text
stringlengths
3
16.2k
GAVANA Anne Waiguru wa Kirinyaga yupo kwenye njiapanda kuhusu mwelekeo wa kisiasa atakaofuata, uchaguzi mkuu wa 2022... Na CHARLES WASONGA
MASWALI mengi yameibuliwa kuhusu sababu ya kushirikishwa kwa Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya katika mikutano... Na WANDERI KAMAU
NI kinaya kuwa Bw Mwangi Kiunjuri na Bw Moses Kuria ndio wanaoongoza harakati za kushinikiza muungano wa kisiasa... Na BENSON MATHEKA MSIMAMO mkali wa baadhi ya vinara wanaosuka muungano wa One Kenya Alliance (OKA) wa kukataa kumuunga kiongozi wa chama... Na BENSON MATHEKA Vigogo wa kisiasa wanaomezea mate urais wanaendelea kuviziana kila moja akisubiri kuona hatua ambayo mwenzake... Na BENSON MATHEKA KIONGOZI wa chama cha ODM Raila Odinga ameweka mikakati tosha ya kuyumbisha muungano wa One Kenya Alliance (OKA)... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na BRIAN OCHARO MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji amelaumu mitandao ya mabwenyenye kwa kutatiza kesi zinazowahusu... NA FAUSTINE NGILA MARAIS kadhaa na wakuu wa serikali duniani wametajwa katika ufichuzi wa hivi majuzi wa upelelezi wa jinsi mali ya... JOSEPH WANGUI na RICHARD MUNGUTI VITA dhidi ya ufisadi vimeanza kuzaa matunda kwa mara ya kwanza katika historia ya Kenya huku watu... Na IBRAHIM ORUKO WASHUKIWA wanaokabiliwa na ufisadi huenda siku zijazo wakahepa kufungwa gerezani iwapo watakubali kushirikiana na Afisi... Na CHARLES WASONGA WANASIASA na maafisa wa serikali ambao wameshtakiwa kwa ufisadi sasa watazuiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao,... Na RICHARD MUNGUTI ALIYEKUWA waziri wa Michezo na Jinsia, Dkt Hassan Wario huenda akasukumwa jela miaka 10 baada ya kupatikana na hatia... Na LEONARD ONYANGO MARA baada ya kutangaza kushirikiana na kinara wa ODM Raila Odinga mnamo Machi 2018, almaarufu handisheki, Rais Uhuru... Na PETER MBURU MIRADI inayofadhiliwa na fedha za walipa ushuru ndiyo inayotafunwa zaidi na maafisa fisadi serikalini, ripoti ya Mkaguzi... Na MAUREEN ONGALA CHAMA cha Walimu wa Sekondari (KUPPET) kimeomba Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) ianzishe uchunguzi... Na LEONARD ONYANGO KILA mara magavana wanapohutubia Wakenya kuhusiana na hali ya ugonjwa wa corona katika kaunti zao, wanaangua kilio... Na KAMAU MAICHUHIE MZOZO wa uongozi umechipuka kati ya Gavana wa Kiambu, James Nyoro, na Senata Kimani Wamatangi kuhusu madai ya ufujaji... NA AP ALIYEKUWA rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ametakiwa kupendekeza kifungo ambacho angependa kupewa kwa kukwepa vikao vya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved YALA, Siaya Na JOHN MUTUKU SAMUEL KALAMENI eneo hili alibubujikwa na machozi na kujitupa miguuni mwa demu kumuomba asimteme lakini... Na MWANDISHI WETU Kangemi, Nairobi  Jombi mtaani hapa ambaye ni seremala tajika aliamua kukarabati kitanda cha jirani yake bila... Na Nicholas Cheruiyot Mwanasiasa limbukeni alivunjika moyo mpango wake wa kumhamisha nduguye kwake ili amuachie boma atumie kujipigia... Na John Mutuku Samuel Kisa cha kushangaza kilitokea mtaani hapa, baada ya demu aliyezuru wazazi wa mumewe kufumaniwa usiku akirandaranda... Na Mwandishi Wetu KANGEMI, NAIROBI  JOMBI mmoja mtaani hapa anaendelea kuuguza majeraha kwenye nyeti zake baada ya kushambuliwa na... NA DENNIS SINYO JOMBI mmoja ambaye alikuwa akiheshimiwa na wenzake alishangaza watu alipomkana mkewe hadharani ili asimkasirishe mpango... Na Mirriam Mutunga KATHWANA, THARAKA NITHI MWANADADA mmoja kutoka hapa alidondokwa na machozi mpenzi wake wa awali alipomuoa dada... HURUMA, NAIROBI Na MWANDISHI WETU Pasta wa kanisa moja mtaani humu, aliwakasirisha waumini kwa kuwatangazia kuwa atafunga kanisa kwa... Na MASHIRIKA Frankfurt, Ujerumani MWANAMKE mmoja katika mji huu alishangaza jamaa na marafiki kwa kusema kuwa heri mumewe angekufa... Na TOBBIE WEKESA KERICHO KIPUSA mtaani hapa aliwashangaza wengi alipoamua kuuza suti mpya ya mumewe ili apate fedha za kumwezesha... Na MWANDISHI WETU VOI MJINI Jamaa aliyekuwa paparazzi maarufu mjini humu anajuta kuuza simu na kamera yake kwa bei ya kutupa ili... KAPKATET, KERICHO NA NICHOLAS CHERUIYOT ILIBIDI polo wa hapa akubali kwa haraka kufanya kazi za jikoni ili kuokoa ndoa yake baada ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na MASHIRIKA NEYMAR Jr alipachika wavuni mabao mawili na kusaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kufungua mwanya wa alama 10... Na MASHIRIKA KIUNGO Paul Pogba amesema Manchester United wana ulazima wa “kubadilisha mbinu zao za kutandaza soka” iwapo wana ndoto ya... Na JOHN KIMWERE CHANGAMOTO zimekuwa chungu nzima, lakini hazijazuia wachezaji wa Kiganjo Kings kutia bidii, kwani lengo lao ni kutua... Na GEOFFREY ANENE KLABU ya Dandora Youth kutoka ligi ya daraja ya tano ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF), imejawa motisha ya kutafuta... NA ABDULRAHMAN SHERIFF WASICHANA wanne, watatu wanafunzi wa shule za upili na mwingine wa shule ya msingi kutoka Kaunti ya Taita... Na MASHIRIKA TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO KIUNGO wa Chelsea, Christian Pulisic, alifunga bao katika dakika za mwisho na kusaidia timu... Na GEOFFREY ANENE TIMU ya Kenya ya raga ya wanaume ya wachezaji 15 kila upande ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 maarufu kama... Na GEOFFREY ANENE MKIMBIAJI mkimbizi Francois Msafiri amepokea mapokezi ya kishujaa mtaani mwake Syokimau baada ya kukamilisha mbio za... Na GEOFFREY ANENE VISSEL Kobe anayochezea Ayub Masika inakodolea macho kubanduliwa kwenye kipute cha Levain Cup baada ya kupoteza mechi... Na MASHIRIKA TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO KIUNGO mvamizi Andre Ayew, 31, ataagana na Swansea City mwishoni mwa Juni 2021 baada ya mkataba... NA RICHARD MAOSI KIKOSI cha Mogotio United kinajivunia wachezaji mahiri ambao wanasakata soka katika kiwango cha Kaunti ya Baringo... NA ABDULRAHMAN SHERIFF CONGO Boys FC inaonelea fahari kuu ikiwa timu kubwa mbili za hapa nchini, Gor Mahia na AFC Leopards zitacheza mechi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved KWAKO shangazi. Nimekuwa na mpenzi kwa miaka mitatu. Wiki mbili zilizopita aliondoka akaniambia anaenda kuwatembelea wazazi wake... Na SHANGAZI HUJAMBO shangazi? Nina umri wa miaka 28 na nilipata mtoto punde tu baada ya kukamilisha elimu ya shule ya upili. Mwanamume... Na SHANGAZI VIPI shangazi? Nilioa miaka mitano iliyopita na tuna watoto wawili. Ilifika wakati mama watoto akashindwa kunishibisha na... Na SHANGAZI VIPI shangazi? Nilimpa mimba mwanamke mpenzi wangu na nikamuoa kwa sababu nampenda kwa dhati. Ingawa nimeajiriwa, mshahara... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Nilikuwa na mpenzi niliyempenda sana na alikuwa ameahidi kunioa. Hata hivyo, wazazi wake walipinga mpango... Na SHANGAZI VIPI shangazi? Huu ni mwaka wa pili tangu niolewe na tumejaliwa mtoto mmoja. Ninashuku kuna kitu kinachoendelea kati ya mume... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 36 na nimeolewa. Nina uhusiano wa pembeni na bosi wangu na nimegundua... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Nina umri wa miaka 39 na huu ni mwaka wa pili nikitafuta mchumba na bado sijapata. Wanawake ni wengi na... Na SHANGAZI HABARI zako shangazi? Nina umri wa miaka 36 na nina mtoto ingawa sijaolewa. Nimekuwa katika uhusiano wa kimapenzi na... Na SHANGAZI SHIKAMOO shangazi! Nina jambo ambalo linanitatiza moyoni. Kuna mwanamke fulani ambaye amenasa moyo wangu na ninatamani sana... Na SHANGAZI HUJAMBO shangazi? Nina mke ambaye tumeishi pamoja kwa mwaka mmoja sasa. Hata hivyo kuna jambo fulani ambalo nimegundua... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Nimekuwa na mpenzi kwa karibu mwaka mmoja. Amekuwa akiniahidi kuwa atanioa ingawa bado hajanitambulisha kwa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved VICTOR RABALLA NA KASSIM ADINASI WAWANIAJI viti katika ngome ya kiongozi wa ODM Raila Odinga ya Luo Nyanza, wameonywa dhidi ya mivutano... Na WINNIE ONYANDO KINARA wa ODM Raila Odinga na Naibu Rais William Ruto kufikia sasa wako bega kwa bega kwenye kinyang’anyiro... Na LEONARD ONYANGO KINARA wa ODM, Raila Odinga amewatema baadhi ya washauri wake alioshirikiana nao kwa karibu kwenye uchaguzi mkuu wa... BRIAN OCHARO na VALENTINE OBARA UBABE wa kisiasa kati ya Kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, na Naibu Rais William Ruto katika Kaunti ya... Na CHARLES WASONGA HATUA ya Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga kushikilia kuwa wawaniaji wanaounga azma zao za... Na WANDERI KAMAU KIONGOZI wa chama cha ODM, Bw Raila Odinga, jana alianza rasmi safari yake ya kuelekea Ikulu 2022, huku akipata... Na ANTHONY KITIMO GAVANA wa Mombasa, Bw Hassan Joho, amehudhuria mkutano wa dharura na Kiongozi wa chama cha ODM, Bw Raila Odinga, kabla... Na KENNEDY KIMANTHI MABWANYENYE wa eneo la Mlima Kenya leo wanatarajiwa kumwidhinisha rasmi kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, kama... Na CHARLES WASONGA NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga wanaonekana kuendeleza mbinu za kampeni za kulambana visigino... Na LEONARD ONYANGO MATAMSHI ya zamani ya Rais Uhuru Kenyatta ya kumdhalilisha Kiongozi wa ODM Raila Odinga yamegeuka kuwa kizingiti... Na SAMMY WAWERU KIONGOZI wa ODM, Raila Odinga Jumamosi anaendeleza kampeni zake kutafuta uungwaji mkono eneo la Mlima Kenya kumrithi... MAUREEN ONGALA na ALEX KALAMA GAVANA wa Kaunti ya Kilifi, Bw Amason Kingi, anakabiliwa na kibarua kigumu cha kuamua mwelekeo ambao chama... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved NA WALLAH BIN WALLAH KUFIKIRI ni kazi. Ubongo wako hauwezi kukupa majibu sahihi ya maswali unayoulizwa bila ya ubongo kufanya kazi ya... NA ENOCK NYARIKI MOJA kati ya maneno mawili yatumiwayo na watu kurejelea chakula ni mlo. Kuna jingine ambalo aghalabu hukosewa katika... Na CHRIS ADUNGO CHAMA cha Kiswahili katika Shule ya Msingi ya Stelurm Elite, Nairobi kimewawezesha wanafunzi kupiga hatua na kutia fora... Nitaanza makala haya kwa kuuliza swali lifuatalo: Je, mtu huwa na uhakika wa jambo au hakika ya jambo? Vipo baadhi ya vielezi ambavyo... Na CHRIS ADUNGO CHAMA cha Kiswahili katika Shule ya Upili ya St Louis Butula Boys, Kaunti ya Busia (CHAKIBU), kiliasisiwa kwa nia ya... Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya habari ya Nation Media Group imeimarisha juhudi zake za kukuza matumizi ya Kiswahili kwa kutenga siku moja... Na MARY WANGARI   WAKENYA Jumatatu wameungana na jamii ya kimataifa kumboleza kifo cha Mama Sara Obama kwa kutuma risala zao za... Na MARY WANGARI Lugha huundwa kwa sauti ambazo huunganishwa ili kuunda neno au sehemu ya neno, kisha maneno huungana kuunda miundo... NA MARY WANGARI DHANA ya mawasiliano ni mchakato wa kuwasilisha taarifa kwa njia ya ubadilishanaji wa hisia, mawazo, matarajio,... Na CHRIS ADUNGO USIOGOPE kukosea. Kupotea njia ndiko kujua njia. Jaribu tu. Ipo siku ambapo mghafala utaisha. Zidi kumulika uendako kwa... MTIHANI huzua changamoto kwa yeyote anayepania kuufanya. Nakisia ni kwa sababu ya ushindani unaohusishwa nao, hasa nchini mwetu. Aghalabu... Na ENOCK NYARIKI KWA mara ya kwanza kabisa, mitihani ya Kidato cha Nne na Darasa la Nane ambayo hufanywa katika mwezi wa Kumi na Kumi na... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na MARY WANGARI WINGU la majonzi liligubika Kenya wikendi wakati nyota mchanga wa Olimpiki, Agnes Tirop, alipopumzishwa nyumbani kwao... Na MARY WAMBUI SERIKALI ya Uingereza imeshinikizwa kufanya uchunguzi wa ndani na kumshtaki mwanajeshi wake, anayetuhumiwa kumuua... Na BRIAN OJAMAA MWILI wa Masten Wanjala, mwanamume aliyekamatwa kwa mauaji ya watoto, bado uko katika mochari ya Hospitali ya Rufaa ya... WYCLIFFE NYABERI na CHARLES WASONGA WANAUME wanne wanaoshukiwa kuwateketeza wanawake wakongwe kwa tuhuma za uchawi eneo la Marani,... Na Hilary Kimuyu POLISI katika mji wa Uhispania wa Seville wanamzuilia mwanamke Mkenya anayedaiwa kuuma na kula vidole viwili vya... Na GEORGE MUNENE Mtu mmoja ameuawa  kwa risasi huku taharuki ikizidi kutanda mjini Kianjokoma, Kaunti ya Embu kufuatia mauaji ya vijana... Na GEORGE MUNENE Mama mmoja jana alisimulia mahakamani jinsi alivyopata chooni mifupa ya mwanawe na mjukuu wake ambao walikuwa... Na AFP PORT-AU-PRINCE, Haiti WATU wasiojulikana Jumatano waliingia katika makazi ya Rais Jovenel Moise wa Haiti na kumpiga risasi,... Na JOHN NJOROGE UTATA unaendelea kuzingira kifo cha mfanyabiashara na mkurugenzi wa kampuni moja ya maua, Justus Metho Muinde katika... STANLEY NGOTHO NA SIMON CIURI MIILI ya watatu kati ya wanaume wanne waliotoweka mjini Kitengela, Kaunti ya Kajiado mnamo Aprili 19,... SIMON CIURI na MERCY MWENDE MWANAFUNZI wa chuo kikuu, Lawrence Warunge, aliyehusishwa na mauaji ya familia yake ya watu wanne na mjakazi... NA MASHIRIKA MAANDAMANO makubwa jana yalizuka viungani mwa jiji la Mineapolis, Amerika baada ya polisi kumpiga risasi raia mweusi karibu... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved NA CHARLES WASONGA SERIKALI iliyopita ya Jubilee imelaumiwa kwa kutumia jumla ya Sh55 bilioni, bila idhini ya Bunge, kwa miezi mwili na... NA BENSON MATHEKA HUKU serikali ya Jubilee ikikaribia kuondoka mamlakani baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti 9, viongozi wake wameonyesha... NA ONYANGO K’ONYANGO CHAMA cha Jubilee sasa kimeanza mchakato wa kushawishi wandani wa Rais Uhuru Kenyatta waliokuwa wameunda vyama... NA MWANGI MURURI RAIS Uhuru Kenyatta ameripotiwa kukasirishwa na washauri wake kuhusu ripoti zao za hali ya kisiasa katika eneo la Mlima... NA MWANGI MUIRURI WANDANI wa Rais Uhuru Kenyatta wamelaumiwa kwa kuchangia kudidimia kwa umaarufu na ushawishi wake katika eneo la Mlima... Na PSCU RAIS Uhuru Kenyatta amekariri kujitolea kwa serikali katika kuboresha maslahi ya walemavu, akisema watasaidiwa kushiriki... Na WANDERI KAMAU RAIS Uhuru Kenyatta kwa mara nyingine alionyesha dalili za kuunga mkono azimio la kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga,... Na CHARLES WASONGA RAIS Uhuru Kenyatta Jumanne alitoa kumbukumbu ya nyakati ambapo alihudumu bungeni kama Mbunge Maalum, Kiongozi wa... Na SAMMY WAWERU RAIS Uhuru Kenyatta anahutubia taifa leo Jumanne alasiri katika kikao cha pamoja cha bunge, wengi wakisubiri kusikia... Na CHARLES WASONGA RAIS Uhuru Kenyatta leo Jumanne anatarajiwa kuangazia mikakati ya serikali ya kukabiliana na changamoto zinazolikumba... Na CHARLES WASONGA RAIS Uhuru Kenyatta atatoa hotuba kuhusu Hali ya Taifa katika kikao maalum cha Bunge la Kitaifa na Seneti mnamo... Na BENSON MATHEKA SERIKALI imeonywa kuwa mazoea ya maafisa wake, akiwemo Rais Uhuru Kenyatta ya kukaidi maagizo ya mahakama na utawala... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na MACHARIA MWANGI WAZIRI wa Leba Simon Chelugui ameziomba kampuni mbalimbali zihakikishe kuwa haziwafuti wafanyakazi wao hata... Na WANGU KANURI TEKNOLOJIA imeiboresha sekta ya upishi haswa kwa wale ambao waliendeleza huduma zao mtandaoni licha ya janga la... Na WANGU KANURI WAKENYA wanaoishi na ulemavu pamoja na wale  wakongwe sasa wataweza kupokea huduma wanazotaka kidijitali za mawasiliano... Na FAUSTINE NGILA LABDA hujasikia hili lakini linakuathiri moja kwa moja kwa kuwa wewe ni mteja wa M-Pesa. Majuzi rafiki yangu alimfaa... Na STEPHEN ODUOR VIJANA katika Kaunti ya Tana River, wametaka mafunzo ya kisasa yatolewe katika taasisi na vyuo vya kiufundi ili... NA FAUSTINE NGILA MAGARI mengi yanayomilikiwa humu nchini na duniani kote yanatumia dizeli au petroli, mafuta ambayo yanachafua... Na FAUSTINE NGILA SUALA muhimu lililojitokeza katika ziara ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uingereza wiki iliyopita, lilikuwa azma ya... Na FAUSTINE NGILA NI miaka mitatu sasa tangu Ripoti ya Blockcheni na Akili Bandia (AI) iwasilishwe kwa serikali kwa ajili ya utekelezaji... Na Ruth Mbula SPIKA wa Bunge la Kitaifa, Bw Justin Muturi, amewarai wadau wa afya kuharakisha utekelezaji wa taratibu za kutumia... [caption id=attachment_77341" align="alignnone" width="843"] Wataalamu wakagua uvunaji wa bitcoin katika kituo cha Bitfarms eneo la Saint... Na FAUSTINE NGILA
Inashangaza kuwa licha ya Kenya kupiga hatua kubwa katika maendeleo ya kiteknolojia, karatasi bado zinatumika katika... Na MASHIRIKA
Kutokana na ongezeko la matumizi ya simu tamba na za kisasa pamoja na kuimarishwa kwa mitandao, imekuwa rahisi kwa idadi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na RICHARD MUNGUTI
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi Ijumaa alizimwa na mahakama kupeperusha katika mitandao ya kijamii video... Na RICHARD MUNGUTI
KUNDI jipya la mawakili sita waliokuwa wanamwakilisha aliyekuwa gavana wa Nairobi Bw Mike Sonko Jumanne walijiondoa... Na RICHARD MUNGUTI
RIPOTI ya daktari wa tiba za akili imesema Alhamisi kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko anaugua maradhi ya... Na RICHARD MUNGUTI
MAHAKAMA ilielezwa jana kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko angali amelazwa katika Nairobi Hospital... Na RICHARD MUNGUTI
UFICHUZI wa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko kwamba mtu aliingia kwenye seli anamozuiliwa katika kituo cha... Na BENSON MATHEKA
Aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko anajuta kwa vitendo alivyofanya akiwa mamlakani; akiepuka kuadhibiwa kwa... Na RICHARD MUNGUTI
KAMA kuna wakati wenye changamoto tele kwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko ni sasa.
Maji yalizidi unga hata... Na RICHARD MUNGUTI
MASAIBU ya aliyekuwa gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko, yaliongezeka Jumatano ilipofichuka kuwa serikali inapanga... Na RICHARD MUNGUTI
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi, Mike Sonko aliangua kilio kortini Jumatano wakati wa kusikizwa kwa kesi ya ufisadi wa... Na CHARLES WASONGA
WANASIASA na watu ambao majina yao yatawekwa katika orodha ya aibu ya Tume ya Uwiano na Utangamano ya Kitaifa (NCIC)... BENSON MATHEKA na SIMON CIURI
Masaibu ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Mike Sonko yaliendelea kuongezeka jana alipozuiliwa rumande baada... Na RICHARD MUNGUTI
MASAIBU ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi Gidion Kioko yameongezeka baada ya  kusukumwa ndani hadi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAMMY WAWERU MSANII tajika wa nyimbo Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda ametengana na mpenzi wake mwanasiasa Karen Nyamu. Hii ni kutokana na video iliyochipuka ambayo anaskika akisema “nilikuwa kwenye ndoa ya mitara, sasa niko singo”. Samidoh amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Seneta Maalum Karen Nyamu, na wamejaaliwa kupata watoto wawili. Msanii huyo wa nyimbo za Agikuyu, alifichua kuachana na Karen kupitia video ya mbashara ya Tiktok (live) ambapo alikuwa akijibu maswali ya mashabiki wake. Wakati wa mafichuzi hayo, alionekana kuwa kwenye eneo la burudani alikoandamana na msichana ambaye hakuweka wazi endapo ndiye mchumba wake mpya. “Ati hongera kwa kuwa na mpenzi mpya…” Samidoh akasoma mojawapo ya jumbe zilizotumwa na mashabiki wake. Alijibu, “Si wewe pekee ulishushwa madaraka kutoka kiwango cha hadhi hadi dereva wangu…Nilikuwa kwenye ndoa ya mitara ila sasa niko singo”. Mfuasi huyo aliendelea kumdadisi, akitaka kujua iwapo Samidoh anafahamu kuhusu ukurasa wa kimitandao unaohusishwa na mchumba wake – Karen Nyamu Fun Page. Kwa ucheshi, mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Kairetu Gakwa (Binti yangu) na Ndiri Mutwe Mwega (Sina kichwa kizuri) alisema kwa sasa anajishughulisha na biashara. “Kwa sasa, ninajishughulisha na masuala biashara. Ikiwa si mradi au biashara, ishi na mama yako,” alielezea. Shabiki wake alimkejeli akitaka kujua aliko nina yake, isijulikane ikiwa alimaanisha mama yake mzazi au mpenzi wake. “Ameoleka na kwa sasa anafurahia fungate (honeymoon),” Samidoh alidokeza. Kidosho aliyeandamana naye alitambua shabiki huyo kama Shabaan, akisema kwamba yeye ni mchochezi. “Wee acha hiyo, unajua Shabaan wewe ni mchochezi sana… (Yuko hapa (akimaanisha Karen Nyamu),” mwanadada huyo alisema. Naye Samidoh aliendelea, “Tunataka Karen, naona hivo ndivo mchango safuni unasema…Naona, lakini sasa yuko online kweli?” Kipusa aliyeandamana naye, alijibu, “Yuko online, mjaribu”. Aidha, shabiki wa Samidoh alitaka Karen Nyamu ajumuishwe kwenye mazungumzo hayo ya mbashara Tiktok. Kilichoshangaza zaidi na kuashiria utengano wa Samidoh na Karen, ni kudai kwamba alimbloki mtandaoni na angeweza kushiriki endapo atamuondoa alikomuweka. “Yuko kwenye orodha ya kublokiwa, sasa hiyo ndio shida. Labda nisitishe mazungumzo haya ya moja kwa moja ili nimuondoa aweze kujumuika nasi,” Samidoh alifafanua. Mahusiano kati ya Samidoh na Karen, ndiyo yalichangia kuachana na mkewe, Edday Nderitu ambaye alihamia Amerika Mei 2023. Edday alikuwa ameonya msanii huyo mapema 2023, akisisitiza kwamba hakuwa tayari kuwa kwenye ndoa ya mitara. Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAMMY WAWERU MSANII tajika wa nyimbo Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda ametengana na mpenzi wake mwanasiasa Karen Nyamu. Hii ni kutokana na video iliyochipuka ambayo anaskika akisema “nilikuwa kwenye ndoa ya mitara, sasa niko singo”. Samidoh amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Seneta Maalum Karen Nyamu, na wamejaaliwa kupata watoto wawili. Msanii huyo wa nyimbo za Agikuyu, alifichua kuachana na Karen kupitia video ya mbashara ya Tiktok (live) ambapo alikuwa akijibu maswali ya mashabiki wake. Wakati wa mafichuzi hayo, alionekana kuwa kwenye eneo la burudani alikoandamana na msichana ambaye hakuweka wazi endapo ndiye mchumba wake mpya. “Ati hongera kwa kuwa na mpenzi mpya…” Samidoh akasoma mojawapo ya jumbe zilizotumwa na mashabiki wake. Alijibu, “Si wewe pekee ulishushwa madaraka kutoka kiwango cha hadhi hadi dereva wangu…Nilikuwa kwenye ndoa ya mitara ila sasa niko singo”. Mfuasi huyo aliendelea kumdadisi, akitaka kujua iwapo Samidoh anafahamu kuhusu ukurasa wa kimitandao unaohusishwa na mchumba wake – Karen Nyamu Fun Page. Kwa ucheshi, mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Kairetu Gakwa (Binti yangu) na Ndiri Mutwe Mwega (Sina kichwa kizuri) alisema kwa sasa anajishughulisha na biashara. “Kwa sasa, ninajishughulisha na masuala biashara. Ikiwa si mradi au biashara, ishi na mama yako,” alielezea. Shabiki wake alimkejeli akitaka kujua aliko nina yake, isijulikane ikiwa alimaanisha mama yake mzazi au mpenzi wake. “Ameoleka na kwa sasa anafurahia fungate (honeymoon),” Samidoh alidokeza. Kidosho aliyeandamana naye alitambua shabiki huyo kama Shabaan, akisema kwamba yeye ni mchochezi. “Wee acha hiyo, unajua Shabaan wewe ni mchochezi sana… (Yuko hapa (akimaanisha Karen Nyamu),” mwanadada huyo alisema. Naye Samidoh aliendelea, “Tunataka Karen, naona hivo ndivo mchango safuni unasema…Naona, lakini sasa yuko online kweli?” Kipusa aliyeandamana naye, alijibu, “Yuko online, mjaribu”. Aidha, shabiki wa Samidoh alitaka Karen Nyamu ajumuishwe kwenye mazungumzo hayo ya mbashara Tiktok. Kilichoshangaza zaidi na kuashiria utengano wa Samidoh na Karen, ni kudai kwamba alimbloki mtandaoni na angeweza kushiriki endapo atamuondoa alikomuweka. “Yuko kwenye orodha ya kublokiwa, sasa hiyo ndio shida. Labda nisitishe mazungumzo haya ya moja kwa moja ili nimuondoa aweze kujumuika nasi,” Samidoh alifafanua. Mahusiano kati ya Samidoh na Karen, ndiyo yalichangia kuachana na mkewe, Edday Nderitu ambaye alihamia Amerika Mei 2023. Edday alikuwa ameonya msanii huyo mapema 2023, akisisitiza kwamba hakuwa tayari kuwa kwenye ndoa ya mitara. Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAKAZI wa mtaa wa Mazembe viungani mwa mji wa Nakuru wamekiri kuhangaishwa na wezi ambao huwaibia na kuwasindikiza hadi nyumbani. Huwawekea ulinzi huo makusudi ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafika nyumbani salama salimini. Kwa kawaida, wahuni wamebuni mbinu mpya ya kutembea na mbwa wakubwa nyakati za usiku, ili kujiwekea ulinzi wa kibinafsi. Owen Shibala mwendeshaji bodaboda kati ya Nakuru mjini na Mazembe, anasema hajui walikotoa ujasiri walio nao kushika doria usiku utadhani ni polisi. Mazembe ni mojawapo ya mitaa ambayo hushuhudia visa vya kihalifu na utumiaji wa mihadarati mara kwa mara. “Ukikutana nao usiku ni lazima usalimishe kila kitu lau sivyo utaona cha mtema kuni. Watakucharaza viboko na kuiba kila kitu cha nguvu,”akasema. Hata hivyo, wanapoiba hujitwika jukuma la kuwasindikiza wakazi, wasije wakakutana na vibaka wengine barabarani. Aidha, wanalia sare za polisi jambo linalowafanya baadhi ya raia kuamini huenda wanashirikiana na maafisa wa polisi. Baadhi yao wanajifanya ni maafisa wa polisi ambao huwa wameshika doria, wakilenga kuhangaisha wapita njia wanaotoka kazini usiku. Agnes Wahome mfanyibiashara mtaani Rhonda anasema huwa wamejihami kwa visu, rungu na wako tayari kupigana. Kulingana na Bi Wahome, hii ni hali ya kawaida siku hizi katika mitaa ya Manyani, Bondeni na Freearea ambapo vijana wengi wamejiingiza kwenye uhalifu. Bi Wahome anasema wahalifu wengi wanajulikana, kwani ni vijana wadogo kutoka mitaa jirani ya Flamingo na Lakeview. Mkazi huyo angependa polisi kushika doria katika maeneo husika ili kuzuia kuzuka kwa magenge hatari yanayohangaisha wenyeji. Hili linajiri siku chache baada ya Taifa Leo Dijitali kufichua visa vya wizi ambapo baadhi ya wezi kutoka kwenye mtaa wa Gioto, Nakuru wamekuwa wakipika chakula katika kila nyumba wanamoingia kuiba. Mtaa wa Bondeni, Kaunti ya Nakuru ambapo wezi huwaibia wakazi na kuwasindikiza mpaka nyumbani. PICHA|RICHARD MAOSI
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAKAZI wa mtaa wa Mazembe viungani mwa mji wa Nakuru wamekiri kuhangaishwa na wezi ambao huwaibia na kuwasindikiza hadi nyumbani. Huwawekea ulinzi huo makusudi ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafika nyumbani salama salimini. Kwa kawaida, wahuni wamebuni mbinu mpya ya kutembea na mbwa wakubwa nyakati za usiku, ili kujiwekea ulinzi wa kibinafsi. Owen Shibala mwendeshaji bodaboda kati ya Nakuru mjini na Mazembe, anasema hajui walikotoa ujasiri walio nao kushika doria usiku utadhani ni polisi. Mazembe ni mojawapo ya mitaa ambayo hushuhudia visa vya kihalifu na utumiaji wa mihadarati mara kwa mara. “Ukikutana nao usiku ni lazima usalimishe kila kitu lau sivyo utaona cha mtema kuni. Watakucharaza viboko na kuiba kila kitu cha nguvu,”akasema. Hata hivyo, wanapoiba hujitwika jukuma la kuwasindikiza wakazi, wasije wakakutana na vibaka wengine barabarani. Aidha, wanalia sare za polisi jambo linalowafanya baadhi ya raia kuamini huenda wanashirikiana na maafisa wa polisi. Baadhi yao wanajifanya ni maafisa wa polisi ambao huwa wameshika doria, wakilenga kuhangaisha wapita njia wanaotoka kazini usiku. Agnes Wahome mfanyibiashara mtaani Rhonda anasema huwa wamejihami kwa visu, rungu na wako tayari kupigana. Kulingana na Bi Wahome, hii ni hali ya kawaida siku hizi katika mitaa ya Manyani, Bondeni na Freearea ambapo vijana wengi wamejiingiza kwenye uhalifu. Bi Wahome anasema wahalifu wengi wanajulikana, kwani ni vijana wadogo kutoka mitaa jirani ya Flamingo na Lakeview. Mkazi huyo angependa polisi kushika doria katika maeneo husika ili kuzuia kuzuka kwa magenge hatari yanayohangaisha wenyeji. Hili linajiri siku chache baada ya Taifa Leo Dijitali kufichua visa vya wizi ambapo baadhi ya wezi kutoka kwenye mtaa wa Gioto, Nakuru wamekuwa wakipika chakula katika kila nyumba wanamoingia kuiba. Mtaa wa Bondeni, Kaunti ya Nakuru ambapo wezi huwaibia wakazi na kuwasindikiza mpaka nyumbani. PICHA|RICHARD MAOSI
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI MASKWOTA wapatao 10,000 wamewasilisha upya kesi katika Mahakama ya Upeo wakiomba ibatilishe uamuzi kwamba wafukuzwe kutoka kwa shamba la ukubwa wa ekari 25,000 wanalong’ang’ania umiliki wake na familia ya mwanasiasa marehemu Mark Too. Maskwota hao wanaodai mababu zao ndio waliotimuliwa kutoka kwa shamba hilo enzi za ukoloni, wanasema walipewa shamba hilo rasmi na aliyekuwa Rais hayati Daniel arap Moi, kisha Kamishna wa Ardhi M Okundu akaratibisha uamuzi huo mwaka 2007. Katika ombi lililowasilishwa na wakili William Arusei chini ya sheria za dharura, kikundi cha maskwota hao–Sirikiwa Squatters Group–kimeomba mahakama ibatilishe uamuzi huo kwa vile ilitegemea ushahidi ambao haukuwa umewasilishwa katika kesi waliyoshtaki katika Mahakama ya kuamua kesi za mashamba (ELC), Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu. Pia wameeleza bayana Jaji Mkuu Martha Koome, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu, majaji Mohammed Ibrahim, Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Isaack Lenaola, na William Ouko walitegemea ushahidi wa Afisa wa Ugavi wa Mashamba R J Simiyu kutoa uamuzi wang’atuke shambani. Maskwota hao wamesema ushahidi wa Bw Simiyu uliowasilishwa mbele majaji hao saba kwa njia ya afidaviti ni mpya na kamwe “haukuwasilishwa mbele ya Jaji Antony Ombwayo aliposikiliza na kuamua kesi hiyo 2017.” Pia wanasema ushahidi huo haukuwasilishwa Mahakama ya Rufaa iliyosikiliza rufaa iliyowasilishwa na kampuni ya Fanikiwa, familia ya marehemu Mark Too, kampuni ya Lonrho Agribusiness (EA) Ltd, na Bw David K Korir. Hivyo basi, maskwota hao wanaeleza mahakama hii ya upeo kwamba ni kinyume cha sheria kutegemea ushahidi mpya kutoa uamuzi wa kesi hii iliyo na umuhimu mkubwa kwa umma. “Uamuzi huu wa Mahakama ya Juu wa Desemba 15, 2023, hauna mashiko kisheria na kamwe hauna nguvu kisheria kuwatimua maskwota hawa kutoka kwa shamba lao,” asema Bw Arusei. Pia maskwota hawa wanadai kwamba badala ya Mahakama ya Juu kujadili masuala ya kikatiba jinsi ilivyo jukumu lake, majaji hao walianza kufafanua na kutafsiri ushahidi wa watu binafsi na kuelezea maana ya ‘skwota’. Mahakama hii imeombwa ikague upya uamuzi iliyotoa kwa vile ilidanganywa na walalamishi na pia kutendewa ujanja. Akinukuu maamuzi ya majaji wastahiki kama vile Lord Dening, Bw Arusei amesema, mahakama ikigundua ilipotoshwa au kudanganywa na upande mmoja, iko na mamlaka na uwezo wa kufutilia mbali uamuzi iliyotoa na kuandika mwingine. Maskwota hao wanaomba Mahakama ya Juu iwarudishe shambani kama ilivyokuwa imeamuliwa na Jaji Ombwayo na Mahakama ya Rufaa. Vile vile mahakama hiyo imekosolewa kwa kumshambulia hayati Moi katika uamuzi huo pasi kutoa agizo wasimamizi wa mali yake wafike mbele yao kutoa mwanga kuhusu suala la umiliki wa shamba hili lililorudishwa kwa serikali na kampuni iliyokuwa inakuza miti inayotumika katika viwanda vya ngozi. Naibu msajili wa Mahakama ya Juu Nelly Kariuki aliwaamuru maskwota hao wawakabidhi nakala za kesi hii yao mpya wahusika wote kabla ya Januari 31, 2024, kesi itakapotajwa tena kwa maagizo zaidi. Jaji aliyesikiliza kesi hii mpya hakuiratibisha kuwa ya dharura ila aliamuru pande zote ziwasilishe ushahidi katika muda wa siku 14 kuanzia Desemba 21, 2023. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAMILIKI wa nyumba za wapangaji mtaani Kayole wameamua kulala mchana na kukaa macho usiku ili kupambana na wahalifu ambao wametawala ploti zao. Aidha wapangaji wanapoendelea kufurahia sikukuu wakiwa mashambani, wezi kwa upande mwingine wanavunja nyumba na kuiba bidhaa kutoka ploti moja hadi nyingine. Mbali na Kayole, maeneo mengine ambapo wizi umeripotiwa ni Kangemi, Korogocho, Githurai, Umoja, Kariobangi, Starehe, Syokimau, na Buruburu. Wanavunja nyumba na kuiba vyombo, fanicha, mitungi ya gesi ya kupikia, televisheni, na redio, huku hatimaye bidhaa hizo zikiuzwa kwa bei ya kutupa mtaani. Bw Gilbert Ambani ambaye ni mlinzi katika mojawapo ya ploti eneo la Syokimau, anasema wezi wengi huko katika msimu huu wa shamrashamra wanalenga vyuma chakavu kwa sababu huwapatia hela za haraka. “Baadhi ya wezi wanabomoa lango kuu na kuchukua vyuma huku wengine wakivunja mifereji,” Bw Ambani akaambia Taifa Leo. Naye Amon Andika ambaye ni landilodi mtaani Kayole, alisema kwamba imemlazimu kufanya kazi ya ziada ya kulinda nyumba za wapangaji wake ambao wengi walienda mashambani almaarufu ‘ushago’. Anasema mwaka 2023 ameamua kufanya kazi ya usoja kama wengi wanavyoiita, baada ya kubaini kuwa baadhi walinzi wake wa awali walikuwa wakishirikiana na wezi kutekeleza wizi. Bw Andika ameingia gharama ya kuwekeza upya kwenye mradi wa maji baada ya wezi kuvunja mfereji wake usiku wa Desemba 24, 2023, na kutoweka na paipu ya thamani ya Sh70,000. Anasema kwa sababu ya hali ngumu ya kiuchumi, hana uwezo wa kuajiri soja wa usiku. Ndiposa imemlazimu kuhatarisha maisha yake kwa kulinda mali mpaka ifikapo Mwaka Mpya 2024. Anasema ni desturi yake kila mwaka wapangaji wanapokuwa wameelekea ‘ushago’ kufurahia sikukuu, yeye anadumisha usalama. Mnamo Desemba 27, 2023, washukiwa 34 wa wizi walikamatwa katika eneobunge la Starehe katika operesheni iliyoongozwa na chifu na maafisa wa polisi. Hali ni kinyume na baina ya mwaka wa 2020 na 2021 ambapo wakazi wengi wa jiji waliamua kutosafiri kwa sababu ya mlipuko wa janga la Covid-19. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA KIONGOZI wa Narc-Kenya Martha Karua amesema kuwa muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya ulitoka mikono mitupu katika mazungumzo kati yake na mrengo wa Kenya Kwanza (KKA). Kwenye mahojiano na runinga ya Citizen mnamo Alhamisi usiku, Bi Karua alidai wanachama wa Azimio katika Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo (Nadco) walisaidia KKA kuendeleza ajenda zao. “Kwa mtazamo wangu, mazungumzo hayo hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu hakuna muafaka uliofikiwa kuhusu ajenda zetu tatu kuu ambazo ni gharama ya maisha, haki katika uchaguzi, na heshima kwa demokrasia ya vyama vingi,” akasema Bi Karua. Akaongeza: “Muafaka ulipatikana kuhusu ajenda za Kenya Kwanza kama vile kuundwa kwa afisi ya kiongozi rasmi wa upinzani, na kuhalalishwa kwa afisi ya Mkuu wa Mawaziri, ambazo tayari Ruto alikwisha kuwasilisha bungeni.” Kiongozi huyo wa Narc Kenya alieleza kuwa vikao vya kamati ya Nadco vilivyodumu kwa miezi minane vilikuwa ni vya kuwapotezea Wakenya hela na muda kwa sababu serikali haikuongozwa na nia njema iliposhiriki mazungumzo na upinzani. “Mazungumzo hayo yalilenga kutuchezea shere na kutuliza maandamano. Matokeo ya mazungumzo yetu na utawala wa KKA hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu Wakenya bado wanaumizwa na kupanda kwa gharama ya maisha. Kwa mtazamo wangu, ripoti ya Nadco haina maana yoyote kwa Wakenya kwa sababu haishughulikii madhila yao,” Bi Karua, ambaye alikuwa ni mgombea mwenza wa Raila Odinga katika uchaguzi wa urais wa Agosti 9, 2022, akaongeza. Alielekeza lawama kwa utawala wa Kenya Kwanza kwa kile alichodai ni kufeli kufikiwa kwa malengo ya mazungumzo yake na upinzani. “Licha ya sisi kama upinzani na wananchi kuendelea kuushinikiza utawala huu upunguze gharama ya maisha, walipuuza na badala yake kuendelea kuongeza bei ya bidhaa za kimsingi na kuanzisha aina nyingine za ushuru,” akasema. Ili mazungumzo yoyote yafaulu, kulingana na Bi Karua, chama au mrengo ulioko mamlakani ni sharti kuonyesha nia njema kwa sababu wao ndio wanasukumwa kutimiza matakwa ya wananchi. Kiongozi huyo wa Narc-Kenya aliutaja utawala wa sasa kama ambao hauheshimu sheria na maamuzi ya mahakama. “Utawala huu unaendesha majukumu ya serikali kwa namna ambayo haijeshimu sheria na kudharau maoni ya wananchi ulivyofanya wakati wa ukusanyaji maoni ya umma kuhusu Sheria ya Fedha,” akasema. “Unapodharua Katiba na watu ambao walikupa mamlaka na matakwa ya wengi, unageuka serikali mbaya,” akaeleza alipoulizwa sababu yake ya kuirejelea serikali hivyo. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FARHIYA HUSSEIN MWAKA 2023, unyama uliokuwa ukifanywa ndani ya wa Shakahola katika Kaunti ya Kilifi, ulifichuliwa ambapo zaidi ya watu 400 walipoteza maisha yao kwa itikadi kali za kidini. Mhubiri Paul Mackenzie ambaye alitajwa kuwa kiongozi wa wafuasi wake, anachunguzwa kwa madai ya kuwapotosha katika mafundisho ya kidini ambapo waumini walichanganyikiwa, wakiwemo watoto, wakaanza kufunga au kususia chakula hadi wakaanza kudhoofika na hatimaye kuanza kuaga dunia mmoja baada ya mwingine. Habari hizo zilipofahamika, idadi hii ya watu waliopoteza maisha ilikuwa nyingi sana, jambo liloshangazaa ulimwengu mzima. Walionusurika waliozungumza na Taifa Leo alisema waliokufa waliambiwa wafunge hadi kufa ili wakutane na ‘Yesu’. Miezi tisa baadaye, miili zaidi ya 400 inaendelea kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha muda katika Kaunti ya Kilifi, ukumbusho wa kusikitisha kuashiria msimamo wao mkali wa kidini waliofuatilia. Watu hawa, ambao walitajwa na jamaa zao kuwa watu wachangamfu na maisha hapo awali walionekana kuishi maisha ya kudhoofisha na ya hali ya kusikitisha, maisha yao yalikatishwa na imani zile walizofuatilia kwa kina. Msitu huo ambao hapo awali ulikuwa sehemu nzuri ya mandhari ya kiasili, sasa umekuwa shahidi kwa ukatili uliofanywa huko ndani. Shakahola, kijiji katika Kaunti ya Kilifi, kilikuwa kimegubikwa na ukimya wa kutisha kwa miezi kadhaa. Makazi hayo ambayo wanakijiji walitaja zamani yalikuwa ya uchangamfu na yenye shughuli nyingi, sasa yalionekana yametawaliwa na ukimya mkuu. Katika msitu huo wa Shakahola, nyumba zilikuwa za udongo huku zikiezekwa kwa mapaa ya makuti. Njia zilizokuwa na watu wengi sasa zilikuwa kimya kwa kutisha, kana kwamba wanakijiji walikuwa wametoweka wakiacha nyuma vitu vya kibinafsi kama vile Biblia, ushahidi kuwa waliondoka ghafla. Sahani zilizotelekezwa zilizofunikwa ziliashiria ‘mlo wa mwisho’ wa wafuasi wa Kanisa la Good News International la Mchungaji Paul Mackenzie, ambalo inadaiwa lilichochea wao kuchukua mkondo hatari wa kufunga hadi kufa. Katika mazingira haya ya kutatanisha, ambapo ibada inayodhaniwa ilikuwa imezama katika unabii wa apocalyptic, cha kusikitisha ni kwamba baadhi yao hawakunusurika katika safari ya kuenda katika Hospitali Kuu ya Malindi. Wahanga walizikwa bila mpangilio makaburi yao yakiashiria kuzikwa kwao kwa haraka. Miezi kadhaa baadaye, miili yao ilifukuliwa. Watu hawa walionekana kutengwa na kusukumwa kwenye ukingo wa jamii, sauti zao zikiwa zimenyamazishwa na nguvu za itikadi kali. Maisha yao yalipochukuliwa kwa uchungu, heshima waliyostahili katika umauti wa iliondolewa pia. Ni wale tu walioaga dunia wangejua ikiwa kweli walikutana na Mungu wao. Miili yao ilizikwa kwa haraka msituni Shakahola, jambo lililodhihirishwa na jinsi makaburi hayo yalivyofukuliwa ambapo kwa kila mojawapo, miili zaidi ya mmoja ilipatikana ndani. Waumini hao hawakuzikwa na sanduku kama ilivyo kwa Wakristo bali walifunikwa na blanketi na nguzo nyinginezo. Miezi tisa baadaye, chumba cha kuhifadhia maiti cha muda bado kimesalia katika hopsitali ya Malindi, ukumbusho wa mkasa uliotokea mwaka 2023. Waathiriwa wamesalia katika hali ya kutatanisha, utambulisho wao bado haujathibitishwa, hadithi zao kubaini kiini cha kilichotokea ndani ya msitu wa Shakahola bado haijabainika. Hata katika kifo, ibada iliwanyima utambulisho wao, na kuacha miili hiyo ‘haijulikani’ kutokana na ukosefu wa nyaraka zozote. Ukweli uligundulika ni kwamba baadhi ya wanachama hao walitoka kaunti za mbali katika mikoa mingine nchini, jambo la kutatanisha katika kutambua na kudai miili hiyo. Mwezi Mei, serikali ilianzisha mpango wa DNA kulenga familia zinazoshuku kuwa jamaa zao waliopotea au walioaga wanaweza kuhusishwa na msitu wa Kilifi’ Shakahola. Takriban miezi saba imepita tangu kuzinduliwa kwake, lakini familia zinalalmikia kungoja matokeo ya DNA kwa hamu. Miongoni mwa walioathiriwa ni Bw Rodgers Mwibo, ambaye anatafuta mama yake, dada yake, na mpwa wake amabye alisema ni wafuasi waaminifu wa mhubiri Paul Mackenzie kutoka Kanisa la Good News International, waliohamia kwenye msitu huo mwaka mmoja uliopita. Akielezea masikitiko yake, Bw Mwibo alieleza kuwa kufuatia tangazo la serikali, alitoa sampuli zake za DNA kaunti za Nairobi na Malindi. “Badala ya kupata faraja, huku kusubiri kwa muda mrefu kunazidisha kiwewe changu. Kila nikiona picha ya mama yangu, natamani sana uwepo wake, hata kama ni kumuaga tu,” alilalamika Bw Mwibo huku akihoji ufanisi wa taratibu za DNA za serikali. Kulingana na Bw Mwibo, uhakikisho ulitolewa kwamba matokeo yatatolewa mara moja baada ya ukusanyaji wa DNA. Hata hivyo, kile kilichoahidiwa kuwa kipindi kifupi kimeongezeka hadi mwaka mmoja, na kumuacha yeye na wengine katika hali ya huzuni ya kihisia moyo. “Ni katika nchi gani miili hubaki kuhifadhiwa kwenye friji huku familia zikistahimili uchungu huu?” aliuliza Bw Mwibo. Jamaa mwingine, Bi Mary Mwikali anabainisha kuwa hatajua iwapo dadake na mpwa wake ni miongoni mwa waliofukuliwa kutoka msitu wa Shakahola au la. Kusubiri kwa hamu kunaendelea, na kuwaacha wakihangaika na sintofahamu ikiwa wapendwa wao bado wako hai au ni miongoni mwa watu 400 na zaidi wakiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Malindi. Afisa wa Masuala ya Dharura katika Shirika la Haki Africa, Bw Mathias Shipeta, alisema wasiwasi wake ni kwamba serikali imechukua muda mrefu unaohitajika ili kulinganisha na kulinganua DNA. “Inachukua muda gani hadi ulinganishaji wa DNA ukamilike? Familia zinamaliza mwaka bila kujua jamaa zao waliko. Haijafahamika wazi kama wameaga dunia au wapo hai. Ili kulifunga suala hili, ulinganishaji wa DNA lazima ukamilike na kukamilika kwa wakati kabla ya mwisho wa mwaka,” Bw Shipeta alisisitiza. Mwezi Julai, sampuli 266 zilikusanywa kwa madhumuni ya utambulisho wa vinasaba DNA. Uchunguzi wa DNA ni ulinganifu wa kisayansi wa maelezo ya kinasaba ya watu wasiojulikana au waliokufa na yale ya watu waliotambuliwa (waliokufa au walio hai). Mchakato huo ni muhimu kwa sababu za kisheria na za kibinadamu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MASHABIKI wa klabu ya Arsenal mjini Murang’a sasa wameonywa na wenzao wa Manchester United na Chelsea wajiandae kumpokea ndovu wao akianguka pasipo hiari kutoka juu ya mti kumaanisha kushuka katika jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL). “Huku kulimwa ambako mmeanza kulimwa ni mwanzo tu wa namna ambavyo mambo yatakuwa magumu kwenu katika mzunguko wa pili,” akafoka Bw David Njuguna ambaye ni mshirikishi wa the Red Devils mjini humo. Cheo chake hakitambuliki rasmi na klabu ya Manchester United. Bw Njuguna alisema kwamba Arsenal kuwa juu ya jedwali hata kwa mwanya wa pointi 10 sio tishio kwa kuwa katika mkondo wa lala salama, wao huwa butu, wasio na maono na mwelekeo na lazima wajihujumu wao wenyewe kama ilivyokuwa msimu jana. Katika mechi ya usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, Arsenal walirambishwa magoli 2-0 na West Ham. “Hata hamna heshima na wawekezajj na mnatuchomea beti. Kwa kuwa sikuamini kabisa mngeshinda hicho kipute, nilikuwa nimebashiri timu zote mbili angalau zingejipa goli. Sasa ona hamkufunga hata la kukataliwa,” akafoka Stacy Keach, mfuasi wa Chelsea. Janga hilo kwa wanabunduki Arsenal limewaacha katika nafasi ya pili kwenye jedwali wakiwa na pointi 40 huku Liverpool ikibakia kidedea kwa pointi 42. Hii ina maana kwamba Man City ambayo iko na pointi 37 kwa sasa lakini ikiwa imecheza mechi 18 Arsenal ikiwa imecheza mara 19 itaifurusha kutoka nafasi hiyo ya pili iwapo itachapa Sheffield United hapo Jumamosi kwa ubora wa magoli. “Kuna uwezekano mkubwa kwamba Arsenal itaingia mwaka Mpya ikiwa nambari tano nyuma ya Liverpool, Man City, Aston Villa na Tottenham na kabla ya tufike mechi ya 27, hata West Ham, Man United… watakuwa mbele ya Arsenal,” akasema Junita Kasyoki ambaye anashabikia Man United. Ni usiku ambao wafuasi wa Arsenal hawakujibu mipigo, waliondoka polepole na kimyakimya kutoka kwa mkahawa wa Green Park ambapo wengi walikuwa wakifuatilia mtanange huo ulioanza saa tano na robo usiku. “Lakini hata hivyo kushindwa kwetu kulisaidia West Ham kuruka Man United katika jedwali. Tungeshinda mchuano huo Man U wangebakia nafasi ya sita lakini kung’atwa kwetu kulisaidia Mashetani Wekundu kuteremka hadi nafasi ya saba,” akajituliza Bw Simon Ngonjo. Kwa sasa, maombi ya Arsenal ni kuzuke mikosi ya kushindwa kwa timu zote zilizo katika kumi bora katika mechi ya 20 lakini wao washinde ndipo warejee juu ya jedwali na presha ya kutwaa ligi ipungue. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MWANAMUME mmoja wa umri wa miaka 33 aliuawa usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, kwa kupigwa na majirani wa wakwe zake baada ya kile kinadaiwa alijaribu kutekeleza mauaji katika boma hilo alimokuwa amelala na bibi yake. David Kimani alikuwa amesafiri kutoka kijiji cha Kiunyu kilichoko eneobunge la Gatanga kwa msingi kwamba alikuwa na nia ya kumuona mkewe waliyetengana, binti yake wa umri wa miaka sita na pia mama mkwe. Mwanamume huyo alikuwa ametengana na Bi Esther Nyawira, 28, kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu na katika shamrashamra za msimu huu wa sherehe, akafika kwa boma la wakwe Desemba 28, 2023, katika kijiji cha Mung’etho kilichoko eneobunge la Maragua, akisema alienda kuwajulia hali. Lakini hata baada ya giza kuingia, hakuonyesha nia ya kuondoka arejee kwao na ndipo akakubaliwa alale kwa nyumba ya mama mkwe akiwa na bibi huyo wake. Mwendo wa saa sita usiku, Kimani anasemwa kwamba aliamka na akatwaa kisu na akaanza kumshambulia bibi yake aliyekuwa amelala huku kwa sauti akiapa kumuua na kisha aue mama mkwe na pia mtoto. Kwa mujibu wa Kaimu Naibu Kamishna wa Murang’a Kusini Bw Joshua Okello, mwanamume huyo baada ya kujaribu mara kadha warejeane na bibi yake pasipo mafanikio, akaamua kufika katika boma hilo akijipamba kama malaika wa mauti. Aliongeza kwamba mshukiwa alimdunga mwanamke huyo visu vitano “mara moja umbavuni upande wa kulia na mara nne kwa mkono wa kulia, majeraha yote yakiwa matano”. Bw Okello aliongeza kwamba sauti za juu za mwanamume huyo zilimwamusha mama mkwe na alipiga nduru ambayo iliwavutia majirani waliofurika katika boma hilo huku mvamizi baada ya kuingiwa na taharuki akitimua mbio hadi nje ya nyumba na akaingia katika kichaka. “Huku mwaathiriwa akikimbizwa hadi hospitali ya Murang’a kutibiwa, majirani nao walizindua msako ulioishia kumnasa Bw Kimani akiwa amejikunyata ndani ya kichaka hicho na wakamuua kwa kumpiga kwa vifaa butu,” akasema Bw Okello. Afisa huyo aliongeza kwamba ndani ya mkoba ambao marehemu alikuwa nao kulikuwa na sumu ya kuua wadudu kwa mimea na pia waraka wa mauti unaoaminika ulikuwa umeandikwa na mwanamume huyo. “Alikuwa amefichua katika waraka huo kwamba alinuia kuua mama mkwe, bibi yake na mtoto wake wa kike aliyekuwa akiishi kwa wakwe hao na kisha yeye mwenyewe ajitoe uhai,” akasema. Mwanamume huyo alikuwa aidha ameteta kwamba mama mkwe ndiye alikuwa kizingiti cha ndoa yake kupata uthabiti na kwa kuwa hakuwa na nia ya kumpenda mwingine, akaafikia uamuzi wa kuwaua watatu hao na kisha naye ajitume kuzimu akome mahangaiko ya mapenzi. Bw Okello alisema kwamba “huu ni mkasa ambao ungeepukika iwapo mwanamume huyo ambaye alikuwa mfanyabiashara Jijini Nairobi angepata ushauri nasaha ili kuwajibika changamoto zake za kimapenzi ndani ya mashauriano”. Alisema kwamba “ndipo ifike kiwango hicho cha kupanga mauaji ni kumaanisha alikuwa akisaka mbinu ya kusuluhisha changamoto hiyo lakini akaamua kufuata ushawishi wa pepo mbaya kujipa afueni”. Huku akiwakemea waliomuua mwanamume huyo na kuahidi uchunguzi wa kunasa washukiwa, Bw Okello alisema “hata jamii inafaa kuwa macho kuwatambua wanaoonekana kusombwa na mawazo na usaidizi wa ushauri usakwe kabla ya vishawishi vya janga kuzuka”. Bw Okello alionya watu wa kijiji hicho cha Mung’etho kwamba “kwa sasa mnaweza kuwa mnasherehekea mkisema eti ni umati wa raia uliotekeleza mauaji hayo lakini wakati kutajitokeza shahidi aseme alikuona wewe ukishiriki mauaji hayo ndipo utajua ni watu binafsi wala si kundi ambalo huvunja sheria”. “Mchango wa raia katika kuimarisha usalama ni kupitia kutupasha habari kuhusu washukiwa na visa na wakimnasa mshukiwa, kazi yao inafaa tu kutuita tumtie mbaroni au wamwasilishe katika kituo cha polisi kilicho karibu,” akasema Bw Okello. Mwili wa marehemu ulipelekwa hadi mochari ya Murang’a. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MUSTAKABALI wa Kanisa Katoliki uko kwenye njia panda barani Afrika, kufuatia agizo la Papa Francis kwa mapadre katika kanisa hilo kubariki wapenzi wa jinsia moja. Ingawa lengo kuu la agizo hilo linaonekana kama njia ya kuwavutia washiriki zaidi na kutowabagua watu hao, wachambuzi na wasomi wa masuala ya dini wanasema huenda agizo hilo lilitolewa bila Papa kupewa ushauri wa kina na uongozi wa kanisa hilo. Kanisa Katoliki lina mamilioni ya washiriki hapa Kenya na barani Afrika kwa jumla. Kulingana na takwimu kutoka kwa serikali, kanisa hilo ndilo linaloongoza kwa kuwa na washiriki wengi nchini, huku likifuatwa na makanisa ya Kiprotestanti. Tangu Papa Francis alipotoa agizo hilo, viongozi tofauti wa kanisa wameeleza na kutoa hisia tofauti,  baadhi wakijitokeza wazi kulipinga. Baadhi ya viongozi wakuu ambao wamejitokeza kulipinga ni kiongozi wa kanisa hilo nchini, Askofu Philip Anyolo, ambaye pia ndiye Askofu Mkuu katika Dayosisi ya Nairobi. Kulingana na askofu huyo, agizo hilo linakinzana vikali na tamaduni za Kiafrika, hivyo hawataliruhusu. “Kiafrika, ndoa za jinsia moja hazikubaliki hata kidogo. Ndoa hizo pia zinaenda kinyume na mafunzo ya Biblia,” akasema Askofu Anyolo. Maaskofu wengine ambao wamejitokeza wazi kupinga agizo hilo ni Cornelius Odiwa wa Homa Bay na mwenzake wa dayosisi ya Eldoret, Askofu Dominic Kimengich. Askofu Odiwa alisema watafuata msimamo wa Askofu Anyolo, kwani ndiye kiongozi wa kanisa hilo nchini. Pia, alisema ndoa hizo hazikubaliki kabisa Kiafrika. Kando na viongozi wa Kanisa Katoliki, watu kutoka dini nyingine pia wameunga mkono pingamizi hizo. Baadhi yao ni Bw Samuel Kamitha, ambaye ni mwanahistoria na msomi wa masuala ya dini. Bw Kamitha pia ni mmoja wa waandalizi wakuu wa maombi maalum ambayo hufanyika Desemba 27 kila mwaka karibu na Mlima Kenya. Mnamo Jumatano, wakati wa maombi hayo, Bw Kamitha alisema hawatakubali hata kidogo tamaduni za kigeni kutumika kuharibu desturi asilia za Kiafrika. “Tunasimama kidete kupinga uhalalishaji wa ndoa za jinsia moja nchini. Hilo ni jambo linalokinzana kabisa na tamaduni zetu,” akasema. Maombi hayo yalihudhuriwa na Wakristo, Waislamu, watu wanaofuata dini za kitamaduni kati ya madhehebu mengine. Kutokana na hisia hizo, wasomi wa masuala ya dini wanasema kuwa mwelekeo huo mpya unafaa kuufungua macho uongozi wa Kanisa Katoliki kuhusu mustakabali wake barani Afrika. “Kikawaida, maagizo yote kutoka Vatican (makao makuu ya Kanisa Katoliki) huwa hayapingwi hata kidogo. Ni vigumu kusikia usemi au agizo la Papa likikosolewa au kupingwa. Hata hivyo, viongozi kadhaa wanapojitokeza wazi kupinga agizo lake, basi hiyo ni ishara wazi kuwa kuna tatizo kubwa ambalo lazima litatuliwe,” asema Dkt Rita Khamisi, ambaye ni msomi wa historia ya dini. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU SHUGHULI zilitatizika kwa muda katika uwanja wa ndege wa Manda, Kaunti ya Lamu Jumatatu jioni pale ndege ya kibinafsi iliyokuwa ikitua uwanjani humo ilipata panchari. Ndege hiyo ya kibinafsi ya kampuni ya Scenic Air Safaris ilisababisha kucheleweshwa kwa safari za ndege nyingine zilizofaa kutua na kupaa kutoka uwanjani humo majira ya saa kumi alasiri. Akithibitisha tukio hilo, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Manda Bw Felix Wanga, amesema Mamlaka ya Usimamizi Wa Viwanja vya Ndege nchini (KAA) ililazimika kuzielekeza ndege zilizofaa kutua kwa wakati huo hadi uwanja wa ndege wa Malindi, Kaunti ya Kilifi ambapo zilitua kwa muda kwa sababu ya kuzingatia usalama wa abiria waliokuwa ndegeni. Bw Wanga aidha aliwasihi wasafiri na wananchi kuwa watulivu wakati KAA ikifanya jitihada kurekebisha tatizo hilo. “Ni kweli kumekuwa na ndege ya kibinafsi iliyokuwa ikitua uwanjani Manda hivi jioni. Ilipata panchari ya gurudumu lake hivyo kukwama katikati ya uwanja. Uwanja wetu nafasi yake tayari haitoshi, hivyo haiwezekani kuruhusu ndege kutua au kupaa wakati ile iliyoharibika ikiwa uwanjani. Tumefanya mawasiliano ya haraka, ambapo ndege mbili zilizofaa kutua uwanjani Manda hivi jioni tumezielekeza kwenye uwanja wa ndege wa Malindi ambapo zitatua kwa muda wakati tukishughulikia Na kutatua tatizo lililopo. Watu wasiwe na Shaka,” akasema Bw Wanga. Tukio la kupasuka kwa gurudumu la ndege na kuikwamisha katikati ya uwanja wa ndege wa Manda limesababisha kucheleweshwa kwa safari za baadhi ya wasafiri,hasa wale waliokuwa tayari kuondoka uwanjani Manda kuelekea Nairobi na Malindi na pia wale waliokuwa wakija Lamu kutoka Nairobi. Baadhi ya abiria waliohojiwa na Taifa Leo na kudinda kutaja majina walieleza kusikitishwa kwao na tukio hilo, wakiisihi KAA kufanya hima kutatua tatizo hilo na kuruhusu safari zao kuendelea. “Haturidhishwi kamwe na mipangilio ya uwanja huu. Kama ndege imepata panchari na kukwama uwanjani,kwa nini isiburutwe Na kuwekwa kando ili kuruhusu shughuli za kawaida kuendelea uwanjani hapa. Wengine tunalazimika kukatiza mipango yetu kutokana na kucheleweshwa kwa safari na hatuoni dalili ya ni lini tatizo litatatuliwa. Hii si haki kamwe,” akasema mmoja wa maabiria. Miongoni mwa walioathiriwa na panchari ya ndege na safari zao kucheleweshwa ni watalii ambao tayari walikuwa wamekwama hotelini Lamu tangu Jumamosi pale mafuriko yaliposomba eneo la Gamba, kwenye barabara kuu ya Lamu-Witu-Garsen, hivyo kukatiza usafiri wa barabarani. Ndege iliyopata panchari ilikuwa imefikishwa Lamu kuwachukua watalii hao. “Hiki ni kisirani. Mafuriko yalitulazimu kukaa Lamu siku ya pili sasa tangu tamasha za utamaduni wa Lamu kukamilika Jumamosi usiku. Tulitarajia kufika Malindi Na Nairobi mapema lakini kisirani cha panchari nacho ndicho hiki,” akasema mmoja wa wasafiri aliyedinda kutaja jina. Si mara ya kwanza kwa ndege kukwama uwanjani Manda,kaunti ya Lamu na kupelekea safari za abiria kucheleweshwa. Mnamo Septemba 2023, ndege ya kampuni ya Jambo Jet ilikwama kwenye shimo uwanjani Manda wakati ikipaa. Hali hiyo ilizua taharuki miongoni mwa abiria waliokuwa ndani,wengine wakitaka kirika kutoka ndegeni. Hata hivyo hakuna abiria aliyejeruhiwa wakati wa tukio hilo. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU SHUGHULI zilitatizika kwa muda katika uwanja wa ndege wa Manda, Kaunti ya Lamu Jumatatu jioni pale ndege ya kibinafsi iliyokuwa ikitua uwanjani humo ilipata panchari. Ndege hiyo ya kibinafsi ya kampuni ya Scenic Air Safaris ilisababisha kucheleweshwa kwa safari za ndege nyingine zilizofaa kutua na kupaa kutoka uwanjani humo majira ya saa kumi alasiri. Akithibitisha tukio hilo, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Manda Bw Felix Wanga, amesema Mamlaka ya Usimamizi Wa Viwanja vya Ndege nchini (KAA) ililazimika kuzielekeza ndege zilizofaa kutua kwa wakati huo hadi uwanja wa ndege wa Malindi, Kaunti ya Kilifi ambapo zilitua kwa muda kwa sababu ya kuzingatia usalama wa abiria waliokuwa ndegeni. Bw Wanga aidha aliwasihi wasafiri na wananchi kuwa watulivu wakati KAA ikifanya jitihada kurekebisha tatizo hilo. “Ni kweli kumekuwa na ndege ya kibinafsi iliyokuwa ikitua uwanjani Manda hivi jioni. Ilipata panchari ya gurudumu lake hivyo kukwama katikati ya uwanja. Uwanja wetu nafasi yake tayari haitoshi, hivyo haiwezekani kuruhusu ndege kutua au kupaa wakati ile iliyoharibika ikiwa uwanjani. Tumefanya mawasiliano ya haraka, ambapo ndege mbili zilizofaa kutua uwanjani Manda hivi jioni tumezielekeza kwenye uwanja wa ndege wa Malindi ambapo zitatua kwa muda wakati tukishughulikia Na kutatua tatizo lililopo. Watu wasiwe na Shaka,” akasema Bw Wanga. Tukio la kupasuka kwa gurudumu la ndege na kuikwamisha katikati ya uwanja wa ndege wa Manda limesababisha kucheleweshwa kwa safari za baadhi ya wasafiri,hasa wale waliokuwa tayari kuondoka uwanjani Manda kuelekea Nairobi na Malindi na pia wale waliokuwa wakija Lamu kutoka Nairobi. Baadhi ya abiria waliohojiwa na Taifa Leo na kudinda kutaja majina walieleza kusikitishwa kwao na tukio hilo, wakiisihi KAA kufanya hima kutatua tatizo hilo na kuruhusu safari zao kuendelea. “Haturidhishwi kamwe na mipangilio ya uwanja huu. Kama ndege imepata panchari na kukwama uwanjani,kwa nini isiburutwe Na kuwekwa kando ili kuruhusu shughuli za kawaida kuendelea uwanjani hapa. Wengine tunalazimika kukatiza mipango yetu kutokana na kucheleweshwa kwa safari na hatuoni dalili ya ni lini tatizo litatatuliwa. Hii si haki kamwe,” akasema mmoja wa maabiria. Miongoni mwa walioathiriwa na panchari ya ndege na safari zao kucheleweshwa ni watalii ambao tayari walikuwa wamekwama hotelini Lamu tangu Jumamosi pale mafuriko yaliposomba eneo la Gamba, kwenye barabara kuu ya Lamu-Witu-Garsen, hivyo kukatiza usafiri wa barabarani. Ndege iliyopata panchari ilikuwa imefikishwa Lamu kuwachukua watalii hao. “Hiki ni kisirani. Mafuriko yalitulazimu kukaa Lamu siku ya pili sasa tangu tamasha za utamaduni wa Lamu kukamilika Jumamosi usiku. Tulitarajia kufika Malindi Na Nairobi mapema lakini kisirani cha panchari nacho ndicho hiki,” akasema mmoja wa wasafiri aliyedinda kutaja jina. Si mara ya kwanza kwa ndege kukwama uwanjani Manda,kaunti ya Lamu na kupelekea safari za abiria kucheleweshwa. Mnamo Septemba 2023, ndege ya kampuni ya Jambo Jet ilikwama kwenye shimo uwanjani Manda wakati ikipaa. Hali hiyo ilizua taharuki miongoni mwa abiria waliokuwa ndani,wengine wakitaka kirika kutoka ndegeni. Hata hivyo hakuna abiria aliyejeruhiwa wakati wa tukio hilo. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI JAMAA wa wanaume walioshtakiwa kwa wizi wa Sh94 milioni za dukakuu la QuickMart wamelia mahakamani baada ya sita hao kuachiliwa kwa dhamana ya Sh4 milioni kila mmoja. “Sasa tutatoa wapi Sh4 milioni? Watu wetu watapata taabu,” mamake mmoja wa washtakiwa hao amesikitika. Jamaa hao walikaa sakafuni huku wakilia kwa vikundi. Hakimu mkuu katika mahakama ya Milimani Lucas Onyina aliwaachilia washtakiwa hao kwa dhamana ya Sh4 milioni na mdhamini mmoja wa kiasi sawa na hicho kila mmoja. Katika uamuzi wake, Bw Onyina alisema kiwango cha pesa zilizoibwa ni kikubwa mno na polisi wanaendelea kuandama washukiwa wengine. Ijumaa wiki iliyopita, Bw Onyina aliamuru washtakiwa wazuiliwe gerezani ajifahamishe na ripoti ya urekebishaji tabia ya washtakiwa. “Nahitaji muda kusoma na kujifahamisha na ripoti za urekebishaji tabia za washukiwa wote sita ndipo niweke viwango vya dhamana,” Bw Onyina aliwaeleza washtakiwa Ijumaa. Waliofikishwa kortini kuhusiana na wizi wa pesa hizo za QuickMart ni James Mbatia Kariuki, Ismael Patrick Gitonga, Martin Nderi Ng’ang’a, Joel Oyuchi Mwelesi, Harrison Mugendi Njeru na Ronald Ouma Oluu. Sita hawa wanakabiliwa na shtaka la kula njama za kuiba Sh94,918,750 za QuickMart zilizokuwa zinapelekwa katika benki ya Family Bank mnamo Novemba 6, 2023. Washukiwa hao pia wamefunguliwa shtaka la kupatikana na zaidi ya Sh9 milioni kati ya pesa zilizoibwa. Mahakama ilifahamishwa washtakiwa hao pamoja na washtakiwa wengine ambao hawakufikishwa kortini, waliiba Sh94,918,750 kutoka kwa gari la kampuni ya Wells Fargo nambari KBA 517 T lililokuwa linapeleka pesa hizo katika benki ya Family Bank. Nderi Ng’ang’a alishtakiwa kupatikana Sh9,101,300 katika eneo la Roybain Heights kaunti ya Nairobi akijua zimeibwa ama kupatikana kwa njia isiyo halali. Patrick Gitonga na Nderi Ng’ang’a wameshtakiwa kujaribu kupindua rangi ya gari nambari KBM 751W aina ya Toyota Fielder wakijua lilikuwa likitakiwa na polisi kwa tuhuma za kubeba pesa hizo zilizoibwa. Washtakiwa walipatikana wakipaka gari hilo rangi mnamo Novemba 11, 2023, katika eneo la Mihang’o jijini Nairobi. Ismael Mbatia na Patrick Gitonga walishtakiwa kwa kupatikana na sanduku lililokuwa linabebea pesa hizo. Hakimu aliamuru idara ya magereza impeleke Gitonga hospitalini baada ya kudai alitandikwa na polisi na kupata majeraha. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI JAMAA wa wanaume walioshtakiwa kwa wizi wa Sh94 milioni za dukakuu la QuickMart wamelia mahakamani baada ya sita hao kuachiliwa kwa dhamana ya Sh4 milioni kila mmoja. “Sasa tutatoa wapi Sh4 milioni? Watu wetu watapata taabu,” mamake mmoja wa washtakiwa hao amesikitika. Jamaa hao walikaa sakafuni huku wakilia kwa vikundi. Hakimu mkuu katika mahakama ya Milimani Lucas Onyina aliwaachilia washtakiwa hao kwa dhamana ya Sh4 milioni na mdhamini mmoja wa kiasi sawa na hicho kila mmoja. Katika uamuzi wake, Bw Onyina alisema kiwango cha pesa zilizoibwa ni kikubwa mno na polisi wanaendelea kuandama washukiwa wengine. Ijumaa wiki iliyopita, Bw Onyina aliamuru washtakiwa wazuiliwe gerezani ajifahamishe na ripoti ya urekebishaji tabia ya washtakiwa. “Nahitaji muda kusoma na kujifahamisha na ripoti za urekebishaji tabia za washukiwa wote sita ndipo niweke viwango vya dhamana,” Bw Onyina aliwaeleza washtakiwa Ijumaa. Waliofikishwa kortini kuhusiana na wizi wa pesa hizo za QuickMart ni James Mbatia Kariuki, Ismael Patrick Gitonga, Martin Nderi Ng’ang’a, Joel Oyuchi Mwelesi, Harrison Mugendi Njeru na Ronald Ouma Oluu. Sita hawa wanakabiliwa na shtaka la kula njama za kuiba Sh94,918,750 za QuickMart zilizokuwa zinapelekwa katika benki ya Family Bank mnamo Novemba 6, 2023. Washukiwa hao pia wamefunguliwa shtaka la kupatikana na zaidi ya Sh9 milioni kati ya pesa zilizoibwa. Mahakama ilifahamishwa washtakiwa hao pamoja na washtakiwa wengine ambao hawakufikishwa kortini, waliiba Sh94,918,750 kutoka kwa gari la kampuni ya Wells Fargo nambari KBA 517 T lililokuwa linapeleka pesa hizo katika benki ya Family Bank. Nderi Ng’ang’a alishtakiwa kupatikana Sh9,101,300 katika eneo la Roybain Heights kaunti ya Nairobi akijua zimeibwa ama kupatikana kwa njia isiyo halali. Patrick Gitonga na Nderi Ng’ang’a wameshtakiwa kujaribu kupindua rangi ya gari nambari KBM 751W aina ya Toyota Fielder wakijua lilikuwa likitakiwa na polisi kwa tuhuma za kubeba pesa hizo zilizoibwa. Washtakiwa walipatikana wakipaka gari hilo rangi mnamo Novemba 11, 2023, katika eneo la Mihang’o jijini Nairobi. Ismael Mbatia na Patrick Gitonga walishtakiwa kwa kupatikana na sanduku lililokuwa linabebea pesa hizo. Hakimu aliamuru idara ya magereza impeleke Gitonga hospitalini baada ya kudai alitandikwa na polisi na kupata majeraha. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAM KIPLAGAT MAHAKAMA Kuu imesitisha kwa muda mpango wa serikali kuuza mashirika 11 ikiwemo jengo la Mikutano ya Kimataifa la KICC na kampuni ya Kenya Pipeline Company (KPC) baada ya kesi kuwasilishwa na chama cha Raila Odinga cha Orange Democratic Movement (ODM). Jaji Chacha Mwita ameamuru kwamba masuala yaliyoibuliwa na ODM yanaangazia masuala nyeti ya kikatiba na kisheria ambayo yana umuhimu mkubwa kwa umma na hivyo ni muhimu yaangaziwe kwa umakini mkubwa na mahakama. Jaji Mwita ameamuru ODM kumkabidhi Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetang’ula, Mwanasheria Mkuu Justin Muturi na Waziri wa Fedha Prof Njuguna Ndung’u nakala za kesi hiyo bila kupoteza muda. “Agizo la muda linatolewa kuzima utekelezaji wa kipengee 21(1) cha Sheria ya Ubinafsishaji ya 2023 na au uamuzi wowote uliofikiwa hadi Februari 6, 2024,” jaji Mwita amesema kwenye uamuzi wake. Chama cha ODM kinadai katika kesi hiyo kwamba mashirika yanayotaka kuuzwa ni ya umuhimu mkubwa kwa Wakenya na hivyo yanaweza yakauzwa tu ikiwa raia wenyewe wametoa idhini kupitia kwa kura ya maamuzi yaani refarenda. Mashirika ambayo serikali ya Kenya Kwanza inayoongozwa na Rais William Ruto inapanga kuuza ni KICC, KPC, kampuni ya maziwa ya New Kenya Cooperative Creameries (New-KCC), shirika la uchapishaji la Kenya Literature Bureau (KLB), shirika la mafuta la National Oil Corporation of Kenya (NOCK) na kampuni ya mbegu ya Kenya Seed Company Limited (KSC). Mengine ni Mwea Rice Mills Ltd (MRM), Western Kenya Rice Mills Ltd (WKRM), Numerical Machining Complex Limited (NMC), Kenya Vehicle Manufacturers Limited (KVM) na kiwanda cha nguo cha Rivatex East Africa Limited (REAL) kinachomilikiwa na Chuo Kikuu cha Moi. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAM KIPLAGAT MAHAKAMA Kuu imesitisha kwa muda mpango wa serikali kuuza mashirika 11 ikiwemo jengo la Mikutano ya Kimataifa la KICC na kampuni ya Kenya Pipeline Company (KPC) baada ya kesi kuwasilishwa na chama cha Raila Odinga cha Orange Democratic Movement (ODM). Jaji Chacha Mwita ameamuru kwamba masuala yaliyoibuliwa na ODM yanaangazia masuala nyeti ya kikatiba na kisheria ambayo yana umuhimu mkubwa kwa umma na hivyo ni muhimu yaangaziwe kwa umakini mkubwa na mahakama. Jaji Mwita ameamuru ODM kumkabidhi Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetang’ula, Mwanasheria Mkuu Justin Muturi na Waziri wa Fedha Prof Njuguna Ndung’u nakala za kesi hiyo bila kupoteza muda. “Agizo la muda linatolewa kuzima utekelezaji wa kipengee 21(1) cha Sheria ya Ubinafsishaji ya 2023 na au uamuzi wowote uliofikiwa hadi Februari 6, 2024,” jaji Mwita amesema kwenye uamuzi wake. Chama cha ODM kinadai katika kesi hiyo kwamba mashirika yanayotaka kuuzwa ni ya umuhimu mkubwa kwa Wakenya na hivyo yanaweza yakauzwa tu ikiwa raia wenyewe wametoa idhini kupitia kwa kura ya maamuzi yaani refarenda. Mashirika ambayo serikali ya Kenya Kwanza inayoongozwa na Rais William Ruto inapanga kuuza ni KICC, KPC, kampuni ya maziwa ya New Kenya Cooperative Creameries (New-KCC), shirika la uchapishaji la Kenya Literature Bureau (KLB), shirika la mafuta la National Oil Corporation of Kenya (NOCK) na kampuni ya mbegu ya Kenya Seed Company Limited (KSC). Mengine ni Mwea Rice Mills Ltd (MRM), Western Kenya Rice Mills Ltd (WKRM), Numerical Machining Complex Limited (NMC), Kenya Vehicle Manufacturers Limited (KVM) na kiwanda cha nguo cha Rivatex East Africa Limited (REAL) kinachomilikiwa na Chuo Kikuu cha Moi. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU NDEGE ya kibinafsi yakwama katika uwanja wa ndege wa Manda wakati ikijiandaa kupaa baada ya tairi kupata panchari. Abiria katika ndege hiyo wamelazimika kuchelewesha safari yao.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU NDEGE ya kibinafsi yakwama katika uwanja wa ndege wa Manda wakati ikijiandaa kupaa baada ya tairi kupata panchari. Abiria katika ndege hiyo wamelazimika kuchelewesha safari yao.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI ALIYEKUWA Mbunge wa Kabete George Muchai, walinzi wake wawili, na dereva wake waliuawa na majambazi waliotumia bunduki ya serikali aina ya G3 ambayo walimnyang’anya polisi mwaka 2014 katika eneo la Kitisuru, Nairobi. Mahakama imeambiwa Muchai aliuawa chini ya nusu dakika na jambazi aliyekuwa amekubuhu kwa uhalifu. Muchai, walinzi wake Konstebo Samwel Lekakeny na Konstebo Samwel Kimathi na dereva wake Stephen Wambugu, walimiminiwa risasi tano na jambazi Eric Isabwa almaarufu Chairman kando ya barabara ya Kenyatta Avenue katika eneo mkabala na GPO Februari 7, 2015. Akitoa ushahidi mbele ya Jaji Kanyi Kimondo, afisa wa upelelezi wa jina Sajini Moses Otiu Opiyo, alifichua kwamba bunduki  iliyotumika kuwaangamiza Muchai, Lekakeny, Kimathi na Wambugu ilikuwa imenyang’anywa kutoka kwa Koplo Patrick Wamae mnamo Oktoba 2014 katika eneo la Kitisuru akilinda jengo la serikali. Sajini Opiyo alieleza Jaji huyo bunduki hiyo ya G3 na bastola aliyong’anywa Konstebo Lekakeny ndizo silaha zilizopatikana katika makazi ya Isabwa na mkewe Margaret Njeri. Polisi walipata bunduki hiyo katika makazi ya Isabwa na Njeri yaliyoko Kinoo. Sajini Opiyo alieleza mahakama kwamba Isamba na jambazi mwingine Raphael Kimani walikuwa wamevalia maski kwenye nyuso zao walipomwangamiza Muchai ambaye wakati huo alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini-COTU. Baada ya kuwaua wanne hao, Isabwa na Kimani walimpigia dereva wa teksi simu kuwaondoa haraka. “Baada ya mauaji ya Muchai na wenzake, Kimani alimpigia simu dereva wa teksi kuja kuwachukua kutoka GPO,” alisema Sajini Opiyo. Afisa huyo wa upelelezi alimweleza Jaji Kanyi Kimondo kwamba Isabwa na Kimani wako na rekodi ya kufungwa miaka minane gerezani kwa wizi wa mabavu. “Nilichunguza kutoka kwa idara ya kupeleleza uhalifu na kupata historia ya Isabwa na Kimani kwamba waliwahi kufungwa jela kwa wizi wa mabavu,” Sajini Opiyo alimweleza Jaji Kimondo. Mbali na Isabwa, Kimani na Njeri, washtakiwa wengine ni Simon Wambugu Gachamba, Stephen Lipapa, Mustafa Maina Wanyonyi na Jane Wanjiru almaarufu Shiro. Walipokamatwa, polisi walimpata Isabwa na simu 10 za kiunga mbali, Wanjiru naye alikuwa na simu 14  za kiunga mbali na Kimani alikuwa na simu 10. Washtakiwa hao saba wamekana waliwaua Muchai, Lekakeny, Kimathi, na Wambugu. Washukiwa hao wa ujambazi walikuwa wamewateka nyara watu watatu na kuwasukuma ndani ya buti ya gari yao muundo wa Mercedes Benz. Walitumia Benz hiyo kuwaandama Muchai na wenzake kutoka Westlands alipokuwa ameenda kumnunulia mkewe na watu wengine wa familia yake maankuli ya jioni. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI ALIYEKUWA Mbunge wa Kabete George Muchai, walinzi wake wawili, na dereva wake waliuawa na majambazi waliotumia bunduki ya serikali aina ya G3 ambayo walimnyang’anya polisi mwaka 2014 katika eneo la Kitisuru, Nairobi. Mahakama imeambiwa Muchai aliuawa chini ya nusu dakika na jambazi aliyekuwa amekubuhu kwa uhalifu. Muchai, walinzi wake Konstebo Samwel Lekakeny na Konstebo Samwel Kimathi na dereva wake Stephen Wambugu, walimiminiwa risasi tano na jambazi Eric Isabwa almaarufu Chairman kando ya barabara ya Kenyatta Avenue katika eneo mkabala na GPO Februari 7, 2015. Akitoa ushahidi mbele ya Jaji Kanyi Kimondo, afisa wa upelelezi wa jina Sajini Moses Otiu Opiyo, alifichua kwamba bunduki  iliyotumika kuwaangamiza Muchai, Lekakeny, Kimathi na Wambugu ilikuwa imenyang’anywa kutoka kwa Koplo Patrick Wamae mnamo Oktoba 2014 katika eneo la Kitisuru akilinda jengo la serikali. Sajini Opiyo alieleza Jaji huyo bunduki hiyo ya G3 na bastola aliyong’anywa Konstebo Lekakeny ndizo silaha zilizopatikana katika makazi ya Isabwa na mkewe Margaret Njeri. Polisi walipata bunduki hiyo katika makazi ya Isabwa na Njeri yaliyoko Kinoo. Sajini Opiyo alieleza mahakama kwamba Isamba na jambazi mwingine Raphael Kimani walikuwa wamevalia maski kwenye nyuso zao walipomwangamiza Muchai ambaye wakati huo alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini-COTU. Baada ya kuwaua wanne hao, Isabwa na Kimani walimpigia dereva wa teksi simu kuwaondoa haraka. “Baada ya mauaji ya Muchai na wenzake, Kimani alimpigia simu dereva wa teksi kuja kuwachukua kutoka GPO,” alisema Sajini Opiyo. Afisa huyo wa upelelezi alimweleza Jaji Kanyi Kimondo kwamba Isabwa na Kimani wako na rekodi ya kufungwa miaka minane gerezani kwa wizi wa mabavu. “Nilichunguza kutoka kwa idara ya kupeleleza uhalifu na kupata historia ya Isabwa na Kimani kwamba waliwahi kufungwa jela kwa wizi wa mabavu,” Sajini Opiyo alimweleza Jaji Kimondo. Mbali na Isabwa, Kimani na Njeri, washtakiwa wengine ni Simon Wambugu Gachamba, Stephen Lipapa, Mustafa Maina Wanyonyi na Jane Wanjiru almaarufu Shiro. Walipokamatwa, polisi walimpata Isabwa na simu 10 za kiunga mbali, Wanjiru naye alikuwa na simu 14  za kiunga mbali na Kimani alikuwa na simu 10. Washtakiwa hao saba wamekana waliwaua Muchai, Lekakeny, Kimathi, na Wambugu. Washukiwa hao wa ujambazi walikuwa wamewateka nyara watu watatu na kuwasukuma ndani ya buti ya gari yao muundo wa Mercedes Benz. Walitumia Benz hiyo kuwaandama Muchai na wenzake kutoka Westlands alipokuwa ameenda kumnunulia mkewe na watu wengine wa familia yake maankuli ya jioni. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA TITUS OMINDE SERIKALI kupitia kwa Idara ya Elimu na Mafunzo ya kiufundi itatoa ufadhili wa kima cha Sh8.8 bilioni kwa taasisi 70 za TVET kote nchini. Ufadhili huo ni pamoja na ununuzi wa vifaa vya kisasa, upanuzi, na ujenzi wa miundomsingi miongoni mwa matakwa mengine. Katibu katika idara ya TVET Esther Muoria alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa taasisi zote za umma za TVET zimewekewa vifaa vya kisasa. Hatua hiyo inapania kukabilia na uhaba wa wafanyakazi wenye ujuzi wa kiufundi katika sekta mbalimbali nchini. Bi Muoria alisema kuwa taasisi nyingi za TVET zinakabiliwa na uhaba wa vifaa, jambo ambalo linatatiza huduma kutoka kwa wafanyakazi wenye ujuzi wa kiufundi. Alipokuwa akizungumza katika Chuo cha kiufundi cha Kitaifa cha Eldoret Bi Muoria alikariri kujitolea kwa serikali kuhakikisha taasisi za Tvet zina vifaa na mashine bora za kutoa mafunzo ambayo yanaweza kuandana na viwango vya tasnia husika. “Serikali imeanzisha mpango kabambe wa kununua vifaa vya kisasa vya mafunzo kwa taasisi 70 za TVET kwa gharama ya Sh8.8 bilioni ili kuongeza watu wenye ujuzi tayari kujiunga na soko la ajira,” alisema Bi Muoria. Katibu huyo alisema hayo katika taasisi ya kiufundi ya Eldoret National Polytechnic katika Kaunti ya Uasin Gishu ambapo aliongoza kufungwa kwa warsha ya siku tatu ya wasimamizi wa taasisi za kitaifa za mafunzo ya TVET, na wafanyakazi wakuu wa kiufundi na wakuu wa idara lengwa kutoka Rift Valley. Bi Muoria alitoa changamoto kwa wanafunzi kunufaika na mpango wa serikali wa kuzipa taasisi za TVET mashine na vifaa vya hali ya juu ili kutoa mafunzo ya ustadi wa hali ya juu kukimu matakwa ya walengwa na kubuni ajira katika sekta mbalimbali nchini na katika viwango vya kitaifa. Wizara hiyo inapania kushirikiana na wadau wote kutafutia wahitimu nafasi za ajira katika ngazi ya kitaifa. “Serikali iko tayari kuwaunganisha wahitimu waliofaulu kutoka taasisi za TVET na soko la ajira ndani na nje ya nchi na pia kuwasaidia kupata mapato kutokana na ujuzi husika,” aliongeza Bi Muoria. Anasema TVET huwa na jukumu muhimu katika kuwezesha vijana kupata mafunzo ya kiufundi ambayo yatawasaidia kushiriki katika ukuaji wa uchumi wa nchi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA TITUS OMINDE SERIKALI kupitia kwa Idara ya Elimu na Mafunzo ya kiufundi itatoa ufadhili wa kima cha Sh8.8 bilioni kwa taasisi 70 za TVET kote nchini. Ufadhili huo ni pamoja na ununuzi wa vifaa vya kisasa, upanuzi, na ujenzi wa miundomsingi miongoni mwa matakwa mengine. Katibu katika idara ya TVET Esther Muoria alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa taasisi zote za umma za TVET zimewekewa vifaa vya kisasa. Hatua hiyo inapania kukabilia na uhaba wa wafanyakazi wenye ujuzi wa kiufundi katika sekta mbalimbali nchini. Bi Muoria alisema kuwa taasisi nyingi za TVET zinakabiliwa na uhaba wa vifaa, jambo ambalo linatatiza huduma kutoka kwa wafanyakazi wenye ujuzi wa kiufundi. Alipokuwa akizungumza katika Chuo cha kiufundi cha Kitaifa cha Eldoret Bi Muoria alikariri kujitolea kwa serikali kuhakikisha taasisi za Tvet zina vifaa na mashine bora za kutoa mafunzo ambayo yanaweza kuandana na viwango vya tasnia husika. “Serikali imeanzisha mpango kabambe wa kununua vifaa vya kisasa vya mafunzo kwa taasisi 70 za TVET kwa gharama ya Sh8.8 bilioni ili kuongeza watu wenye ujuzi tayari kujiunga na soko la ajira,” alisema Bi Muoria. Katibu huyo alisema hayo katika taasisi ya kiufundi ya Eldoret National Polytechnic katika Kaunti ya Uasin Gishu ambapo aliongoza kufungwa kwa warsha ya siku tatu ya wasimamizi wa taasisi za kitaifa za mafunzo ya TVET, na wafanyakazi wakuu wa kiufundi na wakuu wa idara lengwa kutoka Rift Valley. Bi Muoria alitoa changamoto kwa wanafunzi kunufaika na mpango wa serikali wa kuzipa taasisi za TVET mashine na vifaa vya hali ya juu ili kutoa mafunzo ya ustadi wa hali ya juu kukimu matakwa ya walengwa na kubuni ajira katika sekta mbalimbali nchini na katika viwango vya kitaifa. Wizara hiyo inapania kushirikiana na wadau wote kutafutia wahitimu nafasi za ajira katika ngazi ya kitaifa. “Serikali iko tayari kuwaunganisha wahitimu waliofaulu kutoka taasisi za TVET na soko la ajira ndani na nje ya nchi na pia kuwasaidia kupata mapato kutokana na ujuzi husika,” aliongeza Bi Muoria. Anasema TVET huwa na jukumu muhimu katika kuwezesha vijana kupata mafunzo ya kiufundi ambayo yatawasaidia kushiriki katika ukuaji wa uchumi wa nchi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA JOSEPH OPENDA CHAMA cha United Democratic Alliance (UDA) kimetisha kuwachukulia hatua za kinidhamu wanachama watakaopatikana wakipinga msimamo wa serikali. Katibu Mkuu wa Chama hicho, Cleophas Malala, amesisitiza kuwa UDA imejitolea kwa dhati kumuunga mkono kiongozi wake, Rais William Ruto. Amewaonya wanachama dhidi ya kupigia debe ajenda zinazokinzana na msimamo wa serikali kuhusu masuala mbalimbali akisema wanachama kama hao wamekosa kuelewa mipango ya serikali na manifesto ya chama hicho walichochaguliwa kwa tikiti yake. “Kiongozi wetu amekuwa akifanya kazi kwa bidii kutekeleza miradi inayolenga kuokoa taifa hili kutokana na uchumi kuzorota lakini tuna wanachama ambao hawaelewi hivi. Wamekuwa wakipinga hadharani misimamo na miradi ya serikali. Hatutastahimili wanachama wa UDA wanaopinga miradi ya serikali. Kuanzia sasa, tutaanzisha mikakati ya ndani kwa ndani kukabiliana na wanachama kama hao,” alitahadharisha Bw Malala. Alizungumza haya katika uzinduzi wa afisi za chama hicho jijini Nakuru ambapo alisema UDA imebuni mifumo inayopaswa kutumiwa na wanachama kuwasilisha malalamishi, ikiwemo mkutano wa kundi la bunge. Alisema hatua ya kuahirisha uchaguzi za mashinani ilinuiwa kutoa nafasi kwa usajili wa wanachama zaidi. Alifichua kuwa majadiliano yanaendelea kwa vyama tanzu vya Kenya Kwanza kuvunjwa ili kuunda chama kimoja. “Tunataka kuwa na chama kimoja imara sawa na Chama cha Kikomunisti nchini China. Tunashiriki mazungumzo na vyama tanzu ili kuvishawishi kuvunjiliwa mbali vyama na kujiunga na UDA,” alisema. Kuhusu ushirikiano na Chama cha Kikomunisti cha China, Bw Malala alisema unalenga kuwezesha mchakato wa haki katika uchaguzi kidijitali na usaidizi katika kubuni afisi za kisasa za makao makuu ya UDA. “Tayari tumenunua ardhi ya kujenga afisi ya kisasa ambayo vilevile itakuwa na shule ya UDA kuhusu uongozi ili kuwapa mwongozo vijana wachanga watakaorithi kizazi cha sasa cha viongozi,” alisema. Bw Malala alisisitiza msimamo wa chama hicho wa kupinga kura ya maamuzi iliyopendekezwa na muungano wa Azimio la Umoja, akisema mapendekezo yote yatatekelezwa kupitia Bunge. Gavana wa Nakuru, Susan Kihika naye aliwataka wanachama wanaopinga miradi ya chama hicho kujiuzulu na kutafuta mamlaka mapya kupitia vyama vingine. Alikashifu upinzani kwa kujaribu kurejesha nchi katika hali ya uchaguzi kupitia kura ya maamuzi. “Hatuna muda wala nguvu ya kuruhusu wazo la kura ya maamuzi tunaposhughulika na uchumi wetu. Lakini iwapo itafanyika, msimamo wetu utasalia ulivyokuwa wakati wa Mpango wa Maridhiano (BBI),” alisema Gavana Kihika. Kenya Kwanza ilipinga kura ya maamuzi iliyopendekezwa katika BBI. Kiongozi wa Wajumbe wa Chama cha Kikomunisti China, Mao Ding Zhi, alielezea kujitolea kwa chama hicho kufanya kazi na UDA.
Tags
You can share this post!
Previous article
COP28: Wanaharakati wakubaliwa kuandamana kupinga matumizi...
Next article
Mashirika yapigania haki ya ‘boychild’ visa vya...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA JOSEPH OPENDA CHAMA cha United Democratic Alliance (UDA) kimetisha kuwachukulia hatua za kinidhamu wanachama watakaopatikana wakipinga msimamo wa serikali. Katibu Mkuu wa Chama hicho, Cleophas Malala, amesisitiza kuwa UDA imejitolea kwa dhati kumuunga mkono kiongozi wake, Rais William Ruto. Amewaonya wanachama dhidi ya kupigia debe ajenda zinazokinzana na msimamo wa serikali kuhusu masuala mbalimbali akisema wanachama kama hao wamekosa kuelewa mipango ya serikali na manifesto ya chama hicho walichochaguliwa kwa tikiti yake. “Kiongozi wetu amekuwa akifanya kazi kwa bidii kutekeleza miradi inayolenga kuokoa taifa hili kutokana na uchumi kuzorota lakini tuna wanachama ambao hawaelewi hivi. Wamekuwa wakipinga hadharani misimamo na miradi ya serikali. Hatutastahimili wanachama wa UDA wanaopinga miradi ya serikali. Kuanzia sasa, tutaanzisha mikakati ya ndani kwa ndani kukabiliana na wanachama kama hao,” alitahadharisha Bw Malala. Alizungumza haya katika uzinduzi wa afisi za chama hicho jijini Nakuru ambapo alisema UDA imebuni mifumo inayopaswa kutumiwa na wanachama kuwasilisha malalamishi, ikiwemo mkutano wa kundi la bunge. Alisema hatua ya kuahirisha uchaguzi za mashinani ilinuiwa kutoa nafasi kwa usajili wa wanachama zaidi. Alifichua kuwa majadiliano yanaendelea kwa vyama tanzu vya Kenya Kwanza kuvunjwa ili kuunda chama kimoja. “Tunataka kuwa na chama kimoja imara sawa na Chama cha Kikomunisti nchini China. Tunashiriki mazungumzo na vyama tanzu ili kuvishawishi kuvunjiliwa mbali vyama na kujiunga na UDA,” alisema. Kuhusu ushirikiano na Chama cha Kikomunisti cha China, Bw Malala alisema unalenga kuwezesha mchakato wa haki katika uchaguzi kidijitali na usaidizi katika kubuni afisi za kisasa za makao makuu ya UDA. “Tayari tumenunua ardhi ya kujenga afisi ya kisasa ambayo vilevile itakuwa na shule ya UDA kuhusu uongozi ili kuwapa mwongozo vijana wachanga watakaorithi kizazi cha sasa cha viongozi,” alisema. Bw Malala alisisitiza msimamo wa chama hicho wa kupinga kura ya maamuzi iliyopendekezwa na muungano wa Azimio la Umoja, akisema mapendekezo yote yatatekelezwa kupitia Bunge. Gavana wa Nakuru, Susan Kihika naye aliwataka wanachama wanaopinga miradi ya chama hicho kujiuzulu na kutafuta mamlaka mapya kupitia vyama vingine. Alikashifu upinzani kwa kujaribu kurejesha nchi katika hali ya uchaguzi kupitia kura ya maamuzi. “Hatuna muda wala nguvu ya kuruhusu wazo la kura ya maamuzi tunaposhughulika na uchumi wetu. Lakini iwapo itafanyika, msimamo wetu utasalia ulivyokuwa wakati wa Mpango wa Maridhiano (BBI),” alisema Gavana Kihika. Kenya Kwanza ilipinga kura ya maamuzi iliyopendekezwa katika BBI. Kiongozi wa Wajumbe wa Chama cha Kikomunisti China, Mao Ding Zhi, alielezea kujitolea kwa chama hicho kufanya kazi na UDA.
Tags
You can share this post!
Previous article
COP28: Wanaharakati wakubaliwa kuandamana kupinga matumizi...
Next article
Mashirika yapigania haki ya ‘boychild’ visa vya...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA JACOB WALTER Akiwa DUBAI, UAE HATIMAYE wanaharakati wamekubaliwa kuandamana jijini Dubai katika Milki za Kiarabu (UAE) ili kutoa malalamishi yao kuhusiana na michakato kadhaa inayojadiliwa kwenye kongamano la Umoja wa Mataifa la COP28. Maandamano yalianza Jumamosi ambapo wakereketwa wa haki za kibinadamu walitaka ukomeshaji wa mauaji ya raia wa Palestina katika eneo la ukanda wa Gaza katika uvamizi ambao umekuwa ukiendelezwa na Israel dhidi ya Hamas. Aidha, Jumapili wanaharakati kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Kenya, walihanikiza sauti zao wakitaka utekelezwaji upesi wa ukomeshaji wa uchafuzi wa hewa na mazingira unaoendelezwa na mataifa tajiri duniani. Maandamano hayo yamefanyika pia Jumatatu asubuhi. Wakibeba mabango yalioandikwa ‘no more fossil fuels’ kumaanisha hukupswi kuwepo tena kwa mafuta ya visukuku na ‘let Lake Victoria Breathe Again’ kumaanisha ‘acha Ziwa Victoria lipumue tena’, wanaharakati hao walipata nafasi ya kuelezea malalamishi yao kwa umma kwa muda wa saa moja. Akiongea na Taifa Leo, mwanaharakati na Afisa Mkuu Mtendaji wa shirika la Eurogroup for Animal tawi la Kisumu Miriam Wanjiku ameeleza kuwa wanaharakati hao walilazimika kupaza sauti zao kulalamikia kile walisema ni misimamo isiyoaminika kuhusu kupigwa marufuku kwa aina za kawi zenye athari kubwa kwa uchafuzi wa mazingira. Amesikitika kuwa athari za mabadiliko ya tabianchi zimeendelea kufanya maisha kuwa magumu zaidi kwa mataifa maskini. “Nasikitika kuwa mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuathiri pakubwa wananchi hohehahe katika mataifa ambayo ndiyo yanajaribu kuinukia kama Kenya ilhali hawapati fidia. Hii ndiyo sababu yetu kusisitiza kuwa sharti waathiriwa sasa wapate fidia na pia ni sharti mataifa yote yakome kutumia kawi ya visukuku,” akaeleza Bi Wanjiku. Maisha ya viumbe hai yameendelea kudorora kutoka kwa binadamu ,wanyama na miti na mimea mingine kutokana na uchafuzi unaoendelezwa na nchi zinazojiweza kiuchumi kupitia kwa gesi zenye sumu kama hewa ukaa na vichafuzi vinginevyo kulingana na mwanaharakati huyo. Alitoa mfano wa jinsi Ziwa Victoria linavyozidi kuchafuka na kusababisha hata aina za samaki waliojulikana kwa muda mrefu, kuanza kudidimia kwa kasi mno. Mifumo yote ya maji kama maziwa, bahari, chemchemi na mito imeathirika pia, huku maisha ya viumbe hai yakiwa taabani. Kaulimbiu yake katika maandamano ni ‘Ruhusuni Ziwa Victoria kupumua tena’. Aidha Bi Wanjiru amesikitika kuwa maisha ya mianzi ya matumbawe (coral reefs) katika Bahari Hindi pia ni ya kuzua hofu akisema kuwa uchafuzi wa mazingira ndio wa kulaumiwa. Haya yanapojiri, baadhi ya wanasayansi kutoka Kenya pia wameeleza kutoridhishwa kwao na hatua zilizochukuliwa na mataifa yanayojiweza katika ukomeshaji wa matumizi ya kawi ya visukuku (fossil fuel). Amesikitikia sana kuongezeka kwa majanga yanayosababishwa na tabia nchi kama mafuriko na ukame yameendelea kuongezeka katika bara la Afrika. Amesikitika kuwa hatima ya vizazi vijavyo iko taabani endapo viongozi wa leo watakosa kutimiza malengo yaliyowekwa. Mwanasayansi  wa mazingira kutoka jijini Kisumu Bw Clifford Omondi, ameonya kuwa hali itazidi kudorora zaidi endapo mataifa tajiri yatakosa kuharakisha ukomeshaji wa matumizi ya kawi ya visukuku. Bw Omondi pia ametoa changamoto kuhusu ahadi za fedha za kufidia waathirika wa mabadiliko ya tabianchi chini ya mpango wa ‘Loss and Damage Fund’ akidai huenda ukawa ahadi tupu za kufumba macho mataifa maskini na akataka mataifa tajiri kutimiza ahadi zao upesi. “Hatutasalia na sayari hii tena endapo juhudi za kukomesha matumizi ya mafuta ya visukuku hazitapigiwa jeki,” Bw Omondi akasema. Kulingana na ripoti ya Shirika la Mpango wa Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) kuhusu kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (Climate Adaptation) iliyotangazwa katika COP28, ni kuwa mwaka wa 2022 ndiyo ulikuwa mwaka wa sita kuwa na joto zaidi juu ya viwango vilivyoripotiwa katika karne ya 20 na tangu mwaka wa 1880. UAE hujulikana kwa sheria kali zinazozuia maandamano ya wafanyakazi, wanaharakati na hata maandamano ya kisiasa. Kutumia hata mabango yoyote katika nchi hiyo, sharti watu au mashirika yapate idhini ya serikali. Hofu ilitandaa kabla ya kongamano hilo huku wanaharakati wengi wa mabadiliko ya tabianchi wakihofia kuwa wangezuiliwa kufanya maandamano yao kuhusu mapengo mengi ambayo bado yapo kwenye vita dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Mnamo Desemba 2, 2023, zaidi ya mataifa 117 yalitia saini mkataba wa kutaka kukomesha matumizi ya mafuta ya visukuku ifikapo mwaka wa 2050. Matifa hayo ni pamoja na Brazil, Nigeria, Australia, Japan, Canada, Chile, na Barbados. Hata hivyo, mataifa ya China na India yalitoa tu kiashiria kuwa huenda yakakomesha matumizi ya mafuta hayo ifikapo mwaka wa 2030. Kulingana na mkataba ulioafikiwa na viongozi wa kimataifa katika kongmano na COP28, mataifa yote yanatarajiwa kuungana katika kupunguza gesi ya kaboni kwa aslimia 43 ifikapo mwaka wa 2030. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA JACOB WALTER Akiwa DUBAI, UAE HATIMAYE wanaharakati wamekubaliwa kuandamana jijini Dubai katika Milki za Kiarabu (UAE) ili kutoa malalamishi yao kuhusiana na michakato kadhaa inayojadiliwa kwenye kongamano la Umoja wa Mataifa la COP28. Maandamano yalianza Jumamosi ambapo wakereketwa wa haki za kibinadamu walitaka ukomeshaji wa mauaji ya raia wa Palestina katika eneo la ukanda wa Gaza katika uvamizi ambao umekuwa ukiendelezwa na Israel dhidi ya Hamas. Aidha, Jumapili wanaharakati kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Kenya, walihanikiza sauti zao wakitaka utekelezwaji upesi wa ukomeshaji wa uchafuzi wa hewa na mazingira unaoendelezwa na mataifa tajiri duniani. Maandamano hayo yamefanyika pia Jumatatu asubuhi. Wakibeba mabango yalioandikwa ‘no more fossil fuels’ kumaanisha hukupswi kuwepo tena kwa mafuta ya visukuku na ‘let Lake Victoria Breathe Again’ kumaanisha ‘acha Ziwa Victoria lipumue tena’, wanaharakati hao walipata nafasi ya kuelezea malalamishi yao kwa umma kwa muda wa saa moja. Akiongea na Taifa Leo, mwanaharakati na Afisa Mkuu Mtendaji wa shirika la Eurogroup for Animal tawi la Kisumu Miriam Wanjiku ameeleza kuwa wanaharakati hao walilazimika kupaza sauti zao kulalamikia kile walisema ni misimamo isiyoaminika kuhusu kupigwa marufuku kwa aina za kawi zenye athari kubwa kwa uchafuzi wa mazingira. Amesikitika kuwa athari za mabadiliko ya tabianchi zimeendelea kufanya maisha kuwa magumu zaidi kwa mataifa maskini. “Nasikitika kuwa mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuathiri pakubwa wananchi hohehahe katika mataifa ambayo ndiyo yanajaribu kuinukia kama Kenya ilhali hawapati fidia. Hii ndiyo sababu yetu kusisitiza kuwa sharti waathiriwa sasa wapate fidia na pia ni sharti mataifa yote yakome kutumia kawi ya visukuku,” akaeleza Bi Wanjiku. Maisha ya viumbe hai yameendelea kudorora kutoka kwa binadamu ,wanyama na miti na mimea mingine kutokana na uchafuzi unaoendelezwa na nchi zinazojiweza kiuchumi kupitia kwa gesi zenye sumu kama hewa ukaa na vichafuzi vinginevyo kulingana na mwanaharakati huyo. Alitoa mfano wa jinsi Ziwa Victoria linavyozidi kuchafuka na kusababisha hata aina za samaki waliojulikana kwa muda mrefu, kuanza kudidimia kwa kasi mno. Mifumo yote ya maji kama maziwa, bahari, chemchemi na mito imeathirika pia, huku maisha ya viumbe hai yakiwa taabani. Kaulimbiu yake katika maandamano ni ‘Ruhusuni Ziwa Victoria kupumua tena’. Aidha Bi Wanjiru amesikitika kuwa maisha ya mianzi ya matumbawe (coral reefs) katika Bahari Hindi pia ni ya kuzua hofu akisema kuwa uchafuzi wa mazingira ndio wa kulaumiwa. Haya yanapojiri, baadhi ya wanasayansi kutoka Kenya pia wameeleza kutoridhishwa kwao na hatua zilizochukuliwa na mataifa yanayojiweza katika ukomeshaji wa matumizi ya kawi ya visukuku (fossil fuel). Amesikitikia sana kuongezeka kwa majanga yanayosababishwa na tabia nchi kama mafuriko na ukame yameendelea kuongezeka katika bara la Afrika. Amesikitika kuwa hatima ya vizazi vijavyo iko taabani endapo viongozi wa leo watakosa kutimiza malengo yaliyowekwa. Mwanasayansi  wa mazingira kutoka jijini Kisumu Bw Clifford Omondi, ameonya kuwa hali itazidi kudorora zaidi endapo mataifa tajiri yatakosa kuharakisha ukomeshaji wa matumizi ya kawi ya visukuku. Bw Omondi pia ametoa changamoto kuhusu ahadi za fedha za kufidia waathirika wa mabadiliko ya tabianchi chini ya mpango wa ‘Loss and Damage Fund’ akidai huenda ukawa ahadi tupu za kufumba macho mataifa maskini na akataka mataifa tajiri kutimiza ahadi zao upesi. “Hatutasalia na sayari hii tena endapo juhudi za kukomesha matumizi ya mafuta ya visukuku hazitapigiwa jeki,” Bw Omondi akasema. Kulingana na ripoti ya Shirika la Mpango wa Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) kuhusu kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (Climate Adaptation) iliyotangazwa katika COP28, ni kuwa mwaka wa 2022 ndiyo ulikuwa mwaka wa sita kuwa na joto zaidi juu ya viwango vilivyoripotiwa katika karne ya 20 na tangu mwaka wa 1880. UAE hujulikana kwa sheria kali zinazozuia maandamano ya wafanyakazi, wanaharakati na hata maandamano ya kisiasa. Kutumia hata mabango yoyote katika nchi hiyo, sharti watu au mashirika yapate idhini ya serikali. Hofu ilitandaa kabla ya kongamano hilo huku wanaharakati wengi wa mabadiliko ya tabianchi wakihofia kuwa wangezuiliwa kufanya maandamano yao kuhusu mapengo mengi ambayo bado yapo kwenye vita dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Mnamo Desemba 2, 2023, zaidi ya mataifa 117 yalitia saini mkataba wa kutaka kukomesha matumizi ya mafuta ya visukuku ifikapo mwaka wa 2050. Matifa hayo ni pamoja na Brazil, Nigeria, Australia, Japan, Canada, Chile, na Barbados. Hata hivyo, mataifa ya China na India yalitoa tu kiashiria kuwa huenda yakakomesha matumizi ya mafuta hayo ifikapo mwaka wa 2030. Kulingana na mkataba ulioafikiwa na viongozi wa kimataifa katika kongmano na COP28, mataifa yote yanatarajiwa kuungana katika kupunguza gesi ya kaboni kwa aslimia 43 ifikapo mwaka wa 2030. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RUSHDIE OUDIA VIONGOZI wa Azimio sasa wanataka vinara wao Raila Odinga na Kalonzo Musyoka wadumishe umoja na ushirikiano wao hadi wakati wa uchaguzi mkuu wa 2027.  Wanasiasa wa muungano huo pia wamewataka wabunge, maseneta magavana na madiwani wawe imara na kusalia Azimio na kupuuza vishawishi vya muungano tawala wa Kenya Kwanza. Gavana wa Siaya, James Orengo na Kiongozi wa Wachache Bungeni, Opiyo Wandayi, wikendi walimiminia sifa Bw Musyoka wakimshukuru kwa kumuunga mkono Bw Odinga katika chaguzi za 2013, 2017 na 2022. “Tunakushukuru sana Kalonzo kwa kusalia imara. Ulikuwa nasi wakati wa maandamano Nairobi na hatutakusahau daima. Kama Waluo, huwa tunafahamu kiongozi kwa kuangalia iwapo ni jasiri, ana uwazi na pia hababaiki,” akasema Bw Wandayi. Bw Orengo naye alimsifia kinara huyo wa Wiper akisema kweli amesimama na Bw Odinga na hakika ni rafiki wa kweli. “Kalonzo tunakukaribisha Gem. Umesimama nasi kwa kipindi kirefu na hili ni jambo ambalo hatutalisahau,” akasema Gavana Orengo. Bw Musyoka naye aliwataka watu wa Nyanza wasipoteze imani na waendelee kuwapigania Wakenya. Alikuwa pamoja na wanasiasa hao pamoja na mkewe Bw Odinga, Mama Idah (mkewe Raila Odinga), katika eneo la Wagai, eneobunge la Gem wakati wa mchango kwa kundi kituo kimoja cha elimu. “Endeleeni kuwa jasiri. Tumekuja kuwapa moyo muendelee kuwa na ujasiri kama Jakom (Raila). Tumepokonywa ushindi mara tatu ila tusikate tamaa na tulinde demokrasia yetu,” akasema Bw Musyoka. Makamu huyo wa rais wa zamani aliongeza kuwa Bw Odinga ameendelea kukosoa serikali na akaahidi kuendelea kushirikiana naye kisiasa. Aliyekuwa Kiongozi wa Mungiki, Maina Njenga ambaye aliandamana na Bw Musyoka, aliwataka viongozi wa Azimio wasalie imara, akisema hiyo ndiyo njia pekee ya kuiondoa Kenya Kwanza 2027. “Lazima tusalie tumeungana jinsi ilivyokuwa wakati wa maandamano. Sielewi Raila anasubiri nini kwa sababu tuko tayari kurejea barabarani,” akasema Bw Njenga. Viongozi wa Ukambani walioandamana na Bw Musyoka ni wabunge Robert Mbui (Kathiani), Stephen Mule (Matungulu), Mbunge Mwakilishi wa Kitui Irene Kasalu na Spika wa Kaunti ya Makueni, Douglas Mwilu. Wakati wa hafla hiyo, Bi Odinga alimshutumu Mbunge wa Gem, Elisha Odhiambo, ambaye anashirikiana na Kenya Kwanza licha ya kuchaguliwa kwa tikiti ya ODM. Bi Odinga alisema mwelekeo wa kisiasa aliochukua Bw Odhiambo ni usaliti kwa wakazi waliomchagua. “Gem imekuwa vyema isipokuwa Elisha ambaye ameamua kutuaibisha. Huenda kuna jambo ambalo linamsumbua. Kama ni mgonjwa tutamtibu lakini kama amefanya hivyo kimakusudi, basi kuna viongozi wengi hapa Gem,” akasema Bi Odinga. Bw Wandayi alisema kuwa uongozi wa ODM ulikosea kwa kuamini na kuwapa baadhi ya viongozi waliokuwa wakitetea viti vyao 2022, tikiti ya chama. “Tulifanya makosa hapa Siaya ila nataka kuwahakikishia kuwa hilo halitajirudia tena. Hatutawachagua tena wasaliti,” akasisitiza. Bw Orengo naye aliapa kuwa atahakikisha ODM inasalia imara kwenye kaunti hiyo, akisema UDA haina nafasi yoyote ya kuwika Nyanza. “Elisha anatuaibisha kila mahali aendako. Hatutaki UDA hapa Gem na mkimwona, mwaambieni,” akasema gavana huyo.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RUSHDIE OUDIA VIONGOZI wa Azimio sasa wanataka vinara wao Raila Odinga na Kalonzo Musyoka wadumishe umoja na ushirikiano wao hadi wakati wa uchaguzi mkuu wa 2027.  Wanasiasa wa muungano huo pia wamewataka wabunge, maseneta magavana na madiwani wawe imara na kusalia Azimio na kupuuza vishawishi vya muungano tawala wa Kenya Kwanza. Gavana wa Siaya, James Orengo na Kiongozi wa Wachache Bungeni, Opiyo Wandayi, wikendi walimiminia sifa Bw Musyoka wakimshukuru kwa kumuunga mkono Bw Odinga katika chaguzi za 2013, 2017 na 2022. “Tunakushukuru sana Kalonzo kwa kusalia imara. Ulikuwa nasi wakati wa maandamano Nairobi na hatutakusahau daima. Kama Waluo, huwa tunafahamu kiongozi kwa kuangalia iwapo ni jasiri, ana uwazi na pia hababaiki,” akasema Bw Wandayi. Bw Orengo naye alimsifia kinara huyo wa Wiper akisema kweli amesimama na Bw Odinga na hakika ni rafiki wa kweli. “Kalonzo tunakukaribisha Gem. Umesimama nasi kwa kipindi kirefu na hili ni jambo ambalo hatutalisahau,” akasema Gavana Orengo. Bw Musyoka naye aliwataka watu wa Nyanza wasipoteze imani na waendelee kuwapigania Wakenya. Alikuwa pamoja na wanasiasa hao pamoja na mkewe Bw Odinga, Mama Idah (mkewe Raila Odinga), katika eneo la Wagai, eneobunge la Gem wakati wa mchango kwa kundi kituo kimoja cha elimu. “Endeleeni kuwa jasiri. Tumekuja kuwapa moyo muendelee kuwa na ujasiri kama Jakom (Raila). Tumepokonywa ushindi mara tatu ila tusikate tamaa na tulinde demokrasia yetu,” akasema Bw Musyoka. Makamu huyo wa rais wa zamani aliongeza kuwa Bw Odinga ameendelea kukosoa serikali na akaahidi kuendelea kushirikiana naye kisiasa. Aliyekuwa Kiongozi wa Mungiki, Maina Njenga ambaye aliandamana na Bw Musyoka, aliwataka viongozi wa Azimio wasalie imara, akisema hiyo ndiyo njia pekee ya kuiondoa Kenya Kwanza 2027. “Lazima tusalie tumeungana jinsi ilivyokuwa wakati wa maandamano. Sielewi Raila anasubiri nini kwa sababu tuko tayari kurejea barabarani,” akasema Bw Njenga. Viongozi wa Ukambani walioandamana na Bw Musyoka ni wabunge Robert Mbui (Kathiani), Stephen Mule (Matungulu), Mbunge Mwakilishi wa Kitui Irene Kasalu na Spika wa Kaunti ya Makueni, Douglas Mwilu. Wakati wa hafla hiyo, Bi Odinga alimshutumu Mbunge wa Gem, Elisha Odhiambo, ambaye anashirikiana na Kenya Kwanza licha ya kuchaguliwa kwa tikiti ya ODM. Bi Odinga alisema mwelekeo wa kisiasa aliochukua Bw Odhiambo ni usaliti kwa wakazi waliomchagua. “Gem imekuwa vyema isipokuwa Elisha ambaye ameamua kutuaibisha. Huenda kuna jambo ambalo linamsumbua. Kama ni mgonjwa tutamtibu lakini kama amefanya hivyo kimakusudi, basi kuna viongozi wengi hapa Gem,” akasema Bi Odinga. Bw Wandayi alisema kuwa uongozi wa ODM ulikosea kwa kuamini na kuwapa baadhi ya viongozi waliokuwa wakitetea viti vyao 2022, tikiti ya chama. “Tulifanya makosa hapa Siaya ila nataka kuwahakikishia kuwa hilo halitajirudia tena. Hatutawachagua tena wasaliti,” akasisitiza. Bw Orengo naye aliapa kuwa atahakikisha ODM inasalia imara kwenye kaunti hiyo, akisema UDA haina nafasi yoyote ya kuwika Nyanza. “Elisha anatuaibisha kila mahali aendako. Hatutaki UDA hapa Gem na mkimwona, mwaambieni,” akasema gavana huyo.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WYCLIFFE NYABERI KIONGOZI wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye amemsuta Rais ya nchi hiyo Yoweri Museveni kwa kukwamilia uongozini. Besigye aidha amekosoa vikali hatua ya Bunge la Uganda kufanyia katiba ya nchi hiyo marekebisho ili kuondoa sharti kwamba wawaniaji wa urais wawe chini ya umri wa miaka 75. Marekebisho hayo yalifanyika mwaka 2017 na kufuatia kupitishwa kwake Bungeni, Rais Museveni alipata fursa nyingine ya kuzidi kuwania urais wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Bw Museveni amekuwa mamlakani tangu taifa hilo lijinyakulie uhuru wake. Akizungumza mnano Desemba 3, 2023, alipohudhuria mazishi ya aliyekuwa mbunge wa zamani wa Mugirango Magharibi, Benson Kegoro katika Kaunti ya Nyamira, Besigye alimpiga vijembe Museveni kwa kusema japo aliifanyia katiba mabadiliko ili kumpa nafasi kuzidi kutawala, hawezi kufanyia Bibilia mageuzi kwani kitabu hicho kitakatifu kinakadiria maisha ya binadamu ulimwenguni kuwa miaka 70. “Huko kwetu kulikuwa na koma kwa miaka ambayo viongozi hawawezi kuwania urais tena wakizidi miaka 75. Hivi karibuni, ilifika kiongozi wetu akasema aah, iondolewe. Iliondolewa na haiko tena kwenye katiba. Lakini alisahau kwamba kuna koma iliyowekwa na Bibilia na Bibilia haiwezi ikabadilishwa. Ni katiba ambayo haiwezi ikabadilishwa,” Besigye akasema. Mwanasiasa huyo ambaye amejaribu kuwania urais wa Uganda kwa safari nyingi bila mafanikio, alieleza mazishini humo umuhimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuzidi kushikana. “Nilikuwa nikikaa huko Uganda bila kuja maeneo haya yote. Lakini sasa nimekuja kama mtalii na haya ndiyo tunayofaa kuzidi kukuza. Wakenya na Waganda ni watu wamoja na tuzidi kushirikiana kwa faida zetu,” Besigye aliongeza. Alitoa wito kwa viongozi wote wa Afrika kuunganisha bara hili kwa kujenga umoja na undugu baina ya watu. Aliwataka marais Waafrika waliomo mamlakani kutokuwa viongozi wa kukandamiza raia, bali wa kuboresha viwango vya maisha yao kwa kuwapa huduma nzuri. Mazishi hayo ya mwendazake Kegoro yalihudhuriwa pia na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga na aliyekuwa mwaniaji mwenza wake katika uchaguzi mkuu 2022, Martha Karua. Bw Odinga aliibua ucheshi pale aliposema kwamba ikiwa kuna mtu anayefahamu jinsi mwaniaji huhisi wakati kura huibiwa, basi hakukuwa na mfano mwingine bora kuliko Bw Besigye. Viongozi wengine kutoka jamii ya Abagusii pia walihudhuria hafla hiyo ya buriani. Wote walimtaja mwenda zake kama kiongozi shupavu aliyewatumikia raia wake kwa bidii wakati wa uongozi wake.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WYCLIFFE NYABERI KIONGOZI wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye amemsuta Rais ya nchi hiyo Yoweri Museveni kwa kukwamilia uongozini. Besigye aidha amekosoa vikali hatua ya Bunge la Uganda kufanyia katiba ya nchi hiyo marekebisho ili kuondoa sharti kwamba wawaniaji wa urais wawe chini ya umri wa miaka 75. Marekebisho hayo yalifanyika mwaka 2017 na kufuatia kupitishwa kwake Bungeni, Rais Museveni alipata fursa nyingine ya kuzidi kuwania urais wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Bw Museveni amekuwa mamlakani tangu taifa hilo lijinyakulie uhuru wake. Akizungumza mnano Desemba 3, 2023, alipohudhuria mazishi ya aliyekuwa mbunge wa zamani wa Mugirango Magharibi, Benson Kegoro katika Kaunti ya Nyamira, Besigye alimpiga vijembe Museveni kwa kusema japo aliifanyia katiba mabadiliko ili kumpa nafasi kuzidi kutawala, hawezi kufanyia Bibilia mageuzi kwani kitabu hicho kitakatifu kinakadiria maisha ya binadamu ulimwenguni kuwa miaka 70. “Huko kwetu kulikuwa na koma kwa miaka ambayo viongozi hawawezi kuwania urais tena wakizidi miaka 75. Hivi karibuni, ilifika kiongozi wetu akasema aah, iondolewe. Iliondolewa na haiko tena kwenye katiba. Lakini alisahau kwamba kuna koma iliyowekwa na Bibilia na Bibilia haiwezi ikabadilishwa. Ni katiba ambayo haiwezi ikabadilishwa,” Besigye akasema. Mwanasiasa huyo ambaye amejaribu kuwania urais wa Uganda kwa safari nyingi bila mafanikio, alieleza mazishini humo umuhimu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuzidi kushikana. “Nilikuwa nikikaa huko Uganda bila kuja maeneo haya yote. Lakini sasa nimekuja kama mtalii na haya ndiyo tunayofaa kuzidi kukuza. Wakenya na Waganda ni watu wamoja na tuzidi kushirikiana kwa faida zetu,” Besigye aliongeza. Alitoa wito kwa viongozi wote wa Afrika kuunganisha bara hili kwa kujenga umoja na undugu baina ya watu. Aliwataka marais Waafrika waliomo mamlakani kutokuwa viongozi wa kukandamiza raia, bali wa kuboresha viwango vya maisha yao kwa kuwapa huduma nzuri. Mazishi hayo ya mwendazake Kegoro yalihudhuriwa pia na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga na aliyekuwa mwaniaji mwenza wake katika uchaguzi mkuu 2022, Martha Karua. Bw Odinga aliibua ucheshi pale aliposema kwamba ikiwa kuna mtu anayefahamu jinsi mwaniaji huhisi wakati kura huibiwa, basi hakukuwa na mfano mwingine bora kuliko Bw Besigye. Viongozi wengine kutoka jamii ya Abagusii pia walihudhuria hafla hiyo ya buriani. Wote walimtaja mwenda zake kama kiongozi shupavu aliyewatumikia raia wake kwa bidii wakati wa uongozi wake.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MHARIRI
BAADHI ya shule nchini zimejitokeza na kupinga matokeo ya Mtihani ya Darasa la Nane (KCPE) yaliyotangazwa Jumatano na Waziri... NA MHARIRI