text
stringlengths 3
16.2k
|
---|
VUTA nikuvute imezuka kati ya Rais William Ruto na kiongozi wa Azimio Raila Odinga kuhusiana na mswada unaopendekeza... NA JAMES MURIMI |
MWANIAJI urais wa chama cha Azimio La Umoja-One Kenya Raila Odinga anasisitiza kuwa Wakenya wanapaswa kuchagua kati ya... NA PIUS MAUNDU |
KINARA wa ODM, Raila Odinga amelaani vurugu iliyotokea Kaunti ya Machakos. |
Akizungumza Ijumaa katika hafla ya kampeni,... NA JUMA NAMLOLA |
NAIBU Rais William Ruto ametoa onyo kali kwa mgombeaji urais wa chama cha Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga... NA GEORGE ODIWUOR |
MGOMBEA urais wa muungano wa Azimio la Umoja One Kenya amesihi wakazi katika ngome yake ya Nyanza wajitokeze kwa wingi... NA LEONARD ONYANGO |
UCHAGUZI |
Siku moja baada ya kinara wa Narc-K, Martha Karua kumeza chambo cha mwaniaji urais kwa tikiti ya Azimio... NA BENSON MATHEKA |
KIONGOZI wa chama cha ODM na mgombea urais wa muungano wa Azimio La Umoja Raila Odinga, anazuru Uingereza katika ziara... Na PIUS MAUNDU |
VITA vya ubabe vinavyoendelea kati ya magavana watatu wa eneo la Ukambani kwa upande mmoja na viongozi wa Wiper kwa... Na CHARLES WASONGA |
HISTORIA ya kinyanga’anyiro cha urais nchini inaonyesha ushindi wa Agosti 9 unaweza kwenda upande wowote kati ya... Na WAANDISHI WETU |
NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga jana walivamia eneo la Mlima Kenya kusaka kura za urais huku... Na LEONARD ONYANGO |
KINARA wa Azimio la Umoja Raila Odinga leo Jumamosi anatarajiwa kutumia mkutano wake uwanjani Ihura, Kaunti ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
Na LEONARD ONYANGO |
CHAMA cha Pamoja African Alliance (PAA) chake Gavana wa Kilifi Amason Kingi kiko katika hatari kubwa ya kuzuiliwa... Na WANDERI KAMAU |
JUHUDI za kuliunganisha eneo la Mlima Kenya ielekeapo 2022 zinaonekana kukumbwa na changamoto tele, wadadisi wakisema... Na WANDERI KAMAU |
KUMEIBUKA hofu huenda kutajwa kwa Rais Uhuru Kenyatta kuwa miongoni mwa watu walioficha mabilioni ya fedha ng’ambo... Na BENSON MATHEKA |
MABWANYENYE kutoka Mlima Kenya wanaodadisi wagombeaji urais wanakabiliwa na kibarua kigumu kumuidhinisha atakayeweza... Na WANDERI KAMAU |
HATUA ya kutangazwa kwa kiongozi wa Narck-Kenya, Bi Martha Karua, kama kaimu msemaji wa ukanda wa Mlima Kenya, imeibua... Na CHARLES WASONGA |
MSIMAMO wa Naibu Rais William Ruto kwamba chama cha United Democratic Alliance (UDA) hakitabuni muungano na vyama... Na WANDERI KAMAU |
GAVANA Anne Waiguru wa Kirinyaga yupo kwenye njiapanda kuhusu mwelekeo wa kisiasa atakaofuata, uchaguzi mkuu wa 2022... Na CHARLES WASONGA |
MASWALI mengi yameibuliwa kuhusu sababu ya kushirikishwa kwa Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya katika mikutano... Na WANDERI KAMAU |
NI kinaya kuwa Bw Mwangi Kiunjuri na Bw Moses Kuria ndio wanaoongoza harakati za kushinikiza muungano wa kisiasa... Na BENSON MATHEKA
MSIMAMO mkali wa baadhi ya vinara wanaosuka muungano wa One Kenya Alliance (OKA) wa kukataa kumuunga kiongozi wa chama... Na BENSON MATHEKA
Vigogo wa kisiasa wanaomezea mate urais wanaendelea kuviziana kila moja akisubiri kuona hatua ambayo mwenzake... Na BENSON MATHEKA
KIONGOZI wa chama cha ODM Raila Odinga ameweka mikakati tosha ya kuyumbisha muungano wa One Kenya Alliance (OKA)... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na BRIAN OCHARO
MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji amelaumu mitandao ya mabwenyenye kwa kutatiza kesi zinazowahusu... NA FAUSTINE NGILA
MARAIS kadhaa na wakuu wa serikali duniani wametajwa katika ufichuzi wa hivi majuzi wa upelelezi wa jinsi mali ya... JOSEPH WANGUI na RICHARD MUNGUTI
VITA dhidi ya ufisadi vimeanza kuzaa matunda kwa mara ya kwanza katika historia ya Kenya huku watu... Na IBRAHIM ORUKO
WASHUKIWA wanaokabiliwa na ufisadi huenda siku zijazo wakahepa kufungwa gerezani iwapo watakubali kushirikiana na Afisi... Na CHARLES WASONGA
WANASIASA na maafisa wa serikali ambao wameshtakiwa kwa ufisadi sasa watazuiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao,... Na RICHARD MUNGUTI
ALIYEKUWA waziri wa Michezo na Jinsia, Dkt Hassan Wario huenda akasukumwa jela miaka 10 baada ya kupatikana na hatia... Na LEONARD ONYANGO
MARA baada ya kutangaza kushirikiana na kinara wa ODM Raila Odinga mnamo Machi 2018, almaarufu handisheki, Rais Uhuru... Na PETER MBURU
MIRADI inayofadhiliwa na fedha za walipa ushuru ndiyo inayotafunwa zaidi na maafisa fisadi serikalini, ripoti ya Mkaguzi... Na MAUREEN ONGALA
CHAMA cha Walimu wa Sekondari (KUPPET) kimeomba Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) ianzishe uchunguzi... Na LEONARD ONYANGO
KILA mara magavana wanapohutubia Wakenya kuhusiana na hali ya ugonjwa wa corona katika kaunti zao, wanaangua kilio... Na KAMAU MAICHUHIE
MZOZO wa uongozi umechipuka kati ya Gavana wa Kiambu, James Nyoro, na Senata Kimani Wamatangi kuhusu madai ya ufujaji... NA AP
ALIYEKUWA rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ametakiwa kupendekeza kifungo ambacho angependa kupewa kwa kukwepa vikao vya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
YALA, Siaya
Na JOHN MUTUKU SAMUEL
KALAMENI eneo hili alibubujikwa na machozi na kujitupa miguuni mwa demu kumuomba asimteme lakini... Na MWANDISHI WETU
Kangemi, Nairobi
Jombi mtaani hapa ambaye ni seremala tajika aliamua kukarabati kitanda cha jirani yake bila... Na Nicholas Cheruiyot
Mwanasiasa limbukeni alivunjika moyo mpango wake wa kumhamisha nduguye kwake ili amuachie boma atumie kujipigia... Na John Mutuku Samuel
Kisa cha kushangaza kilitokea mtaani hapa, baada ya demu aliyezuru wazazi wa mumewe kufumaniwa usiku akirandaranda... Na Mwandishi Wetu
KANGEMI, NAIROBI
JOMBI mmoja mtaani hapa anaendelea kuuguza majeraha kwenye nyeti zake baada ya kushambuliwa na... NA DENNIS SINYO
JOMBI mmoja ambaye alikuwa akiheshimiwa na wenzake alishangaza watu alipomkana mkewe hadharani ili asimkasirishe mpango... Na Mirriam Mutunga
KATHWANA, THARAKA NITHI
MWANADADA mmoja kutoka hapa alidondokwa na machozi mpenzi wake wa awali alipomuoa dada... HURUMA, NAIROBI
Na MWANDISHI WETU
Pasta wa kanisa moja mtaani humu, aliwakasirisha waumini kwa kuwatangazia kuwa atafunga kanisa kwa... Na MASHIRIKA
Frankfurt, Ujerumani
MWANAMKE mmoja katika mji huu alishangaza jamaa na marafiki kwa kusema kuwa heri mumewe angekufa... Na TOBBIE WEKESA
KERICHO
KIPUSA mtaani hapa aliwashangaza wengi alipoamua kuuza suti mpya ya mumewe ili apate fedha za kumwezesha... Na MWANDISHI WETU
VOI MJINI
Jamaa aliyekuwa paparazzi maarufu mjini humu anajuta kuuza simu na kamera yake kwa bei ya kutupa ili... KAPKATET, KERICHO
NA NICHOLAS CHERUIYOT
ILIBIDI polo wa hapa akubali kwa haraka kufanya kazi za jikoni ili kuokoa ndoa yake baada ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na MASHIRIKA
NEYMAR Jr alipachika wavuni mabao mawili na kusaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kufungua mwanya wa alama 10... Na MASHIRIKA
KIUNGO Paul Pogba amesema Manchester United wana ulazima wa “kubadilisha mbinu zao za kutandaza soka” iwapo wana ndoto ya... Na JOHN KIMWERE
CHANGAMOTO zimekuwa chungu nzima, lakini hazijazuia wachezaji wa Kiganjo Kings kutia bidii, kwani lengo lao ni kutua... Na GEOFFREY ANENE
KLABU ya Dandora Youth kutoka ligi ya daraja ya tano ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF), imejawa motisha ya kutafuta... NA ABDULRAHMAN SHERIFF
WASICHANA wanne, watatu wanafunzi wa shule za upili na mwingine wa shule ya msingi kutoka Kaunti ya Taita... Na MASHIRIKA
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO
KIUNGO wa Chelsea, Christian Pulisic, alifunga bao katika dakika za mwisho na kusaidia timu... Na GEOFFREY ANENE
TIMU ya Kenya ya raga ya wanaume ya wachezaji 15 kila upande ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 maarufu kama... Na GEOFFREY ANENE
MKIMBIAJI mkimbizi Francois Msafiri amepokea mapokezi ya kishujaa mtaani mwake Syokimau baada ya kukamilisha mbio za... Na GEOFFREY ANENE
VISSEL Kobe anayochezea Ayub Masika inakodolea macho kubanduliwa kwenye kipute cha Levain Cup baada ya kupoteza mechi... Na MASHIRIKA
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO
KIUNGO mvamizi Andre Ayew, 31, ataagana na Swansea City mwishoni mwa Juni 2021 baada ya mkataba... NA RICHARD MAOSI
KIKOSI cha Mogotio United kinajivunia wachezaji mahiri ambao wanasakata soka katika kiwango cha Kaunti ya Baringo... NA ABDULRAHMAN SHERIFF
CONGO Boys FC inaonelea fahari kuu ikiwa timu kubwa mbili za hapa nchini, Gor Mahia na AFC Leopards zitacheza mechi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
KWAKO shangazi. Nimekuwa na mpenzi kwa miaka mitatu. Wiki mbili zilizopita aliondoka akaniambia anaenda kuwatembelea wazazi wake... Na SHANGAZI
HUJAMBO shangazi? Nina umri wa miaka 28 na nilipata mtoto punde tu baada ya kukamilisha elimu ya shule ya upili. Mwanamume... Na SHANGAZI
VIPI shangazi? Nilioa miaka mitano iliyopita na tuna watoto wawili. Ilifika wakati mama watoto akashindwa kunishibisha na... Na SHANGAZI
VIPI shangazi? Nilimpa mimba mwanamke mpenzi wangu na nikamuoa kwa sababu nampenda kwa dhati. Ingawa nimeajiriwa, mshahara... Na SHANGAZI
KWAKO shangazi. Nilikuwa na mpenzi niliyempenda sana na alikuwa ameahidi kunioa. Hata hivyo, wazazi wake walipinga mpango... Na SHANGAZI
VIPI shangazi? Huu ni mwaka wa pili tangu niolewe na tumejaliwa mtoto mmoja. Ninashuku kuna kitu kinachoendelea kati ya mume... Na SHANGAZI
KWAKO shangazi. Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 36 na nimeolewa. Nina uhusiano wa pembeni na bosi wangu na nimegundua... Na SHANGAZI
KWAKO shangazi. Nina umri wa miaka 39 na huu ni mwaka wa pili nikitafuta mchumba na bado sijapata. Wanawake ni wengi na... Na SHANGAZI
HABARI zako shangazi? Nina umri wa miaka 36 na nina mtoto ingawa sijaolewa. Nimekuwa katika uhusiano wa kimapenzi na... Na SHANGAZI
SHIKAMOO shangazi! Nina jambo ambalo linanitatiza moyoni. Kuna mwanamke fulani ambaye amenasa moyo wangu na ninatamani sana... Na SHANGAZI
HUJAMBO shangazi? Nina mke ambaye tumeishi pamoja kwa mwaka mmoja sasa. Hata hivyo kuna jambo fulani ambalo nimegundua... Na SHANGAZI
KWAKO shangazi. Nimekuwa na mpenzi kwa karibu mwaka mmoja. Amekuwa akiniahidi kuwa atanioa ingawa bado hajanitambulisha kwa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
VICTOR RABALLA NA KASSIM ADINASI
WAWANIAJI viti katika ngome ya kiongozi wa ODM Raila Odinga ya Luo Nyanza, wameonywa dhidi ya mivutano...
Na WINNIE ONYANDO
KINARA wa ODM Raila Odinga na Naibu Rais William Ruto kufikia sasa wako bega kwa bega kwenye kinyang’anyiro... Na LEONARD ONYANGO
KINARA wa ODM, Raila Odinga amewatema baadhi ya washauri wake alioshirikiana nao kwa karibu kwenye uchaguzi mkuu wa... BRIAN OCHARO na VALENTINE OBARA
UBABE wa kisiasa kati ya Kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, na Naibu Rais William Ruto katika Kaunti ya... Na CHARLES WASONGA
HATUA ya Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga kushikilia kuwa wawaniaji wanaounga azma zao za... Na WANDERI KAMAU
KIONGOZI wa chama cha ODM, Bw Raila Odinga, jana alianza rasmi safari yake ya kuelekea Ikulu 2022, huku akipata... Na ANTHONY KITIMO
GAVANA wa Mombasa, Bw Hassan Joho, amehudhuria mkutano wa dharura na Kiongozi wa chama cha ODM, Bw Raila Odinga, kabla... Na KENNEDY KIMANTHI
MABWANYENYE wa eneo la Mlima Kenya leo wanatarajiwa kumwidhinisha rasmi kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, kama... Na CHARLES WASONGA
NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga wanaonekana kuendeleza mbinu za kampeni za kulambana visigino... Na LEONARD ONYANGO
MATAMSHI ya zamani ya Rais Uhuru Kenyatta ya kumdhalilisha Kiongozi wa ODM Raila Odinga yamegeuka kuwa kizingiti... Na SAMMY WAWERU
KIONGOZI wa ODM, Raila Odinga Jumamosi anaendeleza kampeni zake kutafuta uungwaji mkono eneo la Mlima Kenya kumrithi... MAUREEN ONGALA na ALEX KALAMA
GAVANA wa Kaunti ya Kilifi, Bw Amason Kingi, anakabiliwa na kibarua kigumu cha kuamua mwelekeo ambao chama... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WALLAH BIN WALLAH
KUFIKIRI ni kazi. Ubongo wako hauwezi kukupa majibu sahihi ya maswali unayoulizwa bila ya ubongo kufanya kazi ya... NA ENOCK NYARIKI
MOJA kati ya maneno mawili yatumiwayo na watu kurejelea chakula ni mlo. Kuna jingine ambalo aghalabu hukosewa katika... Na CHRIS ADUNGO
CHAMA cha Kiswahili katika Shule ya Msingi ya Stelurm Elite, Nairobi kimewawezesha wanafunzi kupiga hatua na kutia fora... Nitaanza makala haya kwa kuuliza swali lifuatalo: Je, mtu huwa na uhakika wa jambo au hakika ya jambo? Vipo baadhi ya vielezi ambavyo... Na CHRIS ADUNGO
CHAMA cha Kiswahili katika Shule ya Upili ya St Louis Butula Boys, Kaunti ya Busia (CHAKIBU), kiliasisiwa kwa nia ya... Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya habari ya Nation Media Group imeimarisha juhudi zake za kukuza matumizi ya Kiswahili kwa kutenga siku moja... Na MARY WANGARI
WAKENYA Jumatatu wameungana na jamii ya kimataifa kumboleza kifo cha Mama Sara Obama kwa kutuma risala zao za... Na MARY WANGARI
Lugha huundwa kwa sauti ambazo huunganishwa ili kuunda neno au sehemu ya neno, kisha maneno huungana kuunda miundo... NA MARY WANGARI
DHANA ya mawasiliano ni mchakato wa kuwasilisha taarifa kwa njia ya ubadilishanaji wa hisia, mawazo, matarajio,... Na CHRIS ADUNGO
USIOGOPE kukosea. Kupotea njia ndiko kujua njia. Jaribu tu. Ipo siku ambapo mghafala utaisha. Zidi kumulika uendako kwa... MTIHANI huzua changamoto kwa yeyote anayepania kuufanya. Nakisia ni kwa sababu ya ushindani unaohusishwa nao, hasa nchini mwetu. Aghalabu... Na ENOCK NYARIKI
KWA mara ya kwanza kabisa, mitihani ya Kidato cha Nne na Darasa la Nane ambayo hufanywa katika mwezi wa Kumi na Kumi na... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na MARY WANGARI
WINGU la majonzi liligubika Kenya wikendi wakati nyota mchanga wa Olimpiki, Agnes Tirop, alipopumzishwa nyumbani kwao... Na MARY WAMBUI
SERIKALI ya Uingereza imeshinikizwa kufanya uchunguzi wa ndani na kumshtaki mwanajeshi wake, anayetuhumiwa kumuua... Na BRIAN OJAMAA
MWILI wa Masten Wanjala, mwanamume aliyekamatwa kwa mauaji ya watoto, bado uko katika mochari ya Hospitali ya Rufaa ya... WYCLIFFE NYABERI na CHARLES WASONGA
WANAUME wanne wanaoshukiwa kuwateketeza wanawake wakongwe kwa tuhuma za uchawi eneo la Marani,... Na Hilary Kimuyu
POLISI katika mji wa Uhispania wa Seville wanamzuilia mwanamke Mkenya anayedaiwa kuuma na kula vidole viwili vya... Na GEORGE MUNENE
Mtu mmoja ameuawa kwa risasi huku taharuki ikizidi kutanda mjini Kianjokoma, Kaunti ya Embu kufuatia mauaji ya vijana... Na GEORGE MUNENE
Mama mmoja jana alisimulia mahakamani jinsi alivyopata chooni mifupa ya mwanawe na mjukuu wake ambao walikuwa... Na AFP
PORT-AU-PRINCE, Haiti
WATU wasiojulikana Jumatano waliingia katika makazi ya Rais Jovenel Moise wa Haiti na kumpiga risasi,... Na JOHN NJOROGE
UTATA unaendelea kuzingira kifo cha mfanyabiashara na mkurugenzi wa kampuni moja ya maua, Justus Metho Muinde katika... STANLEY NGOTHO NA SIMON CIURI
MIILI ya watatu kati ya wanaume wanne waliotoweka mjini Kitengela, Kaunti ya Kajiado mnamo Aprili 19,... SIMON CIURI na MERCY MWENDE
MWANAFUNZI wa chuo kikuu, Lawrence Warunge, aliyehusishwa na mauaji ya familia yake ya watu wanne na mjakazi... NA MASHIRIKA
MAANDAMANO makubwa jana yalizuka viungani mwa jiji la Mineapolis, Amerika baada ya polisi kumpiga risasi raia mweusi karibu... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA
SERIKALI iliyopita ya Jubilee imelaumiwa kwa kutumia jumla ya Sh55 bilioni, bila idhini ya Bunge, kwa miezi mwili na... NA BENSON MATHEKA
HUKU serikali ya Jubilee ikikaribia kuondoka mamlakani baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti 9, viongozi wake wameonyesha... NA ONYANGO K’ONYANGO
CHAMA cha Jubilee sasa kimeanza mchakato wa kushawishi wandani wa Rais Uhuru Kenyatta waliokuwa wameunda vyama... NA MWANGI MURURI
RAIS Uhuru Kenyatta ameripotiwa kukasirishwa na washauri wake kuhusu ripoti zao za hali ya kisiasa katika eneo la Mlima... NA MWANGI MUIRURI
WANDANI wa Rais Uhuru Kenyatta wamelaumiwa kwa kuchangia kudidimia kwa umaarufu na ushawishi wake katika eneo la Mlima... Na PSCU
RAIS Uhuru Kenyatta amekariri kujitolea kwa serikali katika kuboresha maslahi ya walemavu, akisema watasaidiwa kushiriki... Na WANDERI KAMAU
RAIS Uhuru Kenyatta kwa mara nyingine alionyesha dalili za kuunga mkono azimio la kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga,... Na CHARLES WASONGA
RAIS Uhuru Kenyatta Jumanne alitoa kumbukumbu ya nyakati ambapo alihudumu bungeni kama Mbunge Maalum, Kiongozi wa... Na SAMMY WAWERU
RAIS Uhuru Kenyatta anahutubia taifa leo Jumanne alasiri katika kikao cha pamoja cha bunge, wengi wakisubiri kusikia... Na CHARLES WASONGA
RAIS Uhuru Kenyatta leo Jumanne anatarajiwa kuangazia mikakati ya serikali ya kukabiliana na changamoto zinazolikumba... Na CHARLES WASONGA
RAIS Uhuru Kenyatta atatoa hotuba kuhusu Hali ya Taifa katika kikao maalum cha Bunge la Kitaifa na Seneti mnamo... Na BENSON MATHEKA
SERIKALI imeonywa kuwa mazoea ya maafisa wake, akiwemo Rais Uhuru Kenyatta ya kukaidi maagizo ya mahakama na utawala... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na MACHARIA MWANGI
WAZIRI wa Leba Simon Chelugui ameziomba kampuni mbalimbali zihakikishe kuwa haziwafuti wafanyakazi wao hata... Na WANGU KANURI
TEKNOLOJIA imeiboresha sekta ya upishi haswa kwa wale ambao waliendeleza huduma zao mtandaoni licha ya janga la... Na WANGU KANURI
WAKENYA wanaoishi na ulemavu pamoja na wale wakongwe sasa wataweza kupokea huduma wanazotaka kidijitali za mawasiliano... Na FAUSTINE NGILA
LABDA hujasikia hili lakini linakuathiri moja kwa moja kwa kuwa wewe ni mteja wa M-Pesa. Majuzi rafiki yangu alimfaa... Na STEPHEN ODUOR
VIJANA katika Kaunti ya Tana River, wametaka mafunzo ya kisasa yatolewe katika taasisi na vyuo vya kiufundi ili... NA FAUSTINE NGILA
MAGARI mengi yanayomilikiwa humu nchini na duniani kote yanatumia dizeli au petroli, mafuta ambayo yanachafua... Na FAUSTINE NGILA
SUALA muhimu lililojitokeza katika ziara ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uingereza wiki iliyopita, lilikuwa azma ya... Na FAUSTINE NGILA
NI miaka mitatu sasa tangu Ripoti ya Blockcheni na Akili Bandia (AI) iwasilishwe kwa serikali kwa ajili ya utekelezaji... Na Ruth Mbula
SPIKA wa Bunge la Kitaifa, Bw Justin Muturi, amewarai wadau wa afya kuharakisha utekelezaji wa taratibu za kutumia... [caption id=attachment_77341" align="alignnone" width="843"] Wataalamu wakagua uvunaji wa bitcoin katika kituo cha Bitfarms eneo la Saint... Na FAUSTINE NGILA |
Inashangaza kuwa licha ya Kenya kupiga hatua kubwa katika maendeleo ya kiteknolojia, karatasi bado zinatumika katika... Na MASHIRIKA |
Kutokana na ongezeko la matumizi ya simu tamba na za kisasa pamoja na kuimarishwa kwa mitandao, imekuwa rahisi kwa idadi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
Na RICHARD MUNGUTI |
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi Ijumaa alizimwa na mahakama kupeperusha katika mitandao ya kijamii video... Na RICHARD MUNGUTI |
KUNDI jipya la mawakili sita waliokuwa wanamwakilisha aliyekuwa gavana wa Nairobi Bw Mike Sonko Jumanne walijiondoa... Na RICHARD MUNGUTI |
RIPOTI ya daktari wa tiba za akili imesema Alhamisi kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko anaugua maradhi ya... Na RICHARD MUNGUTI |
MAHAKAMA ilielezwa jana kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko angali amelazwa katika Nairobi Hospital... Na RICHARD MUNGUTI |
UFICHUZI wa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko kwamba mtu aliingia kwenye seli anamozuiliwa katika kituo cha... Na BENSON MATHEKA |
Aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko anajuta kwa vitendo alivyofanya akiwa mamlakani; akiepuka kuadhibiwa kwa... Na RICHARD MUNGUTI |
KAMA kuna wakati wenye changamoto tele kwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko ni sasa. |
Maji yalizidi unga hata... Na RICHARD MUNGUTI |
MASAIBU ya aliyekuwa gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko, yaliongezeka Jumatano ilipofichuka kuwa serikali inapanga... Na RICHARD MUNGUTI |
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi, Mike Sonko aliangua kilio kortini Jumatano wakati wa kusikizwa kwa kesi ya ufisadi wa... Na CHARLES WASONGA |
WANASIASA na watu ambao majina yao yatawekwa katika orodha ya aibu ya Tume ya Uwiano na Utangamano ya Kitaifa (NCIC)... BENSON MATHEKA na SIMON CIURI |
Masaibu ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Mike Sonko yaliendelea kuongezeka jana alipozuiliwa rumande baada... Na RICHARD MUNGUTI |
MASAIBU ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi Gidion Kioko yameongezeka baada ya kusukumwa ndani hadi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA SAMMY WAWERU MSANII tajika wa nyimbo Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda ametengana na mpenzi wake mwanasiasa Karen Nyamu. Hii ni kutokana na video iliyochipuka ambayo anaskika akisema “nilikuwa kwenye ndoa ya mitara, sasa niko singo”. Samidoh amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Seneta Maalum Karen Nyamu, na wamejaaliwa kupata watoto wawili. Msanii huyo wa nyimbo za Agikuyu, alifichua kuachana na Karen kupitia video ya mbashara ya Tiktok (live) ambapo alikuwa akijibu maswali ya mashabiki wake. Wakati wa mafichuzi hayo, alionekana kuwa kwenye eneo la burudani alikoandamana na msichana ambaye hakuweka wazi endapo ndiye mchumba wake mpya. “Ati hongera kwa kuwa na mpenzi mpya…” Samidoh akasoma mojawapo ya jumbe zilizotumwa na mashabiki wake. Alijibu, “Si wewe pekee ulishushwa madaraka kutoka kiwango cha hadhi hadi dereva wangu…Nilikuwa kwenye ndoa ya mitara ila sasa niko singo”. Mfuasi huyo aliendelea kumdadisi, akitaka kujua iwapo Samidoh anafahamu kuhusu ukurasa wa kimitandao unaohusishwa na mchumba wake – Karen Nyamu Fun Page. Kwa ucheshi, mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Kairetu Gakwa (Binti yangu) na Ndiri Mutwe Mwega (Sina kichwa kizuri) alisema kwa sasa anajishughulisha na biashara. “Kwa sasa, ninajishughulisha na masuala biashara. Ikiwa si mradi au biashara, ishi na mama yako,” alielezea. Shabiki wake alimkejeli akitaka kujua aliko nina yake, isijulikane ikiwa alimaanisha mama yake mzazi au mpenzi wake. “Ameoleka na kwa sasa anafurahia fungate (honeymoon),” Samidoh alidokeza. Kidosho aliyeandamana naye alitambua shabiki huyo kama Shabaan, akisema kwamba yeye ni mchochezi. “Wee acha hiyo, unajua Shabaan wewe ni mchochezi sana… (Yuko hapa (akimaanisha Karen Nyamu),” mwanadada huyo alisema. Naye Samidoh aliendelea, “Tunataka Karen, naona hivo ndivo mchango safuni unasema…Naona, lakini sasa yuko online kweli?” Kipusa aliyeandamana naye, alijibu, “Yuko online, mjaribu”. Aidha, shabiki wa Samidoh alitaka Karen Nyamu ajumuishwe kwenye mazungumzo hayo ya mbashara Tiktok. Kilichoshangaza zaidi na kuashiria utengano wa Samidoh na Karen, ni kudai kwamba alimbloki mtandaoni na angeweza kushiriki endapo atamuondoa alikomuweka. “Yuko kwenye orodha ya kublokiwa, sasa hiyo ndio shida. Labda nisitishe mazungumzo haya ya moja kwa moja ili nimuondoa aweze kujumuika nasi,” Samidoh alifafanua. Mahusiano kati ya Samidoh na Karen, ndiyo yalichangia kuachana na mkewe, Edday Nderitu ambaye alihamia Amerika Mei 2023. Edday alikuwa ameonya msanii huyo mapema 2023, akisisitiza kwamba hakuwa tayari kuwa kwenye ndoa ya mitara. Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA SAMMY WAWERU MSANII tajika wa nyimbo Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda ametengana na mpenzi wake mwanasiasa Karen Nyamu. Hii ni kutokana na video iliyochipuka ambayo anaskika akisema “nilikuwa kwenye ndoa ya mitara, sasa niko singo”. Samidoh amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Seneta Maalum Karen Nyamu, na wamejaaliwa kupata watoto wawili. Msanii huyo wa nyimbo za Agikuyu, alifichua kuachana na Karen kupitia video ya mbashara ya Tiktok (live) ambapo alikuwa akijibu maswali ya mashabiki wake. Wakati wa mafichuzi hayo, alionekana kuwa kwenye eneo la burudani alikoandamana na msichana ambaye hakuweka wazi endapo ndiye mchumba wake mpya. “Ati hongera kwa kuwa na mpenzi mpya…” Samidoh akasoma mojawapo ya jumbe zilizotumwa na mashabiki wake. Alijibu, “Si wewe pekee ulishushwa madaraka kutoka kiwango cha hadhi hadi dereva wangu…Nilikuwa kwenye ndoa ya mitara ila sasa niko singo”. Mfuasi huyo aliendelea kumdadisi, akitaka kujua iwapo Samidoh anafahamu kuhusu ukurasa wa kimitandao unaohusishwa na mchumba wake – Karen Nyamu Fun Page. Kwa ucheshi, mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Kairetu Gakwa (Binti yangu) na Ndiri Mutwe Mwega (Sina kichwa kizuri) alisema kwa sasa anajishughulisha na biashara. “Kwa sasa, ninajishughulisha na masuala biashara. Ikiwa si mradi au biashara, ishi na mama yako,” alielezea. Shabiki wake alimkejeli akitaka kujua aliko nina yake, isijulikane ikiwa alimaanisha mama yake mzazi au mpenzi wake. “Ameoleka na kwa sasa anafurahia fungate (honeymoon),” Samidoh alidokeza. Kidosho aliyeandamana naye alitambua shabiki huyo kama Shabaan, akisema kwamba yeye ni mchochezi. “Wee acha hiyo, unajua Shabaan wewe ni mchochezi sana… (Yuko hapa (akimaanisha Karen Nyamu),” mwanadada huyo alisema. Naye Samidoh aliendelea, “Tunataka Karen, naona hivo ndivo mchango safuni unasema…Naona, lakini sasa yuko online kweli?” Kipusa aliyeandamana naye, alijibu, “Yuko online, mjaribu”. Aidha, shabiki wa Samidoh alitaka Karen Nyamu ajumuishwe kwenye mazungumzo hayo ya mbashara Tiktok. Kilichoshangaza zaidi na kuashiria utengano wa Samidoh na Karen, ni kudai kwamba alimbloki mtandaoni na angeweza kushiriki endapo atamuondoa alikomuweka. “Yuko kwenye orodha ya kublokiwa, sasa hiyo ndio shida. Labda nisitishe mazungumzo haya ya moja kwa moja ili nimuondoa aweze kujumuika nasi,” Samidoh alifafanua. Mahusiano kati ya Samidoh na Karen, ndiyo yalichangia kuachana na mkewe, Edday Nderitu ambaye alihamia Amerika Mei 2023. Edday alikuwa ameonya msanii huyo mapema 2023, akisisitiza kwamba hakuwa tayari kuwa kwenye ndoa ya mitara. Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA RICHARD MAOSI WAKAZI wa mtaa wa Mazembe viungani mwa mji wa Nakuru wamekiri kuhangaishwa na wezi ambao huwaibia na kuwasindikiza hadi nyumbani. Huwawekea ulinzi huo makusudi ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafika nyumbani salama salimini. Kwa kawaida, wahuni wamebuni mbinu mpya ya kutembea na mbwa wakubwa nyakati za usiku, ili kujiwekea ulinzi wa kibinafsi. Owen Shibala mwendeshaji bodaboda kati ya Nakuru mjini na Mazembe, anasema hajui walikotoa ujasiri walio nao kushika doria usiku utadhani ni polisi. Mazembe ni mojawapo ya mitaa ambayo hushuhudia visa vya kihalifu na utumiaji wa mihadarati mara kwa mara. “Ukikutana nao usiku ni lazima usalimishe kila kitu lau sivyo utaona cha mtema kuni. Watakucharaza viboko na kuiba kila kitu cha nguvu,”akasema. Hata hivyo, wanapoiba hujitwika jukuma la kuwasindikiza wakazi, wasije wakakutana na vibaka wengine barabarani. Aidha, wanalia sare za polisi jambo linalowafanya baadhi ya raia kuamini huenda wanashirikiana na maafisa wa polisi. Baadhi yao wanajifanya ni maafisa wa polisi ambao huwa wameshika doria, wakilenga kuhangaisha wapita njia wanaotoka kazini usiku. Agnes Wahome mfanyibiashara mtaani Rhonda anasema huwa wamejihami kwa visu, rungu na wako tayari kupigana. Kulingana na Bi Wahome, hii ni hali ya kawaida siku hizi katika mitaa ya Manyani, Bondeni na Freearea ambapo vijana wengi wamejiingiza kwenye uhalifu. Bi Wahome anasema wahalifu wengi wanajulikana, kwani ni vijana wadogo kutoka mitaa jirani ya Flamingo na Lakeview. Mkazi huyo angependa polisi kushika doria katika maeneo husika ili kuzuia kuzuka kwa magenge hatari yanayohangaisha wenyeji. Hili linajiri siku chache baada ya Taifa Leo Dijitali kufichua visa vya wizi ambapo baadhi ya wezi kutoka kwenye mtaa wa Gioto, Nakuru wamekuwa wakipika chakula katika kila nyumba wanamoingia kuiba. Mtaa wa Bondeni, Kaunti ya Nakuru ambapo wezi huwaibia wakazi na kuwasindikiza mpaka nyumbani. PICHA|RICHARD MAOSI |
Tags |
You can share this post! |
Previous article |
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya... |
Next article |
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika... |
T L |
Tags |
You can share this post! |
Previous article |
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya... |
Next article |
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika... |
T L |
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA RICHARD MAOSI WAKAZI wa mtaa wa Mazembe viungani mwa mji wa Nakuru wamekiri kuhangaishwa na wezi ambao huwaibia na kuwasindikiza hadi nyumbani. Huwawekea ulinzi huo makusudi ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafika nyumbani salama salimini. Kwa kawaida, wahuni wamebuni mbinu mpya ya kutembea na mbwa wakubwa nyakati za usiku, ili kujiwekea ulinzi wa kibinafsi. Owen Shibala mwendeshaji bodaboda kati ya Nakuru mjini na Mazembe, anasema hajui walikotoa ujasiri walio nao kushika doria usiku utadhani ni polisi. Mazembe ni mojawapo ya mitaa ambayo hushuhudia visa vya kihalifu na utumiaji wa mihadarati mara kwa mara. “Ukikutana nao usiku ni lazima usalimishe kila kitu lau sivyo utaona cha mtema kuni. Watakucharaza viboko na kuiba kila kitu cha nguvu,”akasema. Hata hivyo, wanapoiba hujitwika jukuma la kuwasindikiza wakazi, wasije wakakutana na vibaka wengine barabarani. Aidha, wanalia sare za polisi jambo linalowafanya baadhi ya raia kuamini huenda wanashirikiana na maafisa wa polisi. Baadhi yao wanajifanya ni maafisa wa polisi ambao huwa wameshika doria, wakilenga kuhangaisha wapita njia wanaotoka kazini usiku. Agnes Wahome mfanyibiashara mtaani Rhonda anasema huwa wamejihami kwa visu, rungu na wako tayari kupigana. Kulingana na Bi Wahome, hii ni hali ya kawaida siku hizi katika mitaa ya Manyani, Bondeni na Freearea ambapo vijana wengi wamejiingiza kwenye uhalifu. Bi Wahome anasema wahalifu wengi wanajulikana, kwani ni vijana wadogo kutoka mitaa jirani ya Flamingo na Lakeview. Mkazi huyo angependa polisi kushika doria katika maeneo husika ili kuzuia kuzuka kwa magenge hatari yanayohangaisha wenyeji. Hili linajiri siku chache baada ya Taifa Leo Dijitali kufichua visa vya wizi ambapo baadhi ya wezi kutoka kwenye mtaa wa Gioto, Nakuru wamekuwa wakipika chakula katika kila nyumba wanamoingia kuiba. Mtaa wa Bondeni, Kaunti ya Nakuru ambapo wezi huwaibia wakazi na kuwasindikiza mpaka nyumbani. PICHA|RICHARD MAOSI |
Tags |
You can share this post! |
Previous article |
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya... |
Next article |
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika... |
T L |
Tags |
You can share this post! |
Previous article |
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya... |
Next article |
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika... |
T L |
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA RICHARD MUNGUTI MASKWOTA wapatao 10,000 wamewasilisha upya kesi katika Mahakama ya Upeo wakiomba ibatilishe uamuzi kwamba wafukuzwe kutoka kwa shamba la ukubwa wa ekari 25,000 wanalong’ang’ania umiliki wake na familia ya mwanasiasa marehemu Mark Too. Maskwota hao wanaodai mababu zao ndio waliotimuliwa kutoka kwa shamba hilo enzi za ukoloni, wanasema walipewa shamba hilo rasmi na aliyekuwa Rais hayati Daniel arap Moi, kisha Kamishna wa Ardhi M Okundu akaratibisha uamuzi huo mwaka 2007. Katika ombi lililowasilishwa na wakili William Arusei chini ya sheria za dharura, kikundi cha maskwota hao–Sirikiwa Squatters Group–kimeomba mahakama ibatilishe uamuzi huo kwa vile ilitegemea ushahidi ambao haukuwa umewasilishwa katika kesi waliyoshtaki katika Mahakama ya kuamua kesi za mashamba (ELC), Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu. Pia wameeleza bayana Jaji Mkuu Martha Koome, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu, majaji Mohammed Ibrahim, Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Isaack Lenaola, na William Ouko walitegemea ushahidi wa Afisa wa Ugavi wa Mashamba R J Simiyu kutoa uamuzi wang’atuke shambani. Maskwota hao wamesema ushahidi wa Bw Simiyu uliowasilishwa mbele majaji hao saba kwa njia ya afidaviti ni mpya na kamwe “haukuwasilishwa mbele ya Jaji Antony Ombwayo aliposikiliza na kuamua kesi hiyo 2017.” Pia wanasema ushahidi huo haukuwasilishwa Mahakama ya Rufaa iliyosikiliza rufaa iliyowasilishwa na kampuni ya Fanikiwa, familia ya marehemu Mark Too, kampuni ya Lonrho Agribusiness (EA) Ltd, na Bw David K Korir. Hivyo basi, maskwota hao wanaeleza mahakama hii ya upeo kwamba ni kinyume cha sheria kutegemea ushahidi mpya kutoa uamuzi wa kesi hii iliyo na umuhimu mkubwa kwa umma. “Uamuzi huu wa Mahakama ya Juu wa Desemba 15, 2023, hauna mashiko kisheria na kamwe hauna nguvu kisheria kuwatimua maskwota hawa kutoka kwa shamba lao,” asema Bw Arusei. Pia maskwota hawa wanadai kwamba badala ya Mahakama ya Juu kujadili masuala ya kikatiba jinsi ilivyo jukumu lake, majaji hao walianza kufafanua na kutafsiri ushahidi wa watu binafsi na kuelezea maana ya ‘skwota’. Mahakama hii imeombwa ikague upya uamuzi iliyotoa kwa vile ilidanganywa na walalamishi na pia kutendewa ujanja. Akinukuu maamuzi ya majaji wastahiki kama vile Lord Dening, Bw Arusei amesema, mahakama ikigundua ilipotoshwa au kudanganywa na upande mmoja, iko na mamlaka na uwezo wa kufutilia mbali uamuzi iliyotoa na kuandika mwingine. Maskwota hao wanaomba Mahakama ya Juu iwarudishe shambani kama ilivyokuwa imeamuliwa na Jaji Ombwayo na Mahakama ya Rufaa. Vile vile mahakama hiyo imekosolewa kwa kumshambulia hayati Moi katika uamuzi huo pasi kutoa agizo wasimamizi wa mali yake wafike mbele yao kutoa mwanga kuhusu suala la umiliki wa shamba hili lililorudishwa kwa serikali na kampuni iliyokuwa inakuza miti inayotumika katika viwanda vya ngozi. Naibu msajili wa Mahakama ya Juu Nelly Kariuki aliwaamuru maskwota hao wawakabidhi nakala za kesi hii yao mpya wahusika wote kabla ya Januari 31, 2024, kesi itakapotajwa tena kwa maagizo zaidi. Jaji aliyesikiliza kesi hii mpya hakuiratibisha kuwa ya dharura ila aliamuru pande zote ziwasilishe ushahidi katika muda wa siku 14 kuanzia Desemba 21, 2023. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA RICHARD MAOSI WAMILIKI wa nyumba za wapangaji mtaani Kayole wameamua kulala mchana na kukaa macho usiku ili kupambana na wahalifu ambao wametawala ploti zao. Aidha wapangaji wanapoendelea kufurahia sikukuu wakiwa mashambani, wezi kwa upande mwingine wanavunja nyumba na kuiba bidhaa kutoka ploti moja hadi nyingine. Mbali na Kayole, maeneo mengine ambapo wizi umeripotiwa ni Kangemi, Korogocho, Githurai, Umoja, Kariobangi, Starehe, Syokimau, na Buruburu. Wanavunja nyumba na kuiba vyombo, fanicha, mitungi ya gesi ya kupikia, televisheni, na redio, huku hatimaye bidhaa hizo zikiuzwa kwa bei ya kutupa mtaani. Bw Gilbert Ambani ambaye ni mlinzi katika mojawapo ya ploti eneo la Syokimau, anasema wezi wengi huko katika msimu huu wa shamrashamra wanalenga vyuma chakavu kwa sababu huwapatia hela za haraka. “Baadhi ya wezi wanabomoa lango kuu na kuchukua vyuma huku wengine wakivunja mifereji,” Bw Ambani akaambia Taifa Leo. Naye Amon Andika ambaye ni landilodi mtaani Kayole, alisema kwamba imemlazimu kufanya kazi ya ziada ya kulinda nyumba za wapangaji wake ambao wengi walienda mashambani almaarufu ‘ushago’. Anasema mwaka 2023 ameamua kufanya kazi ya usoja kama wengi wanavyoiita, baada ya kubaini kuwa baadhi walinzi wake wa awali walikuwa wakishirikiana na wezi kutekeleza wizi. Bw Andika ameingia gharama ya kuwekeza upya kwenye mradi wa maji baada ya wezi kuvunja mfereji wake usiku wa Desemba 24, 2023, na kutoweka na paipu ya thamani ya Sh70,000. Anasema kwa sababu ya hali ngumu ya kiuchumi, hana uwezo wa kuajiri soja wa usiku. Ndiposa imemlazimu kuhatarisha maisha yake kwa kulinda mali mpaka ifikapo Mwaka Mpya 2024. Anasema ni desturi yake kila mwaka wapangaji wanapokuwa wameelekea ‘ushago’ kufurahia sikukuu, yeye anadumisha usalama. Mnamo Desemba 27, 2023, washukiwa 34 wa wizi walikamatwa katika eneobunge la Starehe katika operesheni iliyoongozwa na chifu na maafisa wa polisi. Hali ni kinyume na baina ya mwaka wa 2020 na 2021 ambapo wakazi wengi wa jiji waliamua kutosafiri kwa sababu ya mlipuko wa janga la Covid-19. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA CHARLES WASONGA KIONGOZI wa Narc-Kenya Martha Karua amesema kuwa muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya ulitoka mikono mitupu katika mazungumzo kati yake na mrengo wa Kenya Kwanza (KKA). Kwenye mahojiano na runinga ya Citizen mnamo Alhamisi usiku, Bi Karua alidai wanachama wa Azimio katika Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo (Nadco) walisaidia KKA kuendeleza ajenda zao. “Kwa mtazamo wangu, mazungumzo hayo hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu hakuna muafaka uliofikiwa kuhusu ajenda zetu tatu kuu ambazo ni gharama ya maisha, haki katika uchaguzi, na heshima kwa demokrasia ya vyama vingi,” akasema Bi Karua. Akaongeza: “Muafaka ulipatikana kuhusu ajenda za Kenya Kwanza kama vile kuundwa kwa afisi ya kiongozi rasmi wa upinzani, na kuhalalishwa kwa afisi ya Mkuu wa Mawaziri, ambazo tayari Ruto alikwisha kuwasilisha bungeni.” Kiongozi huyo wa Narc Kenya alieleza kuwa vikao vya kamati ya Nadco vilivyodumu kwa miezi minane vilikuwa ni vya kuwapotezea Wakenya hela na muda kwa sababu serikali haikuongozwa na nia njema iliposhiriki mazungumzo na upinzani. “Mazungumzo hayo yalilenga kutuchezea shere na kutuliza maandamano. Matokeo ya mazungumzo yetu na utawala wa KKA hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu Wakenya bado wanaumizwa na kupanda kwa gharama ya maisha. Kwa mtazamo wangu, ripoti ya Nadco haina maana yoyote kwa Wakenya kwa sababu haishughulikii madhila yao,” Bi Karua, ambaye alikuwa ni mgombea mwenza wa Raila Odinga katika uchaguzi wa urais wa Agosti 9, 2022, akaongeza. Alielekeza lawama kwa utawala wa Kenya Kwanza kwa kile alichodai ni kufeli kufikiwa kwa malengo ya mazungumzo yake na upinzani. “Licha ya sisi kama upinzani na wananchi kuendelea kuushinikiza utawala huu upunguze gharama ya maisha, walipuuza na badala yake kuendelea kuongeza bei ya bidhaa za kimsingi na kuanzisha aina nyingine za ushuru,” akasema. Ili mazungumzo yoyote yafaulu, kulingana na Bi Karua, chama au mrengo ulioko mamlakani ni sharti kuonyesha nia njema kwa sababu wao ndio wanasukumwa kutimiza matakwa ya wananchi. Kiongozi huyo wa Narc-Kenya aliutaja utawala wa sasa kama ambao hauheshimu sheria na maamuzi ya mahakama. “Utawala huu unaendesha majukumu ya serikali kwa namna ambayo haijeshimu sheria na kudharau maoni ya wananchi ulivyofanya wakati wa ukusanyaji maoni ya umma kuhusu Sheria ya Fedha,” akasema. “Unapodharua Katiba na watu ambao walikupa mamlaka na matakwa ya wengi, unageuka serikali mbaya,” akaeleza alipoulizwa sababu yake ya kuirejelea serikali hivyo. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA FARHIYA HUSSEIN MWAKA 2023, unyama uliokuwa ukifanywa ndani ya wa Shakahola katika Kaunti ya Kilifi, ulifichuliwa ambapo zaidi ya watu 400 walipoteza maisha yao kwa itikadi kali za kidini. Mhubiri Paul Mackenzie ambaye alitajwa kuwa kiongozi wa wafuasi wake, anachunguzwa kwa madai ya kuwapotosha katika mafundisho ya kidini ambapo waumini walichanganyikiwa, wakiwemo watoto, wakaanza kufunga au kususia chakula hadi wakaanza kudhoofika na hatimaye kuanza kuaga dunia mmoja baada ya mwingine. Habari hizo zilipofahamika, idadi hii ya watu waliopoteza maisha ilikuwa nyingi sana, jambo liloshangazaa ulimwengu mzima. Walionusurika waliozungumza na Taifa Leo alisema waliokufa waliambiwa wafunge hadi kufa ili wakutane na ‘Yesu’. Miezi tisa baadaye, miili zaidi ya 400 inaendelea kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha muda katika Kaunti ya Kilifi, ukumbusho wa kusikitisha kuashiria msimamo wao mkali wa kidini waliofuatilia. Watu hawa, ambao walitajwa na jamaa zao kuwa watu wachangamfu na maisha hapo awali walionekana kuishi maisha ya kudhoofisha na ya hali ya kusikitisha, maisha yao yalikatishwa na imani zile walizofuatilia kwa kina. Msitu huo ambao hapo awali ulikuwa sehemu nzuri ya mandhari ya kiasili, sasa umekuwa shahidi kwa ukatili uliofanywa huko ndani. Shakahola, kijiji katika Kaunti ya Kilifi, kilikuwa kimegubikwa na ukimya wa kutisha kwa miezi kadhaa. Makazi hayo ambayo wanakijiji walitaja zamani yalikuwa ya uchangamfu na yenye shughuli nyingi, sasa yalionekana yametawaliwa na ukimya mkuu. Katika msitu huo wa Shakahola, nyumba zilikuwa za udongo huku zikiezekwa kwa mapaa ya makuti. Njia zilizokuwa na watu wengi sasa zilikuwa kimya kwa kutisha, kana kwamba wanakijiji walikuwa wametoweka wakiacha nyuma vitu vya kibinafsi kama vile Biblia, ushahidi kuwa waliondoka ghafla. Sahani zilizotelekezwa zilizofunikwa ziliashiria ‘mlo wa mwisho’ wa wafuasi wa Kanisa la Good News International la Mchungaji Paul Mackenzie, ambalo inadaiwa lilichochea wao kuchukua mkondo hatari wa kufunga hadi kufa. Katika mazingira haya ya kutatanisha, ambapo ibada inayodhaniwa ilikuwa imezama katika unabii wa apocalyptic, cha kusikitisha ni kwamba baadhi yao hawakunusurika katika safari ya kuenda katika Hospitali Kuu ya Malindi. Wahanga walizikwa bila mpangilio makaburi yao yakiashiria kuzikwa kwao kwa haraka. Miezi kadhaa baadaye, miili yao ilifukuliwa. Watu hawa walionekana kutengwa na kusukumwa kwenye ukingo wa jamii, sauti zao zikiwa zimenyamazishwa na nguvu za itikadi kali. Maisha yao yalipochukuliwa kwa uchungu, heshima waliyostahili katika umauti wa iliondolewa pia. Ni wale tu walioaga dunia wangejua ikiwa kweli walikutana na Mungu wao. Miili yao ilizikwa kwa haraka msituni Shakahola, jambo lililodhihirishwa na jinsi makaburi hayo yalivyofukuliwa ambapo kwa kila mojawapo, miili zaidi ya mmoja ilipatikana ndani. Waumini hao hawakuzikwa na sanduku kama ilivyo kwa Wakristo bali walifunikwa na blanketi na nguzo nyinginezo. Miezi tisa baadaye, chumba cha kuhifadhia maiti cha muda bado kimesalia katika hopsitali ya Malindi, ukumbusho wa mkasa uliotokea mwaka 2023. Waathiriwa wamesalia katika hali ya kutatanisha, utambulisho wao bado haujathibitishwa, hadithi zao kubaini kiini cha kilichotokea ndani ya msitu wa Shakahola bado haijabainika. Hata katika kifo, ibada iliwanyima utambulisho wao, na kuacha miili hiyo ‘haijulikani’ kutokana na ukosefu wa nyaraka zozote. Ukweli uligundulika ni kwamba baadhi ya wanachama hao walitoka kaunti za mbali katika mikoa mingine nchini, jambo la kutatanisha katika kutambua na kudai miili hiyo. Mwezi Mei, serikali ilianzisha mpango wa DNA kulenga familia zinazoshuku kuwa jamaa zao waliopotea au walioaga wanaweza kuhusishwa na msitu wa Kilifi’ Shakahola. Takriban miezi saba imepita tangu kuzinduliwa kwake, lakini familia zinalalmikia kungoja matokeo ya DNA kwa hamu. Miongoni mwa walioathiriwa ni Bw Rodgers Mwibo, ambaye anatafuta mama yake, dada yake, na mpwa wake amabye alisema ni wafuasi waaminifu wa mhubiri Paul Mackenzie kutoka Kanisa la Good News International, waliohamia kwenye msitu huo mwaka mmoja uliopita. Akielezea masikitiko yake, Bw Mwibo alieleza kuwa kufuatia tangazo la serikali, alitoa sampuli zake za DNA kaunti za Nairobi na Malindi. “Badala ya kupata faraja, huku kusubiri kwa muda mrefu kunazidisha kiwewe changu. Kila nikiona picha ya mama yangu, natamani sana uwepo wake, hata kama ni kumuaga tu,” alilalamika Bw Mwibo huku akihoji ufanisi wa taratibu za DNA za serikali. Kulingana na Bw Mwibo, uhakikisho ulitolewa kwamba matokeo yatatolewa mara moja baada ya ukusanyaji wa DNA. Hata hivyo, kile kilichoahidiwa kuwa kipindi kifupi kimeongezeka hadi mwaka mmoja, na kumuacha yeye na wengine katika hali ya huzuni ya kihisia moyo. “Ni katika nchi gani miili hubaki kuhifadhiwa kwenye friji huku familia zikistahimili uchungu huu?” aliuliza Bw Mwibo. Jamaa mwingine, Bi Mary Mwikali anabainisha kuwa hatajua iwapo dadake na mpwa wake ni miongoni mwa waliofukuliwa kutoka msitu wa Shakahola au la. Kusubiri kwa hamu kunaendelea, na kuwaacha wakihangaika na sintofahamu ikiwa wapendwa wao bado wako hai au ni miongoni mwa watu 400 na zaidi wakiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Malindi. Afisa wa Masuala ya Dharura katika Shirika la Haki Africa, Bw Mathias Shipeta, alisema wasiwasi wake ni kwamba serikali imechukua muda mrefu unaohitajika ili kulinganisha na kulinganua DNA. “Inachukua muda gani hadi ulinganishaji wa DNA ukamilike? Familia zinamaliza mwaka bila kujua jamaa zao waliko. Haijafahamika wazi kama wameaga dunia au wapo hai. Ili kulifunga suala hili, ulinganishaji wa DNA lazima ukamilike na kukamilika kwa wakati kabla ya mwisho wa mwaka,” Bw Shipeta alisisitiza. Mwezi Julai, sampuli 266 zilikusanywa kwa madhumuni ya utambulisho wa vinasaba DNA. Uchunguzi wa DNA ni ulinganifu wa kisayansi wa maelezo ya kinasaba ya watu wasiojulikana au waliokufa na yale ya watu waliotambuliwa (waliokufa au walio hai). Mchakato huo ni muhimu kwa sababu za kisheria na za kibinadamu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA MWANGI MUIRURI MASHABIKI wa klabu ya Arsenal mjini Murang’a sasa wameonywa na wenzao wa Manchester United na Chelsea wajiandae kumpokea ndovu wao akianguka pasipo hiari kutoka juu ya mti kumaanisha kushuka katika jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL). “Huku kulimwa ambako mmeanza kulimwa ni mwanzo tu wa namna ambavyo mambo yatakuwa magumu kwenu katika mzunguko wa pili,” akafoka Bw David Njuguna ambaye ni mshirikishi wa the Red Devils mjini humo. Cheo chake hakitambuliki rasmi na klabu ya Manchester United. Bw Njuguna alisema kwamba Arsenal kuwa juu ya jedwali hata kwa mwanya wa pointi 10 sio tishio kwa kuwa katika mkondo wa lala salama, wao huwa butu, wasio na maono na mwelekeo na lazima wajihujumu wao wenyewe kama ilivyokuwa msimu jana. Katika mechi ya usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, Arsenal walirambishwa magoli 2-0 na West Ham. “Hata hamna heshima na wawekezajj na mnatuchomea beti. Kwa kuwa sikuamini kabisa mngeshinda hicho kipute, nilikuwa nimebashiri timu zote mbili angalau zingejipa goli. Sasa ona hamkufunga hata la kukataliwa,” akafoka Stacy Keach, mfuasi wa Chelsea. Janga hilo kwa wanabunduki Arsenal limewaacha katika nafasi ya pili kwenye jedwali wakiwa na pointi 40 huku Liverpool ikibakia kidedea kwa pointi 42. Hii ina maana kwamba Man City ambayo iko na pointi 37 kwa sasa lakini ikiwa imecheza mechi 18 Arsenal ikiwa imecheza mara 19 itaifurusha kutoka nafasi hiyo ya pili iwapo itachapa Sheffield United hapo Jumamosi kwa ubora wa magoli. “Kuna uwezekano mkubwa kwamba Arsenal itaingia mwaka Mpya ikiwa nambari tano nyuma ya Liverpool, Man City, Aston Villa na Tottenham na kabla ya tufike mechi ya 27, hata West Ham, Man United… watakuwa mbele ya Arsenal,” akasema Junita Kasyoki ambaye anashabikia Man United. Ni usiku ambao wafuasi wa Arsenal hawakujibu mipigo, waliondoka polepole na kimyakimya kutoka kwa mkahawa wa Green Park ambapo wengi walikuwa wakifuatilia mtanange huo ulioanza saa tano na robo usiku. “Lakini hata hivyo kushindwa kwetu kulisaidia West Ham kuruka Man United katika jedwali. Tungeshinda mchuano huo Man U wangebakia nafasi ya sita lakini kung’atwa kwetu kulisaidia Mashetani Wekundu kuteremka hadi nafasi ya saba,” akajituliza Bw Simon Ngonjo. Kwa sasa, maombi ya Arsenal ni kuzuke mikosi ya kushindwa kwa timu zote zilizo katika kumi bora katika mechi ya 20 lakini wao washinde ndipo warejee juu ya jedwali na presha ya kutwaa ligi ipungue. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA MWANGI MUIRURI MWANAMUME mmoja wa umri wa miaka 33 aliuawa usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, kwa kupigwa na majirani wa wakwe zake baada ya kile kinadaiwa alijaribu kutekeleza mauaji katika boma hilo alimokuwa amelala na bibi yake. David Kimani alikuwa amesafiri kutoka kijiji cha Kiunyu kilichoko eneobunge la Gatanga kwa msingi kwamba alikuwa na nia ya kumuona mkewe waliyetengana, binti yake wa umri wa miaka sita na pia mama mkwe. Mwanamume huyo alikuwa ametengana na Bi Esther Nyawira, 28, kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu na katika shamrashamra za msimu huu wa sherehe, akafika kwa boma la wakwe Desemba 28, 2023, katika kijiji cha Mung’etho kilichoko eneobunge la Maragua, akisema alienda kuwajulia hali. Lakini hata baada ya giza kuingia, hakuonyesha nia ya kuondoka arejee kwao na ndipo akakubaliwa alale kwa nyumba ya mama mkwe akiwa na bibi huyo wake. Mwendo wa saa sita usiku, Kimani anasemwa kwamba aliamka na akatwaa kisu na akaanza kumshambulia bibi yake aliyekuwa amelala huku kwa sauti akiapa kumuua na kisha aue mama mkwe na pia mtoto. Kwa mujibu wa Kaimu Naibu Kamishna wa Murang’a Kusini Bw Joshua Okello, mwanamume huyo baada ya kujaribu mara kadha warejeane na bibi yake pasipo mafanikio, akaamua kufika katika boma hilo akijipamba kama malaika wa mauti. Aliongeza kwamba mshukiwa alimdunga mwanamke huyo visu vitano “mara moja umbavuni upande wa kulia na mara nne kwa mkono wa kulia, majeraha yote yakiwa matano”. Bw Okello aliongeza kwamba sauti za juu za mwanamume huyo zilimwamusha mama mkwe na alipiga nduru ambayo iliwavutia majirani waliofurika katika boma hilo huku mvamizi baada ya kuingiwa na taharuki akitimua mbio hadi nje ya nyumba na akaingia katika kichaka. “Huku mwaathiriwa akikimbizwa hadi hospitali ya Murang’a kutibiwa, majirani nao walizindua msako ulioishia kumnasa Bw Kimani akiwa amejikunyata ndani ya kichaka hicho na wakamuua kwa kumpiga kwa vifaa butu,” akasema Bw Okello. Afisa huyo aliongeza kwamba ndani ya mkoba ambao marehemu alikuwa nao kulikuwa na sumu ya kuua wadudu kwa mimea na pia waraka wa mauti unaoaminika ulikuwa umeandikwa na mwanamume huyo. “Alikuwa amefichua katika waraka huo kwamba alinuia kuua mama mkwe, bibi yake na mtoto wake wa kike aliyekuwa akiishi kwa wakwe hao na kisha yeye mwenyewe ajitoe uhai,” akasema. Mwanamume huyo alikuwa aidha ameteta kwamba mama mkwe ndiye alikuwa kizingiti cha ndoa yake kupata uthabiti na kwa kuwa hakuwa na nia ya kumpenda mwingine, akaafikia uamuzi wa kuwaua watatu hao na kisha naye ajitume kuzimu akome mahangaiko ya mapenzi. Bw Okello alisema kwamba “huu ni mkasa ambao ungeepukika iwapo mwanamume huyo ambaye alikuwa mfanyabiashara Jijini Nairobi angepata ushauri nasaha ili kuwajibika changamoto zake za kimapenzi ndani ya mashauriano”. Alisema kwamba “ndipo ifike kiwango hicho cha kupanga mauaji ni kumaanisha alikuwa akisaka mbinu ya kusuluhisha changamoto hiyo lakini akaamua kufuata ushawishi wa pepo mbaya kujipa afueni”. Huku akiwakemea waliomuua mwanamume huyo na kuahidi uchunguzi wa kunasa washukiwa, Bw Okello alisema “hata jamii inafaa kuwa macho kuwatambua wanaoonekana kusombwa na mawazo na usaidizi wa ushauri usakwe kabla ya vishawishi vya janga kuzuka”. Bw Okello alionya watu wa kijiji hicho cha Mung’etho kwamba “kwa sasa mnaweza kuwa mnasherehekea mkisema eti ni umati wa raia uliotekeleza mauaji hayo lakini wakati kutajitokeza shahidi aseme alikuona wewe ukishiriki mauaji hayo ndipo utajua ni watu binafsi wala si kundi ambalo huvunja sheria”. “Mchango wa raia katika kuimarisha usalama ni kupitia kutupasha habari kuhusu washukiwa na visa na wakimnasa mshukiwa, kazi yao inafaa tu kutuita tumtie mbaroni au wamwasilishe katika kituo cha polisi kilicho karibu,” akasema Bw Okello. Mwili wa marehemu ulipelekwa hadi mochari ya Murang’a. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA WANDERI KAMAU MUSTAKABALI wa Kanisa Katoliki uko kwenye njia panda barani Afrika, kufuatia agizo la Papa Francis kwa mapadre katika kanisa hilo kubariki wapenzi wa jinsia moja. Ingawa lengo kuu la agizo hilo linaonekana kama njia ya kuwavutia washiriki zaidi na kutowabagua watu hao, wachambuzi na wasomi wa masuala ya dini wanasema huenda agizo hilo lilitolewa bila Papa kupewa ushauri wa kina na uongozi wa kanisa hilo. Kanisa Katoliki lina mamilioni ya washiriki hapa Kenya na barani Afrika kwa jumla. Kulingana na takwimu kutoka kwa serikali, kanisa hilo ndilo linaloongoza kwa kuwa na washiriki wengi nchini, huku likifuatwa na makanisa ya Kiprotestanti. Tangu Papa Francis alipotoa agizo hilo, viongozi tofauti wa kanisa wameeleza na kutoa hisia tofauti, baadhi wakijitokeza wazi kulipinga. Baadhi ya viongozi wakuu ambao wamejitokeza kulipinga ni kiongozi wa kanisa hilo nchini, Askofu Philip Anyolo, ambaye pia ndiye Askofu Mkuu katika Dayosisi ya Nairobi. Kulingana na askofu huyo, agizo hilo linakinzana vikali na tamaduni za Kiafrika, hivyo hawataliruhusu. “Kiafrika, ndoa za jinsia moja hazikubaliki hata kidogo. Ndoa hizo pia zinaenda kinyume na mafunzo ya Biblia,” akasema Askofu Anyolo. Maaskofu wengine ambao wamejitokeza wazi kupinga agizo hilo ni Cornelius Odiwa wa Homa Bay na mwenzake wa dayosisi ya Eldoret, Askofu Dominic Kimengich. Askofu Odiwa alisema watafuata msimamo wa Askofu Anyolo, kwani ndiye kiongozi wa kanisa hilo nchini. Pia, alisema ndoa hizo hazikubaliki kabisa Kiafrika. Kando na viongozi wa Kanisa Katoliki, watu kutoka dini nyingine pia wameunga mkono pingamizi hizo. Baadhi yao ni Bw Samuel Kamitha, ambaye ni mwanahistoria na msomi wa masuala ya dini. Bw Kamitha pia ni mmoja wa waandalizi wakuu wa maombi maalum ambayo hufanyika Desemba 27 kila mwaka karibu na Mlima Kenya. Mnamo Jumatano, wakati wa maombi hayo, Bw Kamitha alisema hawatakubali hata kidogo tamaduni za kigeni kutumika kuharibu desturi asilia za Kiafrika. “Tunasimama kidete kupinga uhalalishaji wa ndoa za jinsia moja nchini. Hilo ni jambo linalokinzana kabisa na tamaduni zetu,” akasema. Maombi hayo yalihudhuriwa na Wakristo, Waislamu, watu wanaofuata dini za kitamaduni kati ya madhehebu mengine. Kutokana na hisia hizo, wasomi wa masuala ya dini wanasema kuwa mwelekeo huo mpya unafaa kuufungua macho uongozi wa Kanisa Katoliki kuhusu mustakabali wake barani Afrika. “Kikawaida, maagizo yote kutoka Vatican (makao makuu ya Kanisa Katoliki) huwa hayapingwi hata kidogo. Ni vigumu kusikia usemi au agizo la Papa likikosolewa au kupingwa. Hata hivyo, viongozi kadhaa wanapojitokeza wazi kupinga agizo lake, basi hiyo ni ishara wazi kuwa kuna tatizo kubwa ambalo lazima litatuliwe,” asema Dkt Rita Khamisi, ambaye ni msomi wa historia ya dini. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA KALUME KAZUNGU SHUGHULI za uchukuzi zimekatizwa katika eneo la Gamba kwenye barabara kuu ya Lamu-Witu-Garsen baada ya maji ya mafuriko kuzagaa katika barabara hiyo mnamo Jumamosi. Mafuriko hayo yamechangiwa na Mto Tana kuvunja kingo zake ghafla kutokana na mvua ya El-Nino inayoendelea kunyesha katika maeneo ya nyanda za juu. Zaidi ya magari 50 ya uchukuzi wa umma, yakiwemo mabasi na matatu na hata magari ya kibinafsi yaliyokuwa yametoka Lamu kuelekea jijini Mombasa, yalilazimika kugeuza safari kurudi na kupakishwa mjini Witu kusubiri iwapo mafuriko yatapungua na kuruhusu safari kuendelea. Mamia ya abiria walisalia wasijue cha kufanya baada ya kushuhudia mafuriko hayo, hasa katika eneo ambalo hawakudhania yangeweza kutokea. “Nilikuwa nimerauka kuabiri gari kuelekea mjini Mombasa kumuona daktari. Nilifaa nimuone saa nane na sasa bado nipo hapa Witu kusubiri hali ya kawaida kurejea katika barabara hiyo. Hii inamaanisha kuwa miadi yangu na daktari haitawezekana leo wala kesho kwani sijui maji yatapungua saa ngapi ili kuruhusu safari yetu kuendelea,” akasema Bi Betty Waweru. Naye Bi Halima Abdallah anasema alikuwa akisafiri kuelekea mjini Malindi kwa hafla ya harusi ya mtoto wa dadake. Anasema hana la kufanya kwa sasa kwani safari yake imekatizwa kutokana na mafuriko yaliyosomba barabara eneo la Gamba. “Sijakula tangu niamke. Nimeraukia safari nikijua fika kwamba kufikia saa tano asubuhi ningekuwa mjini Malindi. Ni masikitiko kwamba safari imekatizwa. Sina senti za matumizi kula hapa mjini Witu ambapo magari yamepakiwa kusubiri mafuriko yapungue. Allah (Mungu) atusaidie,” akasema Bi Abdallah. Katika kituo cha polisi cha Gamba, maji pia yalikuwa yameanza kufikia baadhi ya nyumba za polisi kuishi. Si mara ya kwanza kwa kituo cha polisi cha Gamba kuathiriwa na mafuriko kila wakati mvua iliyopitiliza inaposhuhudiwa nchini. Mmoja wa makondakta wa mabasi ya usafiri wa umma, Bw Said Swaleh alisema yeye pia amelazimika kusalia mjini Witu na makumi ya abiria wake baada ya basi lao kushindwa kuvuka eneo la Gamba kutokana na mafuriko hayo. “Tumegeuza gari kurudi mjini Witu. Barabara haivukiki eneo la Gamba. Maji yametapakaa kila mahali na ni hatari kwetu kuvukisha gari. Twasubiri hadi mafuriko yapungue,” akasema Bw Swaleh. Hali ilikuwa ile ile kwa wahudumu wa uchukuzi kutoka Malindi na Mombasa wakielekea Lamu kwani walilazimika kugeuza magari yao na kuyapakisha eneo la Minjila baada ya kushuhudia mafuriko eneo hilo la Gamba. “Wa kutoka Lamu kuelekea Mombasa na yule wa Mombasa kuelekea Lamu, wote hawawezi kuvuka kutoka Gamba na kufululiza kwa safari zao. Hali ni mbaya hapa. Maji yamefurika kwelikweli eneo hili na ni hatari kwetu kuyavuka,” akasema Bw Paul Kariuki ambaye ni dereva wa probox. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA KALUME KAZUNGU SHUGHULI za uchukuzi zimekatizwa katika eneo la Gamba kwenye barabara kuu ya Lamu-Witu-Garsen baada ya maji ya mafuriko kuzagaa katika barabara hiyo mnamo Jumamosi. Mafuriko hayo yamechangiwa na Mto Tana kuvunja kingo zake ghafla kutokana na mvua ya El-Nino inayoendelea kunyesha katika maeneo ya nyanda za juu. Zaidi ya magari 50 ya uchukuzi wa umma, yakiwemo mabasi na matatu na hata magari ya kibinafsi yaliyokuwa yametoka Lamu kuelekea jijini Mombasa, yalilazimika kugeuza safari kurudi na kupakishwa mjini Witu kusubiri iwapo mafuriko yatapungua na kuruhusu safari kuendelea. Mamia ya abiria walisalia wasijue cha kufanya baada ya kushuhudia mafuriko hayo, hasa katika eneo ambalo hawakudhania yangeweza kutokea. “Nilikuwa nimerauka kuabiri gari kuelekea mjini Mombasa kumuona daktari. Nilifaa nimuone saa nane na sasa bado nipo hapa Witu kusubiri hali ya kawaida kurejea katika barabara hiyo. Hii inamaanisha kuwa miadi yangu na daktari haitawezekana leo wala kesho kwani sijui maji yatapungua saa ngapi ili kuruhusu safari yetu kuendelea,” akasema Bi Betty Waweru. Naye Bi Halima Abdallah anasema alikuwa akisafiri kuelekea mjini Malindi kwa hafla ya harusi ya mtoto wa dadake. Anasema hana la kufanya kwa sasa kwani safari yake imekatizwa kutokana na mafuriko yaliyosomba barabara eneo la Gamba. “Sijakula tangu niamke. Nimeraukia safari nikijua fika kwamba kufikia saa tano asubuhi ningekuwa mjini Malindi. Ni masikitiko kwamba safari imekatizwa. Sina senti za matumizi kula hapa mjini Witu ambapo magari yamepakiwa kusubiri mafuriko yapungue. Allah (Mungu) atusaidie,” akasema Bi Abdallah. Katika kituo cha polisi cha Gamba, maji pia yalikuwa yameanza kufikia baadhi ya nyumba za polisi kuishi. Si mara ya kwanza kwa kituo cha polisi cha Gamba kuathiriwa na mafuriko kila wakati mvua iliyopitiliza inaposhuhudiwa nchini. Mmoja wa makondakta wa mabasi ya usafiri wa umma, Bw Said Swaleh alisema yeye pia amelazimika kusalia mjini Witu na makumi ya abiria wake baada ya basi lao kushindwa kuvuka eneo la Gamba kutokana na mafuriko hayo. “Tumegeuza gari kurudi mjini Witu. Barabara haivukiki eneo la Gamba. Maji yametapakaa kila mahali na ni hatari kwetu kuvukisha gari. Twasubiri hadi mafuriko yapungue,” akasema Bw Swaleh. Hali ilikuwa ile ile kwa wahudumu wa uchukuzi kutoka Malindi na Mombasa wakielekea Lamu kwani walilazimika kugeuza magari yao na kuyapakisha eneo la Minjila baada ya kushuhudia mafuriko eneo hilo la Gamba. “Wa kutoka Lamu kuelekea Mombasa na yule wa Mombasa kuelekea Lamu, wote hawawezi kuvuka kutoka Gamba na kufululiza kwa safari zao. Hali ni mbaya hapa. Maji yamefurika kwelikweli eneo hili na ni hatari kwetu kuyavuka,” akasema Bw Paul Kariuki ambaye ni dereva wa probox. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA MERCY KOSKEI WAKAZI wa kijiji cha Bagaria kilichoko eneobunge la Njoro katika Kaunti ya Nakuru wanaishi na wasiwasi baada ya kupata kipande cha jeneza kikiwa kimetupwa barabarani. Wakazi hao kwa sasa wanaishi kwa hofu huku wakiamini jeneza hilo lililoondolewa katika kaburi lililofukuliwa na watu wasiojulikana, ni la Rose Njeri ambaye alizikwa Septemba alipoaga dunia baada ya kuugua saratani. Mama huyo wa watoto wawili aliaga dunia mnamo Septemba 2023 akiwa na umri wa miaka 61. Alizikwa katika shamba lake la ekari tatu. Kulingana na binti ya marehemu Bi Esther Wanjiru, aliondoka kuelekea shambani Jumanne asubuhi na dadake mkubwa walipogundua kuwa kaburi la mama yao lilikuwa limeharibiwa. Anasema kuwa waliposogea karibu, walibaini kuwa watu wasiojulikana walikuwa wamehitilafiana na kaburi hilo, huku mchanga ukionyesha kuwa lilikuwa limechimbwa upya. Aidha, hapo kulikuwa na alama za miguu. Kulingana na Bi Wanjiru, baada ya kupumzisha mama yao, familia ilizingira kaburi hilo na uzio wa mbao lakini mbao zenyewe zilikuwa zimeondolewa na vipande kutupwa mita chache kutoka kwenye kaburi hilo. “Huwa tunafika hapa kuangalia mazao yetu, lakini Jumanne tulibaini jambo lisilo la kawaida. Kaburi lilionekana kuwa limevurugwa. Tulishtuka tusijue la kufanya. Tulimwarifu shangazi ambaye alitushauri kuondoka na kutoa taarifa kwa chifu,” akaeleza Bi Wanjiru. Aliongeza kwamba baada ya kumfahamisha chifu wa eneo hilo, aliwashauri kuripoti kisa hicho katika Kituo cha Polisi cha Naishi. Hata hivyo, siku mbili baadaye, wakazi walipata vipande vya jeneza kando ya barabara, jambo ambalo liliipa familia wasiwasi na kuwaacha na maswali iwapo jamaa yao alifukuliwa na mwili kutupwa kwingineko. Jioni sehemu nyingine ilipatikana mita chache karibu na mto. Kulingana na Bi Wanjiru, mamake alinunua shamba hilo miaka michache iliyopita na kufichua kuwa hakuna mgogoro kwani wana hati miliki. “Hatukulala usiku, hatujui ikiwa baada ya kufukua waliuchukua mwili huo na kuutupa mtoni au ikiwa tutaamka na kukuta mabaki ya mama yetu mlangoni au hata kando ya barabara,” alisema. Dadake marehemu, Florence Wambui alisema kuwa aliarifiwa na mpwa wake kuwa kaburi la mama yao lilikuwa na dalili za kufukuliwa. Alisema kuwa aliwashauri watoe taarifa kwa Polisi hili waazishe uchunguzi. Kulingana na Wambui, dadake amekuwa akiugua kwa miaka mingi. Mnamo Aprili alikimbizwa katika Hospitali ya Kenyatta baada ya hali yake kuwa mbaya na kulazwa hospitalini kwa miezi sita.Alifariki Septemba 9,2023. Alisema kuwa familia ililazimika kuweka hati miliki ili waruhusiwe kuchukua mwili baada ya kuacha biili kubwa ya matibabu. ‘Tuliumia roho alipoaga dunia, hata hivyo tulilazimika kumwacha apumzike baada ya kuugua kwa muda mrefu. Lakini sasa wamefungua kidonda hicho, hatuna amani kwani kaburi lake limechezewa. Hatujui ikiwa mabaki yake yapo au waliichukua,” alisema. Familia hiyo ilisema kuwa wanatakiwa kutoa Sh75, 000 ili kupata agizo la mahakama kabla ya kufukuliwa ili kubaini ikiwa mwili huo uko. Chifu wa eneo hilo Bw David Githiga alisema kuwa baada ya Bi Njoki kufariki, aliipatia familia hiyo kibali cha kuzika. Alisema kuwa mnamo Jumanne, familia ilimjulisha kuhusu matukio hayo na wanasubiri amri ya mahakama kabla ya kufukuliwa. “Kwa kuwa hawakuupata mwili huo Jumanne, walishauriwa kusubiri uchunguzi. Lakini baada ya kupata sehemu ya jeneza, sasa maswali tele yameibuka. Hatujawahi kushuhudia kitu kama hiki, ni ajabu. Hakuna kitakachofanyika hadi amri ya mahakama itolewe,” alibainisha. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA MERCY KOSKEI WAKAZI wa kijiji cha Bagaria kilichoko eneobunge la Njoro katika Kaunti ya Nakuru wanaishi na wasiwasi baada ya kupata kipande cha jeneza kikiwa kimetupwa barabarani. Wakazi hao kwa sasa wanaishi kwa hofu huku wakiamini jeneza hilo lililoondolewa katika kaburi lililofukuliwa na watu wasiojulikana, ni la Rose Njeri ambaye alizikwa Septemba alipoaga dunia baada ya kuugua saratani. Mama huyo wa watoto wawili aliaga dunia mnamo Septemba 2023 akiwa na umri wa miaka 61. Alizikwa katika shamba lake la ekari tatu. Kulingana na binti ya marehemu Bi Esther Wanjiru, aliondoka kuelekea shambani Jumanne asubuhi na dadake mkubwa walipogundua kuwa kaburi la mama yao lilikuwa limeharibiwa. Anasema kuwa waliposogea karibu, walibaini kuwa watu wasiojulikana walikuwa wamehitilafiana na kaburi hilo, huku mchanga ukionyesha kuwa lilikuwa limechimbwa upya. Aidha, hapo kulikuwa na alama za miguu. Kulingana na Bi Wanjiru, baada ya kupumzisha mama yao, familia ilizingira kaburi hilo na uzio wa mbao lakini mbao zenyewe zilikuwa zimeondolewa na vipande kutupwa mita chache kutoka kwenye kaburi hilo. “Huwa tunafika hapa kuangalia mazao yetu, lakini Jumanne tulibaini jambo lisilo la kawaida. Kaburi lilionekana kuwa limevurugwa. Tulishtuka tusijue la kufanya. Tulimwarifu shangazi ambaye alitushauri kuondoka na kutoa taarifa kwa chifu,” akaeleza Bi Wanjiru. Aliongeza kwamba baada ya kumfahamisha chifu wa eneo hilo, aliwashauri kuripoti kisa hicho katika Kituo cha Polisi cha Naishi. Hata hivyo, siku mbili baadaye, wakazi walipata vipande vya jeneza kando ya barabara, jambo ambalo liliipa familia wasiwasi na kuwaacha na maswali iwapo jamaa yao alifukuliwa na mwili kutupwa kwingineko. Jioni sehemu nyingine ilipatikana mita chache karibu na mto. Kulingana na Bi Wanjiru, mamake alinunua shamba hilo miaka michache iliyopita na kufichua kuwa hakuna mgogoro kwani wana hati miliki. “Hatukulala usiku, hatujui ikiwa baada ya kufukua waliuchukua mwili huo na kuutupa mtoni au ikiwa tutaamka na kukuta mabaki ya mama yetu mlangoni au hata kando ya barabara,” alisema. Dadake marehemu, Florence Wambui alisema kuwa aliarifiwa na mpwa wake kuwa kaburi la mama yao lilikuwa na dalili za kufukuliwa. Alisema kuwa aliwashauri watoe taarifa kwa Polisi hili waazishe uchunguzi. Kulingana na Wambui, dadake amekuwa akiugua kwa miaka mingi. Mnamo Aprili alikimbizwa katika Hospitali ya Kenyatta baada ya hali yake kuwa mbaya na kulazwa hospitalini kwa miezi sita.Alifariki Septemba 9,2023. Alisema kuwa familia ililazimika kuweka hati miliki ili waruhusiwe kuchukua mwili baada ya kuacha biili kubwa ya matibabu. ‘Tuliumia roho alipoaga dunia, hata hivyo tulilazimika kumwacha apumzike baada ya kuugua kwa muda mrefu. Lakini sasa wamefungua kidonda hicho, hatuna amani kwani kaburi lake limechezewa. Hatujui ikiwa mabaki yake yapo au waliichukua,” alisema. Familia hiyo ilisema kuwa wanatakiwa kutoa Sh75, 000 ili kupata agizo la mahakama kabla ya kufukuliwa ili kubaini ikiwa mwili huo uko. Chifu wa eneo hilo Bw David Githiga alisema kuwa baada ya Bi Njoki kufariki, aliipatia familia hiyo kibali cha kuzika. Alisema kuwa mnamo Jumanne, familia ilimjulisha kuhusu matukio hayo na wanasubiri amri ya mahakama kabla ya kufukuliwa. “Kwa kuwa hawakuupata mwili huo Jumanne, walishauriwa kusubiri uchunguzi. Lakini baada ya kupata sehemu ya jeneza, sasa maswali tele yameibuka. Hatujawahi kushuhudia kitu kama hiki, ni ajabu. Hakuna kitakachofanyika hadi amri ya mahakama itolewe,” alibainisha. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA SHABAN MAKOKHA KIONGOZI wa Upinzani Raila Odinga amesema changamoto zinazoikumba serikali ya Kenya Kwanza ni kwa sababu imesakamwa na kile alichodai ni ‘kumuibia’ ushindi wake katika kura za 2022. Bw Odinga ambaye alikuwa katika hafla ya kusajili wanachama wapya wa chama chake cha ODM Ijumaa Desemba 1, 2023 katika Kaunti ya Kakamega alishikilia kwamba yeye ndiye aliyeshinda urais dhidi ya Rais wa sasa William Ruto. Kura ya urais ilifanyiwa uamuzi wa mwisho katika Mahakama ya Upeo ambapo ilishikilia kwamba Dkt Ruto alichaguliwa kwa kura 7.1 milioni njia halali, dhidi ya Bw Odinga 6.9 milioni, katika uamuzi ulioungwa mkono na majaji wote wa mahakama hiyo mwaka jana. Hata hivyo, mrengo wa Azimio la Umoja ambao ndio Bw Odinga aliotumia kuwania urais akiwa na mgombea mwenza Martha Karua umeshikilia hadi leo kwamba walinyimwa ushindi (kwa mara nyingine). Ni kauli ambayo Bw Odinga alirejelea akiwa mbele ya umati, eneo la Lurambi, Ijumaa: “Sasa, unajua waliiba kura yetu. Si waliiba?” Umati: “Ndio baba” Raila: “Hata kama waliiba, imekwama kwa koo. Imekataa kuteremka. Wanatafuna lakini haiteremki. Wanafanya ..ehe..ehee..ehee” Umati: [Kicheko] Raila: “Inawanyonga. Si inawanyonga?” Umati: [Kicheko] “Ndio baba” Aliendelea na hotuba akielezea kwa nini ameanza mapema usajili wa wanachama, akifafanua kwamba huu ndio wakati mwafaka, ambao wananchi tayari wameshapoa kutokana na mishemishe za uchaguzi. Akasema kwamba ameona heri kuanza zoezi la usajili akidai kwamba kuna hatari ya mabwanyenye kumwaga pesa nyingi dakika za mwisho mwisho na kuzuga akili wapiga kura. Katika hafla hiyo hiyo, kiongozi huyo wa Azimio ambaye amewania urais kwa mara tano bila kufanikiwa alisalia kimya pale viongozi wa ODM walipomtaka atangaze kwamba atawania tena 2027. Viongozi wa chama hicho katika kaunti ya Kakamega walitangaza kuwa Bw Odinga ndiye chaguo lao katika kinyang’anyiro kijacho cha urais wakisema ndiye anaweza kurekebisha makosa ya utawala huu wa Rais William Ruto. Waliisuta serikali hii kwa kuuboronga uchumi kupitia kile walichokitaja kama uporaji wa mali ya umma. Wakiongozwa na Gavana wa Kakamega, Fernandes Barasa, viongozi hao, wakiwemo Naibu Gavana Ayub Savula na wabunge Tindi Mwale, walimtaka Bw Odinga kutoachia mtu mwingine kibarua cha kung’oa mamlakani Rais Ruto. Walitaja ongezeko la bei za bidhaa za kimsingi kama chakula na mafuta, ubomoaji wa majengo ya kibinafsi na kukithiri kwa ufisadi kama mapungufu ya utawala wa Rais Ruto. -Ripoti ya ziada na uhariri – FATUMA BARIKI You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA SHABAN MAKOKHA KIONGOZI wa Upinzani Raila Odinga amesema changamoto zinazoikumba serikali ya Kenya Kwanza ni kwa sababu imesakamwa na kile alichodai ni ‘kumuibia’ ushindi wake katika kura za 2022. Bw Odinga ambaye alikuwa katika hafla ya kusajili wanachama wapya wa chama chake cha ODM Ijumaa Desemba 1, 2023 katika Kaunti ya Kakamega alishikilia kwamba yeye ndiye aliyeshinda urais dhidi ya Rais wa sasa William Ruto. Kura ya urais ilifanyiwa uamuzi wa mwisho katika Mahakama ya Upeo ambapo ilishikilia kwamba Dkt Ruto alichaguliwa kwa kura 7.1 milioni njia halali, dhidi ya Bw Odinga 6.9 milioni, katika uamuzi ulioungwa mkono na majaji wote wa mahakama hiyo mwaka jana. Hata hivyo, mrengo wa Azimio la Umoja ambao ndio Bw Odinga aliotumia kuwania urais akiwa na mgombea mwenza Martha Karua umeshikilia hadi leo kwamba walinyimwa ushindi (kwa mara nyingine). Ni kauli ambayo Bw Odinga alirejelea akiwa mbele ya umati, eneo la Lurambi, Ijumaa: “Sasa, unajua waliiba kura yetu. Si waliiba?” Umati: “Ndio baba” Raila: “Hata kama waliiba, imekwama kwa koo. Imekataa kuteremka. Wanatafuna lakini haiteremki. Wanafanya ..ehe..ehee..ehee” Umati: [Kicheko] Raila: “Inawanyonga. Si inawanyonga?” Umati: [Kicheko] “Ndio baba” Aliendelea na hotuba akielezea kwa nini ameanza mapema usajili wa wanachama, akifafanua kwamba huu ndio wakati mwafaka, ambao wananchi tayari wameshapoa kutokana na mishemishe za uchaguzi. Akasema kwamba ameona heri kuanza zoezi la usajili akidai kwamba kuna hatari ya mabwanyenye kumwaga pesa nyingi dakika za mwisho mwisho na kuzuga akili wapiga kura. Katika hafla hiyo hiyo, kiongozi huyo wa Azimio ambaye amewania urais kwa mara tano bila kufanikiwa alisalia kimya pale viongozi wa ODM walipomtaka atangaze kwamba atawania tena 2027. Viongozi wa chama hicho katika kaunti ya Kakamega walitangaza kuwa Bw Odinga ndiye chaguo lao katika kinyang’anyiro kijacho cha urais wakisema ndiye anaweza kurekebisha makosa ya utawala huu wa Rais William Ruto. Waliisuta serikali hii kwa kuuboronga uchumi kupitia kile walichokitaja kama uporaji wa mali ya umma. Wakiongozwa na Gavana wa Kakamega, Fernandes Barasa, viongozi hao, wakiwemo Naibu Gavana Ayub Savula na wabunge Tindi Mwale, walimtaka Bw Odinga kutoachia mtu mwingine kibarua cha kung’oa mamlakani Rais Ruto. Walitaja ongezeko la bei za bidhaa za kimsingi kama chakula na mafuta, ubomoaji wa majengo ya kibinafsi na kukithiri kwa ufisadi kama mapungufu ya utawala wa Rais Ruto. -Ripoti ya ziada na uhariri – FATUMA BARIKI You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA ALEX KALAMA Mhubiri tatanishi Paul Mackenzie wa Kanisa la Good News International mnamo Ijumaa amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja bila faini, baada ya kupatikana na hatia ya kutumia filamu ambazo hazijaidhinishwa na bodi ya filamu nchini, kuendesha mahubiri yake kanisani. Filamu hizo zinasemekana kuchochea watoto kususia masomo, na hata wazazi kugoma kuwapeleka wana wao shuleni. Mahakama ya Malindi ilimkuta na hatia ya kukiuka sheria za uainishaji na usambazaji wa filamu. Mackenzie mwezi uliopita alipatikana na hatia ya shtaka la kumiliki na kusambaza filamu kwa umma ambazo hazijachunguzwa na kuainishwa na Bodi ya Uainishaji wa Filamu nchini (KFCB) kinyume na kifungu cha 12 cha Sheria ya Filamu na Jukwaa kwa kuendesha filamu na studio bila leseni. Awali, Hakimu Mkazi wa Malindi Onalo Olga alikuwa amesema upande wa mashtaka ulithibitisha bila shaka yoyote mashtaka mawili ya kumiliki filamu ambazo hazijaainishwa, na kuendesha studio ya kurekodia filamu bila leseni zaidi ya shaka. “Mshukiwa amepatikana na hatia kwa mashtaka mawili ya kumiliki na kusambaza filamu kwa umma ambazo hazijachunguzwa na kuainishwa na Bodi ya Uainishaji wa Filamu Nchini (KFCB) na kuendesha studio ya kurekodi filamu na kutengeneza filamu bila leseni halali,” alisema hakimu. Hakimu huyo hata hivyo alimuachiliaa huru Mackenzie katika shtaka la kwanza ambapo alishtakiwa kwa kuchochea umma kukiuka sheria. Hapa, serikali ilidai kuwa Mackenzie alichochea watoto dhidi ya kuhudhuria shule na kutumia zaidi filamu hizo kuwachochea watu dhidi ya Wahindu, Wabudha, na Waislamu. “Upande wa mashtaka haujathibitisha shtaka hilo kwa kiwango kinachotakiwa kisheria, hivyo basi mshukiwa ameachiliwa kwa kosa la kwanza la uchochezi wa uvunjaji wa sheria,” alisema hakimu huyo. Mackenzie alikuwa amejitetea kwamba hajawahi kusababisha migogoro kati ya dini kupitia mahubiri yake, ambayo alisema yalilenga ujumbe wa nyakati za mwisho kwa wafuasi wake na wale waliojali kusikiliza. “Yaliyomo katika kanda ya DVD yalikuwa maudhui ya wachungaji na makanisa mbalimbali duniani kote. Nilikuwa na kituo cha runinga cha Kanisa la Good News International Church lakini upande wa mashtaka haukuleta ushahidi kuonyesha kuwa vidio zilizofikishwa mahakamani zilipeperushwa na kituo cha runinga cha Times,” alisema. Mackenzie aliiambia mahakama kuwa anafahamu kuwa jumbe zake za nyakati za mwisho ziko kwenye chaneli ya YouTube inayoitwa Times Tv na kwamba yeye ndiye alizipakia huko ili kuwasilisha mafundisho yake. Hata hivyo, mahakama ilisema kuwa serikali kupitia kwa Kiongozi wa Mashtaka Joseph Mwangi ilithibitisha kesi dhidi ya Mackenzie bila shaka yoyote. Hakimu alibaini kuwa Mackenzie alishindwa kujiondoa kutoka kwa ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashtaka na vielelezo vikiwemo kanda za video akitoa mahubiri hayo makali. Pia, mahakama iliona kuwa Mackenzie alikiri kuwa Televisheni ya Times ilikuwa ya kanisa lake, ambapo filamu za DVD zenye mahubiri ya wakati wa mwisho zilipatikana ofisini kwake. Akitoa huku mnamo Ijumaa, Hakimu Onalo alisema mhubiri atatumikia kifungo cha miezi 12 gerezani bila faini. Inadaiwa kuwa Mackenzie alirekodi filamu hizo kati ya Januari na Aprili 2019 katika kanisa lake lililoko eneo la Furunzi mjini Malindi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA ALEX KALAMA Mhubiri tatanishi Paul Mackenzie wa Kanisa la Good News International mnamo Ijumaa amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja bila faini, baada ya kupatikana na hatia ya kutumia filamu ambazo hazijaidhinishwa na bodi ya filamu nchini, kuendesha mahubiri yake kanisani. Filamu hizo zinasemekana kuchochea watoto kususia masomo, na hata wazazi kugoma kuwapeleka wana wao shuleni. Mahakama ya Malindi ilimkuta na hatia ya kukiuka sheria za uainishaji na usambazaji wa filamu. Mackenzie mwezi uliopita alipatikana na hatia ya shtaka la kumiliki na kusambaza filamu kwa umma ambazo hazijachunguzwa na kuainishwa na Bodi ya Uainishaji wa Filamu nchini (KFCB) kinyume na kifungu cha 12 cha Sheria ya Filamu na Jukwaa kwa kuendesha filamu na studio bila leseni. Awali, Hakimu Mkazi wa Malindi Onalo Olga alikuwa amesema upande wa mashtaka ulithibitisha bila shaka yoyote mashtaka mawili ya kumiliki filamu ambazo hazijaainishwa, na kuendesha studio ya kurekodia filamu bila leseni zaidi ya shaka. “Mshukiwa amepatikana na hatia kwa mashtaka mawili ya kumiliki na kusambaza filamu kwa umma ambazo hazijachunguzwa na kuainishwa na Bodi ya Uainishaji wa Filamu Nchini (KFCB) na kuendesha studio ya kurekodi filamu na kutengeneza filamu bila leseni halali,” alisema hakimu. Hakimu huyo hata hivyo alimuachiliaa huru Mackenzie katika shtaka la kwanza ambapo alishtakiwa kwa kuchochea umma kukiuka sheria. Hapa, serikali ilidai kuwa Mackenzie alichochea watoto dhidi ya kuhudhuria shule na kutumia zaidi filamu hizo kuwachochea watu dhidi ya Wahindu, Wabudha, na Waislamu. “Upande wa mashtaka haujathibitisha shtaka hilo kwa kiwango kinachotakiwa kisheria, hivyo basi mshukiwa ameachiliwa kwa kosa la kwanza la uchochezi wa uvunjaji wa sheria,” alisema hakimu huyo. Mackenzie alikuwa amejitetea kwamba hajawahi kusababisha migogoro kati ya dini kupitia mahubiri yake, ambayo alisema yalilenga ujumbe wa nyakati za mwisho kwa wafuasi wake na wale waliojali kusikiliza. “Yaliyomo katika kanda ya DVD yalikuwa maudhui ya wachungaji na makanisa mbalimbali duniani kote. Nilikuwa na kituo cha runinga cha Kanisa la Good News International Church lakini upande wa mashtaka haukuleta ushahidi kuonyesha kuwa vidio zilizofikishwa mahakamani zilipeperushwa na kituo cha runinga cha Times,” alisema. Mackenzie aliiambia mahakama kuwa anafahamu kuwa jumbe zake za nyakati za mwisho ziko kwenye chaneli ya YouTube inayoitwa Times Tv na kwamba yeye ndiye alizipakia huko ili kuwasilisha mafundisho yake. Hata hivyo, mahakama ilisema kuwa serikali kupitia kwa Kiongozi wa Mashtaka Joseph Mwangi ilithibitisha kesi dhidi ya Mackenzie bila shaka yoyote. Hakimu alibaini kuwa Mackenzie alishindwa kujiondoa kutoka kwa ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashtaka na vielelezo vikiwemo kanda za video akitoa mahubiri hayo makali. Pia, mahakama iliona kuwa Mackenzie alikiri kuwa Televisheni ya Times ilikuwa ya kanisa lake, ambapo filamu za DVD zenye mahubiri ya wakati wa mwisho zilipatikana ofisini kwake. Akitoa huku mnamo Ijumaa, Hakimu Onalo alisema mhubiri atatumikia kifungo cha miezi 12 gerezani bila faini. Inadaiwa kuwa Mackenzie alirekodi filamu hizo kati ya Januari na Aprili 2019 katika kanisa lake lililoko eneo la Furunzi mjini Malindi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA AFP ISRAEL, JERUSALEM JESHI la Israeli limeanza tena mapigano Gaza, huku mashambulizi ya anga na risasi yakiripotiwa katika mji wa Gaza. Haya yanajiri wakati ambapo muda wa makubaliano ya kusitisha mapigano hayo ukifika mwisho. “Kundi la Hamas halikutii makubaliano yetu. Hii ndio maana vikosi vya Ulinzi vya Israeli vimeanza tena mapambano dhidi ya kundi hilo la kigaidi katika Ukanda wa Gaza,” jeshi la Israeli lilisema. Tangazo hilo limejiri muda mfupi baada ya jeshi kusema kuwa limenasa roketi iliyorushwa kutoka Gaza, ikiwa ni ya kwanza kutoka eneo hilo tangu kombora liliporushwa dakika chache kabla ya siku ya kwanza ya kusitisha mapigano. Ndani ya Gaza, mwandishi wa habari wa AFP alisema ndege za kivita za Israeli zilifanya mashambulizi, na kuripoti ufyatuaji wa mizinga katika mji wa Gaza. Ndege zisizo na rubani pia ziliweza kusikika angani kusini mwa eneo hilo kwa mara ya kwanza tangu kusitishwa kwa makubaliano hayo, mwandishi wa AFP katika eneo hilo alisema. Kuanza tena kwa mapigano kulikatisha matumaini ya kurefushwa kwa mapatano ya siku saba ambayo yamewafanya mateka kadhaa kuachiliwa huru. Makubaliano hayo pia yaliruhusu msaada zaidi kuingia katika eneo lililoharibiwa la Ukanda wa Gaza. Siku ya Alhamisi, mwanadiplomasia mkuu wa Amerika, Antony Blinken, alikutana na maafisa wa Israeli na Palestina, na kutoa wito wa kusitishwa kwa mapigano hayo kuongezwa. Kando na hayo, alionya kuw ikiwa mapigano hayo yataanzishwa tena, basi raia wanafaa kulindwa. Wakati wa mapatano yaliyosimamiwa na Qatar, mateka 80 wa Israeli waliachiliwa na pia wafungwa 240 wa Kipalestina. Zaidi ya wageni 20, pia waliachiliwa. Waisraeli sita zaidi, wengine wakiwa na uraia wa nchi mbili, waliachiliwa, saa chache baada ya wanawake wawili kuachiliwa. Hilo lilifanya jumla ya walioachiliwa Alhamisi kufikia wanane, badala ya mateka 10 kwa siku. Chanzo kilicho karibu na kundi hilo la wanamgambo kilisema kinawahesabu wanawake wawili wa Urusi-Israeli walioachiliwa Jumatano kama sehemu ya kundi la saba. Kuachiliwa huko kulileta afueni kwa Keren Shem, ambaye binti yake Mia alikuwa miongoni mwa wale walioachiliwa. Wakati uo huo, Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu alisema alimuagiza waziri wake wa mambo ya nje, Eli Cohen, kumwita balozi wa Uhispania ili kutoa karipio. Hii ni kufuatia kauli ya aibu ya waziri mkuu wa Uhispania katika siku ambayo magaidi wa Hamas walipowauwa Waisraeli katika mji wa Jerusalem. Wapiganaji wawili wa kundi la Hamas waliwaua raia watatu katika kituo cha mabasi cha Jerusalem asubuhi siku ya Alhamisi. Kundi hilo la Palestina lina ngome yake katika Ukanda wa Gaza, ambako lilianzisha mashambulio ya Oktoba 7 nchini Israeli, na kusababisha vita. |
Tags |
You can share this post! |
Previous article |
Mawaidha ya Kiislamu: Tuthibitishe tunamhusudu Mungu... |
Next article |
Mhubiri Paul Mackenzie sasa asukumwa jela mwaka mzima |
T L |
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved |
NA AFP ISRAEL, JERUSALEM JESHI la Israeli limeanza tena mapigano Gaza, huku mashambulizi ya anga na risasi yakiripotiwa katika mji wa Gaza. Haya yanajiri wakati ambapo muda wa makubaliano ya kusitisha mapigano hayo ukifika mwisho. “Kundi la Hamas halikutii makubaliano yetu. Hii ndio maana vikosi vya Ulinzi vya Israeli vimeanza tena mapambano dhidi ya kundi hilo la kigaidi katika Ukanda wa Gaza,” jeshi la Israeli lilisema. Tangazo hilo limejiri muda mfupi baada ya jeshi kusema kuwa limenasa roketi iliyorushwa kutoka Gaza, ikiwa ni ya kwanza kutoka eneo hilo tangu kombora liliporushwa dakika chache kabla ya siku ya kwanza ya kusitisha mapigano. Ndani ya Gaza, mwandishi wa habari wa AFP alisema ndege za kivita za Israeli zilifanya mashambulizi, na kuripoti ufyatuaji wa mizinga katika mji wa Gaza. Ndege zisizo na rubani pia ziliweza kusikika angani kusini mwa eneo hilo kwa mara ya kwanza tangu kusitishwa kwa makubaliano hayo, mwandishi wa AFP katika eneo hilo alisema. Kuanza tena kwa mapigano kulikatisha matumaini ya kurefushwa kwa mapatano ya siku saba ambayo yamewafanya mateka kadhaa kuachiliwa huru. Makubaliano hayo pia yaliruhusu msaada zaidi kuingia katika eneo lililoharibiwa la Ukanda wa Gaza. Siku ya Alhamisi, mwanadiplomasia mkuu wa Amerika, Antony Blinken, alikutana na maafisa wa Israeli na Palestina, na kutoa wito wa kusitishwa kwa mapigano hayo kuongezwa. Kando na hayo, alionya kuw ikiwa mapigano hayo yataanzishwa tena, basi raia wanafaa kulindwa. Wakati wa mapatano yaliyosimamiwa na Qatar, mateka 80 wa Israeli waliachiliwa na pia wafungwa 240 wa Kipalestina. Zaidi ya wageni 20, pia waliachiliwa. Waisraeli sita zaidi, wengine wakiwa na uraia wa nchi mbili, waliachiliwa, saa chache baada ya wanawake wawili kuachiliwa. Hilo lilifanya jumla ya walioachiliwa Alhamisi kufikia wanane, badala ya mateka 10 kwa siku. Chanzo kilicho karibu na kundi hilo la wanamgambo kilisema kinawahesabu wanawake wawili wa Urusi-Israeli walioachiliwa Jumatano kama sehemu ya kundi la saba. Kuachiliwa huko kulileta afueni kwa Keren Shem, ambaye binti yake Mia alikuwa miongoni mwa wale walioachiliwa. Wakati uo huo, Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu alisema alimuagiza waziri wake wa mambo ya nje, Eli Cohen, kumwita balozi wa Uhispania ili kutoa karipio. Hii ni kufuatia kauli ya aibu ya waziri mkuu wa Uhispania katika siku ambayo magaidi wa Hamas walipowauwa Waisraeli katika mji wa Jerusalem. Wapiganaji wawili wa kundi la Hamas waliwaua raia watatu katika kituo cha mabasi cha Jerusalem asubuhi siku ya Alhamisi. Kundi hilo la Palestina lina ngome yake katika Ukanda wa Gaza, ambako lilianzisha mashambulio ya Oktoba 7 nchini Israeli, na kusababisha vita. |
Subsets and Splits
No saved queries yet
Save your SQL queries to embed, download, and access them later. Queries will appear here once saved.