text
stringlengths
3
16.2k
VUTA nikuvute imezuka kati ya Rais William Ruto na kiongozi wa Azimio Raila Odinga kuhusiana na mswada unaopendekeza... NA JAMES MURIMI
MWANIAJI urais wa chama cha Azimio La Umoja-One Kenya Raila Odinga anasisitiza kuwa Wakenya wanapaswa kuchagua kati ya... NA PIUS MAUNDU
KINARA wa ODM, Raila Odinga amelaani vurugu iliyotokea Kaunti ya Machakos.
Akizungumza Ijumaa katika hafla ya kampeni,... NA JUMA NAMLOLA
NAIBU Rais William Ruto ametoa onyo kali kwa mgombeaji urais wa chama cha Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga... NA GEORGE ODIWUOR
MGOMBEA urais wa muungano wa Azimio la Umoja One Kenya amesihi wakazi katika ngome yake ya Nyanza wajitokeze kwa wingi... NA LEONARD ONYANGO
UCHAGUZI
Siku moja baada ya kinara wa Narc-K, Martha Karua kumeza chambo cha mwaniaji urais kwa tikiti ya Azimio... NA BENSON MATHEKA
KIONGOZI wa chama cha ODM na mgombea urais wa muungano wa Azimio La Umoja Raila Odinga, anazuru Uingereza katika ziara... Na PIUS MAUNDU
VITA vya ubabe vinavyoendelea kati ya magavana watatu wa eneo la Ukambani kwa upande mmoja na viongozi wa Wiper kwa... Na CHARLES WASONGA
HISTORIA ya kinyanga’anyiro cha urais nchini inaonyesha ushindi wa Agosti 9 unaweza kwenda upande wowote kati ya... Na WAANDISHI WETU
NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga jana walivamia eneo la Mlima Kenya kusaka kura za urais huku... Na LEONARD ONYANGO
KINARA wa Azimio la Umoja Raila Odinga leo Jumamosi anatarajiwa kutumia mkutano wake uwanjani Ihura, Kaunti ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na LEONARD ONYANGO
CHAMA cha Pamoja African Alliance (PAA) chake Gavana wa Kilifi Amason Kingi kiko katika hatari kubwa ya kuzuiliwa... Na WANDERI KAMAU
JUHUDI za kuliunganisha eneo la Mlima Kenya ielekeapo 2022 zinaonekana kukumbwa na changamoto tele, wadadisi wakisema... Na WANDERI KAMAU
KUMEIBUKA hofu huenda kutajwa kwa Rais Uhuru Kenyatta kuwa miongoni mwa watu walioficha mabilioni ya fedha ng’ambo... Na BENSON MATHEKA
MABWANYENYE kutoka Mlima Kenya wanaodadisi wagombeaji urais wanakabiliwa na kibarua kigumu kumuidhinisha atakayeweza... Na WANDERI KAMAU
HATUA ya kutangazwa kwa kiongozi wa Narck-Kenya, Bi Martha Karua, kama kaimu msemaji wa ukanda wa Mlima Kenya, imeibua... Na CHARLES WASONGA
MSIMAMO wa Naibu Rais William Ruto kwamba chama cha United Democratic Alliance (UDA) hakitabuni muungano na vyama... Na WANDERI KAMAU
GAVANA Anne Waiguru wa Kirinyaga yupo kwenye njiapanda kuhusu mwelekeo wa kisiasa atakaofuata, uchaguzi mkuu wa 2022... Na CHARLES WASONGA
MASWALI mengi yameibuliwa kuhusu sababu ya kushirikishwa kwa Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya katika mikutano... Na WANDERI KAMAU
NI kinaya kuwa Bw Mwangi Kiunjuri na Bw Moses Kuria ndio wanaoongoza harakati za kushinikiza muungano wa kisiasa... Na BENSON MATHEKA MSIMAMO mkali wa baadhi ya vinara wanaosuka muungano wa One Kenya Alliance (OKA) wa kukataa kumuunga kiongozi wa chama... Na BENSON MATHEKA Vigogo wa kisiasa wanaomezea mate urais wanaendelea kuviziana kila moja akisubiri kuona hatua ambayo mwenzake... Na BENSON MATHEKA KIONGOZI wa chama cha ODM Raila Odinga ameweka mikakati tosha ya kuyumbisha muungano wa One Kenya Alliance (OKA)... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na BRIAN OCHARO MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji amelaumu mitandao ya mabwenyenye kwa kutatiza kesi zinazowahusu... NA FAUSTINE NGILA MARAIS kadhaa na wakuu wa serikali duniani wametajwa katika ufichuzi wa hivi majuzi wa upelelezi wa jinsi mali ya... JOSEPH WANGUI na RICHARD MUNGUTI VITA dhidi ya ufisadi vimeanza kuzaa matunda kwa mara ya kwanza katika historia ya Kenya huku watu... Na IBRAHIM ORUKO WASHUKIWA wanaokabiliwa na ufisadi huenda siku zijazo wakahepa kufungwa gerezani iwapo watakubali kushirikiana na Afisi... Na CHARLES WASONGA WANASIASA na maafisa wa serikali ambao wameshtakiwa kwa ufisadi sasa watazuiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao,... Na RICHARD MUNGUTI ALIYEKUWA waziri wa Michezo na Jinsia, Dkt Hassan Wario huenda akasukumwa jela miaka 10 baada ya kupatikana na hatia... Na LEONARD ONYANGO MARA baada ya kutangaza kushirikiana na kinara wa ODM Raila Odinga mnamo Machi 2018, almaarufu handisheki, Rais Uhuru... Na PETER MBURU MIRADI inayofadhiliwa na fedha za walipa ushuru ndiyo inayotafunwa zaidi na maafisa fisadi serikalini, ripoti ya Mkaguzi... Na MAUREEN ONGALA CHAMA cha Walimu wa Sekondari (KUPPET) kimeomba Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) ianzishe uchunguzi... Na LEONARD ONYANGO KILA mara magavana wanapohutubia Wakenya kuhusiana na hali ya ugonjwa wa corona katika kaunti zao, wanaangua kilio... Na KAMAU MAICHUHIE MZOZO wa uongozi umechipuka kati ya Gavana wa Kiambu, James Nyoro, na Senata Kimani Wamatangi kuhusu madai ya ufujaji... NA AP ALIYEKUWA rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ametakiwa kupendekeza kifungo ambacho angependa kupewa kwa kukwepa vikao vya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved YALA, Siaya Na JOHN MUTUKU SAMUEL KALAMENI eneo hili alibubujikwa na machozi na kujitupa miguuni mwa demu kumuomba asimteme lakini... Na MWANDISHI WETU Kangemi, Nairobi  Jombi mtaani hapa ambaye ni seremala tajika aliamua kukarabati kitanda cha jirani yake bila... Na Nicholas Cheruiyot Mwanasiasa limbukeni alivunjika moyo mpango wake wa kumhamisha nduguye kwake ili amuachie boma atumie kujipigia... Na John Mutuku Samuel Kisa cha kushangaza kilitokea mtaani hapa, baada ya demu aliyezuru wazazi wa mumewe kufumaniwa usiku akirandaranda... Na Mwandishi Wetu KANGEMI, NAIROBI  JOMBI mmoja mtaani hapa anaendelea kuuguza majeraha kwenye nyeti zake baada ya kushambuliwa na... NA DENNIS SINYO JOMBI mmoja ambaye alikuwa akiheshimiwa na wenzake alishangaza watu alipomkana mkewe hadharani ili asimkasirishe mpango... Na Mirriam Mutunga KATHWANA, THARAKA NITHI MWANADADA mmoja kutoka hapa alidondokwa na machozi mpenzi wake wa awali alipomuoa dada... HURUMA, NAIROBI Na MWANDISHI WETU Pasta wa kanisa moja mtaani humu, aliwakasirisha waumini kwa kuwatangazia kuwa atafunga kanisa kwa... Na MASHIRIKA Frankfurt, Ujerumani MWANAMKE mmoja katika mji huu alishangaza jamaa na marafiki kwa kusema kuwa heri mumewe angekufa... Na TOBBIE WEKESA KERICHO KIPUSA mtaani hapa aliwashangaza wengi alipoamua kuuza suti mpya ya mumewe ili apate fedha za kumwezesha... Na MWANDISHI WETU VOI MJINI Jamaa aliyekuwa paparazzi maarufu mjini humu anajuta kuuza simu na kamera yake kwa bei ya kutupa ili... KAPKATET, KERICHO NA NICHOLAS CHERUIYOT ILIBIDI polo wa hapa akubali kwa haraka kufanya kazi za jikoni ili kuokoa ndoa yake baada ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na MASHIRIKA NEYMAR Jr alipachika wavuni mabao mawili na kusaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kufungua mwanya wa alama 10... Na MASHIRIKA KIUNGO Paul Pogba amesema Manchester United wana ulazima wa “kubadilisha mbinu zao za kutandaza soka” iwapo wana ndoto ya... Na JOHN KIMWERE CHANGAMOTO zimekuwa chungu nzima, lakini hazijazuia wachezaji wa Kiganjo Kings kutia bidii, kwani lengo lao ni kutua... Na GEOFFREY ANENE KLABU ya Dandora Youth kutoka ligi ya daraja ya tano ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF), imejawa motisha ya kutafuta... NA ABDULRAHMAN SHERIFF WASICHANA wanne, watatu wanafunzi wa shule za upili na mwingine wa shule ya msingi kutoka Kaunti ya Taita... Na MASHIRIKA TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO KIUNGO wa Chelsea, Christian Pulisic, alifunga bao katika dakika za mwisho na kusaidia timu... Na GEOFFREY ANENE TIMU ya Kenya ya raga ya wanaume ya wachezaji 15 kila upande ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 maarufu kama... Na GEOFFREY ANENE MKIMBIAJI mkimbizi Francois Msafiri amepokea mapokezi ya kishujaa mtaani mwake Syokimau baada ya kukamilisha mbio za... Na GEOFFREY ANENE VISSEL Kobe anayochezea Ayub Masika inakodolea macho kubanduliwa kwenye kipute cha Levain Cup baada ya kupoteza mechi... Na MASHIRIKA TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO KIUNGO mvamizi Andre Ayew, 31, ataagana na Swansea City mwishoni mwa Juni 2021 baada ya mkataba... NA RICHARD MAOSI KIKOSI cha Mogotio United kinajivunia wachezaji mahiri ambao wanasakata soka katika kiwango cha Kaunti ya Baringo... NA ABDULRAHMAN SHERIFF CONGO Boys FC inaonelea fahari kuu ikiwa timu kubwa mbili za hapa nchini, Gor Mahia na AFC Leopards zitacheza mechi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved KWAKO shangazi. Nimekuwa na mpenzi kwa miaka mitatu. Wiki mbili zilizopita aliondoka akaniambia anaenda kuwatembelea wazazi wake... Na SHANGAZI HUJAMBO shangazi? Nina umri wa miaka 28 na nilipata mtoto punde tu baada ya kukamilisha elimu ya shule ya upili. Mwanamume... Na SHANGAZI VIPI shangazi? Nilioa miaka mitano iliyopita na tuna watoto wawili. Ilifika wakati mama watoto akashindwa kunishibisha na... Na SHANGAZI VIPI shangazi? Nilimpa mimba mwanamke mpenzi wangu na nikamuoa kwa sababu nampenda kwa dhati. Ingawa nimeajiriwa, mshahara... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Nilikuwa na mpenzi niliyempenda sana na alikuwa ameahidi kunioa. Hata hivyo, wazazi wake walipinga mpango... Na SHANGAZI VIPI shangazi? Huu ni mwaka wa pili tangu niolewe na tumejaliwa mtoto mmoja. Ninashuku kuna kitu kinachoendelea kati ya mume... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 36 na nimeolewa. Nina uhusiano wa pembeni na bosi wangu na nimegundua... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Nina umri wa miaka 39 na huu ni mwaka wa pili nikitafuta mchumba na bado sijapata. Wanawake ni wengi na... Na SHANGAZI HABARI zako shangazi? Nina umri wa miaka 36 na nina mtoto ingawa sijaolewa. Nimekuwa katika uhusiano wa kimapenzi na... Na SHANGAZI SHIKAMOO shangazi! Nina jambo ambalo linanitatiza moyoni. Kuna mwanamke fulani ambaye amenasa moyo wangu na ninatamani sana... Na SHANGAZI HUJAMBO shangazi? Nina mke ambaye tumeishi pamoja kwa mwaka mmoja sasa. Hata hivyo kuna jambo fulani ambalo nimegundua... Na SHANGAZI KWAKO shangazi. Nimekuwa na mpenzi kwa karibu mwaka mmoja. Amekuwa akiniahidi kuwa atanioa ingawa bado hajanitambulisha kwa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved VICTOR RABALLA NA KASSIM ADINASI WAWANIAJI viti katika ngome ya kiongozi wa ODM Raila Odinga ya Luo Nyanza, wameonywa dhidi ya mivutano... Na WINNIE ONYANDO KINARA wa ODM Raila Odinga na Naibu Rais William Ruto kufikia sasa wako bega kwa bega kwenye kinyang’anyiro... Na LEONARD ONYANGO KINARA wa ODM, Raila Odinga amewatema baadhi ya washauri wake alioshirikiana nao kwa karibu kwenye uchaguzi mkuu wa... BRIAN OCHARO na VALENTINE OBARA UBABE wa kisiasa kati ya Kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, na Naibu Rais William Ruto katika Kaunti ya... Na CHARLES WASONGA HATUA ya Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga kushikilia kuwa wawaniaji wanaounga azma zao za... Na WANDERI KAMAU KIONGOZI wa chama cha ODM, Bw Raila Odinga, jana alianza rasmi safari yake ya kuelekea Ikulu 2022, huku akipata... Na ANTHONY KITIMO GAVANA wa Mombasa, Bw Hassan Joho, amehudhuria mkutano wa dharura na Kiongozi wa chama cha ODM, Bw Raila Odinga, kabla... Na KENNEDY KIMANTHI MABWANYENYE wa eneo la Mlima Kenya leo wanatarajiwa kumwidhinisha rasmi kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, kama... Na CHARLES WASONGA NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga wanaonekana kuendeleza mbinu za kampeni za kulambana visigino... Na LEONARD ONYANGO MATAMSHI ya zamani ya Rais Uhuru Kenyatta ya kumdhalilisha Kiongozi wa ODM Raila Odinga yamegeuka kuwa kizingiti... Na SAMMY WAWERU KIONGOZI wa ODM, Raila Odinga Jumamosi anaendeleza kampeni zake kutafuta uungwaji mkono eneo la Mlima Kenya kumrithi... MAUREEN ONGALA na ALEX KALAMA GAVANA wa Kaunti ya Kilifi, Bw Amason Kingi, anakabiliwa na kibarua kigumu cha kuamua mwelekeo ambao chama... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved NA WALLAH BIN WALLAH KUFIKIRI ni kazi. Ubongo wako hauwezi kukupa majibu sahihi ya maswali unayoulizwa bila ya ubongo kufanya kazi ya... NA ENOCK NYARIKI MOJA kati ya maneno mawili yatumiwayo na watu kurejelea chakula ni mlo. Kuna jingine ambalo aghalabu hukosewa katika... Na CHRIS ADUNGO CHAMA cha Kiswahili katika Shule ya Msingi ya Stelurm Elite, Nairobi kimewawezesha wanafunzi kupiga hatua na kutia fora... Nitaanza makala haya kwa kuuliza swali lifuatalo: Je, mtu huwa na uhakika wa jambo au hakika ya jambo? Vipo baadhi ya vielezi ambavyo... Na CHRIS ADUNGO CHAMA cha Kiswahili katika Shule ya Upili ya St Louis Butula Boys, Kaunti ya Busia (CHAKIBU), kiliasisiwa kwa nia ya... Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya habari ya Nation Media Group imeimarisha juhudi zake za kukuza matumizi ya Kiswahili kwa kutenga siku moja... Na MARY WANGARI   WAKENYA Jumatatu wameungana na jamii ya kimataifa kumboleza kifo cha Mama Sara Obama kwa kutuma risala zao za... Na MARY WANGARI Lugha huundwa kwa sauti ambazo huunganishwa ili kuunda neno au sehemu ya neno, kisha maneno huungana kuunda miundo... NA MARY WANGARI DHANA ya mawasiliano ni mchakato wa kuwasilisha taarifa kwa njia ya ubadilishanaji wa hisia, mawazo, matarajio,... Na CHRIS ADUNGO USIOGOPE kukosea. Kupotea njia ndiko kujua njia. Jaribu tu. Ipo siku ambapo mghafala utaisha. Zidi kumulika uendako kwa... MTIHANI huzua changamoto kwa yeyote anayepania kuufanya. Nakisia ni kwa sababu ya ushindani unaohusishwa nao, hasa nchini mwetu. Aghalabu... Na ENOCK NYARIKI KWA mara ya kwanza kabisa, mitihani ya Kidato cha Nne na Darasa la Nane ambayo hufanywa katika mwezi wa Kumi na Kumi na... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na MARY WANGARI WINGU la majonzi liligubika Kenya wikendi wakati nyota mchanga wa Olimpiki, Agnes Tirop, alipopumzishwa nyumbani kwao... Na MARY WAMBUI SERIKALI ya Uingereza imeshinikizwa kufanya uchunguzi wa ndani na kumshtaki mwanajeshi wake, anayetuhumiwa kumuua... Na BRIAN OJAMAA MWILI wa Masten Wanjala, mwanamume aliyekamatwa kwa mauaji ya watoto, bado uko katika mochari ya Hospitali ya Rufaa ya... WYCLIFFE NYABERI na CHARLES WASONGA WANAUME wanne wanaoshukiwa kuwateketeza wanawake wakongwe kwa tuhuma za uchawi eneo la Marani,... Na Hilary Kimuyu POLISI katika mji wa Uhispania wa Seville wanamzuilia mwanamke Mkenya anayedaiwa kuuma na kula vidole viwili vya... Na GEORGE MUNENE Mtu mmoja ameuawa  kwa risasi huku taharuki ikizidi kutanda mjini Kianjokoma, Kaunti ya Embu kufuatia mauaji ya vijana... Na GEORGE MUNENE Mama mmoja jana alisimulia mahakamani jinsi alivyopata chooni mifupa ya mwanawe na mjukuu wake ambao walikuwa... Na AFP PORT-AU-PRINCE, Haiti WATU wasiojulikana Jumatano waliingia katika makazi ya Rais Jovenel Moise wa Haiti na kumpiga risasi,... Na JOHN NJOROGE UTATA unaendelea kuzingira kifo cha mfanyabiashara na mkurugenzi wa kampuni moja ya maua, Justus Metho Muinde katika... STANLEY NGOTHO NA SIMON CIURI MIILI ya watatu kati ya wanaume wanne waliotoweka mjini Kitengela, Kaunti ya Kajiado mnamo Aprili 19,... SIMON CIURI na MERCY MWENDE MWANAFUNZI wa chuo kikuu, Lawrence Warunge, aliyehusishwa na mauaji ya familia yake ya watu wanne na mjakazi... NA MASHIRIKA MAANDAMANO makubwa jana yalizuka viungani mwa jiji la Mineapolis, Amerika baada ya polisi kumpiga risasi raia mweusi karibu... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved NA CHARLES WASONGA SERIKALI iliyopita ya Jubilee imelaumiwa kwa kutumia jumla ya Sh55 bilioni, bila idhini ya Bunge, kwa miezi mwili na... NA BENSON MATHEKA HUKU serikali ya Jubilee ikikaribia kuondoka mamlakani baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti 9, viongozi wake wameonyesha... NA ONYANGO K’ONYANGO CHAMA cha Jubilee sasa kimeanza mchakato wa kushawishi wandani wa Rais Uhuru Kenyatta waliokuwa wameunda vyama... NA MWANGI MURURI RAIS Uhuru Kenyatta ameripotiwa kukasirishwa na washauri wake kuhusu ripoti zao za hali ya kisiasa katika eneo la Mlima... NA MWANGI MUIRURI WANDANI wa Rais Uhuru Kenyatta wamelaumiwa kwa kuchangia kudidimia kwa umaarufu na ushawishi wake katika eneo la Mlima... Na PSCU RAIS Uhuru Kenyatta amekariri kujitolea kwa serikali katika kuboresha maslahi ya walemavu, akisema watasaidiwa kushiriki... Na WANDERI KAMAU RAIS Uhuru Kenyatta kwa mara nyingine alionyesha dalili za kuunga mkono azimio la kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga,... Na CHARLES WASONGA RAIS Uhuru Kenyatta Jumanne alitoa kumbukumbu ya nyakati ambapo alihudumu bungeni kama Mbunge Maalum, Kiongozi wa... Na SAMMY WAWERU RAIS Uhuru Kenyatta anahutubia taifa leo Jumanne alasiri katika kikao cha pamoja cha bunge, wengi wakisubiri kusikia... Na CHARLES WASONGA RAIS Uhuru Kenyatta leo Jumanne anatarajiwa kuangazia mikakati ya serikali ya kukabiliana na changamoto zinazolikumba... Na CHARLES WASONGA RAIS Uhuru Kenyatta atatoa hotuba kuhusu Hali ya Taifa katika kikao maalum cha Bunge la Kitaifa na Seneti mnamo... Na BENSON MATHEKA SERIKALI imeonywa kuwa mazoea ya maafisa wake, akiwemo Rais Uhuru Kenyatta ya kukaidi maagizo ya mahakama na utawala... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved Na MACHARIA MWANGI WAZIRI wa Leba Simon Chelugui ameziomba kampuni mbalimbali zihakikishe kuwa haziwafuti wafanyakazi wao hata... Na WANGU KANURI TEKNOLOJIA imeiboresha sekta ya upishi haswa kwa wale ambao waliendeleza huduma zao mtandaoni licha ya janga la... Na WANGU KANURI WAKENYA wanaoishi na ulemavu pamoja na wale  wakongwe sasa wataweza kupokea huduma wanazotaka kidijitali za mawasiliano... Na FAUSTINE NGILA LABDA hujasikia hili lakini linakuathiri moja kwa moja kwa kuwa wewe ni mteja wa M-Pesa. Majuzi rafiki yangu alimfaa... Na STEPHEN ODUOR VIJANA katika Kaunti ya Tana River, wametaka mafunzo ya kisasa yatolewe katika taasisi na vyuo vya kiufundi ili... NA FAUSTINE NGILA MAGARI mengi yanayomilikiwa humu nchini na duniani kote yanatumia dizeli au petroli, mafuta ambayo yanachafua... Na FAUSTINE NGILA SUALA muhimu lililojitokeza katika ziara ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uingereza wiki iliyopita, lilikuwa azma ya... Na FAUSTINE NGILA NI miaka mitatu sasa tangu Ripoti ya Blockcheni na Akili Bandia (AI) iwasilishwe kwa serikali kwa ajili ya utekelezaji... Na Ruth Mbula SPIKA wa Bunge la Kitaifa, Bw Justin Muturi, amewarai wadau wa afya kuharakisha utekelezaji wa taratibu za kutumia... [caption id=attachment_77341" align="alignnone" width="843"] Wataalamu wakagua uvunaji wa bitcoin katika kituo cha Bitfarms eneo la Saint... Na FAUSTINE NGILA
Inashangaza kuwa licha ya Kenya kupiga hatua kubwa katika maendeleo ya kiteknolojia, karatasi bado zinatumika katika... Na MASHIRIKA
Kutokana na ongezeko la matumizi ya simu tamba na za kisasa pamoja na kuimarishwa kwa mitandao, imekuwa rahisi kwa idadi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na RICHARD MUNGUTI
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi Ijumaa alizimwa na mahakama kupeperusha katika mitandao ya kijamii video... Na RICHARD MUNGUTI
KUNDI jipya la mawakili sita waliokuwa wanamwakilisha aliyekuwa gavana wa Nairobi Bw Mike Sonko Jumanne walijiondoa... Na RICHARD MUNGUTI
RIPOTI ya daktari wa tiba za akili imesema Alhamisi kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko anaugua maradhi ya... Na RICHARD MUNGUTI
MAHAKAMA ilielezwa jana kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko angali amelazwa katika Nairobi Hospital... Na RICHARD MUNGUTI
UFICHUZI wa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko kwamba mtu aliingia kwenye seli anamozuiliwa katika kituo cha... Na BENSON MATHEKA
Aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko anajuta kwa vitendo alivyofanya akiwa mamlakani; akiepuka kuadhibiwa kwa... Na RICHARD MUNGUTI
KAMA kuna wakati wenye changamoto tele kwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko ni sasa.
Maji yalizidi unga hata... Na RICHARD MUNGUTI
MASAIBU ya aliyekuwa gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko, yaliongezeka Jumatano ilipofichuka kuwa serikali inapanga... Na RICHARD MUNGUTI
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi, Mike Sonko aliangua kilio kortini Jumatano wakati wa kusikizwa kwa kesi ya ufisadi wa... Na CHARLES WASONGA
WANASIASA na watu ambao majina yao yatawekwa katika orodha ya aibu ya Tume ya Uwiano na Utangamano ya Kitaifa (NCIC)... BENSON MATHEKA na SIMON CIURI
Masaibu ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Mike Sonko yaliendelea kuongezeka jana alipozuiliwa rumande baada... Na RICHARD MUNGUTI
MASAIBU ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi Gidion Kioko yameongezeka baada ya  kusukumwa ndani hadi... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAMMY WAWERU MSANII tajika wa nyimbo Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda ametengana na mpenzi wake mwanasiasa Karen Nyamu. Hii ni kutokana na video iliyochipuka ambayo anaskika akisema “nilikuwa kwenye ndoa ya mitara, sasa niko singo”. Samidoh amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Seneta Maalum Karen Nyamu, na wamejaaliwa kupata watoto wawili. Msanii huyo wa nyimbo za Agikuyu, alifichua kuachana na Karen kupitia video ya mbashara ya Tiktok (live) ambapo alikuwa akijibu maswali ya mashabiki wake. Wakati wa mafichuzi hayo, alionekana kuwa kwenye eneo la burudani alikoandamana na msichana ambaye hakuweka wazi endapo ndiye mchumba wake mpya. “Ati hongera kwa kuwa na mpenzi mpya…” Samidoh akasoma mojawapo ya jumbe zilizotumwa na mashabiki wake. Alijibu, “Si wewe pekee ulishushwa madaraka kutoka kiwango cha hadhi hadi dereva wangu…Nilikuwa kwenye ndoa ya mitara ila sasa niko singo”. Mfuasi huyo aliendelea kumdadisi, akitaka kujua iwapo Samidoh anafahamu kuhusu ukurasa wa kimitandao unaohusishwa na mchumba wake – Karen Nyamu Fun Page. Kwa ucheshi, mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Kairetu Gakwa (Binti yangu) na Ndiri Mutwe Mwega (Sina kichwa kizuri) alisema kwa sasa anajishughulisha na biashara. “Kwa sasa, ninajishughulisha na masuala biashara. Ikiwa si mradi au biashara, ishi na mama yako,” alielezea. Shabiki wake alimkejeli akitaka kujua aliko nina yake, isijulikane ikiwa alimaanisha mama yake mzazi au mpenzi wake. “Ameoleka na kwa sasa anafurahia fungate (honeymoon),” Samidoh alidokeza. Kidosho aliyeandamana naye alitambua shabiki huyo kama Shabaan, akisema kwamba yeye ni mchochezi. “Wee acha hiyo, unajua Shabaan wewe ni mchochezi sana… (Yuko hapa (akimaanisha Karen Nyamu),” mwanadada huyo alisema. Naye Samidoh aliendelea, “Tunataka Karen, naona hivo ndivo mchango safuni unasema…Naona, lakini sasa yuko online kweli?” Kipusa aliyeandamana naye, alijibu, “Yuko online, mjaribu”. Aidha, shabiki wa Samidoh alitaka Karen Nyamu ajumuishwe kwenye mazungumzo hayo ya mbashara Tiktok. Kilichoshangaza zaidi na kuashiria utengano wa Samidoh na Karen, ni kudai kwamba alimbloki mtandaoni na angeweza kushiriki endapo atamuondoa alikomuweka. “Yuko kwenye orodha ya kublokiwa, sasa hiyo ndio shida. Labda nisitishe mazungumzo haya ya moja kwa moja ili nimuondoa aweze kujumuika nasi,” Samidoh alifafanua. Mahusiano kati ya Samidoh na Karen, ndiyo yalichangia kuachana na mkewe, Edday Nderitu ambaye alihamia Amerika Mei 2023. Edday alikuwa ameonya msanii huyo mapema 2023, akisisitiza kwamba hakuwa tayari kuwa kwenye ndoa ya mitara. Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAMMY WAWERU MSANII tajika wa nyimbo Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda ametengana na mpenzi wake mwanasiasa Karen Nyamu. Hii ni kutokana na video iliyochipuka ambayo anaskika akisema “nilikuwa kwenye ndoa ya mitara, sasa niko singo”. Samidoh amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Seneta Maalum Karen Nyamu, na wamejaaliwa kupata watoto wawili. Msanii huyo wa nyimbo za Agikuyu, alifichua kuachana na Karen kupitia video ya mbashara ya Tiktok (live) ambapo alikuwa akijibu maswali ya mashabiki wake. Wakati wa mafichuzi hayo, alionekana kuwa kwenye eneo la burudani alikoandamana na msichana ambaye hakuweka wazi endapo ndiye mchumba wake mpya. “Ati hongera kwa kuwa na mpenzi mpya…” Samidoh akasoma mojawapo ya jumbe zilizotumwa na mashabiki wake. Alijibu, “Si wewe pekee ulishushwa madaraka kutoka kiwango cha hadhi hadi dereva wangu…Nilikuwa kwenye ndoa ya mitara ila sasa niko singo”. Mfuasi huyo aliendelea kumdadisi, akitaka kujua iwapo Samidoh anafahamu kuhusu ukurasa wa kimitandao unaohusishwa na mchumba wake – Karen Nyamu Fun Page. Kwa ucheshi, mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Kairetu Gakwa (Binti yangu) na Ndiri Mutwe Mwega (Sina kichwa kizuri) alisema kwa sasa anajishughulisha na biashara. “Kwa sasa, ninajishughulisha na masuala biashara. Ikiwa si mradi au biashara, ishi na mama yako,” alielezea. Shabiki wake alimkejeli akitaka kujua aliko nina yake, isijulikane ikiwa alimaanisha mama yake mzazi au mpenzi wake. “Ameoleka na kwa sasa anafurahia fungate (honeymoon),” Samidoh alidokeza. Kidosho aliyeandamana naye alitambua shabiki huyo kama Shabaan, akisema kwamba yeye ni mchochezi. “Wee acha hiyo, unajua Shabaan wewe ni mchochezi sana… (Yuko hapa (akimaanisha Karen Nyamu),” mwanadada huyo alisema. Naye Samidoh aliendelea, “Tunataka Karen, naona hivo ndivo mchango safuni unasema…Naona, lakini sasa yuko online kweli?” Kipusa aliyeandamana naye, alijibu, “Yuko online, mjaribu”. Aidha, shabiki wa Samidoh alitaka Karen Nyamu ajumuishwe kwenye mazungumzo hayo ya mbashara Tiktok. Kilichoshangaza zaidi na kuashiria utengano wa Samidoh na Karen, ni kudai kwamba alimbloki mtandaoni na angeweza kushiriki endapo atamuondoa alikomuweka. “Yuko kwenye orodha ya kublokiwa, sasa hiyo ndio shida. Labda nisitishe mazungumzo haya ya moja kwa moja ili nimuondoa aweze kujumuika nasi,” Samidoh alifafanua. Mahusiano kati ya Samidoh na Karen, ndiyo yalichangia kuachana na mkewe, Edday Nderitu ambaye alihamia Amerika Mei 2023. Edday alikuwa ameonya msanii huyo mapema 2023, akisisitiza kwamba hakuwa tayari kuwa kwenye ndoa ya mitara. Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAKAZI wa mtaa wa Mazembe viungani mwa mji wa Nakuru wamekiri kuhangaishwa na wezi ambao huwaibia na kuwasindikiza hadi nyumbani. Huwawekea ulinzi huo makusudi ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafika nyumbani salama salimini. Kwa kawaida, wahuni wamebuni mbinu mpya ya kutembea na mbwa wakubwa nyakati za usiku, ili kujiwekea ulinzi wa kibinafsi. Owen Shibala mwendeshaji bodaboda kati ya Nakuru mjini na Mazembe, anasema hajui walikotoa ujasiri walio nao kushika doria usiku utadhani ni polisi. Mazembe ni mojawapo ya mitaa ambayo hushuhudia visa vya kihalifu na utumiaji wa mihadarati mara kwa mara. “Ukikutana nao usiku ni lazima usalimishe kila kitu lau sivyo utaona cha mtema kuni. Watakucharaza viboko na kuiba kila kitu cha nguvu,”akasema. Hata hivyo, wanapoiba hujitwika jukuma la kuwasindikiza wakazi, wasije wakakutana na vibaka wengine barabarani. Aidha, wanalia sare za polisi jambo linalowafanya baadhi ya raia kuamini huenda wanashirikiana na maafisa wa polisi. Baadhi yao wanajifanya ni maafisa wa polisi ambao huwa wameshika doria, wakilenga kuhangaisha wapita njia wanaotoka kazini usiku. Agnes Wahome mfanyibiashara mtaani Rhonda anasema huwa wamejihami kwa visu, rungu na wako tayari kupigana. Kulingana na Bi Wahome, hii ni hali ya kawaida siku hizi katika mitaa ya Manyani, Bondeni na Freearea ambapo vijana wengi wamejiingiza kwenye uhalifu. Bi Wahome anasema wahalifu wengi wanajulikana, kwani ni vijana wadogo kutoka mitaa jirani ya Flamingo na Lakeview. Mkazi huyo angependa polisi kushika doria katika maeneo husika ili kuzuia kuzuka kwa magenge hatari yanayohangaisha wenyeji. Hili linajiri siku chache baada ya Taifa Leo Dijitali kufichua visa vya wizi ambapo baadhi ya wezi kutoka kwenye mtaa wa Gioto, Nakuru wamekuwa wakipika chakula katika kila nyumba wanamoingia kuiba. Mtaa wa Bondeni, Kaunti ya Nakuru ambapo wezi huwaibia wakazi na kuwasindikiza mpaka nyumbani. PICHA|RICHARD MAOSI
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAKAZI wa mtaa wa Mazembe viungani mwa mji wa Nakuru wamekiri kuhangaishwa na wezi ambao huwaibia na kuwasindikiza hadi nyumbani. Huwawekea ulinzi huo makusudi ili kuhakikisha kwamba wateja wao wanafika nyumbani salama salimini. Kwa kawaida, wahuni wamebuni mbinu mpya ya kutembea na mbwa wakubwa nyakati za usiku, ili kujiwekea ulinzi wa kibinafsi. Owen Shibala mwendeshaji bodaboda kati ya Nakuru mjini na Mazembe, anasema hajui walikotoa ujasiri walio nao kushika doria usiku utadhani ni polisi. Mazembe ni mojawapo ya mitaa ambayo hushuhudia visa vya kihalifu na utumiaji wa mihadarati mara kwa mara. “Ukikutana nao usiku ni lazima usalimishe kila kitu lau sivyo utaona cha mtema kuni. Watakucharaza viboko na kuiba kila kitu cha nguvu,”akasema. Hata hivyo, wanapoiba hujitwika jukuma la kuwasindikiza wakazi, wasije wakakutana na vibaka wengine barabarani. Aidha, wanalia sare za polisi jambo linalowafanya baadhi ya raia kuamini huenda wanashirikiana na maafisa wa polisi. Baadhi yao wanajifanya ni maafisa wa polisi ambao huwa wameshika doria, wakilenga kuhangaisha wapita njia wanaotoka kazini usiku. Agnes Wahome mfanyibiashara mtaani Rhonda anasema huwa wamejihami kwa visu, rungu na wako tayari kupigana. Kulingana na Bi Wahome, hii ni hali ya kawaida siku hizi katika mitaa ya Manyani, Bondeni na Freearea ambapo vijana wengi wamejiingiza kwenye uhalifu. Bi Wahome anasema wahalifu wengi wanajulikana, kwani ni vijana wadogo kutoka mitaa jirani ya Flamingo na Lakeview. Mkazi huyo angependa polisi kushika doria katika maeneo husika ili kuzuia kuzuka kwa magenge hatari yanayohangaisha wenyeji. Hili linajiri siku chache baada ya Taifa Leo Dijitali kufichua visa vya wizi ambapo baadhi ya wezi kutoka kwenye mtaa wa Gioto, Nakuru wamekuwa wakipika chakula katika kila nyumba wanamoingia kuiba. Mtaa wa Bondeni, Kaunti ya Nakuru ambapo wezi huwaibia wakazi na kuwasindikiza mpaka nyumbani. PICHA|RICHARD MAOSI
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI MASKWOTA wapatao 10,000 wamewasilisha upya kesi katika Mahakama ya Upeo wakiomba ibatilishe uamuzi kwamba wafukuzwe kutoka kwa shamba la ukubwa wa ekari 25,000 wanalong’ang’ania umiliki wake na familia ya mwanasiasa marehemu Mark Too. Maskwota hao wanaodai mababu zao ndio waliotimuliwa kutoka kwa shamba hilo enzi za ukoloni, wanasema walipewa shamba hilo rasmi na aliyekuwa Rais hayati Daniel arap Moi, kisha Kamishna wa Ardhi M Okundu akaratibisha uamuzi huo mwaka 2007. Katika ombi lililowasilishwa na wakili William Arusei chini ya sheria za dharura, kikundi cha maskwota hao–Sirikiwa Squatters Group–kimeomba mahakama ibatilishe uamuzi huo kwa vile ilitegemea ushahidi ambao haukuwa umewasilishwa katika kesi waliyoshtaki katika Mahakama ya kuamua kesi za mashamba (ELC), Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu. Pia wameeleza bayana Jaji Mkuu Martha Koome, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu, majaji Mohammed Ibrahim, Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Isaack Lenaola, na William Ouko walitegemea ushahidi wa Afisa wa Ugavi wa Mashamba R J Simiyu kutoa uamuzi wang’atuke shambani. Maskwota hao wamesema ushahidi wa Bw Simiyu uliowasilishwa mbele majaji hao saba kwa njia ya afidaviti ni mpya na kamwe “haukuwasilishwa mbele ya Jaji Antony Ombwayo aliposikiliza na kuamua kesi hiyo 2017.” Pia wanasema ushahidi huo haukuwasilishwa Mahakama ya Rufaa iliyosikiliza rufaa iliyowasilishwa na kampuni ya Fanikiwa, familia ya marehemu Mark Too, kampuni ya Lonrho Agribusiness (EA) Ltd, na Bw David K Korir. Hivyo basi, maskwota hao wanaeleza mahakama hii ya upeo kwamba ni kinyume cha sheria kutegemea ushahidi mpya kutoa uamuzi wa kesi hii iliyo na umuhimu mkubwa kwa umma. “Uamuzi huu wa Mahakama ya Juu wa Desemba 15, 2023, hauna mashiko kisheria na kamwe hauna nguvu kisheria kuwatimua maskwota hawa kutoka kwa shamba lao,” asema Bw Arusei. Pia maskwota hawa wanadai kwamba badala ya Mahakama ya Juu kujadili masuala ya kikatiba jinsi ilivyo jukumu lake, majaji hao walianza kufafanua na kutafsiri ushahidi wa watu binafsi na kuelezea maana ya ‘skwota’. Mahakama hii imeombwa ikague upya uamuzi iliyotoa kwa vile ilidanganywa na walalamishi na pia kutendewa ujanja. Akinukuu maamuzi ya majaji wastahiki kama vile Lord Dening, Bw Arusei amesema, mahakama ikigundua ilipotoshwa au kudanganywa na upande mmoja, iko na mamlaka na uwezo wa kufutilia mbali uamuzi iliyotoa na kuandika mwingine. Maskwota hao wanaomba Mahakama ya Juu iwarudishe shambani kama ilivyokuwa imeamuliwa na Jaji Ombwayo na Mahakama ya Rufaa. Vile vile mahakama hiyo imekosolewa kwa kumshambulia hayati Moi katika uamuzi huo pasi kutoa agizo wasimamizi wa mali yake wafike mbele yao kutoa mwanga kuhusu suala la umiliki wa shamba hili lililorudishwa kwa serikali na kampuni iliyokuwa inakuza miti inayotumika katika viwanda vya ngozi. Naibu msajili wa Mahakama ya Juu Nelly Kariuki aliwaamuru maskwota hao wawakabidhi nakala za kesi hii yao mpya wahusika wote kabla ya Januari 31, 2024, kesi itakapotajwa tena kwa maagizo zaidi. Jaji aliyesikiliza kesi hii mpya hakuiratibisha kuwa ya dharura ila aliamuru pande zote ziwasilishe ushahidi katika muda wa siku 14 kuanzia Desemba 21, 2023. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAMILIKI wa nyumba za wapangaji mtaani Kayole wameamua kulala mchana na kukaa macho usiku ili kupambana na wahalifu ambao wametawala ploti zao. Aidha wapangaji wanapoendelea kufurahia sikukuu wakiwa mashambani, wezi kwa upande mwingine wanavunja nyumba na kuiba bidhaa kutoka ploti moja hadi nyingine. Mbali na Kayole, maeneo mengine ambapo wizi umeripotiwa ni Kangemi, Korogocho, Githurai, Umoja, Kariobangi, Starehe, Syokimau, na Buruburu. Wanavunja nyumba na kuiba vyombo, fanicha, mitungi ya gesi ya kupikia, televisheni, na redio, huku hatimaye bidhaa hizo zikiuzwa kwa bei ya kutupa mtaani. Bw Gilbert Ambani ambaye ni mlinzi katika mojawapo ya ploti eneo la Syokimau, anasema wezi wengi huko katika msimu huu wa shamrashamra wanalenga vyuma chakavu kwa sababu huwapatia hela za haraka. “Baadhi ya wezi wanabomoa lango kuu na kuchukua vyuma huku wengine wakivunja mifereji,” Bw Ambani akaambia Taifa Leo. Naye Amon Andika ambaye ni landilodi mtaani Kayole, alisema kwamba imemlazimu kufanya kazi ya ziada ya kulinda nyumba za wapangaji wake ambao wengi walienda mashambani almaarufu ‘ushago’. Anasema mwaka 2023 ameamua kufanya kazi ya usoja kama wengi wanavyoiita, baada ya kubaini kuwa baadhi walinzi wake wa awali walikuwa wakishirikiana na wezi kutekeleza wizi. Bw Andika ameingia gharama ya kuwekeza upya kwenye mradi wa maji baada ya wezi kuvunja mfereji wake usiku wa Desemba 24, 2023, na kutoweka na paipu ya thamani ya Sh70,000. Anasema kwa sababu ya hali ngumu ya kiuchumi, hana uwezo wa kuajiri soja wa usiku. Ndiposa imemlazimu kuhatarisha maisha yake kwa kulinda mali mpaka ifikapo Mwaka Mpya 2024. Anasema ni desturi yake kila mwaka wapangaji wanapokuwa wameelekea ‘ushago’ kufurahia sikukuu, yeye anadumisha usalama. Mnamo Desemba 27, 2023, washukiwa 34 wa wizi walikamatwa katika eneobunge la Starehe katika operesheni iliyoongozwa na chifu na maafisa wa polisi. Hali ni kinyume na baina ya mwaka wa 2020 na 2021 ambapo wakazi wengi wa jiji waliamua kutosafiri kwa sababu ya mlipuko wa janga la Covid-19. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA KIONGOZI wa Narc-Kenya Martha Karua amesema kuwa muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya ulitoka mikono mitupu katika mazungumzo kati yake na mrengo wa Kenya Kwanza (KKA). Kwenye mahojiano na runinga ya Citizen mnamo Alhamisi usiku, Bi Karua alidai wanachama wa Azimio katika Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo (Nadco) walisaidia KKA kuendeleza ajenda zao. “Kwa mtazamo wangu, mazungumzo hayo hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu hakuna muafaka uliofikiwa kuhusu ajenda zetu tatu kuu ambazo ni gharama ya maisha, haki katika uchaguzi, na heshima kwa demokrasia ya vyama vingi,” akasema Bi Karua. Akaongeza: “Muafaka ulipatikana kuhusu ajenda za Kenya Kwanza kama vile kuundwa kwa afisi ya kiongozi rasmi wa upinzani, na kuhalalishwa kwa afisi ya Mkuu wa Mawaziri, ambazo tayari Ruto alikwisha kuwasilisha bungeni.” Kiongozi huyo wa Narc Kenya alieleza kuwa vikao vya kamati ya Nadco vilivyodumu kwa miezi minane vilikuwa ni vya kuwapotezea Wakenya hela na muda kwa sababu serikali haikuongozwa na nia njema iliposhiriki mazungumzo na upinzani. “Mazungumzo hayo yalilenga kutuchezea shere na kutuliza maandamano. Matokeo ya mazungumzo yetu na utawala wa KKA hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu Wakenya bado wanaumizwa na kupanda kwa gharama ya maisha. Kwa mtazamo wangu, ripoti ya Nadco haina maana yoyote kwa Wakenya kwa sababu haishughulikii madhila yao,” Bi Karua, ambaye alikuwa ni mgombea mwenza wa Raila Odinga katika uchaguzi wa urais wa Agosti 9, 2022, akaongeza. Alielekeza lawama kwa utawala wa Kenya Kwanza kwa kile alichodai ni kufeli kufikiwa kwa malengo ya mazungumzo yake na upinzani. “Licha ya sisi kama upinzani na wananchi kuendelea kuushinikiza utawala huu upunguze gharama ya maisha, walipuuza na badala yake kuendelea kuongeza bei ya bidhaa za kimsingi na kuanzisha aina nyingine za ushuru,” akasema. Ili mazungumzo yoyote yafaulu, kulingana na Bi Karua, chama au mrengo ulioko mamlakani ni sharti kuonyesha nia njema kwa sababu wao ndio wanasukumwa kutimiza matakwa ya wananchi. Kiongozi huyo wa Narc-Kenya aliutaja utawala wa sasa kama ambao hauheshimu sheria na maamuzi ya mahakama. “Utawala huu unaendesha majukumu ya serikali kwa namna ambayo haijeshimu sheria na kudharau maoni ya wananchi ulivyofanya wakati wa ukusanyaji maoni ya umma kuhusu Sheria ya Fedha,” akasema. “Unapodharua Katiba na watu ambao walikupa mamlaka na matakwa ya wengi, unageuka serikali mbaya,” akaeleza alipoulizwa sababu yake ya kuirejelea serikali hivyo. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FARHIYA HUSSEIN MWAKA 2023, unyama uliokuwa ukifanywa ndani ya wa Shakahola katika Kaunti ya Kilifi, ulifichuliwa ambapo zaidi ya watu 400 walipoteza maisha yao kwa itikadi kali za kidini. Mhubiri Paul Mackenzie ambaye alitajwa kuwa kiongozi wa wafuasi wake, anachunguzwa kwa madai ya kuwapotosha katika mafundisho ya kidini ambapo waumini walichanganyikiwa, wakiwemo watoto, wakaanza kufunga au kususia chakula hadi wakaanza kudhoofika na hatimaye kuanza kuaga dunia mmoja baada ya mwingine. Habari hizo zilipofahamika, idadi hii ya watu waliopoteza maisha ilikuwa nyingi sana, jambo liloshangazaa ulimwengu mzima. Walionusurika waliozungumza na Taifa Leo alisema waliokufa waliambiwa wafunge hadi kufa ili wakutane na ‘Yesu’. Miezi tisa baadaye, miili zaidi ya 400 inaendelea kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha muda katika Kaunti ya Kilifi, ukumbusho wa kusikitisha kuashiria msimamo wao mkali wa kidini waliofuatilia. Watu hawa, ambao walitajwa na jamaa zao kuwa watu wachangamfu na maisha hapo awali walionekana kuishi maisha ya kudhoofisha na ya hali ya kusikitisha, maisha yao yalikatishwa na imani zile walizofuatilia kwa kina. Msitu huo ambao hapo awali ulikuwa sehemu nzuri ya mandhari ya kiasili, sasa umekuwa shahidi kwa ukatili uliofanywa huko ndani. Shakahola, kijiji katika Kaunti ya Kilifi, kilikuwa kimegubikwa na ukimya wa kutisha kwa miezi kadhaa. Makazi hayo ambayo wanakijiji walitaja zamani yalikuwa ya uchangamfu na yenye shughuli nyingi, sasa yalionekana yametawaliwa na ukimya mkuu. Katika msitu huo wa Shakahola, nyumba zilikuwa za udongo huku zikiezekwa kwa mapaa ya makuti. Njia zilizokuwa na watu wengi sasa zilikuwa kimya kwa kutisha, kana kwamba wanakijiji walikuwa wametoweka wakiacha nyuma vitu vya kibinafsi kama vile Biblia, ushahidi kuwa waliondoka ghafla. Sahani zilizotelekezwa zilizofunikwa ziliashiria ‘mlo wa mwisho’ wa wafuasi wa Kanisa la Good News International la Mchungaji Paul Mackenzie, ambalo inadaiwa lilichochea wao kuchukua mkondo hatari wa kufunga hadi kufa. Katika mazingira haya ya kutatanisha, ambapo ibada inayodhaniwa ilikuwa imezama katika unabii wa apocalyptic, cha kusikitisha ni kwamba baadhi yao hawakunusurika katika safari ya kuenda katika Hospitali Kuu ya Malindi. Wahanga walizikwa bila mpangilio makaburi yao yakiashiria kuzikwa kwao kwa haraka. Miezi kadhaa baadaye, miili yao ilifukuliwa. Watu hawa walionekana kutengwa na kusukumwa kwenye ukingo wa jamii, sauti zao zikiwa zimenyamazishwa na nguvu za itikadi kali. Maisha yao yalipochukuliwa kwa uchungu, heshima waliyostahili katika umauti wa iliondolewa pia. Ni wale tu walioaga dunia wangejua ikiwa kweli walikutana na Mungu wao. Miili yao ilizikwa kwa haraka msituni Shakahola, jambo lililodhihirishwa na jinsi makaburi hayo yalivyofukuliwa ambapo kwa kila mojawapo, miili zaidi ya mmoja ilipatikana ndani. Waumini hao hawakuzikwa na sanduku kama ilivyo kwa Wakristo bali walifunikwa na blanketi na nguzo nyinginezo. Miezi tisa baadaye, chumba cha kuhifadhia maiti cha muda bado kimesalia katika hopsitali ya Malindi, ukumbusho wa mkasa uliotokea mwaka 2023. Waathiriwa wamesalia katika hali ya kutatanisha, utambulisho wao bado haujathibitishwa, hadithi zao kubaini kiini cha kilichotokea ndani ya msitu wa Shakahola bado haijabainika. Hata katika kifo, ibada iliwanyima utambulisho wao, na kuacha miili hiyo ‘haijulikani’ kutokana na ukosefu wa nyaraka zozote. Ukweli uligundulika ni kwamba baadhi ya wanachama hao walitoka kaunti za mbali katika mikoa mingine nchini, jambo la kutatanisha katika kutambua na kudai miili hiyo. Mwezi Mei, serikali ilianzisha mpango wa DNA kulenga familia zinazoshuku kuwa jamaa zao waliopotea au walioaga wanaweza kuhusishwa na msitu wa Kilifi’ Shakahola. Takriban miezi saba imepita tangu kuzinduliwa kwake, lakini familia zinalalmikia kungoja matokeo ya DNA kwa hamu. Miongoni mwa walioathiriwa ni Bw Rodgers Mwibo, ambaye anatafuta mama yake, dada yake, na mpwa wake amabye alisema ni wafuasi waaminifu wa mhubiri Paul Mackenzie kutoka Kanisa la Good News International, waliohamia kwenye msitu huo mwaka mmoja uliopita. Akielezea masikitiko yake, Bw Mwibo alieleza kuwa kufuatia tangazo la serikali, alitoa sampuli zake za DNA kaunti za Nairobi na Malindi. “Badala ya kupata faraja, huku kusubiri kwa muda mrefu kunazidisha kiwewe changu. Kila nikiona picha ya mama yangu, natamani sana uwepo wake, hata kama ni kumuaga tu,” alilalamika Bw Mwibo huku akihoji ufanisi wa taratibu za DNA za serikali. Kulingana na Bw Mwibo, uhakikisho ulitolewa kwamba matokeo yatatolewa mara moja baada ya ukusanyaji wa DNA. Hata hivyo, kile kilichoahidiwa kuwa kipindi kifupi kimeongezeka hadi mwaka mmoja, na kumuacha yeye na wengine katika hali ya huzuni ya kihisia moyo. “Ni katika nchi gani miili hubaki kuhifadhiwa kwenye friji huku familia zikistahimili uchungu huu?” aliuliza Bw Mwibo. Jamaa mwingine, Bi Mary Mwikali anabainisha kuwa hatajua iwapo dadake na mpwa wake ni miongoni mwa waliofukuliwa kutoka msitu wa Shakahola au la. Kusubiri kwa hamu kunaendelea, na kuwaacha wakihangaika na sintofahamu ikiwa wapendwa wao bado wako hai au ni miongoni mwa watu 400 na zaidi wakiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Malindi. Afisa wa Masuala ya Dharura katika Shirika la Haki Africa, Bw Mathias Shipeta, alisema wasiwasi wake ni kwamba serikali imechukua muda mrefu unaohitajika ili kulinganisha na kulinganua DNA. “Inachukua muda gani hadi ulinganishaji wa DNA ukamilike? Familia zinamaliza mwaka bila kujua jamaa zao waliko. Haijafahamika wazi kama wameaga dunia au wapo hai. Ili kulifunga suala hili, ulinganishaji wa DNA lazima ukamilike na kukamilika kwa wakati kabla ya mwisho wa mwaka,” Bw Shipeta alisisitiza. Mwezi Julai, sampuli 266 zilikusanywa kwa madhumuni ya utambulisho wa vinasaba DNA. Uchunguzi wa DNA ni ulinganifu wa kisayansi wa maelezo ya kinasaba ya watu wasiojulikana au waliokufa na yale ya watu waliotambuliwa (waliokufa au walio hai). Mchakato huo ni muhimu kwa sababu za kisheria na za kibinadamu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MASHABIKI wa klabu ya Arsenal mjini Murang’a sasa wameonywa na wenzao wa Manchester United na Chelsea wajiandae kumpokea ndovu wao akianguka pasipo hiari kutoka juu ya mti kumaanisha kushuka katika jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL). “Huku kulimwa ambako mmeanza kulimwa ni mwanzo tu wa namna ambavyo mambo yatakuwa magumu kwenu katika mzunguko wa pili,” akafoka Bw David Njuguna ambaye ni mshirikishi wa the Red Devils mjini humo. Cheo chake hakitambuliki rasmi na klabu ya Manchester United. Bw Njuguna alisema kwamba Arsenal kuwa juu ya jedwali hata kwa mwanya wa pointi 10 sio tishio kwa kuwa katika mkondo wa lala salama, wao huwa butu, wasio na maono na mwelekeo na lazima wajihujumu wao wenyewe kama ilivyokuwa msimu jana. Katika mechi ya usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, Arsenal walirambishwa magoli 2-0 na West Ham. “Hata hamna heshima na wawekezajj na mnatuchomea beti. Kwa kuwa sikuamini kabisa mngeshinda hicho kipute, nilikuwa nimebashiri timu zote mbili angalau zingejipa goli. Sasa ona hamkufunga hata la kukataliwa,” akafoka Stacy Keach, mfuasi wa Chelsea. Janga hilo kwa wanabunduki Arsenal limewaacha katika nafasi ya pili kwenye jedwali wakiwa na pointi 40 huku Liverpool ikibakia kidedea kwa pointi 42. Hii ina maana kwamba Man City ambayo iko na pointi 37 kwa sasa lakini ikiwa imecheza mechi 18 Arsenal ikiwa imecheza mara 19 itaifurusha kutoka nafasi hiyo ya pili iwapo itachapa Sheffield United hapo Jumamosi kwa ubora wa magoli. “Kuna uwezekano mkubwa kwamba Arsenal itaingia mwaka Mpya ikiwa nambari tano nyuma ya Liverpool, Man City, Aston Villa na Tottenham na kabla ya tufike mechi ya 27, hata West Ham, Man United… watakuwa mbele ya Arsenal,” akasema Junita Kasyoki ambaye anashabikia Man United. Ni usiku ambao wafuasi wa Arsenal hawakujibu mipigo, waliondoka polepole na kimyakimya kutoka kwa mkahawa wa Green Park ambapo wengi walikuwa wakifuatilia mtanange huo ulioanza saa tano na robo usiku. “Lakini hata hivyo kushindwa kwetu kulisaidia West Ham kuruka Man United katika jedwali. Tungeshinda mchuano huo Man U wangebakia nafasi ya sita lakini kung’atwa kwetu kulisaidia Mashetani Wekundu kuteremka hadi nafasi ya saba,” akajituliza Bw Simon Ngonjo. Kwa sasa, maombi ya Arsenal ni kuzuke mikosi ya kushindwa kwa timu zote zilizo katika kumi bora katika mechi ya 20 lakini wao washinde ndipo warejee juu ya jedwali na presha ya kutwaa ligi ipungue. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MWANAMUME mmoja wa umri wa miaka 33 aliuawa usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, kwa kupigwa na majirani wa wakwe zake baada ya kile kinadaiwa alijaribu kutekeleza mauaji katika boma hilo alimokuwa amelala na bibi yake. David Kimani alikuwa amesafiri kutoka kijiji cha Kiunyu kilichoko eneobunge la Gatanga kwa msingi kwamba alikuwa na nia ya kumuona mkewe waliyetengana, binti yake wa umri wa miaka sita na pia mama mkwe. Mwanamume huyo alikuwa ametengana na Bi Esther Nyawira, 28, kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu na katika shamrashamra za msimu huu wa sherehe, akafika kwa boma la wakwe Desemba 28, 2023, katika kijiji cha Mung’etho kilichoko eneobunge la Maragua, akisema alienda kuwajulia hali. Lakini hata baada ya giza kuingia, hakuonyesha nia ya kuondoka arejee kwao na ndipo akakubaliwa alale kwa nyumba ya mama mkwe akiwa na bibi huyo wake. Mwendo wa saa sita usiku, Kimani anasemwa kwamba aliamka na akatwaa kisu na akaanza kumshambulia bibi yake aliyekuwa amelala huku kwa sauti akiapa kumuua na kisha aue mama mkwe na pia mtoto. Kwa mujibu wa Kaimu Naibu Kamishna wa Murang’a Kusini Bw Joshua Okello, mwanamume huyo baada ya kujaribu mara kadha warejeane na bibi yake pasipo mafanikio, akaamua kufika katika boma hilo akijipamba kama malaika wa mauti. Aliongeza kwamba mshukiwa alimdunga mwanamke huyo visu vitano “mara moja umbavuni upande wa kulia na mara nne kwa mkono wa kulia, majeraha yote yakiwa matano”. Bw Okello aliongeza kwamba sauti za juu za mwanamume huyo zilimwamusha mama mkwe na alipiga nduru ambayo iliwavutia majirani waliofurika katika boma hilo huku mvamizi baada ya kuingiwa na taharuki akitimua mbio hadi nje ya nyumba na akaingia katika kichaka. “Huku mwaathiriwa akikimbizwa hadi hospitali ya Murang’a kutibiwa, majirani nao walizindua msako ulioishia kumnasa Bw Kimani akiwa amejikunyata ndani ya kichaka hicho na wakamuua kwa kumpiga kwa vifaa butu,” akasema Bw Okello. Afisa huyo aliongeza kwamba ndani ya mkoba ambao marehemu alikuwa nao kulikuwa na sumu ya kuua wadudu kwa mimea na pia waraka wa mauti unaoaminika ulikuwa umeandikwa na mwanamume huyo. “Alikuwa amefichua katika waraka huo kwamba alinuia kuua mama mkwe, bibi yake na mtoto wake wa kike aliyekuwa akiishi kwa wakwe hao na kisha yeye mwenyewe ajitoe uhai,” akasema. Mwanamume huyo alikuwa aidha ameteta kwamba mama mkwe ndiye alikuwa kizingiti cha ndoa yake kupata uthabiti na kwa kuwa hakuwa na nia ya kumpenda mwingine, akaafikia uamuzi wa kuwaua watatu hao na kisha naye ajitume kuzimu akome mahangaiko ya mapenzi. Bw Okello alisema kwamba “huu ni mkasa ambao ungeepukika iwapo mwanamume huyo ambaye alikuwa mfanyabiashara Jijini Nairobi angepata ushauri nasaha ili kuwajibika changamoto zake za kimapenzi ndani ya mashauriano”. Alisema kwamba “ndipo ifike kiwango hicho cha kupanga mauaji ni kumaanisha alikuwa akisaka mbinu ya kusuluhisha changamoto hiyo lakini akaamua kufuata ushawishi wa pepo mbaya kujipa afueni”. Huku akiwakemea waliomuua mwanamume huyo na kuahidi uchunguzi wa kunasa washukiwa, Bw Okello alisema “hata jamii inafaa kuwa macho kuwatambua wanaoonekana kusombwa na mawazo na usaidizi wa ushauri usakwe kabla ya vishawishi vya janga kuzuka”. Bw Okello alionya watu wa kijiji hicho cha Mung’etho kwamba “kwa sasa mnaweza kuwa mnasherehekea mkisema eti ni umati wa raia uliotekeleza mauaji hayo lakini wakati kutajitokeza shahidi aseme alikuona wewe ukishiriki mauaji hayo ndipo utajua ni watu binafsi wala si kundi ambalo huvunja sheria”. “Mchango wa raia katika kuimarisha usalama ni kupitia kutupasha habari kuhusu washukiwa na visa na wakimnasa mshukiwa, kazi yao inafaa tu kutuita tumtie mbaroni au wamwasilishe katika kituo cha polisi kilicho karibu,” akasema Bw Okello. Mwili wa marehemu ulipelekwa hadi mochari ya Murang’a. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MUSTAKABALI wa Kanisa Katoliki uko kwenye njia panda barani Afrika, kufuatia agizo la Papa Francis kwa mapadre katika kanisa hilo kubariki wapenzi wa jinsia moja. Ingawa lengo kuu la agizo hilo linaonekana kama njia ya kuwavutia washiriki zaidi na kutowabagua watu hao, wachambuzi na wasomi wa masuala ya dini wanasema huenda agizo hilo lilitolewa bila Papa kupewa ushauri wa kina na uongozi wa kanisa hilo. Kanisa Katoliki lina mamilioni ya washiriki hapa Kenya na barani Afrika kwa jumla. Kulingana na takwimu kutoka kwa serikali, kanisa hilo ndilo linaloongoza kwa kuwa na washiriki wengi nchini, huku likifuatwa na makanisa ya Kiprotestanti. Tangu Papa Francis alipotoa agizo hilo, viongozi tofauti wa kanisa wameeleza na kutoa hisia tofauti,  baadhi wakijitokeza wazi kulipinga. Baadhi ya viongozi wakuu ambao wamejitokeza kulipinga ni kiongozi wa kanisa hilo nchini, Askofu Philip Anyolo, ambaye pia ndiye Askofu Mkuu katika Dayosisi ya Nairobi. Kulingana na askofu huyo, agizo hilo linakinzana vikali na tamaduni za Kiafrika, hivyo hawataliruhusu. “Kiafrika, ndoa za jinsia moja hazikubaliki hata kidogo. Ndoa hizo pia zinaenda kinyume na mafunzo ya Biblia,” akasema Askofu Anyolo. Maaskofu wengine ambao wamejitokeza wazi kupinga agizo hilo ni Cornelius Odiwa wa Homa Bay na mwenzake wa dayosisi ya Eldoret, Askofu Dominic Kimengich. Askofu Odiwa alisema watafuata msimamo wa Askofu Anyolo, kwani ndiye kiongozi wa kanisa hilo nchini. Pia, alisema ndoa hizo hazikubaliki kabisa Kiafrika. Kando na viongozi wa Kanisa Katoliki, watu kutoka dini nyingine pia wameunga mkono pingamizi hizo. Baadhi yao ni Bw Samuel Kamitha, ambaye ni mwanahistoria na msomi wa masuala ya dini. Bw Kamitha pia ni mmoja wa waandalizi wakuu wa maombi maalum ambayo hufanyika Desemba 27 kila mwaka karibu na Mlima Kenya. Mnamo Jumatano, wakati wa maombi hayo, Bw Kamitha alisema hawatakubali hata kidogo tamaduni za kigeni kutumika kuharibu desturi asilia za Kiafrika. “Tunasimama kidete kupinga uhalalishaji wa ndoa za jinsia moja nchini. Hilo ni jambo linalokinzana kabisa na tamaduni zetu,” akasema. Maombi hayo yalihudhuriwa na Wakristo, Waislamu, watu wanaofuata dini za kitamaduni kati ya madhehebu mengine. Kutokana na hisia hizo, wasomi wa masuala ya dini wanasema kuwa mwelekeo huo mpya unafaa kuufungua macho uongozi wa Kanisa Katoliki kuhusu mustakabali wake barani Afrika. “Kikawaida, maagizo yote kutoka Vatican (makao makuu ya Kanisa Katoliki) huwa hayapingwi hata kidogo. Ni vigumu kusikia usemi au agizo la Papa likikosolewa au kupingwa. Hata hivyo, viongozi kadhaa wanapojitokeza wazi kupinga agizo lake, basi hiyo ni ishara wazi kuwa kuna tatizo kubwa ambalo lazima litatuliwe,” asema Dkt Rita Khamisi, ambaye ni msomi wa historia ya dini. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAMMY WAWERU ALIYEKUWA kiongozi wa kundi haramu la Mungiki, Maina Njenga ameeleza imani yake kuwa mikakati aliyoweka kuleta pamoja jamii ya Mlima Kenya itamuwezesha kuwa msemaji wa eneo hilo – Kingpin. Kulingana na mwanasiasa huyu ambaye pia ni Askofu wa Kanisa la Hope International, kwa sasa yuko mbioni kuunganisha jamii ya Agikuyu. Anasema anaamini baada ya oparesheni hiyo, chini ya baraka za Mwenyezi Mungu jamii ya Eneo la Kati itamtawaza kama msemaji. Muhimu kwa sasa, Njenga anasema si kufikiria ni nani msemaji ila ni kuleta watu pamoja. “Kitu cha maana ni umoja, upendo wa nchi na vile watu watakuja pamoja,” Bw Njenga akasema, kupitia video. Katika matamshi yaliyoashiria kulenga Naibu wa Rais, Rigathi Gachagua na baadhi ya wanasiasa Mlimani, Njenga ambaye pia ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Wakfu wa Amani Sasa, alisema viongozi waliochaguliwa Mlima Kenya wanaonekana kujali maslahi yao pekee, ikiwa ni pamoja na kulinda biashara zao “badala ya kutetea nafasi ya Mkikuyu serikalini”. Alisema ndio sababu amepata shinikizo kujituma kuleta jamii ya pamoja. “Kitu ambacho nimeanza kusimama nacho ni umoja…Yule atakayeunganisha watu wake wote, na kuwaonyesha upendo na njia, huyo ndiye atakuwa Msemaji Mlimani,” alielezea. Bw Gachagua, akiwa ndiye kiongozi wa pili mashuhuri katika serikali ya Kenya Kwanza, anachukuliwa kama Msemaji wa Eneo la Kati, ila Njenga anasema kofia hiyo ingali imevaliwa na Rais mstaafu, Uhuru Kenyatta. “Uhuru Kenyatta hajastaafu kama mwenyekiti wa Jubilee na Azimio. Hata hivyo, mambo yakinyooka tutaita sherehe kutawaza atakayeteuliwa kuongoza jamii ya Mlima Kenya,” Bw Njenga alisema. “Kwa sasa tuko mbioni kuleta pamoja watu wote, na ninaamini mwisho kabisa mimi nitakuwa – Kingpin. Nitakuwa, nikimaliza hii kazi. Maana wengine wote, sioni kama kunaye ako tayari. Wengine wako biashara zao. Mimi niko tayari kushikana na watu wa Mlima, kuwaonyesha njia, kuwajulisha tunaenda wapi, tunatoka wapi na kuwafunza maneno ya biashara ili tusimame imara kama Mlima.” Jitihada zake, alisema zisitafsiriwe isivyofaa kwani eneo la Bonde la Ufa lina chama tawala cha UDA – Kinachoongozwa na Rais William Ruto, Nyanza ODM (Raila Odinga) na Ukambani, Wiper (Kalonzo Musyoka). Bidii alizonazo, Maina Njenga anasema zitasaidia jamii ya Mlimani kupata minofu mikubwa hasa baada ya Ripoti ya Kamati ya Maridhiano, kati ya upinzani – Azimio na Serikali ya Kenya Kwanza kutangazwa. “Tukiwa na umoja kama jamii, ripoti ya kamati ya maridhiano ikitangazwa tutakuwa na sauti na msimamo mmoja kuagiza tunachotaka serikalini.” Bw Njenga, alisema baada ya kuafikia malengo yake kuleta jamii pamoja, atatangaza uwezekano wa eneo la Mlima Kenya kuwa na chama. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA SAMMY WAWERU ALIYEKUWA kiongozi wa kundi haramu la Mungiki, Maina Njenga ameeleza imani yake kuwa mikakati aliyoweka kuleta pamoja jamii ya Mlima Kenya itamuwezesha kuwa msemaji wa eneo hilo – Kingpin. Kulingana na mwanasiasa huyu ambaye pia ni Askofu wa Kanisa la Hope International, kwa sasa yuko mbioni kuunganisha jamii ya Agikuyu. Anasema anaamini baada ya oparesheni hiyo, chini ya baraka za Mwenyezi Mungu jamii ya Eneo la Kati itamtawaza kama msemaji. Muhimu kwa sasa, Njenga anasema si kufikiria ni nani msemaji ila ni kuleta watu pamoja. “Kitu cha maana ni umoja, upendo wa nchi na vile watu watakuja pamoja,” Bw Njenga akasema, kupitia video. Katika matamshi yaliyoashiria kulenga Naibu wa Rais, Rigathi Gachagua na baadhi ya wanasiasa Mlimani, Njenga ambaye pia ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Wakfu wa Amani Sasa, alisema viongozi waliochaguliwa Mlima Kenya wanaonekana kujali maslahi yao pekee, ikiwa ni pamoja na kulinda biashara zao “badala ya kutetea nafasi ya Mkikuyu serikalini”. Alisema ndio sababu amepata shinikizo kujituma kuleta jamii ya pamoja. “Kitu ambacho nimeanza kusimama nacho ni umoja…Yule atakayeunganisha watu wake wote, na kuwaonyesha upendo na njia, huyo ndiye atakuwa Msemaji Mlimani,” alielezea. Bw Gachagua, akiwa ndiye kiongozi wa pili mashuhuri katika serikali ya Kenya Kwanza, anachukuliwa kama Msemaji wa Eneo la Kati, ila Njenga anasema kofia hiyo ingali imevaliwa na Rais mstaafu, Uhuru Kenyatta. “Uhuru Kenyatta hajastaafu kama mwenyekiti wa Jubilee na Azimio. Hata hivyo, mambo yakinyooka tutaita sherehe kutawaza atakayeteuliwa kuongoza jamii ya Mlima Kenya,” Bw Njenga alisema. “Kwa sasa tuko mbioni kuleta pamoja watu wote, na ninaamini mwisho kabisa mimi nitakuwa – Kingpin. Nitakuwa, nikimaliza hii kazi. Maana wengine wote, sioni kama kunaye ako tayari. Wengine wako biashara zao. Mimi niko tayari kushikana na watu wa Mlima, kuwaonyesha njia, kuwajulisha tunaenda wapi, tunatoka wapi na kuwafunza maneno ya biashara ili tusimame imara kama Mlima.” Jitihada zake, alisema zisitafsiriwe isivyofaa kwani eneo la Bonde la Ufa lina chama tawala cha UDA – Kinachoongozwa na Rais William Ruto, Nyanza ODM (Raila Odinga) na Ukambani, Wiper (Kalonzo Musyoka). Bidii alizonazo, Maina Njenga anasema zitasaidia jamii ya Mlimani kupata minofu mikubwa hasa baada ya Ripoti ya Kamati ya Maridhiano, kati ya upinzani – Azimio na Serikali ya Kenya Kwanza kutangazwa. “Tukiwa na umoja kama jamii, ripoti ya kamati ya maridhiano ikitangazwa tutakuwa na sauti na msimamo mmoja kuagiza tunachotaka serikalini.” Bw Njenga, alisema baada ya kuafikia malengo yake kuleta jamii pamoja, atatangaza uwezekano wa eneo la Mlima Kenya kuwa na chama. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU RAIS William Ruto, Naibu wake Rigathi Gachagua na Waziri wa Ulinzi Kenya, Aden Duale wametangaza vita vikali dhidi ya Al-Shabaab ambao wamekuwa wakihangaisha Lamu na kaunti zingine za Kaskazini mwa Kenya, wakiwataka magaidi hao kuhama Kenya ama kusafiri kwenda mbinguni. Wakihutubia umma katika kisiwa cha Kizingitini huko Lamu Mashariki wakati wa ziara ya kuzindua miradi ya maendeleo, viongozi hao walieleza kukerwa kwao na hulka ya magaidi kupenya nchini, kuvamia na hata kuua wananchi wasio na hatia na kuharibu mali. Kati ya Juni na Septemba mwaka huu, 2023, vijiji, hasa vile vya Lamu Magharibi na vichache vya Lamu Mashariki vimeshuhudia uvamizi wa Al-Shabaab, ambapo watu zaidi ya 30, wakiwemo walinda usalama na raia wameuawa na nyumba zaidi ya 20 na makanisa yakiteketezwa na magaidi hao. Baadhi ya vijiji vilivyoshuhudia mashambulizi hayo ni Juhudi, Salama, Widho, Marafa, Ukumbi, Mashogoni, Nyongoro, Lango la Simba, Pandanguo na Mlima Faru, vyote vikipatikana Lamu Magharibi ilhali vile vya Lamu Mashariki ni pamoja na Bodhei, Baure, Mararani, Sarira, Milimani na viunga mwake. Kwenye hotuba yake, Rais Ruto alishikilia kuwa utawala wake katu hautaruhusu magaidi kuendelea kutawala nchini, akidokeza kuwa tayari amezungumza na mawaziri, hasa wale wanaohusiana na usalama wa ndani na ulinzi wa nchi kuona kwamba vita dhidi ya Al-Shabaab vinazidishwa nguvu. “Nataka kuweka wazi kwamba wale magaidi wanaojidai kuhangaisha Lamu mjue tutapambana na nyinyi. Hatuwezi kuruhusu wahalifu na magaidi waje kujenga kibanda hapa. Na ndio sababu tumekubaliana na mawaziri kwamba magaidi lazima watoke hii Lamu, na wasipotoka tutapambana na wao. Mambo ya magaidi hapa ni aidha watoke Kenya ama wasafiri waende mbinguni,” akasema Dkt Ruto. Naibu wa Rais Rigathi Gachagua naye aliwasihi wananchi wa Lamu na viongozi kuepuka kugawanywa na magaidi na badala yake waungane kumpiga na kumshinda adui huyo. “Mambo ya usalama ningependa kushauri hivi; Viongozi hapa mko na jukumu la kuwazungumzia wananchi kwa njia inayofaa ili baadaye isije kubadilika kuwa uchochezi na kuleta uhasama kati ya jamii, makabila na dini,” akasema Bw Gachagua. Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi, Aden Duale aliwasisitizia viongozi wa Lamu na wananchi kuungana na kumtambua adui mmoja anayefaa kumalizwa ambaye ni Al-Shabaab. Bw Duale alisema serikali iko chonjo kumpiga Al-Shabaab ndani ya Somalia na pia kwenye mpaka wa Kenya na nchi hiyo jirani. Waziri huyo wa Ulinzi, hata hivyo, aliwaonya wale wanaoshirikiana na magaidi kutekeleza uvamizi Lamu, akisema siku zao zimehesabiwa. Bw Duale, hata hivyo, alitaja kuwa ziara zake za kila mara Lamu, ambapo amekuwa akikutana na kujadiliana na viongozi na wananchi zimezaa matunda kwani idadi ya visa vya mashambulizi ya magaidi vimepungua pakubwa eneo hilo siku za hivi karibuni. “Nawashukuru nyinyi viongozi na wananchi hapa Lamu. Ujio wangu wa kila mara hapa naona tayari umezaa matunda. Tuko chonjo. Ukikadiria utapata kuwa ni majuma mengi yamepita bila kushuhudia mashambulio ya Al-Shabaab. Tuzidi kushirikiana na kuepuka kunyosheana vidole vya lawama. Tujue kwamba tunamuwinda na kumkabili adui mmoja dhidi yetu ambaye ni Al-Shabaab na tutamshinda,” akasema Bw Duale. Naye Gavana wa Lamu, Issa Timamy, aliishukuru serikali kuu, kupitia Wizara za Ulinzi na ile ya Usalama wa Ndani kwa kuhakikisha utovu wa usalama unaochangiwa na magaidi Lamu unakabiliwa vilivyo na kupunguzwa. “Twashukuru serikali kuu na maafisa wetu wa usalama, wakiwemo wanajeshi (KDF) kwa juhudi zao katika kuhakikisha Lamu iko na amani. Tutazidi kushirikiana kuhakikisha Lamu na nchi nzima kwa ujumla ni tulivu ili maendeleo yaafikiwe ipasavyo,” akasema Bw Timamy.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU RAIS William Ruto, Naibu wake Rigathi Gachagua na Waziri wa Ulinzi Kenya, Aden Duale wametangaza vita vikali dhidi ya Al-Shabaab ambao wamekuwa wakihangaisha Lamu na kaunti zingine za Kaskazini mwa Kenya, wakiwataka magaidi hao kuhama Kenya ama kusafiri kwenda mbinguni. Wakihutubia umma katika kisiwa cha Kizingitini huko Lamu Mashariki wakati wa ziara ya kuzindua miradi ya maendeleo, viongozi hao walieleza kukerwa kwao na hulka ya magaidi kupenya nchini, kuvamia na hata kuua wananchi wasio na hatia na kuharibu mali. Kati ya Juni na Septemba mwaka huu, 2023, vijiji, hasa vile vya Lamu Magharibi na vichache vya Lamu Mashariki vimeshuhudia uvamizi wa Al-Shabaab, ambapo watu zaidi ya 30, wakiwemo walinda usalama na raia wameuawa na nyumba zaidi ya 20 na makanisa yakiteketezwa na magaidi hao. Baadhi ya vijiji vilivyoshuhudia mashambulizi hayo ni Juhudi, Salama, Widho, Marafa, Ukumbi, Mashogoni, Nyongoro, Lango la Simba, Pandanguo na Mlima Faru, vyote vikipatikana Lamu Magharibi ilhali vile vya Lamu Mashariki ni pamoja na Bodhei, Baure, Mararani, Sarira, Milimani na viunga mwake. Kwenye hotuba yake, Rais Ruto alishikilia kuwa utawala wake katu hautaruhusu magaidi kuendelea kutawala nchini, akidokeza kuwa tayari amezungumza na mawaziri, hasa wale wanaohusiana na usalama wa ndani na ulinzi wa nchi kuona kwamba vita dhidi ya Al-Shabaab vinazidishwa nguvu. “Nataka kuweka wazi kwamba wale magaidi wanaojidai kuhangaisha Lamu mjue tutapambana na nyinyi. Hatuwezi kuruhusu wahalifu na magaidi waje kujenga kibanda hapa. Na ndio sababu tumekubaliana na mawaziri kwamba magaidi lazima watoke hii Lamu, na wasipotoka tutapambana na wao. Mambo ya magaidi hapa ni aidha watoke Kenya ama wasafiri waende mbinguni,” akasema Dkt Ruto. Naibu wa Rais Rigathi Gachagua naye aliwasihi wananchi wa Lamu na viongozi kuepuka kugawanywa na magaidi na badala yake waungane kumpiga na kumshinda adui huyo. “Mambo ya usalama ningependa kushauri hivi; Viongozi hapa mko na jukumu la kuwazungumzia wananchi kwa njia inayofaa ili baadaye isije kubadilika kuwa uchochezi na kuleta uhasama kati ya jamii, makabila na dini,” akasema Bw Gachagua. Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi, Aden Duale aliwasisitizia viongozi wa Lamu na wananchi kuungana na kumtambua adui mmoja anayefaa kumalizwa ambaye ni Al-Shabaab. Bw Duale alisema serikali iko chonjo kumpiga Al-Shabaab ndani ya Somalia na pia kwenye mpaka wa Kenya na nchi hiyo jirani. Waziri huyo wa Ulinzi, hata hivyo, aliwaonya wale wanaoshirikiana na magaidi kutekeleza uvamizi Lamu, akisema siku zao zimehesabiwa. Bw Duale, hata hivyo, alitaja kuwa ziara zake za kila mara Lamu, ambapo amekuwa akikutana na kujadiliana na viongozi na wananchi zimezaa matunda kwani idadi ya visa vya mashambulizi ya magaidi vimepungua pakubwa eneo hilo siku za hivi karibuni. “Nawashukuru nyinyi viongozi na wananchi hapa Lamu. Ujio wangu wa kila mara hapa naona tayari umezaa matunda. Tuko chonjo. Ukikadiria utapata kuwa ni majuma mengi yamepita bila kushuhudia mashambulio ya Al-Shabaab. Tuzidi kushirikiana na kuepuka kunyosheana vidole vya lawama. Tujue kwamba tunamuwinda na kumkabili adui mmoja dhidi yetu ambaye ni Al-Shabaab na tutamshinda,” akasema Bw Duale. Naye Gavana wa Lamu, Issa Timamy, aliishukuru serikali kuu, kupitia Wizara za Ulinzi na ile ya Usalama wa Ndani kwa kuhakikisha utovu wa usalama unaochangiwa na magaidi Lamu unakabiliwa vilivyo na kupunguzwa. “Twashukuru serikali kuu na maafisa wetu wa usalama, wakiwemo wanajeshi (KDF) kwa juhudi zao katika kuhakikisha Lamu iko na amani. Tutazidi kushirikiana kuhakikisha Lamu na nchi nzima kwa ujumla ni tulivu ili maendeleo yaafikiwe ipasavyo,” akasema Bw Timamy.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI. WANAFUNZI wengi wa vyuo vikuu nchini wanalala njaa, Bodi ya Ufadhili wa Masomo ya Juu (HELB) ikizidi kuchelewa kutuma pesa. Wanakula mlo mmoja kwa siku, huku baadhi wakilazimika kusaka vibarua mjini. Kwenye mahojiano na baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Machakos, wanasema hawana budi ila kuingia Mjini Machakos na Wote kusaka vibarua kukidhi mahitaji yao ya kimsingi kama vile kununua chakula, mavazi na data za simu. Wanasisitiza ni wajibu wa serikali kugharamia masomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao, bila changamoto zozote kwani pesa zenyewe huwa zimetengwa na serikali. Taifa Leo Dijitali ilipozuru Chuo Kikuu Cha Machakos, tulishangaa kugundua hadi kufikia sasa idadi kubwa ya wanafunzi – Comrades wanasubiri kupokea mikopo ya HELB, huu ukiwa ni mwezi wa tatu tangu muhula uanze. “Comrades tunateseka na kwa sababu hiyo tumepatia serikali makataa ya wiki moja kutuma pesa za HELB la sivyo tutaitisha maandamano,” anasema Irene Kakui, mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika kitivo cha Elimu. Bi Kakui anasema wanafunzi wengi wanajiandaa kukalia mtihani wa mwisho wa mwaka, kabla ya kutawanyika kwa ajili ya Sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya. Ila cha kuvunja moyo haitawezekana kufanya mtihani kwa sababu hawajalipa karo. Kulingana na Kakui, huu ni wakati mwafaka kwa serikali na Wizara ya Elimu kuanza kuangazia matatizo ya wanafunzi, ikizingatiwa kuwa wengi wao wanatoka kwa familia maskini na hawana ufadhili. “Nchi ikiendelea kukabiliwa na mzozo mkali wa kiuchumi, wanafunzi wengine mpaka leo hawajawahi kukanyaga darasani kwa sababu ya kuhangaika wakifanya kazi,” akasema. Kauli ya mwanafunzi huyo inapigwa jeki na Brian Koech, ambaye pia anasomea kozi ya ualimu. “Ndio maana wengi hushiriki kwenye visa vya udanganyifu wa mitihani au kuwalipa wenzao ili kuwafanyia mitihani,” Koech akasema. Anashauri washikadau katika sekta ya elimu, kutafuta suluhu ya kudumu ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapokea hela za matumizi kwa wakati unaofaa ili wasitaabike.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI. WANAFUNZI wengi wa vyuo vikuu nchini wanalala njaa, Bodi ya Ufadhili wa Masomo ya Juu (HELB) ikizidi kuchelewa kutuma pesa. Wanakula mlo mmoja kwa siku, huku baadhi wakilazimika kusaka vibarua mjini. Kwenye mahojiano na baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Machakos, wanasema hawana budi ila kuingia Mjini Machakos na Wote kusaka vibarua kukidhi mahitaji yao ya kimsingi kama vile kununua chakula, mavazi na data za simu. Wanasisitiza ni wajibu wa serikali kugharamia masomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao, bila changamoto zozote kwani pesa zenyewe huwa zimetengwa na serikali. Taifa Leo Dijitali ilipozuru Chuo Kikuu Cha Machakos, tulishangaa kugundua hadi kufikia sasa idadi kubwa ya wanafunzi – Comrades wanasubiri kupokea mikopo ya HELB, huu ukiwa ni mwezi wa tatu tangu muhula uanze. “Comrades tunateseka na kwa sababu hiyo tumepatia serikali makataa ya wiki moja kutuma pesa za HELB la sivyo tutaitisha maandamano,” anasema Irene Kakui, mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika kitivo cha Elimu. Bi Kakui anasema wanafunzi wengi wanajiandaa kukalia mtihani wa mwisho wa mwaka, kabla ya kutawanyika kwa ajili ya Sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya. Ila cha kuvunja moyo haitawezekana kufanya mtihani kwa sababu hawajalipa karo. Kulingana na Kakui, huu ni wakati mwafaka kwa serikali na Wizara ya Elimu kuanza kuangazia matatizo ya wanafunzi, ikizingatiwa kuwa wengi wao wanatoka kwa familia maskini na hawana ufadhili. “Nchi ikiendelea kukabiliwa na mzozo mkali wa kiuchumi, wanafunzi wengine mpaka leo hawajawahi kukanyaga darasani kwa sababu ya kuhangaika wakifanya kazi,” akasema. Kauli ya mwanafunzi huyo inapigwa jeki na Brian Koech, ambaye pia anasomea kozi ya ualimu. “Ndio maana wengi hushiriki kwenye visa vya udanganyifu wa mitihani au kuwalipa wenzao ili kuwafanyia mitihani,” Koech akasema. Anashauri washikadau katika sekta ya elimu, kutafuta suluhu ya kudumu ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapokea hela za matumizi kwa wakati unaofaa ili wasitaabike.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU RAIS William Ruto, Naibu wake Rigathi Gachagua na Waziri wa Ulinzi Aden Duale wametangaza vita vikali dhidi ya Al-Shabaab ambao wamekuwa wakihangaisha Lamu na kaunti nyingine za Kaskazini mwa Kenya, wakiwataka magaidi hao kujua ujanja wao umefika kikomo.  Wakihutubia umma katika kisiwa cha Kizingitini huko Lamu Mashariki wakati wa ziara ya kuzindua miradi ya maendeleo, viongozi hao walieleza kukerwa kwao na hulka ya magaidi kupenya nchini, kuvamia na hata  kuua wananchi wasio na hatia na kuharibu mali. Kati ya Juni na Septemba mwaka huu, vijiji, hasa vile vya Lamu Magharibi na vichache vya Lamu Mashariki vimeshuhudia uvamizi wa Al-Shabaab, ambapo watu zaidi ya 30, ikiwemo walinda usalama na raia wameuawa ilhali nyumba zaidi ya 20 na kanisa vikiteketezwa na magaidi hao. Baadhi ya vijiji vilivyoshuhudia mashambulizi hayo ni Juhudi, Salama, Widho, Marafa, Ukumbi, Mashogoni, Nyongoro, Lango la Simba, Pandanguo na Mlima Faru, vyote vikipatikana Lamu Magharibi ilhali vile vya Lamu Mashariki ni pamoja na Bodhei, Baure, Mararani, Sarira, Milimani na viungani mwake. Kwenye hotuba yake, Rais Ruto alishikilia kuwa utawala wake katu hautaruhusu magaidi kuendelea kutawala nchini, akitaja kuwa tayari amezungumza na mawaziri, hasa wale wanaohusiana na usalama wa ndani na ulinzi wan chi kuona kwamba vita dhidi ya Al-Shabaab vinazidishwa nguvu. “Nataka kuweka wazi kwamba wale magaidi wanaojidai kuhangaisha Lamu mjue tutapambana na nyinyi. Hatuwezi kuruhusu wahalifu na magaidi waje kujenga kibanda hapa. Na ndio sababu tumekubaliana na mawaziri kwamba magaidi lazima watoke hii Lamu, na wasipotoka tutapambana na wao . Mambo ya magaidi hapa aidha watoke Kenya ama wasafiri waende mbinguni,” akasema Dkt Ruto. Naibu wa Rais Rigathi Gachagua aliwasihi wananchi wa Lamu na viongozi kuepuka kugawanywa na magaidi na badala yake waungane kumpiga na kumshinda adui huyo. “Mambo ya usalama ningependa kushauri hivi. Viongozi hapa mko na jukumu la kuwazungumzia wananchi kwa njia inayofaa ili baadaye isije kubadilika kuwa uchochezi na kuleta uhasama kati ya jamii, makabila na dini,” akasema Dkt Gachagua. Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi, Aden Duale aliwasisitizia viongozi wa Lamu na wananchi kuungana na kumtambua adui mmoja anayefaa kumalizwa ambaye ni Al-Shabaab. Bw Duale alisema serikali iko chonjo kumpiga Al-Shabaab ndani ya Somalia na pia kwenye mpaka wa Kenya nan chi hiyo jirani. Waziri huyo wa Ulinzi hata hivyo aliwaonya wale wanaoshirikiana na magaidi kutekeleza uvamizi Lamu, akisema siku zao zimehesabiwa. Bw Duale hata hivyo alitaja kuwa ziara zake za kila mara Lamu, ambapo amekuwa akikutana na kujadiliana na viongozi na wananchi zimezaa matunda kwani idadi ya visa vya mashambulio ya magaidi vimepungua pakubwa eneo hilo siku za hivi karibuni. “Nawashukuru nyinyi viongozi na wananchi hapa Lamu. Ujio wangu wa kila mara hapa naona tayari umezaa matunda. Tuko chonjo. Ukikadiria utapata kuwa ni majuma mengi yamepita bila kushuhudia mashambulio ya Al-Shabaab. Tuzidi kushirikiana na kuepuka kunyosheana vidole vya lawama. Tujue kwamba tunamwinda na kumkabili adui mmoja dhidi yetu ambaye ni Al-Shabaab na tutamshinda,” akasema Bw Duale. Naye Gavana wa Lamu, Issa Timamy, aliishukuru serikali kuu, kupitia Wizara za Ulinzi na ile ya Usalama wa Ndani kwa kuhakikisha utovu wa usalama unaochangiwa na magaidi Lamu unakabiliwa vilivyo na kupunguzwa. “Twashukuru serikali kuu na maafisa wetu wa usalama, wakiwemo wanajeshi (KDF) kwa juhudi zao katika kuhakikisha Lamu iko na amani. Tutazidi kushirikiana kuhakikisha Lamu na nchi nzima kwa ujumla ni tulivu ili maendeleo yaafikiwe ipasavyo,” akasema Bw Timamy. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA KALUME KAZUNGU RAIS William Ruto, Naibu wake Rigathi Gachagua na Waziri wa Ulinzi Aden Duale wametangaza vita vikali dhidi ya Al-Shabaab ambao wamekuwa wakihangaisha Lamu na kaunti nyingine za Kaskazini mwa Kenya, wakiwataka magaidi hao kujua ujanja wao umefika kikomo.  Wakihutubia umma katika kisiwa cha Kizingitini huko Lamu Mashariki wakati wa ziara ya kuzindua miradi ya maendeleo, viongozi hao walieleza kukerwa kwao na hulka ya magaidi kupenya nchini, kuvamia na hata  kuua wananchi wasio na hatia na kuharibu mali. Kati ya Juni na Septemba mwaka huu, vijiji, hasa vile vya Lamu Magharibi na vichache vya Lamu Mashariki vimeshuhudia uvamizi wa Al-Shabaab, ambapo watu zaidi ya 30, ikiwemo walinda usalama na raia wameuawa ilhali nyumba zaidi ya 20 na kanisa vikiteketezwa na magaidi hao. Baadhi ya vijiji vilivyoshuhudia mashambulizi hayo ni Juhudi, Salama, Widho, Marafa, Ukumbi, Mashogoni, Nyongoro, Lango la Simba, Pandanguo na Mlima Faru, vyote vikipatikana Lamu Magharibi ilhali vile vya Lamu Mashariki ni pamoja na Bodhei, Baure, Mararani, Sarira, Milimani na viungani mwake. Kwenye hotuba yake, Rais Ruto alishikilia kuwa utawala wake katu hautaruhusu magaidi kuendelea kutawala nchini, akitaja kuwa tayari amezungumza na mawaziri, hasa wale wanaohusiana na usalama wa ndani na ulinzi wan chi kuona kwamba vita dhidi ya Al-Shabaab vinazidishwa nguvu. “Nataka kuweka wazi kwamba wale magaidi wanaojidai kuhangaisha Lamu mjue tutapambana na nyinyi. Hatuwezi kuruhusu wahalifu na magaidi waje kujenga kibanda hapa. Na ndio sababu tumekubaliana na mawaziri kwamba magaidi lazima watoke hii Lamu, na wasipotoka tutapambana na wao . Mambo ya magaidi hapa aidha watoke Kenya ama wasafiri waende mbinguni,” akasema Dkt Ruto. Naibu wa Rais Rigathi Gachagua aliwasihi wananchi wa Lamu na viongozi kuepuka kugawanywa na magaidi na badala yake waungane kumpiga na kumshinda adui huyo. “Mambo ya usalama ningependa kushauri hivi. Viongozi hapa mko na jukumu la kuwazungumzia wananchi kwa njia inayofaa ili baadaye isije kubadilika kuwa uchochezi na kuleta uhasama kati ya jamii, makabila na dini,” akasema Dkt Gachagua. Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi, Aden Duale aliwasisitizia viongozi wa Lamu na wananchi kuungana na kumtambua adui mmoja anayefaa kumalizwa ambaye ni Al-Shabaab. Bw Duale alisema serikali iko chonjo kumpiga Al-Shabaab ndani ya Somalia na pia kwenye mpaka wa Kenya nan chi hiyo jirani. Waziri huyo wa Ulinzi hata hivyo aliwaonya wale wanaoshirikiana na magaidi kutekeleza uvamizi Lamu, akisema siku zao zimehesabiwa. Bw Duale hata hivyo alitaja kuwa ziara zake za kila mara Lamu, ambapo amekuwa akikutana na kujadiliana na viongozi na wananchi zimezaa matunda kwani idadi ya visa vya mashambulio ya magaidi vimepungua pakubwa eneo hilo siku za hivi karibuni. “Nawashukuru nyinyi viongozi na wananchi hapa Lamu. Ujio wangu wa kila mara hapa naona tayari umezaa matunda. Tuko chonjo. Ukikadiria utapata kuwa ni majuma mengi yamepita bila kushuhudia mashambulio ya Al-Shabaab. Tuzidi kushirikiana na kuepuka kunyosheana vidole vya lawama. Tujue kwamba tunamwinda na kumkabili adui mmoja dhidi yetu ambaye ni Al-Shabaab na tutamshinda,” akasema Bw Duale. Naye Gavana wa Lamu, Issa Timamy, aliishukuru serikali kuu, kupitia Wizara za Ulinzi na ile ya Usalama wa Ndani kwa kuhakikisha utovu wa usalama unaochangiwa na magaidi Lamu unakabiliwa vilivyo na kupunguzwa. “Twashukuru serikali kuu na maafisa wetu wa usalama, wakiwemo wanajeshi (KDF) kwa juhudi zao katika kuhakikisha Lamu iko na amani. Tutazidi kushirikiana kuhakikisha Lamu na nchi nzima kwa ujumla ni tulivu ili maendeleo yaafikiwe ipasavyo,” akasema Bw Timamy. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA NDUBI MOTURI KIONGOZI wa chama cha Wiper, Bw Kalonzo Musyoka, ameilaumu serikali kutokana na kuongezeka ufisadi kwenye bajeti na kuanza utekelezaji wa vitambulisho vya kidijitali, licha ya hali ngumu ya kiuchumi ambayo nchi inapitia. Bw Musyoka alisema utekelezaji wa mpango huo si muhimu kwa sasa, licha ya kupewa kipao mbele na serikali. Kiongozi huyo alisema kuwa ufichuzi wa Msimamizi Mkuu wa Bajeti (COB) Margaret Nyakang’o, kwamba amekuwa akilipwa mshahara wake mara tatu zaidi ya kiwango kinachotakikana wakati nchi inapitia hali ngumu, ni ishara kwamba utawala wa Kenya Kwanza umepoteza mwelekeo. “Msimamizi wa bajeti alifika mbele ya Kamati ya Mazungumzo ya Maridhiano na alizungumza kama mtaalamu. Tulimsikiliza kwa makini. Aliwasilisha takwimu, ambapo mambo aliyosema yalituacha katika mshangao. Alisema hakupata ufafanuzi kuhusu sababu ambapo mshahara wake ulizidishwa mara tatu huku, ukilipwa watu wengine, wala si yeye. Tunangoja maelezo kutoka kwa serikali,” akasema Bw Musyoka. Alisema pia Wizara ya Fedha inafaa kujitokeza wazi na kutoa ufafanuzi kuhusu ufichuzi uliotolewa na Bi Nyakang’o kuhusu wizi wa fedha za umma. Akirejelea mazungumzo ya maridhiano yanayoendelea na ambayo ripoti yake inatarajiwa kutolewa wiki chache zijazo, Bw Musyoka alisema kwa mrengo wa Azimio la Umoja bado unashikilia kuwa lazima kuwe na ukaguzi kuhusu uchaguzi wa urais mwaka 2022 na kushughulikiwa kwa gharama ya juu ya maisha. Bw Musyoka alionya kwamba muungano huo utachukua hatua ikiwa masuala hayo mawili hayatashughulikiwa. “Nawarai wabunge wasiisaliti nchi. Tunawahitaji watu waadilifu kama msimamizi wa bajeti. Kama Wakenya, msitamauke. Bado hatujapata suluhisho kuhusu yale yaliyofanyika kwenye uchaguzi wa urais mwaka 2022. Wakenya wanapitia hali ngumu ya kimaisha, lakini serikali ishaanza kampeni za 2027. Tunaendelea na mazungumzo. Ikiwa hawatafanya tunavyowaagiza, mtaona,” akasema. Vile vile, alimlaumu Rais William Ruto kuhusu mipango ya kuanzisha vitambulisho vya kidijitali, akiitaja kuwa kinyume na azma ya Wakenya wengi. “Serikali imesema inataka kuanzisha vitambulisho vya kidijitali. Hiyo ni ishara kwamba nyakati za mwisho zimefika. Wahubiri na viongozi wa kidini wanafaa kujitokeza na kutueleza. Rais Ruto mwenyewe alisema watakuwa wakitumia macho yenu kuwatambua. Eti mtoto wako akizaliwa, atawekwa kidude. Tumekataa hayo,” akaongeza. Bw Musyoka, aliyehudumu kama Makamu wa Rais kati ya 2008 na 2013, alikuwa akihutubu katika Kanisa la Kiadventista la Umoja II, Nairobi, ambapo alikuwa ameandamana na Maseneta na wabunge kutoka Azimio. Wakati wa hafla hiyo, viongozi walisema kuwa gharama ya juu ya maisha ndilo suala linalofaa kupewa kipao mbele kwenye ripoti ya kamati ya mazungumzo ya maridhiano. Walisema kuwa ikiwa hilo halitatimizwa, basi Wakenya wataanza kuandamana tena. Viongozi kadhaa pia walimsifu Bw Musyoka kwa ushujaa wake, wakisema kuwa atakuwa debeni kwenye uchaguzi mkuu wa urais 2027. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA NDUBI MOTURI KIONGOZI wa chama cha Wiper, Bw Kalonzo Musyoka, ameilaumu serikali kutokana na kuongezeka ufisadi kwenye bajeti na kuanza utekelezaji wa vitambulisho vya kidijitali, licha ya hali ngumu ya kiuchumi ambayo nchi inapitia. Bw Musyoka alisema utekelezaji wa mpango huo si muhimu kwa sasa, licha ya kupewa kipao mbele na serikali. Kiongozi huyo alisema kuwa ufichuzi wa Msimamizi Mkuu wa Bajeti (COB) Margaret Nyakang’o, kwamba amekuwa akilipwa mshahara wake mara tatu zaidi ya kiwango kinachotakikana wakati nchi inapitia hali ngumu, ni ishara kwamba utawala wa Kenya Kwanza umepoteza mwelekeo. “Msimamizi wa bajeti alifika mbele ya Kamati ya Mazungumzo ya Maridhiano na alizungumza kama mtaalamu. Tulimsikiliza kwa makini. Aliwasilisha takwimu, ambapo mambo aliyosema yalituacha katika mshangao. Alisema hakupata ufafanuzi kuhusu sababu ambapo mshahara wake ulizidishwa mara tatu huku, ukilipwa watu wengine, wala si yeye. Tunangoja maelezo kutoka kwa serikali,” akasema Bw Musyoka. Alisema pia Wizara ya Fedha inafaa kujitokeza wazi na kutoa ufafanuzi kuhusu ufichuzi uliotolewa na Bi Nyakang’o kuhusu wizi wa fedha za umma. Akirejelea mazungumzo ya maridhiano yanayoendelea na ambayo ripoti yake inatarajiwa kutolewa wiki chache zijazo, Bw Musyoka alisema kwa mrengo wa Azimio la Umoja bado unashikilia kuwa lazima kuwe na ukaguzi kuhusu uchaguzi wa urais mwaka 2022 na kushughulikiwa kwa gharama ya juu ya maisha. Bw Musyoka alionya kwamba muungano huo utachukua hatua ikiwa masuala hayo mawili hayatashughulikiwa. “Nawarai wabunge wasiisaliti nchi. Tunawahitaji watu waadilifu kama msimamizi wa bajeti. Kama Wakenya, msitamauke. Bado hatujapata suluhisho kuhusu yale yaliyofanyika kwenye uchaguzi wa urais mwaka 2022. Wakenya wanapitia hali ngumu ya kimaisha, lakini serikali ishaanza kampeni za 2027. Tunaendelea na mazungumzo. Ikiwa hawatafanya tunavyowaagiza, mtaona,” akasema. Vile vile, alimlaumu Rais William Ruto kuhusu mipango ya kuanzisha vitambulisho vya kidijitali, akiitaja kuwa kinyume na azma ya Wakenya wengi. “Serikali imesema inataka kuanzisha vitambulisho vya kidijitali. Hiyo ni ishara kwamba nyakati za mwisho zimefika. Wahubiri na viongozi wa kidini wanafaa kujitokeza na kutueleza. Rais Ruto mwenyewe alisema watakuwa wakitumia macho yenu kuwatambua. Eti mtoto wako akizaliwa, atawekwa kidude. Tumekataa hayo,” akaongeza. Bw Musyoka, aliyehudumu kama Makamu wa Rais kati ya 2008 na 2013, alikuwa akihutubu katika Kanisa la Kiadventista la Umoja II, Nairobi, ambapo alikuwa ameandamana na Maseneta na wabunge kutoka Azimio. Wakati wa hafla hiyo, viongozi walisema kuwa gharama ya juu ya maisha ndilo suala linalofaa kupewa kipao mbele kwenye ripoti ya kamati ya mazungumzo ya maridhiano. Walisema kuwa ikiwa hilo halitatimizwa, basi Wakenya wataanza kuandamana tena. Viongozi kadhaa pia walimsifu Bw Musyoka kwa ushujaa wake, wakisema kuwa atakuwa debeni kwenye uchaguzi mkuu wa urais 2027. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FARHIYA HUSSEIN “WALIVUNJA mlango wangu saa nane usiku nikiwa nimelala karibu na mtoto wangu wa umri wa mwaka mmoja. Mlango huo wa chuma uliharibu kuta na athari ilijeruhi mkono wangu wa kushoto… Nina majeraha kwenye mapaja yangu.” Haya yalikuwa maneno ya machungu ya Bi Mwanaisha Abdallah mkazi wa Mombasa aliyekuwa akirejelea shambulio la Alhamisi nyumbani kwake, ambapo usiku huo mumewe alitekwa nyara na watu wasiojulikana. “Nilisikia mtu akijaribu kufungua mlango lakini dakika chache baadaye niliona giza. Waliingia zaidi ya wanaume 10 waliovalia sare za kivita zinazofanana na magwanda ya wanajeshi. Walikuwa na silaha kamili na wakiwa wamefunika nyuso zao,” anaeleza Bi Abdallah. Anasema kitu kama guruneti kilitupwa mlangoni. Kulingana na Bi Abdallah, watu hao wasiojulikana walimwagiza mumewe Bw Hassan Lamini amkabidhi mtoto wao wa umri wa mwaka mmoja ambaye alikuwa amembeba. “Mume wangu aliamrishwa kutoa simu yake ya mkononi, kisha watu hao ambao walikuwa wameficha nyuso zao wakaelekea chumbani mwetu na chooni ambako walipekua kwa kina kana kwamba walikuwa wakitafuta kitu,” aeleza Bi Abdallah, akisema watu hao wasiojulikana walimpatia huduma ya kwanza baada ya kuona anavuja damu nyingi kutoka kwa mkono. Bi Abdallah anasema baada ya watu hao kukosa walichokuwa wakitafuta, walimtia pingu mumewe na kuondoka naye, na hadi kufikia sasa familia haijui yuko wapi. Baba yake Hassan, Bw Lamini Omar anasema mwanawe ni mtu mpole na alikuwa nchini kwa muda usiozidi mwaka mmoja baada ya kurejea kutoka Qatar ambako alikuwa akifanya kazi ya usafi. “Anatakiwa kurejea Qatar mwezi ujao, tumeshalipa Sh50,000 na tupo kwenye harakati za kukamilisha taratibu za safari yake. Mwanangu hajawahi kukamatwa na ndiyo maana nawasihi waliomteka nyara wamrudishe kwa wema na ikiwa ana kesi ya kujibu basi afikishwe mahakamani,” akasema Bw Omar. Mama yake Hassan, Bi Fatuma Badi ambaye anaishi na ulemavu wa macho, amesikitishwa na hali iliyomtokea mwanaye wa kiume. “Yeye ndiye kitinda mimba na mwana wa kiume pekee. Ninaomba kwa upole kurejeshwa kwa mwanangu. Nilifanyiwa upasuaji wa jicho juzi na hali imezidi kuwa mbaya zaidi,” alisema Bi Badi huku akilia. Afisa wa Dharura Shirika la Haki Africa, Bw Mathias Shipeta alibainisha kuwa hii ni kesi ya nne ya watu kupotezwa kwa njia ya kutatanisha eneo la Pwani katika muda wa wiki moja. “Rais alibaini kuwa utekaji nyara wa nguvu utakomeshwa, nini kinatokea? Tunaomba serikali iingilie kati na kutafuta suluhu. Kesi nne ambazo tumepokea, moja ilikuwa ya Lamu na tatu kutoka Kaunti ya Mombasa,” alisema Bw Shipeta. Familia ya kijana mwenye umri wa miaka 22 ambaye anashukiwa kutekwa nyara siku ya Jumatatu imefichua kwamba alichukuliwa na gari aina ya Land Cruiser siku hiyo jioni na hajaonekana tangu wakati huo. Akizungumza na Taifa Jumapili, Bi Husna Sharrif, ambaye ni dada mkubwa wa Abdulkadir Sharrif Ali ameelezea jinsi kaka yake alivyochukuliwa na watu wasiojulikana ambao waliondoka naye. “Nilipokea simu kutoka kwa mtu ambaye alinijulisha kuwa Abdulkadir alichukuliwa na wanaume sita waliovalia sare za polisi na hatujamsikia wala kumuona tangu kutokea kwa tukio hilo,” akasema Bi Shariff. Abdulkadir aliripotiwa kutekwa nyara na maafisa wa usalama mwezi Oktoba 30, 2023, huko Witu, Lamu, mwendo wa saa kumi jioni. Tukio hili liliripotiwa katika Kituo cha Polisi cha Wito chini ya nambari ya OB. 26/30/10/2023. Aidha Husna alisema kuwa gari hilo aina ya Land Cruiser halikuwa na alama za kuonyesha lilipotoka na kuongeza kuwa watu wanne walikuwa nyuma na wawili wakiwa wamekaa mbele. Alimtaja kaka yake kama mtu mtulivu ambaye alikuwa amesafiri kufanya kazi nchini Qatar kwa mwaka mmoja tangu 2018 na alirejea nchini mwaka wa 2019 baada ya mkataba wake kumalizika. “Tangu aliporudi kutoka Qatar, kaka yangu amekuwa akifanya kazi za mkono ili kujikimu. Ni mwanafunzi aliyemaliza Kidato cha Nne,” aliongeza. Bi Husna aliongeza kuwa Abdulkadir hajawahi kukamatwa na hajawahi kumweleza kuhusu mtu yeyote kumfuatilia. Pia aliongeza kuwa Abdulkadir ni baba wa mtoto mmoja na mke wake ni mjamzito wa miezi mitano sasa. Alitoweka vipi? Shahidi aliyezaliwa na kukulia huko Witu, Kaunti ya Lamu, Bw Issa Ahmed, alisema si tukio la kwanza na kwamba vijana wengi wameathiriwa na kupotea kwa njia tatanishi. “Tunaiomba serikali kumrejesha mmoja wetu akiwa salama baada ya kumfahamu kuwa mtulivu na mpenda amani,” alisema Bw Ahmed. Aliiambia Taifa Jumapili kuwa Abdulkadir alichukuliwa mbele yake na marafiki wake katika hoteli ya Bash Bash alipokuwa na mazungumzo na rafiki mmoja. “Alichukuliwa na wanaume wanne waliovalia sare zinazofanana na za wanajeshi alipokuwa akiongea na rafiki wake. Nyuso zao zilikuwa zimefichwa na walikuwa wamebeba bunduki,” aliongeza. Issa ambaye pia ni dereva wa babake Abdulkadir alisema watu wasiojulikana walimchukua Abdulkadir na mwingine ambaye aliondoka nao. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FARHIYA HUSSEIN “WALIVUNJA mlango wangu saa nane usiku nikiwa nimelala karibu na mtoto wangu wa umri wa mwaka mmoja. Mlango huo wa chuma uliharibu kuta na athari ilijeruhi mkono wangu wa kushoto… Nina majeraha kwenye mapaja yangu.” Haya yalikuwa maneno ya machungu ya Bi Mwanaisha Abdallah mkazi wa Mombasa aliyekuwa akirejelea shambulio la Alhamisi nyumbani kwake, ambapo usiku huo mumewe alitekwa nyara na watu wasiojulikana. “Nilisikia mtu akijaribu kufungua mlango lakini dakika chache baadaye niliona giza. Waliingia zaidi ya wanaume 10 waliovalia sare za kivita zinazofanana na magwanda ya wanajeshi. Walikuwa na silaha kamili na wakiwa wamefunika nyuso zao,” anaeleza Bi Abdallah. Anasema kitu kama guruneti kilitupwa mlangoni. Kulingana na Bi Abdallah, watu hao wasiojulikana walimwagiza mumewe Bw Hassan Lamini amkabidhi mtoto wao wa umri wa mwaka mmoja ambaye alikuwa amembeba. “Mume wangu aliamrishwa kutoa simu yake ya mkononi, kisha watu hao ambao walikuwa wameficha nyuso zao wakaelekea chumbani mwetu na chooni ambako walipekua kwa kina kana kwamba walikuwa wakitafuta kitu,” aeleza Bi Abdallah, akisema watu hao wasiojulikana walimpatia huduma ya kwanza baada ya kuona anavuja damu nyingi kutoka kwa mkono. Bi Abdallah anasema baada ya watu hao kukosa walichokuwa wakitafuta, walimtia pingu mumewe na kuondoka naye, na hadi kufikia sasa familia haijui yuko wapi. Baba yake Hassan, Bw Lamini Omar anasema mwanawe ni mtu mpole na alikuwa nchini kwa muda usiozidi mwaka mmoja baada ya kurejea kutoka Qatar ambako alikuwa akifanya kazi ya usafi. “Anatakiwa kurejea Qatar mwezi ujao, tumeshalipa Sh50,000 na tupo kwenye harakati za kukamilisha taratibu za safari yake. Mwanangu hajawahi kukamatwa na ndiyo maana nawasihi waliomteka nyara wamrudishe kwa wema na ikiwa ana kesi ya kujibu basi afikishwe mahakamani,” akasema Bw Omar. Mama yake Hassan, Bi Fatuma Badi ambaye anaishi na ulemavu wa macho, amesikitishwa na hali iliyomtokea mwanaye wa kiume. “Yeye ndiye kitinda mimba na mwana wa kiume pekee. Ninaomba kwa upole kurejeshwa kwa mwanangu. Nilifanyiwa upasuaji wa jicho juzi na hali imezidi kuwa mbaya zaidi,” alisema Bi Badi huku akilia. Afisa wa Dharura Shirika la Haki Africa, Bw Mathias Shipeta alibainisha kuwa hii ni kesi ya nne ya watu kupotezwa kwa njia ya kutatanisha eneo la Pwani katika muda wa wiki moja. “Rais alibaini kuwa utekaji nyara wa nguvu utakomeshwa, nini kinatokea? Tunaomba serikali iingilie kati na kutafuta suluhu. Kesi nne ambazo tumepokea, moja ilikuwa ya Lamu na tatu kutoka Kaunti ya Mombasa,” alisema Bw Shipeta. Familia ya kijana mwenye umri wa miaka 22 ambaye anashukiwa kutekwa nyara siku ya Jumatatu imefichua kwamba alichukuliwa na gari aina ya Land Cruiser siku hiyo jioni na hajaonekana tangu wakati huo. Akizungumza na Taifa Jumapili, Bi Husna Sharrif, ambaye ni dada mkubwa wa Abdulkadir Sharrif Ali ameelezea jinsi kaka yake alivyochukuliwa na watu wasiojulikana ambao waliondoka naye. “Nilipokea simu kutoka kwa mtu ambaye alinijulisha kuwa Abdulkadir alichukuliwa na wanaume sita waliovalia sare za polisi na hatujamsikia wala kumuona tangu kutokea kwa tukio hilo,” akasema Bi Shariff. Abdulkadir aliripotiwa kutekwa nyara na maafisa wa usalama mwezi Oktoba 30, 2023, huko Witu, Lamu, mwendo wa saa kumi jioni. Tukio hili liliripotiwa katika Kituo cha Polisi cha Wito chini ya nambari ya OB. 26/30/10/2023. Aidha Husna alisema kuwa gari hilo aina ya Land Cruiser halikuwa na alama za kuonyesha lilipotoka na kuongeza kuwa watu wanne walikuwa nyuma na wawili wakiwa wamekaa mbele. Alimtaja kaka yake kama mtu mtulivu ambaye alikuwa amesafiri kufanya kazi nchini Qatar kwa mwaka mmoja tangu 2018 na alirejea nchini mwaka wa 2019 baada ya mkataba wake kumalizika. “Tangu aliporudi kutoka Qatar, kaka yangu amekuwa akifanya kazi za mkono ili kujikimu. Ni mwanafunzi aliyemaliza Kidato cha Nne,” aliongeza. Bi Husna aliongeza kuwa Abdulkadir hajawahi kukamatwa na hajawahi kumweleza kuhusu mtu yeyote kumfuatilia. Pia aliongeza kuwa Abdulkadir ni baba wa mtoto mmoja na mke wake ni mjamzito wa miezi mitano sasa. Alitoweka vipi? Shahidi aliyezaliwa na kukulia huko Witu, Kaunti ya Lamu, Bw Issa Ahmed, alisema si tukio la kwanza na kwamba vijana wengi wameathiriwa na kupotea kwa njia tatanishi. “Tunaiomba serikali kumrejesha mmoja wetu akiwa salama baada ya kumfahamu kuwa mtulivu na mpenda amani,” alisema Bw Ahmed. Aliiambia Taifa Jumapili kuwa Abdulkadir alichukuliwa mbele yake na marafiki wake katika hoteli ya Bash Bash alipokuwa na mazungumzo na rafiki mmoja. “Alichukuliwa na wanaume wanne waliovalia sare zinazofanana na za wanajeshi alipokuwa akiongea na rafiki wake. Nyuso zao zilikuwa zimefichwa na walikuwa wamebeba bunduki,” aliongeza. Issa ambaye pia ni dereva wa babake Abdulkadir alisema watu wasiojulikana walimchukua Abdulkadir na mwingine ambaye aliondoka nao. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA BARNABAS BII WASAGAJI nchini wanakadiria hasara kutokana na kupungua kwa mauzo ya unga wa mahindi wa pakiti, baada ya wateja wengi kuegemea aina tofauti ya chakula kutokana na kupanda kwa bei ya unga na bidhaa nyingine za matumizi ya msingi. Wakenya wengi sasa wameamua kutumia unga wa mahindi wa kisiagi badala ya ule wa pakiti, kwani bei yake ni ya chini, ikilinganishwa na wa pakiti. Ni hali ambayo imeathiri sana mauzo ya wasagaji. “Huwa ninanunua kilo mbili za mahindi kwa Sh100 na kuzisaga kwa Sh20. Gharama hiyo ni ya chini sana kuliko kununua unga wa pakiti,” akasema Bi Jane Kosgei, kutoka eneo la Saos, Kaunti ya Nandi. Pakiti ya kilo mbili ya unga wa mahindi inauzwa kwa kati ya Sh165 na Sh195 katika maduka mengi ya jumla katika eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa. Wakulima wengi wanataja bei hizo kuwa za juu sana, ikizingatiwa kuwa huu ni msimu wa mavuno. Pia, kuna mahindi ambayo yamekuwa yakiingizwa nchini kutoka mataifa ya Tanzania na Uganda. Bei za mahindi zimeshuka kutoka Sh6, 200 hadi Sh3, 600 kwa miezi miwili iliyopita, hali ambayo imekuwa afueni kwa Wakenya wengi.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA BARNABAS BII WASAGAJI nchini wanakadiria hasara kutokana na kupungua kwa mauzo ya unga wa mahindi wa pakiti, baada ya wateja wengi kuegemea aina tofauti ya chakula kutokana na kupanda kwa bei ya unga na bidhaa nyingine za matumizi ya msingi. Wakenya wengi sasa wameamua kutumia unga wa mahindi wa kisiagi badala ya ule wa pakiti, kwani bei yake ni ya chini, ikilinganishwa na wa pakiti. Ni hali ambayo imeathiri sana mauzo ya wasagaji. “Huwa ninanunua kilo mbili za mahindi kwa Sh100 na kuzisaga kwa Sh20. Gharama hiyo ni ya chini sana kuliko kununua unga wa pakiti,” akasema Bi Jane Kosgei, kutoka eneo la Saos, Kaunti ya Nandi. Pakiti ya kilo mbili ya unga wa mahindi inauzwa kwa kati ya Sh165 na Sh195 katika maduka mengi ya jumla katika eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa. Wakulima wengi wanataja bei hizo kuwa za juu sana, ikizingatiwa kuwa huu ni msimu wa mavuno. Pia, kuna mahindi ambayo yamekuwa yakiingizwa nchini kutoka mataifa ya Tanzania na Uganda. Bei za mahindi zimeshuka kutoka Sh6, 200 hadi Sh3, 600 kwa miezi miwili iliyopita, hali ambayo imekuwa afueni kwa Wakenya wengi.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA BARNABAS BII WASAGAJI nchini wanakadiria hasara kutokana na kupungua kwa mauzo ya unga wa mahindi wa pakiti, baada ya wateja wengi kuegemea aina tofauti ya chakula kutokana na kupanda kwa bei ya unga na bidhaa nyingine za matumizi ya msingi. Wakenya wengi ambao awali walikuwa na maringo, sasa wameamua kutumia unga wa mahindi wa ‘kisiagi’ badala ya ule wa pakiti, kwani bei yake ni ya chini, ikilinganishwa na wa pakiti. Ni hali ambayo imeathiri sana mauzo ya wasagaji. “Huwa ninanunua kilo mbili za mahindi kwa Sh100 na kuzisaga kwa Sh20. Gharama hiyo ni ya chini sana kuliko kununua unga wa pakiti,” akasema Bi Jane Kosgei, kutoka eneo la Saos, Kaunti ya Nandi. Pakiti ya kilo mbili za unga wa mahindi inauzwa kwa kati ya Sh165 na Sh195 katika maduka mengi ya jumla katika eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa. Wakulima wengi wanataja bei hizo kuwa za juu sana, ikizingatiwa kuwa huu ni msimu wa mavuno. Pia, kuna mahindi ambayo yamekuwa yakiingizwa nchini kutoka mataifa ya Tanzania na Uganda. Bei za mahindi zimeshuka kutoka Sh6,200 hadi Sh3,600 kwa miezi miwili iliyopita, hali ambayo imekuwa afueni kwa Wakenya wengi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA BARNABAS BII WASAGAJI nchini wanakadiria hasara kutokana na kupungua kwa mauzo ya unga wa mahindi wa pakiti, baada ya wateja wengi kuegemea aina tofauti ya chakula kutokana na kupanda kwa bei ya unga na bidhaa nyingine za matumizi ya msingi. Wakenya wengi ambao awali walikuwa na maringo, sasa wameamua kutumia unga wa mahindi wa ‘kisiagi’ badala ya ule wa pakiti, kwani bei yake ni ya chini, ikilinganishwa na wa pakiti. Ni hali ambayo imeathiri sana mauzo ya wasagaji. “Huwa ninanunua kilo mbili za mahindi kwa Sh100 na kuzisaga kwa Sh20. Gharama hiyo ni ya chini sana kuliko kununua unga wa pakiti,” akasema Bi Jane Kosgei, kutoka eneo la Saos, Kaunti ya Nandi. Pakiti ya kilo mbili za unga wa mahindi inauzwa kwa kati ya Sh165 na Sh195 katika maduka mengi ya jumla katika eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa. Wakulima wengi wanataja bei hizo kuwa za juu sana, ikizingatiwa kuwa huu ni msimu wa mavuno. Pia, kuna mahindi ambayo yamekuwa yakiingizwa nchini kutoka mataifa ya Tanzania na Uganda. Bei za mahindi zimeshuka kutoka Sh6,200 hadi Sh3,600 kwa miezi miwili iliyopita, hali ambayo imekuwa afueni kwa Wakenya wengi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MHARIRI
BAADHI ya shule nchini zimejitokeza na kupinga matokeo ya Mtihani ya Darasa la Nane (KCPE) yaliyotangazwa Jumatano na Waziri... NA MHARIRI