinsi ya kuangalia matokeo ya form two hatua zote ziko hapa danfald chaneltv date 09 january 2018 tags matokeo ya kidato cha nne 2018 2019 video download
matokeo kidato cha pili 2019 form two results 2019 ftna results 2019 matokeo necta 2019/2020 matokeo kidato cha pili form two results 20192020 the national examinations council of tanzania (necta) is government institution which was established by the parliamentary act no 21 of 1973 matokeo ya kidato cha pili haya hapa
jan 01 2020 · necta form two results | ftna results | matokeo kidato cha pili ftna 2019 results matokeo kidato cha pili 2019 form two national assessment (ftna) is the exam that conducted by form two students to assess their knowledge so as to join form three for ordinary level in tanzania ftna exams are supervised by national examinations council of tanzania (necta)
matokeo ya kidato cha nne 2020 form four (csee) necta results 2019 2020 dar es salaam tanzania certificate of secondary education examination (csee) is as prescribed by circular number 1 of the ministry of education and vocational training (moevt) of april 2006
form two national assessment (ftna) results | matokeo ya kidato cha pili 2019 163 views tanzania january 16 2020 matokeo2019 others form two national assessment (ftna) results | form two examinations results | necta form two results all years ©2019 | ajirazotecom is not affiliated in any way with the companies whose vacancies are
necta form two results app kwaajili ya matokeo ya kidato cha pili 2019/2020 tazama matokeo ya form 2 necta kupitia app hii matokeo ya kidato cha pili 2019 101 apk download boxback top matokeo ya kidato cha pili 2019 20 apk download version 20 min sdk android 40x ice cream sandwich (sdk 14)
matokeo ya kidato cha pili&darasa la nne form two & standard four national assessment results january 2018/2019 the nat matokeo ya kidato cha pili&darasa la nne form two & standard four national assessment results january 2018/2019 the national examinations council of tanzania has announced the form two and standard four national assessment
matokeo mapya ya kidato cha nne haya hapa 1079 chikuyu s1080 muheza muslim s1082 mtii s1083 bumbuli s1084 vuma s1085 laureate international school s1086 ludewa s1088 tumbi s1089 kilimatinde s1090 chala s1091 bungurere s1092 kwemaramba s1093 aldersgate s1094 jihad s1095 wotta s1096 mitundu
jan 09 2020 · matokeo ya form four 2019/2020 story page loading unsubscribe from story page matokeo ya form four yaangalie live duration 045 danfald chaneltv 58494 views
jan 05 2019 · matokeo ya kidato cha plili&darasa la nne form two & standard four national assessment results january 2018/2019 posted on january 5 2019 by admin the national examinations council of tanzania has announced the form two and standard four national assessment results
eaa witness compact grips
dell r510 passthrough tax refunds kent
festival of sail tacoma 2019 jv characteristics of solar cell
the crown hotel napier meg peter quotes
hath ki silai onli taaty karti ladaki video
super automaticas semillas
examples of prejudice in healthcare razor 20 firmware
nba 2k14 team ratings ertugrul season 5 episode 16 vimeo
woolrich autumn ridge slipperschild law
http srs wsu edu et reviewhorsin around farm
premiere pro unsupported video driver70 aud to usd
template creatormitsubishi lancer timing chain replacement
plague vendor bioconstant mesh gearbox design calculations
tomas rimkus plunge
beretta 92x centurion pricelittle cat in chinese
commander root youtube
dec 13 2015 · on this page you can read or download matokeo ya mock exemination form four in pdf format if you don't see any interesting for you use our search form on bottom ↓ matokeo ya kidato cha nne 2020 form four (csee) necta results 2019 2020 dar es salaam tanzania certificate of secondary education examination (csee) is as prescribed by circular number 1 of the ministry of education and vocational training (moevt) of april 2006 jan 28 2019 · seaching for loan for jinsi ya kuomba mkopo wa chuo 2019/2020 hslb 2019 maombi ya mkopo wa chuo 2019bodi ya mikopo 2019/220bodi ya mikopo 2019/20bodi ya mikopo elimu ya juu 2019/2020majina ya waliopata mkopo 2019/2020fomu za bodi ya mikopomajina ya waliopata mkopo 2019/20fomu za bodi ya mikopo 2019/2020majina ya waliokosea kuomba mkopo 2019/2020 all news about higher education news matokeo ya form two katika matokeo ya kidato cha pili yaliyotangazwa na baraza la taifa la mitihani (necta) shule attached below is a copy of tusiime results as posted on necta website *this copy does not contain any matokeo ya kidato cha pili 2019 form two necta result 2019 click here to see form two examinations results 2019 | form two national assessment (ftna) results 2019 | necta form two results 2019 the united republic of tanzania for form form four and standard four results click here summary of necta's history after []
matokeo ya kidato cha plili&darasa la nne form two & standard four national assessment results january 2018/2019 the national link 1 click here for form two national assessment results after council darasa la nne kidato cha pili national plili standard matokeo darasa la saba 2017 pitia hapa matokeo ya mtihani wa darasa la saba 2017 gadiola emanuel october 20 2017 arusha elimu habari matukio contact form matokeo ya form two 2019/2020 online from 2016 the national examination council of tanzania (necta) developed online matokeo ya form two systems through the official website (wwwnectagotz) here is a guide on how to check the form two results online from the necta official website
dec 13 2015 · on this page you can read or download matokeo ya mock form 4 in pdf format if you don't see any interesting for you use our search form on bottom ↓
martin curbishley automotive
oct 15 2019 · form two ftna results 2019/20 (matokeo ya kidato cha pili) standard four sfna results 2019/2020 (matokeo darasa la nne) like us on facebook top 10 trending this week matokeo ya mtihani wa taifa kwa ngazi mbali mbali mwaka 2018 matokeo ya kidato cha pili mwaka 2018 matokeo ya darasa la sita mwaka 2018 matokeo ya darasa la nne mwaka 2018 idadi ya wanafunzi wanaorudia kidato cha pili mwaka 2018 idadi ya wanafunzi waliofaulu na skuli walizopangiwa mwaka 2018breaking news matokeo ya kidato cha pili 2018/2019 | form two national assessment results 2018/2019 | released today 04th january 2019 please share with your friends background the national examinations council of tanzania (necta) is government institution which was established by the parliamentary act no 21 of 1973 necta is responsible
baraza la mitihani la taifa (necta) limetangaza matokeo ya kidato nne ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia saba jumla ya watahiniwa 385 767 walisailiwa kufanya mtihani kidato cha nne mwaka 2017 kati yao 287713 sawa na asilimia 7709 ndio wamefaulu ambapo wasichana ni 143728 sawa na asilimia 7521 na wavulana 143985 sawa na asilimia 7906 necta matokeo ya kidato cha sita 2019/2020 | form six results 2019 form six results 2019 | matokeo kidato cha sita 2019 | necta form six results 2019 | kidato cha 6 matokeo 2019 | matokeo necta 2019 | form six 2019 results | to form six 2019 | form 6 best schools 2019 | shule 10 bora kidato cha sita 2019 | mwanafunzi bora form six 2019 |10 best girls form six 2019 |10 best boys form six 2019 matokeo ya form two necta form two results | ftna results | matokeo kidato cha pili ftna 2019 results matokeo kidato cha pili 2019 recommended check scholarships opportunities to study apply to job share this page on get new jobs for this search by email send me new jobs by email you can cancel emails at any time
form two results click here form two ftna results 2019/20 (matokeo ya kidato cha pili) reviewed by maujanjamusic on january 09 2020 rating 5 dear reader leave a comment below tazama matokeo ya kidato cha pili 2019 form two results 2019 here form two examination results 2019/2020 how to watch matokeo ya kidato cha pili 2019 bonyeza hapa matokeo ya kidato cha nne 2019 bonyeza 24 signs that show some wants to start love relationship with younecta form two results app kwaajili ya matokeo ya kidato cha pili 2019/2020 tazama matokeo ya form 2 necta kupitia app hiinecta certificate of secondary education examination(csee) this is an achievement test offered to candidates who have completed four years of secondary education in tanzania so as to get those who will pass their exams to join with advanced level for two year to study form five and six also to get students who will be chosen to join various technical college in tanzania
matokeo ya kidato cha pili & darasa la nne 2018/2019 ashel january 4 2019 the national examinations council of tanzania has announced the form two and standard four national assessment results
dream of driving off a bridge into water
honda rebel 250 replacement carburetor
august 10 celeb birthdays | 2020-08-04T05:59:54 | https://oedl.lawandicome.co/matokeo-ya-form-two-2019.html |
msaidizi wa mafuta
kwa sasa tuna 23 / 07 / 18 10 01
mitambo maalum ruhusa kupunguza matumizi ya mafuta ⇒ msaidizi wa mafuta
ujumbe zisizo lupar tembo » 15/09/06 0826
kwa njia ya mchezo wa mifumo ya kiungo cha matangazo hapa ni nini kinachopatikana kwa kubonyeza moja ya viungo vya umma juu ya ukurasa wa nyumbani wa tovuti yetu mpendwa
christophe hatukulaumii lakini ikiwa una uwezo wa kuchagua haipaswi kuwa tunapitia gugusses
ujumbe zisizo lupar denis » 15/09/06 0926
ni katika mstari wa mawazo yetu lakini kama kawaida matokeo ya utani
ujumbe zisizo lupar denis » 15/09/06 0934
kama injini hp2 kujaribu lakini ni ufanisi kutokana na bei ya bidhaa ni bidhaa za muujiza sina imani kubwa sana
ingekuwa nafuu sana ikiwa inaepuka kujenga upya injini
re msaidizi wa mafuta
ujumbe zisizo lupar christophe » 15/09/06 1209
tembo aliandika hivi christophe hatukulaumii lakini ikiwa una uwezo wa kuchagua haipaswi kuwa tunapitia gugusses
blacklisté nakumbusha kwamba kuna mada kwenye jukwaa hasa kwa https//wwweconologiecom/forums/lessponso t1714html
nimefunga jambo hili
10019 maoni
6975 maoni
6777 maoni
1808 maoni
2578 maoni | 2018-07-23T08:01:50 | https://sw.econologie.com/forums/consommer-moins-auto/economiseur-di-carbu-t2296.html |
tetesi za soka leo ulaya jumatatu leroy sane gareth bale bruno fernandesnicolas pepe wilfried zaha mwanaharakati mzalendo ™
admin 104900 am bruno fernandes gareth bale leroy sane michezo nicolas pepe wilfried zaha
by admin muda 104900 am
labels bruno fernandes gareth bale leroy sane michezo nicolas pepe wilfried zaha | 2019-09-21T10:59:32 | https://www.mwanaharakatimzalendo.co.tz/2019/07/tetesi-za-soka-leo-ulaya-jumatatu.html |
luka 2neno bibilia takatifu (snt) kuzaliwa kwa yesu2 siku zile kaisari augusto mtawala wa milki ya kirumi aliamuru ya kwamba watu wote wa milki yake waandikishwe 2 hii ilikuwa ni sensa ya kwanza kufanyika nayo ilitokea wakati kirenio alipokuwa liwali wa siria 3 watu wote walikwenda katika sehemu walikozaliwa ili waandikishwe huko 4 yusufu alitoka mji wa nazareti uliopo galilaya akaenda mpaka bethlehemu mji wa daudi kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo wa daudi 5 alikwenda huko kujiandikisha pamoja na mchumba wake mariamu ambaye kwa wakati huu alikuwa mja mzito 6 walipokuwa bethlehemu wakati wa mariamu kujifungua uli fika 7 naye akamzaa mtoto wa kiume kifungua mimba akamfunika kwa vinguo na kumlaza horini kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni wachungaji wapata habari8 usiku ule walikuwako wachungaji wakilinda kondoo zao nje ya mji 9 ghafla malaika wa bwana akawatokea na utukufu wa mungu ukawangazia pande zote wakajawa na hofu kuu 10 lakini malaika akawatuliza akisema msiogope nawaletea habari njema ya furaha kubwa na habari hii ni kwa faida ya watu wote 11 kwa maana leo katika mji wa bethlehemu amezaliwa mwokozi ambaye ndiye kristo bwana 12 na hivi ndivyo mtakavyomtambua mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa vinguo na kulazwa horini 13 mara jeshi kubwa la malaika wa mbinguni likatokea na pamoja wakamsifu mungu wakiimba 14 atukuzwe mungu juu mbin guni na duniani iwepo amani kwa watu ambao amependezwa nao 15 malaika hao waliporudi mbinguni wale wachungaji walish auriana jamani twendeni bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotokea ambayo bwana ametufahamisha 16 kwa hiyo wakaenda haraka bethlehemu wakawakuta mariamu na yusufu na yule mtoto mchanga alikuwa amelala mahali pa kulia ngombe 17 walipomwona mtoto wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa 18 na wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wachungaji 19 lakini mariamu akayaweka mambo haya yote moyoni mwake akayafikiria mara kwa mara 20 wale wachungaji wakarudi huku wakimtukuza mungu na kum sifu kwa yale waliyoyasikia na kuyaona 21 hata baada ya siku nane ilipotimia siku ya kumtahiri mtoto aliitwa yesu jina alilopewa na malaika kabla hata haja chukuliwa mimba yesu apelekwa hekaluni22 baada ya kutimia kwa muda wa utakaso wa yusufu na mar iamu kwa mujibu wa sheria ya musa walimpeleka mtoto yerusalemu wakamtoa kwa bwana 23 kama ilivyotakiwa na sheria ya bwana kila mtoto wa kiume wa kwanza atakabidhiwa kwa bwana 24 pia walitoa sadaka kama ilivyotakiwa na sheria ya bwana hua wawili au makinda ya njiwa wawili 25 na alikuwepo huko yerusalemu mzee mmoja jina lake simeoni ambaye alikuwa mwenye haki na mcha mungu siku zote alikuwa akitarajia ukombozi wa israeli na roho mtakatifu alikuwa juu yake 26 pia roho mtaka tifu alikuwa amemhakikishia kuwa hangekufa kabla ya kumwona kristo wa bwana 27 kwa hiyo akiwa ameongozwa na roho mtaka tifu simeoni alikwenda hekaluni wazazi walipomleta mtoto yesu ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria 28 simeoni alimpokea mtoto mikononi mwake akamshukuru mungu akisema 29 sasa bwana niruhusu mimi mtumishi wako niende kwa amani kama ulivyoniahidi 30 kwa sababu macho yangu yameuona wokovu 31 ulioandaa mbele ya watu wote 32 nuru itakayowaangazia watu wa mataifa na kuleta utukufu kwa watu wako israeli 33 wazazi wa mtoto walistaajabu kwa yale yaliyokuwa yakisemwa kumhusu mtoto wao 34 simeoni akawabariki kisha akamwambia mariamu mama yake mtoto huyu amechaguliwa na mungu kwa makusudi ya kuanga mizwa na kuokolewa kwa wengi katika israeli atakuwa ishara ya onyo kutoka kwa mungu ambayo watu wengi wataikataa 35 ili kudhi hirisha mawazo yao ya ndani na uchungu kama kisu kikali utaku choma moyoni 3637 tena alikuwepo hekaluni nabii mmoja mwanamke mzee sana jina lake ana binti wa fanueli wa kabila la asheri nabii ana alikuwa mjane wa miaka themanini na minne naye alikuwa ameolewa kwa miaka saba tu mumewe akafariki yeye aliishi humo hekaluni daima akimwabudu mungu na kuomba na kufunga 38 wakati huo huo ana alikuja mbele akamshukuru mungu na kueleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa yerusalemu 39 yusufu na mariamu walipokamilisha mambo yote yaliyotakiwa na sheria ya mungu walirudi nyumbani kwao nazareti katika wilaya ya galilaya 40 yesu aliendelea kukua akawa kijana mwenye nguvu na hekima akijaa baraka za mtoto yesu adhihirisha hekima yake41 kila mwaka wazazi wake walikwenda yerusalemu kushiriki katika siku kuu ya pasaka 42 yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama desturi ilivyokuwa 43 sikukuu ilipokwisha walianza safari ya kurudi nyumbani yesu akabaki yerusalemu pasipo wazazi wake kujua 44 wao walidhani yupo nao kwenye msafara kwa hiyo wakaenda mwendo wa siku nzima walipotambua kwamba hawakuwa naye walianza kumtafuta kati ya jamaa na marafiki 45 hawakumpata kwa hiyo wakarudi yerusalemu wakimtafuta 46 siku ya tatu wakamkuta hek aluni ameketi kati ya walimu wa sheria akiwasikiliza na kuwau liza maswali 47 wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa na majibu aliyoyatoa 48 wazazi wake walipomwona walishangaa mama yake akamwul iza mwanangu mbona umetufanyia hivi baba yako na mimi tume hangaika kukutafuta kila mahali kwa wasiwasi mkubwa 49 lakini yeye akajibu kwa nini mlihangaika kunitafuta hamkujua ninge kuwa hapa hekaluni kwenye nyumba ya baba yangu 50 lakini wao hawakuelewa maana ya jibu lake 51 akarudi pamoja na wazazi wake hadi nazareti akawa aki watii na mama yake akayaweka moyoni mambo haya yote 52 basi yesu akaendelea kuongezeka katika kimo na hekima akipendwa na neno bibilia takatifu (snt) copyright © 1989 by biblica | 2017-07-21T02:49:56 | https://www.biblegateway.com/passage/?search=Luka+2&version=SNT |
tanzanian canadian association 50 cent achonga
mwanamuziki maarufu wa hiphop nchini marekani amepungua uzito kiasi cha kushangaza watu fiddy kama baadhi wanavyomuita amepungua toka 216 mpaka 140 kwa kunywa vimiminika na mazoezi mengine yote haya ni katika kutengeneza filamu ambayo amecheza kama mchezaji wa football aliyeugua kansa sinema hiyo itaitwa things fall apart kwa wapenzi wake wasiwe na wasi kwani ameshaanza kula baada ya kumaliza kazi na atarudia afya na mwili wake wa kawaida
posted by tanzanian canadian association at 924 pm | 2018-12-13T04:00:18 | http://tanzcan.blogspot.com/2010/05/50-cent-achonga.html |
hotuba ya balozi baraka h luvanda wakati wa mahafali ya wanafunzi na wanachama wa umoja wa wanafunzi wa mysore(tasam) 17 machi2018
ndugu rais wa tasam na mwenyeji wetu
ndugu viongozi katika meza kuu
ndugu wahitimu
marafiki wa tasam
kama ulivyokwisha kudokeza katika hotuba yako leo sio siku ya kupoteza muda kwa kusikiliza hotuba ndefu nami ninaitikia mwongozo wako kwa kuongea kwa ufupi
kwanza kabisa ni shukrani ninawashukuru sana kwa kunialika kuja kujumuika nanyi katika kufurahia wenzetu kuweza kutimiza lengo na dhumuni lililokuwa limewaleta india hongereni sana wahitimu wote
aidha nawapongeza na kuwashukuru wakufunzi wenu waliowapatia elimu ujuzi na maarifa na kuwawekeni katika hali ya utayari kwenda kukabiliana na changamoto za maisha yanayoanza leo
mahafali ni tukio laa kipekee sana popote pale kwa wahitimu tukio ni muda mahsusi wa kusherehekea ni muda pekee wa kutathimini mafanikio ya masaa mengi waliyotumia katika kuhakikisha wanafikia malengo yao lakini pia siku kama ya leo mara sherehe hizi zinapohitimishwa ni muda kwa wahitimu kutafakari ukurasa mpya wa maisha mlango wa dunia unafunguka na furaha maumivu na wajibu mpya nayasema haya si kwa kuwaogopesha bali hiyo ndiyo hali halisi inayowakabili
wahitimu wetu hawa wamefanya jitihada kubwa hadi kufikia siku ya leo lakini pia ni ukweli kuwa wazazi wao wametekeleza wajibu wao vizuri wa kuhakikisha mazingira rafiki yamekuwepo wakati wote wa safari yao ya masomo wakufunzi halikadhalika wamekuwa sehemu ya mafanikio haya kwa ajili ya kuwapongeza wote niliowataja naomba tupige makofi mengi
takwimu zilizopo zinaonesha kuwa kila mwaka tanzania inazalisha wahitimu wapatao laki nane na wote hao wanaingia katika soko la ajira changamoto kubwa imekuwa ni ufinyu wa ajira zenyewe iwe kwa sekta ya umma au kwa sekta binafsi na mbaya zaidi kwa upande wa sekta binafsi ni kuwa na ajira zisizodumu ninalitaja jambo hili kwenu ili kuwaandaa kisaikolojia
baadhi yenu watakuwa na matarajio ya kuajiriwa hakuna shaka kuwa watapata ajira baada ya kuhangaika sana lakini sina uhakika kama mmeshakutana na neon ujasiriamalina kama linafahamika miongoni mwenu basi naamini mtakuwa mmejiweka vizuri kukabiliana na changamoto za kimaisha zinazoanza leo kwa wale ambao kwa bahati mbaya hawakuwahi kukutana na neno hili nawasihi watumie simu zao kubofya na kupata maana yake watanufaika sana na maelezo na mifano inayotolewa
kwa kuwa niliahidi kuitikia rai ya kutumia muda mfupi naomba nimalizie nasaha zangu kwa kuongezea yafuatayo
matarajio ya wazazi wenu ni makubwa matarajio ya wadogo zenu ni makubwa matarajio ya nchi ni makubwa na hata matarajio ya familia zenu pia ni makubwa na kama ilivyokwishakusemwaninanukuu our prime purpose in life is to help others and if you cant help them at least dont hurt them nikiwaangalia nyuso zenu sioni hata mmoja wa kumuumiza mtu aliyechangia kumfikisha hapa siku ya leo
na kwa kuhitimisha naomba nitoe rai hii mmehitimu ngazi hii ya elimu na katika fani mbali mbali hii sote tunajumuika kukupongezeni sana lakini ninashawishika kuamini kuwa wengi wenu bado mna hamu na uwezo kujiendeleza zaidi ya hapo
nawasihi fursa ya kujiendeleza zaidi ikijitokeza ichangamkieni bila kusita kwani ni ukweli usiofichika kuwa when you buy a car or a piece of equipment it comes with a users manual with maintenance instructions you have to service it regularly to ensure it continues to serve you well how much more important is it to regularly service your brain after graduation i know there are graduates who find no time to read a book again after graduation dont be like that for a mind is like a garden if it is not watered and cultivated weeds will take over
kwa mara nyingine nawashukuruni sana kwa kunialika katika furaha hii na ninaamini kuwa huu ni mwanzo tu | 2018-04-23T22:43:39 | http://tanzrepdelhi.com/17_03_2018.html |
82032pm
maamuma anayeswali nyuma ya imamu kumeshurutizwa sharti kadhaa ili kumfuata kwake imamu kusihi miongoni mwa sharti muhimu ni kama zifuatavyo
1) mfuataji (maamuma) asijue kubatilika kwa swala ya imamu wake au kuitakidi hivyo
mfano watu wawili wamefanya jitihadi katika kujua upande kilipo qiblah
kila mmoja wa wawili hawa akaitakidi kwamba qiblah kiko upande ule auonao yeye na wala hakiko upande auonao mwenzake
katika hali kama hii hakujuzu kwa mmojawapo wa wawili hawa waliokhitalifiana katika upande kilioko qiblah jambo ambalo ni mojawapo ya nguzo za swala
hakumjuzii kumfuata mwenzake akamfanya kuwa ndio imamu wake na yeye akawa maamuma nyuma yake
kutokujuzu huku kunatokana na ile itikadi ya kila mmoja wa wawili hawa kwamba mwenzake amekosea welekea/upande wa qiblah sasa basi maadam amekosea qiblah basi na swala yake anayoiswali kuelekea upande huo itakuwa sio sahihi ni batili tu na si vinginevyo kwa itikadi yake hiyo
2) imamu asiwe umiyi (asiyejua kusoma wala kuandika) na ilhali maamuma ni msomi
muradi wa makusudio ya umiyi hapa ni mtu asiyeweza kuisoma vizuri suratilfaatihah (alhamdu) kwa hukumu zake za usomaji kama zilivyotajwa katika vitabu vya fani ya tajweed angalia ikiwa imamu na maamuma wote ni maumiyi basi kutamjuzia kila mmoja wao kumfuata mwenzake
3) imamu asiwe mwanamke na maamuma akawa ni mwanamume
mwanamke hana mamlaka kisheria kumtangulia mwanamume katika swala akawa ndio imamu wa mwanamume hili ndilo agizo la mtume wa allahrehema na amani zimshukiekatika kauli yake mwanamke asimswalishe mwanamume ibn maajahallah amrehemu | 2017-11-19T01:20:21 | http://www.uislamu.org/index.php/en/fiqhi-na-sheria-02/sura-ya-pili-02/swala-ya-jamaa/sharti-za-maamuma |
tanzania yazidi kupaa katika mapambano dhidi ya rushwa dar24
7 months ago comments off on tanzania yazidi kupaa katika mapambano dhidi ya rushwa
waziri wa nchi ofisi ya rais (menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora) george mkuchika amesema kuwa tanzania inaendelea kupata heshima kubwa katika jumuiya ya kimataifa katika vita vya mapambano dhidi ya rushwa kutokana na mshikamano na nguvu ya pamoja iliyopo katika vyombo na taasisi zinazosimamia utawala bora nchini
ameyasema hayo jijini dar es salaam katika kongamano la siku maalum dhidi ya rushwa katika maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba ambapo amesema kuwa utafiti uliofanywa na taasisi hizo zimesifu juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano na kuitaja tanzania kuwa ni nchi ya mfano katika vita vya mapambano dhidi ya rushwa
amesema kuwa taasisi hizo zikiwemo mo ibrahim transparency international aprm na taasisi nyingine kubwa duniani zinazosimamia masuala ya utawala bora zimefanya utafiti na kusifu juhudi kubwa zinazofanywa na serikali ya tanzania chini ya rais dkt john pombe magufuli katika mapambano dhidi ya rushwa ambapo tafiti mbalimbali zimeifanya tanzania kushika nafasi ya pili nyuma ya nchi ya rwanda
kwa sasa vyombo vyetu vyote serikalini si takukuru pekee bali pia polisi tiss (usalama wa taifa) ofisi ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali icag) na vingine vyote vimeendelea kuunga katika kusimamia masuala ya utawala bora na hili limeleta msukumo na hamasa mpya katika vita dhidi ya rushwa hapa nchiniamesema mkuchika
akizungumzia rushwa katika sekta ya viwanda na biashara waziri mkuchika amesema kuwa serikali imeendelea kuweka mikakati mbalimbali katika kupunguza tatizo hilo ambalo limekuwa likiathiri sekta binafsi ambayo imekuwa mshirika wa karibu wa serikali katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini
kwa mujibu wa waziri huyo rushwa katika sekta ya biashara imekuwa ikiathiri sana masuala ya uwekezaji wa kigeni ambapo eneo lililoonyesha kutawala kwa rushwa ni katika eneo la utoaji wa vibali na leseni kutoka katika taasisi na idara muhimu za serikalini na hivyo serikali imeendelea kulifanyia kazi ili kuhakikisha kuwa vikwazo hivyo vinaondolewa kwa wawekezaji na hivyo kuharakisha ukuaji wa uchumi
kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (takukuru) diwani athumani amesema kuwa serikali imeendelea kushirikiana na wadau wa sekta binafsi kupitia mpango mkakati dhidi ya mapambano ya rushwa (nascapiii) ili kuhakikisha kuwa mapambano na vita dhidi ya rushwa yanapata mafanikio nchini
kamanda wa polisi arusha ajibu mapigo kaangalieni katiba ya ccm
habari kubwa katika magazeti ya tanzania leo julai 4 2019
afya/habari 4 mins ago comments off on waziri atangaza maeneo waliyotenga kutibu watakao pata virusi vya corona
habari 27 mins ago comments off on video historia fupi ya marehemu doglas mwandishi tbc mwili uligundulika siku ya nne ulianza kutoa harufu | 2020-01-29T13:46:53 | http://dar24.com/tanzania-yazidi-kupaa-katika-mapambano-dhidi-ya-rushwa/ |
dc muheza awataka wafanyabiashara wa soko la samaki kuhamia eneo la soko la michungwani | politiksi kurunzini
home arusha news biashara habari utawala dc muheza awataka wafanyabiashara wa soko la samaki kuhamia eneo la soko la michungwani
seriajr tw tuesday july 19 2016 arusha news biashara habari utawala edit | 2017-12-15T10:05:39 | https://arusha255.blogspot.com/2016/07/dc-muheza-awataka-wafanyabiashara-wa.html |
mfungo wa siku 30 za miujiza na maajabu | yesunibwana
home › mafunzo › mfungo wa siku 30 za miujiza na maajabu
mfungo wa siku 30 za miujiza na maajabu
posted on january 7 2016 by yesunibwana 1 comment
kusudi la mfungo
kutafuta uso wa mungu kwa ajili ya 2016 mwaka wa kujionesha
ni mfungo wa masaa 12 ifikapo saa 1200 jioni ruksa kufungulia
tunaomba muda gani
asubuhi muda wa chai
mchana muda wa lunch
jioni kabla ya kufungulia
tumeanza leo 05/01/2016 tunamaliza 04/02/2016
maombi ya asubuhi hii
utakaso wa mioyo yetu
zaburi 661820
kama ningaliwaza maovu moyoni mwangubwana asingelinisikia
moyo ambao una mambo mengi yasiyo na utukufu kama vile kuumizwa visasi kutosamehe uchungu maumivu majeraha kudhalilishwa kutelekezwa kudhulumiwa unakuwa kizuizi cha kujibiwa na mungu
mungu hujibu maombi kwa kuangalia hali ya moyo wa mwombaji kwanza
hatutajitesa bure kufunga na tusipate matokeo kisa mioyo yetu ina mambo yasiyofaa mbele za bwana yesu
tutaanza kwa kujitakasa mioyo yetu
usifanye yale matoba ya jumla jumla matoba ya juu kwa juu ya kukurupuka hapana
kaa chini tafakari maisha yako tangu umejielewa hadi hapo ulipo angalia waliokuumiza waliokujeruhi waliokudhalilisha waliokudhulumu waliokujeruhi halafu tengeneza achilia hayo achilia hao watu achilia hayo matukio
moyo uwa mdanganyifu una ugonjwa wa kufisha ni nani awezaye kuujua mimi bwana nauchunguza moyo na kuvijaribu viuno
mungu ana tabia ya kuangalia moyo wa muombaji kuliko maneno mazuri anayotamka maandiko anayosema au ukiri wake
moyo ni kituo kikuu cha mahusiano na mawasiliano kati ya mtu na mungu
watu hawa huniheshimu kwa midomo ila mioyo yao iko mbali na mimi
unapokuja mbele za mungu anachokiangalia cha kwanza ni moyo na si mdomo
kila mmoja anaweza kuongea ila si kila mtu anaweza kuwa sawa na asemayo mdomoni mungu yuko serious mno na hali ya moyo wa mtu kuliko maneno ya mdomo wa mtu
zaburi 731
hakika mungu ni mwema kwa israeli (watu wake) kwao hao walio safi mioyo yao
wema wa mungu kwa mtu unategemea hali ya moyo wa mtu
zaburi 1017
bwana umeisikia tamaa ya wanyonge utaitengeneza mioyi yao utalitega sikio lako
kabla mungu hajakutegea sikio lake mpe nafasi akutengeneze moyo wako kwanza
anza na moyo wako tengeneza moyo wako kwanza
tukutane mchana ukiwa na moyo mwingine
moyo uliopondeka
(isaya 6612)
moyo wa nyama na si wa jiwe
(ezekieli 1119 ezekieli 3626)
kwa kuamua kufunga tu maaajabu na miujiza imeanza kwako
nb muda wa lunch (saa 630730 mchana) nitaleta maombi ya mchana
nb nina nafasi kadhaa za wale ambao mlikuwa bado mnajishauri moyoni kujiunga na mfungo huu wa siku 30 kabla ya saa 630 mchana ukiona uko tayari niambie nitakuunganisha kwenye group tukimbize maelfu pamoja
group maalum ya whatsapp ya maombi haya 0655 466 67
‹ mfungo wa siku 30
siku 30 za maombi ya miujiza na maajabu [day 2] ›
tagged with 2016 maombi mdungo siku30
one comment on mfungo wa siku 30 za miujiza na maajabu
gracembwambo says
mungu akubariki kwa huduma hii nimetiwa moyo sana na mafundisho haya ya mfungo name nitayafuatilia kwa karibu japo siku nanyi tangu mwanzo | 2018-02-23T12:52:05 | https://yesunibwana.org/2016/01/07/mfungo-wa-siku-30-za-miujiza-na-maajabu/ |
heslb act & amendments national higher education policy 1999 heslb strategic plan client service charter education policy 2014 heslb annual reports speeches criteria for loans issuance
wanafunzi 698 washinda rufaa na kupangiwa mikopo yenye thamani ya tzs 246 bilioni | 2020-08-14T23:19:33 | https://mail.heslb.go.tz/Post/view_post?post=19 |
halmashauri ya jiji la tanga yaendelea kuwa kinara utoaji wa mikopo kwa asilimia 10 rc sheigella zanzinews
home habari matukio halmashauri ya jiji la tanga yaendelea kuwa kinara utoaji wa mikopo kwa asilimia 10 rc sheigella
halmashauri ya jiji la tanga yaendelea kuwa kinara utoaji wa mikopo kwa asilimia 10 rc sheigella
rto wa mkoa wa tanga solomon mwangamilo kushoto akiwa na na kaimu kamanda wa polisi mkoa wa tanga leons rwegasira wakijitambulisha kwenye mkutano wa hadhara wa mkuu wa mkoa wa tanga martine shigella | 2019-09-15T16:46:18 | http://www.zanzinews.com/2019/09/halmashauri-ya-jiji-la-tanga-yaendelea.html |
the superstars tz aibu mtoto amfumania mama yake akijiuza jijini dar pages
aibu mtoto amfumania mama yake akijiuza jijini dar na issa mnally na richard bukosishabaash kijana aliyefahamika kwa jina moja la hamis mkazi wa tandale jijini dar hivi karibuni alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kumfuma mama yake mdogo akijiuza usikutukio
hilo la kufedhehesha lilitokea usiku wa kuamkia juzi (jumatano) maeneo ya sinza mapambano ambapo mapaparazi wetu walikuwa katika operesheni ya kuwasaka wanawake wanaojihusisha na biashara hiyo haramu
maeneo hayo waandishi wetu walimuona kijana mmoja akiwa amejiinamia baada ya kumfuata na kumhoji kilichompata alidai kuwa alipewa taarifa juu ya mzazi wake huyo aliyemtaja kwa jina la mama husna kujiuza na siku
hiyo alimuona akiwa kwenye mawindojamani niacheni maana nilichoshuhudia kimeniumiza sanamama yangu anafikia hatua ya kuja kijiuza hukuamekosa niniau ni huu ugumu wa maisha dah alisikika kijana huyo aliyekuwa akiliakatika kuthibitisha kile anachokizungumza hamis aliwaonesha waandishi wetu kundi la wanawake waliokuwa sokoni na kuelekeza kuwa aliyekuwa amevaa nguo ya mauamaua ndiye mama yake mdogo (angalia picha ukurasa wa 16)
kupata utamu wa stori hiyo mapaparazi wetu waliwavaa wanawake hao na kuwafotoa picha ambapo walitawanyika huku kila mmoja akishika njia yakeaidha
maelezo yaliyopatikana kutoka kwa shuhuda mmoja aliyedai kumfahamu vizuri mama husna alisema amekuwa akifika eneo hilo akiwa ameongozana na wapangaji wenzake ambao ni maarufu kwa biashara hiyo ya kujiuzambali
na tukio hilo la aibu waandishi wetu walitembelea mitaa ya kinondoni posta maeneo ya las vegas ohio jolly club na kwingineko jijini dar na kushuhudia idadi kubwa ya wanawake wakijiuzauchunguzi umebaini kuwa biashara hiyo imekuwa akishamiri kadiri siku zinavyokwenda licha ya operesheni zinazofanywa na polisi huku ugumu wa maisha ukitajwa kuwa ndiyo chanzogazeti hili linawaomba wanawake wanaojihusisha na biashara hii haramu kuacha mara moja kwani ni hatari kwa maisha yao
credit glp | 2016-12-04T03:53:04 | http://thesuperstarstz.blogspot.com/2013/12/aibu-mtoto-amfumania-mama-yake-akijiuza.html |
tehama kusaidia kupunguza msongamano ofisi za dc na rc dar24
tehama kusaidia kupunguza msongamano ofisi za dc na rc
10 months ago comments off on tehama kusaidia kupunguza msongamano ofisi za dc na rc
mkuu wa mkoa wa rukwa joachim wangabo amesema maboresho ya teknolojia ya habari na mawasiliano (tehama) yanayofanywa na mhimili wa mahakama nchini utasaidia kupunguza foleni za wananchi wanaofika ofisi za wakuu wa wilaya na kwa mkuu wa mkoa kutafuta haki zao
mwaka 2018 na jitihada zilizofanyika na mahakama umekuwa mwanzo mzuri wananchi watajitokeza kutafuta elimu hii ya sheria na wanapoipata itatupunguzia msongamano kwenye ofisi zetu za mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa ili tufanye kazi za maendeleo sio kusuluhisha migogo ya ndoa mirathi na ardhi ambayo yote imekaa katika misingi ya kisheria ameeleza
ameongeza kuwa elimu ya sheria iendelee kutolewa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wakati huku wakizingatia kaulimbiu ya maadhimisho hayo inayosema matumizi ya tehama kwa kutoa haki kwa wakati na kuzingatia maadili
aidha jaji mfawidhi wa mahakama kuu ya tanzania kanda ya sumbawanga john mgeta ametahadahrisha matumizi mabaya ya teknolojia katika kuvunja maadili na misingi ya mahakama na utu kwani watu hutumia teknolojia hiyo kuendeleza rushwa kupitia namba za simu za mahakama
mtumishi wa mahakama anaweza kutumia simu kuwasiliana na mtu akimuomba rushwa au kufanya miamala ya pesa vyombo vya habari na wananchi ambao wanakiuka maadili kwa kutumia simu na tehama sisi tunasisitiza matumizi haya yazingatie maadili amebainisha
video mzee kingunge alirejea katoliki kabla ya mauti chadema wajitosa majaji wala 'bata'
habari 57 mins ago comments off on ofisa elimu azuia wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kwenda likizo | 2018-12-12T10:02:12 | http://dar24.com/tehama-kusaidia-kupunguza-msongamano-ofisi-za-dc-na-rc/ |
katibu mkuu kampeni ya marufuku ya mifuko ya plastiki inaenda vizuri mtaa kwa mtaa blog
home habari katibu mkuu kampeni ya marufuku ya mifuko ya plastiki inaenda vizuri
katibu mkuu kampeni ya marufuku ya mifuko ya plastiki inaenda vizuri
othman michuzi june 21 2019 habari
serikali imesema kampeni ya kupiga marufuku mifuko ya plastiki inakwenda vizuri na kusisitiza ni makosa kisheria kubadili matumizi ya vifungashio vya bidhaa maalumu na kutumika kama mifuko ya kubebea bidhaa mbalimbali huku
katibu mkuu ofisi ya makamu wa rais mhandisi joseph malongo amebainisha hayo leo jijini dodoma alipozungumzia azma ya serikali ya kuendesha operesheni maalumu nchi nzima ya uzingatiaji wa sheria ya usimamizi wa mazingira juu ya marufuku ya mifuko ya plastiki na matumizi endelevu ya mifuko mbadala
alisema adhabu stahiki zitatolewa kwa watengenezaji waingizaji wasambazaji na watumiaji wa vifungashio vya plastiki vilivyozalishwa ama kuingizwa nchini na kutumika kama vibebeo vya bidhaa
baada ya kuanza kwa utekelezaji wa katazo la kutumia mifuko ya plastiki imebainika kuwa baadhi ya wazalishaji na wasambazaji wamebadilisha matumizi ya mifuko laini ya plastiki isiyokuwa na mishikio na kuitumia kama vibebeo vya bidhaa alisema mhandisi malongo
alisema ofisi ya makamu wa rais kwa kushirikiana na kikosi kazi inaendelea na zoezi la kuelimisha umma juu ya jambo hili pamoja na kuhamasisha matumizi ya mifuko mbadala
kwa mujibu wa kanuni za usimamizi wa mazingira za kupiga marufuku mifuko ya plastiki za mwaka 2019 ni marufuku kuzalisha kuingiza nchini kusambaza na kutumia mifuko ya plastiki iliyotajwa katika katazo hili
alisema kanuni ya 9 inatoa msamaha kwa baadhi ya vifungashio vya plastiki kwa ajili ya huduma za afya au ambavyo vinatumika kwenye kufungashia bidhaa za viwandani sekta ya ujenzi sekta ya kilimo vyakula au usafi na udhibiti wa taka
shirika la viwango tanzania (tbs) linaanda viwango kwa vifungashio hivi ambavyo vitalazimisha kiwango cha unene uwekwaji lakiri na kutambulisha bidhaa iliyofungashwa kabla ya kuuzwa alisema
katibu mkuu ofisi ya makamu wa rais mhandisi joseph malongo (katikati) akifafanua kuhusu vifungashio alipozungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)jijini dodoma wengine pichani kushoto ni naibu katibu mkuu ofisi ya makamu wa rais balozi joseph sokoine na mkurugenzi mkuu baraza la hifadhi na usimamizi wa mazingira (nemc) dkt samuel gwamaka
katibu mkuu ofisi ya makamu wa rais mhandisi joseph malongo akionesha baadhi ya viungashio vinavyotumika kwa matumizi ya kubebea bidhaa nyingine tofauti na inayotakiwa
naibu katibu ofisi ya makamu wa rais balozi joseph sokoine akifafanua jambo kwa waandishi wa habari
katibu mkuu ofisi ya makamu wa rais mhandisi joseph malongo akionesha mfuko mbadala unaoruhusiwa kubebea
katibu mkuu ofisi ya makamu wa rais mhandisi joseph malongo akionesha kifungashio kilichofungwa nyama bila kukidhi vigezo vinavyotwakiwa
waandishi wa habari wakifuatilia mkutano kutoka ofisi ya makamu wa rais kufafanua nkuhusu vifungashio
posted by othman michuzi at june 21 2019
kumbukumbu december (37) november (87) october (220) september (216) august (113) july (240) june (190) may (244) april (255) march (319) february (344) january (376) december (356) november (356) october (414) september (418) august (240) july (329) june (335) may (330) april (292) march (337) february (252) january (332) december (376) november (471) october (506) september (498) august (586) july (471) june (420) may (530) april (416) march (482) february (400) january (473) december (414) november (493) october (283) september (344) august (569) july (552) june (401) may (378) april (393) march (499) february (531) january (501) december (579) november (385) october (656) september (653) august (509) july (381) june (392) may (353) april (298) march (329) february (228) january (201) december (254) november (204) october (260) september (251) august (287) july (239) june (195) may (202) april (214) march (150) february (214) january (238) december (235) november (199) october (233) september (251) august (283) july (266) june (306) may (303) april (259) march (268) february (227) january (242) december (280) november (228) october (240) september (212) august (265) july (306) june (317) may (287) april (216) march (177) february (179) january (217) december (217) november (196) october (204) september (240) august (174) july (193) june (193) may (178) april (177) march (167) february (106) january (136) december (136) november (141) october (142) september (179) august (151) july (144) june (130) may (137) april (129) march (206) february (152) january (91) december (123) november (124) october (108) september (135) august (149) july (95) june (73) may (54) april (74) march (48) december (1) november (22) october (66) september (70) august (89) july (117) june (115) may (81) april (60) march (8) february (95) january (76) december (59) november (75) october (97) | 2019-12-09T21:17:27 | http://www.mtaakwamtaa.co.tz/2019/06/katibu-mkuu-kampeni-ya-marufuku-ya.html |
vodacom tanzania plc yamzawadia shmilioni mia moja na hamsini mshindi wa shindano la tusua mapene | full shangwe blog
home burudani vodacom tanzania plc yamzawadia shmilioni mia moja na hamsini mshindi
vodacom tanzania plc yamzawadia shmilioni mia moja na hamsini mshindi wa shindano la tusua mapene
mkurugenzi wa kitengo cha dijitali na huduma za ziada vodacom tanzania plc nguvu kamando (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi 150000000/ mshindi wa shindano la tusua mapene na vodacom eveneth rutiyomba ambaye ni fundi cherehani mkazi wa kimara bucha hafla ya makabidhiano ilifanyika kimara jijini dar es salaam jana pichani katikati ni afisa wa huduma za ziada vodacom paulina bisheko
mkurugenzi wa kitengo cha dijitali na huduma za ziada vodacom tanzania plc nguvu kamando (kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na mshindi wa shindano la tusua mapene eveneth rutiyomba (kulia) pamoja na wazazi wake john ndebisa na fasness ndebisa
previous articledcc tabora yapitisha mapendekezo ya bajeti ya bilioni 52 ya mwaka ujao
next articlebrela yatoa semina elekezi kwa wabunge kamati ya kudumu ya bunge viwanda biashara na mazingira jijini dodoma | 2020-06-05T11:22:11 | https://fullshangweblog.co.tz/2020/01/19/vodacom-tanzania-plc-yamzawadia-sh-milioni-mia-moja-na-hamsini-mshindi-wa-shindano-la-tusua-mapene/ |
bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa
home > bidhaa > bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa (jumla ya 24 bidhaa kwa bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa)
bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa mtengenezaji kiwanda muuzaji kutoka china
sisi ni maalumu bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa wazalishaji na wasambazaji / kiwanda kutoka china ya jumla bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa na ubora wa juu kama bei ya chini / bei nafuu mojawapo ya bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa bidhaa za kuongoza kutoka china jining fuyuan fruits and vegetables co ltd
bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa jumla kutoka china direct buy kutoka china wazalishaji wa kuongoza kwa bei nafuu kiwanda pata bidhaa bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa jumla kwenye jining fuyuan fruits and vegetables co ltd na kupata ubora wa juu bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa moja kwa moja kutoka kwa wauzaji wa jumla wa china bonde la njano vitunguu vilivyopendezwa na wasambazaji tuma mahitaji yako ya kununua & pata majibu ya haraka | 2019-07-18T15:21:24 | http://sw.fuyuanfv.com/dp-bonde-la-njano-vitunguu-vilivyopendezwa.html |
mahakama ya wilaya ya mbozi lawamani kwa kuchelewesha kesi ~ chimbuko letu
228 am kona ya mahusiano na mapenzi no comments | 2017-10-20T14:26:59 | http://chimbukoletu.blogspot.com/2012/10/mahakama-ya-wilaya-ya-mbozi-lawamani.html |
ripple bei xrp kubadilisha fedha online
btc/usd117660901099eth/usd3918495149ltc/usd584454070dash/usd1000300203xmr/usd949668133nxt/usd00139075etc/usd69396208doge/usd00035006zec/usd968992339bts/usd00261010dgb/usd00277138xrp/usd02963121btcd/usd295596098ppc/usd02927044craig/usd00022099xbs/usd00239098xpy/usd00584099prc/usd00081100ybc/usd18957346102dank/usd00032097give/usd00005097kobo/usd00045148dt/usd10857ceti/usd00004098
bei na kubadilisha fedha ripple (xrp)
uko hapa pengine kwa sababu unahitaji kubadilisha (pata bei) ripple (xrp) kwa sarafu ya kigeni au fedha za crypto online hakuna kitu rahisi kuliko kubadilisha zaidi 170 sarafu na 2500 fedha za crypto hapa sarafu yetu ya kubadilisha fedha mtandaoni itasaidia kufanya hivyo hivi sasa jisikie huru kubadilisha si tu ripple lakini pia sarafu nyingine yoyote inapatikana
bei $0296
kichwa cha soko $10 508 100 67400
inapatikana ugavi 438180087170
ugavi mkubwa 100000000000
ugavi wa jumla 999910684790
labda itakuwa ya kuvutia kwa wewe kuangalia yote viwango vya kubadilishana ripple kwenye ukurasa mmoja
xrp/usd chati
bei ya ripple sarafu kubwa duniani
ripplexrp kwa dola ya marekaniusd$0296ripplexrp kwa yuroeur€0251ripplexrp kwa pauni ya uingerezagbp£0227ripplexrp kwa faranga ya uswisichfsfr027ripplexrp kwa krone ya norwenokkr268ripplexrp kwa krone ya denmakidkkkr187ripplexrp kwa koruna ya jamhuri ya chekiczkkč661ripplexrp kwa zloty ya polandiplnzł111ripplexrp kwa dola ya kanadacad$0397ripplexrp kwa dola ya australiaaud$0414ripplexrp kwa peso ya meksikomxnmex$663ripplexrp kwa dola ya hong konghkdhk$23ripplexrp kwa real ya brazilbrlr$161ripplexrp kwa rupia ya indiainr₹2223ripplexrp kwa rupia ya pakistanipkrre4975ripplexrp kwa dola ya singaporesgds$0407ripplexrp kwa dola ya nyuzilandinzd$0449ripplexrp kwa baht ya tailandithb฿925ripplexrp kwa yuan ya uchinacny¥206ripplexrp kwa yen ya japanijpy¥3139ripplexrp kwa won ya korea kusinikrw₩35235ripplexrp kwa naira ya nijeriangn₦11215ripplexrp kwa ruble ya urusirub₽2184ripplexrp kwa hryvnia ya ukraniauah₴819
ripplexrp kwa bitcoinbtc000003 ripplexrp kwa ethereumeth0000756 ripplexrp kwa litecoinltc000507 ripplexrp kwa digitalcashdash000296 ripplexrp kwa moneroxmr000312 ripplexrp kwa nxtnxt2135 ripplexrp kwa ethereum classicetc00427 ripplexrp kwa dogecoindoge8394 ripplexrp kwa zcashzec000306 ripplexrp kwa bitsharesbts1134 ripplexrp kwa digibytedgb1071
ripplexrp kwa bitcoindarkbtcd001 ripplexrp kwa peercoinppc101 ripplexrp kwa craigscoincraig13253 ripplexrp kwa bitstakexbs1241 ripplexrp kwa paycoinxpy508 ripplexrp kwa prospercoinprc3649 ripplexrp kwa ybcoinybc0000156 ripplexrp kwa darkkushdank9327 ripplexrp kwa givecoingive62952 ripplexrp kwa kobocoinkobo6646 ripplexrp kwa darktokendt0273 ripplexrp kwa cetus coinceti83938
viwango vya exchange vilivyosasishwa sat 08 aug 2020 154002 +0000 | 2020-08-08T15:42:58 | https://sw.currencyconvert.online/xrp |
hii ni plugin kwa ultimate mteja meneja lite edition tafadhali kuhakikisha una kununuliwa na imewekwa toleo la karibuni la mwisho meneja mteja kabla ya kutumia plugin hii
kalenda export feature
hii plugin rahisi hutoa ical nje kutoka mfumo ucm hii inaruhusu alerts na vitu todo kutoka ucm dashibodi kuonekana katika google yako kalenda binafsi au outlook kalenda ya (au kalenda yoyote kwamba inasaidia kuagiza ical url wa)
hiari sifa pia kufunga ucm fedha plugin kupokea entries kalenda kwa ajili imepangwa muswada malipo ankara muafaka na zaidi
kupata leseni kificho yako kwa plugin hii ( click here kwa maelekezo)
kwenda mazingira> kuboresha katika mfumo wako
bofya + kifungo kwa kuongeza ziada ya leseni kificho
kuingia leseni kificho yako kwa plugin hii
bofya kuboresha kifungo
hii itakuwa kufunga toleo la karibuni la plugin kwa ajili yenu na kuitunza updated katika siku zijazo
kalenda zilizopo ambazo zinaweza kuagiza kutoka ical url ya (mfano google kalenda)
angalia mfumo wa kuboresha kazi kwa sababu mwenyeji (katika mipangilio> kuboresha)
kipengele orodha na bidhaa kulinganisha
kama unahitaji msaada tafadhali jisikie huru kutumia mfumo wa kusaidia wetu kwa kubonyeza hapa tafadhali wala post msaada maombi juu ya mjadala wa bodi ya bidhaa haya si checked mara kwa mara na swali lako ili waende unanswered kwa muda wa wiki
5 julai 12 badiliko la mwisho
ecommerce ecommerce vitu wote kalenda kalenda ya kuuza nje kalenda mteja kalenda wateja kalenda google ical mawaidha orodha todo ucm ultimate meneja mteja | 2017-11-22T23:56:29 | https://sw.worldwidescripts.net/ucm-plugin-calendar-ical-google-calendar-export-40757 |
Subsets and Splits