text
stringlengths
3
16.2k
NA ELVIS ONDIEKI MMOJA wa watoto walioponea mauti kanisa lilipochomwa kijijini Kiambaa, kaunti ya Uasin Gishu, mnamo Januari 1, 2008, amesema amewasamehe wote waliomdhuru. Anthony Mbuthia, 26, alikuwa na umri wa miaka 10 mkasa huo ulipotokea. Anakumbuka kusafiri kutoka kijiji cha Yamumbi, mwendo wa kama dakika 30 kwa gari hadi Kiambaa. Alikuwa amesafiri na familia yake kusherehekea Krismasi na nyanya yake maafa yalipotokea. Kwa sasa, Anthony anaishi Marekani, ambako anamiliki kampuni ya kupiga picha na kutengeneza filamu. Katika mahojiano na Taifa Jumapili wiki jana, alisema hana sababu ya kumchukia yeyote. Pia anasema imani yake kwa Mungu haitatikisika. “Pale Marekani, watu wamekuwa wakiniuliza, ‘Mbona bado waenda kanisani? Mbona bado wajihushisha na kanisa? Ulichomwa ndani ya kanisa, mbona huna machungu?’ Wanataraji niwe na hasira, nichukie watu. Lakini naamini kuwa kiasi kingi cha kupona kwangu kimefanyika ndani yangu na nje kupitia kwa kusamehe. Niliweza kuwasamehe walionifanyia walichonifanyia,” alisema. “Wakati mwingine mimi hujilinganisha na Yesu aliposema msalabani, ‘Wasamehe kwa vile hawajui watendalo.’ Usemi hio ni wenye nguvu kwa sababu ilinibidi kuwasamehe watu ndipo nipone,” aliongeza Anthony. Kutokana na makovu ya usoni yaliyosababishwa na kuchomeka mikononi, usoni na kichwani, Anthony alidhihakiwa sana na watoto wenzake darasani ambao walimbandika majina ya kukera na hata kumvua kofia yake kwa lazima ili kuona “kama ana ubongo”. Kwa sasa, anawahimiza watoto wowote watakaosimangwa kwa muonekano wao kujipa moyo. “Usije ukadhani ni wewe mwenye shida. Usikubali maneno ya wanaokudhihaki yakuingie akilini. Hao ni watu wenye shida kivyao,” anashauri. “Kilicho ndani yako kinafaa kusikika zaidi ya kile unachokisikia nje.” Anthony ameandika kitabu kipya, Triumph over Adversity, ambacho alikizindua pale Marekani mwezi Oktoba. Kitabu hicho pia kinauzwa nchini kwenye duka la vitabu la Nuria. Mnamo 2019, babake Anthony, Peter Mbuthia – ambaye aliwahi kujitokeza wazi akisema alikuwa shahidi kwenye kesi ya mauaji ya halaiki kwenye International Criminal Court – alichapisha kitabu chenye anwani Scars of a Nation. Kwenye kitabu chake, Anthony anasimulia kilichotendeka Jumanne ile walipojikuta kwenye ua wa kanisa la Kenya Assemblies of God, wakidhani hawangeshambuliwa wakijisitiri kanisani. Wakazi wengi wa Kiambaa walikuwa wakimuunga mkono rais Mwai Kibaki ilihali eneo hilo lilikuwa ngome ya Raila Odinga wakati huo. Anasema kuwa kundi la watu waliokuwa wamepaka rangi nyuso zao lilivamia eneo hilo wakati wa adhuhuri. Kuwasili kwa kundi hilo lililokuwa limejihami kuliwalazimu Anthony na ndugu zake wawili kutorokea kanisani. Watu wengi walitorokea mle, wasijue kuwa washambuliaji wangewasha moto baadaye. Anthony anasimulia kuwa alikanyagwa akiwa sakafuni na watu waliokuwa waking’ang’ana kutafuta upenyu baada ya moto kuwashwa, na kuwa alikuwa miongoni mwa watu wa mwisho kabisa kuondoka mle. Watu wasiopungua 18 walichomwa hadi kufa ndani ya kanisa hilo. Anthony anasimulia kuwa kunusurika kwake kulikuwa muujiza kwani hadi leo hajaelewa fika ni vipi alitoka kwenye kanisa lile. Baadaye alipata gari la Msamaria Mwema lililosafirisha walionusurika moto huo hadi Moi Teaching and Referral Hospital. Alitibiwa pale kwa miezi mitatu kabla ya kuhamishwa hadi hospitali ya Kijabe. Baada ya kutoka Kijabe, alikokaa kwa takriban miezi saba, alihudhuria masomo kwa kipindi kifupi kabla ya kusafiri Marekani. Safari ya Marekani iliwezeshwa kupitia mchango wa wahisani. Kutokana na kampeni iliyowekwa kuwaauni watoto waliohasirika Kiambaa, Rais Mwai Kibaki alikutana na watoto hao katika ikulu ya Nairobi kabla wasafiri kupata matibabu zaidi. Anthony alitibiwa kwa takriban miaka mitano, huku akifanyiwa upasuaji mara kadha. Anakadiria kuwa alifanyiwa upasuaji mara 100, na baadhi ya matibabu yalijumuisha kukatwa ngozi kwenye sehemu moja ya mwili na kuipachika katika sehemu nyingine. Anthony na wasichana watatu waliosafiri Marekani, ambao walibandikwa jina “The Kiambaa Four”, sasa wamekita mizizi pale Marekani. “Kunaye ailiyeitwa Mary. Ameolewa na ana watoto ninaoamini ni wanne. Pia kuna Mercy. Alipata masomo na alipata shahada yake mwaka 2023 kwenye chuo cha UC Davis. Pia ameolewa na ana mtoto. Mimi bado sijaoa, niko soko. Halafu kunaye Jedidah. Kwa sasa ni mwanafunzi katika Sacramento State University,” alisema Anthony. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA ELVIS ONDIEKI MMOJA wa watoto walioponea mauti kanisa lilipochomwa kijijini Kiambaa, kaunti ya Uasin Gishu, mnamo Januari 1, 2008, amesema amewasamehe wote waliomdhuru. Anthony Mbuthia, 26, alikuwa na umri wa miaka 10 mkasa huo ulipotokea. Anakumbuka kusafiri kutoka kijiji cha Yamumbi, mwendo wa kama dakika 30 kwa gari hadi Kiambaa. Alikuwa amesafiri na familia yake kusherehekea Krismasi na nyanya yake maafa yalipotokea. Kwa sasa, Anthony anaishi Marekani, ambako anamiliki kampuni ya kupiga picha na kutengeneza filamu. Katika mahojiano na Taifa Jumapili wiki jana, alisema hana sababu ya kumchukia yeyote. Pia anasema imani yake kwa Mungu haitatikisika. “Pale Marekani, watu wamekuwa wakiniuliza, ‘Mbona bado waenda kanisani? Mbona bado wajihushisha na kanisa? Ulichomwa ndani ya kanisa, mbona huna machungu?’ Wanataraji niwe na hasira, nichukie watu. Lakini naamini kuwa kiasi kingi cha kupona kwangu kimefanyika ndani yangu na nje kupitia kwa kusamehe. Niliweza kuwasamehe walionifanyia walichonifanyia,” alisema. “Wakati mwingine mimi hujilinganisha na Yesu aliposema msalabani, ‘Wasamehe kwa vile hawajui watendalo.’ Usemi hio ni wenye nguvu kwa sababu ilinibidi kuwasamehe watu ndipo nipone,” aliongeza Anthony. Kutokana na makovu ya usoni yaliyosababishwa na kuchomeka mikononi, usoni na kichwani, Anthony alidhihakiwa sana na watoto wenzake darasani ambao walimbandika majina ya kukera na hata kumvua kofia yake kwa lazima ili kuona “kama ana ubongo”. Kwa sasa, anawahimiza watoto wowote watakaosimangwa kwa muonekano wao kujipa moyo. “Usije ukadhani ni wewe mwenye shida. Usikubali maneno ya wanaokudhihaki yakuingie akilini. Hao ni watu wenye shida kivyao,” anashauri. “Kilicho ndani yako kinafaa kusikika zaidi ya kile unachokisikia nje.” Anthony ameandika kitabu kipya, Triumph over Adversity, ambacho alikizindua pale Marekani mwezi Oktoba. Kitabu hicho pia kinauzwa nchini kwenye duka la vitabu la Nuria. Mnamo 2019, babake Anthony, Peter Mbuthia – ambaye aliwahi kujitokeza wazi akisema alikuwa shahidi kwenye kesi ya mauaji ya halaiki kwenye International Criminal Court – alichapisha kitabu chenye anwani Scars of a Nation. Kwenye kitabu chake, Anthony anasimulia kilichotendeka Jumanne ile walipojikuta kwenye ua wa kanisa la Kenya Assemblies of God, wakidhani hawangeshambuliwa wakijisitiri kanisani. Wakazi wengi wa Kiambaa walikuwa wakimuunga mkono rais Mwai Kibaki ilihali eneo hilo lilikuwa ngome ya Raila Odinga wakati huo. Anasema kuwa kundi la watu waliokuwa wamepaka rangi nyuso zao lilivamia eneo hilo wakati wa adhuhuri. Kuwasili kwa kundi hilo lililokuwa limejihami kuliwalazimu Anthony na ndugu zake wawili kutorokea kanisani. Watu wengi walitorokea mle, wasijue kuwa washambuliaji wangewasha moto baadaye. Anthony anasimulia kuwa alikanyagwa akiwa sakafuni na watu waliokuwa waking’ang’ana kutafuta upenyu baada ya moto kuwashwa, na kuwa alikuwa miongoni mwa watu wa mwisho kabisa kuondoka mle. Watu wasiopungua 18 walichomwa hadi kufa ndani ya kanisa hilo. Anthony anasimulia kuwa kunusurika kwake kulikuwa muujiza kwani hadi leo hajaelewa fika ni vipi alitoka kwenye kanisa lile. Baadaye alipata gari la Msamaria Mwema lililosafirisha walionusurika moto huo hadi Moi Teaching and Referral Hospital. Alitibiwa pale kwa miezi mitatu kabla ya kuhamishwa hadi hospitali ya Kijabe. Baada ya kutoka Kijabe, alikokaa kwa takriban miezi saba, alihudhuria masomo kwa kipindi kifupi kabla ya kusafiri Marekani. Safari ya Marekani iliwezeshwa kupitia mchango wa wahisani. Kutokana na kampeni iliyowekwa kuwaauni watoto waliohasirika Kiambaa, Rais Mwai Kibaki alikutana na watoto hao katika ikulu ya Nairobi kabla wasafiri kupata matibabu zaidi. Anthony alitibiwa kwa takriban miaka mitano, huku akifanyiwa upasuaji mara kadha. Anakadiria kuwa alifanyiwa upasuaji mara 100, na baadhi ya matibabu yalijumuisha kukatwa ngozi kwenye sehemu moja ya mwili na kuipachika katika sehemu nyingine. Anthony na wasichana watatu waliosafiri Marekani, ambao walibandikwa jina “The Kiambaa Four”, sasa wamekita mizizi pale Marekani. “Kunaye ailiyeitwa Mary. Ameolewa na ana watoto ninaoamini ni wanne. Pia kuna Mercy. Alipata masomo na alipata shahada yake mwaka 2023 kwenye chuo cha UC Davis. Pia ameolewa na ana mtoto. Mimi bado sijaoa, niko soko. Halafu kunaye Jedidah. Kwa sasa ni mwanafunzi katika Sacramento State University,” alisema Anthony. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FRIDAH OKACHI SIMU za mikopo zinazopatikana kwa urahisi mitaani zimetajwa kuwa ‘mwokozi’ wa raia wa mapato ya chini. Wananchi katika kiwango hicho wamekumbatia mbinu hiyo ya kukopa simu na kulipia kiasi kidogokidogo cha pesa ili kuwezesha mawasiliano na jamaa zao wawapo mbali. Bi Mary Wanjiru ambaye ni mkazi wa Ngando aliambia Taifa Jumapili kuwa kununua simu hiyo ya bei kwa mpango wa ‘lipa polepole’ kunamwezesha kufanya shughuli zake za kila siku bila wasiwasi. Anawasiliana na jamaa zake nyumbani kwa siku tatu kila juma. “Niliona ni afadhali ninunue simu hii ya Sh28,500. Nalipia mdogomdogo. Kila siku ninalipa Sh79 ili kuwezesha mawasiliano,” alisema Bi Wanjiru. Alifichua kuwa “nisipolipa hakuna mawasiliano nitafanya kwa sababu inafungwa”. Simu hizo zinauzwa dukani, zikiwa na bei tofauti. Ya bei ya juu ikiwa ni Sh50,000 na ya chini zaidi ikiwa nin ya Sh19,000. Bi Wanjiru anasifia njia hiyo ambayo alisema itawezesha watu wengi kuwa na simu. “Saa hii kila mtu anafaa kuwa na Smartphone. Sihitaji kwenda mjini kusubiri offer kama hapo nyuma. Sh50 hadi 80 unaweza lipa iwapo unafanya kibarua cha kila siku. Kijana Hussein Kingi mwenye umri wa miaka 29 alisema alichukua hatua ya kununua simu hiyo baada ya kuvamiwa na wezi akitoka kazini majira ya jioni. Alichukua hatua ya kununua upesi ili asikose wateja wake ambao hununua bidhaa zake za useremala. “Hii kazi yangu nahitaji kuwa na simu kila wakati. Lau ningesusia kufanya maamuzi ya haraka ningepoteza wateja,” alisema Bw Kingi. Bw Kingi ambaye ni seremala hutengemea simu kufanya kazi zake za kila siku kwa kupakia picha za bidhaa zake mtandaoni ili kuvutia wateja. “Mbinu hiyo imenisaidia kuwezesha wateja wangu kuangalia meza na viti vinavyowapendeza,” akaeleza Bw Kingi. Muuzaji katika duka la Ruby Hub Bw Christopher Wambua alisema kila siku hupata wateja zaidi ya 10 ambao huchukua na kuanza kulipia simu hizo. Bw Wambua alisema biashara ya kuuza simu hizo kunoga siku za wikendi. “Wengi wanaonunua simu hizo kwa mpangilio huo wa malipo ya polepole ni wanawake na vijana. Wateja hao huja kutokana na simu zao kuwa zimeharibika na wakati huo hakuwa amepangia kununua. Hii inawapa uwezo huo,” alisema Bw Wambua. “Hapa wateja wangu hukosa kulipa kila siku na badala yake kulipia mnamo wikendi. Wengi wao huwa wamelipwa na hivyo mteja analipa Sh548. Hiyo ikiwa ni zile pesa za kila siku kwa wiki,” aliongeza Bw Wambua. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA), ni asilimia 61 ya Wakenya wanaomiliki simu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FRIDAH OKACHI SIMU za mikopo zinazopatikana kwa urahisi mitaani zimetajwa kuwa ‘mwokozi’ wa raia wa mapato ya chini. Wananchi katika kiwango hicho wamekumbatia mbinu hiyo ya kukopa simu na kulipia kiasi kidogokidogo cha pesa ili kuwezesha mawasiliano na jamaa zao wawapo mbali. Bi Mary Wanjiru ambaye ni mkazi wa Ngando aliambia Taifa Jumapili kuwa kununua simu hiyo ya bei kwa mpango wa ‘lipa polepole’ kunamwezesha kufanya shughuli zake za kila siku bila wasiwasi. Anawasiliana na jamaa zake nyumbani kwa siku tatu kila juma. “Niliona ni afadhali ninunue simu hii ya Sh28,500. Nalipia mdogomdogo. Kila siku ninalipa Sh79 ili kuwezesha mawasiliano,” alisema Bi Wanjiru. Alifichua kuwa “nisipolipa hakuna mawasiliano nitafanya kwa sababu inafungwa”. Simu hizo zinauzwa dukani, zikiwa na bei tofauti. Ya bei ya juu ikiwa ni Sh50,000 na ya chini zaidi ikiwa nin ya Sh19,000. Bi Wanjiru anasifia njia hiyo ambayo alisema itawezesha watu wengi kuwa na simu. “Saa hii kila mtu anafaa kuwa na Smartphone. Sihitaji kwenda mjini kusubiri offer kama hapo nyuma. Sh50 hadi 80 unaweza lipa iwapo unafanya kibarua cha kila siku. Kijana Hussein Kingi mwenye umri wa miaka 29 alisema alichukua hatua ya kununua simu hiyo baada ya kuvamiwa na wezi akitoka kazini majira ya jioni. Alichukua hatua ya kununua upesi ili asikose wateja wake ambao hununua bidhaa zake za useremala. “Hii kazi yangu nahitaji kuwa na simu kila wakati. Lau ningesusia kufanya maamuzi ya haraka ningepoteza wateja,” alisema Bw Kingi. Bw Kingi ambaye ni seremala hutengemea simu kufanya kazi zake za kila siku kwa kupakia picha za bidhaa zake mtandaoni ili kuvutia wateja. “Mbinu hiyo imenisaidia kuwezesha wateja wangu kuangalia meza na viti vinavyowapendeza,” akaeleza Bw Kingi. Muuzaji katika duka la Ruby Hub Bw Christopher Wambua alisema kila siku hupata wateja zaidi ya 10 ambao huchukua na kuanza kulipia simu hizo. Bw Wambua alisema biashara ya kuuza simu hizo kunoga siku za wikendi. “Wengi wanaonunua simu hizo kwa mpangilio huo wa malipo ya polepole ni wanawake na vijana. Wateja hao huja kutokana na simu zao kuwa zimeharibika na wakati huo hakuwa amepangia kununua. Hii inawapa uwezo huo,” alisema Bw Wambua. “Hapa wateja wangu hukosa kulipa kila siku na badala yake kulipia mnamo wikendi. Wengi wao huwa wamelipwa na hivyo mteja analipa Sh548. Hiyo ikiwa ni zile pesa za kila siku kwa wiki,” aliongeza Bw Wambua. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA), ni asilimia 61 ya Wakenya wanaomiliki simu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MATATIZO ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA), jijini Nairobi, yameibua maswali kuhusu ikiwa Kenya iko tayari kutekeleza mpango wa kuondoa hitaji la stakabadhi ya viza kwa wageni wanaowasili nchini kutoka nchi za nje. Kwa miaka michache iliyopita, JKIA pamoja na Shirika la Kenya Airways (KQ) zimekuwa zikiandamwa na kila aina ya matatizo. Kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita, KQ imekuwa ikipata hasara ya mabilioni ya pesa karibu kila mwaka, licha ya juhudi za serikali kujaribu kuisaidia kuanza kupata faida. Ni hali ambayo kwa wakati mmoja ilizua ghadhabu miongoni mwa Wakenya, kwamba serikali ilikuwa ikielekeza mabilioni ya fedha katika shirika hilo, licha ya juhudi hizo kutozaa matunda. Kando na shirika hilo, msururu wa matatizo umekuwa ukishuhudiwa katika uwanja wa JKIA, hali ambayo imezua tashwishi kuhusu ikiwa Kenya itafaulu kutekeleza mpango wa kuwaruhusu raia wa kigeni kuingia nchini bila viza kuanzia mwaka 2024, kama alivyoahidi Rais William Ruto wakati wa sherehe za Sikukuu ya Jamhuri mnamo Desemba 12, 2023. Kulingana na wataalamu wa masuala ya kiuchumi, matatizo hayo yanahatarisha mustakabali wa KQ, ikiwa serikali haitachukua hatua za haraka kulainisha baadhi ya matatizo yaliyopo. “Shirika la KQ lilikuwa linasifika sana katika miaka ya 1990 na 2000 kutokana na ubora wa huduma zake.  Lilikuwa kwenye ligi moja na mashirika mengine ya ndege duniani kama vile  Lufthansa, Panama, Delta, KLM kati ya mengine. Hata hivyo, matatizo yanayolikumba yanazua hofu kuhusu ikiwa liko tayari kuwapokea watu kutoka kote duniani kuanzia Januari, ikiwa serikali itafutilia mbali hitaji la viza,” asema Bw James Shikwati, ambaye ni mtaalamu na mdadisi wa masuala ya kiuchumi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MATATIZO ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA), jijini Nairobi, yameibua maswali kuhusu ikiwa Kenya iko tayari kutekeleza mpango wa kuondoa hitaji la stakabadhi ya viza kwa wageni wanaowasili nchini kutoka nchi za nje. Kwa miaka michache iliyopita, JKIA pamoja na Shirika la Kenya Airways (KQ) zimekuwa zikiandamwa na kila aina ya matatizo. Kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita, KQ imekuwa ikipata hasara ya mabilioni ya pesa karibu kila mwaka, licha ya juhudi za serikali kujaribu kuisaidia kuanza kupata faida. Ni hali ambayo kwa wakati mmoja ilizua ghadhabu miongoni mwa Wakenya, kwamba serikali ilikuwa ikielekeza mabilioni ya fedha katika shirika hilo, licha ya juhudi hizo kutozaa matunda. Kando na shirika hilo, msururu wa matatizo umekuwa ukishuhudiwa katika uwanja wa JKIA, hali ambayo imezua tashwishi kuhusu ikiwa Kenya itafaulu kutekeleza mpango wa kuwaruhusu raia wa kigeni kuingia nchini bila viza kuanzia mwaka 2024, kama alivyoahidi Rais William Ruto wakati wa sherehe za Sikukuu ya Jamhuri mnamo Desemba 12, 2023. Kulingana na wataalamu wa masuala ya kiuchumi, matatizo hayo yanahatarisha mustakabali wa KQ, ikiwa serikali haitachukua hatua za haraka kulainisha baadhi ya matatizo yaliyopo. “Shirika la KQ lilikuwa linasifika sana katika miaka ya 1990 na 2000 kutokana na ubora wa huduma zake.  Lilikuwa kwenye ligi moja na mashirika mengine ya ndege duniani kama vile  Lufthansa, Panama, Delta, KLM kati ya mengine. Hata hivyo, matatizo yanayolikumba yanazua hofu kuhusu ikiwa liko tayari kuwapokea watu kutoka kote duniani kuanzia Januari, ikiwa serikali itafutilia mbali hitaji la viza,” asema Bw James Shikwati, ambaye ni mtaalamu na mdadisi wa masuala ya kiuchumi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WYCLIFFE NYABERI RAIS William Ruto amesema hana uwezo wowote wa kupunguza bei ya mafuta ya petroli na bidhaa zake kwa kuwa bei hiyo huamuliwa na wauzaji. Kiongozi wa taifa badala yake amesema bei ambazo anaweza kushughulikia kuzizusha ni zile zinazoambatana na gharama ya maisha, akisisitiza kuwa ameweka juhudi kubadilisha hali. Akihutubu Jumamosi alipozuru Kaunti ya Kisii, Dkt Ruto alisema ana mpango kabambe utakaowawezesha Wakenya kupata afueni na wataanza kuona matunda ya kazi yake hivi karibuni. “Nilipokuwa nikitafuta kazi hii nilikuwa na mpango. Tuambiane ukweli. Sina uwezo wa kushusha bei ya mafuta kwa kuwa hiyo inaamuliwa na wanaoyauza. Yale nitakayofanya ili kushusha gharama ya maisha ni kupunguza bei ya mbolea ili wakulima wazalishe chakula kwa wingi. Nitazidi kuajiri walimu, kujenga nyumba za gharama nafuu na vituo vya kidijitali ili vijana wetu wapate nafasi na ajira za kujimudu,” Dkt Ruto akasema alipohudhuria hafla ya kuchangisha pesa katika Kanisa Katoliki la Dayosisi ya Kisii katika eneo la Mosocho. Mbali na kudondoa yale ambayo ameyafanya kwa mwaka mmoja afisini, aliwarai Wakenya waunge mkono utawala wake huku akitetea safari zake za mara kwa mara nje ya nchi, akisema zina manufaa mengi kwa taifa hili. “Siwezi kukaa Sugoi tu wakati ninafaa kuipigia Kenya debe. Kuna makelele mengi yanayopigwa kuhusu safari zangu lakini acheni niwaambie kwamba safari hizo ni za manufaa tele. Kila mtu sasa anataka kuja hapa Kenya na ndiyo sababu mliona tukisema watu hawafai kuwa na visa ili kuzuru,” Dkt Ruto alisema. Kwenye ziara hiyo, rais aliandamana na naibu wake Rigathi Gachagua, Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu, magavana Simba Arati (Kisii), Amos Nyaribo (Nyamira), wabunge kadha na viongozi wengine. Bw Rigathi aliwaeleza watu wa jamii ya Abagusii kukumbatia mpango wa serikali wa kujenga nyumba za bei nafuu kwani  nyumba hizo zitawafaa. Naibu Rais ambaye ni mbunge wa zamani wa Mathira, pia aliwaomba wakazi wa Gusii kuunga mkono utawala wa Kenya Kwanza huku akisema watu wa eneo hilo hawafai kuachwa kwenye kijibaridi cha kutokuwa ndani ya serikali. “Watu wa Gusii jipangeni nyuma ya huyu rais. Yeye ndiye mwenye kisu cha kugawa nyama na hivyo msipotelee msituni,” Bw Gachagua alirai. Mbunge wa Nyaribari Chache Zaheer Jhanda na Naibu Gavana wa Kisii Dkt Robert Monda, walipata wakati mgumu kuhutubia waumini hao kanisani. Soma Pia: Mbunge Zaheer Jhanda azomewa kwa kudai Rais Ruto hana uwezo kupunguza bei ya mafuta You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WYCLIFFE NYABERI RAIS William Ruto amesema hana uwezo wowote wa kupunguza bei ya mafuta ya petroli na bidhaa zake kwa kuwa bei hiyo huamuliwa na wauzaji. Kiongozi wa taifa badala yake amesema bei ambazo anaweza kushughulikia kuzizusha ni zile zinazoambatana na gharama ya maisha, akisisitiza kuwa ameweka juhudi kubadilisha hali. Akihutubu Jumamosi alipozuru Kaunti ya Kisii, Dkt Ruto alisema ana mpango kabambe utakaowawezesha Wakenya kupata afueni na wataanza kuona matunda ya kazi yake hivi karibuni. “Nilipokuwa nikitafuta kazi hii nilikuwa na mpango. Tuambiane ukweli. Sina uwezo wa kushusha bei ya mafuta kwa kuwa hiyo inaamuliwa na wanaoyauza. Yale nitakayofanya ili kushusha gharama ya maisha ni kupunguza bei ya mbolea ili wakulima wazalishe chakula kwa wingi. Nitazidi kuajiri walimu, kujenga nyumba za gharama nafuu na vituo vya kidijitali ili vijana wetu wapate nafasi na ajira za kujimudu,” Dkt Ruto akasema alipohudhuria hafla ya kuchangisha pesa katika Kanisa Katoliki la Dayosisi ya Kisii katika eneo la Mosocho. Mbali na kudondoa yale ambayo ameyafanya kwa mwaka mmoja afisini, aliwarai Wakenya waunge mkono utawala wake huku akitetea safari zake za mara kwa mara nje ya nchi, akisema zina manufaa mengi kwa taifa hili. “Siwezi kukaa Sugoi tu wakati ninafaa kuipigia Kenya debe. Kuna makelele mengi yanayopigwa kuhusu safari zangu lakini acheni niwaambie kwamba safari hizo ni za manufaa tele. Kila mtu sasa anataka kuja hapa Kenya na ndiyo sababu mliona tukisema watu hawafai kuwa na visa ili kuzuru,” Dkt Ruto alisema. Kwenye ziara hiyo, rais aliandamana na naibu wake Rigathi Gachagua, Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu, magavana Simba Arati (Kisii), Amos Nyaribo (Nyamira), wabunge kadha na viongozi wengine. Bw Rigathi aliwaeleza watu wa jamii ya Abagusii kukumbatia mpango wa serikali wa kujenga nyumba za bei nafuu kwani  nyumba hizo zitawafaa. Naibu Rais ambaye ni mbunge wa zamani wa Mathira, pia aliwaomba wakazi wa Gusii kuunga mkono utawala wa Kenya Kwanza huku akisema watu wa eneo hilo hawafai kuachwa kwenye kijibaridi cha kutokuwa ndani ya serikali. “Watu wa Gusii jipangeni nyuma ya huyu rais. Yeye ndiye mwenye kisu cha kugawa nyama na hivyo msipotelee msituni,” Bw Gachagua alirai. Mbunge wa Nyaribari Chache Zaheer Jhanda na Naibu Gavana wa Kisii Dkt Robert Monda, walipata wakati mgumu kuhutubia waumini hao kanisani. Soma Pia: Mbunge Zaheer Jhanda azomewa kwa kudai Rais Ruto hana uwezo kupunguza bei ya mafuta You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA MKUU wa Mawaziri na Waziri wa Masuala ya Kigeni Musalia Mudavadi amewakashifu wakosoaji wa mpango wa serikali wa kubinafsisha baadhi ya mashirika ya umma akisema hiyo ni mojawapo ya njia za kukwamua uchumi wa nchi. Bw Mudavadi alisema kuwa kile ambacho watu hao wanafaa kuzingatia ni iwapo mchakato huo unaendeshwa kwa njia ya uwazi na kwa mujibu wa sheria wala sio kuupinga. “Ukweli ni kwamba kama serikali tunakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi. Kwa kuwa tumetumia njia mbili za kupata pesa kama vile utozaji wa ushuru na ukopaji na kufikia hatua ambayo sasa inaumiza, sharti tusake njia nyingine za kupata pesa. “Mojawapo ya njia hizo ni kuuza mashirikia ambayo hayaleti faida bali yanategemea ufadhili kutoka kwa serikali kila mara. Masharika haya yanafaa kuwekwa chini ya usimamizi mpya ili yazalishe faida,” akasema Jumamosi alipotuhutubu katika kongomano la kila mwaka la Chama cha Walimu wa Shule za Upili na Vyuo vya Kadri (Kuppet). Kongamano hilo, ambalo liliandaliwa kuwa uwanja wa kimataifa wa michezo, Kasarani, Nairobi pia lilitumika kuadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwa chama hicho. “Kama serikali sharti tukomeshe huu mtindo wa kuendelea kuwatoza ushuru Wakenya bali tusake njia mbadala za kupata rasilimali za kutatua changamoto zinazowakumba nyie walimu na wanafunzi wenu,” Bw Mudavadi akasisitiza. Juzi, Waziri wa Fedha Njuguna Ndung’u aliorodhesha jumla ya mashirika 11 ambayo serikali inapania kubinafsisha hivi karibuni. Miongoni mwa mashirika hayo ni Jumba la Mikutano ya Kimataifa la Kenyatta (KICC), Shirika la Uchapishaji la Kenya Literature Bureau (KLB), Shirika la Kitaifa la Mafuta la National Oil (NOCK), Kampuni ya Mbegu Nchini (KSC) na Kampuni ya Mchele ya Mwea (MRM). Pia serikali inapania kubinafisha kampuni ya mchele ya Western Kenya (WKRM), Kampuni ya Usafirishaji Mafuta Nchini (KPC), kampuni ya maziwa ya New KCC, Numerical Machining Complex (NMC), Kenya Vehicle Manufacturers (KVM) na kampuni ya kutengeneza nguo ya Rivatex (REAL). Kulingana na Profesa Ndung’u, serikali inalenga kukusanya zaidi ya Sh200 bilioni baada ya kuuza hisa zake katika mashirika hayo. Bw Mudavadi aidha anatoa changamoto kwa Kuppet kununua hisa katika jumba la KICC ili liweze kuzalisha faida. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA MKUU wa Mawaziri na Waziri wa Masuala ya Kigeni Musalia Mudavadi amewakashifu wakosoaji wa mpango wa serikali wa kubinafsisha baadhi ya mashirika ya umma akisema hiyo ni mojawapo ya njia za kukwamua uchumi wa nchi. Bw Mudavadi alisema kuwa kile ambacho watu hao wanafaa kuzingatia ni iwapo mchakato huo unaendeshwa kwa njia ya uwazi na kwa mujibu wa sheria wala sio kuupinga. “Ukweli ni kwamba kama serikali tunakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi. Kwa kuwa tumetumia njia mbili za kupata pesa kama vile utozaji wa ushuru na ukopaji na kufikia hatua ambayo sasa inaumiza, sharti tusake njia nyingine za kupata pesa. “Mojawapo ya njia hizo ni kuuza mashirikia ambayo hayaleti faida bali yanategemea ufadhili kutoka kwa serikali kila mara. Masharika haya yanafaa kuwekwa chini ya usimamizi mpya ili yazalishe faida,” akasema Jumamosi alipotuhutubu katika kongomano la kila mwaka la Chama cha Walimu wa Shule za Upili na Vyuo vya Kadri (Kuppet). Kongamano hilo, ambalo liliandaliwa kuwa uwanja wa kimataifa wa michezo, Kasarani, Nairobi pia lilitumika kuadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwa chama hicho. “Kama serikali sharti tukomeshe huu mtindo wa kuendelea kuwatoza ushuru Wakenya bali tusake njia mbadala za kupata rasilimali za kutatua changamoto zinazowakumba nyie walimu na wanafunzi wenu,” Bw Mudavadi akasisitiza. Juzi, Waziri wa Fedha Njuguna Ndung’u aliorodhesha jumla ya mashirika 11 ambayo serikali inapania kubinafsisha hivi karibuni. Miongoni mwa mashirika hayo ni Jumba la Mikutano ya Kimataifa la Kenyatta (KICC), Shirika la Uchapishaji la Kenya Literature Bureau (KLB), Shirika la Kitaifa la Mafuta la National Oil (NOCK), Kampuni ya Mbegu Nchini (KSC) na Kampuni ya Mchele ya Mwea (MRM). Pia serikali inapania kubinafisha kampuni ya mchele ya Western Kenya (WKRM), Kampuni ya Usafirishaji Mafuta Nchini (KPC), kampuni ya maziwa ya New KCC, Numerical Machining Complex (NMC), Kenya Vehicle Manufacturers (KVM) na kampuni ya kutengeneza nguo ya Rivatex (REAL). Kulingana na Profesa Ndung’u, serikali inalenga kukusanya zaidi ya Sh200 bilioni baada ya kuuza hisa zake katika mashirika hayo. Bw Mudavadi aidha anatoa changamoto kwa Kuppet kununua hisa katika jumba la KICC ili liweze kuzalisha faida. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WYCLIFFE NYABERI MBUNGE wa Nyaribari Chache Zaheer Jhanda amepata wakati mgumu kuhutubia umma katika uwanja wa Cardinal Otunga Mosocho, Kisii, alipozomewa kwa kusema Rais William Ruto hahusiki kivyovyote na kuongezeka au kupungua kwa bei ya mafuta. Mbunge huyo wa awamu ya kwanza, alipigiwa kelele alipomtetea Rais Ruto aliyekuwa katika hafla hiyo ya Kanisa Katoliki ambapo waumini walifika kuchangisha pesa za Dayosisi ya Kanisa Katoliki. “Hakuna… hakuna… bei ya mafuta ishuke,” akasikika mmoja wa Wakenya waliohudhuria hafla hiyo. Sauti za kilio cha aina hiyo ziliendelea kusikika kwa dakika chache. Licha ya kupigiwa kelele hata hivyo, Bw Jhanda alijibidiisha na kumaliza hotuba yake japo kwa ukali. Aidha Naibu Rais Rigathi Gachagua naye alikuwa kwenye hafla hiyo ya kuchangisha pesa. Awali, Mbunge wa Kitutu Chache Kusini Anthony Kibagendi alikuwa amemwambia Rais Ruto ateremshe bei ya mafuta hadi Sh150 kwa lita ndiposa Wakenya walala hoi wapate afueni. Seneta wa Kisii Richard Onyonka alikubaliana na ombi la mbunge Kibagendi kwa kiongozi wa nchi ambapo pia alimtaka rais atafute namna ya kushughulikia muhimu la kuwapunguzia Wakenya mzigo kwa kupunguza gharama ya maisha. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WYCLIFFE NYABERI MBUNGE wa Nyaribari Chache Zaheer Jhanda amepata wakati mgumu kuhutubia umma katika uwanja wa Cardinal Otunga Mosocho, Kisii, alipozomewa kwa kusema Rais William Ruto hahusiki kivyovyote na kuongezeka au kupungua kwa bei ya mafuta. Mbunge huyo wa awamu ya kwanza, alipigiwa kelele alipomtetea Rais Ruto aliyekuwa katika hafla hiyo ya Kanisa Katoliki ambapo waumini walifika kuchangisha pesa za Dayosisi ya Kanisa Katoliki. “Hakuna… hakuna… bei ya mafuta ishuke,” akasikika mmoja wa Wakenya waliohudhuria hafla hiyo. Sauti za kilio cha aina hiyo ziliendelea kusikika kwa dakika chache. Licha ya kupigiwa kelele hata hivyo, Bw Jhanda alijibidiisha na kumaliza hotuba yake japo kwa ukali. Aidha Naibu Rais Rigathi Gachagua naye alikuwa kwenye hafla hiyo ya kuchangisha pesa. Awali, Mbunge wa Kitutu Chache Kusini Anthony Kibagendi alikuwa amemwambia Rais Ruto ateremshe bei ya mafuta hadi Sh150 kwa lita ndiposa Wakenya walala hoi wapate afueni. Seneta wa Kisii Richard Onyonka alikubaliana na ombi la mbunge Kibagendi kwa kiongozi wa nchi ambapo pia alimtaka rais atafute namna ya kushughulikia muhimu la kuwapunguzia Wakenya mzigo kwa kupunguza gharama ya maisha. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA TITUS OMINDE BARAZA la Wahubiri na Maimamu nchini (CIPK) limepinga sera mpya ya Wizara ya Elimu ya vigezo vipya vya uainishaji wa masomo ya kutumiwa kutathmini alama na gredi ambapo kwa Kiingereza na Kiswahili, mtahiniwa atatuzwa alama kwa somo moja tu.   Mwenyekiti wa CIPK North Rift Abubakar Bini amesema hatua hiyo ni njama pana ya kudunisha lugha ya Kiswahili ambayo ni kiungo muhimu katika maadili ya Kiafrika miongoni mwa wanafunzi. Akihutubia wanahabari mjini Eldoret mnamo Ijumaa, Sheikh Bini alisema baraza hilo litatumia kila mbinu kupinga pendekezo hilo. “Wizara ya Elimu itahatarisha maadili ya watoto wetu kwa sababu Kiswahili ni somo la Kiafrika linaloweka zingatio kwa kufundisha maadili mema. Tusidunishe somo hili kwa nia ya kuendelea kupandisha hadhi ya Kiingereza ambacho kiukweli ni lugha ya kigeni,” alilalama Sheikh Bini. Sheikh Bini alitilia mkazo kwamba somo la Kiswahili ni lazima liwe la lazima. Kiongozi huyo alitaka vyama vya walimu kupinga pendekezo la kufanya somo hilo liwe la ‘hiari’ kwa namna iliyofichika. “Vyama vya walimu lazima viungane nasi kupinga sera hii. Sheria ya bunge iliidhinisha Kiswahili kuwa Lugha Rasmi sawia na Kiingereza. Itakuaje tena wizara inaondoa somo hilo miongoni mwa masomo ya lazima?” akauliza. Kiongozi huyo wa dini alionya kuwa iwapo sera hiyo itatekelezwa kwa lazima, baraza la CIPK litaandaa maandamano ya kupinga hatua hiyo. Vile vile Sheikh Bini aliongeza kuwa baraza hilo litashauriana na mawakili wake ili kutafuta uwezekano wa kufika mahakamani kutafuta suluhu ya kisheria kuhusu sera lengwa. Msimamo sawa na huo ulitolewa na wakereketwa wa Kiswahili nchini ambao wamepinga mpango wa kuondoa somo la Kiswahili miongoni mwa masomo ya lazima. Tayari Seneta wa Tana River Danson Mungatana amesema atawasilisha bungeni mswada wa kupinga pendekezo la kufanya Kiswahili somo la hiari. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA TITUS OMINDE BARAZA la Wahubiri na Maimamu nchini (CIPK) limepinga sera mpya ya Wizara ya Elimu ya vigezo vipya vya uainishaji wa masomo ya kutumiwa kutathmini alama na gredi ambapo kwa Kiingereza na Kiswahili, mtahiniwa atatuzwa alama kwa somo moja tu.   Mwenyekiti wa CIPK North Rift Abubakar Bini amesema hatua hiyo ni njama pana ya kudunisha lugha ya Kiswahili ambayo ni kiungo muhimu katika maadili ya Kiafrika miongoni mwa wanafunzi. Akihutubia wanahabari mjini Eldoret mnamo Ijumaa, Sheikh Bini alisema baraza hilo litatumia kila mbinu kupinga pendekezo hilo. “Wizara ya Elimu itahatarisha maadili ya watoto wetu kwa sababu Kiswahili ni somo la Kiafrika linaloweka zingatio kwa kufundisha maadili mema. Tusidunishe somo hili kwa nia ya kuendelea kupandisha hadhi ya Kiingereza ambacho kiukweli ni lugha ya kigeni,” alilalama Sheikh Bini. Sheikh Bini alitilia mkazo kwamba somo la Kiswahili ni lazima liwe la lazima. Kiongozi huyo alitaka vyama vya walimu kupinga pendekezo la kufanya somo hilo liwe la ‘hiari’ kwa namna iliyofichika. “Vyama vya walimu lazima viungane nasi kupinga sera hii. Sheria ya bunge iliidhinisha Kiswahili kuwa Lugha Rasmi sawia na Kiingereza. Itakuaje tena wizara inaondoa somo hilo miongoni mwa masomo ya lazima?” akauliza. Kiongozi huyo wa dini alionya kuwa iwapo sera hiyo itatekelezwa kwa lazima, baraza la CIPK litaandaa maandamano ya kupinga hatua hiyo. Vile vile Sheikh Bini aliongeza kuwa baraza hilo litashauriana na mawakili wake ili kutafuta uwezekano wa kufika mahakamani kutafuta suluhu ya kisheria kuhusu sera lengwa. Msimamo sawa na huo ulitolewa na wakereketwa wa Kiswahili nchini ambao wamepinga mpango wa kuondoa somo la Kiswahili miongoni mwa masomo ya lazima. Tayari Seneta wa Tana River Danson Mungatana amesema atawasilisha bungeni mswada wa kupinga pendekezo la kufanya Kiswahili somo la hiari. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA LAWRENCE ONGARO SERIKALI itafanya juhudi kuwafidia wakulima na wafugaji waliopata hasara baada ya mvua ya El-Nino kusababisha mafuriko na kuharibu mazao na malisho. Katibu katika Wizara ya Kilimo Dkt Paul Rono alisema kwa wakati huu, serikali inalenga wafugaji kutoka maeneo ya Kaskazini Mashariki ili wapate namna ya kulisha mifugo. Alisema kaunti za Wajir, Garissa, Mandera, Marsabit, na Turkana ziliathirika kwa asilimia 70. Katibu huyo alizuru kituo cha utafiti wa mimea cha KALRO eneo la Kandara, Kaunti ya Murang’a, aliposhuhudia upanzi wa miti 1,500. Alisema serikali inaendelea kutathmini hasara iliyopatikana ya wakulima na wafugaji kupoteza mimea na mifugo ili ipange jinsi ya kuwafidia popote walipo kote nchini. “Mvua ya El- Nino imeleta hasara kubwa nchini na ndiyo maana serikali iko mbioni kuona ya kwamba inashughulikia wakulima na wafugaji haraka iwezekanavyo,” alisema Dkt Rono. Alisema maeneo ya Kaskazini Mashariki yameathirika ambapo shughuli za usafiri kuingia na kutoka maeneo hayo ni shida. Alisema serikali inafanya juhudi kushirikiana na sekta za kibinafsi kwa lengo la kuwapa misaada wahasiriwa. “Tunataka tuwe makini ili tujue idadi kamili ya wahasiriwa katika kila kona ya nchi,” alisema. Kulingana na katibu huyo, baada ya serikali kusambaza mbolea kwa wingi katika maeneo mengi hapa nchini inatarajia kwamba mavuno ya magunia 44 milioni ya mahindi yatapatikana mwaka 2023. Alisema mbolea itasambazwa wakati ufaao mwaka 2024 ili ifikapa mwaka wa 2027,  mazao ya mahindi yawe magunia 72 milioni. “Serikali itafanya juhudi kuona ya kwamba mbolea inamfikia hata mkulima aliye mashinani,” alisema. Alieleza kuwa mwaka 2022 serikali ilisambaza magunia 53 milioni ya mbolea kwa wakulima wapatao 550,000 kote nchini. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA LAWRENCE ONGARO SERIKALI itafanya juhudi kuwafidia wakulima na wafugaji waliopata hasara baada ya mvua ya El-Nino kusababisha mafuriko na kuharibu mazao na malisho. Katibu katika Wizara ya Kilimo Dkt Paul Rono alisema kwa wakati huu, serikali inalenga wafugaji kutoka maeneo ya Kaskazini Mashariki ili wapate namna ya kulisha mifugo. Alisema kaunti za Wajir, Garissa, Mandera, Marsabit, na Turkana ziliathirika kwa asilimia 70. Katibu huyo alizuru kituo cha utafiti wa mimea cha KALRO eneo la Kandara, Kaunti ya Murang’a, aliposhuhudia upanzi wa miti 1,500. Alisema serikali inaendelea kutathmini hasara iliyopatikana ya wakulima na wafugaji kupoteza mimea na mifugo ili ipange jinsi ya kuwafidia popote walipo kote nchini. “Mvua ya El- Nino imeleta hasara kubwa nchini na ndiyo maana serikali iko mbioni kuona ya kwamba inashughulikia wakulima na wafugaji haraka iwezekanavyo,” alisema Dkt Rono. Alisema maeneo ya Kaskazini Mashariki yameathirika ambapo shughuli za usafiri kuingia na kutoka maeneo hayo ni shida. Alisema serikali inafanya juhudi kushirikiana na sekta za kibinafsi kwa lengo la kuwapa misaada wahasiriwa. “Tunataka tuwe makini ili tujue idadi kamili ya wahasiriwa katika kila kona ya nchi,” alisema. Kulingana na katibu huyo, baada ya serikali kusambaza mbolea kwa wingi katika maeneo mengi hapa nchini inatarajia kwamba mavuno ya magunia 44 milioni ya mahindi yatapatikana mwaka 2023. Alisema mbolea itasambazwa wakati ufaao mwaka 2024 ili ifikapa mwaka wa 2027,  mazao ya mahindi yawe magunia 72 milioni. “Serikali itafanya juhudi kuona ya kwamba mbolea inamfikia hata mkulima aliye mashinani,” alisema. Alieleza kuwa mwaka 2022 serikali ilisambaza magunia 53 milioni ya mbolea kwa wakulima wapatao 550,000 kote nchini. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI JACQUE Maribe, mtangazaji wa zamani, anayekabiliwa na kesi ya mauaji Ijumaa, Desemba 15, 2023 alizirai na kushindwa kutembea uamuazi wa kesi inayomkabili pamoja na aliyekuwa mpenzi wake, Joseph Irungu almaarufu Jowie, ulipoahirishwa hadi Januari 26 mwaka ujao, 2023. Bi Maribe alitoka nje ya mahakama nambari 18 katika Mahakama Kuu ya Milimani, kisha akazirai alipokuwa akiteremka kwenye ngazi. Jacque alisaidiwa na watu wa familia kusimama lakini akaamua kuketi kwenye ngazi akilia, huku akiwa amejishika tumbo. Baada ya kuona hayo, mama yake pamoja na watu wengine wa familia waliangua kilio. Jacque alisaidiwa kutoka nje ya mahakama na kukaa ndani ya gari, watu wa familia, pamoja na Wakili Katwa Kigen anayemtetea wakifanya mkutano wa dharura. Alipopata nguvu, Jacque aliabiri gari aina ya Mercedez Benz na kufululiza kwa kasi na kutoweka. Baadhi ya waliofika kortini, ni pamoja na aliyekuwa mkurugenzi wa masuala ya mawasiliano Ikulu ya Nairobi, Dennis Itumbi. Hii ni mara ya pili kesi hiyo kuahirishwa kutokana na sababu sisizoepukika. Uamuzi wa ikiwa washukiwa hao wawili watafungwa au kauchiliwa huru uliahirishwa mara ya kwanza Oktoba 6,2023 Jaji Grace Nzioka alipougua na kupewa likizo. Akiahirisha uamuzi huo tena, Jaji Nzioka alifichua kwamba alipokea ushahidi uliotoweka katika kesi hiyo na upande wa mashtaka usiku wa Desemba 11, 2023 na hajapata muda wa kutosha kuuandaa. Maribe na Jowie wanaoshtakiwa kwa kumuua Monica Kimani mnamo Septemba 2018, walikuwa na matumaini kujua ikiwa wamepatikana na hatia ya kumuua Monica Kimani au la. Wakipatikana na hatia mahakama itawahukumu. Punde tu uamuzi huo ulipoahirishwa kwa mara ya pili, Maribe alizirai katika veranda huku akilia akiuliza “Nitapata haki lini? Kila wakati uamuzi katika kesi hii inaahirishwa bila sababu maalum.” Bi Maribe alisaidiwa kusimama na watu wa familia yake. Mtangazaji huyo wa zamani katika kituo kimoja cha televisheni nchini, alipelekwa nje ya mahakama kisha akaingizwa kwa gari muundo wa Mercedez Benz. Kesi hiyo ilipotajwa kwa njia ya mtandao na Jaji Nzioka anayehudumu katika Mahakama Kuu Naivasha alisema “samahani wote, sijamaliza kutayarisha uamuzi katika kesi hii. Nilipokea ushahidi katika kesi hii usiku wa Desemba 11, 2023 na sijauangalia na kuukagua ipasavyo.” Aidha, Jaji huyo alisema anahitaji muda wa kutosha kukagua ushahidi ili “atoe uamuzi unaoridhia na wa haki.” Jaji Nzioka alitwaa usukani wa kusikiza kesi hiyo kutoka kwa Jaji James Wakiaga aliyehamishwa kutoka kitengo cha kusikiza kesi za mauaji hadi kuamua kesi za biashara. Wawili hao walishtakiwa Oktoba 2018 na kuzuiliwa katika magereza ya Viwandani (Jowie) na Lang’ata (Maribe). Mahakama ilimwachilia Maribe kwa dhamana lakini Jowie akanyimwa hadi pale mashahidi fulani waliodai wanahofia maisha yao akiachiliwa kwa dhamana walipokamilisha kutoa ushahidi. Maiti ya Monica ilikutwa ndani ya bafu katika mtaa wa Kilimani akiwa amefungwa mikono na shingo imekatwa kwa kisu. Maji ya mfereji katika bafu ya Monica yalikuwa yamefunguliwa. Mashahidi waliofika kortini, walieleza mahakama Jowie ndiye alikuwa mtu wa mwisho kuonekana na Monica. Ushahidi mwingine ni kwamba Jowie alitumia gari la Maribe kuenda katika makazi ya Monica usiku alipouawa. Akiwa mtangazaji katika kituo cha televisheni, Maribe ndiye alipeperusha habari za mauaji ya Monica. Jaji Nzioka alielezwa kwamba Jowie alikuwa ameomba bastola ya jirani wa Maribe. Lakini wote wamejitenga na mauaji hayo wakisema hawakuhusika kamwe. Wawili hao wako nje kwa dhamana. Alipokumbana na mauti, Monica alikuwa ametua Nairobi kutoka Sudan Kusini ambapo alikuwa akifanya biashara.     You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI JACQUE Maribe, mtangazaji wa zamani, anayekabiliwa na kesi ya mauaji Ijumaa, Desemba 15, 2023 alizirai na kushindwa kutembea uamuazi wa kesi inayomkabili pamoja na aliyekuwa mpenzi wake, Joseph Irungu almaarufu Jowie, ulipoahirishwa hadi Januari 26 mwaka ujao, 2023. Bi Maribe alitoka nje ya mahakama nambari 18 katika Mahakama Kuu ya Milimani, kisha akazirai alipokuwa akiteremka kwenye ngazi. Jacque alisaidiwa na watu wa familia kusimama lakini akaamua kuketi kwenye ngazi akilia, huku akiwa amejishika tumbo. Baada ya kuona hayo, mama yake pamoja na watu wengine wa familia waliangua kilio. Jacque alisaidiwa kutoka nje ya mahakama na kukaa ndani ya gari, watu wa familia, pamoja na Wakili Katwa Kigen anayemtetea wakifanya mkutano wa dharura. Alipopata nguvu, Jacque aliabiri gari aina ya Mercedez Benz na kufululiza kwa kasi na kutoweka. Baadhi ya waliofika kortini, ni pamoja na aliyekuwa mkurugenzi wa masuala ya mawasiliano Ikulu ya Nairobi, Dennis Itumbi. Hii ni mara ya pili kesi hiyo kuahirishwa kutokana na sababu sisizoepukika. Uamuzi wa ikiwa washukiwa hao wawili watafungwa au kauchiliwa huru uliahirishwa mara ya kwanza Oktoba 6,2023 Jaji Grace Nzioka alipougua na kupewa likizo. Akiahirisha uamuzi huo tena, Jaji Nzioka alifichua kwamba alipokea ushahidi uliotoweka katika kesi hiyo na upande wa mashtaka usiku wa Desemba 11, 2023 na hajapata muda wa kutosha kuuandaa. Maribe na Jowie wanaoshtakiwa kwa kumuua Monica Kimani mnamo Septemba 2018, walikuwa na matumaini kujua ikiwa wamepatikana na hatia ya kumuua Monica Kimani au la. Wakipatikana na hatia mahakama itawahukumu. Punde tu uamuzi huo ulipoahirishwa kwa mara ya pili, Maribe alizirai katika veranda huku akilia akiuliza “Nitapata haki lini? Kila wakati uamuzi katika kesi hii inaahirishwa bila sababu maalum.” Bi Maribe alisaidiwa kusimama na watu wa familia yake. Mtangazaji huyo wa zamani katika kituo kimoja cha televisheni nchini, alipelekwa nje ya mahakama kisha akaingizwa kwa gari muundo wa Mercedez Benz. Kesi hiyo ilipotajwa kwa njia ya mtandao na Jaji Nzioka anayehudumu katika Mahakama Kuu Naivasha alisema “samahani wote, sijamaliza kutayarisha uamuzi katika kesi hii. Nilipokea ushahidi katika kesi hii usiku wa Desemba 11, 2023 na sijauangalia na kuukagua ipasavyo.” Aidha, Jaji huyo alisema anahitaji muda wa kutosha kukagua ushahidi ili “atoe uamuzi unaoridhia na wa haki.” Jaji Nzioka alitwaa usukani wa kusikiza kesi hiyo kutoka kwa Jaji James Wakiaga aliyehamishwa kutoka kitengo cha kusikiza kesi za mauaji hadi kuamua kesi za biashara. Wawili hao walishtakiwa Oktoba 2018 na kuzuiliwa katika magereza ya Viwandani (Jowie) na Lang’ata (Maribe). Mahakama ilimwachilia Maribe kwa dhamana lakini Jowie akanyimwa hadi pale mashahidi fulani waliodai wanahofia maisha yao akiachiliwa kwa dhamana walipokamilisha kutoa ushahidi. Maiti ya Monica ilikutwa ndani ya bafu katika mtaa wa Kilimani akiwa amefungwa mikono na shingo imekatwa kwa kisu. Maji ya mfereji katika bafu ya Monica yalikuwa yamefunguliwa. Mashahidi waliofika kortini, walieleza mahakama Jowie ndiye alikuwa mtu wa mwisho kuonekana na Monica. Ushahidi mwingine ni kwamba Jowie alitumia gari la Maribe kuenda katika makazi ya Monica usiku alipouawa. Akiwa mtangazaji katika kituo cha televisheni, Maribe ndiye alipeperusha habari za mauaji ya Monica. Jaji Nzioka alielezwa kwamba Jowie alikuwa ameomba bastola ya jirani wa Maribe. Lakini wote wamejitenga na mauaji hayo wakisema hawakuhusika kamwe. Wawili hao wako nje kwa dhamana. Alipokumbana na mauti, Monica alikuwa ametua Nairobi kutoka Sudan Kusini ambapo alikuwa akifanya biashara.     You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MHARIRI
BAADHI ya shule nchini zimejitokeza na kupinga matokeo ya Mtihani ya Darasa la Nane (KCPE) yaliyotangazwa Jumatano na Waziri... NA MHARIRI
SERIKALI za kaunti zitalazimika kutafuta mbinu za usimamizi wa fedha iwapo magavana wanataka kujitolea kutimiza ahadi zao kwa... NA MHARIRI
KILA Juni 14, ulimwengu huadhimisha Siku ya watu kuchangia damu duniani. Mwaka huu, kaulimbiu ilikuwa “Utoaji damu ni suala... NA MHARIRI
UCHAGUZI mkuu wa Agosti 9 ulikuwa wa kipekee kwa jinsi ulivyokuwa na ushindani mkali kuliko mwingineo wowote ambao umewahi... NA MHARIRI
MNAMO Ijumaa Rais William Ruto alipozuru eneo la Magharibi mwa Kenya, alisisitiza ahadi yake ya kuhakikisha kuwa viwanda vya... NA MHARIRI
TANGAZO la Benki Kuu ya Kenya (CBK) kwamba wateja wataanza kutozwa ada ya kutoa pesa kutoka kwa benki hadi simu zao linajiri... NA MHARIRI
RIPOTI ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali inayoonyesha kuwa mabunge ya kaunti yanapitisha bajeti kiholela bila kuhusisha... NA MHARIRI
MKOPO wa Hustler Fund ulioanza kutolewa kwa wananchi wenye uwezo mdogo kimapato mnamo Jumatano huenda usiwafaidi raia jinsi... NA MHARIRI
UZINDUZI wa Hazina ya Hustler jana Jumatano sasa unawapa matumaini mamia ya mama mboga, wanabodaboda na wafanyibiashara ndogo... NA MHARIRI
HATUA ya serikali kuondoa marufuku dhidi ya mahindi ya GMO imezua mjadala mkali nchini.
Suala la GMO limetekwa nyara na... NA MHARIRI
KWA wiki chache sasa, kumekuwa na wasiwasi katika baadhi ya sehemu za nchi kuhusu homa ambayo inaonekana kuenea kwa... NA MHARIRI
RIPOTI kwamba wabunge, kupitia Tume ya Huduma ya Bunge (PSC), wanataka kushinikiza Tume ya Mishahara na Marupurupu (SRC)... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na BENSON MATHEKA
NAIBU wa Rais William Ruto atatumia muungano ‘ulioundwa’ mwaka 2021 na kiongozi wa Amani National Congress (ANC)... Na WANDERI KAMAU
Naibu Rais William Ruto na waandani wake wameapa kufanya kila wawezalo kulemaza juhudi za Kiongozi wa ODM, Raila Odinga... Na CHARLES WASONGA
WABUNGE wandani wa Naibu Rais William Ruto jana walifaulu kuzuia kupitishwa kwa Mswada tata wa marekebisho ya Sheria... BRIAN OCHARO na VALENTINE OBARA
UBABE wa kisiasa kati ya Kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, na Naibu Rais William Ruto katika Kaunti ya... Na CHARLES WASONGA
HATUA ya Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga kushikilia kuwa wawaniaji wanaounga azma zao za... Na WANDERI KAMAU
SUALA lililozua gumzo wiki hii ni majibizano yaliyozuka kati ya mrengo wa Naibu Rais William Ruto na mwanasiasa Maina... Na JUSTUS WANGA
GAVANA wa Meru Kiraitu Murungi amekiri kwamba umaarufu wa Naibu Rais William Ruto umekita mizizi zaidi katika eneo la... Na CECIL ODONGO
INASIKITISHA kuwa Naibu Rais Dkt William Ruto na Seneta wa Baringo Gideon Moi sasa wanalitumia suala la msitu wa Mau kwa... Na WYCLIFFE NYABERI
NAIBU Rais Dkt William Ruto amemshambulia Rais Uhuru Kenyatta huku akisema ataondoka mamlakani bila kulipa deni la... Na CHARLES WASONGA
NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga wanaonekana kuendeleza mbinu za kampeni za kulambana visigino... Na IAN BYRON
HATUA ya Gavana Okoth Obado kujihusisha na siasa za chama cha United Democratic Alliance (UDA) cha Naibu Rais, Dkt William... BENSON MATHEKA NA CHARLES WASONGA
?WASHIRIKA wa Naibu Rais William Ruto wamegeuka kupe kwa ‘ kufyoza mamilioni ya fedha anazoyapa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na MASHIRIKA
LONDON, Uingereza
WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson, jana alitangaza masharti makali kudhibiti maambukizi ya... Na ELIZABETH MERAB
WANASAYANSI wanachunguza kuhusu mchipuko wa virusi vipya vya corona aina ya Delta, katika nchi za Amerika, Uingereza,... Na MAUREEN ONGALA
MASAIBU ambayo wagonjwa wa Covid-19 hupitia katika kaunti za Pwani, yameanikwa wazi baada ya kifo cha afisa mkuu wa... SIAGO CECE na ANTHONY KITIMO
UFISADI miongoni mwa baadhi ya maafisa wa serikali katika mpaka wa Kenya na Tanzania, umezidi kuwaweka... Na WAANDISHI WETU
WINGU la maangamizi limetanda kote nchini huku aina mpya ya corona maarufu kama 'Delta' ikiua watu kwa... Na WINNIE ONYANDO
HUENDA visa vya wasafiri kulazimishwa kupima upya corona mpakani mwa Kenya na Tanzania vikakoma baada ya serikali hizo... NA WANGU KANURI
AGIZO la serikali la kudhibiti mkurupuko wa ugonjwa wa corona mwaka jana limewashurutisha Wakenya wengi kufanyia kazi... Na Titus Ominde
VIONGOZI wa kidini Kaskazini mwa Rift Valley (North Rift) wameshutumu wanasiasa kwa kupepeta usambazaji wa virusi vya... Na WANTO WARUI
Huku wanafunzi wa kidato cha kwanza wakiripoti katika shule zao mpya za sekondari hii leo, kuna uwezekano wa maambukizi... Na CHARLES WASONGA
NAKUBALIANA na kauli ya maafisa wa afya katika kaunti ya Nairobi kwamba wanasiasa ndio wanachochea ongezeko la visa... Na SAMMY WAWERU
DICKSON Muceri amekuwa mkazi wa Nairobi kwa muda wa miaka kadhaa ila sasa kitovu hicho cha jiji kuu la nchi hakikaliki... Na MARY WANGARI
WANASAYANSI wamethibitisha kuwa kuchelewesha upokeaji dozi ya pili ya chanjo ya Covid-19 kwa kiasi cha miezi 10 baada ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na KINYUA BIN KINGORI
WAKATI huu viongozi wa kisiasa wameanza mapema kampeni zao kwa kuzuru maeneo mbalimbali nchini, ili kushawishi... Na WANDERI KAMAU
KULINGANA na Ripoti ya Jaji Mstaafu Akilano Akiwumi (1997) kuhusu chimbuko la ghasia za kikabila nchini, wanasiasa ndio... Na WANTO WARUI
KWA mara nyingine tena tuzo inayoenziwa sana kote ulimwenguni imerudi katika eneo letu la Afrika Mashariki mara hii... Na DOUGLAS MUTUA
MWAFRIKA akiwajibishwa na Mzungu hupiga kamsa na kudai anaonewa, ati msingi wa maonevu ni ubaguzi wa rangi... Na WANDERI KAMAU
MOJA ya changamoto kuu zinazokikumba kizazi cha sasa nchini ni ukosefu wa ufahamu wa lugha zao asili.
Ingawa lugha... Na KINYUA BIN KINGORI
JUHUDI za kuhakikisha taifa limefanikiwa kupiga vita ufisadi lazima ziendeshwe kuambatana na Katiba, bila njama... Na WANDERI KAMAU
UFICHUZI wa sakata ambapo watu maarufu duniani wamekuwa wakificha mabilioni ya fedha katika akaunti za siri ng’ambo... Na FAUSTINE NGILA
NINA imani kuwa iwapo kufikia sasa hujawahi kuelewa teknolojia ya blokcheni, leo utaelewa kwa kuwa jana uliathirika... Na CHARLES WASONGA
NI jambo la kusikitisha kuwa ni wakati kama huu ambapo uchaguzi mkuu unakaribia ndipo wanasiasa wametambua umuhimu wa... Na MARY WANGARI
IDADI ya watu wanaoandaa hafla za uchangishaji pesa za kugharamia matibabu imeongezeka pakubwa katika siku za hivi... Na CECIL ODONGO
CHAMA cha Kanu bado kina safari ndefu kurejelea umaarufu wake wa enzi za utawala wa chama kimoja na miaka ya 90 hata... Na CHARLES WASONGA
UTEUZI wa waliokuwa maafisa wanne wa ngazi za juu katika Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kushikilia nyadhifa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Naomi Wamboi, 21, ndiye anatupambia yeye ni mwanamitindo aliyewahi kushinda tuzo za Miss Nakuru. Akipata muda anapenda kusafiri na... Winnie Miriam Nechesa 21, ni mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu Cha Maasai Mara kaunti ya Narok.Anapenda kuchora, na kujumuika na... Lilian Njeri mwenye umri wa miaka 21 ndiye anatupambia jarida letu leo.Yeye ni mwanamitindo na mkaazi wa Narok.Uraibu wake ni kusafiri na... Mary Njeri mwenye umri wa miaka 21 ni mkaazi wa mtaa wa Langalanga kaunti ya Nakuru.Yeye ni mwanafasheni wa mapambo na vipodozi.Uraibu wake... Marylene Watiri mwenye umri wa miaka 22 ni mtaalam wa Beauty Therapy jijini Nairobi, aidha yeye ni mwanamitindo na mlimbwende.Uraibu wake... Zaweria Njoki mwenye umri wa miaka 21 ni Video Vixen kutoka kaunti ya Nakuru.Uraibu wake ni kuandika makala ya kitaaluma na kujumuika na...
Malkia wetu leo ni  Babra Ingasiani mwenye umri wa miaka 21, yeye ni mzaliwa wa kaunti ya Kakamega.Uraibu wake ni kusakata densi ya... Pauline Kimani mwenye umri wa miaka 23 ndiye anatupambia jarida letu leo.Yeye ni mkaazi wa eneo la Lanet na mfanyikazi mjini Nakuru.Uraibu...
Sayfer Godez ni mkaazi wa Nakuru .Anapenda kushiriki kwenye majukwaa ya mapambo na urembo.Uraibu wake ni kusafiri na kujumuika na... Sylvia Wangeci 23 ni mzaliwa wa Molo, na mwanafunzi katika Chuo Kikuu Cha MKU tawi la Nakuru.Uraibu wake ni kusafiri na... Mical Abulatsia Imbukwa, 28, ni mwanahabari katika shirika moja jijini Nairobi. Uraibu wake ni kutazama filamu za Afro sinema na kujumuika... Faith Karungari mwenye umri wa miaka 22 ni mwanafasheni na mwanamitindo maarufu kutoka Nakuru.Uraibu wake ni kuogelea na kusikiliza muziki... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na RICHARD MUNGUTI
MAHAKAMA ya Juu jana ilianza kusikiza rufaa ya mpango wa kubadilisha katiba (BBI) huku Mwanasheria Mkuu Bw Paul... Na BENSON MATHEKA
RAIS Uhuru Kenyatta jana Jumapili alisema kuwa ndoto yake ya kubadilisha katiba ya Kenya iliyopitishwa 2010 kupitia... Na CHARLES WASONGA
KWA mara nyingine Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza kuwa mageuzi ya katiba yaliyopendekezwa katika Mswada wa Mpango wa... Na JOSEPH WANGUI
Mwanasheria Mkuu, Paul Kihara Kariuki hatimaye amewasilisha rasmi rufaa katika Mahakama ya Juu kupinga uamuzi wa... Na Gitonga Marete
KIONGOZI wa chama cha Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi amesisitiza kuwa Bunge linapaswa kurejelea Mpango... Na Leonard Onyango
NAIBU wa Rais William Ruto amewataka wabunge kujadili masuala nyeti yanayoathiri Wakenya badala ya kujaribu kufufua... Na CHARLES WASONGA
JUHUDI za wabunge wanaoegemea mrengo wa Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga kutumia bunge kupitisha... Na WALTER MENYA
JUHUDI za kuokoa mchakato wa marekebisho ya katiba kupitia mpango wa maridhiano (BBI) zimefikishwa rasmi katika Mahakama... Na FRANCIS MUREITHI
KUSAMBARATIKA kwa Mpango wa Kubadilisha Katiba (BBI) kumefifisha pakubwa ushawishi wa kisiasa wa mwenyekiti wa Kanu,... Na WANDERI KAMAU
KUHARAMISHWA kwa Mpango wa Kubadilisha Katiba (BBI) na Mahakama ya Rufaa kunatarajiwa kutoa mwelekeo mpya kwa siasa za... Na WANDERI KAMAU
NAIBU Rais William Ruto jana alimtaka Rais Uhuru Kenyatta kurejelea miradi ya maendeleo iliyoanzishwa na Jubilee, baada... Na Cecil Odongo
BAADA ya Mahakama ya Rufaa kukubaliana na uamuzi wa mahakama kuu wa kuzima mswada wa Mpango wa Maridhiano (BBI) Ijumaa,... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MAUREEN ONGALA
SERIKALI ya kaunti ya Kilifi imeonya wamiliki wa maeneo ya burudani wanaocheza muziki kwa sauti ya juu bila kuwa na... NA PETER MBURU
WAKENYA wanazidi kulishwa ahadi butu na wagombeaji wakuu wa urais, hasa Raila Odinga na William Ruto kuhusu jinsi maisha... Na LEONARD ONYANGO
HOFU ya kuangushwa kwenye mchujo na wawaniaji chipukizi imesukuma baadhi ya wanasiasa kung’ang’ania wakuu wa... Na BENSON MATHEKA
Maisha ya kisiasa ya kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga yamebadilika pakubwa uchaguzi mkuu wa mwaka ujao... Na SAMMY WAWERU
NI rasmi sasa kiongozi wa ODM, Raila Odinga atakuwa debeni kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao,... NA JUMA NAMLOLA
WIKI hii hapa katika meza ya habari ya Taifa Leo tuliangazia mambo ambayo wanasiasa wote waliojitokeza kutamani uraia... NA WANDERI KAMAU
JE, taswira ya urais wa kiongozi wa ODM, Raila Odinga, itakuwa vipi ikiwa ataibuka mshindi kwenye uchaguzi mkuu wa... NA BENSON MATHEKA
Kila dalili zinaonyesha kuwa Naibu Rais William Ruto anahofia kwamba ataibiwa kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.... NA KIPKOECH CHEPKWONY
NAIBU Rais Dkt William Ruto Jumatatu amewataka wapinzani wake, akiwemo kinara wa ODM Raila Odinga, kukataa kuungana... NA PAUL WAFULA
AHADI za kuimarisha uchumi zinazotolewa na Naibu Rais William Ruto na Kiongozi wa ODM Raila Odinga zitaongeza matatizo ya... Na CHARLES WASONGA